Monday, July 6, 2026
Saturday, July 4, 2026
Friday, July 3, 2026
MHE. RIDHIWANI KIKWETE AZINDUA TAFITI SITA ZITAKAZOFANYA TPSC KUWA KITOVU CHA MAARIFA NA USHAHIDI WA KISAYANSI KATIKA KUBORESHA UTUMISHI WA UMMA
Na. Veronica Mwafisi-Dar es Salaam
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete amezindua tafiti tumizi sita zitakazokifanya Chuo cha
Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) kuwa kitovu cha maarifa na ushahidi wa
kisayansi kwa ajili ya kuboresha Utumishi wa Umma.
Akizungumza
katika hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma
Tanzania, Waziri Kikwete amesema Serikali inahitaji tafiti zitakazotoa
suluhisho kwa changamoto halisi zinazokabili taasisi za umma.
“Tunahitaji
tafiti zinatakazosaidia kufanya maamuzi sahihi ya sera, kuboresha mifumo ya
kazi, na kuongeza ufanisi wa huduma kwa wananchi”, amesema Mhe. Kikwete.
Aidha,
Waziri Kikwete amewapongeza watafiti wote walioshiriki katika kazi ya utafiti na
kutoa rai kwa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania kuendelea kuimarisha
ushirikiano na Wizara, Idara Zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Mamlaka za
Serikali za Mitaa, Vyuo Vikuu na taasisi nyingine ili tafiti zake ziwe na
mchango mkubwa katika maendeleo ya Taifa.
Waziri
Kikwete ameongeza kuwa, anaamini miaka 25 ijayo itakuwa kipindi cha mafanikio
makubwa zaidi, ambapo Chuo hicho kitaendelea kuwa kinara wa maendeleo ya
rasilimali watu, tafiti tumizi, na ushauri wa kitaalamu kwa ajili ya kuimarisha
Utumishi wa Umma na kuchochea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani
Kikwete akibonyeza kitufe wakati akizindua tafiti
tumizi sita wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo
cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) zitakazokifanya Chuo hicho kuwa kitovu cha
maarifa na ushahidi wa kisayansi kwa ajili ya kuboresha Utumishi wa Umma.
Viongozi mbalimbali, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakipiga makofi baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) kuzindua tafiti tumizi sita wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete
akizungumza baada ya kuzindua tafiti tumizi sita wakati
wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma
Tanzania (TPSC) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano
cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete (kushoto) akifurahia jambo na Katibu Mkuu wa ofisi yake, Bw.
Juma Mkomi (kulia) baada ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI kukabidhiwa Tuzo ya Utambuzi iliyotolewa na Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania
(TPSC) wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo hicho yaliyofanyika
katika Ukumbi wa Kituo
cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI
na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) akielekea katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha
Julius Nyerere wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya
Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC). Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha
Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Florens Turuka na kushoto kwake ni Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu, Chuo cha
Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Dkt. Ernest Mabonesho.
Menejimenti,
Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao baada ya kuzindua tafiti
tumizi sita wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha
Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi
wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius
Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Wadau
na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao baada ya kuzindua tafiti
tumizi sita wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha
Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi
wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius
Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Wadau
na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao baada ya kuzindua tafiti
tumizi sita wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha
Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi
wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius
Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.
MIAKA 25 YA CHUO CHA UTUMISHI WA UMMA TANZANIA, MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA KUJENGA RASILIMALIWATU YENYE TIJA
Na. Veronica Mwafisi-Dar ES Salaam
Tarehe 03 Julai, 2026
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema miaka 25 ya
Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) ina nafasi ya kipekee katika kujenga
na kuendeleza uwezo wa kiutendaji wa watumishi wa umma ambao ndio watekelezaji
wa majukumu ya Serikali kila siku.
Waziri Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 03
Julai, 2026 wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya TPSC
yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha
Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Mhe. Kikwete amesema, Serikali ya Awamu ya
Sita chini ya Uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea
kuweka kipaumbele katika uimarishaji wa Utumishi wa Umma ili kuhakikisha
wananchi wanapata huduma bora, za haraka na zenye tija.
Mhe. Kikwete ameongeza kuwa, Chuo cha
Utumishi wa Umma Tanzania si tu taasisi ya mafunzo, bali ni nguzo muhimu ya
Serikali katika kujenga rasilimaliwatu yenye maarifa, stadi, maadili na
uzalendo unaohitajika katika kutumikia umma kwa ufanisi.
Katika hatua nyingine, Mhe. Kikwete amesema
kuwa, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inatutaka kuwa na Taifa lenye uchumi wa
kisasa, ushindani wa kimataifa, matumizi makubwa ya teknolojia, na huduma za
umma zenye ufanisi wa hali ya juu. Hivyo, mafanikio ya Dira hiyo yatategemea
kwa kiasi kikubwa uwepo wa watumishi wenye sifa, ujuzi na uwezo wa kuongoza
mabadiliko hayo.
“Chuo hiki kina wajibu mkubwa wa kuhakikisha Watumishi wa Umma wanapata maarifa na stadi
zinazolingana na mahitaji ya karne ya ishirini na moja ili kuwepo wa watumishi
wenye sifa, ujuzi na uwezo wa kuongoza mabadiliko hayo,” amesema Waziri
Kikwete.
Aidha, Mhe. Kikwete amewapongeza watangulizi
wake kwa usimamizi mzuri ambao umechangia mafanikio makubwa ya Chuo hicho huku
akimshukuru Katibu Mkuu wa Ofisi yake, Bw. Juma Mkomi kwa kuendelea kusimamia
Chuo hicho kiutendaji.
Vilevile, Waziri Kikwete ameipongeza Bodi ya
Ushauri ya TPSC, Menejimenti, Watumishi, Wanafunzi na wadau wote kwa mchango
wao katika safari ya kutimiza miaka 25 ya mafanikio ya chuo hicho.
Akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha
Mhe. Waziri kuzungumza na wadau katika hafla hiyo, Katibu Mkuu Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi ametoa wito kwa waajiri kutumia Kampasi za TPSC
zilizo katika kanda zao ili kuwawezesha watumishi ikiwemo waajiriwa wapya
kupata mafunzo ya awali.
“Kampasi katika Kanda hizo zimewekwa
kimkakati ili kusogeza huduma za chuo katika mikoa mbalimbali, hivyo Waajiri wazitumie
kikamilifu kwa watumishi kupata mafunzo kwa lengo la kuboresha utendaji kazi.”
Amesisitiza Katibu Mkuu Mkomi.
Amezitaja Kampasi hizo kuwa ni Dar es Salaam,
Mbeya, Tanga, Singida, Tabora na Mtwara na kuongeza kuwa Ofisi ya Rais-UTUMISHI
itaendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na TPSC za kumiliki majengo yao
ambapo Kampasi ya Singida inaendelea na ujenzi wa majengo 30 na Kampasi ya
Tanga majengo 15.
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TPSC,
Dkt. Florens Turuka amesema Bodi itaendelea kutoa ushauri ili Chuo kiendelee
kuwa kinara katika masuala mbalimbali ikiwemo kujenga rasilimaliwatu yenye
maadili, na yenye tija kwa taifa.
Akiwasilisha taarifa ya miaka 25 ya TPSC, Mkuu
wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Ernest
Mabonesho amesema tangu kuanzishwa kwake, Chuo kimepata mafanikio makubwa
katika maeneo mbalimbali ikiwemo taaluma, rasilimaliwatu na miundombinu.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani
Kikwete akizungumza wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya
Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano
cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Viongozi mbalimbali, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akiteta
jambo na Katibu Mkuu wa ofisi yake Bw. Juma Mkomi (kulia) wakati wa kilele cha
maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC)
yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere
kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Menejimenti,
Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya
kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania
yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere
kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete (kulia) akifurahia jambo na Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu, Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC),
Dkt. Ernest Mabonesho (kushoto) wakati wa hafla ya kilele cha
maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika
katika Ukumbi wa Kituo
cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Wanafunzi
wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania
(TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani)
alipokuwa akizungumza nao kwenye hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya
Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha
Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Menejimenti,
Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya
kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania
yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere
kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Thursday, July 2, 2026
SERIKALI YARIDHISHWA NA MAENDELEO YA MIRADI YA NYUMBA ZA WATUMISHI WA UMMA KIGOMA
Na. Antonia Mbwambo–Kigoma
Tarehe 2 Julai, 2026
Serikali
imeeleza kuridhishwa na Maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa Ujenzi wa Nyumba
za Watumishi wa Umma Awamu ya Pili katika Mkoa wa Kigoma kufuatia ukaguzi
uliofanywa na timu ya Wataalamu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora kwa kushirikiana na Watumishi Housing Investimentsl.
Hayo
yamesemwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Bw. Patrick
Allute, wakati wakihitimisha ziara ya ukaguzi wa miradi ya makazi ya Watumishi
wa Umma Mkoani Kigoma ambapo timu ilikagua mradi ya nyumba za Watumishi katika
Shule ya Sekondari Muhunga, Wilaya ya Kasulu, na Kituo cha Afya Muyama, Wilaya
ya Buhigwe,Mkoa wa Kigoma
Akizungumza
baada ya kuhitimisha ziara hiyo, Bw. Allute amepongeza wasimamizi wa mradi,
Watumishi Housing na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa usimamizi unaowezesha
miradi hiyo kutekelezwa kwa ufanisi. Amesema hatua iliyofikiwa inaakisi dhamira
ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuboresha mazingira ya kazi na
ustawi wa Watumishi wa Umma.
Aidha,
ameutaja mradi wa nyumba za Watumishi katika Kituo cha Afya Muyama kuwa
miongoni mwa miradi iliyofanya vizuri zaidi kati ya miradi 15 iliyokaguliwa
katika Mikoa mbalimbali ya Tanzania kutokana na kasi ya utekelezaji na ubora wa
kazi inayoendelea kuonekana.
"Mradi
wa nyumba za Watumishi katika Kituo cha Afya Muyama umeonesha kiwango cha juu
cha utekelezaji. Kazi nyingi muhimu, ikiwemo mfumo wa umeme, zimekamilika na
mradi umebakiza hatua chache kabla ya kukamilika na kuanza kutumika," amesema Bw. Allute.
Kwa
upande wake, Msimamizi wa Mradi wa Kituo cha Afya Muyama ameishukuru timu ya
ukaguzi kwa ushauri na maelekezo yaliyotolewa, akisema yataendelea kufanyiwa
kazi ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na kuanza kutoa huduma kwa Watumishi
wa Umma waliokusudiwa kunufaika nao.
Wataalamu kutoka Ofisi ya Rais–UTUMISHI na
Watumishi Housing
Investment (WHI) wakijadili jambo mara baada ya kufanya
ukaguzi wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa
Timu
ya wataalamu kutoka Ofisi
ya Rais–UTUMISHI na Watumishi
Housing Investment (WHI) wakiwa katika picha ya pamoja na Kaimu
Mganga Mfawidhi Kituo cha Afya Muyama Bw. Kwima Juma Buanza (wa tatu kutoka
kushoto), mara baada ya timu hiyo kukamilisha ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa
nyumba za watumishi wa kituo hicho kiiilichopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa
Kigoma.
Mkurugenzi wa Fedha na Uwekezaji kutoka Watumishi
Housing Investiment (WHI) Bw. Paskali Massawe (aliyenyoosha mkono)
akielezea jambo kwa Wataalamu alioambatana nao katika ukaguzi wa mradi wa
ujenzi wa Kituo
cha Afya Muyama, Wilaya ya Buhigwe, Mkoani Kigoma, mara baada ya kufika kwenye
eneo hilo Julai 2, 2026
Wataalamu
kutoka Ofisi ya
Rais–UTUMISHI na Watumishi
Housing Investment (WHI) wakijadili jambo mara baada ya
kufanya ukaguzi wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya
Watumishi wa Shule ya Sekondari Muhunga iliyopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa
Kigoma.
Mkurugenzi
wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Patrick Allute (wa
tano kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mipango na Bajeti,
wa Ofisi hiyo, Bi. Julieth Magambo
wakati
wa ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa nyumba ya makazi ya watumishi wa Shule ya
Sekondari Muhunga iliyopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma.
Wataalamu
kutoka Ofisi ya
Rais–UTUMISHI na Watumishi
Housing Investment (WHI) wakijadili jambo mara baada ya
kufanya ukaguzi wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya
Watumishi wa Shule ya Sekondari Muhunga iliyopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa
Kigoma.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na
Tathmini, Bw. Patrick
Allute, (aliyenyoosha mikono), akitoa maelekezo kwa Makamu Mkuu
wa Shule ya Sekondari Muhunga Mwl. Beatus Damiani,(wa pili kutoka kushoto) wakati
wa ukaguzi wa SHule hiyo iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Mkoa wa
Kigoma, leo tarehe 2 Julai, 2026.
Muonekano wa
mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma Shule ya Sekondari
Muhunga iliyopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Patrick Allute (wanne kutoka kushoto) akiagana na Kaimu Afisa Elimu Sekondari, Halmashauri ya Mji wa Kasulu Mwl. Jeremiah Ntiboneka mara baada ya Timu ya Wataalamu kutoka Ofisi ya Rais–UTUMISHI na Watumishi Housing Investment (WHI) kukagua mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari Muhunga iliyopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma.
Tuesday, June 30, 2026
Monday, June 29, 2026
KATIBU MKUU MKOMI AMPONGEZA NA KUMTAKIA HERI KATIBU MTEULE WA TUME YA UTUMISHI WA UMMA, AMUASA KUZINGATIA FALSAFA YA KAZI NA UTU KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU
Na. Veronica Mwafisi-Dodoma
Katibu Mkuu ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma, Bw. Juma Mkomi amempongeza na kumtakia heri aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye
ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda.
Katibu Mkuu Mkomi ameyasema hayo jijini Dodoma
baada ya kuhitimishwa kwa mafunzo yanayofanyika kila Jumatatu kwa watumishi wa
Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambapo pia alitumia wasaa huo kumuaga Bw. Kipanda.
Bw. Mkomi amemuasa Katibu mteule huyo kutumia
falsafa ya kazi na utu wakati wa utekelezaji wa majukumu yake ili aweze kutenda
haki katika kufanya maamuuzi.
Amesema, matatizo mengi yanayowapata Watumishi wa Umma
wakati mwingine yanatokana na kukosekana kwa utu wa waajiri hivyo, amemtaka Bw.
Kipanda kufanya maamuzi yaliyo sahihi ili kutenda haki.
“Ninaamini Bw. Kipanda
utaenda kutenda haki na kutuwakilisha vizuri, fanya kazi kwa kuzingatia Sheria,
Kanuni, Taratibu na Utu. Taasisi uliyoteuliwa kufanya kazi inahusika na utoaji
wa haki kwa Watumishi wa Umma, hivyo pamoja na kutumia taratibu, ukazingatie
pia suala la utu katika kufanya maamuzi.
Vilevile, Bw. Mkomi amemuahidi
Bw. Kipanda ushirikiano pale atakapohitaji ikiwa ni pamoja na ushauri katika
kazi kwani itasaidia kuimarisha zaidi utendaji kazi.
Kwa upande wake Katibu
Mteule wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda amemshukuru Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na
kumteua kuiongoza Taasisi hiyo.
Bw. Kipanda amewashukuru
Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora kwa kufanya kazi nao kwa muda mrefu na kuomba kuendelea kumpatia
ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake mapya kwa maendeleo ya Taifa.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Katibu Mkuu Mstaafu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (kushoto). Kulia ni aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda
Katibu Mkuu,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akizungumza
jambo kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa
Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya
Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda baada ya kumaliza mafunzo kwa
watumishi wa ofisi hiyo yaliyolenga kuwajengea uwezo katika Mji wa Serikali
Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa nasaha wakati wa kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda
Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda (kulia)akipokea keki alipokuwa akiagwa na Watumishi wa Ofisi hiyo mara baada ya kuteuliwa kuwa Katibu wa Tume hiyo.
Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya
Uendelezaji wa Taasisi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Bw. Nolasco Kipanda ambaye kwa sasa ni Katibu wa Tume ya Utumishi
wa Umma akikata keki akiwa anaagwa na watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI
jijini Dodoma
Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa
Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.
Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco
Kipanda akitoa neno la shukrani
kwa Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI alipokuwa
akiwaaga katika ofisi hiyo Mji wa Serikali
Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye
ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda (hayupo pichani) wakati akitoa neno
la shukrani kwa Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI
alipokuwa akiwaaga baada ya kupata teuzi hiyo.
Mkurugenzi wa Idara ya
Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bw. Musa Magufuli akimlisha keki aliyekuwa Mkurugenzi wa
Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya
Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipandabaada ya kutoa neno la shukrani kwa
Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI alipokuwa akiwaaga
baada ya kupata teuzi hiyo.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi
(hayupo pichani) alipokuwa akitoa nasaha wakati wa kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa
Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.
Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco
Kipanda.
SERIKALI YAENDELEA KUBORESHA MAZINGIRA YA WATUMISHI WA UMMA KUPITIA UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI
Na. Antonia Mbwambo- Mbeya
Tarehe 29
Juni, 2026
Serikali
imeendelea kuboresha mazingira ya kazi kwa Watumishi wa Umma kupitia
utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa nyumba za makazi, hatua inayolenga kuongeza
ufanisi wa utendaji kazi na utoaji wa huduma kwa wananchi.
Hayo
yamesemwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute,
wakati wa ziara ya kukagua ujenzi wa nyumba za watumishi katika Shule za Msingi
Ngolela, Wilaya ya Kyela na Idweli, Wilaya ya Rungwe, mkoani Mbeya,
iliyohusisha wataalamu kutoka Ofisi hiyo pamoja na Watumishi Housing Investments
(WHI).
Bw.
Allute amesema makazi bora yataongeza ari ya kazi kwa Walimu na kuboresha
utoaji wa huduma. Aidha, amewataka Watumishi watakaonufaika na nyumba hizo
kuzitunza vizuri mara zitakapokamilika kwa kuwa ni mali za umma na zinazopaswa
kudumu ili kuwanufaisha Watumishi wa baadae.
"Serikali
inaendelea kuwekeza fedha nyingi katika kuboresha mazingira ya kazi kwa Watumishi
wa Umma, hivyo ni wajibu wa kila mnufaika kuhakikisha nyumba hizi zinatunzwa
vizuri mara zitakapokamilika na kuanza kutumika ili ziendelee kuhudumia
watumishi wa sasa na wa baadae," Bw. Allute amesema
Kwa
upande wake, Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mipango na Bajeti, kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI,
Bi. Julieth Magambo, amesema Serikali inaendelea kuwekeza katika ujenzi wa
nyumba za watumishi ili kuhakikisha wanapata mazingira bora, salama na yenye
utulivu yatakayowawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.
Awali,
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ngolela, Bw. Samsoni Anyosisye, ameishukuru
Serikali kwa mradi huo, huku akieleza kuwa nyumba zilizopo zimechakaa na
hazifai kwa matumizi, hali iliyowalazimu Walimu wengi kuishi mbali na shule.
Naye
Mwalimu wa Shule ya Msingi Idweli, Bw. Tejile Mathew, amesema kukamilika kwa
nyumba hizo kutaleta motisha ya kazi na kuongeza ufanisi katika utoaji wa
huduma ya Elimu.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (aliyenyoosha mkono) akitaka ufafanuzi wa jambo wakati wa ukaguzi wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Shule ya msingi Ngolela iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mipango na Bajeti,Bi Julieth Magambo wa Ofisi hiyo.
Muonekano wa mbele wa jengo la
mradi wa makazi ya watumishi wa umma wa Shule ya msingi
Ngolela, iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoa wa Mbeya.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya
Msingi Ngolela, Bw. Samsoni Anyosisye (wanne kutoka kushoto) akitoa maelezo kwa Mkurugenzi wa Kitengo cha
Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (wa kwanza kutoka kulia) wakati wa ukaguzi
wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Shule ya msingi
Ngolela iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya
Muonekano wa mbele wa jengo la
zamani walilokuwa wakiishi Waalimu wa shule ya msingi Ngolela iliyopo Kyela
Mkoani Mbeya kabla ya jengo hilo kuchakaa na kushindwa kutumika kwa makazi
Timu ya wataalamu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watumishi Housing
Investment (WHI) ikiwa katika picha ya pamoja na Mwalimu Mkuu wa Shule ya
Msingi Ngolela, Bw. Samsoni Anyosisye (wanne kutoka kushoto) mara baada ya timu
hiyo kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa Shule ya
msingi Ngolela iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya
Muonekano wa nyuma wa jengo la
zamani walilokuwa wakiishi Waalimu wa shule ya msingi Ngolela iliyopo Kyela
Mkoani Mbeya kabla ya jengo hilo kuchakaa na kushindwa kutumika kwa makazi
Timu ya wataalamu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watumishi Housing
Investment (WHI) wakiwa katika picha ya pamoja na Mwalimu wa Shule ya Msingi
Idweli, Bw. Tejile Mathew pamoja na mafundi wanaosimamia mradi huo mara baada
ya timu hiyo kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa makazi ya Watumishi wa
Shule ya msingi Ngolela iliyopo Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya
Muonekano wa mbele wa jengo la
mradi wa makazi ya watumishi wa umma wa Shule ya msingi Idwelu,
iliyopo Wilaya ya Rugwe Mkoa wa Mbeya


























