Timu ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watumishi Housing Investments (WHI) imeendelea na ziara ya kukagua miradi ya ujenzi wa nyumba za Watumishi katika Mkoa wa Lindi ambapo leo tarehe 27 Juni, 2026 imekagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba za Watumishi katika Kituo cha Afya Hoteli Tatu, Shule ya Sekondari Matanda, Shule ya Msingi Runyu, Kituo cha Afya Mvuleni na Shule ya Sekondari Mvuleni.
Timu ya wataalamu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ikikagua ubora wa kazi
za ujenzi wa nyumba ya watumishi katika Kituo cha Afya Hoteli Tatu, Wilaya ya
Kilwa, Mkoani Lindi leo tarehe 27 Juni 2026
Mkurugenzi
wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw.
Patrick Allute (aliyenyoosha mkomo) akijadili jambo na Wataalamu kutoka Ofisi
hiyo na Watumishi Housing Investments (WHI) mara baada ya kukagua utekelezaji
wa mradi wa ujenzi wa nyumba za Watumishi wa Shule ya Sekondari Mvuleni iliyopo
katika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi,Mkoa wa Lindi
Muonekano wa mbele wa jengo la mradi
wa makazi ya Watumishi wa Umma wa
Kituo cha Afya Mvuleni kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi.
Muonekano wa ndani wa jengo la mradi
wa makazi ya Watumishi wa Umma wa
Kituo cha Afya Mvuleni kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi.
Timu ya wataalam
kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Watumishi Housing Investments ikiongozwa na Mkurugenzi
wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Patrick Allute kukagua mradi wa
maendeleo wa ujenzi wa Kituo cha Afya Mvuleni kilichopo Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi.
Mhandisi Salum Chanzi kutoka Watumishi Housing Investments (wa nne kutoka kulia) akifafanua jambo wakati wa ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya Mvuleni kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi

.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)



No comments:
Post a Comment