Tuesday, June 16, 2026

Monday, June 15, 2026

MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

Wakurugenzi na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakitoa elimu kwa wananchi kuhusu huduma zinazotolewa na Ofisi hiyo wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma leo Juni 16, 2026 Chinangali Jijini Dodoma.

Aidha miongoni mwa Huduma zinazotolewa ni pamoja na elimu ya Mifumo ya e-Wekeza, GSP, e-Huduma, e-Mkopo, e-Msawazo, Gazeti la Serikali, e-Mrejesho, e-Utendaji, e-Watumishi, e-Likizo na e-Ajira.



 







NAFASI ZA KAZI



 

Monday, June 8, 2026

NAIBU KATIBU MKUU UTUMISHI AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA MABALOZI WA HUDUMA BORA KWA WANANCHI

 Na Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 8 Juni, 2026

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi amewataka Watumishi wa Umma kuendelea kuzingatia maadili ya kazi, kuwa na tabia njema na kuwahudumia wananchi kwa weledi ili kuongeza ufanisi wa huduma za umma utakaochangia katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Bw. Daudi ametoa rai hiyo wakati akihitimisha mada ya mafunzo kuhusu Usimamizi wa Utendaji Kazi yaliyotolewa kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao Juni 8, 2026   katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.

Bw. Daudi alisema, mafanikio ya Taasisi za Umma hayapimwi tu kwa utekelezaji wa Mipango na Sera, bali pia kwa namna Watumishi wanavyowahudumia Wananchi wanaowategemea katika kupata huduma. Alisisitiza kuwa tabia njema, uadilifu na uwajibikaji ni sifa muhimu zinazopaswa kuonekana kwa kila Mtumishi wa Umma.

“Tunapaswa kutambua kuwa kila Mwananchi anayefika kupata huduma ni mteja muhimu wa Serikali. Jukumu letu ni kuhakikisha anahudumiwa kwa heshima, usikivu na kwa wakati. Hii ndiyo njia bora ya kujenga imani ya Wananchi kwa Taasisi za Umma na kuimarisha utawala bora,” Bw. Daudi alisema.

Aliongeza kuwa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inalenga kuwa na taifa lenye maendeleo jumuishi, uchumi imara na huduma bora za kijamii, hali ambayo inahitaji Watumishi wa Umma kuwa sehemu ya mabadiliko hayo kwa kuzingatia maadili na kuongeza ufanisi katika kazi zao.

Kwa upande wake mwezeshaji kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Oswin Mkinga, alieleza kuwa usimamizi wa utendaji kazi ni muhimu katika kuboresha matokeo ya Taasisi za Umma kwa kuwa utendaji bora huanza kwa upangaji mzuri wa malengo, ufuatiliaji wa utekelezaji wake na tathmini ya mara kwa mara ili kubaini mafanikio na maeneo yanayohitaji maboresho.

Bw. Mkinga alisisitiza kuwa, usimamizi wa utendaji kazi ni chombo muhimu katika kuimarisha uwajibikaji wa Watumishi na kuongeza thamani ya huduma zinazotolewa kwa Wananchi hivyo, ni lazima kila mtumishi akaelewa mchango wake katika kufanikisha malengo ya taasisi na taifa kwa ujumla.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akihitimisha mada ya mafunzo kuhusu Usimamizi wa Utendaji Kazi leo Juni 8, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.



Baadhi ya Viongozi na Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji katika eneo la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.

Afisa kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Oswin Mkinga akifafanua mada kuhusu Usimamizi wa Utendaji Kazi kwa watumishi wa Ofisi hiyo wakati wa mafunzo ambayo hufanyika kila jumatatu ya wiki katika eneo maalumu la Ofisi hiyo kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao.


Baadhi ya Wakurugenzi wasaidizi na watumishi kutoka Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji katika eneo la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.


Baadhi ya  Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji katika eneo la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.

Wednesday, June 3, 2026

UTAWALA BORA NA USIMAMIZI MAKINI WA RASILIMALIWATU NI MSINGI WA UTUMISHI WA UMMA WENYE MATOKEO – MHE. QWARAY

Na Antonia Mbwambo –Dodoma

Tarehe 3 Juni, 2026

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray, amewataka Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele katika kusimamia haki, uwajibikaji na uzingatiaji wa sheria katika Utumishi wa Umma ili kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma kwa wananchi.

Mhe. Qwaray ameyasema hayo Juni 3, 2026 wakati akifunga Kikao Kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi waRasilimaliwatu Serikalini kilichowakutanisha viongozi kutoka Wizara, Wakala, Taasisi za Umma, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Jijini Dodoma.

Amesema, mafanikio ya Serikali yanategemea kwa kiwango kikubwa ubora wa usimamizi wa rasilimaliwatu.

“Rasilimaliwatu ndiyo injini ya maendeleo ya taifa; isimamiwe kwa weledi, haki na uwajibikaji.” – Mhe. Regina Qwaray alisema.

Aidha Mhe. Qwaray alibainisha kuwa Serikali imeendelea kupokea malalamiko yanayohusiana na ucheleweshaji wa kupandishwa vyeo, malipo ya stahili za watumishi na ukiukwaji wa taratibu za kiutumishi, hivyo kuwataka wataalamu wa Utawala na Rasilimaliwatu kuwa washauri waaminifu kwa viongozi wao na walinzi wa utawala wa sheria katika taasisi wanazozihudumia.

Pia alisisitiza umuhimu wa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma, matumizi salama ya teknolojia na ulinzi wa taarifa za Serikali, huku akitoa wito kwa waajiri kuwajengea watumishi uwezo kuhusu matumizi sahihi ya Akili Unde (AI) na mifumo ya kidijiti.

Katika kuongeza ufanisi wa utendaji kazi, aliagiza utekelezaji wa Mfumo wa e-Utendaji usimamiwe kwa ukaribu zaidi, na kwamba wasimamizi watakaoshindwa kutekeleza wajibu wao wa kutathmini utendaji wa watumishi wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma.

Ameongeza kuwa kufungwa kwa kikao hicho hakumaanishi mwisho wa juhudi za kuboresha Utumishi wa Umma, bali ni hatua ya kuanza kutekeleza kwa vitendo maazimio na maelekezo yaliyokubaliwa.

Kumalizika kwa kikao hiki si mwisho wa kazi, bali ni mwanzo wa utekelezaji wa maazimio na maelekezo yaliyotolewa kwa lengo la kujenga Utumishi wa Umma sikivu, jumuishi, na wenye matokeo,” alisisitiza Mhe. Qwaray.

Kwa upande wake Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi amesema ni matarajio yake kuwa kikao hicho kitaleta matokeo chanya kwa viongozi hao yatakayoboresha utekelezaji wa majukumu na kuongea tija katika utumishi wa umma.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza katika kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu (hawapo pichani) wakati Naibu Waziri huyo alipokuwa akifunga kikao kazi kilicholenga kuimarisha utawala na usimamizi wa rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma  tarehe 3 Juni, 2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (kulia) akimkabidhi Mkurugenzi wa Uendelezaji Taasisi wa Ofisi hiyo Bw. Nolasco Kipanda tuzo ya shukrani kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI mstaafu Dkt. Laurean Ndumbaro, kwa kushiriki na kuwasilisha mada katika kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini jijini Dodoma

Com

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray,(kulia) akiteta jambo na Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Huma Mkomi, wakati wa kufunga kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini Tarehe 3 Juni, 2026 jijini Dodoma

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray,(kushoto) akisalimiana na viongozi wa Ofisi hiyo mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa Mabele jijini Dodoma kufunga kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini leo Tarehe 3 Juni, 2026 jijini Dodoma

Comm


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi hiyo, mara baada ya Naibu Waziri huyo kufunga kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini leo Tarehe 3 Juni, 2023 jijini Dodoma


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi hiyo, mara baada ya Naibu Waziri huyo kufunga kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini leo Tarehe 3 Juni, 2023 jijini Dodoma

Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray kufunga kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini leo Tarehe 3 Juni, 2023 jijini Dodoma

Comments

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiwa katika picha ya pamoja na Sekretarieti ya watumishi kutoka Ofisi hiyo, mara baada ya Naibu Waziri huyo kufunga kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini leo Tarehe 3 Juni, 2023 jijini Dodoma.



Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (wa pili kushoto) mara baada ya Naibu Waziri huyo kufunga kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini leo Tarehe 3 Juni, 2026 jijini Dodoma. Wa pili kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (wa pili kulia) akimkabidhi Mkurugenzi wa Huduma za Uwezeshaji katika Taasisi ya Uongozi Bw. Deo Usangira tuzo ya shukrani kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa Taasisi hiyo, Bw. Kadari Singo kwa kushiriki na kuwasilisha mada katika kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini jijini Dodoma

Comme

Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (kushoto) akimkabidhi Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray kwa kushiriki katika mkutano wa Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini leo Tarehe 3 Juni, 2023 jijini Dodoma

Comme