Tuesday, July 28, 2026
Monday, July 27, 2026
KAPINGA AHIMIZA WATUMISHI WA UMMA KUTUMIA KUWEKEZA KUPITIA MFUMO WA e-WEKEZA
Na. Eric Amani, Dodoma
27 Julai, 2026
Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Cyrus Kapinga, amewahimiza watumishi wa umma nchini kujenga utamaduni wa uwekezaji kwa kutumia mfumo wae-Wekeza kwa kuwa ni mfumo salama na wenye uwazi katika uwekezaji unakuza kipato.
Bw. Kapinga ametoa wito huo leo, Julai 27, 2026, wakati wa mafunzo ya kila Jumatatu yanayoandaliwa na Ofisi hiyo na kufanyika katika eneo maalum la mafunzo Mtumba, Jijini Dodoma.
Bw. Kapinga aliongeza kuwa uwekezaji ni nguzo muhimu ya kujenga ustawi wa kifedha wa mtumishi wa umma, hivyo ametoa rai kwa kila mtumishi wa umma kutumia fursa zilizopo ili kuweka akiba, kuongeza kipato na uwezo wa kukabiliana na changamoto za kiuchumi zinazoweza kumfanya mtumishi kushindwa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.
“Ni muhimu kwa mtumishi wa umma kujenga tabia ya kuwekeza mapema na taratibu kupitia mfumo wa e-Wekeza ili kuimarisha ustawi wa kifedha,” alisema Bw. Kapinga.
Bw. Kapinga amesema matumizi ya teknolojia kupitia mfumo wa e-Wekeza yameondoa vikwazo vilivyokuwa vinawakabili wawekezaji wengi kwa kuwawezesha kupata huduma za uwekezaji mahali popote walipo bila kulazimika kufika katika ofisi za taasisi husika.
Kwa upande wao, wataalamu kutoka Watumishi Housing Investments (WHI), ambao ndio wasimamizi wa mfumo wa e-Wekeza, walieleza kuwa mfumo huo umeundwa ili kurahisisha ushiriki wa watumishi wa umma katika uwekezaji kwa njia ya kidijiti.
![]() |
Afisa
Masoko Kutokea Watumishi Housing Investment (WHI) Bw, Jafari Yakubu akiwasilisha
mada ya uwekezaji katika mfuko wa Pamoja (FAIDA FUND) kupitia dirisha la e-
Wekeza (WATUMISHI PORTAL) kwa watumishi wa Ofisi ya Rais - UTUMISHI wakati
wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa
Serikali Mtumba, jijini Dodoma. |
Wednesday, July 22, 2026
WARATIBU WA KUDHIBITI VVU, UKIMWI NA MAGONJWA SUGU YASIYOAMBUKIZA WATAKIWA KUTOA ELIMU JUU YA UDHIBITI MAGONJWA MAHALI PA KAZI ILI KUFIKIA MALENGO YA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050
Veronica Mwafisi -Dodoma
Tarehe 22 Julai, 2026
Waratibu
wa ngazi ya Mikoa Mahali
pa Kazi katika Utumishi wa Umma wametakiwa Kutoa elimu kwa watumishi wa umma juu ya udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa
Yasiyoambukiza ili kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050
inayolenga kujenga taifa lenye watu wenye afya, tija, ustawi na ufanisi ambao watatoa
huduma bora kwa wananchi.
Kauli
hiyo imetolewa leo na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya
Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu
ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles
Kato wakati akifungua semina elekezi kwa Waratibu wa ngazi ya Mikoa
kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika
Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.
Dkt.
Kato amesema katika kutekeleza afua za kuimarisha afya kwa watumishi ni vema
kuwa na program za upimaji wa afya pamoja na mazoezi ya viungo kwa watumishi
katika maeneo yao ya kazi ili kufikia utekelezaji huo wa Dira 2050.
Ameongeza
kuwa, itakuwa vema kuandaa mafunzo pia kwa watumishi pamoja na msaada wa
kisaikolojia ili kuwasaidia zaidi katika utekelezaji wa majukumu yao.
Aidha,
Dkt. Kato amewataka waratibu hao kuandaa taarifa za utekelezaji wa
Mwongozo na Waraka Na. 2 wa mwaka 2014 kuhusu kudhibiti VVU, UKIMWI na Magonjwa
Yasiyoambukiza Mahali pa Kazi katika Utumishi wa Umma ikiwa ni pamoja na
kuwajengea uwezo.
Kwa upande wake, Kaimu
Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii ambaye ni Afisa Ustawi
wa Jamii Mkuu, Bi. Herieth Mpili akitoa neno la utangulizi kabla ya
kumkaribisha mgeni rasmi amesema kuwa lengo la semina hiyo ni kukuza uelewa na
ufahamu juu ya majukumu ya Waratibu hao na kuwawezesha kuandaa mipango ya muda
mrefu na mfupi wa utekelezaji wa afua za kudhibiti Magonjwa Yasiyoambukiza
Mahali pa Kazi katika Utumishi wa Umma ili kuleta ufanisi katika utekelezaji wa majukumu kama
ilivyokusudiwa na Serikali.
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora itaendelea kushirikiana na Sekretarieti za Mikoa yote
nchini kwa lengo la kusimamia masuala ya Anuai za Jamii na kutoa mafunzo kwa
maafisa au waratibu watakaoteuliwa kuratibu afua hizo katika mikoa yao ili
kuhakikisha kunakuwa na afya imara na ustawi wa watumishi wote nchini.
Kaimu
Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi
Msaidizi Sehemu ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato akizungumza
na Waratibu wa ngazi ya Mikoa wakati wa semina elekezi kuhusu udhibiti
wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa
Umma iliyofanyika jijini
Dodoma.
Sehemu ya Waratibu
wa ngazi ya Mikoa wakimsikiliza, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya
Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu
ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato wakati
akifungua semina
elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa
Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.
Sehemu ya Waratibu
wa ngazi ya Mikoa wakimsikiliza, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya
Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu
ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato wakati
akifungua semina
elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa
Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.
Kaimu
Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii ambaye ni Afisa Ustawi
wa Jamii Mkuu, Bi. Herieth Mpili akitoa neno la utangulizi kabla ya
kumkaribisha Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI,
Dkt. Charles Kato kuzungumza na Waratibu wa ngazi ya Mikoa wakati wa semina
elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa
Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.
Afisa Maendeleo ya Jamii, Sehemu
ya Menejimenti Anuai za Jamii,
Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Neema Range akifafanua jambo wakati akiwasilisha
mada kuhusu Anuai za Jamii na Ujumuishwaji wa Mwongozo Wa Kudhibiti VVU, UKIMWI
na MSY na Waraka (2014) kwa Waratibu wa ngazi ya Mikoa wakati wa semina elekezi kuhusu
udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika
Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.
Bingwa
wa Afya ya Akili kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Dkt. Garvin
Kweka akisisitiza jambo wakati akiwasilisha mada kuhusu Afya ya Akili kwa Waratibu
wa ngazi ya Mikoa wakati
wa semina elekezi iliyoandaliwa na Sehemu ya
Menejimenti Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI kuhusu udhibiti wa VVU,
UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma
iliyofanyika jijini Dodoma.
Sehemu ya
Waratibu wa ngazi ya Mikoa wakifuatilia mada
mbalimbali wakati wa semina elekezi iliyoandaliwa na
Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI kuhusu udhibiti wa
VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma
iliyofanyika jijini Dodoma.
Mratibu
wa ngazi ya Mkoa kutoka Kagera ambaye ni Afisa Rasilimaliwatu Mkuu, Bw. Emily
Ishegoma akiwasilisha maoni yake wakati wa majadiliano kwenye semina elekezi
iliyoandaliwa na Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI
kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika
Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.
Mwakilishi
kutoka Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania, Dkt. Theresiaglory Tety akifafanua
jambo alipokuwa akiwasilisha mada kuhusu Hali Halisi kuhusu VVU na UKIMWI wakati
wa semina elekezi kwa Waratibu wa ngazi ya Mikoa iliyoandaliwa
na Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI kuhusu udhibiti
wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa
Umma iliyofanyika jijini Dodoma.
Kaimu
Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni
Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato (katikati) akiwa katika picha ya pamoja
na Waratibu wa ngazi ya Mikoa mara baada ya
kufungua semina elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa
Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini
Dodoma.
Kaimu
Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni
Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato (katikati) akiwa katika picha ya pamoja
na Waratibu wa ngazi ya Mikoa mara baada ya
kufungua semina elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa
Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini
Dodoma.
Maafisa
kutoka Idara ya Uendelezaji Sera, Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii,
Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia jambo wakati wa semina elekezi kwa Waratibu
wa ngazi ya Mikoa kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza
Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.
Kaimu
Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni
Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato (katikati) akiwa katika picha ya pamoja
na Sekretarieti kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI mara
baada ya kufungua semina elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa
Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini
Dodoma.
Sehemu ya Waratibu
wa ngazi ya Mikoa wakimsikiliza, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya
Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu
ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato wakati
akifungua semina
elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa
Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.
Monday, July 20, 2026
DAFTARI LA HUDUMA ZA SERIKALI (GSD) KUIMARISHA UTOAJI WA HUDUMA ZA UMMA KWA NJIA YA KIDIJITI
Na. Veronica Mwafisi-Dodoma
Tarehe
20 Julai, 2026.
Daftari la Huduma za Serikali (GSD) ni Mfumo
wa kidijitali ambao unalenga kuwapatia wananchi, wafanyabiashara na wageni
fursa taarifa na maombi ya huduma za serikali katika Wizara, Idara, Wakala,
Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa hivyo, kurahisisha utoaji
wa huduma kwa umma kwa njia ya kidijiti.
Hayo yameelezwa leo na Kaimu Mkurugenzi
Msaidizi, Sehemu ya Mifumo na Viwango vya Kimenejimenti kutoka Idara ya
Uendelezaji Taasisi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Noah Mkasanga wakati
akiwasilisha mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali kwenye mafunzo ya
kuwajengea uwezo Watumishi wa Ofisi hiyo iliyopo Mtumba Jijini Dodoma.
Bw. Noah amesema kuwa, kupitia mfumo wa GSD wananchi wataweza kupata huduma
zote za Serikali kidijitali kupitia dirisha moja, ikiwa ni pamoja na kuona
huduma zinazotolewa, gharama zake, masharti au vitu vinavyohitajika ili kupata
huduma na namna ya kuzipokea hata wakiwa nyumbani kwa kutumia anwani za makazi
(NAPA).
“Daftari hili linarahisisha utoaji wa huduma mbalimbali
za Serikali kwa umma kupitia dirisha moja kwa kuainisha huduma zote
zinazotolewa na taasisi za umma pamoja na mahitaji yao na kuziweka wazi kwa
wananchi wanapotaka kupata huduma husika kwa njia ya kidijiti”, amesema Bw. Noah.
Akifafanua
kuhusu umuhimu wa Daftari la Huduma za Serikali (GSD) Bw. Noah amesema, litaongeza
ufanisi na uwajibikaji ikiwa ni pamoja na kupunguza gharama kwa wateja na
urahisi wa kutoa huduma kupitia mfumo mmoja.
Kadhalika,
Bw. Noah, amesema kuwa Daftari la Huduma za Serikali (GSD) litasaidia
kupunguza mianya ya rushwa kwa kuwa huduma hiyo inatolewa kwa njia ya
kidijitali.
Kuanzishwa kwa Daftari la Huduma za Serikali (GSD) ni jitihada za Serikali za kutumia teknolojia ya kisasa katika
kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi na kuimarisha usalama wa taarifa za
umma.
Kaimu Mkurugenzi
Msaidizi, Sehemu ya Mifumo na Viwango vya Kimenejimenti kutoka Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Noah Mkasanga akiwasilisha mada kuhusu Daftari la Huduma za
Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika kila Jumatatu kwa
watumishi hao katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi Wasaidizi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Kaimu Mkurugenzi
Msaidizi, Sehemu ya Mifumo na Viwango vya Kimenejimenti kutoka Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Noah Mkasanga akifafanua jambo kuhusu Daftari la Huduma za
Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika kila Jumatatu kwa
watumishi hao katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi Wasaidizi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi, Wakurugenzi Wasaidizi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi
ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakiwa
katika mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji
wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakiwa katika mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Friday, July 17, 2026
Monday, July 13, 2026
KATIBU MKUU MKOMI AWATAKA WATUMISHI KUONGEZA KASI YA UTENDAJI KUFIKIA MALENGO YA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050
Na. Antonia Mbwambo – Dodoma
13 Julai, 2026
Katibu
Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, amewataka Watumishi wa Umma
kuongeza kasi ya utendaji na kuzingatia weledi ili kuchangia kikamilifu katika
utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Katibu
Mkuu Mkomi ametoa wito huo leo Julai 13, 2026, wakati akihitimisha mafunzo
kuhusu umuhimu wa afya ya akili kwa Watumishi wa Umma yaliyofanyika katika eneo
maalumu la Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Mtumba, jijini Dodoma kwa lengo la
kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi hao.
Bw.
Mkomi amesema mafanikio ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050
yanategemea uwepo wa Watumishi wa Umma wenye afya bora ya akili, maadili ya
kazi, ubunifu na uwajibikaji, huku akisisitiza kuwa afya ya akili ni msingi wa
utendaji wenye tija na utoaji wa huduma bora Serikalini.
"Afya
ya akili si suala la mtu mmoja mmoja, bali ni msingi wa kuongeza tija katika Utumishi
wa Umma. Mtumishi mwenye afya bora ya akili anakuwa na uwezo mkubwa wa kutoa
huduma bora, kushirikiana na wenzake na kuleta matokeo chanya kwa Taasisi na
Taifa kwa ujumla," amesema Bw. Mkomi.
Aidha,
Bw. Mkomi amewaelekeza Wachumi wa Ofisi hiyo kufanya tafakuri za kitaaluma na
kuibua mawazo bunifu yatakayochangia Serikali kufikia malengo ya Dira ya Taifa
ya Maendeleo 2050.
Kwa
upande wake, Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma,
Dkt. Elihuruma Elias, ambaye alikuwa Mwezeshaji wa mafunzo hayo, amesema afya
ya akili ni nguzo muhimu ya ustawi wa mtumishi na ina mchango mkubwa katika
kuongeza tija pamoja na kuboresha mazingira ya kazi.
Ameeleza
kuwa changamoto za afya ya akili kwa watumishi wa Umma mara nyingi husababishwa
na mpangilio duni wa kazi, mzigo mkubwa wa majukumu unaozidi uwezo wao, kazi za
kujirudia rudia na mazingira magumu ya kazi. Amewahimiza watumishi kuzingatia
mtindo bora wa maisha kwa kufanya mazoezi ya mara kwa mara, kula lishe bora,
kupata mapumziko ya kutosha na kutafuta ushauri wa Wataalamu wanapokabiliwa na
changamoto za afya ya akili.
Aidha,
Dkt. Elias amewataka viongozi kuendelea kuzingatia usawa kwa watumishi
wanaowasimamia, kupinga unyanyapaa dhidi ya wenye changamoto za afya ya akili
na kutambua mapema dalili za changamoto hizo ili kuwawezesha watumishi kupata
huduma stahiki kwa wakati.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akifurahia jambo wakati alipokuwa akihitimisha mafunzo ya uelewa kwa Watumishi wa Ofisi hiyo Julai 13, 2026 Mtumba Jijini Dodoma
Katibu
Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, akizungumza na Watumishi wa
Ofisi yake wakati alipokuwa akihitimisha Mafunzo ya uelewa kuhusu Umuhimu wa
Afya ya Akili kwa Watumishi wa Umma yaliyofanyika Julai 13, 2026 katika eneo
maalumu la Ofisi hiyo, Mtumba jijini Dodoma
Baadhi
ya Wakurugenzi kutoka Idara na Vitengo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa
Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo
pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika
eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma.
Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma
Bingwa
wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma
Elias akitoa mada ya mafunzo kuhusu Umuhimu wa Afya ya Akili kwa Watumishi wa Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora yaliyofanyika Julai
13, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Jijini Dodoma
Baadhi
ya Wakurugenzi kutoka Idara na Vitengo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa
Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo
pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika
eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma.
Bingwa
wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma
Elias akitoa mada ya mafunzo kuhusu Umuhimu wa Afya ya Akili kwa Watumishi wa Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora yaliyofanyika Julai
13, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Jijini Dodoma
Baadhi
ya Wakurugenzi kutoka Idara na Vitengo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa
Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo
pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika
eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma.
Baadhi
ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka
Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa
mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.
Baadhi
ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka
Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa
mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.
Baadhi
ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka
Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa
mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.
Sunday, July 12, 2026
ZIARA YA KIKAZI YA MHE. RIDHIWANI KIKWETE MKOANI TABORA
YALIYOJIRI KATIKA ZIARA YA KIKAZI YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA, MHE. RIDHIWANI KIKWETE ILIYOLENGA KUKAGUA NA KUZINDUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI TABORA























































