Monday, August 17, 2026

WATUMISHI WAPATIWA ELIMU KUHUSU HATI YA KUSAFIRI, NAIBU KATIBU MKUU LWANGILI ASISITIZA UMUHIMU WA MAFUNZO YA MARA KWA MARA KUJENGA UTUMISHI WA UMMA WENYE WELEDI

 Na Eric Amani, Jijini Dodoma

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili, amesisitiza umuhimu wa mafunzo ya mara kwa mara kwa watumishi wa Umma, akieleza kuwa mafunzo hayo ni muhimu katika kuongeza maarifa na ujuzi, kujenga uwezo na kuwawezesha watumishi kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na weledi.

Bi. Lwangili ameyasema hayo leo wakati akihitimisha mafunzo yaliyohusu uelewa na maarifa ya watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu hati ya kusafiri, ikiwemo taratibu za kuomba, kupata na kutumia hati hiyo kwa usahihi yaliyofanyika leo Agosti 17, 2026, katika eneo la wazi la Ofisi hiyo jijini Dodoma.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, Naibu Katibu Mkuu Lwangili amesema kuwa kuendelea kuwawezesha watumishi kupata elimu na ujuzi katika maeneo mbalimbali ni sehemu ya juhudi za Serikali za kujenga Utumishi wa Umma wenye weledi, ufanisi na unaozingatia viwango vya ubora katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Awali akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Mrakibu Msaidizi wa Uhamiaji, Bw. Segere Zonzo, amewakumbusha watumishi umuhimu wa kuwa na uelewa sahihi wa taratibu za kupata na kutumia hati ya kusafiri.

Bw. Zonzo amesema kuwa uelewa huo utawawezesha watumishi kuzingatia taratibu na kutumia hati hiyo kwa usahihi, hivyo kurahisisha safari zao za nje ya nchi, hususan wanaposafiri kwa ajili ya kutekeleza majukumu ya kikazi au shughuli binafsi.

Mafunzo hayo ni sehemu ya utaratibu wa Ofisi ya Rais – Utumishi wa kuwawezesha watumishi kuendelea kujifunza na kupata elimu kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu Utumishi wa Umma, sambamba na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Prisca Lwangili akizingumza na watumishi wa ofisi hiyo (hawapo pichani) mara baada ya mafunzo ya kuongeza uwezo yanayofanyika kila jumatatu katika ukimbi wa ofisi hiyo, Agosti 17, 2026


Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma Bw. Baraka Manono akizingumza na watumishi wa ofisi hiyo (hawapo pichani) kabla kuanza kwa mafunzo ya kuongeza uwezo yanayofanyika kila jumatatu katika ukimbi wa ofisi hiyo, Agosti 17, 2026


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Prisca Lwangili akiwa na Wakurugenzi na Wakurugenzi wasaidizi wakipata elimu juu ya hati ua kusafiri Agosti 17, 2026.


Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Rais – UTUMISHI wakipatiwa elimu kuhusu hati ya kusafiri kutoka kwa Afisa wa Idara ya uhamiaji Mrakibu Msaidizi Bw. Segere Zonzo (Hayupo pichani) Agosti 17, 2026 katika ukumbi wa ofisi hiyo.



Mrakibu Msaidizi wa Idara ya Uhamiaji Bw. Monge Mnzava akitoa elimu kuhusu hati ya kusafiri kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais – UTUMISHI wakati wa mafunzo ya kuongeza uwezo katika ofisi hiyo.


Mrakibu Msaidizi wa Idara ya Uhamiaji Bw. Segere Zonzo akitoa elimu kuhusu hati ya kusafiri kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais – UTUMISHI wakati wa mafunzo ya kuongeza uwezo katika ofisi hiyo.



 

Friday, August 14, 2026

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YAIPONGEZA TASAF KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO, YASISITIZA KUENDELEZA UWAZI NA UWAJIBIKAJI KATIKA KUFIKIA WALENGWA WALIOKUSUDIWA ILI KUTIMIZA MALENGO YA PSSN III

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 14 Agosti, 2026 

Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imepokea taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III) na kutoa maelekezo ya kuendeleza misingi ya utekelezaji wenye ufanisi, uwazi na uwajibikaji katika kufikia walengwa waliokusudiwa na kutimiza malengo ya PSSN III.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amezungumza hayo leo tarehe 14 Agosti, 2026 Bungeni jijini Dodoma alipokuwa akiongoza kikao cha Kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kilicholenga kupokea taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).

Vilevile, Mhe. Dkt. Ndumbaro ameipongeza TASAF kwa utekelezaji mzuri wa Miradi ya Maendeleo ikiwemo ujenzi kwenye sekta ya elimu na afya.

“Kwa niaba ya Kamati yangu nitoe pongezi nyingi kwa ofisi hii, kwa hakika mnafanya kazi nzuri katika mpango wa kunusuru kaya maskini, lakini pia mnatekeleza vizuri Miradi ya Maendeleo ikiwemo ujenzi  kwenye sekta ya elimu na afya, mnamwakilisha vizuri Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika utekelezaji wa miradi hii’’ Amesema Mhe. Dkt. Ndumbaro

Awali akiwasilisha kwa Kamati hiyo taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III), Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray amesema, PSSN III iliidhinishwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Benki ya Dunia tarehe 10 Aprili 2026, na kwa sasa ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha maandalizi kabla ya kuanza utekelezaji.

Naibu Waziri Qwaray amesema kuwa, katika maandalizi ya utekelezaji wa PSSN III, hatua muhimu zimekamilika ikiwemo kukamilisha usanifu wa Mpango, kuandaa nyaraka mbalimbali za utekelezaji, miongozo ya kiutendaji na kuimarisha mifumo ya TEHAMA inayosimamia shughuli za Mpango.

Aidha ameongeza kuwa, mchakato wa utambuzi wa Mamlaka za Maeneo ya Utekelezaji yatakayoshiriki kwenye utekelezaji wa Mpango unaendelea na unaojumuisha timu ya wataalamu kutoka TASAF, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar (OCGS), pamoja na wataalamu wa mazingira ambapo uchambuzi na uchakataji huo utazingatia viwango vya umaskini katika ngazi ya Halmashauri pamoja na viashiria vya athari za kimazingira, ikiwemo uwezekano wa maeneo kuathiriwa na mabadiliko ya tabianchi na majanga mbalimbali.

Vilevile, Mhe. Qwaray amesema kupitia mpango huo unatarajiwa kuongeza uwezo wa kaya maskini na zilizo katika mazingira hatarishi kukabiliana na changamoto za kiuchumi, kijamii na kimazingira, kuongeza ujuzi na taaluma kwa vijana kutoka kaya maskini na zinazoishi katika mazingira hatarishi zitakazoweza kujiajiri na kuajiriwa, kuwa na masijala ya kitaifa (kanzi data) yenye taarifa muhimu ya kaya maskini na zilizopo katika mazingira hatarishi pamoja na urasimishwaji wa TASAF kama taasisi ya umma ya kutekeleza na kusimamia utoaji wa huduma za msaada ya kijamii itakayohakikisha uendelevu, ufanisi na uratibu wa utoaji wa huduma hizo nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bw. Shedrack Mziray ameishukuru Kamati hiyo kwa maoni na ushauri mbalimbali ambao wameutoa na kuahidi kufanyia kazi ili kuimarisha na kuboresha utendaji kazi wa Taasisi hiyo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akisisitiza jambo wakati wa kikao cha Kamati yake kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kilicholenga kupokea taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (aliyesimama kulia) akiwasilisha kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III). Wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akifurahia jambo wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bw. Shedrack Mziray akisikiliza maoni kutoka kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo Bungeni jijini Dodoma na Watendaji hao kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Nyamizi Mhoja akiwasilisha hoja kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).

Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Sikudhani Chikambo akiwasilisha hoja kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akifafanua hoja Bungeni jijini Dodoma wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (kulia) akiteta jambo na Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (kushoto) wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).

Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (aliyesimama) akifafanua hoja iliyowasilishwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bw. Shedrack Mziray (kulia) akiandika maoni yaliyokuwa yakiwasilishwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III). Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, SACP. Ibrahim Mahumi. 


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (aliyesimama mbele) akiwasilisha kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III). Wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora.


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Saashisha Mafuwe akiwasilisha hoja kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Yohana Msita akiwasilisha hoja kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).

Sehemu ya Wakurugenzi na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza kwenye kikao Bungeni jijini Dodoma mara baada ya Watendaji wa ofisi hiyo kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).

Sehemu ya Wakurugenzi Wasaidizi na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza kwenye kikao Bungeni jijini Dodoma mara baada ya Watendaji wa ofisi hiyo kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).






Thursday, August 13, 2026

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YAIELEKEZA SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA KUTOA HUDUMA KIDIJITI

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 13 Agosti, 2026


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imepokea taarifa ya utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambapo imeielekeza Taasisi hiyo kujikita zaidi kidijiti katika utoaji wa huduma mbalimbali kuhusu namna Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma inavyofanya kazi jambo ambalo litawasaidia Viongozi wanaowajibika chini ya Sheria ya Maadili kuhusu Ujazaji wa Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni pamoja na Hati ya Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi wa Umma na Uwajibikaji wa pamoja ili waweze kukamilisha kwa wakati taarifa zitakazohitajika katika ujazaji wa fomu hizo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro ametoa kauli hiyo leo jijini Dodoma alipokuwa akihitimisha kikao cha Kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kilichokuwa na lengo la kupokea taarifa ya Utendaji wa Taasisi hiyo kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa maadili ya Viongozi wa Umma ikiwemo uhakiki wa uzingatiaji wa ahadi za uadilifu, tamko la mali na madeni na ushughulikiaji wa malalamiko na mashauri.

Mhe. Dkt Ndumbaro pia amesisitiza suala la kuongeza juhudi za kutoa elimu zaidi ya namna ya kujaza fomu mbalimbali za Maadili kwa Viongozi ili kuepukana na changamoto ya kuchelewesha ujazaji wa taarifa kwani, kuna baadhi ya Viongozi wanakuwa wapya katika uongozi hivyo inawalazimu kupewa uelewa mpana utakaowaongoza katika ujazaji wa fomu hizo.

Ameongeza kuwa, utoaji wa elimu zaidi utasaidia jamii kuona namna Taasisi hiyo inavyofanya kazi kubwa kwa maendeleo ya nchi.

“Ni vema kuongeza elimu zaidi kuhusu ujazaji wa fomu za maadili kwa Viongozi wanaowajibika chini ya sheria ili kuepukana na changamoto mbalimbali, wakati mwingine tunapata Viongozi wapya ambao hawana uelewa mpana juu ya ujazaji wa fomu hizo, hivyo elimu itakapotolewa itasaidia kupunguza changamoto hizo na kujaza kwa wakati fomu husika lakini pia elimu hiyo itawapa wananchi uelewa zaidi wa namna Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma inavyotekeleza majukumu yake kwa ufanisi,’’ Amesema Mhe. Dkt. Ndumbaro

Akiwasilisha taarifa hiyo, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, Naibu Waziri wa ofisi hiyo, Mhe. Regina Qwaray amesema Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ina jukumu la kusimamia tabia na mienendo ya Viongozi wa Umma ili kukidhi matakwa ya Sheria ya Maadili.

Mhe. Qwaray amesema, Majukumu ya Msingi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ni pamoja na kupokea na kufanya uhakiki wa Matamko ya Viongozi wa Umma kuhusu Rasilimali, kufanya utafiti juu ya hali ya Maadili na kushauri na kuweka mikakati katika masuala yanayohusu Uadilifu nchini, kufanya uchunguzi kuhusu ukiukwaji wa maadili yaliyotajwa na Sheria, kupokea na kushughulikia malalamiko na taarifa za ukiukwaji wa Maadili kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kutoka kwa wananchi pamoja na kutoa elimu ya Maadili kwa Viongozi wa Umma.

Naibu Waziri Qwaray ameongeza kuwa, Katika kipindi cha Julai 2025 hadi Juni 2026, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imetekeleza kazi za usimamizi na ushughulikiaji wa maadili ya viongozi wa umma ikiwemo uhakiki wa uzingatiaji wa ahadi za uadilifu, tamko la mali na madeni na ushughulikiaji wa malalamiko na mashauri pamoja na kusaini hati husika pindi viongozi wanapoteuliwa, kuajiriwa au kuchaguliwa

Pia Mhe. Qwaray amesema, elimu ya maadili itaendelea kutolewa katika shule na vyuo kupitia klabu za maadili ili kuweza kujenga na kuimarisha maadili ya kitaifa na kuyafanya yawe sehemu ya jamii pamoja na kuzuia mmomonyoko wa maadili nchini pamoja na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu Sheria ya Ulinzi wa watoa taarifa ambayo inamhakikishia usalama na ulinzi.

Akitoa neno la shukrani kwa Kamati hiyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kwa kuendelea kutoa miongozo na maelekezo ya kiutendaji ambayo yanaongeza chachu na ufanisi katika kuboresha na kuimarisha utendaji kazi na kuleta tija katika kuwahudumia Viongozi na Wananchi kwa lengo la kujenga na kuimarisha Utawala Bora nchini.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria ikiwa katika kikao na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Taasisi hiyo kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (wa kwanza kushoto) akifuatilia taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakati wa kikao cha Kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Taasisi hiyo kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifafanua hoja Bungeni jijini Dodoma wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiwasilisha kwa Kamati ya  Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma wakati wa kikao kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma. 


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Aziza Ally (wa kwanza kulia) akiwasilisha hoja kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa kikao kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma.

Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa na Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa ofisi hiyo kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.


Kamshina wa Maadili Mhe. Jaji (Mst.) Sivangilwa Mwangesi (katikati), akiandika maoni yaliyokuwa yakiwasilishwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo Bungeni jijini Dodoma na Watendaji hao kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Taasisi hiyo kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.




Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Yahaya Nawanda (katikati) akiwasilisha hoja kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa kikao kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Nyamizi Mhoja akifuatilia jambo wakati wa kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Mariam Yahya (wa kwanza kushoto) akiwasilisha hoja kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa kikao kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma.


Watendaji na Maafisa wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa na Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa ofisi hiyo kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.

 



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) akisikiliza hoja zilizokuwa zikiwasilishwa na sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa ofisi hiyo kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma. Wa kwanza kushoto ni Naibu Waziri wa ofisi yake Mhe. Regina Qwaray.


Watendaji na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza Bungeni jijini Dodoma kwenye kikao cha Kamati hiyo na Ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.