Thursday, September 27, 2018

MHE. MKUCHIKA ASHUHUDIA MAFANIKIO YA WANUFAIKA WA TASAF KATA YA MUHUNGA WILAYANI KASULU



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) akizungumza na wananchi na wanufaika wa TASAF kata ya Muhunga wilayani Kasulu, alipowatembelea ili kujionea utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini nchini.

Baadhi ya wanakijiji na wanufaika wa TASAF wa kata ya Muhunga wilayani Kasulu wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) (hayupo pichani) alipoitembelea kata hiyo ili kujionea utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini nchini.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) na Mbunge wa Kasulu Mjini (CCM), Mhe. Daniel Nsanzugwanko (Mb) wakiwa katika picha ya pamoja na Bi. Monica Jackson Mavuli mnufaika wa TASAF kata ya Muhunga wilayani Kasulu mbele ya nyumba ya mnufaika huyo iliyojengwa kwa fedha za ruzuku ya Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini nchini.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) akiwa na mmoja wa wanufaika wa TASAF kata ya Muhunga wilayani Kasulu mbele ya nyumba ya mnufaika huyo iliyojengwa kwa fedha za ruzuku ya Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini nchini.

Tuesday, September 25, 2018

WANUFAIKA WA TASAF KIJIJI CHA KITAGATA WAPONGEZWA KWA KUBORESHA MAISHA YAO NA KUTOA RAMBIRAMBI KWA WAHANGA WA AJALI YA KIVUKO CHA MV. NYERERE




Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) akizungumza na wananchi na wanufaika wa TASAF, kijiji cha Kitagata Wilayani Kasulu alipowatembelea ili kujionea utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini nchini.

Baadhi ya wanakijiji na wanufaika wa TASAF wa kijiji cha Kitagata Wilayani Kasulu wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) (hayupo pichani) alipotembelea kijiji hicho ili kujionea utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini nchini.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na watoto wa kijiji cha Kitagata Wilayani Kasulu ambao ni watoto wa mnufaika wa TASAF  alipokitembelea kijiji hicho ili kujionea utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini nchini.

Sunday, September 23, 2018

MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI ULIBUNIWA NA SERIKALI KWA LENGO LA KUPAMBANA NA UMASKINI NCHINI



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) akizungumza na wananchi na wanufaika wa TASAF, Kata ya Lusimbi, Manispaa ya Kigoma Ujiji alipowatembelea ili kujionea utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini nchini.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanufaika wa TASAF, Kata ya Lusimbi iliyopo Manispaa ya Kigoma Ujiji mara baada kuwatembelea wanufaika hao kwa lengo la kujionea utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini nchini.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na wanufaika wa TASAF mbele ya nyumba ya mganga wa zahanati iliyopo Kata ya Lusimbi, Kigoma Ujiji iliyojengwa kwa mchango wa wananchi na TASAF.