Na. Lusungu Helela- Dar es Salaam
Akizungumza
leo Ijumaa Mei 16, 2025 Jijini Dar es Salaam katika Mahafali ya Nane ya
Programu za Uongozi zitolewazo na Taasisi ya UONGOZI, Mhe. Simbachawene amesema, uongozi
bora ni nguzo ya Maendeleo Endelevu ya nchi huku akisisitiza kuwa
hili litafanikiwa kwa kuwa na mikakati thabiti ya kuwajenga na
kuwaendeleza viongozi.
Amebainisha kuwa mikakati
ya pamoja na kuwa na programu maalumu za kuendeleza viongozi wa ngazi za
juu na wanaochipukia katika sekta ya umma, sekta binafsi na Asasi zisizo
za Kiserikali ni jambo lisiloepukika.
Aidha Mhe. Simbachawene
ameipongeza Taasisi ya UONGOZI kwa kuanza maandalizi ya kuwa na programu
maalumu ya kuwezesha viongozi chipukizi ambao ni viongozi muhimu sana
kwani wana kipindi kirefu cha kulitumikia taifa.
Amefafanua kuwa, kuwandaa na
kuwajenga mapema viongozi hao chipukizi kutaisaidia Serikali kuwa na
kundi la viongozi ambao wanaweza kupatikana pale watakapohitajika kuhudumu
katika nafasi mbalimbali za uongozi.
Kufuatia hatua
hiyo, Mhe.Simbachawene amesema Agenda ya Umoja wa Afrika ya Mwaka 2063
itaweza kutimia kwa kuwa na viongozi makini na wenye kujenga Bara la
Afrika lenye taswira bora zaidi yenye maono kwa kupunguza vikwazo
vinavyorudisha nyuma maendeleo ya Bara hilo.
Awali, Mtendaji Mkuu wa
Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo, amesema programu zinazotolewa na
Taasisi hiyo ni mahsusi katika kuwaanda na kuwajenga viongozi ili wakalete
mapinduzi mahali pa kazi
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya
Wakurugenzi wa Taasisi ya UONGOZI, Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Balozi Ombeni
Sefue, amewataka Wahitimu hao wakawe chachu ya kuleta mabadiliko na kuhamasisha
uvumbuzi na kutekeleza sera zinazokuza maendeleo jumuishi na endelevu ya Bara
la Afrika kwa ujumla.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akizungumza
Wahitimu kwenye mahafali ya nane ya programu za uongozi zitolewazo
na Taasisi ya Uongozi yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Maadili katika Utumishi wa Umma kutoka Ofisi ya Rais, UTUMISHI Na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli akitunukiwa cheti cha Programu ya Uongozi kwa Wanawake na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene kwenye mahafali ya nane ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini kutoka Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Bi. Isabella Katondo akitunukiwa cheti cha Programu ya Uongozi kwa Wanawake na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene kwenye mahafali ya nane ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Bi. Christina na Mwangosi akitunukiwa cheti cha Programu ya Uongozi kwa Wanawake na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene kwenye mahafali ya nane ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wahitimu wa Programu ya Uongozi kwa Wanawake wakiwa mbele mara baada ya kutunukiwa vyeti vyao na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene kwenye mahafali ya nane ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi wa Taasisi ya UONGOZI, Balozi. Ombeni Sefue
akizungumza na Wahitimu kwenye mahafali ya
nane ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi
yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam mara baada ya kutunukiwa vyeti
vyao.
Baadhi ya Wahitimu kwenye mahafali ya nane ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wahitimu wa Programu ya Uongozi kwa Wanawake wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi, Bw. Kadari Singo mara baada ya kutunukiwa vyeti vyao na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene kwenye mahafali ya nane ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.













No comments:
Post a Comment