Sunday, August 23, 2026

TUZO YA RAIS WA AWAMU YA KWANZA NA MBEBA MAONO WA TAIFA LA TANZANIA, HAYATI MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE

Tuzo ya Rais wa Awamu ya Kwanza na mbeba maono wa Taifa la Tanzania, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kwa kutambua mchango wake katika kuasisi na kuwa na maono ya ujenzi wa Mradi wa Bwawa la Mwalimu Julius Nyerere.

Imepokelewa kwa niaba yake na   Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili.

Tuzo hii ni ishara ya heshima na kutambua mchango wake katika kuasisi maono ya Taifa ya kuwa ba umeme wa uhakika kwa maendeleo ya Tanzania.



TUZO YA RAIS WA AWAMU YA TATU, HAYATI BENJAMIN WILLIAM MKAPA

Tuzo ya Rais wa Awamu ya Tatu, Hayati Benjamin William Mkapa, kwa kutambua, mchango wake katika kuhakikisha utekelezaji wake wa Mradi wa Bwawa la Mwalimu Julius Nyerere.

Imepokelewa kwa niaba yake na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili.

Tuzo hii ni ishara ya heshima na kutambua mchango wake katika kutimiza maono ya Taifa ya kuwa na umeme wa uhakika kwa maendeleo ya Tanzania.



Friday, August 21, 2026

WAZIRI KIKWETE: SERIKALI YAONGEZA TAASISI ZINAZOKAGULIWA KUHUSU UZINGATIAJI WA SHERIA KATIKA UTUMISHI WA UMMA ILI KUIMARISHA UWAJIBIKAJI

Na Lusungu Helela, Morogoro

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, amesema Serikali imeongeza idadi ya taasisi zitakazokaguliwa kuhusu uzingatiaji wa sheria katika usimamizi wa utumishi wa umma kutoka 160 mwaka 2025/26 hadi 300 mwaka 2026/27

Mhe. Kikwete ametoa kauli hiyo leo, Ijumaa, Agosti 21, 2026, mkoani Morogoro, wakati akizungumza na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, mara baada ya kuzindua zoezi la ukaguzi katika halmashauri hiyo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.

Amesema hatua hiyo inaonesha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuimarisha uadilifu, uwajibikaji na utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Amesema ukaguzi huo unafanyika kwa mujibu wa Kifungu cha 12(1)(c) cha Sheria ya Utumishi wa Umma, Sura ya 298, Marejeo ya Mwaka 2023, kwa lengo la kufuatilia na kutathmini kiwango cha uzingatiaji wa sheria, kanuni, taratibu na miongozo katika usimamizi wa masuala ya kiutumishi na kiutawala.

Kwa mujibu wa Mhe. Kikwete, ukaguzi huo utasaidia taasisi kubaini na kurekebisha kasoro za kiutendaji, kuimarisha uwajibikaji, kupunguza migogoro ya kiutumishi na kuongeza ufanisi katika utendaji kazi.

Ameongeza kuwa ukaguzi huo utaiwezesha Serikali kupata taarifa kuhusu hali ya utumishi wa umma nchini na kutoa mapendekezo ya kuboresha sera, sheria na kanuni za utumishi wa umma.

Katika hatua nyingine, Mhe. Kikwete amewataka watumishi wa umma kuzingatia maadili na wajibu wao, huku akiwaagiza waajiri kutoa motisha kwa wanaofanya vizuri na kuchukua hatua stahiki dhidi ya wanaokiuka maadili ya utumishi.

Amesisitiza kuwa rasilimaliwatu ni msingi muhimu wa maendeleo kwa kuwa ndiyo inayosimamia rasilimali nyingine zote, hivyo inapaswa kusimamiwa kwa ufanisi.

Aidha, Mhe. Kikwete amesema Serikali inaendelea kuboresha maslahi ya watumishi wa umma kwa kuzingatia uwezo wa bajeti, ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kwa weledi na ufanisi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma, Jaji Mstaafu Hamisa Kalombola, ameishukuru Serikali kwa kuiwezesha Tume kuendelea kuimarisha shughuli zake, ikiwemo matumizi ya mifumo ya TEHAMA katika kutekeleza majukumu ya ukaguzi.

Amesema matumizi ya teknolojia yamerahisisha kwa kiasi kikubwa kazi ya ukaguzi kwa kuwezesha ukusanyaji, uchambuzi na ufuatiliaji wa taarifa kwa ufanisi zaidi, hivyo kuongeza kasi na ubora wa utekelezaji wa majukumu ya Tume.

Awali, Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda, amesema ukaguzi huo ni muhimu katika kubaini maeneo yenye changamoto na kusaidia waajiri kuchukua hatua za kuboresha usimamizi wa rasilimaliwatu. “Lengo ni kuhakikisha waajiri na watumishi wanatekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu zilizowekwa ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi,” amesema Kipanda.

Ameongeza kuwa zoezi hilo la ukaguzi linafanyika katika mikoa 16 na linatekelezwa na wataalamu wa Tume hiyo anayoiongoza.

Naye, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Bw. Emmanuel Mkongo, amesema halmashauri hiyo itaendelea kushirikiana na Tume ya Utumishi wa Umma kuhakikisha usimamizi wa utumishi unazingatia Sheria na Kanuni zilizopo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro  mara baada ya kuzindua zoezi la ukaguzi katika halmashauri hiyo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na baadhi viongozi  wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na vingozi wa  Tume ya Utumishi wa Umma, mara baada ya kuwasili kwa ajili ya kuzindua zoezi la ukaguzi katika halmashauri hiyo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma, Jaji Mstaafu Hamisa Kalombola mara baada ya kuwasili kwa ajili ya kuzindua zoezi la ukaguzi katika halmashauri hiyo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, mara baada ya kuwasili kwa ajili ya kuzindua zoezi la ukaguzi katika halmashauri hiyo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.

Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma, Jaji Mstaafu Hamisa Kalombola akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kwa ajili ya kuzungumza  na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwenye uzinduzi wa zoezi la ukaguzi katika halmashauri hiyo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.

Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda akizungumza kabla Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete  kuzungumza  na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwenye uzinduzi wa zoezi la ukaguzi katika halmashauri hiyo,


Baadhi ya watumishi wa umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro wakimsililiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete wakati  akizungumza nao mara baada ya kuzindua zoezi la ukaguzi katika halmashauri hiyo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.


 

 

 

 

 

 

 

 

WAZIRI KIKWETE AISISITIZA TAKUKURU KUJIRIDHISHA NA USHAHIDI WA KESI ZA WATUHUMIWA KABLA YA KUZIPELEKA MAHAKAMANI


Na Lusungu Helela, Morogoro

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, ameisisitiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kujiridhisha na ushahidi wa kutosha kabla ya kufikisha kesi mahakamani ili kuepuka kuwapotezea watu muda, hasa pale ambapo mtuhumiwa huachiwa au kushinda kesi kutokana na kukosekana kwa ushahidi.

Mhe. Kikwete ametoa kauli hiyo leo  Alhamisi Juni 20, 2026, alipokuwa akizungumza na watumishi wa TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi.

Amesema katika miaka ya hivi karibuni TAKUKURU imeshindwa kufanikiwa kwenye baadhi ya kesi na hii sio kwamba inaonewa, yawezekana kuna sehemu katika ushahidi hawajajipanga vizuri.

“Nawaombeni sana Maafisa Uchunguzi wetu tujiridhishe, msitumike katika kuwapotezea watu muda, ni muhimu tukajiridhisha juu ya ushahidi wa kesi zetu na utayari wa kupeleka kesi Mahakamani. Haipendezi kesi kuendeshwa kwa zaidi ya miezi mitano, halafu mwisho mtuhumiwa ashinde kwa kukosekana kwa ushahidi wa kutosha,” amesema.

Ameongeza kuwa watumishi wa taasisi hiyo wanapaswa kuhakikisha haki inatendeka bila kumuonea haya mtu yeyote wala kupindisha Sheria, Taratibu na Kanuni katika kila hatua ya uchunguzi.

Aidha, ameipongeza Taasisi hiyo kwani pamoja na kutofanikiwa katika baadhi ya kesi kwa kukosa ushahidi lakini amewapongeza kwa kesi walizoshinda ambazo zilikuwa na ushahidi wa kutosha huku akiwataka kuendelea kufanya kazi kwa bidii.

Amesema takwimu za mwaka uliopita zinaonyesha TAKUKURU imeshinda zaidi ya asilimia 70 ya kesi za rushwa ilizofikisha mahakamani.

Awali , Mkurugenzi  Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin  Chalamila, amesema taasisi hiyo itaendelea kutanguliza uzalendo, weledi, uwajibikaji na haki katika kushughulikia kesi za rushwa na uhujumu uchumi.

Chalamila amesema TAKUKURU ina Kitengo cha Maadili ya Watumishi kinachoongozwa na Mkurugenzi na moja ya majukumu yake ya msingi ni kuchunguza watumishi wa taasisi hiyo ili kuhakikisha wanakuwa mfano bora kwa jamii.

“Tuna Kitengo cha Maadili ya Watumishi wa TAKUKURU na kinaongozwa na Mkurugenzi. Moja ya jukumu lake la msingi ni kuwachunguza watumishi ili tuwe mfano na kioo bora kwa jamii,” alisema


 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, (katikati) akiwa ameongozana na viongozi wengine akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Usimamizi Miliki ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Dkt. Emmanuel Kiabo kuhusiana na jengo la   Ofisi ya TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila 



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, akizungumza na watumishi wa TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi.

Baadhi ya Watumishi wa TAKUKURU  wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, wakati akizungumza nao leo Mkoani wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, akisalimiana na baadhi ya viongozi na  watumishi mara baada ya kuwasili katika  Ofisi za TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya viongozi na watumishi wa TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi.

 Mkurugenzi  Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, kuzungumza na watumishi wa TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Itumishi wa Umma na Utawala Bora, akipanda mti mara baada ya  kuzungumza na watumishi wa TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Itumishi wa Umma na Utawala Bora, akimwagilia  mti mara baada ya kuupanda katika Ofisi za  TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi.

 

 

 

 

Karibu Tukuhudumie

 




Mpendwa Mteja Wetu, Mrejesho wako ni muhimu sana kwetu.

 





Monday, August 17, 2026

WATUMISHI WAPATIWA ELIMU KUHUSU HATI YA KUSAFIRI, NAIBU KATIBU MKUU LWANGILI ASISITIZA UMUHIMU WA MAFUNZO YA MARA KWA MARA KUJENGA UTUMISHI WA UMMA WENYE WELEDI

 Na Eric Amani, Jijini Dodoma

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili, amesisitiza umuhimu wa mafunzo ya mara kwa mara kwa watumishi wa Umma, akieleza kuwa mafunzo hayo ni muhimu katika kuongeza maarifa na ujuzi, kujenga uwezo na kuwawezesha watumishi kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na weledi.

Bi. Lwangili ameyasema hayo leo wakati akihitimisha mafunzo yaliyohusu uelewa na maarifa ya watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu hati ya kusafiri, ikiwemo taratibu za kuomba, kupata na kutumia hati hiyo kwa usahihi yaliyofanyika leo Agosti 17, 2026, katika eneo la wazi la Ofisi hiyo jijini Dodoma.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, Naibu Katibu Mkuu Lwangili amesema kuwa kuendelea kuwawezesha watumishi kupata elimu na ujuzi katika maeneo mbalimbali ni sehemu ya juhudi za Serikali za kujenga Utumishi wa Umma wenye weledi, ufanisi na unaozingatia viwango vya ubora katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Awali akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Mrakibu Msaidizi wa Uhamiaji, Bw. Segere Zonzo, amewakumbusha watumishi umuhimu wa kuwa na uelewa sahihi wa taratibu za kupata na kutumia hati ya kusafiri.

Bw. Zonzo amesema kuwa uelewa huo utawawezesha watumishi kuzingatia taratibu na kutumia hati hiyo kwa usahihi, hivyo kurahisisha safari zao za nje ya nchi, hususan wanaposafiri kwa ajili ya kutekeleza majukumu ya kikazi au shughuli binafsi.

Mafunzo hayo ni sehemu ya utaratibu wa Ofisi ya Rais – Utumishi wa kuwawezesha watumishi kuendelea kujifunza na kupata elimu kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu Utumishi wa Umma, sambamba na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Prisca Lwangili akizingumza na watumishi wa ofisi hiyo (hawapo pichani) mara baada ya mafunzo ya kuongeza uwezo yanayofanyika kila jumatatu katika ukimbi wa ofisi hiyo, Agosti 17, 2026


Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma Bw. Baraka Manono akizingumza na watumishi wa ofisi hiyo (hawapo pichani) kabla kuanza kwa mafunzo ya kuongeza uwezo yanayofanyika kila jumatatu katika ukimbi wa ofisi hiyo, Agosti 17, 2026


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Prisca Lwangili akiwa na Wakurugenzi na Wakurugenzi wasaidizi wakipata elimu juu ya hati ua kusafiri Agosti 17, 2026.


Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Rais – UTUMISHI wakipatiwa elimu kuhusu hati ya kusafiri kutoka kwa Afisa wa Idara ya uhamiaji Mrakibu Msaidizi Bw. Segere Zonzo (Hayupo pichani) Agosti 17, 2026 katika ukumbi wa ofisi hiyo.



Mrakibu Msaidizi wa Idara ya Uhamiaji Bw. Monge Mnzava akitoa elimu kuhusu hati ya kusafiri kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais – UTUMISHI wakati wa mafunzo ya kuongeza uwezo katika ofisi hiyo.


Mrakibu Msaidizi wa Idara ya Uhamiaji Bw. Segere Zonzo akitoa elimu kuhusu hati ya kusafiri kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais – UTUMISHI wakati wa mafunzo ya kuongeza uwezo katika ofisi hiyo.



 

Friday, August 14, 2026

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YAIPONGEZA TASAF KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO, YASISITIZA KUENDELEZA UWAZI NA UWAJIBIKAJI KATIKA KUFIKIA WALENGWA WALIOKUSUDIWA ILI KUTIMIZA MALENGO YA PSSN III

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 14 Agosti, 2026 

Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imepokea taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III) na kutoa maelekezo ya kuendeleza misingi ya utekelezaji wenye ufanisi, uwazi na uwajibikaji katika kufikia walengwa waliokusudiwa na kutimiza malengo ya PSSN III.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amezungumza hayo leo tarehe 14 Agosti, 2026 Bungeni jijini Dodoma alipokuwa akiongoza kikao cha Kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kilicholenga kupokea taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).

Vilevile, Mhe. Dkt. Ndumbaro ameipongeza TASAF kwa utekelezaji mzuri wa Miradi ya Maendeleo ikiwemo ujenzi kwenye sekta ya elimu na afya.

“Kwa niaba ya Kamati yangu nitoe pongezi nyingi kwa ofisi hii, kwa hakika mnafanya kazi nzuri katika mpango wa kunusuru kaya maskini, lakini pia mnatekeleza vizuri Miradi ya Maendeleo ikiwemo ujenzi  kwenye sekta ya elimu na afya, mnamwakilisha vizuri Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika utekelezaji wa miradi hii’’ Amesema Mhe. Dkt. Ndumbaro

Awali akiwasilisha kwa Kamati hiyo taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III), Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray amesema, PSSN III iliidhinishwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Benki ya Dunia tarehe 10 Aprili 2026, na kwa sasa ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha maandalizi kabla ya kuanza utekelezaji.

Naibu Waziri Qwaray amesema kuwa, katika maandalizi ya utekelezaji wa PSSN III, hatua muhimu zimekamilika ikiwemo kukamilisha usanifu wa Mpango, kuandaa nyaraka mbalimbali za utekelezaji, miongozo ya kiutendaji na kuimarisha mifumo ya TEHAMA inayosimamia shughuli za Mpango.

Aidha ameongeza kuwa, mchakato wa utambuzi wa Mamlaka za Maeneo ya Utekelezaji yatakayoshiriki kwenye utekelezaji wa Mpango unaendelea na unaojumuisha timu ya wataalamu kutoka TASAF, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar (OCGS), pamoja na wataalamu wa mazingira ambapo uchambuzi na uchakataji huo utazingatia viwango vya umaskini katika ngazi ya Halmashauri pamoja na viashiria vya athari za kimazingira, ikiwemo uwezekano wa maeneo kuathiriwa na mabadiliko ya tabianchi na majanga mbalimbali.

Vilevile, Mhe. Qwaray amesema kupitia mpango huo unatarajiwa kuongeza uwezo wa kaya maskini na zilizo katika mazingira hatarishi kukabiliana na changamoto za kiuchumi, kijamii na kimazingira, kuongeza ujuzi na taaluma kwa vijana kutoka kaya maskini na zinazoishi katika mazingira hatarishi zitakazoweza kujiajiri na kuajiriwa, kuwa na masijala ya kitaifa (kanzi data) yenye taarifa muhimu ya kaya maskini na zilizopo katika mazingira hatarishi pamoja na urasimishwaji wa TASAF kama taasisi ya umma ya kutekeleza na kusimamia utoaji wa huduma za msaada ya kijamii itakayohakikisha uendelevu, ufanisi na uratibu wa utoaji wa huduma hizo nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bw. Shedrack Mziray ameishukuru Kamati hiyo kwa maoni na ushauri mbalimbali ambao wameutoa na kuahidi kufanyia kazi ili kuimarisha na kuboresha utendaji kazi wa Taasisi hiyo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akisisitiza jambo wakati wa kikao cha Kamati yake kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kilicholenga kupokea taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (aliyesimama kulia) akiwasilisha kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III). Wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akifurahia jambo wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bw. Shedrack Mziray akisikiliza maoni kutoka kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo Bungeni jijini Dodoma na Watendaji hao kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Nyamizi Mhoja akiwasilisha hoja kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).

Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Sikudhani Chikambo akiwasilisha hoja kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akifafanua hoja Bungeni jijini Dodoma wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (kulia) akiteta jambo na Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (kushoto) wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).

Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (aliyesimama) akifafanua hoja iliyowasilishwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bw. Shedrack Mziray (kulia) akiandika maoni yaliyokuwa yakiwasilishwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III). Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, SACP. Ibrahim Mahumi. 


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (aliyesimama mbele) akiwasilisha kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III). Wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora.


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Saashisha Mafuwe akiwasilisha hoja kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Yohana Msita akiwasilisha hoja kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).

Sehemu ya Wakurugenzi na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza kwenye kikao Bungeni jijini Dodoma mara baada ya Watendaji wa ofisi hiyo kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).

Sehemu ya Wakurugenzi Wasaidizi na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza kwenye kikao Bungeni jijini Dodoma mara baada ya Watendaji wa ofisi hiyo kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).