Friday, July 3, 2026

MHE. RIDHIWANI KIKWETE AZINDUA TAFITI SITA ZITAKAZOFANYA TPSC KUWA KITOVU CHA MAARIFA NA USHAHIDI WA KISAYANSI KATIKA KUBORESHA UTUMISHI WA UMMA

Na. Veronica Mwafisi-Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amezindua tafiti tumizi sita zitakazokifanya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) kuwa kitovu cha maarifa na ushahidi wa kisayansi kwa ajili ya kuboresha Utumishi wa Umma.

 

Akizungumza katika hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Waziri Kikwete amesema Serikali inahitaji tafiti zitakazotoa suluhisho kwa changamoto halisi zinazokabili taasisi za umma.

 

“Tunahitaji tafiti zinatakazosaidia kufanya maamuzi sahihi ya sera, kuboresha mifumo ya kazi, na kuongeza ufanisi wa huduma kwa wananchi”, amesema Mhe. Kikwete.

 

Aidha, Waziri Kikwete amewapongeza watafiti wote walioshiriki katika kazi ya utafiti na kutoa rai kwa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania kuendelea kuimarisha ushirikiano na Wizara, Idara Zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Vyuo Vikuu na taasisi nyingine ili tafiti zake ziwe na mchango mkubwa katika maendeleo ya Taifa.

 

Waziri Kikwete ameongeza kuwa, anaamini miaka 25 ijayo itakuwa kipindi cha mafanikio makubwa zaidi, ambapo Chuo hicho kitaendelea kuwa kinara wa maendeleo ya rasilimali watu, tafiti tumizi, na ushauri wa kitaalamu kwa ajili ya kuimarisha Utumishi wa Umma na kuchochea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akibonyeza kitufe wakati akizindua tafiti tumizi sita wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) zitakazokifanya Chuo hicho kuwa kitovu cha maarifa na ushahidi wa kisayansi kwa ajili ya kuboresha Utumishi wa Umma.


Viongozi mbalimbali, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakipiga makofi baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) kuzindua tafiti tumizi sita wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza baada ya kuzindua tafiti tumizi sita wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akifurahia jambo na Katibu Mkuu wa ofisi yake, Bw. Juma Mkomi (kulia) baada ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI kukabidhiwa Tuzo ya Utambuzi iliyotolewa na Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo hicho yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) akielekea katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC). Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Florens Turuka  na kushoto kwake ni Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu, Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Dkt. Ernest Mabonesho.


Menejimenti, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao baada ya kuzindua tafiti tumizi sita wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao baada ya kuzindua tafiti tumizi sita wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao baada ya kuzindua tafiti tumizi sita wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.



MIAKA 25 YA CHUO CHA UTUMISHI WA UMMA TANZANIA, MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA KUJENGA RASILIMALIWATU YENYE TIJA

Na. Veronica Mwafisi-Dar ES Salaam

Tarehe 03 Julai, 2026

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) ina nafasi ya kipekee katika kujenga na kuendeleza uwezo wa kiutendaji wa watumishi wa umma ambao ndio watekelezaji wa majukumu ya Serikali kila siku.

 

Waziri Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 03 Julai, 2026 wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya TPSC yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

 

Mhe. Kikwete amesema, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuweka kipaumbele katika uimarishaji wa Utumishi wa Umma ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, za haraka na zenye tija.

 

Mhe. Kikwete ameongeza kuwa, Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania si tu taasisi ya mafunzo, bali ni nguzo muhimu ya Serikali katika kujenga rasilimaliwatu yenye maarifa, stadi, maadili na uzalendo unaohitajika katika kutumikia umma kwa ufanisi.

 

Katika hatua nyingine, Mhe. Kikwete amesema kuwa, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inatutaka kuwa na Taifa lenye uchumi wa kisasa, ushindani wa kimataifa, matumizi makubwa ya teknolojia, na huduma za umma zenye ufanisi wa hali ya juu. Hivyo, mafanikio ya Dira hiyo yatategemea kwa kiasi kikubwa uwepo wa watumishi wenye sifa, ujuzi na uwezo wa kuongoza mabadiliko hayo.

 

“Chuo hiki kina wajibu mkubwa wa kuhakikisha  Watumishi wa Umma wanapata maarifa na stadi zinazolingana na mahitaji ya karne ya ishirini na moja ili kuwepo wa watumishi wenye sifa, ujuzi na uwezo wa kuongoza mabadiliko hayo,” amesema Waziri Kikwete.

 

Aidha, Mhe. Kikwete amewapongeza watangulizi wake kwa usimamizi mzuri ambao umechangia mafanikio makubwa ya Chuo hicho huku akimshukuru Katibu Mkuu wa Ofisi yake, Bw. Juma Mkomi kwa kuendelea kusimamia Chuo hicho kiutendaji.

 

Vilevile, Waziri Kikwete ameipongeza Bodi ya Ushauri ya TPSC, Menejimenti, Watumishi, Wanafunzi na wadau wote kwa mchango wao katika safari ya kutimiza miaka 25 ya mafanikio ya chuo hicho.

 

Akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mhe. Waziri kuzungumza na wadau katika hafla hiyo, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi ametoa wito kwa waajiri kutumia Kampasi za TPSC zilizo katika kanda zao ili kuwawezesha watumishi ikiwemo waajiriwa wapya kupata mafunzo ya awali.

 

“Kampasi katika Kanda hizo zimewekwa kimkakati ili kusogeza huduma za chuo katika mikoa mbalimbali, hivyo Waajiri wazitumie kikamilifu kwa watumishi kupata mafunzo kwa lengo la kuboresha utendaji kazi.” Amesisitiza Katibu Mkuu Mkomi.

 

Amezitaja Kampasi hizo kuwa ni Dar es Salaam, Mbeya, Tanga, Singida, Tabora na Mtwara na kuongeza kuwa Ofisi ya Rais-UTUMISHI itaendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na TPSC za kumiliki majengo yao ambapo Kampasi ya Singida inaendelea na ujenzi wa majengo 30 na Kampasi ya Tanga majengo 15.

 

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TPSC, Dkt. Florens Turuka amesema Bodi itaendelea kutoa ushauri ili Chuo kiendelee kuwa kinara katika masuala mbalimbali ikiwemo kujenga rasilimaliwatu yenye maadili, na yenye tija kwa taifa.

 

Akiwasilisha taarifa ya miaka 25 ya TPSC, Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Ernest Mabonesho amesema tangu kuanzishwa kwake, Chuo kimepata mafanikio makubwa katika maeneo mbalimbali ikiwemo taaluma, rasilimaliwatu na miundombinu.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


Viongozi mbalimbali, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akiteta jambo na Katibu Mkuu wa ofisi yake Bw. Juma Mkomi (kulia) wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


Menejimenti, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akifurahia jambo na Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu, Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Dkt. Ernest Mabonesho (kushoto) wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao kwenye hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


Menejimenti, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


 

 

Thursday, July 2, 2026

SERIKALI YARIDHISHWA NA MAENDELEO YA MIRADI YA NYUMBA ZA WATUMISHI WA UMMA KIGOMA

 Na. Antonia Mbwambo–Kigoma

Tarehe 2 Julai, 2026

Serikali imeeleza kuridhishwa na Maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa Ujenzi wa Nyumba za Watumishi wa Umma Awamu ya Pili katika Mkoa wa Kigoma kufuatia ukaguzi uliofanywa na timu ya Wataalamu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa kushirikiana na Watumishi Housing Investimentsl.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Bw. Patrick Allute, wakati wakihitimisha ziara ya ukaguzi wa miradi ya makazi ya Watumishi wa Umma Mkoani Kigoma ambapo timu ilikagua mradi ya nyumba za Watumishi katika Shule ya Sekondari Muhunga, Wilaya ya Kasulu, na Kituo cha Afya Muyama, Wilaya ya Buhigwe,Mkoa wa Kigoma

Akizungumza baada ya kuhitimisha ziara hiyo, Bw. Allute amepongeza wasimamizi wa mradi, Watumishi Housing na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa usimamizi unaowezesha miradi hiyo kutekelezwa kwa ufanisi. Amesema hatua iliyofikiwa inaakisi dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuboresha mazingira ya kazi na ustawi wa Watumishi wa Umma.

Aidha, ameutaja mradi wa nyumba za Watumishi katika Kituo cha Afya Muyama kuwa miongoni mwa miradi iliyofanya vizuri zaidi kati ya miradi 15 iliyokaguliwa katika Mikoa mbalimbali ya Tanzania kutokana na kasi ya utekelezaji na ubora wa kazi inayoendelea kuonekana.

"Mradi wa nyumba za Watumishi katika Kituo cha Afya Muyama umeonesha kiwango cha juu cha utekelezaji. Kazi nyingi muhimu, ikiwemo mfumo wa umeme, zimekamilika na mradi umebakiza hatua chache kabla ya kukamilika na kuanza kutumika," amesema Bw. Allute.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Mradi wa Kituo cha Afya Muyama ameishukuru timu ya ukaguzi kwa ushauri na maelekezo yaliyotolewa, akisema yataendelea kufanyiwa kazi ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na kuanza kutoa huduma kwa Watumishi wa Umma waliokusudiwa kunufaika nao.

 

Wataalamu kutoka Ofisi ya Rais–UTUMISHI na Watumishi Housing Investment (WHI) wakijadili jambo mara baada ya kufanya ukaguzi wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Muyama, Wilaya ya Buhigwe, Mkoani Kigoma

Timu ya wataalamu kutoka Ofisi ya Rais–UTUMISHI na Watumishi Housing Investment (WHI) wakiwa katika picha ya pamoja na Kaimu Mganga Mfawidhi Kituo cha Afya Muyama Bw. Kwima Juma Buanza (wa tatu kutoka kushoto), mara baada ya timu hiyo kukamilisha ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa nyumba za watumishi wa kituo hicho kiiilichopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma.


Muonekano wa nyuma wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma wa Kituo cha Afya Muyama kwenye Wilaya ya Buhigwe Mkoa wa Kigoma

Mkurugenzi wa Fedha na Uwekezaji kutoka Watumishi Housing Investiment (WHI) Bw. Paskali Massawe (aliyenyoosha mkono) akielezea jambo kwa Wataalamu alioambatana nao katika ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Muyama, Wilaya ya Buhigwe, Mkoani Kigoma, mara baada ya kufika kwenye eneo hilo Julai 2, 2026 

Wataalamu kutoka Ofisi ya Rais–UTUMISHI na Watumishi Housing Investment (WHI) wakijadili jambo mara baada ya kufanya ukaguzi wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya Watumishi wa Shule ya Sekondari Muhunga iliyopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Patrick Allute (wa tano kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mipango na Bajeti, wa Ofisi hiyo, Bi. Julieth Magambo wakati wa ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa nyumba ya makazi ya watumishi wa Shule ya Sekondari Muhunga iliyopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma.

Wataalamu kutoka Ofisi ya Rais–UTUMISHI na Watumishi Housing Investment (WHI) wakijadili jambo mara baada ya kufanya ukaguzi wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya Watumishi wa Shule ya Sekondari Muhunga iliyopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, Bw. Patrick Allute, (aliyenyoosha mikono), akitoa maelekezo kwa Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Muhunga Mwl. Beatus Damiani,(wa pili kutoka kushoto) wakati wa ukaguzi wa SHule hiyo iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Mkoa wa Kigoma, leo tarehe 2 Julai, 2026.

Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma Shule ya Sekondari Muhunga iliyopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma.


Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Patrick Allute (wanne kutoka kushoto) akiagana na Kaimu Afisa Elimu Sekondari, Halmashauri ya Mji wa Kasulu Mwl. Jeremiah Ntiboneka mara baada ya Timu ya Wataalamu kutoka Ofisi ya Rais–UTUMISHI na Watumishi Housing Investment (WHI) kukagua mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari Muhunga iliyopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma.

Monday, June 29, 2026

JICHO LA PEPMIS, BADO SIKU 1

 


KATIBU MKUU MKOMI AMPONGEZA NA KUMTAKIA HERI KATIBU MTEULE WA TUME YA UTUMISHI WA UMMA, AMUASA KUZINGATIA FALSAFA YA KAZI NA UTU KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Katibu Mkuu ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi amempongeza na kumtakia heri aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda.

Katibu Mkuu Mkomi ameyasema hayo jijini Dodoma baada ya kuhitimishwa kwa mafunzo yanayofanyika kila Jumatatu kwa watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambapo pia alitumia wasaa huo kumuaga Bw. Kipanda.

Bw. Mkomi amemuasa Katibu mteule huyo kutumia falsafa ya kazi na utu wakati wa utekelezaji wa majukumu yake ili aweze kutenda haki katika kufanya maamuuzi.

Amesema, matatizo mengi yanayowapata Watumishi wa Umma wakati mwingine yanatokana na kukosekana kwa utu wa waajiri hivyo, amemtaka Bw. Kipanda kufanya maamuzi yaliyo sahihi ili kutenda haki.

“Ninaamini Bw. Kipanda utaenda kutenda haki na kutuwakilisha vizuri, fanya kazi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na Utu. Taasisi uliyoteuliwa kufanya kazi inahusika na utoaji wa haki kwa Watumishi wa Umma, hivyo pamoja na kutumia taratibu, ukazingatie pia suala la utu katika kufanya maamuzi.

Vilevile, Bw. Mkomi amemuahidi Bw. Kipanda ushirikiano pale atakapohitaji ikiwa ni pamoja na ushauri katika kazi kwani itasaidia kuimarisha zaidi utendaji kazi.

Kwa upande wake Katibu Mteule wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumteua kuiongoza Taasisi hiyo.

Bw. Kipanda amewashukuru Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa kufanya kazi nao kwa muda mrefu na kuomba kuendelea kumpatia ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake mapya kwa maendeleo ya Taifa.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Katibu Mkuu Mstaafu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (kushoto). Kulia ni aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda 

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akizungumza jambo kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda baada ya kumaliza mafunzo kwa watumishi wa ofisi hiyo yaliyolenga kuwajengea uwezo katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa nasaha wakati wa kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda 


Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda (kulia)akipokea keki alipokuwa akiagwa na Watumishi wa Ofisi hiyo mara baada ya kuteuliwa kuwa Katibu wa Tume hiyo. 


Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Nolasco Kipanda ambaye kwa sasa ni Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma akikata keki akiwa anaagwa na watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI jijini Dodoma  


Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda akitoa neno la shukrani kwa Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI alipokuwa akiwaaga katika ofisi hiyo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda (hayupo pichani) wakati akitoa neno la shukrani kwa Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI alipokuwa akiwaaga baada ya kupata teuzi hiyo.


Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bw. Musa Magufuli akimlisha keki aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipandabaada ya kutoa neno la shukrani kwa Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI alipokuwa akiwaaga baada ya kupata teuzi hiyo.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa nasaha wakati wa kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda.



SERIKALI YAENDELEA KUBORESHA MAZINGIRA YA WATUMISHI WA UMMA KUPITIA UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

Na. Antonia Mbwambo- Mbeya

Tarehe 29 Juni, 2026

Serikali imeendelea kuboresha mazingira ya kazi kwa Watumishi wa Umma kupitia utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa nyumba za makazi, hatua inayolenga kuongeza ufanisi wa utendaji kazi na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute, wakati wa ziara ya kukagua ujenzi wa nyumba za watumishi katika Shule za Msingi Ngolela, Wilaya ya Kyela na Idweli, Wilaya ya Rungwe, mkoani Mbeya, iliyohusisha wataalamu kutoka Ofisi hiyo pamoja na Watumishi Housing Investments (WHI).

Bw. Allute amesema makazi bora yataongeza ari ya kazi kwa Walimu na kuboresha utoaji wa huduma. Aidha, amewataka Watumishi watakaonufaika na nyumba hizo kuzitunza vizuri mara zitakapokamilika kwa kuwa ni mali za umma na zinazopaswa kudumu ili kuwanufaisha Watumishi wa baadae.

"Serikali inaendelea kuwekeza fedha nyingi katika kuboresha mazingira ya kazi kwa Watumishi wa Umma, hivyo ni wajibu wa kila mnufaika kuhakikisha nyumba hizi zinatunzwa vizuri mara zitakapokamilika na kuanza kutumika ili ziendelee kuhudumia watumishi wa sasa na wa baadae," Bw. Allute amesema

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mipango na Bajeti, kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Julieth Magambo, amesema Serikali inaendelea kuwekeza katika ujenzi wa nyumba za watumishi ili kuhakikisha wanapata mazingira bora, salama na yenye utulivu yatakayowawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

Awali, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ngolela, Bw. Samsoni Anyosisye, ameishukuru Serikali kwa mradi huo, huku akieleza kuwa nyumba zilizopo zimechakaa na hazifai kwa matumizi, hali iliyowalazimu Walimu wengi kuishi mbali na shule.

Naye Mwalimu wa Shule ya Msingi Idweli, Bw. Tejile Mathew, amesema kukamilika kwa nyumba hizo kutaleta motisha ya kazi na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma ya Elimu.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (aliyenyoosha mkono) akitaka ufafanuzi wa jambo  wakati wa ukaguzi wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Shule ya msingi Ngolela iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mipango na Bajeti,Bi Julieth  Magambo wa Ofisi hiyo.

Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya watumishi wa umma wa Shule ya msingi Ngolela, iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoa wa Mbeya.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ngolela, Bw. Samsoni Anyosisye (wanne kutoka kushoto)  akitoa maelezo kwa Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (wa kwanza kutoka kulia) wakati wa ukaguzi wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Shule ya msingi Ngolela iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya

Muonekano wa mbele wa jengo la zamani walilokuwa wakiishi Waalimu wa shule ya msingi Ngolela iliyopo Kyela Mkoani Mbeya kabla ya jengo hilo kuchakaa na kushindwa kutumika kwa makazi

Timu ya wataalamu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watumishi Housing Investment (WHI) ikiwa katika picha ya pamoja na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ngolela, Bw. Samsoni Anyosisye (wanne kutoka kushoto) mara baada ya timu hiyo kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Shule ya msingi Ngolela iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya

Muonekano wa nyuma wa jengo la zamani walilokuwa wakiishi Waalimu wa shule ya msingi Ngolela iliyopo Kyela Mkoani Mbeya kabla ya jengo hilo kuchakaa na kushindwa kutumika kwa makazi

Timu ya wataalamu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watumishi Housing Investment (WHI) wakiwa katika picha ya pamoja na Mwalimu wa Shule ya Msingi Idweli, Bw. Tejile Mathew pamoja na mafundi wanaosimamia mradi huo mara baada ya timu hiyo kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Shule ya msingi Ngolela iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya

Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya watumishi wa umma wa Shule ya msingi Idwelu, iliyopo Wilaya ya Rugwe Mkoa wa Mbeya