Na Eric Amani, Jijini Dodoma
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili, amesisitiza umuhimu
wa mafunzo ya mara kwa mara kwa watumishi wa Umma, akieleza kuwa mafunzo hayo
ni muhimu katika kuongeza maarifa na ujuzi, kujenga uwezo na kuwawezesha
watumishi kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na weledi.
Bi. Lwangili ameyasema hayo leo wakati
akihitimisha mafunzo yaliyohusu uelewa na maarifa ya watumishi wa Ofisi ya Rais
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuhusu masuala mbalimbali
yanayohusu hati ya kusafiri, ikiwemo taratibu za kuomba, kupata na kutumia hati
hiyo kwa usahihi yaliyofanyika leo Agosti 17, 2026, katika eneo la wazi la Ofisi
hiyo jijini Dodoma.
Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, Naibu Katibu Mkuu Lwangili amesema kuwa
kuendelea kuwawezesha watumishi kupata elimu na ujuzi katika maeneo mbalimbali
ni sehemu ya juhudi za Serikali za kujenga Utumishi wa Umma wenye weledi,
ufanisi na unaozingatia viwango vya ubora katika utoaji wa huduma kwa wananchi.
Awali akizungumza wakati wa mafunzo hayo,
Mrakibu Msaidizi wa Uhamiaji, Bw. Segere Zonzo, amewakumbusha watumishi umuhimu
wa kuwa na uelewa sahihi wa taratibu za kupata na kutumia hati ya kusafiri.
Bw. Zonzo amesema kuwa uelewa huo utawawezesha
watumishi kuzingatia taratibu na kutumia hati hiyo kwa usahihi, hivyo
kurahisisha safari zao za nje ya nchi, hususan wanaposafiri kwa ajili ya
kutekeleza majukumu ya kikazi au shughuli binafsi.
Mafunzo hayo ni sehemu ya utaratibu wa Ofisi ya
Rais – Utumishi wa kuwawezesha watumishi kuendelea kujifunza na kupata elimu
kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu Utumishi wa Umma, sambamba na kuongeza
ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.
![]() |
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Prisca Lwangili akiwa na Wakurugenzi na Wakurugenzi
wasaidizi wakipata elimu juu ya hati ua kusafiri Agosti 17, 2026. |
![]() |
Mrakibu Msaidizi wa Idara ya Uhamiaji Bw. Monge
Mnzava akitoa elimu kuhusu hati ya kusafiri kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais –
UTUMISHI wakati wa mafunzo ya kuongeza uwezo katika ofisi hiyo. |
![]() |
Mrakibu Msaidizi wa Idara ya Uhamiaji Bw.
Segere Zonzo akitoa elimu kuhusu hati ya kusafiri kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais
– UTUMISHI wakati wa mafunzo ya kuongeza uwezo katika ofisi hiyo. |







No comments:
Post a Comment