Tuesday, February 28, 2023

MHE. JENISTA AWATAKA WATUMISHI WA OFISI YAKE KUTOA USHIRIKIANO WA KIUTENDAJI KWA VIONGOZI WAPYA ILI KUENDELEA KUUBORESHA UTUMISHI WA UMMA

 Na. James K. Mwanamyoto-Dodoma

Tarehe 28 Februari, 2023

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama ametoa wito kwa watumishi wa ofisi yake kuendelea kutoa ushirikiano wa kiutendaji kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi walioteuliwa na kuapishwa jana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kutumikia ofisi hiyo.

Mhe. Jenista ametoa wito huo leo jijini Dodoma, wakati wa hafla fupi ya kuwapokea viongozi hao walipowasili ofisini kwa ajili ya kuanza kazi rasmi mara baada ya kuapishwa jana na Rais wa Jamhuri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mhe. Jenista amesema ushirikiano kwa viongozi hao kutoka kwa watumishi utawawezesha kwa kiasi kikubwa kutekeleza majukumu yao kikamilifu na kutoa mchango katika Utumishi wa Umma kama ilivyokusudiwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mhe. Jenista amesema, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, imepata viongozi wenye sifa stahiki kwa ajili ya kuongeza nguvu ya kiutendaji, hivyo hatuna budi kuwapa ushirikiano wa kutosha ili waweze kutekeleza majukumu yao kikamilifu katika kufikia maono ya Rais wa Awamu ya Sita ya kuuboresha Utumishi wa Umma nchini.

Mhe. Jenista ameongeza kuwa, viongozi hao wateule wataendeleza pale walipoishia watangulizi wao katika kuujenga utumishi wa umma wenye uadilifu na unaowajibika kwa wananchi katika kutoa huduma bora.

Kwa upande wake, Naibu Waziri mteule, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa watumishi wote na kuongeza kuwa, atahakikisha anasimamia haki katika kufanya kazi.

Mhe. Ridhiwani amesema, moja ya jukumu lake ni kumsaidia Waziri wake Mhe. Jenista Mhagama kutekeleza jukumu la kusimamia utumishi wa umma na utawala bora kwani kwa kufanya hivyo atakuwa ni sehemu ya utekelezaji wa malengo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ya kuujenga utumishi wa umma unaowajibika kwa wananchi kwa hiari.

Naye Katibu Mkuu mteule, Bw. Juma Mkomi ameahidi kutoa ushirikiano kwa watumishi wa ofisi yake na kuwaomba nao kumpatia ushirikiano ili aweze kutekeleza majukumu aliyopatiwa na Mhe. Rais ya kutoa mchango katika ustawi wa Utumishi wa Umma nchini.

Bw. Mkomi amemshukuru mtangulizi wake, Dkt. Laurean Ndumbaro kwa msingi alioujenga katika utumishi wa umma na kuahidi kuendelea kutumia busara zake katika kuuimarisha utumishi wa umma.

Akitoa neno la shukurani, Katibu Mkuu aliyemaliza muda wake, Dkt. Laurean Ndumbaro, amemshukuru Waziri Jenista Mhagama, Watendaji na watumishi wote wa Ofisi ya Rais-Utumishi kwa ushirikiano waliompatia wakati wa uongozi wake uliowezesha kutekeleza jukumu la kuusimamia utumishi wa umma.

Amewasihi watumishi hao kuendelea kutoa ushirikiano kwa Viongozi wateule, kufanya kazi kwa bidii na uadilifu ili utumishi wa umma uwe na tija kwa ustawi wa taifa.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (wa pili kutoka kushoto) akipokea taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya ofisi yake kutoka kwa mtangulizi wake, Dkt. Laurean Ndumbaro (wa kwanza kulia) mara baada ya Bw. Mkomi kuripoti rasmi katika ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma. Wanaoshuhudia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama (katikati) akizungumza na watumishi wa ofisi yake kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wake Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa kwanza kulia) kuzungumza na watumishi hao mara baada ya kuripoti rasmi katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Juma Mkomi.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa pili kutoka kulia) akizungumza na watumishi wa ofisi hiyo mara baada ya kuripoti rasmi katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma baada ya kuteuliwa na kuapishwa na Mhe. Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan Kulia kwake ni Waziri wa Ofisi hiyo Mhe. Jenista Mhagama.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akizungumza na Menejimenti ya ofisi yake mara baada ya kuripoti rasmi katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma baada ya kuteuliwa na kuapishwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma aliyemaliza muda wake, Dkt. Laurean Ndumbaro (wa kwanza kulia) akitoa neno la shukurani kwa watumishi wa ofisi hiyo alipokuwa akiwaaga. Wengine ni viongozi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akimkaribisha Naibu Waziri wa ofisi yake, Mhe. Ridhiwani Kikwete mara baada ya kuripoti rasmi katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma baada ya kuteuliwa na kuapishwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akimkaribisha Katibu Mkuu wa ofisi yake Bw. Juma Mkomi mara baada ya kuripoti rasmi katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma baada ya kuteuliwa na kuapishwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI. Nyuma ya Mhe. Waziri Jenista ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Maadili, Bi. Leila Mavika mara baada ya Naibu waziri huyo kuripoti rasmi katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma. 


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akisalimiana na watumishi wa ofisi hiyo mara baada ya kuripoti rasmi katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma. Kushoto kwake ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama.


Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama wakati akiwakaribisha Naibu Waziri wa ofisi hiyo na Katibu Mkuu mara baada ya kuripoti rasmi katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama (meza kuu) akizungumza jambo na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (kushoto) mara baada ya Katibu Mkuu huyo kuripoti katika ofisi hizo Mtumba jijini Dodoma. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi.





 

No comments:

Post a Comment