Tuesday, April 14, 2026

WATUMISHI WA UMMA WASISITIZWA KULINDA AFYA

 Na: Eric Amani, Mtumba Dodoma

 13 Aprili, 2026

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Juma Mkomi ametoa rai kwa kila mtumishi wa umma kuhakikisha analinda afya ya mwili na akili kuanzia nyumbani kwa kuwa mtumishi mwenye afya njema anakuwa na uwezo wa kufikiri na kufanya uamuzi sahihi katika utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Rai hiyo imetolewa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Juma Mkomi wakati akiongoza kikao cha kuchagua mfanyakazi bora wa Ofisi yake kilichofanyika Aprili 13, 202katika ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma.

Bw. Mkomi aliongeza kuwa, watumishi wanapaswa kujenga utamaduni wa kujali afya zao kwa kuzingatia lishe bora, kufanya mazoezi ya mwili pamoja na kupata muda wa kupumzika ambapo masuala yote hayo huanzia katika mazingira ya nyumbani.

Watumishi wa umma wanapokuwa na afya dhaifu, utendaji kazi hushuka na hivyo kuathiri moja kwa moja utendaji kazi mahala pa kazi. Hivyo amewakumbusha watumishi hao kuwa afya njema ni msingi imara katika utekelezaji wa majukumu kwa ufanisi.

Aidha, Katibu Mkuu huyo ametumia fursa ya kikao hicho kuitakia kila la kheri Utumishi Sports Club ambayo inaelekea kwenye mashindano ya Mei Mosi yatakayofanyika mkoani Njombe.

Bw. Mkomi amewahimiza wachezaji pamoja na benchi la ufundi kujituma, kudumisha nidhamu na kuzingatia maadili ya michezo ili kuiwakilisha vyema ofisi.

Nendeni kwenye mashindano hayo muhimu na onesheni nidhamu njema na kiwango bora zaidi cha ushindani ukilinganisha na kiwango mlichoonesha wakati wa mashindano ya SHIMIWI 2025 Zingatieni nidhamu, mshikamano na ushirikiano ili kuendelea kuleta ushindi katika ofisi yetu” alisisitiza Bw. Mkomi.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw, Juma Mkomi akizungumza na maofisa wa ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakati wa kikao cha kuchagua Mfanyakazi bora katika Ofisi yake April 13, 2026 katika viwanja vya ofisi hiyo iliyopo Mtumba, Jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Ofisi ya Rais – UTUMISHI Bw. Mussa Magufuli akifungua Kikao cha kuchagua mfanyakazi bora kilichofanyika April 13, 2026 katika Viwanja vya Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi w Umma na Utawala Bora katika Mji wa Serikali Mtumba, Jijini Dodoma.

Sehemu ya Wakurugenzi na Wakurugenzi wasaidizi kutoka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Mwenyekiti (Hayupo Pichani)  wa Kikao cha Kuchagua Mfanyakazi Bora wakati anazungumza na watumishi wa ofisi hiyo kabla ya zoezi la kupiga kura kuanza April 13, 2026 Mtumba Jijini Dodoma.


Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (Aliyesimama) wakati wa akitoa neno kwenye kikao cha kuchagua Mfanyakazi Bora wa ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma April 13, 2026.


Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakipiga Kura kwa ajili ya kuchagua mfanyakazi bora katika kikao cha kuchagua Mfanyakazi Bora wa mwaka 2026 kwenye viwanja vya ofisi hiyo Aprili 13, 2026 Mtumba, Jijini Dodoma.

Picha ya Pamoja ya washiriki wa kinyang’anyiro cha Mfanyakazi Bora katika Ofisi ya Rais – UTUMISHI kutokea Kurugenzi na Idara mbalimbali zilizopo ofisi hiyo wakati wakisubiria kumchagua mfanyakazi bora wa ofisi Mtumba, Jijini Dodoma April 13, 2026.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Juma Mkomi Akimkabidhi Zawadi aliyekuwa Mtumishi wa Ofisi hiyo Bi. Maria Felix baada ya Kumaliza Muda wake wa Utumishi wa Umma katika Ofisi hiyo April 13, 2026 Mtumba, Jijini Dodoma.


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Juma Mkomi akipokea na kuzindua jezi mpya kutoka kwa nahodha wa timu ya mpira wa pete Bi. Elizabeth Fussi Aprili 13, 2026 katika viwanja vya ofisi hiyo kabla ya kuanza safari ya kuelekea Mkoani Njombe kwa ajili ya mashindano ya Mei Mosi.


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Juma Mkomi akipokea na kuzindua jezi mpya kutoka kwa nahodha wa timu ya mpira wa miguu Bw. Cyprian Lasway Aprili 13, 2026 katika viwanja vya ofisi hiyo kabla ya kuanza safari ya kuelekea Mkoani Njombe kwa ajili ya mashindano ya Mei Mosi.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Juma Mkomi  akimpongeza Bi. Gladness Mwanri kutokea Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma kwa kuchaguliwa kuwa Mfanyakazi Bora 2026 wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Aprili 13, 2026 Jijini Dodoma. 



Sehemu ya wachezaji wa timu ya mpira wa pete wakiwa katika viwanja vya ofisi ya Rais – UTUMISHI wakati wa uzinduzi wa jezi yao mpya wanaotarajia kuivaa katika mashindano ya Mei Mosi yanayofanyika Mkoani Njombe. 



Monday, April 13, 2026

WAZIRI KIKWETE AFUNGUA MKUTANO WA 13 WA KAMATI TENDAJI YA SHIRIKISHO LA MAMLAKA ZA KUPAMBANA NA RUSHWA BARANI AFRIKA ATAJA MAENEO MANNE YATAKAYOSAIDIA KUKABILIANA NA RUSHWA

 Na. Veronica Mwafisi-Arusha

Tarehe 13 Aprili, 2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema ili Afrika iweze kuwa na uwezo uliojitosheleza ni lazima kuwe na azimio endelevu la pamoja la kukabiliana na rushwa.

Mhe. Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 13 Aprili, 2026 wakati akifungua Mkutano wa 13 wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika ulioanza leo katika Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.

Waziri Kikwete ameainisha maeneo manne ya kuchukua hatua za makusudi za kukabiliana na rushwa Barani Afrika ikiwemo kuendelea kuimarisha ushirikiano mipakani kwani rushwa imekuwa ni tatizo la kimataifa ambalo linahusisha mtiririko wa fedha haramu na masuala ya kimtandao, huku akisisitiza kubadilishana habari katika maeneo ya urejeshaji wa mali na uchunguzi wa kifedha.

Amesema ni lazima kukubali kuwa teknolojia ina nguvu katika kukuza uwazi na kupunguza mianya ya rushwa ambapo mifumo ya kidijiti imeongeza uwajibikaji kwa kiasi kikubwa katika ununuzi wa umma, ukusanyaji wa mapato na utoaji wa huduma .

Amesisitiza kuwa ni lazima kukuza uongozi wa kimaadili na uadilifu katika ngazi zote za kijamii kwani vita dhidi ya rushwa huanza na maadili ambayo lazima yaonekane katika utumishi wa umma na tabia binafsi. 

Aidha, ameongeza kuwa ni muhimu kushirikisha wananchi, mashirika ya kiraia, na sekta binafsi kama washirika hai katika mapambano dhidi ya rushwa kwani suala hili sio la mtu mmoja au taasisi moja pekee.

Amesema rushwa ni kikwazo katika utoaji haki na huduma muhimu kama vile afya, elimu na miundombinu kwa wananchi wa kawaida, vilevile ni tishio katika mabadiliko ya kiuchumi na inapunguza kasi ya maendeleo katika mataifa yetu.

“Ni imani yangu kwamba mkutano huu utatumika kama jukwaa muhimu la kuimarisha ushirikiano, kubadilishana uzoefu, na kuimarisha azimio letu la pamoja katika kushughulikia mojawapo ya changamoto sugu zinazoendelea kuikabili Afrika,” Mhe. Kikwete amesisitiza.

 

Amesema katika kupambana na rushwa, Tanzania chini ya uongozi wa Rais Mhe.
Dkt. Samia Suluhu Hassan, imekuwa na dhamira thabiti ya kuendeleza uwazi,
uwajibikaji na utawala bora kwa kuimarisha mifumo ya kisheria na kitaasisi,
mifumo ya usimamizi wa fedha za umma na kuboresha utoaji wa huduma katika
sekta zote,” Mhe. Kikwete amesisitiza.

Ameongeza kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ina jukumu muhimu katika kutekeleza ajenda ya kitaifa ya kupambana na rushwa kwa kuhakikisha rasilimali za umma zinasimamiwa kwa manufaa ya wananchi wote.

Amesema kwa pamoja, tunaweza kuijenga Afrika inayofafanuliwa si kwa rushwa, bali kwa uadilifu, si kwa fursa zilizopotea, bali kwa mafanikio ya pamoja, si kwa mifumo dhaifu, bali na taasisi imara na zinazoaminika. Mkutano huu ukaashirie hatua nyingine muhimu kuelekea siku zijazo.

Akitoa neno la utangulizi, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila, amesema lengo la mkutano huo ni kujadili na kubadiliashana uzoefu kuhusu namna bora ya kukabiliana na rushwa ambalo ni tatizo kubwa katika Bara la Afrika. “Tutabadilishana uzoefu kwani tunatamani rushwa itokomezwe kabisa katika Bara la Afrika,” amesisitiza.

Wajumbe wa Kamati Tendaji ya AAACA ni Wakuu wa Mamlaka za Kuzuia na Kupambana na Rushwa kutoka Nchi 9 Wanachama ambazo ni Egypt, Mali, Cameroon, Congo Brazaville, Algeria, SieraLeone, Burundi, Zimbabwe pamoja na Tanzania.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza wakati akifungua Mkutano wa 13 wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katika Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.


Sehemu ya Washiriki wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akifungua Mkutano wa 13 wa Kamati hiyo uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katia Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.


Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila (kulia) akizungumza jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA), Bw. Ali Ali kabla ya kuanza kwa Mkutano wa 13 wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Barani Afrika uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katika Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.


Sehemu ya Washiriki wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akifungua Mkutano wa 13 wa Kamati hiyo uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katia Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akifurahia jambo na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila (kushoto) kabla Waziri huyo kufungua Mkutano wa 13 wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katika Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.


Sehemu ya Washiriki wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akifungua Mkutano wa 13 wa Kamati hiyo uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katia Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza wakati akifungua Mkutano wa 13 wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katika Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.


Sehemu ya Washiriki wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika (mstari wa mbele) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akifungua Mkutano wa 13 wa Kamati hiyo uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katia Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha. Wengine ni Watendaji na Wakurugenzi wa TAKUKURU. 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifuatilia Mkutano wa 13 wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika mara baada ya kufungua mkutano huo uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katika Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Sehemu ya Washiriki wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika mara baada ya Waziri huyo kufungua Mkutano wa 13 wa Kamati hiyo uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katika Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi, Watendaji na Wakurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mara baada ya Waziri huyo kufungua Mkutano wa 13 wa Kamati hiyo uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katika Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha. 




Friday, April 10, 2026

WAZIRI KIKWETE AISISITIZA WAKALA YA NDEGE ZA SERIKALI KUENDELEA KUSIMAMIA MISINGI IMARA ILIYOACHWA NA BODI YA USHAURI YA TAASISI HIYO ILI KULETA TIJA KWA TAIFA

 

Na. Antonia Mbwambo-Dodoma.

Tarehe 10 Aprili, 2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameisisitiza Wakala ya Ndege za Serikali kuendeleza misingi imara iliyoachwa na Bodi ya Ushauri ya Wakala hiyo hususan katika usimamizi wa rasilimali mbalimbali ili ziweze kutumika ipasavyo na kuleta tija kwa Serikali na Taifa kwa ujumla.

Mhe. Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 10 Aprili, 2026 jijini Dodoma wakati wa hafla fupi ya kuwaaga Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Ndege za Serikali iliyomaliza muda wake.

Waziri Kikwete ameishukuru na kuipongeza Bodi hiyo kwa utendaji kazi mzuri walioufanya wakati wote walipokuwa wakitekeleza majukumu yao ya kumshauri. “Kimuundo, Bodi hii ni chombo cha kumshauri Waziri. Ninakiri kuwa nimekuwa nikipata ushauri wa namna ya kuboresha ufanisi wa Wakala hii ili kuweza kufikia malengo ya Serikali na kupitia ushauri huo, malengo ya Wakala yameweza kufanikiwa na utekelezaji wa masuala mbalimbali unaendelea kufanyika kama ilivyoshauriwa,” Mhe. Kikwete amesisitiza.

Ameongeza kuwa, Bodi hiyo imekuwa ikifanya kazi kwa weledi na uzalendo pamoja na kumpa ushirikiano mkubwa katika utekelezaji wa majukumu na kufanya kazi yake kuwa nyepesi. “Nina kila sababu ya kujivunia mafanikio na hatua mbalimbali za mchango wa Bodi hii katika kufanikisha shughuli za Wakala,” ameongeza.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Ndege za Serikali, Prof. Mhandisi Idrissa Mshoro amemshukuru Waziri Kikwete kwa kuendelea kuiamini Bodi hiyo kwa kipindi chote tangu ilipoteuliwa hadi kukamilisha kipindi cha pili cha miaka mitatu.

Naye Afisa Mtendaji wa Wakala ya Ndege za Serikali, Capt. Budodi Budodi amesema Bodi hiyo ya Ushauri iliyomaliza muda wake ilizinduliwa kuhudumu kwa kipindi cha pili kuanzia mwezi Agosti, 2023 na imefikia ukomo wake kwa mujibu wa Sheria.

Capt. Budodi ameyataja majukumu ya Wakala ya Ndege za Serikali kuwa ni pamoja na kumsafirisha kwa njia ya anga Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Viongozi Wakuu wengine wa Kitaifa, kuratibu na kusimamia ununuzi na ukodishaji wa ndege za Serikali kwa Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) na kusimamia mikataba ya ukodishaji ndege hizo, kufanya matengenezo ya ndege za Serikali zinazotoa huduma kwa Viongozi Wakuu wa Kitaifa na kuhakikisha usimamizi madhubuti wa Wakala.

Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Ndege za Serikali, wakimpokea Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete mara baada ya Waziri huyo kuwasili katika hafla ya kuwaaga wajumbe hao jijini Dodoma. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyevaa miwani) akifurahia jambo wakati alipokuwa katika hafla ya kuwaaga Wajumbe wa
Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Ndege za Serikali iliyofanyika Aprili 10, 2026 jijini Dodoma. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Ndege za Serikali iliyomaliza muda wake wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wajumbe hao iliyofanyika Aprili 10, 2026 Jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Ndege za Serikali, Prof. Mhandisi Idrissa Mshoro wakati Waziri huyo alipokuwa akiwasili katika hafla ya kuwaaga wajumbe hao iliyofanyika Aprili 10, 2026 Jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji wa Wakala ya Ndege za Serikali, Capt. Budodi Budodi akitoa neno la utangulizi kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wajumbe wa Bodi hiyo Jijini Dodoma


Tuesday, March 31, 2026

MAAFISA RASILIMALIWATU WATAKIWA KUFANYA TATHMINI KWENYE SUALA LA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA

 

Na. Veronica Mwafisi na Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 01 Aprili, 2026.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw, Juma Mkomi ametoa wito kwa Maafisa Rasilimaliwatu kufanya tathmini kwenye suala la uhamisho kwa watumishi wa umma ili kuondoa vikwazo na kuongeza tija ya utendajikazi katika Utumishi wa Umma.

Bw. Mkomi ameyasema hayo leo jijini Dodoma alipokuwa akifunga mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi kwa Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma yaliyokuwa yakifanyika kwa siku tisa kuanzia tarehe 23 Machi hadi 01 Aprili, 2026 jijini Dodoma.

Bw. Mkomi amesema, uhamisho ni haki ya mtumishi na mwajiri kutaka kumtumia mtumishi fulani katika eneo fulani au ni haki ya mwajiri kuendelea kumtumia mtumishi husika sehemu anayotumikia vizuri.

Hivyo, Bw. Mkomi amewataka Maafisa Rasilimaliwatu hao kufanya tathmini katika maeneo yao ya kazi hasa katika Mfumo wa Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma (e-Msawazo)

“Nitoe msisitizo kuhusu tathmini ya mahitaji ya rasilimaliwatu, naamini ninyi ndio wasimamizi wakubwa katika maeneo mengi na ndio mnaoleta taarifa ya masuala husika ya kiutumishi, utaratibu wa uhamisho una vigezo na vinajulikana hivyo ni vema kupata usahihi wa taarifa za watumishi au mahitaji ya watumishi hao pasipo kuwa na vikwazo au mifarakano isiyokuwa na tija kwa sababu ya uhamisho,” amesisitiza Bw. Mkomi.

Aidha, Bw. Mkomi ameongeza kuwa, Maafisa Rasilimaliwatu wana jukumu la kumshauri vizuri mwajiri linapotokea suala la uhamisho kwa mtumishi ni vema kutoa vigezo sahihi baada ya kufanya tathmini ya kutosha.

“Tunatamani umwambie mwajiri uhamishio wa mtumishi huyu tusiutekeleze kwa sababu tathmini tuliyoifanya ya rasilimaliwatu katika eneo letu tuna upungufu wa afisa husika au uhamisho huu tuutekeleze kwa sababu tuna maafisa wa kutosha kadhaa kwenye eneo letu,” amesema Bw, Mkomi

Vilevile, Bw. Mkomi amesema eneo la uhamisho limeonekana kuwa na changamoto kutokana na watumishi wanaoomba uhamisho kuzuiliwa bila kuwa na sababu za kutosha.

Bw. Mkomi amewataka Maafisa hao kufanyia kazi mafunzo yote waliyoyapata watakaporudi kwenye maeneo yao ya kazi ili yakaongeze tija katika Utumishi wa Umma

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini, Bw. Hamis Mkunga amesema jumla ya washiriki 275 wamepatiwa mafunzo hayo hivyo amewataka washiriki hao kwenda kufanyia kazi ili kuleta matokeo chanya katika maeneo yao ya kazi kwa maendeleo ya ofisi au taasisi husika na taifa kwa ujumla.

Akitoa neno la shukrani Mwenyekiti wa Mafunzo hayo, Bi. Isabela Chilumba amemuahidi Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi kuwa kwa niaba ya washiriki wote watazingatia maelekezo ambayo ameyatoa ili waweze kuboresha utendaji kazi kwa ustawi wa Taifa.

 


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akizungumza na Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma wakati akifunga mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyofanyika kuanzia tarehe 23 Machi - 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.


Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini wa Ofisi hiyo Bw. Hamis Mkunga (kushoto) kabla ya kufunga Mafunzo ya Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma kuhusu Mfumo wa e-Watumishi yaliyofanyika kuanzia tarehe 23 Machi - 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 jijini Dododma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 jijini Dododma.

Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Hamis Mkunga (kushoto)  pamoja na Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya Usimamizi na Payrol Jeanfrida Mushumbusi (kulia)  wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo wakati alipokuwa akifunga mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyojumuisha Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma yaliyofanyika kuanzia tarehe 23 Machi - 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma. 

Afisa kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambaye pia ni Mkufunzi wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini wa Ofisi hiyo Bw. Hamis Mkunga (kulia), kabla ya Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) kufunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akimkabidhi cheti mmojawapo wa washiriki wa mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyojumuisha Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo hayo leo tarehe 1 Aprili, 2026 Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiteta jambo na Afisa Rasilimaliwatu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Chemba Bi. Zuhura Kizuguto baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyotolewa Jijini Dodoma kuanzia tarehe 23 Machi - 01 Aprili, 2026 kwa Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma .

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akimkabidhi cheti mmojawapo wa washiriki wa mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyojumuisha Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo hayo leo tarehe 1 Aprili, 2026 Jijini Dodoma.





 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Monday, March 30, 2026

WATUMISHI WA UMMA WAHIMIZWA KUONGEZA UWAJIBIKAJI KATIKA KUTOA HUDUMA BORA

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 30 Machi, 2026.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma                                                                                                                                     na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi amewahimiza Watumishi wa Umma kuongeza uwajibikaji katika kuwahudumia wananchi.

Bw. Daudi ametoa wito huo leo alipokuwa akiwapongeza Watumishi wa Ofisi hiyo waliozaliwa mwezi Machi, 2026 mara baada ya kuhitimishwa kwa mafunzo yanayofanyika kila siku ya Jumatatu Mtumba Jijini Dodoma kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi watumishi wa ofisi hiyo.

Bw. Daudi amesema, mtumishi wa umma anapoongeza umri imsaidie kuongeza chachu ya utendajikazi ili kutimiza malengo ya Serikali ya kutoa huduma bora kwa wananchi.

''Nitoe wito kwa Watumishi wa Umma mnapoongeza umri na kusherehekea siku yenu ya kuzaliwa, hakikisheni mnawajibika ipasavyo katika maeneo yenu ya kazi hasa mnapotoa huduma kwa Watumishi wa Umma wenzenu na Wananchi, hakikisheni kuwa mnatimiza malengo ya Serikali katika kutoa huduma bora kwa kila Mtanzania.” amesema Bw. Daudi.


Awali katika mafunzo hayo, Afisa Rasilimaliwatu Mkuu kutoka katika ofisi hiyo, Idara ya Mishahara, Maslahi na Marupurupu, Bi. Magreth Banogile akiwasilisha mada kuhusu Motisha katika Utumishi wa Umma alisema, motisha ni manufaa anayoyapata mtumishi baada ya mshahara kutokana na majukumu anayoyatekeleza hivyo ni wajibu wa kila mtumishi wa umma kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi ili aweze kupata stahiki ya motisha husika.

Ameongeza kuwa baadhi ya motisha katika Utumishi wa Umma ni pamoja na mazingira bora ya kazi, vitendea kazi, fursa za mafunzo, huduma ya usafiri wa kwenda na kurudi kutoka kazini, pamoja na fursa ya muda wa kufanya mazoezi.

Aidha, katika mafunzo hayo kulikuwa na mada mbalimbali zilizowasilishwa na Maafisa kutoka katika Idara hiyo ya Mishahara, Maslahi na Marupurupu ambapo Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi Bw. Baraka Kilagu aliwasilisha mada kuhusu Miundo ya Maendeleo ya Utumishi chini ya Wizara pamoja na Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi, Bw. Imani Mtumbi aliyewasilisha mada kuhusu Miundo ya Mishahara katika Utumishi wa Umma.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi (wa tano kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa ofisi hiyo waliokuwa wakiadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa kwao mwezi Machi, 2026. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Musa Magufuli.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akifurahia jambo alipokuwa akizungumza na Watumishi wa ofisi hiyo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yanayofanyika kila Jumatatu kwenye Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Miundo ya Maendeleo ya Utumishi chini ya Wizara wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika ofisi hiyo jijini Dodoma.


Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Idara ya Mishahara, Maslahi na Marupurupu, Bw. Baraka Kilagu (aliyesimama) akiwasilisha mada kuhusu Miundo ya Maendeleo ya Utumishi chini ya Wizara wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika ofisi hiyo jijini Dodoma. Waliokaa wa kwanza kulia ni Afisa Rasilimaliwatu Mkuu kutoka ofisi hiyo Bi. Magreth Banogile na katikati ni Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi, Bw. Imani Mtumbi


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Miundo ya Mishahara katika Utumishi wa Umma wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo ambayo hufanyika katika ofisi hiyo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Miundo ya Mishahara katika Utumishi wa Umma wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo ambayo hufanyika katika ofisi hiyo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika ofisi hiyo jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Musa Magufuli (aliyesimama) akizungumza jambo kabla ya kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi kuzungumza na Watumishi wa ofisi hiyo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji yaliyofanyika katika ofisi hiyo jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Miundo ya Mishahara katika Utumishi wa Umma wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo ambayo hufanyika katika ofisi hiyo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Mhasibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Tumwimbilege Ilomo akikata keki kwa niaba ya Watumishi wa ofisi hiyo wanaoadhimisha  kumbukizi ya kuzaliwa kwao mwezi Machi, 2026.


Mhasibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Tumwimbilege Ilomo (kulia) akimlisha keki Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Maadili, Bi. Felister Shuli (kushoto) kwa niaba ya Watumishi wote waliozaliwa Mwezi Machi, 2026.