Tuesday, June 16, 2026
Monday, June 15, 2026
MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA
Wakurugenzi na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma
na Utawala Bora wakitoa elimu kwa wananchi kuhusu huduma zinazotolewa na Ofisi
hiyo wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma leo Juni 16, 2026
Chinangali Jijini Dodoma.
Aidha miongoni mwa Huduma zinazotolewa ni pamoja na elimu
ya Mifumo ya e-Wekeza, GSP, e-Huduma, e-Mkopo, e-Msawazo, Gazeti la Serikali,
e-Mrejesho, e-Utendaji, e-Watumishi, e-Likizo na e-Ajira.
Saturday, June 13, 2026
Monday, June 8, 2026
NAIBU KATIBU MKUU UTUMISHI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA MABALOZI WA HUDUMA BORA KWA WANANCHI
Na Antonia Mbwambo-Dodoma
Tarehe 8 Juni, 2026
Naibu
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw.
Xavier Daudi amewataka Watumishi wa Umma kuendelea kuzingatia maadili ya kazi,
kuwa na tabia njema na kuwahudumia wananchi kwa weledi ili kuongeza ufanisi wa
huduma za umma utakaochangia katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo
2050.
Bw.
Daudi ametoa rai hiyo wakati akihitimisha mada ya mafunzo kuhusu Usimamizi wa
Utendaji Kazi yaliyotolewa kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi
hao Juni 8, 2026 katika eneo maalumu la
Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Bw.
Daudi alisema, mafanikio ya Taasisi za Umma hayapimwi tu kwa utekelezaji wa
Mipango na Sera, bali pia kwa namna Watumishi wanavyowahudumia Wananchi
wanaowategemea katika kupata huduma. Alisisitiza kuwa tabia njema, uadilifu na
uwajibikaji ni sifa muhimu zinazopaswa kuonekana kwa kila Mtumishi wa Umma.
“Tunapaswa
kutambua kuwa kila Mwananchi anayefika kupata huduma ni mteja muhimu wa Serikali.
Jukumu letu ni kuhakikisha anahudumiwa kwa heshima, usikivu na kwa wakati. Hii
ndiyo njia bora ya kujenga imani ya Wananchi kwa Taasisi za Umma na kuimarisha
utawala bora,” Bw. Daudi alisema.
Aliongeza
kuwa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inalenga kuwa na taifa lenye maendeleo
jumuishi, uchumi imara na huduma bora za kijamii, hali ambayo inahitaji
Watumishi wa Umma kuwa sehemu ya mabadiliko hayo kwa kuzingatia maadili na
kuongeza ufanisi katika kazi zao.
Kwa
upande wake mwezeshaji kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Bw. Oswin Mkinga, alieleza kuwa usimamizi wa utendaji kazi ni
muhimu katika kuboresha matokeo ya Taasisi za Umma kwa kuwa utendaji bora
huanza kwa upangaji mzuri wa malengo, ufuatiliaji wa utekelezaji wake na
tathmini ya mara kwa mara ili kubaini mafanikio na maeneo yanayohitaji
maboresho.
Bw.
Mkinga alisisitiza kuwa, usimamizi wa utendaji kazi ni chombo muhimu katika kuimarisha
uwajibikaji wa Watumishi na kuongeza thamani ya huduma zinazotolewa kwa Wananchi
hivyo, ni lazima kila mtumishi akaelewa mchango wake katika kufanikisha malengo
ya taasisi na taifa kwa ujumla.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akihitimisha mada ya mafunzo kuhusu Usimamizi wa Utendaji Kazi leo Juni 8, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Baadhi ya Viongozi na Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji katika eneo la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Afisa kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Oswin Mkinga akifafanua mada kuhusu
Usimamizi wa Utendaji Kazi kwa watumishi wa Ofisi hiyo wakati wa mafunzo ambayo
hufanyika kila jumatatu ya wiki katika eneo maalumu la Ofisi hiyo kwa lengo la
kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao.
Saturday, June 6, 2026
Friday, June 5, 2026
Wednesday, June 3, 2026
UTAWALA BORA NA USIMAMIZI MAKINI WA RASILIMALIWATU NI MSINGI WA UTUMISHI WA UMMA WENYE MATOKEO – MHE. QWARAY
Na
Antonia Mbwambo –Dodoma
Tarehe
3 Juni, 2026
Naibu
Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Regina Qwaray, amewataka Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
Serikalini kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele katika kusimamia haki,
uwajibikaji na uzingatiaji wa sheria katika Utumishi wa Umma ili kuongeza
ufanisi wa utoaji wa huduma kwa wananchi.
Mhe.
Qwaray ameyasema hayo Juni 3, 2026 wakati akifunga Kikao Kazi cha Wakuu wa
Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi waRasilimaliwatu Serikalini kilichowakutanisha
viongozi kutoka Wizara, Wakala, Taasisi za Umma, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka
za Serikali za Mitaa Jijini Dodoma.
Amesema,
mafanikio ya Serikali yanategemea kwa kiwango kikubwa ubora wa usimamizi wa
rasilimaliwatu.
“Rasilimaliwatu ndiyo injini ya maendeleo ya taifa;
isimamiwe kwa weledi, haki na uwajibikaji.” – Mhe. Regina
Qwaray alisema.
Aidha
Mhe. Qwaray alibainisha kuwa Serikali imeendelea kupokea malalamiko
yanayohusiana na ucheleweshaji wa kupandishwa vyeo, malipo ya stahili za
watumishi na ukiukwaji wa taratibu za kiutumishi, hivyo kuwataka wataalamu wa
Utawala na Rasilimaliwatu kuwa washauri waaminifu kwa viongozi wao na walinzi
wa utawala wa sheria katika taasisi wanazozihudumia.
Pia
alisisitiza umuhimu wa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma, matumizi salama
ya teknolojia na ulinzi wa taarifa za Serikali, huku akitoa wito kwa waajiri
kuwajengea watumishi uwezo kuhusu matumizi sahihi ya Akili Unde (AI) na mifumo
ya kidijiti.
Katika
kuongeza ufanisi wa utendaji kazi, aliagiza utekelezaji wa Mfumo wa e-Utendaji
usimamiwe kwa ukaribu zaidi, na kwamba wasimamizi watakaoshindwa kutekeleza
wajibu wao wa kutathmini utendaji wa watumishi wachukuliwe hatua kwa mujibu wa
sheria, kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma.
Ameongeza kuwa kufungwa kwa
kikao hicho hakumaanishi mwisho wa juhudi za kuboresha Utumishi wa Umma, bali
ni hatua ya kuanza kutekeleza kwa vitendo maazimio na maelekezo yaliyokubaliwa.
“Kumalizika
kwa kikao hiki si mwisho wa kazi, bali ni mwanzo wa utekelezaji wa maazimio na
maelekezo yaliyotolewa kwa lengo la kujenga Utumishi wa Umma sikivu, jumuishi, na
wenye matokeo,” alisisitiza Mhe. Qwaray.
Kwa upande wake Katibu
Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi amesema ni matarajio yake kuwa kikao hicho
kitaleta matokeo chanya kwa viongozi hao yatakayoboresha utekelezaji wa
majukumu na kuongea tija katika utumishi wa umma.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza katika kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu (hawapo pichani) wakati Naibu Waziri huyo alipokuwa akifunga kikao kazi kilicholenga kuimarisha utawala na usimamizi wa rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma tarehe 3 Juni, 2026 jijini Dodoma.





,%20Huduma%20za%20afya%20kutokea%20Muhimbili,%20MOI,%20BMH,%20JKCI,%20H(7).png)




