Tuesday, June 17, 2025

WAZIRI SIMBACHAWENE AZITAKA TAASISI ZA UMMA KUTUMIA MIFUMO YA KIDIJITI KURAHISISHA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANANCHI

Na Mwandishi Wetu - Dodoma 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amezitaka Taasisi zote za Umma kuhakikisha zinatumia mifumo katika kuwahudumia wananchi kwa lengo la kurahisisha utoaji wa huduma bora, urahisi na haraka. 

Mhe. Simbachawene ametoa kauli hiyo leo wakati wa akifungua Wiki ya Utumishi wa Umma 2025 yenye kaulimbiu ya "Himiza matumizi ya mifumo ya kidijiti ili kuongeza upatikanaji wa taarifa na kuchagiza uwajibikaji" 

Amesema Serikali imejenga mifumo mingi ikiwemo wa kufuatilia utendaji kazi wa watumishi ambao umeondoa ubabaishaji.

Kadhalika, Waziri Simbachawene amewataka wananchi kutumia mfumo wa e-malalamiko na e-mrejesho ili kuweza kuainisha changamoto ambazo Serikali itazifanyia kazi kwa wakati na kuboresha utoaji wa huduma.

"Nizielekeze Taasisi zote za Umma kutumia mifumo iliyojengwa ili kurahisisha utoaji wa huduma bora, kwa haraka na kwa urahisi."

Kwa upande wake Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi amesema Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma imeshirikisha Wizara 23, Mikoa 5, Halmashauri 3 na taasisi za umma 101 zimeshiriki.

Amesema kupitia maadhimisho hayo wananchi wanapata fursa ya kuhudumiwa moja kwa moja, kufahamu majukumu ya Taasisi na Wizara kupata mrejesho ili kuboresha utoaji wa huduma.

Katika hatua nyingine, Bw. Mkomi ametoa wito kwa wananchi, watumishi wa umma na wadau mbalimbali kuendelea kutembelea katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma ambapo Maadhimisho hayo yataendelea hadi Juni 27 mwaka huu.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza na watumishi mbalimbali wa Serikali pamoja na wananchi walioshiriki kwenye Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.


Sehemu ya Wananchi na Watumishi wa Umma, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (aliyeshika kipaza sauti) akifafanua jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene baada ya kuwasili katika banda la ofisi yake wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kuzungumza na Wananchi na Watumishi mbalimbali walioshiriki kwenye Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiteta jambo na Katibu Mkuu wa ofisi yake Bw. Juma Mkomi wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (aliyekaa kulia) akimsikiliza Afisa TEHAMA wa ofisi hiyo, Bw. Selemani Sultan alipokuwa akielezea huduma zinazotolewa kwa kutumia mifumo mbalimbali wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma. Aliyekaa kushoto ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Juma Mkomi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (wa kwanza kulia) akitazama namna ya kujisajili kwenye mfumo wa PSSSF alipotembelea banda la ofisi hiyo wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi wa ofisi yake mara baada ya Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (aliyevaa kaunda suti nyeusi) akitazama moja ya kifaa cha moyo kwenye banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alipotembelea banda hilo wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwa kwenye picha ya pamoja na wawakilishi wa Wizara na Taasisi mbalimbali mara baada ya Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akisaini kitabu cha wageni baada ya kutembelea banda la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi Wasaidizi wa ofisi yake mara baada ya Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene (kulia) akisisitiza jambo wakati akizungumza na watumishi wa Bohari Kuu ya Dawa alipotembelea banda la ofisi hiyo wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.

Kwaya ya TAKUKURU ikitumbuiza wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2025 ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma.


No comments:

Post a Comment