Na.
Veronica Mwafisi-Dar es Salaam
Mradi
wa Tanzania ya Kidijitali umeleta mapinduzi makubwa ya miundombinu ya TEHAMA
nchini ikiwemo
kuunganisha jumla ya taasisi za umma 600 ambazo ni Wizara,
Mikoa, Halmashauri na Taasisi zote zilizohamia Dodoma ili kurahisisha
utoaji wa huduma kwa wananchi na watumishi wa umma.
Hayo
yamesemwa na Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala
Bora, Bw. Priscus Kiwango wakati wa
kikao kazi cha kujadili
utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
“Mradi
huu umeleta mafanikio makubwa katika kuunganisha Serikali kwenye mitandao ya
TEHAMA ambapo taasisi 600
ikiwemo Wizara,
Mikoa, Halmashauri na Taasisi zote zilizohamia Dodoma
zimeunganishwa na mifumo ya TEHAMA ili kutoa huduma kwa wananchi na watumishi
wa umma nchini,’’ amesema Bw. Kiwango
Ameongeza
kuwa katika kutoa huduma bora, watumishi wa umma wameendelea kutekeleza
majukumu yao kupitia mifumo
mbalimbali na
kupimwa kupitia mifumo iliyojengwa ya Usimamizi wa Utendaji Kazi katika Utumishi wa Umma na
Taasisi (e-Utendaji).
Aidha, Mfumo wa Daftari la Huduma za Serikali utawasaidia wananchi kupata huduma sehemu moja kwa
urahisi, kwa wakati na kwa uwazi.
Mkurugenzi
Kiwango ametoa wito kwa wananchi kutumia simu zao za viganjani kupiga namba *152*00# kwa ajili ya
kupata huduma mbalimbali za Serikali bila kufika katika ofisi husika endapo
hawatakuwa na ulazima wa kufanya hivyo.
Mkurugenzi
wa TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Priscus
Kiwango akizungumza kwenye kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa
Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi
wa Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bi. Salome Kessy
(katikati) akifurahia jambo na Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI
na Utawala Bora, Bw. Priscus Kiwango (kushoto kwake) wakati wa kikao kazi kilicholenga
kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini
Dar es Salaam. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Uendelezaji wa Mifumo na Huduma za
TEHAMA, Bw. Mohamed Mashaka.

Mwakilishi
wa Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bi. Salome Kessy
(katikati) akifurahia jambo na Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI
na Utawala Bora, Bw. Priscus Kiwango (kushoto kwake) wakati wa kikao kazi kilicholenga
kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini
Dar es Salaam. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Uendelezaji wa Mifumo na Huduma za
TEHAMA, Bw. Mohamed Mashaka.
Mkurugenzi
wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora,
Bi. Mary Mwakapenda (wa kwanza kulia) akiwa katika kikao kazi kilicholenga
kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini
Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wa kikao
kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wakimsikiliza Mkurugenzi wa
TEHAMA Serikalini, Bw. Priscus Kiwango (hayupo pichani) alipokuwa akifafanua
jambo kuhusu TEHAMA wakati wa kikao kazi hicho kilichofanyika jijini Dar es
Salaam.
Mwakilishi
kutoka Benki ya Dunia, Bw. Paul Seadin (aliyesimama) akichangia hoja wakati wa
kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali
kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi
ya washiriki wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa
Tanzania ya Kidijitali wakimsikiliza Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Bw.
Priscus Kiwango (hayupo pichani) alipokuwa akifafanua jambo kuhusu TEHAMA
wakati wa kikao kazi hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wa kikao kazi kilicholenga
kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wakimsikiliza Mwakilishi wa
Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mkurugenzi
wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bi. Salome Kessy (hayupo
pichani) wakati akifungua kikao kazi hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Msaidizi, Sehemu ya Sera za Tehama na Viwango, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na
Utawala Bora, Bw. Ibrahim Toure (wa kwanza kulia) akiwa katika kikao kazi
kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali
kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi
wa Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bi. Salome Kessy
(katikati mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa kikao
kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali
kilichofanyika jijini Dar es Salaam.