Wednesday, February 1, 2023

WAAJIRI SERIKALINI WATAKIWA KUTOKWEPA JUKUMU LA KUWACHUKULIA HATUA WATUMISHI WANAOKIUKA MAADILI

Na. James K. Mwanamyoto-Dodoma

Tarehe 01 Februari, 2023

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi amewataka waajiri katika taasisi za umma kutokwepa jukumu la kuwachukulia hatua za kinidhamu watumishi watakaobanika kukiuka maadili ya utendaji kazi katika taasisi zao.

Bw. Daudi ametoa wito huo jijini Dodoma wakati akifunga kikao kazi cha siku mbili cha wadau wa usimamizi wa maadili katika utumishi wa umma kilicholenga kujadili matokeo ya utafiti ya hali ya uzingatiaji maadili katika utumishi wa umma ya mwaka 2022.

Bw. Daudi amesema pamoja na uwepo wa Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo inayosimamia maadili katika Utumishi wa Umma, bado baadhi ya Watendaji wanashindwa kusimamia maadili na kuchukua hatua stahiki kwa watumishi wanaobainika kukiuka maadili.

“Waajiri wengi mkiwemo baadhi yenu ndani ya kikao hiki ambao mnasimamia masula ya utawala na rasilimawatu, mna kawaida ya kukwepa jukumu la kuchukua hatua za kinidhamu kwa watumishi wasio waadilifu na badala yake mnaelekeza masuala hayo Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala ili yafanyiwe kazi jambo ambalo sio sahihi.” Bw. Daudi amefafanua.

Bw. Daudi ameongeza kuwa, Waajiri watakaowasilisha Ofisi ya Rais-UTUMISHI masuala ya kinidhamu ya watumishi wanaowasimamia, hayatafanyiwa kazi badala yake yatarejeshwa ili waajiri hao watekeleze jukumu lao.

Bw. Daudi amesisitiza kuwa, jukumu la kumchukulia hatua mtumishi ambaye si mwadilifu ni la Mwajiri, hivyo hakuna sababu ya kusita kufanya maamuzi kwa masilahi mapana ya Utumishi wa Umma na kuongeza kuwa, Ofisi ya Rais-UTUMISHI haitashughulikia shauri la kinidhamu la mtumishi lililowasilishwa kwa matarajio ya mtumishi husika kuhamishiwa kituo kingine cha kazi kwani kwa kufanya hivyo ni kuhamisha tatizo.

Akielezea majukumu yaliyotekelezwa na kikao kazi hicho, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Bi. Leila Mavika amesema kikao kazi kimebainisha maeneo yenye changamoto za uadilifu katika Utumishi wa Umma na kuainisha mikakati madhubuti ya kuimarisha uadilifu katika Utumishi wa Umma.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kikao kazi hicho ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mipango Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Cosmas Ngangaji amesema, washiriki wa kikao kazi hicho wametekeleza ipasavyo jukumu lao kwa kutoa mapendekezo yatakayoimarisha maadili katika Utumishi wa Umma kutokana na mapungufu yaliyoainishwa katika taarifa ya utafiti ya hali ya uzingatiaji maadili katika utumishi wa umma ya mwaka 2022

 

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akifunga kikao kazi cha siku mbili cha wadau wa usimamizi wa maadili katika utumishi wa umma kilicholenga kujadili matokeo ya tafiti ya hali ya uzingatiaji maadili katika utumishi wa umma ya mwaka 2022, jijini Dodoma.


Sehemu ya wadau wa usimamizi wa maadili katika utumishi wa umma wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) wakati akifunga kikao kazi cha siku mbili cha wadau hao kilicholenga kujadili matokeo ya tafiti ya hali ya uzingatiaji maadili katika utumishi wa umma ya mwaka 2022, jijini Dodoma.



Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Bi. Leila Mavika akielezea namna kikao kazi cha siku mbili cha wadau wa usimamizi wa maadili katika utumishi wa umma kilivyofanyika kabla ya Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi kufunga kikao kazi cha wadau hao kilicholenga kujadili matokeo ya tafiti ya hali ya uzingatiaji maadili katika utumishi wa umma ya mwaka 2022, jijini Dodoma.

Mwenyekiti wa kikao kazi cha wadau wa usimamizi wa maadili katika utumishi wa umma kilicholenga kujadili matokeo ya tafiti ya hali ya uzingatiaji maadili katika utumishi wa umma ya mwaka 2022, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mipango Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Cosmas Ngangaji akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi kufunga kikao kazi cha wadau hao jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akisikiliza maazimio ya kikao kazi cha siku mbili cha wadau wa usimamizi wa maadili katika utumishi wa umma kilicholenga kujadili matokeo ya tafiti ya hali ya uzingatiaji maadili katika utumishi wa umma ya mwaka 2022 jijini Dodoma. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa kikao kazi hicho, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mipango Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Cosmas Ngangaji na kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Bi. Leila Mavika.


Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Ufuatiliaji wa Uzingatiaji wa Maadili, Bi. Janeth Mishinga akiwasilisha maazimio yaliyopendekezwa na wadau wa usimamizi wa maadili katika utumishi wa umma kabla ya Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi kufunga kikao kazi cha wadau hao cha siku mbili kilicholenga kujadili matokeo ya tafiti ya hali ya uzingatiaji maadili katika utumishi wa umma ya mwaka 2022, jijini Dodoma.



Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akisikiliza hoja ya Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Bi. Leila Mavika alipokuwa akiagana nae mara baada ya Naibu Katibu Mkuu huyo kufunga kikao kazi cha siku mbili cha wadau wa usimamizi wa maadili katika utumishi wa umma kilicholenga kujadili matokeo ya tafiti ya hali ya uzingatiaji maadili katika utumishi wa umma ya mwaka 2022, jijini Dodoma. Kulia kwake ni aliyekuwa Mwenyekiti wa kikao kazi hicho, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mipango Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Cosmas Ngangaji 
 

No comments:

Post a Comment