Tuesday, July 22, 2025

KIKAO KAZI CHA KUJADILI UTEKELEZAJI WA MRADI WA TANZANIA YA KIDIJITALI

 

Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bi. Salome Kessy (kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Priscus Kiwango (kushoto) wakati wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.


Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Priscus Tairo akiwasilisha taarifa ya utekelezaji kuhusu Usimamizi wa Utendaji Kazi katika Utumishi wa Umma na Taasisi (e-Utendaji) wakati wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya washiriki wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wakimsikiliza Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Priscus Tairo (hayupo pichani) alipokuwa akifafanua jambo kuhusu Usimamizi wa Utendaji Kazi katika Utumishi wa Umma na Taasisi (e-Utendaji) wakati wa kikao kazi hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam.

 

Mkurugenzi Msaidizi, Usimamizi wa Mifumo na Viwango vya Kimenejimenti, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bi. Veila Shoo akiwasilisha taarifa ya utekelezaji kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya washiriki wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa kikao kazi hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam.


Mwakilishi kutoka Benki ya Dunia, Bw. Paul Seadin (kulia) akifuatilia mada mbalimbali wakati wa kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.


Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Sera za Tehama na Viwango, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Ibrahim Toure (wa kwanza kulia) akiwa katika kikao kazi kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.

 


No comments:

Post a Comment