Na Mwandishi Wetu, Dodoma
Tarehe 23 Juni, 2026
Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe amezitaka taasisi zote za umma
nchini kuimarisha matumizi ya mifumo ya kidijiti ili kuboresha utoaji wa huduma
kwa Wananchi, kuongeza uwajibikaji na kuimarisha ufanisi katika utumishi wa
umma.
Prof. Shemdoe ametoa kauli
hiyo Juni 23, 2026 jijini Dodoma wakati akimwakilisha Katibu Mkuu Kiongozi,
Balozi Dkt. Moses Kusiluka, katika kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi
wa Umma yaliyofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park.
Alisema, matumizi ya
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) yamekuwa nguzo muhimu katika
kuimarisha utendaji wa Serikali kwa kurahisisha upatikanaji wa huduma, kuongeza
uwazi na kupunguza gharama za utoaji wa huduma kwa wananchi.
Prof. Shemdoe alibainisha
kuwa maadhimisho ya mwaka huu yamehusisha Taasisi 226 za umma zilizotoa huduma
mbalimbali kwa wananchi, zikiwemo huduma za hati za viwanja, vyeti vya
kuzaliwa, vitambulisho vya Taifa, huduma za afya za kibingwa pamoja na huduma
mbalimbali za kiutumishi.
“Utaratibu huu wa kuwaletea
Wananchi huduma karibu nao ni mzuri na unapaswa kuendelezwa kwa kuwa
unarahisisha upatikanaji wa huduma, kuimarisha mawasiliano kati ya Serikali na
Wananchi na kuongeza imani ya wananchi kwa Serikali yao,” alisema Prof.
Shemdoe.
Katika hafla hiyo, Prof.
Shemdoe alizindua mifumo ya GSD na NGAO inayolenga kuboresha utoaji wa huduma
za Serikali na kuimarisha usalama wa mifumo ya kidijiti.
Alieleza kuwa mfumo wa GSD
utawawezesha wananchi kupata huduma mbalimbali za Serikali kupitia dirisha moja
kwa urahisi na kwa wakati, huku mfumo wa NGAO ukiimarisha usalama wa taarifa za
Serikali kwa kutumia teknolojia ya uthibitishaji wa vipengele vingi
(Multi-Factor Authentication).
Aidha, aliielekeza Mamlaka
ya Serikali Mtandao (e-GA) kuendelea kusimamia uunganishaji wa mifumo ya
Serikali ili kuhakikisha Taasisi za Umma zinabadilishana taarifa kwa ufanisi,
kupunguza urudufu wa taarifa na kuongeza tija katika utoaji wa huduma.
Vilevile, Prof. Shemdoe
aliagiza kufanyika kwa tathmini ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa
kipindi cha miaka mitatu iliyopita ili kubaini mafanikio yaliyopatikana,
changamoto zilizojitokeza na kuweka mikakati madhubuti ya kuboresha maadhimisho
yajayo.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu
wa Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, alisema maadhimisho hayo yamelenga
kuimarisha uwajibikaji, uwazi na ubora wa huduma kwa wananchi kupitia matumizi
ya teknolojia za kisasa zinazowezesha utoaji wa huduma kwa haraka na kwa
ufanisi zaidi.
Aliongeza kuwa maadhimisho hayo yameipa Serikali fursa ya kuonesha mafanikio ya uwekezaji uliofanyika katika sekta ya umma, hususan katika matumizi ya TEHAMA ambayo yamechangia kuboresha huduma na kuongeza kuridhika kwa wananchi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe akizungumza na Wananchi
pamoja na Watumishi kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi
wa Umma Juni 23, 2026 kabla ya Waziri huyo kufunga maadhimisho hayo katika
viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma
Watumishi na Wananchi
wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu
(TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe (hayupo pichani) wakati hafla
ya kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Juni 23, 2026
iliyofanyika juni 23, 2026 katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma
Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe (hayupo
pichani) wakati Waziri huyo alipokuwa akizungumza nao katika hafla
ya kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Juni 23, 2026 Jijini
Dodoma
Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe (hayupo
pichani) wakati Waziri huyo alipokuwa akizungumza nao katika hafla
ya kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Juni 23, 2026 Jijini
Dodoma
Watumishi na Wananchi
wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu
(TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe (hayupo pichani) wakati hafla
ya kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Juni 23, 2026
iliyofanyika juni 23, 2026 katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma
Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe (hayupo
pichani) wakati Waziri huyo alipokuwa akizungumza nao katika hafla
ya kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Juni 23, 2026 Jijini
Dodoma
Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe (kushoto) akiteta jambo na Katibu
Mkuu wa Ofisi ya Rais – UTUMISH, Bw. Juma Mkomi, wakati wahafla ya kilele cha
Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Juni 23, 2026 yaliyofanyika katika
viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais
– UTUMISH, Bw. Juma Mkomi, akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe kufunga Maadhimisho
ya Wiki ya Utumishi wa Umma Juni 23, 2026 iliyofanyika juni 23, 2026 katika
viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
No comments:
Post a Comment