Friday, May 30, 2025

SIMBACHAWENE AWAASA WAHITIMU TPSC KUSIMAMIA NA KUTUNZA MAADILI YA TAALUMA WALIZOSOMEA KWA USTAWI WA TAIFA

Na. Veronica Mwafisi-Singida

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene amewaasa wahitimu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) kusimamia na kutunza maadili ya taaluma walizosomea kwa ustawi wa taifa.

Mhe. Simbachawene amesema hayo leo tarehe 30 Mei, 2025 kwenye Mahafali ya 41 ya kuwatunuku wahitimu wa ngazi mbalimbali wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Social Rwoma RC Mission mkoani Singida.

“Kuhitimu ngazi za Shahada, Stashahada na Astashahada katika fani mbalimbali sio jambo dogo, elimu mliyoipata ni kubwa, hakikisheni mnasimamia na kutunza maadili ya elimu hiyo kwa manufaa yenu na ustawi wa taifa” amesisitiza Mhe. Simbachawene.

Mhe. Simbachawene amewataka wahitimu walioajiriwa katika Utumishi wa Umma na watakaoajiriwa kufanya kazi kwa bidii kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo ya Utumishi wa Umma ikiwa ni pamoja na kutunza siri za Serikali na kuepuka rushwa katika utekelezaji wa majukumu yao na wahitimu ambao hawana ajira kutumia ujuzi walioupata kujiajiri kwa maendeleo ya taifa.

Aidha, ametoa rai kwa wahitimu hao kutunza afya zao pamoja na kuepuka Magonjwa Yasiyoambuza kwa kuwa taifa linawahitaji katika kukuza uchumi wa nchi.

Vilevile, Mhe. Simbachawene ameueleza uongozi wa chuo hicho kuwa Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ina matarajio makubwa na Chuo hicho kwa kuwa kimeimarika sana hasa katika kuwajengea uwezo watumishi wa Umma na kutoa wahitimu mahiri na wenye uzalendo wanaoleta chachu ya maendeleo nchini.

Kadhalika, Mhe. Simbachawene amewapongeza Walimu, Wazazi na Walezi wa wahitimu hao kwa jitihada kubwa ambazo kila mmoja kwa nafasi yake amezifanya ili kufanikisha kupata wahitimu hao wa ngazi za Shahada, Stashahada na Astashahada katika fani mbalimbali.

Awali, Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania Dkt. Ernest Mabonesho amemshukuru Waziri Simbachawene kwa kukubali mwaliko wa kuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo na kumtaarifu kuwa jumla ya wanafunzi 1330 wamehitimu kozi mbalimbali katika chuo hicho wakiwemo wanawake 906 na wanaume 224.

Dkt. Mabonesho ameongeza kuwa pamoja na jitihada nyingine zinazofanywa na chuo hicho, wameendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali za ndani ikiwemo Chuo cha Hombolo na vyuo vingine mbalimbali pamoja na vya nje ya nchi kwa lengo la kuboresha ujuzi na kubadilishana uzoefu katika utendajikazi.

“Mhe. Mgeni rasmi tumefanya jitihada mbalimbali ili kuboresha mafunzo yetu kwa kushirikiana na vyuo vingine vya ndani na nje ya nchi hasa vinavyohusika na masuala ya Utumishi wa Umma ikiwemo chuo cha Hombolo pamoja na vyuo vingine ili kuweza kupata fursa ya kujifunza na kuboresha utendajikazi” alisema Dkt. Mabonesho.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, SACP. Ibrahim Mahumi amesema taifa limepata wahitimu ambao ni nguvukazi nyingine watakaosaidia utendajikazi katika Utumishi wa Umma na taifa kwa ujumla.

Aidha, SACP. Mahumi amemshukuru na kumpongeza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene kwa kusimamia miongozo mbalimbali pamoja na taasisi zilizopo chini ya ofisi hiyo ambayo imekisaidia Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania kuhitimisha wanafunzi wanaoweza kutekeleza majukumu mbalimbali pasipokuwa na changamoto zozote.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza na wahitimu wa kozi mbalimbali (hawapo pichani) katika Mahafali ya 41 ya kuwatunuku wahitimu wa ngazi mbalimbali wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Social Rwoma RC Mission mkoani Singida.

Sehemu ya wahitimu wa kozi mbalimbali katika mahafali ya 41 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati akizungumza nao kwenye mahafali hayo yaliyofanyika katika Ukumbi wa Social Rwoma RC Mission mkoani Singida.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (mwenye kofia nyekundu) akijumuika katika maandamano ya wahitimu wa kozi mbalimbali (hawapo pichani) katika Mahafali ya 41 ya kuwatunuku wahitimu hao wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Social Rwoma RC Mission mkoani Singida.


Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, SACP. Ibrahim Mahumi akitoa akitoa neno la utangulizi kwa wahitimu wa kozi mbalimbali (hawapo pichani) kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kuzungumza na wahitimu hao wakati wa Mahafali ya 41 ya kuwatunuku wahitimu wa ngazi mbalimbali wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Social Rwoma RC Mission mkoani Singida.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (kulia) akiteta jambo na Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Ernest Mabonesho (kushoto) wakati wa Mahafali ya 41 ya kuwatunuku wahitimu wa ngazi mbalimbali wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Social Rwoma RC Mission mkoani Singida.


Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Ernest Mabonesho akiwasilisha taarifa ya utendaji wa chuo kwa mgeni rasmi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene wakati wa mahafali ya 41 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Social Rwoma RC Mission mkoani Singida.


Sehemu ya wahitimu wa kozi mbalimbali katika mahafali ya 41 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania wakifurahi wakati wa maandamano yaliyofanyika nje ya Ukumbi wa Social Rwoma RC Mission mkoani Singida.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (mwenye kofia nyekundu) akiteta jambo na Mjumbe wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Prof. Masoud Muruke (wa kwanza kulia) ambaye amemwakilisha Mwenyekiti wa bodi hiyo kwenye Mahafali ya 41 wakati Waziri huyo alipowatunuku wahitimu wa ngazi mbalimbali wa chuo hicho (hawapo pichani) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Social Rwoma RC Mission mkoani Singida. Wa kwanza kushoto ni Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Ernest Mabonesho.


Sehemu ya wazazi na walezi wa wahitimu wa ngazi mbalimbali wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene wakati wa Mahafali ya 41 ya chuo hicho yaliyofanyika katika Ukumbi wa Social Rwoma RC Mission mkoani Singida


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (mwenye kofia nyekundu) akitazama maandamano ya wahitimu wa kozi mbalimbali (hawapo pichani) katika Mahafali ya 41 ya kuwatunuku wahitimu hao wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Social Rwoma RC Mission mkoani Singida. Wengine ni Viongozi wa mkoa huo na Watendaji wa chuo hicho.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na sehemu ya wahitimu wa ngazi mbalimbali wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania wakati wa Mahafali ya 41 ya chuo hicho yaliyofanyika katika Ukumbi wa Social Rwoma RC Mission mkoani Singida.


Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakielekea kwenye Ukumbi wa Social Rwoma RC Mission wakati walipojumuika kwenye msafara wa wahitimu wa ngazi mbalimbali wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi huo mkoani Singida.



Wednesday, May 28, 2025

KATIBU MKUU MKOMI AZISISITIZA TAASISI ZA UMMA KUSHIRIKI KIKAMILIFU WIKI YA UTUMISHI WA UMMA; AWAALIKA WANANCHI KUJITOKEZA KWA WINGI KUPATA HUDUMA


Na Mwandishi wetu-Dodoma.

 Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi amezisisitiza Taasisi za Umma zilizoalikwa kushiriki Maonesho ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kushiriki kikamilifu maonesho hayo yatakayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni, 2025 ili wananchi waweze kupata huduma za papo kwa hapo zitakazotolewa na Taasisi hizo huku akitoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika maonesho hayo.

 

Katibu Mkuu Mkomi ametoa msisitizo huo leo Jumatano, Mei 28, 2025 jijini Dodoma wakati wa Mkutano wake na Waandishi wa Wahabari kuhusu Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kitaifa.

 

Katibu Mkuu Mkomi amezitaja huduma zitakazotolewa papo kwa hapo kuwa ni vyeti vya kuzaliwa, vitambulisho vya taifa (NIDA), hati za viwanja, kupima afya kutoka Hospitali za Benjamin Mkapa, Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Muhimbili, Taasisi ya Mifupa (MOI) pamoja, huduma ya Gazeti la Serikali na nyingine nyingi.

 

“Nipende kutumia fursa hii kuwakaribisha wakazi wa Jiji la Dodoma na maeneo jirani, Watumishi wa Umma na wadau wa utumishi wa umma nchini kuhudhuria maonesho haya adhimu ili kujipatia huduma hizo” amesema Bw. Mkomi.

 

Amesema katika maadhimisho hayo, Wizara, Sekretarieti za Mikoa na Taasisi za Umma zitafanya maonesho hayo na kutoa elimu kuhusu utekelezaji wa majukumu yao huku Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora itaendesha kliniki ya kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa umma nchini papo kwa hapo.

 

Huduma hizo za papo kwa hapo zinaenda sambamba na kaulimbiu ya maadhimisho hayo kitaifa isemayo ‘‘Himiza Matumizi ya Mifumo ya Kidijiti ili Kuongeza Upatikanaji wa Taarifa na Kuchagiza Uwajibikaji’’

Akizungumzia umuhimu wa wananchi kujitokeza kwa wingi katika maonesho hayo, Bw. Mkomi amesema Maadhimisho hayo ya Wiki ya Utumishi wa umma ni jukwaa la Wananchi kupata fursa ya kufahamu wajibu wao na haki zao ili pindi wanapokosa haki zao waweze kujua namna ya kuzipata.

 

Vilevile, Bw. Mkomi ametaja faida na malengo ya maadhimisho hayo kwa Taasisi za Umma kuwa zitapata fursa ya kubadilishana uzoefu juu ya mbinu na mikakati mipya ya namna ya kutoa huduma bora kwa Umma pamoja na kupokea ushauri kutoka kwa wadau mbalimbali wakiwemo Wananchi, AZAKI, na Sekta Binafsi juu ya namna bora ya kuboresha utoaji huduma.

 

Ameongeza kuwa, Taasisi hizo zitapata fursa ya kuonyesha ubunifu waliofanya katika maeneo mbalimbali ya utoaji huduma na kuondoa urasimu usiokuwa wa lazima katika michakato mbalimbali ya utoaji huduma ikiwa ni pamoja na kupata mrejesho na kuutumia mrejesho huo kurekebisha kasoro za utendaji zinazosababisha malalamiko ya wateja ili huduma za Serikali ziboreshwe kukidhi matarajio ya Wananchi

 

Katika hatua nyingine Bw. Mkomi amewataka Watumishi wa Umma wote, kutimiza suala la kikatiba kuelekea katika Uchaguzi Mkuu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge na Madiwani Mwezi Oktoba, 2025 kujitokeza katika Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ili muda wa uchaguzi utakapofika waweze kuchagua viongozi bora kwa maendeleo ya taifa lao katika maeneo wanayofanyia kazi.

 

Wiki ya Utumishi wa Umma nchini huanza tarehe 16 Juni kila mwaka na huadhimishwa kwa kufanya mambo mbalimbali ikiwemo maonesho, kutoa elimu na huduma za papo kwa hapo ili kuifikia Siku ya Utumishi wa Umma ambayo husherehekewa na nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) tarehe 23 Juni kila mwaka.

 

 

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akizungumza wakati  Mkutano wake na Waandishi wa Wahabari kuhusu Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kitaifa yatakayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni, 2025 


 

 

 

 

 

 


Thursday, May 22, 2025

MHE. SIMBACHAWE AITEMBELEA FAMILIA YA HAYATI MSUYA. YAISHUKURU SERIKALI KWA USHIRIKIANO TANGU ENZI ZA UHAI WA BABA YAO MPAKA KIFO CHAKE

Na. Mwandishi Wetu-Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ametoa wito kwa Watanzania kumuenzi aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Mzee Cleopa David Msuya kwa kuendelea kudumisha umoja, amani na mshikamano na kuyaenzi mazuri yote aliyoyafanya enzi za uhai wake.

 

Mhe. Simbachawene ameyasema hayo leo tarehe 22 Mei, 2025 alipoitembelea familia ya Hayati Msuya nyumbani Upanga jijini Dar es Salaam.

 

Mhe. Simbachawene amesema Hayati Mzee Msuya atakumbukwa kwa kuwagusa watu wengi kwa namna alivyokuwa na upendo, kuwasaidia watu wengi pamoja na kuhamasisha maendeleo katika maeneo mbalimbali nchini.

 

Aidha, Mhe. Simbachawene amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwathamini Viongozi Wakuu wa Kitaifa Wastaafu kwa mujibu wa Sheria.

Akiongea kwa niaba ya familia, mtoto wa Hayati Msuya, Bi. Joyce Msuya-Mpanju ameishukuru Serikali kwa mchango wake mkubwa na ushirikiano uliotolewa kwa familia hiyo tangu enzi za uhai wa Baba yao alipoanza kuugua hadi umauti ulipomkuta na kusimama bega kwa bega wakati wa msiba mpaka kukamlisha salama taratibu za mazishi yake.

 “Tunaishukuru sana Serikali kwa kuwa pamoja na familia yetu tangu Mama alipofariki mmekuwa na Baba bega kwa bega, hii ilisaidia sana hata kumfanya Baba aishi maisha marefu maana tunaelewa mtu anapofiwa na Mwenza hali inavyokuwa. Mhe. Waziri tunaomba utufikishie salamu zetu kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samila Suluhu Hassan, Viongozi wote wa Serikali na Ofisi unayoiongoza kwa upendo mliotuonesha kwetu,” Bi. Joyce ameongeza.

Hayati Cleopa Msuya alifariki dunia tarehe 7 Mei, 2025 na kuzikwa nyumbani kwake Kijiji cha Chomvu, Usangi Wilayani Mwanga Mkoani Kilimanjaro tarehe13 Mei, 2025.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza na Familia ya  Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Mzee Cleopa David Msuya (hawapo pichani) alipoitembelea nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akisisitiza jambo kwa Familia ya Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Mzee Cleopa David Msuya (hawapo pichani) alipoitembelea nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akifafanua jambo kwa Familia ya Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Mzee Cleopa David Msuya (hawapo pichani) wakati Waziri wa Ofisi hiyo, Mhe. George Simbachawene (wa kwanza kulia) alipoitembelea Familia hiyo nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam.


Mtoto wa Hayati Mzee Cleopa David Msuya, Bi. Joyce Msuya Mpanju (aliyenyanyua mikono) akitoa shukrani kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipoitembelea Familia hiyo nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam.


Mkurugenzi Msaidizi Utawala na Dawati la Viongozi wa Kitaifa Wastaafu, Bi. Nyasinde Mukono akifafanua jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (wa pili kutoka kulia) wakati Waziri huyo alipoitembelea Familia ya Hayati Mzee Cleopa David Msuya nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam. Watatu kutoka kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi na Wa kwanza kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Bi. Mary Mwakapenda.


Mtoto wa Hayati Mzee Cleopa David Msuya, Bw. Job Msuya (katikati) akizungumza jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipoitembelea Familia hiyo nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiwa katika picha ya pamoja na Familia ya Hayati Mzee Cleopa David Msuya wakati alipoitembelea nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam. Wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI.



Monday, May 19, 2025

WAZIRI SIMBACHAWENE: SERIKALI YA TANZANIA INAHITAJI VIONGOZI WA KIMAGEUZI KATIKA KUSIMAMIA SHUGHULI ZA MAENDELEO

 Na. Lusungu Helela- Dar es Salaam

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amesema Serikali ya Tanzania katika kufikia malengo yake inahitaji viongozi wa kimageuzi wenye sifa, weledi na uwezo wa kuongoza kimkakati katika kusimamia shughuli za maendeleo ya nchi.

 

Akizungumza leo Ijumaa Mei 16, 2025 Jijini Dar es Salaam katika Mahafali ya Nane ya Programu za Uongozi zitolewazo na Taasisi ya UONGOZI, Mhe. Simbachawene amesema, uongozi bora ni nguzo ya Maendeleo Endelevu ya nchi huku akisisitiza kuwa hili litafanikiwa kwa kuwa na mikakati thabiti ya kuwajenga na kuwaendeleza viongozi. 

 

Amebainisha kuwa mikakati ya pamoja na kuwa na programu maalumu za kuendeleza viongozi wa ngazi za juu na wanaochipukia katika sekta ya umma, sekta binafsi na Asasi zisizo za Kiserikali ni jambo lisiloepukika.

 

Aidha Mhe. Simbachawene ameipongeza Taasisi ya UONGOZI kwa kuanza maandalizi ya kuwa na programu maalumu ya kuwezesha viongozi chipukizi ambao ni viongozi muhimu sana kwani wana kipindi kirefu cha kulitumikia taifa.

 

Amefafanua kuwa, kuwandaa na kuwajenga mapema viongozi hao chipukizi  kutaisaidia Serikali kuwa na kundi la viongozi ambao wanaweza kupatikana pale watakapohitajika kuhudumu katika nafasi mbalimbali za uongozi.

 

Kufuatia hatua hiyo, Mhe.Simbachawene amesema Agenda ya Umoja wa Afrika ya Mwaka 2063 itaweza kutimia kwa kuwa na viongozi makini na wenye kujenga Bara la Afrika lenye taswira bora zaidi yenye maono kwa kupunguza vikwazo vinavyorudisha nyuma maendeleo ya Bara hilo.

 

Awali, Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo, amesema programu zinazotolewa na Taasisi hiyo ni mahsusi katika kuwaanda na kuwajenga viongozi ili wakalete mapinduzi mahali pa kazi 

 

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Taasisi ya UONGOZI, Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Balozi Ombeni Sefue, amewataka Wahitimu hao wakawe chachu ya kuleta mabadiliko na kuhamasisha uvumbuzi na kutekeleza sera zinazokuza maendeleo jumuishi na endelevu ya Bara la Afrika kwa ujumla.

 "Tanzania inawahitaji, Afrika inawahitaji na Dunia inawahitaji, nendeni huko mkaoneshe kwa vitendo mlichojifunza kwenye Taasisi ya UONGOZI" amesisitiza Mhe. Balozi Sefue.

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akizungumza Wahitimu  kwenye  mahafali ya nane ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi yaliyofanyika leo  Jijini Dar es Salaam.



Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa  Maadili katika Utumishi wa Umma kutoka Ofisi ya Rais, UTUMISHI Na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli akitunukiwa cheti cha Programu ya Uongozi kwa Wanawake na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene  kwenye  mahafali ya nane ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi  yaliyofanyika leo  Jijini Dar es Salaam.

 

 

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini  kutoka Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Bi. Isabella Katondo akitunukiwa cheti cha Programu ya Uongozi kwa Wanawake na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene  kwenye  mahafali ya nane ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi  yaliyofanyika leo  Jijini Dar es Salaam.

 




Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini   kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Bi. Christina na Mwangosi akitunukiwa cheti cha Programu ya Uongozi kwa Wanawake na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene  kwenye  mahafali ya nane ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi  yaliyofanyika leo  Jijini Dar es Salaam.


 




Baadhi ya Wahitimu wa Programu ya Uongozi kwa Wanawake wakiwa mbele mara baada ya kutunukiwa vyeti vyao na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene  kwenye  mahafali ya nane ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi  yaliyofanyika leo  Jijini Dar es Salaam.


 


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Taasisi ya UONGOZI, Balozi. Ombeni Sefue akizungumza na  Wahitimu  kwenye  mahafali ya nane ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi  yaliyofanyika leo  Jijini Dar es Salaam mara baada ya kutunukiwa vyeti vyao.

 

 




Baadhi ya Wahitimu  kwenye  mahafali ya nane ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene yaliyofanyika leo  Jijini Dar es Salaam.






Baadhi ya Wahitimu wa Programu ya Uongozi kwa Wanawake wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi, Bw. Kadari Singo  mara baada ya kutunukiwa vyeti vyao na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene  kwenye  mahafali ya nane ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi  yaliyofanyika leo  Jijini Dar es Salaam.