Monday, June 29, 2026

JICHO LA PEPMIS, BADO SIKU 1

 


KATIBU MKUU MKOMI AMPONGEZA NA KUMTAKIA HERI KATIBU MTEULE WA TUME YA UTUMISHI WA UMMA, AMUASA KUZINGATIA FALSAFA YA KAZI NA UTU KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Katibu Mkuu ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi amempongeza na kumtakia heri aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda.

Katibu Mkuu Mkomi ameyasema hayo jijini Dodoma baada ya kuhitimishwa kwa mafunzo yanayofanyika kila Jumatatu kwa watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambapo pia alitumia wasaa huo kumuaga Bw. Kipanda.

Bw. Mkomi amemuasa Katibu mteule huyo kutumia falsafa ya kazi na utu wakati wa utekelezaji wa majukumu yake ili aweze kutenda haki katika kufanya maamuuzi.

Amesema, matatizo mengi yanayowapata Watumishi wa Umma wakati mwingine yanatokana na kukosekana kwa utu wa waajiri hivyo, amemtaka Bw. Kipanda kufanya maamuzi yaliyo sahihi ili kutenda haki.

“Ninaamini Bw. Kipanda utaenda kutenda haki na kutuwakilisha vizuri, fanya kazi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na Utu. Taasisi uliyoteuliwa kufanya kazi inahusika na utoaji wa haki kwa Watumishi wa Umma, hivyo pamoja na kutumia taratibu, ukazingatie pia suala la utu katika kufanya maamuzi.

Vilevile, Bw. Mkomi amemuahidi Bw. Kipanda ushirikiano pale atakapohitaji ikiwa ni pamoja na ushauri katika kazi kwani itasaidia kuimarisha zaidi utendaji kazi.

Kwa upande wake Katibu Mteule wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumteua kuiongoza Taasisi hiyo.

Bw. Kipanda amewashukuru Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa kufanya kazi nao kwa muda mrefu na kuomba kuendelea kumpatia ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake mapya kwa maendeleo ya Taifa.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Katibu Mkuu Mstaafu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (kushoto). Kulia ni aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda 

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akizungumza jambo kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda baada ya kumaliza mafunzo kwa watumishi wa ofisi hiyo yaliyolenga kuwajengea uwezo katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa nasaha wakati wa kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda 


Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda (kulia)akipokea keki alipokuwa akiagwa na Watumishi wa Ofisi hiyo mara baada ya kuteuliwa kuwa Katibu wa Tume hiyo. 


Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Nolasco Kipanda ambaye kwa sasa ni Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma akikata keki akiwa anaagwa na watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI jijini Dodoma  


Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda akitoa neno la shukrani kwa Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI alipokuwa akiwaaga katika ofisi hiyo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda (hayupo pichani) wakati akitoa neno la shukrani kwa Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI alipokuwa akiwaaga baada ya kupata teuzi hiyo.


Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bw. Musa Magufuli akimlisha keki aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipandabaada ya kutoa neno la shukrani kwa Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI alipokuwa akiwaaga baada ya kupata teuzi hiyo.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa nasaha wakati wa kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda.



SERIKALI YAENDELEA KUBORESHA MAZINGIRA YA WATUMISHI WA UMMA KUPITIA UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

Na. Antonia Mbwambo- Mbeya

Tarehe 29 Juni, 2026

Serikali imeendelea kuboresha mazingira ya kazi kwa Watumishi wa Umma kupitia utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa nyumba za makazi, hatua inayolenga kuongeza ufanisi wa utendaji kazi na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute, wakati wa ziara ya kukagua ujenzi wa nyumba za watumishi katika Shule za Msingi Ngolela, Wilaya ya Kyela na Idweli, Wilaya ya Rungwe, mkoani Mbeya, iliyohusisha wataalamu kutoka Ofisi hiyo pamoja na Watumishi Housing Investments (WHI).

Bw. Allute amesema makazi bora yataongeza ari ya kazi kwa Walimu na kuboresha utoaji wa huduma. Aidha, amewataka Watumishi watakaonufaika na nyumba hizo kuzitunza vizuri mara zitakapokamilika kwa kuwa ni mali za umma na zinazopaswa kudumu ili kuwanufaisha Watumishi wa baadae.

"Serikali inaendelea kuwekeza fedha nyingi katika kuboresha mazingira ya kazi kwa Watumishi wa Umma, hivyo ni wajibu wa kila mnufaika kuhakikisha nyumba hizi zinatunzwa vizuri mara zitakapokamilika na kuanza kutumika ili ziendelee kuhudumia watumishi wa sasa na wa baadae," Bw. Allute amesema

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mipango na Bajeti, kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Julieth Magambo, amesema Serikali inaendelea kuwekeza katika ujenzi wa nyumba za watumishi ili kuhakikisha wanapata mazingira bora, salama na yenye utulivu yatakayowawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

Awali, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ngolela, Bw. Samsoni Anyosisye, ameishukuru Serikali kwa mradi huo, huku akieleza kuwa nyumba zilizopo zimechakaa na hazifai kwa matumizi, hali iliyowalazimu Walimu wengi kuishi mbali na shule.

Naye Mwalimu wa Shule ya Msingi Idweli, Bw. Tejile Mathew, amesema kukamilika kwa nyumba hizo kutaleta motisha ya kazi na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma ya Elimu.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (aliyenyoosha mkono) akitaka ufafanuzi wa jambo  wakati wa ukaguzi wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Shule ya msingi Ngolela iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mipango na Bajeti,Bi Julieth  Magambo wa Ofisi hiyo.

Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya watumishi wa umma wa Shule ya msingi Ngolela, iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoa wa Mbeya.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ngolela, Bw. Samsoni Anyosisye (wanne kutoka kushoto)  akitoa maelezo kwa Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (wa kwanza kutoka kulia) wakati wa ukaguzi wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Shule ya msingi Ngolela iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya

Muonekano wa mbele wa jengo la zamani walilokuwa wakiishi Waalimu wa shule ya msingi Ngolela iliyopo Kyela Mkoani Mbeya kabla ya jengo hilo kuchakaa na kushindwa kutumika kwa makazi

Timu ya wataalamu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watumishi Housing Investment (WHI) ikiwa katika picha ya pamoja na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ngolela, Bw. Samsoni Anyosisye (wanne kutoka kushoto) mara baada ya timu hiyo kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Shule ya msingi Ngolela iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya

Muonekano wa nyuma wa jengo la zamani walilokuwa wakiishi Waalimu wa shule ya msingi Ngolela iliyopo Kyela Mkoani Mbeya kabla ya jengo hilo kuchakaa na kushindwa kutumika kwa makazi

Timu ya wataalamu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watumishi Housing Investment (WHI) wakiwa katika picha ya pamoja na Mwalimu wa Shule ya Msingi Idweli, Bw. Tejile Mathew pamoja na mafundi wanaosimamia mradi huo mara baada ya timu hiyo kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Shule ya msingi Ngolela iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya

Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya watumishi wa umma wa Shule ya msingi Idwelu, iliyopo Wilaya ya Rugwe Mkoa wa Mbeya


 

UZINGATIAJI WA ITIFAKI KATIKA UTUMISHI WA UMMA KUONGEZA UWAJIBIKAJI NA UADILIFU KIUTENDAJI

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Katibu Mkuu ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi ametoa rai kwa Watumishi wa Umma kuzingatia Itifaki katika Utumishi wa Umma ili kuongeza uwajibikaji na uadilifu kiutendaji kwa maslahi mapana ya Taifa.

Bw. Mkomi ameyasema hayo jijini Dodoma wakati akizungumza na watumishi wa ofisi hiyo katika eneo maalum la mafunzo kwa watumishi hao mara baada ya mkufunzi aliyekuwa akitoa mafunzo kuhusu Itifaki kuhitimisha mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa  kwa lengo la kuwajengea uwezo na uelewa wa Itifaki katika Utumishi wa Umma.

Akiwasilisha mada kuhusu Itifaki, Mwezeshaji wa Mafunzo, Mhadhiri wa Diplomasia, kutoka Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim, Bw. Lucas Humo amesema Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora ina majukumu mengi ikiwemo utoaji wa huduma mbalimbali za kiutumishi hivyo, ni muhimu kila mtumishi akajua wajibu wake ili aweze kuwahudumia Viongozi, Watumishi wa Umma na Wananchi kwa kuzingatia Itifaki mbalimbali zitakazosaidia kuonesha taswira nzuri ya ofisi.

Aidha, Bw. Humo amesema, Itifaki inahusisha namna inavyopaswa kuwasiliana, kushirikiana, na kufanya maamuzi kwa njia inayoheshimu sheria na taratibu zilizowekwa.

“Watumishi wa umma wanatakiwa kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia uadilifu na uwazi kwa namna ya kuwasiliana, kushirikiana na kufanya maamuzi hivyo, wakifuata Itifaki na kuzitekeleza kwa ufanisi itaboresha utendaji kazi”, amesema Bw. Humo.

Bw. Humo, amewaasa watumishi hao kutunza taarifa za ofisi, kuzingatia muda wa kazi wakati wa kuingia na kutoka, kuwajali wageni wanapowasilisha masuala yao ya kiutumishi, kuzingatia mavazi wanapokuwa katika eneo la kazi pamoja na kuwatambua wageni wanapofika katika ofisi hiyo kwa vyeo vyao ili kutoa huduma kwa haki na usawa.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akizungumza jambo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi kwa watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Mhadhiri wa Diplomasia, kutoka Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim, Bw. Lucas Humo akifafanua jambo wakati akiwasilisha mada kuhusu Itifaki wakati wa mafunzo kwa watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI yaliyolenga kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma. Wanaomsikiliza ni Wakurugenzi na Watumishi wa ofisi hiyo.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia mada kuhusu Itifaki wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia mada kuhusu Itifaki wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Mhadhiri wa Diplomasia, kutoka Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim, Bw. Lucas Humo (kulia) akionyesha kwa vitendo Itifaki ya kusalimiana wakati wa mafunzo kwa watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI yaliyolenga kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda.


Sehemu ya Wakurugenzi na  Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia mada kuhusu Itifaki wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Mtumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Joyce Atanas akiuliza swali kuhusu Itifaki mara baada ya Mhadhiri wa Diplomasia, Bw. Lucas Humo (hayupo pichani) kuwasilisha mada kuhusu Itifaki mbalimbali katika Utumishi wa Umma wakati wa mafunzo kwa watumishi wa ofisi hiyo yaliyolenga kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma


Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia jambo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.



Sunday, June 28, 2026

TIMU YA WATAALAMU OFISI YA RAIS - UTUMISHI NA WATUMISHI HOUSING INVESTMENTS (WHI) YAFANYA UKAGUZI WA UTEKELEZAJI WA MIRADI RUANGWA NA MASASI.

Timu ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watumishi Housing Investments (WHI) ipo katika ziara ya kukagua miradi ya ujenzi wa nyumba za Watumishi ambapo leo tarehe 28 Juni, 2026 imekagua maendeleo ya mradi wa Ujenzi wa nyumba ya Watumishi 6:1 katika Shule ya Sekondari Samia Suluhu Hassan - Ruangwa, pamoja na mradi wa Ujenzi wa Nyumba ya Watumishi 3:1 katika Kituo cha Afya Mtandi , Masasi-Mtwara


Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Watumishi Housing Investments (WHI) ikijadili jambo, mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Afya Mtandi , Masasi-Mtwara Juni 28, 2026


Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma shule ya sekondari Samia Suluhu Hassan katika Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi


Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma shule ya sekondari Samia Suluhu Hassan katika Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi


Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Watumishi Housing Investments ikiongozwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Patrick Allute ikikagua mradi wa maendeleo wa Ujenzi wa nyumba ya Watumishi 6:1 katika Shule ya Sekondari Samia Suluhu Hassan Wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi

Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Watumishi Housing Investments (WHI) ikijadili jambo, mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Afya Mtandi , Masasi-Mtwara Juni 28, 2026


Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma
katika Kituo cha Afya Mtandi -Mtwara


Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Watumishi Housing Investments (WHI) na baadhi ya Watumishi wa Kituo cha Afya Mtandi –Mtwara, wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya timu hiyo kukagua maendeleo ya mradi wa makazi ya Watumishi wa Kituo hicho Juni 28, 2026


Saturday, June 27, 2026

TIMU YA WATAALAMU OFISI YA RAIS - UTUMISHI NA WATUMISHI HOUSING INVESTMENTS (WHI) YAENDELEA NA UKAGUZI WA UTEKELEZAJI MIRADI

Timu ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watumishi Housing Investments (WHI) imeendelea na ziara ya kukagua miradi ya ujenzi wa nyumba za Watumishi katika Mkoa wa Lindi ambapo leo tarehe 27 Juni, 2026 imekagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba za Watumishi katika Kituo cha Afya Hoteli Tatu, Shule ya Sekondari Matanda, Shule ya Msingi Runyu, Kituo cha Afya Mvuleni na Shule ya Sekondari Mvuleni.


Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma la Kituo cha Afya Hoteli tatu kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, mkoani Lindi


Timu ya wataalamu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ikikagua ubora wa kazi za ujenzi wa nyumba ya watumishi katika Kituo cha Afya Hoteli Tatu, Wilaya ya Kilwa, Mkoani Lindi leo tarehe 27 Juni 2026


Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Patrick Allute (wa tano kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na timu ya wataalamu kutoka Ofisi hiyo na Watumishi Housing Investment mara baada ya kukamilisha ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa nyumba ya Watumishi katika Kituo cha Afya Hoteli Tatu, Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, Mkoani Lindi


Muonekano wa mbele wa jengo la
mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma wa shule ya sekondari Mvuleni kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Patrick Allute (aliyenyoosha mkomo) akijadili jambo na Wataalamu kutoka Ofisi hiyo na Watumishi Housing Investments (WHI) mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa nyumba za Watumishi wa Shule ya Sekondari Mvuleni iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi,Mkoa wa Lindi


Muonekano wa mbele wa jengo la
mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma wa shule ya sekondari Mvuleni kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi

Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma wa Kituo cha Afya Mvuleni kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi.

Muonekano wa ndani wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma wa Kituo cha Afya Mvuleni kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi.

Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Watumishi Housing Investments ikiongozwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Patrick Allute kukagua mradi wa maendeleo wa ujenzi wa Kituo cha Afya Mvuleni kilichopo Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi.


Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma wa Kituo cha Afya Mvuleni kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi


Mhandisi Salum Chanzi kutoka Watumishi Housing Investments (wa nne kutoka kulia) akifafanua jambo wakati wa ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya Mvuleni kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi