Monday, June 30, 2025

KATIBU MKUU MKOMI AWAASA WATUMISHI WA OFISI YAKE KUJITATHMINI WANAPOTOA HUDUMA KWA UMMA

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi amewaasa watumishi wa ofisi hiyo kujitathmini wanapotoa huduma za kiutumishi kwa Watumishi wa Umma kutoka katika taasisi mbalimbali pamoja na wananchi kwa ujumla

Bw. Mkomi ameyasema hayo wakati akizungumza na watumishi wa ofisi yake, ikiwa ni muendelezo wa mafunzo kwa watumishi hao ambayo hufanyika kila siku ya Jumatatu Mtumba Jijini Dodoma.

“Ofisi yetu inatoa huduma mbalimbali za kiutumishi, ninawaasa mjitathmini kwa namna mnavyotoa huduma kwa Watumishi wa Umma, wadau na wananchi ili tupate mrejesho mzuri kutoka kwao na hatimaye kufikia malengo ya Serikali katika kutoa huduma bora kwa kila Mtanzania.” amesema Bw. Mkomi.

Kwa upande wake Mwezeshaji wa mafunzo Balozi Mhe. Omar Kashera amewataka watumishi hao kutanguliza mbele uzalendo kwa kujenga taswira nzuri ya ofisi hiyo huku akiwataka kufanya maamuzi sahihi pindi wanapowahudumia wateja.

‘’Ili mtoe maamuzi sahihi ni vizuri mkafikiri kwa kina, muwashirikishe watumishi mnaofanya nao kazi ili kupata maamuzi jumuishi yatakayokuwa sahihi kwa maslahi ya Taifa’’ ameongeza Balozi Mhe. Omar Kashera

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akizungumza wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo ya kujengewa uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (aliyesimama kulia) akiteta jambo na Mwezeshaji wa mafunzo Balozi Mhe. Omar Kashera (aliyesimama kushoto) baada ya kuhitimishwa kwa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi, Wakurugenzi Wasaidizi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifurahia jambo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Mwezeshaji wa mafunzo Balozi Mhe. Omar Kashera (aliyesimama) akisisitiza jambo alipokuwa akiwasilisha mada wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


 

No comments:

Post a Comment