Wednesday, April 24, 2024

BIDII, WELEDI NA UADILIFU WAIBUA MFANYAKAZI HODARI OFISI YA RAIS-UTUMISHI

 Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 24 Aprili, 2024.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Sheria, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bibi Hilda Kabissa amewasisitiza watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kufanya kazi kwa bidii, weledi na uadilifu huku wakizingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za Utumishi wa Umma katika kuwahudumia wananchi kwa ustawi wa taifa.

Mkurugenzi Kabissa ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakati wa kikao kazi cha Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi na watumishi hao kilicholenga kuzungumzia masuala ya kiutumishi na kumchagua mfanyakazi hodari wa Ofisi hiyo.

Bibi Kabissa amesema watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wanapaswa kuwa mfano bora kwa wengine katika kuzingatia maadili wakati wa utekelezaji wa majukumu yao wakiwa ofisini na hata nje ya ofisi.

Awali akiongoza kikao kazi chake na watumishi wa Ofisi yake kabla ya kuendelea na majukumu mengine ya kitaifa, Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi aliwasisitiza watumishi wa ofisi yake kumchagua mfanyakazi hodari kwa kuzingatia vigezo vya mfanyakazi hodari vilivyowekwa na sio kupendeleana.

Kwa upande wake Afisa Utumishi Bw. Juma Ijumaa ambaye ndiye alichaguliwa kuwa mfanyakazi hodari wa ofisi hiyo, amewashukuru viongozi na watendaji wa ofisi hiyo kwa kuwaongoza watumishi wote katika kusimamia maadili, kufanya kazi kwa bidii na weledi katika kulitumikia taifa jambo ambalo limemfanya kuwa mfanyakazi hodari wa ofisi hiyo.

Aidha Bw. Ijumaa amewashukuru wafanyakazi wenzake kwa kumpa ushindi wa kwanza kwa kishindo na kuahidi kuendelea kutoa huduma bora kwa watumishi wa umma na wananchi wanaofuata huduma katika Ofisi ya Rais-UTUMISHI akiamini kuwa kitendo hicho kitaendelea kujenga taswira nzuri zaidi ya ofisi pamoja na kutimiza azma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuboresha huduma bora kwa wananchi.

Kwa upande wake, mtumishi aliyeshika nafasi ya pili, Bi. Joyce Atanas ameahidi kuendelea kuwa mwadilifu na mchapa kazi katika kipindi chote cha utumishi wake ili kuchochea maendeleo ya taifa.

Naye, Bw. Elias Mwandu, aliyeshika nafasi ya tatu, hakusita kuwashukuru watumishi wenzake kwa kumchagua kuwa miongoni mwa tatu bora wa Ofisi hiyo na kuongeza kuwa, kitendo hicho hakimaanishi kuwa wao si watumishi bora kiutendaji kwani amekuwa akishirikiana nao katika kuwahudumia wananchi na watumishi wa umma nchini.

Akihitimisha kikao kazi hicho, Mkurugenzi Kabissa, amewahamasisha watumishi wote wa ofisi hiyo ambao hawakubahatika kuchaguliwa kwa mwaka huu wa 2024, kujipanga kwa mwaka utakaofuata kwani anaamini utendajikazi mzuri wa kila mtumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI.

 


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akizungumza na watumishi wa ofisi yake wakati wa kikao kazi chake na watumishi wa ofisi hiyo kilicholenga kuzungumzia masuala ya kiutumishi na kuchagua Mfanyakazi Hodari kwa mwaka 2024 kilichofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati akizungumza nao kuhusu masuala ya kiutumishi na kuchagua Mfanyakazi Hodari wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024 kilichofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati akizungumza nao kuhusu masuala ya kiutumishi na kuchagua Mfanyakazi Hodari wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024 kilichofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Mussa Magufuli akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) kuzungumza na watumishi kuhusu masuala ya kiutumishi na kuchagua Mfanyakazi Hodari wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024 kilichofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Sheria, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bibi Hilda Kabissa akimtangaza mfanyakazi hodari aliyechaguliwa na watumishi wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024.

Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati akizungumza nao kuhusu masuala ya kiutumishi na kuchagua Mfanyakazi Hodari wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024 kilichofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Wafanyakazi hodari wa Idara na Vitengo wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI (mstari wa kwanza) wakiwa katika kikao kazi kilichohusu masuala ya kiutumishi na kuchagua Mfanyakazi Hodari wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024 kilichofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Mtumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Evarist Venant, akichangia hoja wakati wa kikao kazi kilichohusu masuala ya kiutumishi na kuchagua Mfanyakazi Hodari wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024 kilichofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Mussa Magufuli (hayupo pichani) kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) kuzungumza na watumishi hao kwenye kikao kazi kilichohusu masuala ya kiutumishi na kuchagua Mfanyakazi Hodari wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024 kilichofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Mfanyakazi Hodari wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma Ijumaa akitoa neno la shukrani kwa watumishi wa ofisi hiyo, mara baada ya kuchaguliwa kuwa mfanyakazi bora kwa mwaka 2024.

Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakikamilisha zoezi la kupiga kura kumchagua mfanyakazi Hodari wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024.


Wakurugenzi wasaidizi na wawakilishi wa wafanyakazi bora kutoka katika Idara na Vitengo, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakishuhudia zoezi la kuhesabu kura za kumpata mfanyakazi Hodari wa ofisi yake kwa mwaka 2024.








Friday, April 19, 2024

BUNGENI LEO











 

BAJETI YA OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25 YAPITISHWA NA BUNGE



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya ofisi yake kwa Mwaka wa Fedha 2024/25 Bungeni jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene (kushoto) akijadili jambo na Naibu Waziri wake, Mhe. Ridhiwani Kikwete mara baada ya kuwasilisha Hotuba ya Bajeti ya ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2024/25 Bungeni jijini Dodoma.



Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akisalimia Bunge wakati akitambulishwa Bungeni jijini Dodoma kabla ya kuwasilishwa kwa Hotuba ya Bajeti ya ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2024/25.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akisalimia Bunge wakati akitambulishwa Bungeni jijini Dodoma kabla ya kuwasilishwa kwa Hotuba ya Bajeti ya ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2024/25.


Baadhi ya Watendaji na Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia Hotuba ya Bajeti ya ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2024/25 Bungeni jijini Dodoma.


Baadhi ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zilizopo chini ya Ofisi hiyo wakifuatilia Hotuba ya Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2024/25 Bungeni jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Idara ya Mipango, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cosmas Ngangaji (Wakwanza kushoto) akifuatilia Hotuba ya Bajeti ya Ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2024/25 Bungeni jijini Dodoma.



BAJETI YA OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA 2024/25 YAWASILISHWA

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwasili Bungeni tayari kuwasilisha Hotuba ya Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2024/25.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akisalimiana na Katibu Mkuu-IKULU, Bw. Mululi Majula Mahendeka wakati akiwasili Bungeni tayari kuwasilisha Hotuba ya Bajeti ya ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2024/25.



Monday, April 15, 2024

MFUMO WA AJIRA WADUMISHA MUUNGANO WA TANZANIA


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kipindi cha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanikiwa kuweka utaratibu wa mgao wa ajira unaotekelezwa kwa mujibu wa Waraka wa Serikali wa tarehe 10 Mei, 2013 ambapo Tanzania Bara ni asilimia 79 na Tanzania Zanzibar ni asilimia 21.

 

Ameyasema hayo leo Aprili 15, 2024 jijini Dodoma, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya miaka 60 ya Muungano kwa upande wa Ofisi yake.

 Amesema katika kipindi hicho cha miaka 60 ya Muungano, Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imekuwa ikifanya kazi kwa ukaribu na Tume ya Utumishi wa Umma Zanzibar inayoratibu masuala ya ajira katika watumishi wa umma ili kurahisisha zoezi la utangazaji wa nafasi za kazi na upatikanaji wa watumishi.

 Kutokana na ukuaji wa teknolojia, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imesanifu na kujenga mfumo wa kidijitali wa ajira Serikalini ambao ni rafiki kwa watafuta fursa wote katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 Aidha, Mhe. Simbachawene ameongeza kuwa utengenezaji wa programu ya rununu (Ajira Portal Mobile App) inayopatikana kwenye PlayStore na ApStore za simu janja inalenga kuimarisha Muungano kwa kuwarahisishia waombaji wa fursa za ajira kupata taarifa za uwepo wa fursa hizo kiganjani mwao mahali popote.

 Katika hatua nyingine Mhe. Simbachawene amesema Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kupitia Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imedhamiria kuondoa changamoto zinazowakabili waombaji wa fursa za ajira Tanzania Bara na Zanzibar.

 

Aidha, matumizi ya mifumo ya TEHAMA katika kipindi hiki cha miaka 60 ya Muungano imesaidia waombaji kuepuka gharama za usafiri, malazi na changamoto za ajali, wakati Serikali imepunguza muda wa usaili na gharama za uendeshaji wa zoezi hilo.

 

Mhe. Simbachawene amewataka watafuta fursa za ajira wote kutoka pande mbili za Muungano kufahamu akaunti zao, nywila na kuwa mahiri katika matumizi ya kompyuta ili kuepukana na usumbufu.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza kwenye  Mkutano na  Waandishi wa Habari kuhusu mafanikio ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanzania kwenye eneo la Utumishi wa Umma na Utawala bora leo Jijini Dodoma.  

Sehemu ya Waandishi wa Habari wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene wakati  akizungumza kuhusu mafanikio ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanzania kwenye eneo la Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari Maelezo, Bi. Zamaradi Kawawa akitoa neon la utangulizi kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kuzungumza na Waandishi wa Habari  kuhusu mafanikio ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanzania kwenye eneo la Utumishi wa Umma na Utawala bora leo Jijini Dodoma.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (katikati) akiwa na baadhi ya Wakurugenzi baada ya kuzungumza na   Waandishi wa Habari kuhusu mafanikio ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanzania kwenye eneo la Utumishi wa Umma na Utawala bora, wa kwanza kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Mary Mwakapenda

Baadhi ya Watumishi kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wakimsiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene wakati akizungumza na  Waandishi wa Habari kuhusu mafanikio ya Miaka 60 ya Muungano kwenye eneo la Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

 

Friday, April 12, 2024

KUMBUKIZI YA MIAKA 40 YA ALIYEKUWA WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HAYATI EDWARD MORINGE SOKOINE

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi na wananchi katika Kijiji cha Monduli Juu, Wilayani Monduli wakati wa Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, Hayati Edward Moringe Sokoine.

Sehemu ya viongozi na wananchi wakisikiliza hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Ibada maalaum ya kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, Hayati Edward Moringe Sokoine iliyofanyika Kijiji cha Monduli Juu, Wilaya ya Monduli

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akitoa maelezo ya awali kuhusu Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, Hayati Edward Moringe Sokoine kabla ya kumkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuzungumza katika Ibada hiyo iliyofanyika katika Kijiji cha Monduli Juu, Wilaya ya Monduli.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene (kulia) akizungumza jambo na Naibu Waziri wa Ofisi yake, Mhe. Ridhiwani Kikwete kabla ya kuanza kwa Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, Hayati Edward Moringe Sokoine iliyofanyika Kijiji cha Monduli Juu, Wilaya ya Monduli.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akitoa utambulisho wa baadhi ya viongozi na wageni walioshiriki katika Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, Hayati Edward Moringe Sokoine kabla ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuzungumza na viongozi na wananchi katika Ibada hiyo iliyofanyika Kijiji cha Monduli Juu, Wilaya ya Monduli.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akisaini kitabu mara baada ya kuweka shada la maua kwenye kaburi la aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, Hayati Edward Moringe Sokoine katika Kijiji cha Monduli Juu, Wilaya ya Monduli.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (kushoto) akifurahia jambo na Mkurugenzi wa Idara ya  Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bw. Musa Magufuli pamoja na Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala na Dawati la Viongozi Wakuu wa Kitaifa Wastaafu, Bi. Nyasinde Mukono (katikati) kabla ya kuanza kwa Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha Waziri Mkuu huyo iliyofanyika katika Kijiji cha Monduli Juu, Wilaya ya Monduli.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwasili nyumbani kwa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, Hayati Edward Moringe Sokoine wakati wa Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha Waziri Mkuu huyo iliyofanyika katika Kijiji cha Monduli Juu, Wilaya ya Monduli.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na baadhi ya viongozi kabla ya kuanza kwa Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, Hayati Edward Moringe Sokoine iliyofanyika Kijiji cha Monduli Juu, Wilaya ya Monduli.

Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia jambo kabla ya kuanza kwa Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, Hayati Edward Moringe Sokoine iliyofanyika katika Kijiji cha Monduli Juu, Wilaya ya Monduli.