Monday, May 18, 2026

UWEKEZAJI WA MIFUMO YA TEHAMA SERIKALINI KUONGEZA UFANISI NA UWAZI KATIKA UTOAJI WA HUDUMA

 

Na. Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 18/05/2026

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray amesema uwekezaji wa matumizi ya Mifumo ya Tehama Serikalini utasaidia kwa asilimia kubwa kuongeza ufanisi na Uwazi wa huduma zinazotolewa na Watumishi wa umma kwa wananchi kwa maslahi ya Taifa

Mhe. Qwaray ameyasema hayo Mei 18, 2026 wakati akizungumza na Uongozi wa Kituo cha Utafiti na Ubunifu wa Maendeleo ya Serikali Mtandao (eGovRIDC), Menejimenti pamoja na Watumishi kutoka Taasisi ya Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) mara baada ya Naibu Waziri huyo kutembelea Kituo hicho Jijini Dodoma.

“Ni lazima tufahamu kwamba, katika dunia ya sasa, mageuzi ya kidijiti si chaguo tena bali ni msingi wa ufanisi wa Serikali, ushindani wa kiuchumi na maendeleo ya kijamii”. Mhe. Qwaray alisema.

Amesema,Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwekeza katika mifumo ya TEHAMA ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato, kupunguza urasimu na rushwa, kuongeza uwazi, na kurahisisha upatikanaji wa huduma za wananchi popote walipo.

Mhe.Qwaray ameongeza kuwa, Serikali imepata mafanikio makubwa katika matumizi ya mifumo ya Kidijiti katika Sekta mbalimbali ikiwemo kuongeza uwajibikaji, kurahisisha upatikanaji wa huduma na kuboresha utendaji kazi wa Utumishi wa Umma.

Aidha, Mhe Qwaray amesema kituo hicho kimekuwa na mchango chanya katika matumizi ya Mifumo mbalimbali kama vile Mfumo wa   wa kielektroniki unaoiwezesha Serikali kupokea na kushughulikia malalamiko, maoni, pongezi, na maulizo kutoka kwa wananchi kwenda kwenye taasisi zote za umma (e-Mrejesho) pamoja na Mfumo wa Dirisha la Huduma za Serikali ikiwemo tangazo la Gazeti la Serikali na Utoaji wa Vibali vya Likizo bila Malipo.

Mhe. Qwaray ametoa wito kwa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali, Vyuo Vikuu, taasisi za tafiti pamoja na Sekta Binafsi ili tafiti zinazofanyika ziweze kutatua changamoto halisi za wananchi na taasisi za umma.

Vilevile ameitaka Taasisi hiyo kusimamia utekelezaji wa Sheria, Kanuni, na Miongozo ya Serikali Mtandao ili mifumo yote inayotengenezwa iwe salama, yenye kuwasiliana na mifumo mingine na kuleta tija kwa wananchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Mhandisi Benedict Ndomba, amesema Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) ilianzisha Kituo cha Utafiti na Ubunifu wa Maendeleo ya Serikali Mtandao (e-GOVRIDC) kwa lengo la kuratibu shughuli za kitafiti, kubuni na kuendeleza jitihada za Serikali Mtandao, ili kuongeza tija katika utoaji wa huduma kwa umma, kuwajengea uwezo na kukuza vipaji vya vijana wabunifu katika eneo la TEHAMA.

Mhandisi Ndomba amemshukuru Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray kwa kuitikia wito wa kutembelea kituo hicho na kuahidi kwamba wameyapokea na wataenda kuyafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na kiongozi huyo.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (kulia) akisalimiana na baadhi ya Viongozi wa Kituo cha Utafiti na Ubunifu wa Maendeleo ya Serikali Mtandao (eGovRIDC) mara baada ya kuwasili katika kituo hicho kilichopo Jijini Dodoma.



Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (kulia) akikaribishwa na viongozi wa kituo cha Utafiti na Ubunifu wa Maendeleo ya Serikali Mtandao (eGovRIDC) mara baada ya kuwasili Kituoni  hapo Jijini Dodoma.

wa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na viongozi, na Watumishi wa Kituo cha Utafiti na Ubunifu wa Maendeleo ya Serikali Mtandao (eGovRIDC), mara baada ya kuwasili na kutembelea miradi mbalimbali ya kituo hicho Mei 18, 2026 jijini Dodoma

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Utafiti na Ubunifu wa Maendeleo ya Serikali Mtandao (eGovRIDC) katika ziara ya kikazi kituoni hapo Jijini Dodoma.



Menejimenti na Watumishi wa Taasisi ya Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati akizungumza nao katika kituo cha Utafiti na Ubunifu wa Maendeleo ya Serikali Mtandao (eGovRIDC) Jijini Dodoma

Watumishi wa Taasisi ya Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati akizungumza nao katika kituo cha Utafiti na Ubunifu wa Maendeleo ya Serikali Mtandao (eGovRIDC) Jijini Dodoma.



Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA)   Mhandisi Benedict Ndomba akitoa ufafanuzi wa jambo kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray kabla Naibu Waziri huyo kuzungumza na Menejimenti na Watumishi wa Taasisi ya Mamlaka ya
Serikali Mtandao (eGA) jijini Dodoma.


Menejimenti na Watumishi wa Taasisi ya Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) wakimsikiliza  Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA)   Mhandisi Benedict Ndomba  (hayupo pichani) akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray kuhusu utendaji wa kituo cha Utafiti na Ubunifu wa Maendeleo ya Serikali Mtandao (eGovRIDC)   kilichopo Jijini Dodoma.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (aliyeka katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Taasisi ya Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) mara baada ya Naibu Waziri huyo kuzungumza nao katika ziara ya kutembelea kituo cha Utafiti na Ubunifu wa Maendeleo ya Serikali Mtandao (eGovRIDC) Jijini Dodoma.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Taasisi ya Mamlaka ya
Serikali Mtandao (eGA) mara baada ya kuzungumza nao alipokuwa katika ziara ya kutembelea kituo cha Utafiti na Ubunifu wa Maendeleo ya Serikali Mtandao (eGovRIDC) Jijini Dodoma


Friday, May 15, 2026

WAZIRI RIDHIWANI ASISITIZA UADILIFU, NIDHAMU WAHITIMU TAASISI YA UONGOZI

Na. Jawadu Kinyobwa

Waziri wa Nchi, Ofisi ya ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amewataka Wahitimu wa Taasisi ya Uongozi kuwa waadilifu, wenye nidhamu na uthubutu ili kuleta maendeleo katika jamii na taifa kwa ujumla.

Mhe. Ridhiwani amebainisha hayo Mei 15, 2026 katika Sherehe ya Tisa ya Mahafali ya Taasisi ya Uongozi yaliyofanyika Mlimani City, Jijini Dar es salaam.

Aidha, amesema katika ulimwengu wa sasa uadilifu ndio sifa kuu ya kiongozi bora na mwenye kuaminika, hivyo watumie maarifa na ujuzi walioupata chuoni kuwa viongozi wanaozingatia haki, uwajibikaji na weledi katika kila jambo.

“Nawakumbusha umuhimu wa kuwa Viongozi Wenye Uzalendo. Tukumbuke msemo wa wahenga: Adhabu ya msaliti ni malipo ya usaliti wake. Usaliti mkubwa katika uongozi wa umma ni sawa na ubadhirifu wa mali za Umma” amesema.

Akizungumza kuhusu umuhimu wa uadilifu katika uongozi, amewasihi wahitimu hao kuwa viongozi wenye maadili mema, wanaolinda mali za umma na kuweka mbele maslahi ya wananchi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Amesema Taifa linahitaji viongozi waaminifu, wenye uwajibikaji na wanaotumia nafasi zao kusukuma mbele maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa manufaa ya Watanzania wote.

Sambamba na hayo, Mhe. Ridhiwani amesisitiza kuwa, uongozi bora na wa kuzingatia misingi ya haki na uwazi utasaidia kuendelea kuitangaza vyema Tanzania pamoja na Taasisi ya Uongozi ndani na nje ya nchi.

Awali akizungumza Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Bw. Kadari Singo, amesema Taasisi hiyo imetimiza miaka kumi na tano tangu ilipoanzishwa rasmi Julai 2010 kwa Hati ya Rais kama Kituo cha Utaalamu wa Hali ya Juu (Centre of Excellence) cha kujenga na kuimarisha viongozi barani Afrika ili kuleta maendeleo endelevu.

Amebainisha kuwa, Taasisi hiyo imeendelea kufanya kazi kubwa na nzuri katika utoaji wa programu za mafunzo ya uongozi, uandaaji wa mijadala ya kisera, upanuzi wa dimbwi la maarifa kupitia tafiti na machapisho mbalimbali.

Akizungumza kwa niaba ya wahitimu, Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA), Juma Burhan Mohamed amesema mafunzo hayo yamekuwa chachu ya mabadiliko makubwa katika fikra, uwezo wa uongozi na namna ya kufanya maamuzi yenye tija kwa taasisi na jamii.

Amesema mahafali hayo hayakuwa tu sherehe ya kukamilisha mafunzo, bali yalikuwa ishara ya mabadiliko na ukuaji wa kiuongozi walioupata washiriki ndani ya kipindi cha miezi sita ya programu hiyo.

MWISHO.



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisoma nyaraka kabla ya kuzungumza na Wahitimu kwenye mahafali ya tisa ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi. 


Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bi. Mary Mwakapenda akitunukiwa cheti cha Programu ya Uongozi kwa Wanawake na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kwenye mahafali ya tisa ya programu za uongozi iliyotolewa na Taasisi ya Uongozi yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya Wahitimu wa Programu ya Uongozi kwa Wanawake wakiwa mbele mara baada ya kutunukiwa vyeti vyao na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kwenye mahafali ya tisa ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.


Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bi. Mwalibora Mwamtuya kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, akitunukiwa cheti cha Programu ya Uongozi kwa Wanawake na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kwenye mahafali ya tisa ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.



Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bi. Judith Shoo kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora akitunukiwa cheti cha Programu ya Uongozi kwa Wanawake na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kwenye mahafali ya tisa ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi ya Uongozi yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.


Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi, Bw. Kadari Singo akizungumza na Wahitimu wa Programu ya Uongozi kabla ya wahitimu hao kutunukiwa vyeti vyao na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kwenye mahafali ya tisa ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi hiyo yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wahitimu wa Programu ya Uongozi mara baada ya wahitimu hao kutunukiwa vyeti vyao na Waziri huyo kwenye mahafali ya tisa ya programu za uongozi zitolewazo na Taasisi hiyo yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.



Monday, May 11, 2026

SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA MAZINGIRA YA KAZI KWA WATUMISHI WA UMMA

Na. Antonia Mbwambo-Arusha

Tarehe 12 Mei, 2026.

Watumishi wa Umma nchini wamehakikishiwa kuboreshewa mazingira ya kazi kadri uchumi utakavyoruhusu ili kuleta tija katika utendaji kazi kwa maslahi ya umma.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray wakati akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika leo tarehe 12 Mei, 2026 katika ukumbi wa AICC Jijini Arusha.

Mhe. Qwaray amesema, Serikali inatambua na kuthamini mchango wa Watumishi wa Umma wote nchini wakiwemo Wauguzi, hivyo itazingatia changamoto wanazokutana nazo watumishi hao, pamoja na kushughulikia kwa uzito unaostahili ili kutengeneza mazingira mazuri ya utendaji kazi.

"Niwahakikishie Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya kazi na maslahi ya Watumishi wa Umma kadri uchumi utakavyoruhusu kwani tunatambua mchango wenu mkubwa katika kuwahudumia Watanzania, fanyeni kazi, Serikali ipo nanyi." Mhe. Qwaray alisema.

Aidha Mhe. Qwaray ameongeza kuwa, ili kuwa na ufanisi mkubwa katika utoaji wa huduma kwa wananchi Serikali itaendelea kuisimamia sekta ya afya pamoja na kuimarisha ushirikiano wa kitaaluma bila kuathiri misingi ya Utumishi wa Umma, Sheria, Kanuni na Taratibu zilizowekwa ikiwemo uzingatiaji wa maadili.

Aidha amewataka kuwa na kauli nzuri,  huruma na upendo utakaoongeza tija katika utendaji kazi ili kuleta mabadiliko chanya katika Sekta ya afya.

"Ninyi ndiyo watu wa kwanza kukutana na mgonjwa pindi anapofika hospitali na ni watu wa mwisho mgonjwa anapotoka hospitali baada ya matibabu, ikiwa mtakuwa na nyuso za ukatili na ulimi mkali au wa kebehi, mtawakwaza wagonjwa na hata kuwakatisha tamaa jambo ambalo litaonyesha mapungufu katika sekta ya afya.”Mhe. Qwaray alisema.

Vilevile, Mhe. Qwaray amewaahidi Wauguzi hao kuwa Ofisi imepokea masuala yote waliyoyaeleza katika risala yao na kuwaahidi kuyawasilisha kwa ajili ya kufanyiwa kazi ikiwemo masuala ya Muundo Mpya wa Utumishi wa Kada ya Uuguzi na Ukunga na Muundo wa Utawala katika Sekta ya Afya ili kuboresha huduma ya afya na maslahi ya watumishi wa afya nchini.

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Qwaray, ametoa wito kwa wauguzi kuhahakisha wanabadili mienendo na tabia zisizopendeza wala kuendana na maadili ya kazi yao, lakini pia amewapongeza kwa jitihada kubwa wanazozifanya katika kuwahudumia wananchi na kuboresha afya zao.

Kwa upande wake  Rais wa Chama cha Wauguzi (TANNA), Dkt. Ezekiel Mbao amemshukuru Naibu Waziri, Mhe. Regina Qwaray kwa kujumuika nao kwenye maadhimisho ya siku hiyo adhimu.

Maadhimisho hayo ya Siku ya Wauguzi Duniani yamebeba kauli mbiu isemayo Wauguzi Wetu, Mustakabali Wetu, Wauguzi Waliowezeshwa Huokoa Maisha.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Regina Qwaray akizungumza na Wauguzi kutoka Mikoa mbalimbali ya Tanzania (hawapo pichani) wakati Naibu Waziri huyo alipokuwa katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani tarehe 12 Mei, 2026 katika ukumbi wa AICC Jijini Arusha.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Regina Qwaray (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa Maadhimisho ya kilele cha Siku ya Wauguzi Duniani mara tu baada ya Naibu waziri huyo kuhitimisha Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika  kuanzia tarehe 9 hadi 12, Mei, 2026 jijini Arusha

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Regina Qwaray, akitembelea mabanda ya maonesho ya Wauguzi kujionea baadhi ya shughuli wanazozifanya katika kuwahudumia Watanzania kabla ya Naibu Waziri huyo kuhitimisha Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika tarehe 12 Mei, 2026 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC).

Washiriki wa maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Dunuani wakifuatilia hotuba ya Mheni Rasmi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati walipokuwa katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani Jijini Arusha.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Regina Qwaray,akikabidhiwa zawadi ya Chama cha Wauguzi (TANNA) na Raisi wa chama hicho Dkt. Ezekiel Mbao mara baada ya Naibu Waziri huyo kuhitimisha Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani tarehe 12 Mei, 2026 katika ukumbi wa AICC Jijini Arusha.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Regina Qwaray, akisaini kitabu cha wageni,mara tu baada ya kuwasili katika ukumbi wa AICC Arusha kwenye Maadhimisho ya kilele cha Siku ya Wauguzi Duniani

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Regina Qwaray,akisalimiana na baadhi ya viongozi wa chama cha wauguzi (TANNA) mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa AICC Jijini Arusha katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani tarehe 12 Mei,2026.

Washiriki wa maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Dunuani wakifuatilia hotuba ya Mheni Rasmi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati walipokuwa katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani Jijini Arusha.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Regina Qwaray akikabidhi zawadi kwa aliyekuwa Raisi wa chama cha Wauguzi Tanzania (TANNA) katika Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani Jijini Arusha kama ishara ya kutambua mchango alioutoa Raisi huyo wakati alipokuwa kiongozi wa Chama hicho katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Regina Qwaray,akipokea maelezo kuhusu shughuli mbalimbali wanazozifanya Wauguzi katika kuwahudumia wananchi, mara baada ya Naibu Waziri huyo kutembelea mabanda ya maonesho katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC) kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Regina Qwaray akiwasili katika ukumbi wa AICC Arusha tayari kwa kuhitimisha Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika kuanzia tarehe 9 hadi 12, Mei, 2026

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Regina Qwaray,akifurahia jambo wakati alipokuwa akifuatilia Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani,yaliyofanyika katika ukumbi wa AICC jijini Arusha.









 

 


Friday, May 8, 2026

SERIKALI YATAHADHARISHA UZEMBE UPANDISHAJI VYEO WATUMISHI WA UMMA

 Na: Jawadu Kinyobwa – Arusha

Serikali imeagiza waajiri na wasimamizi wa rasilimaliwatu nchini kuhakikisha watumishi wote wenye sifa na waliotengewa bajeti ya kupandishwa Vvyeo Mei mwaka huu wanapandishwa vyeo bila kuwapo kwa ucheleweshaji wowote.

Agizo hilo linasisitiza kukamilika kwa taratibu zote za kisheria na kanuni kwa wakati, huku Serikali ikionya kuwa haitavumilia malalamiko ya watumishi ambao haki zao zinakwama kutokana na uzembe wa maafisa utawala.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete, ametoa msimamo huo wakati akifungua mkutano wa pili wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Rasilimaliwatu (AAPAM Tawi la Tanzania) jijini Arusha Mei 06, 2026.

Amebainisha kuwa Ofisi yake haitegemei kupokea malalamiko ya watumishi walioachwa wenye sifa huku akisisitiza kuwa watumishi waliojiendeleza lazima wabadilishiwe kada kulingana na miongozo iliyowekwa, kwani kufanya kinyume ni kutowajibika ipasavyo.

Waziri Kikwete ameeleza kuwa mageuzi ya utumishi wa umma yanategemea kwa kiasi kikubwa mchango wa wataalamu hao wa utawala na rasilimaliwatu.

Katika hatua nyingine, Waziri Kikwete ameagiza mabadiliko makubwa ya utendaji kazi ndani ya utumishi wa umma, akisisitiza kuwa kuanzia sasa maafisa rasilimaliwatu na utawala nchini lazima wahakikishe wanajenga usalama wa kisaikolojia kwa watumishi.

Aidha Waziri amebainisha kuwa viongozi hao wana wajibu wa kutengeneza mazingira yanayofikika ili watumishi waweze kueleza changamoto zao bila hofu, hatua itakayosaidia kuepuka msongo wa mawazo na kuimarisha afya ya akili maeneo ya kazi.

Katika msisitizo wa matumizi ya teknolojia, Waziri ameelekeza matumizi kamili ya mifumo ya kielektroniki ikiwemo e-uhamisho, ambapo amepiga marufuku matumizi ya barua za kawaida katika mchakato wa uhamisho wa watumishi.

Waziri amesisitiza pia umuhimu wa kuzingatia mwongozo wa kujitolea katika utumishi wa umma wa mwaka 2025, akitaka fursa za vijana kutolewa kwa njia ya uwazi na haki bila upendeleo wowote.

Aidha, amewataka maafisa hao kuwa viongozi wa mageuzi katika taasisi zao kwa kupunguza urasimu na kushughulikia kero za watumishi katika ngazi ya taasisi badala ya kuziacha kuwa mzigo kwa mamlaka za juu. wananchi.

Vilevile, amewaagiza wataalamu hao kuhakikisha wanazingatia uadilifu na uzalendo kwa kuepuka matumizi ya lugha zisizofaa wanapowahudumia wateja wao, jambo ambalo linaharibu taswira ya serikali.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Xavier Daudi, amesema serikali imefanya maboresho ya muundo wa maofisa rasilimali watu tangu Septemba mwaka jana, ikiwa ni pamoja na kuhuisha mitaala na kuanzisha bodi ya kitaaluma kwa maofisa hao ili kuimarisha maadili na utendaji wao.

Naye Mwenyekiti wa AAPAM tawi la Tanzania, Leila Mavika, amesema zaidi ya washiriki 1,300 wamehudhuria mkutano huo, akibainisha kuwa unatoa fursa ya kubadilishana uzoefu na kujadili changamoto za kiutendaji katika sekta ya rasilimali watu.

Kwa upande wake, Rais wa AAPAM Afrika, Dk,John Nakabago, alisisitiza umuhimu wa serikali kuwekeza katika miundombinu ya kidijitali na kuhakikisha upatikanaji wa teknolojia kwa wote ili kufanikisha mageuzi ya kidijitali

Aliongeza kuwa ni muhimu kuwajengea uwezo watumishi wa umma, hususan walioko vijijini, ili waweze kutumia teknolojia ipasavyo. Pia alihimiza ushirikiano kati ya serikali, sekta binafsi, vyuo vikuu na asasi za kiraia katika kukabiliana na changamoto za ajira kwa vijana na mazingira.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa Pili Jumuishi wa Mwaka wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania, Mei 6, 2026, Jijini Arusha.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb), akipokea maelezo kuhusu shughuli na majukumu yanayotekelezwa na Ofisi yake pamoja na yale yanayotekelezwa na eGA, wakati wa Mkutano Mkuu wa Pili Jumuishi wa Mwaka wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania, Mei 6, 2026, Jijini Arusha.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi mara baada ya kuwasili katika Mkutano Mkuu wa Pili Jumuishi wa Mwaka wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania, unaofanyika leo, Mei 6, 2026, Jijini Arusha.



Monday, May 4, 2026

AFYA NI MTAJI – KATIBU MKUU MKOMI AWASISITIZA WATUMISHI WA UMMA KUJILINDA

Na. Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 04 Mei, 2026

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi amewasisitiza watumishi wa umma kulinda na kuimarisha afya zao wakati wote ili zitumike kuwajibika ipasavyo na kuwa mtaji katika kuleta matokeo chanya Serikalini.

Bw. Mkomi ameyasema hayo leo Mei 4, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo, Mtumba Jijini Dodoma wakati akihitimisha mafunzo kuhusu fursa za mimea tiba katika kutibu magonjwa mbalimbali. 

“Ni vizuri kila mtumishi wa umma akawa na uelewa kuhusu faida za utunzaji wa afya aliyo nayo na kuchukua hatua mapema pindi anapopata changamoto ili kuitumia afya hiyo kuwa mtaji Serikalini na kuleta tija katika maslahi ya umma”. Bw. Mkomi alisema.

Amesisitiza kuwa changamoto ya watumishi wengi kuugua mara kwa mara inapunguza kasi ya utendaji, lakini watumishi wanapokuwa na afya bora, hupunguza kuomba likizo za ugonjwa, na hivyo kuongeza bidii ya kazi.

Aidha, Bw. Mkomi amemshukuru Prof. Joseph Ndunguru ambaye ni Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania, (TPHPA) kwa wasilisho lake ambalo limetoa uelewa kwa watumishi utakaojenga hamasa na kuwa nyenzo muhimu ya kuongeza ufanisi katika kazi.

Awali akiwasilisha mada kuhusu fursa za Mimea Tiba katika Kutibu Magonjwa mbalimbali, Prof. Ndunguru alisema Tanzania ina utajiri mkubwa wa mimea yenye uwezo wa kutibu magonjwa mbalimbali lakini bado inahitaji utafiti wa kisayansi ili kuthibitisha usalama na ufanisi wake.

Aliongeza kuwa matumizi ya tiba asili yaliyofanyiwa tafiti za kisayansi yanapunguza magonjwa, hivyo kuongeza kasi ya utekelezaji wa majukumu na kuboresha afya ya watumishi. 

Prof. Ndunguru ametoa wito kwa Serikali na Taasisi za Umma kuwekeza katika tafiti ili kuendeleza tiba asili na kuchangia maendeleo ya afya na uchumi wa Taifa.

Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akizungumza na watumishi wa Ofisi yake wakati alipokuwa akihitimisha mada ya mafunzo ya uelewa kwa ajili ya kuwajengea watumishi hao uwezo wa kiutendaji katika eneo maalumu la Ofisi hiyo lililopo Mtumba Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akitoa neno la shukrani kwa Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania, (TPHPA) Prof. Ndunguru kwa wasilisho ambalo limetoa uelewa kwa watumishi utakaojenga hamasa na kuwa nyenzo muhimu ya kuongeza ufanisi katika kazi.

Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania, (TPHPA) Prof. Ndunguru (kulia) akionesha vitabu ambavyo vinaelezea mikakati juu ya uhifadhi wa Mimea Tiba baada ya katibu Mkuu huyo kuhitimisha mafunzo ya uelewa  Mtumba jijini Dodoma. Katikati ni Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi

Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi wasaidizi Ofisi hiyo baada ya Katibu Mkuu huyo kuhitimisha mafunzo ya uelewa ya kila jumatatu yaliyofanyika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma.kulia kwake ni Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi na kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania, (TPHPA)

Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Ofisi hiyo baada ya mafunzo ya uelewa ya kila jumatatu yaliyofanyika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma.Kulia kwake ni Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi na kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania, (TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru

Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Ofisi hiyo baada ya mafunzo ya uelewa ya kila jumatatu yaliyofanyika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma.Kulia kwake ni Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi na kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania, (TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru

Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo kuwajengea uwezo wa kiutendaji yaliyotolewa tarehe 4 Mei, 2026 na Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania, (TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru (hayupo pichani ) katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma 

Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania, (TPHPA) Prof. Ndunguru akitoa mafunzo kuhusu fursa za mimea tiba katika kutibu magonjwa mbalimbali kwa watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI yaliyofanyika Mei 4, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijini Dodoma.

Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo kuwajengea uwezo wa kiutendaji yaliyotolewa tarehe 4 Mei, 2026 na Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania, (TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru (hayupo pichani ) katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma 


Viongozi na Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo kuwajengea uwezo wa kiutendaji yaliyotolewa tarehe 4 Mei, 2026 na Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania, (TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru (hayupo pichani ) katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma 




Katibu Mkuu-UTUMISHI (kushoto) Bw. Juma Mkomi (kushoto) akipokea pongezi kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania, (TPHPA) Prof. Ndunguru kwa kumkaribisha Mkurugenzi huyo kutoa Mafunzo ya uelewa katika Ofisi yake Mtumba Jijini Dodoma