Friday, April 26, 2024
Wednesday, April 24, 2024
BIDII, WELEDI NA UADILIFU WAIBUA MFANYAKAZI HODARI OFISI YA RAIS-UTUMISHI
Na. Veronica Mwafisi-Dodoma
Tarehe 24 Aprili, 2024.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za
Sheria, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bibi Hilda Kabissa amewasisitiza watumishi wa
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kufanya kazi kwa
bidii, weledi na uadilifu huku wakizingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za
Utumishi wa Umma katika kuwahudumia wananchi kwa ustawi wa taifa.
Mkurugenzi Kabissa ameyasema hayo
leo alipokuwa akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI
wakati wa kikao kazi cha Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi na watumishi hao
kilicholenga kuzungumzia masuala ya kiutumishi na kumchagua mfanyakazi hodari
wa Ofisi hiyo.
Bibi Kabissa amesema watumishi wa
Ofisi ya Rais-UTUMISHI wanapaswa kuwa mfano bora kwa wengine katika kuzingatia
maadili wakati wa utekelezaji wa majukumu yao wakiwa ofisini na hata nje ya
ofisi.
Awali akiongoza kikao kazi chake na
watumishi wa Ofisi yake kabla ya kuendelea na majukumu mengine ya kitaifa,
Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi aliwasisitiza watumishi wa ofisi yake
kumchagua mfanyakazi hodari kwa kuzingatia vigezo vya mfanyakazi hodari
vilivyowekwa na sio kupendeleana.
Kwa upande wake Afisa Utumishi Bw.
Juma Ijumaa ambaye ndiye alichaguliwa kuwa mfanyakazi hodari wa ofisi hiyo, amewashukuru
viongozi na watendaji wa ofisi hiyo kwa kuwaongoza watumishi wote katika kusimamia
maadili, kufanya kazi kwa bidii na weledi katika kulitumikia taifa jambo ambalo
limemfanya kuwa mfanyakazi hodari wa ofisi hiyo.
Aidha Bw. Ijumaa amewashukuru
wafanyakazi wenzake kwa kumpa ushindi wa kwanza kwa kishindo na kuahidi kuendelea kutoa huduma bora kwa watumishi wa umma na wananchi wanaofuata huduma katika Ofisi ya
Rais-UTUMISHI akiamini kuwa kitendo hicho kitaendelea kujenga taswira nzuri zaidi
ya ofisi pamoja na kutimiza azma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.
Samia Suluhu Hassan ya kuboresha huduma bora kwa wananchi.
Kwa upande wake, mtumishi aliyeshika nafasi ya pili, Bi. Joyce Atanas ameahidi kuendelea kuwa mwadilifu na mchapa kazi katika
kipindi chote cha utumishi wake ili kuchochea maendeleo ya taifa.
Naye, Bw. Elias Mwandu, aliyeshika
nafasi ya tatu, hakusita kuwashukuru watumishi wenzake kwa kumchagua kuwa miongoni mwa tatu bora wa Ofisi hiyo na kuongeza kuwa, kitendo hicho
hakimaanishi kuwa wao si watumishi bora kiutendaji kwani amekuwa akishirikiana
nao katika kuwahudumia wananchi na watumishi wa umma nchini.
Akihitimisha kikao kazi hicho, Mkurugenzi Kabissa, amewahamasisha watumishi wote wa ofisi
hiyo ambao hawakubahatika kuchaguliwa kwa mwaka huu wa 2024, kujipanga kwa mwaka utakaofuata kwani
anaamini utendajikazi mzuri wa kila mtumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akizungumza na watumishi wa ofisi yake wakati wa kikao kazi chake na watumishi wa ofisi hiyo kilicholenga kuzungumzia masuala ya kiutumishi na kuchagua Mfanyakazi Hodari kwa mwaka 2024 kilichofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati akizungumza nao kuhusu masuala ya kiutumishi na kuchagua Mfanyakazi Hodari wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024 kilichofanyika
katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (hayupo
pichani) wakati akizungumza nao
kuhusu masuala ya kiutumishi na kuchagua Mfanyakazi Hodari wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024 kilichofanyika
katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Mussa Magufuli akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Katibu
Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) kuzungumza na watumishi kuhusu
masuala
ya kiutumishi na kuchagua Mfanyakazi Hodari wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024 kilichofanyika
katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Kitengo
cha Huduma za Sheria, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Bibi Hilda Kabissa akimtangaza mfanyakazi hodari aliyechaguliwa na
watumishi wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024.
Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati akizungumza nao kuhusu masuala ya kiutumishi na kuchagua Mfanyakazi Hodari wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024 kilichofanyika
katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Wafanyakazi hodari
wa Idara na Vitengo wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI (mstari wa kwanza) wakiwa katika kikao kazi kilichohusu masuala ya kiutumishi na kuchagua Mfanyakazi Hodari wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024 kilichofanyika
katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Mtumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI,
Bw. Evarist Venant, akichangia hoja wakati wa kikao kazi kilichohusu masuala ya kiutumishi na kuchagua Mfanyakazi Hodari wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024 kilichofanyika
katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Baadhi ya watumishi wa Ofisi
ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa
Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
Bw. Mussa Magufuli (hayupo pichani) kabla ya
kumkaribisha Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani)
kuzungumza na watumishi hao kwenye kikao kazi kilichohusu masuala ya kiutumishi na kuchagua Mfanyakazi Hodari wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024 kilichofanyika katika Mji wa Serikali
Mtumba, jijini Dodoma.
Mfanyakazi Hodari wa Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma
Ijumaa akitoa neno la shukrani kwa watumishi wa ofisi hiyo, mara baada ya kuchaguliwa kuwa
mfanyakazi bora kwa mwaka 2024.
Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakikamilisha zoezi la kupiga kura kumchagua mfanyakazi Hodari wa ofisi hiyo kwa mwaka 2024.
Wakurugenzi
wasaidizi na wawakilishi wa wafanyakazi bora kutoka katika Idara na Vitengo, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakishuhudia zoezi la kuhesabu
kura za kumpata mfanyakazi Hodari wa ofisi yake kwa mwaka 2024.
Friday, April 19, 2024
BAJETI YA OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25 YAPITISHWA NA BUNGE
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya ofisi yake kwa Mwaka wa
Fedha 2024/25 Bungeni jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene (kushoto) akijadili
jambo na Naibu Waziri wake, Mhe. Ridhiwani Kikwete mara baada ya kuwasilisha
Hotuba ya Bajeti ya ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2024/25 Bungeni jijini Dodoma.
Katibu Mkuu-IKULU, Bw. Mululi Majula
Mahendeka akisalimia
Bunge wakati akitambulishwa Bungeni jijini Dodoma kabla
ya kuwasilishwa kwa Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2024/25.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma,
Bw. Juma Mkomi akisalimia Bunge wakati akitambulishwa Bungeni jijini Dodoma kabla
ya kuwasilishwa kwa Hotuba ya Bajeti ya ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2024/25.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi
akisalimia Bunge wakati akitambulishwa Bungeni jijini Dodoma kabla
ya kuwasilishwa kwa Hotuba ya Bajeti ya ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2024/25.
Baadhi ya Watendaji na Wakurugenzi
wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia Hotuba
ya Bajeti ya ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2024/25 Bungeni
jijini Dodoma.
Baadhi ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
na Utawala Bora na taasisi zilizopo chini ya Ofisi
hiyo wakifuatilia Hotuba ya Bajeti kwa Mwaka wa Fedha
2024/25 Bungeni jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Idara ya
Mipango, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cosmas Ngangaji (Wakwanza kushoto) akifuatilia
Hotuba ya Bajeti ya Ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2024/25 Bungeni jijini
Dodoma.
BAJETI YA OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA 2024/25 YAWASILISHWA
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwasili Bungeni tayari kuwasilisha Hotuba ya Bajeti kwa
Mwaka wa Fedha 2024/25.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akisalimiana na Katibu
Mkuu-IKULU, Bw. Mululi Majula Mahendeka wakati
akiwasili Bungeni tayari
kuwasilisha Hotuba ya Bajeti ya ofisi hiyo kwa Mwaka wa
Fedha 2024/25.
Monday, April 15, 2024
MFUMO WA AJIRA WADUMISHA MUUNGANO WA TANZANIA
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kipindi cha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanikiwa kuweka utaratibu wa mgao wa ajira unaotekelezwa kwa mujibu wa Waraka wa Serikali wa tarehe 10 Mei, 2013 ambapo Tanzania Bara ni asilimia 79 na Tanzania Zanzibar ni asilimia 21.
Ameyasema hayo leo Aprili 15, 2024 jijini Dodoma, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya miaka 60 ya Muungano kwa upande wa Ofisi yake.
Aidha,
matumizi ya mifumo ya TEHAMA katika kipindi hiki cha miaka 60 ya Muungano imesaidia
waombaji kuepuka gharama za usafiri, malazi na changamoto za ajali, wakati Serikali
imepunguza muda wa usaili na gharama za uendeshaji wa zoezi hilo.
Mhe.
Simbachawene amewataka watafuta fursa za ajira wote kutoka pande mbili za
Muungano kufahamu akaunti zao, nywila na kuwa mahiri katika matumizi ya kompyuta
ili kuepukana na usumbufu.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari Maelezo, Bi. Zamaradi Kawawa akitoa neon la utangulizi kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kuzungumza na Waandishi wa Habari kuhusu mafanikio ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanzania kwenye eneo la Utumishi wa Umma na Utawala bora leo Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (katikati) akiwa na baadhi ya Wakurugenzi baada ya kuzungumza na Waandishi wa Habari kuhusu mafanikio ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanzania kwenye eneo la Utumishi wa Umma na Utawala bora, wa kwanza kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Mary Mwakapenda
Baadhi ya Watumishi kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wakimsiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu mafanikio ya Miaka 60 ya Muungano kwenye eneo la Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
Friday, April 12, 2024
KUMBUKIZI YA MIAKA 40 YA ALIYEKUWA WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HAYATI EDWARD MORINGE SOKOINE
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan akizungumza na viongozi na wananchi katika
Kijiji cha Monduli Juu, Wilayani Monduli wakati wa Ibada maalum ya
kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya
Kwanza, Hayati Edward Moringe Sokoine.
Sehemu ya viongozi na wananchi wakisikiliza hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan wakati wa Ibada maalaum ya kumbukizi ya miaka 40
ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, Hayati Edward
Moringe Sokoine iliyofanyika Kijiji cha Monduli Juu, Wilaya ya Monduli.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akitoa maelezo ya awali kuhusu Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, Hayati Edward Moringe Sokoine kabla ya kumkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuzungumza katika Ibada hiyo iliyofanyika katika Kijiji cha Monduli Juu, Wilaya ya Monduli.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene (kulia) akizungumza
jambo na Naibu Waziri wa Ofisi yake, Mhe. Ridhiwani
Kikwete kabla ya kuanza kwa Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha
aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, Hayati Edward Moringe
Sokoine iliyofanyika Kijiji cha Monduli Juu, Wilaya ya Monduli.
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akitoa utambulisho wa
baadhi ya viongozi na wageni walioshiriki katika Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa
Serikali ya Awamu ya Kwanza, Hayati Edward Moringe Sokoine kabla ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan kuzungumza na viongozi na
wananchi katika Ibada hiyo iliyofanyika Kijiji cha
Monduli Juu, Wilaya ya Monduli.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akisaini kitabu mara
baada ya kuweka shada la maua kwenye kaburi la aliyekuwa Waziri Mkuu wa
Serikali ya Awamu ya Kwanza, Hayati Edward Moringe Sokoine katika Kijiji cha
Monduli Juu, Wilaya ya Monduli.
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (kushoto) akifurahia
jambo na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala
na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bw. Musa Magufuli pamoja na Mkurugenzi Msaidizi
wa Utawala na Dawati la Viongozi Wakuu wa Kitaifa Wastaafu, Bi. Nyasinde Mukono
(katikati) kabla ya kuanza kwa Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka 40 ya kifo
cha Waziri Mkuu huyo iliyofanyika katika Kijiji cha Monduli Juu, Wilaya ya
Monduli.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene akiwasili nyumbani kwa
aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, Hayati Edward Moringe
Sokoine wakati wa Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka 40
ya kifo cha Waziri Mkuu huyo iliyofanyika katika Kijiji cha Monduli Juu, Wilaya
ya Monduli.
Naibu Waziri, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza
na baadhi ya viongozi kabla ya kuanza kwa Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka 40
ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, Hayati Edward
Moringe Sokoine iliyofanyika Kijiji cha Monduli Juu, Wilaya ya Monduli.
Sehemu ya Wakurugenzi
wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia jambo kabla ya kuanza kwa Ibada maalum ya
kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya
Kwanza, Hayati Edward Moringe Sokoine iliyofanyika katika Kijiji cha Monduli
Juu, Wilaya ya Monduli.