Na
Mwandishi Wetu - Dodoma
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amezitaka Taasisi
zote za Umma kuhakikisha zinatumia mifumo katika kuwahudumia wananchi kwa lengo
la kurahisisha utoaji wa huduma bora, urahisi na haraka.
Mhe. Simbachawene ametoa kauli hiyo leo wakati
wa akifungua Wiki ya Utumishi wa Umma 2025 yenye kaulimbiu ya "Himiza
matumizi ya mifumo ya kidijiti ili kuongeza upatikanaji wa taarifa na kuchagiza
uwajibikaji"
Amesema Serikali imejenga mifumo mingi
ikiwemo wa kufuatilia utendaji kazi wa watumishi ambao umeondoa ubabaishaji.
Kadhalika, Waziri Simbachawene amewataka
wananchi kutumia mfumo wa e-malalamiko na e-mrejesho ili kuweza kuainisha
changamoto ambazo Serikali itazifanyia kazi kwa wakati na kuboresha utoaji wa
huduma.
"Nizielekeze Taasisi zote za Umma
kutumia mifumo iliyojengwa ili kurahisisha utoaji wa huduma bora, kwa haraka na
kwa urahisi."
Kwa upande wake Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw.
Juma Mkomi amesema Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma imeshirikisha Wizara
23, Mikoa 5, Halmashauri 3 na taasisi za umma 101 zimeshiriki.
Amesema kupitia maadhimisho hayo wananchi
wanapata fursa ya kuhudumiwa moja kwa moja, kufahamu majukumu ya Taasisi na Wizara
kupata mrejesho ili kuboresha utoaji wa huduma.
Katika hatua nyingine, Bw. Mkomi ametoa wito
kwa wananchi, watumishi wa umma na wadau mbalimbali kuendelea kutembelea katika
Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma ambapo Maadhimisho hayo yataendelea
hadi Juni 27 mwaka huu.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza na
watumishi mbalimbali wa Serikali pamoja na wananchi walioshiriki kwenye Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa
yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.
Sehemu ya Wananchi na Watumishi wa Umma, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene
(hayupo pichani) wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa
yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi
(aliyeshika kipaza sauti) akifafanua jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene baada ya kuwasili katika banda la ofisi yake wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi
akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George
Simbachawene kuzungumza na Wananchi
na Watumishi
mbalimbali walioshiriki kwenye Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George
Simbachawene wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa
yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiteta jambo na
Katibu Mkuu wa ofisi yake Bw. Juma Mkomi wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa
yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali
Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (aliyekaa kulia) akimsikiliza Afisa TEHAMA wa
ofisi hiyo, Bw. Selemani Sultan alipokuwa akielezea huduma zinazotolewa kwa
kutumia mifumo mbalimbali wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa
yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali
Jijini Dodoma. Aliyekaa
kushoto ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Juma Mkomi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (wa kwanza kulia)
akitazama namna ya kujisajili kwenye mfumo wa PSSSF alipotembelea banda la ofisi
hiyo wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa
yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali
Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwa katika picha ya
pamoja na Wakurugenzi wa ofisi yake mara baada ya Ufunguzi
wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa
yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali
Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (aliyevaa kaunda suti
nyeusi) akitazama moja ya kifaa cha moyo kwenye banda la Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) alipotembelea banda hilo wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa
yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali
Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwa kwenye picha ya pamoja na wawakilishi wa Wizara na
Taasisi mbalimbali
mara baada ya Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya
Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali
Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akisaini kitabu cha
wageni baada ya kutembelea banda la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa
yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwa katika picha ya
pamoja na Wakurugenzi Wasaidizi wa ofisi yake mara baada ya Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa
yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali
Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene (kulia) akisisitiza
jambo wakati akizungumza na watumishi wa Bohari Kuu ya Dawa alipotembelea banda
la ofisi hiyo wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa
yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali
Jijini Dodoma.
Kwaya ya TAKUKURU ikitumbuiza wakati wa ufunguzi wa
Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2025 ambayo kitaifa
yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.