Monday, April 27, 2026

WATUMISHI WALIOZALIWA MWEZI APRILI WAPONGEZWA

 Na. Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 27 Aprili, 2026

Mkurugenzi Msaidizi Anuai za Jamii na Mratibu wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza wa Ofisi hiyo Bi. Mwanaamani Mtoo niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI amewapongeza na kuwatakia kila la kheri watumishi wawote waliozaliwa mwezi Aprili ambapo kwa kumbukizi hiyo wamepata nafasi ya kukata keki kama ishara ya kuendeleza umoja na mshikamano ili kuimarisha utendaji kazi.

Matukio mbalilmbali ya picha za watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, waliokuwa wanaadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa ya mwezi Aprili, yaliyofanyika katika Ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma


















MKURUGENZI OFISI YA RAIS UTUMISHI AAGWA RASMI

 Na. Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 27 Aprili, 2026

Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Taasisi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Nolasco Kipanda kwa niaba ya Katibu Mkuu na Watumishi wote wa Ofisi hiyo amemuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu wa Ofisi hiyo Bi. Mariam Mwanilwa ambaye amestaafu kwa kwa mujibu wa Sheria.

Bw. Kipanda ameyasema hayo Aprili 27, 2026 katika eneo maalum la mafunzo lililopo katika ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.

Amesema, Ofisi ya Rais-Utumishi itamkumbuka Mkurugenzi huyo kwa upendo wake, umahiri, ujasiri, mchango na kazi nzuri aliyoifanya ya kuleta tija katika utumishi wa Umma.

Kwa upande wake, Bi. Mwanilwa amewaasa watumishi hao kufanya kazi kwa umoja na kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ya utumishi wa umma ili kutoa huduma kwa haki na usawa.

Bi. Mwanilwa aliwasisitiza watumishi wa umma kufanya kazi kwa kujituma huku wakizingatia maadili ya utendaji ili kuufikia mwisho mwema wa utumishi wao.


Wakurugenzi wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma wakimkabidhi kwa niaba ya Katibu Mkuu –UTUMISHI keki aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu wa Ofisi hiyo Bi. Mariam Mwanilwa (wanne kutoka kulia) ambaye amestaafu, utumishi wake kwa mjibu wa sheria, kama ishara ya kumshukuru kwa mchango wake chanya katika Ofisi hiyo na kumtakia maisha mema anapohitimisha utumishi wake.


Maafisa wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI waliowahi kufanya kazi na Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu wa Ofisi hiyo Bi. Mariam Mwanilwa wakipata picha ya pamoja na Mkurugenzi huyo mara baada ya kumuaga rasmi katika eneo la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijini Dodoma



Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bi. Mariam Mwanilwa (kushoto) akimlisha keki Afisa wa Ofisi hiyo kama ishara ya umoja na mshikamano kati yake na watumishi hao, mara baada ya mkurugenzi huyo kuagwa rasmi katika Ofisi hiyo Aprili 27, 2026 jijini Dodoma



Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu wa Ofisi hiyo Bi. Mariam Mwanilwa (kushoto) akitoa neno la shukrani kwa Katibu Mkuu-UTUMISHI , Menejimenti na watumishi wote wa Ofisi hiyo kwa ushirikiano alioupata kwa kipindi chote alipokuwa Ofisini hapo mara baada ya Mkurugenzi huyo kuagwa rasmi katika Ofisi hiyo Aprili 27, 2026 jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bi. Leila Mavika (kulia) akikabidhi  kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi zawadi  aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu wa Ofisi hiyo Bi. Mariam Mwanilwa (kushoto) mara baada ya Mkurugenzi huyo kufikia ukomo wa Utumishi wake kwa mujibu wa sheria .


Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Taasisi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Nolasco Kipanda (kushoto) akisisitiza jambo kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu wa Ofisi hiyo Bi. Mariam Mwanilwa (wa pili kutoka kushoto) wakati wa alipokuwa akiagwa rasmi katika eneo maalumu la mafunzo la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijini Dodoma. Wa pili na kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu wa Ofisi hiyo Bi. Leila Mavika na kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Anuai za Jamii na Mratibu wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza wa Ofisi hiyo Bi. Mwanaamani Mtoo

Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu Ofisi Rais-UTUMISHI Bi. Mariam Mwanilwa akifurahia jambo wakati alipokuwa akitoa neno la kuwaaga watumishi wa Ofisi hiyo Aprili 27, 2026 katika eneo maalumu la mafunzo lililopo katika Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma  

Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Taasisi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Nolasco Kipanda (kushoto) akitoa neno la shukrani pamoja na kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu wa Ofisi hiyo Bi. Mariam Mwanilwa (aliyesimama katikati) katika eneo maalumu la mafunzo la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijini Dodoma.Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu kwa Ofisi hiyo Bi. Leila Mavika 



Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bi. Mariam Mwanilwa (kushoto) akimlisha keki Afisa wa Ofisi hiyo kama ishara ya umoja na mshikamano kati yake na watumishi hao, mara baada ya mkurugenzi huyo kuagwa rasmi katika Ofisi hiyo Aprili 27, 2026 jijini Dodoma



Mkurugenzi wa Idara ya Mishahara, Motisha na Marupurupu wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bi. Mariam Mwanilwa (kushoto) akimlisha keki Afisa wa Ofisi hiyo kama ishara ya umoja na mshikamano kati yake na watumishi wa Ofisi hiyo, mara baada ya mkurugenzi huyo kuagwa rasmi katika Ofisi hiyo Aprili 27, 2026 jijini Dodoma.

 

 

 

 

 

MAFUNZO YA USIMAMIZI WA VIHATARISHI KWA WATUMISHI WA UMMA KUONGEZA UFANISI

Na. Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 27 Aprili, 2026

Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bi. Leila Mavika amesema mafunzo ya usimamizi wa vihatarishi kwa watumishi wa umma ni muhimu kwa kuwa yanaongeza uelewa wa kutambua, kuchambua na kudhibiti vihatarishi vinavyoweza kuathiri utendaj kazi wa shughuli za Serikali.

Bi. Mavika ameyasema hayo Aprili 27, 2026 wakati akimwakilisha Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi katika kuhitimisha mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi wa Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma.

Bi. Mavika meongeza kuwa, kutokana na uelewa ambao umepatikana wakati wa mafunzo hayo ni imani yake kuwa kila mtumishi wa ofisi hiyo atakuwa na uwezo wa kuchambua na kutambua vihatarishi vilivyopo katika eneo lake la kazi na kuvidhibiti kabla ya madhara kutokea.

Awali, Afisa Ukaguzi Mkuu kutoka Wizara ya Fedha Bi. Adolphina Lugando amesema, Serikali imeweka msisitizo kwa Wizara na Taasisi za umma kuimarisha mifumo ya udhibiti wa vihatarishi ili kuboresha uwajibikaji.

Vilevile Bi. Lugando alitoa wito kwa watumishi wa kila Idara na vitengo kuhakikishe wanatambua vihatarishi vinavyoweza kutokea katika Idara na vitengo vyao ili kuimarisha usalama.



Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bi. Leila Mavika akizungumza na watumishi wa Ofisi hiyo (hawapo pichani) wakati mkurugenzi huyo alipokuwa akihitimisha mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao katika eneo maalumu lla Ofisi hiyo ililopo Mtumba jijini Dodoma. 



Viongozi na watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakifuatilia mafunzo yaliyokuwa yakitolewa katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma na mwezeshaji kutoka Wizara ya fedha Bi. Adolphina Lugando (hayupo pichani) kuhusu kutambua, kuchambua na kudhibiti vihatarishi vinavyoweza kuathiri utendaj kazi kwa lengo la kuwajengea uelewa watumishi hao.



Watumishi wa Ofisi ya Rais, menejimenti ya utumishi wa umma na utawala Bora, wakifuatilia mafunzo ya  uelewa yaliyokuwa yakitolewa na muwezeshaji kutoka Wizara ya Fedha Bi. Adolphina Lugando leo Aprili 27, 2026 ambayo hufanyika kila jumatatu ya wiki katika eneo maalumu la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijini Dodoma

Afisa Ukaguzi Mkuu kutoka Wizara ya Fedha Bi. Adolphina Lugando akitoa mafunzo ya uelewa kuhusu usimamizi wa vihatarishi kwa watumishi wa umma wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora (hawapo pichani) yaliyofanyika katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma.


Watumishi wa Ofisi ya Rais, menejimenti ya utumishi wa umma na utawala Bora, wakifuatilia mafunzo ya  uelewa yaliyokuwa yakitolewa na muwezeshaji kutoka Wizara ya Fedha Bi. Adolphina Lugando leo Aprili 27, 2026 ambayo hufanyika kila jumatatu ya wiki katika eneo maalumu la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijini Dodoma


Watumishi wa Ofisi ya Rais, menejimenti ya utumishi wa umma na utawala Bora, wakifuatilia mafunzo ya  uelewa yaliyokuwa yakitolewa na muwezeshaji kutoka Wizara ya Fedha Bi. Adolphina Lugando leo Aprili 27, 2026 ambayo hufanyika kila jumatatu ya wiki katika eneo maalumu la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijin i Dodoma


Baadhi ya Wakurugenzi na watumishi wa Ofisi ya Rais, menejimenti ya utumishi wa umma na utawala Bora wakifuatilia mafunzo ya  uelewa leo Aprili 27, 2026 ambayo hufanyika kila jumatatun ya wiki katika eneo maalumu la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijin i Dodoma

Watumishi wa Ofisi ya Rais, menejimenti ya utumishi wa umma na utawala Bora, wakifuatilia mafunzo ya  uelewa yaliyokuwa yakitolewa na muwezeshaji kutoka Wizara ya Fedha Bi. Adolphina Lugando leo Aprili 27, 2026 ambayo hufanyika kila jumatatu ya wiki katika eneo maalumu la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijini Dodoma


Baadhi ya Wakurugenzi na watumishi wa Ofisi ya Rais, menejimenti ya utumishi wa umma na utawala Bora wakifuatilia mafunzo ya  uelewa leo Aprili 27, 2026 ambayo hufanyika kila jumatatun ya wiki katika eneo maalumu la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijin i Dodoma


Sunday, April 26, 2026

Wednesday, April 22, 2026

NAIBU KATIBU MKUU,OFISI YA RAIS-UTUMISHI BW. XAVIER DAUDI AKUTANA NA VIONGOZI WA JICA KWA MAZUNGUMZO

 Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais UTUMISHI na Utawala Bora Bw. Xavier Daudi akutana na kufanya mazungumzo na Viongozi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) Ofisini kwake Mtumba Jijini Dodoma. Viongozi hao wamemtambulisha Mwakilishi Mkuu Mpya Bw.Kuge Katsuya baada ya Bw.Ara Hitoshi kumaliza muda wake.


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora Bw. Xavier Daudi (aliyevaa suti ya bluu) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) baada ya viongozi hao kuhitimisha mazungumzo yaliyofanyika Aprili 22, 2026 katika Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma. Kulia kwake ni Mwakilishi Mkuu Mpya Bw.Kuge Katsuya na kushoto kwake ni Mwakilishi Mkuu aliyemaliza mda wake Bw.Ara Hitoshi



Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora Bw. Xavier Daudi (kulia) akipokea baadhi ya nyaraka kutoka kwa Mwakilishi Mkuu Mpya Bw.Kuge Katsuya (kushoto) baada ya viongozi hao kuhitimisha mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma.


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora Bw. Xavier Daudi (wa pili kutoka kulia) akifurahia jambo baada ya kuhitimisha mazungumzo baina ya Ofisi yake na JICA Mtumba Jijini Dodoma.



Tuesday, April 21, 2026

WATUMISHI WA UMMA WASISITIZWA KUSHUGHULIKIA MREJESHO WA WANANCHI KWA HAKI NA KWA WAKATI

 Na. Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 21 Aprili, 2026

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli amewasisitiza Watumishi wa Umma kushughulikia kwa haki na kwa wakati mrejesho unaowasilishwa na wananchi kupitia Mfumo wa (e- Mrejesho) ili kujenga imani na heshima ya Serikali kwa umma.

Bi. Shuli ameyasema hayo leo Aprili 21, 2026 wakati akimuwakilisha Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi katika ufunguzi wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini yake.

“Ili kufikia utumishi wa umma unaowajibika na uliotukuka, ni vizuri tukashughulikia mrejesho wa wananchi kwa haki na uharaka zaidi.” Bi Shuli alisema.

Amesema, Watumishi wa Umma wanapaswa kuwa na mabadiliko katika fikra, mitazamo, mifumo na tabia walizonazo ili kuwa na Utumishi wa Umma wenye matokeo chanya na thamani halisi kwa mwananchi.

Bi Shuli ameongeza kuwa uzingatiaji wa maadili katika utumishi wa umma si kuzifuata tu Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo ya Utumishi wa Umma bali ni pamoja na kuutumia ipasavyo utaalamu unaohusu ushughulikiaji wa mrejesho wa wananchi .

Amesema ni jukumu la kila mshiriki kuonesha ushirikiano na kuzingatia utu hususani wanapotoa huduma kwa wateja pamoja na kuwa waaminifu hasa katika utunzaji siri kwa kuwa kazi watakazofanya zitahitaji kuwa na matumizi sahihi ya taarifa.

Aidha, amewapongeza washiriki wote kwa kuhudhuria mafunzo hayo na kuwataka wajifunze kwa bidii ili wawe wataalamu watakaowajibika kikamilifu

Kwa upande wake mwenyekiti wa kikao hicho ambaye ni Afisa TEHAMA kutoka Watumishi Housing Investiments (WHI) Bw. Albano Lukiano   amemshukuru Bi. Shuli kwa kuwafungulia mafunzo hayo na kuahidi kuwa yale yote watakayofundishwa watayazingatia na kuyafanyia kazi ili kutoa huduma bora kwa manufaa ya umma.



Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister (kushoto) akiteta jambo na Mwenyekiti wa mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho ambaye pia ni Afisa TEHAMA kutoka Watumishi Housing Investiments (WHI) Bw. Albano Lukiano (kulia) kabla ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo hayo jijini Dodoma.  


Mkurugenzi Msaidizi wa Maadili, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Janet Mishinga, akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha mgeni Rasmi kufungua mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi mara baada ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma. 

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli (kushoto) akifurahia jambo mara baada ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo ya kutumia Mfumo wa e-Mrejesho yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Maadili wa Ofisi hiyo Bi. Janet Mishinga


Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi mara baada ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma

Afisa tawala kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Semeni Muyabhaga akiwasilisha mada ya Uwasilishwaji wa Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi kwa kutumia Mfumo wa e-Mrejesho wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika Aprili 21, 2026 katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma. 


Mwenyekiti wa kikao cha mafunzo ya kutumia Mfumo wa e-Mrejesho Bw. Albano Lukiano akitoa neno la shukrani kwa Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli mara baada ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma. 


Washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi wakifuatilia hotuba ya mgeni Rasmi wakati alipokuwa akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika leo Aprili 21, 2026 jijini Dodoma.

Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi Kutoka Idara ya Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Hassan Kilenza akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa mjadala wa hoja mbalimbali kuhusu matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho jijini Dodoma.

Washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi wakifuatilia hotuba ya mgeni Rasmi wakati alipokuwa akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika leo Aprili 21, 2026 jijini Dodoma.

Washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi wakifuatilia hotuba ya mgeni Rasmi wakati alipokuwa akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika leo Aprili 21, 2026 jijini Dodoma.

Washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi wakifuatilia hotuba ya mgeni Rasmi wakati alipokuwa akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika leo Aprili 21, 2026 jijini Dodoma.

Afisa Tawala kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Stella Teri akiwasilisha mada kuhusu uzingatiaji wa Kanuni za Maadili ya Utendeji kwa watumishi wa Umma wakati wa mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma

Afisa rasilimali watu mwaandamizi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Saada Ibrahim akiwasilisha mada ya  Mwngozo wa Ushughulikiaji wa Mrejesho katika Utumishi wa Umma katika mafunzo ya matumizi ya Mfumo huo yaliyofanyika  Aprili 21, 2026 katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma. 


Afisa rasilimali watu mwandamizi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Nasra Iduri akiwasilisha mada ya Dhana ya e-Mrejesho na ushughulikiaji wa malalamiko katika mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho yaliyofanyika Aprili 21, 2026 katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma