Wednesday, June 26, 2019

SERIKALI YAWAASA WANANCHI KUTOTUMIA DAWA ZA KULEVYA ILI KULINDA NGUVUKAZI YA TAIFA



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) akizungumza na wananchi wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Kupiga Vita Dawa za Kulevya duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Tangamano, jijini Tanga.
 
Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) (hayupo pichani) wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Kupiga Vita Dawa za Kulevya duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Tangamano, jijini Tanga.


Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (Mb) akizungumza na wananchi wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Kupiga Vita Dawa za Kulevya duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Tangamano, jijini Tanga. 
Mmojawapo wa waathirika wa dawa za kulevya, Bw. Said Bandawa akitoa ushuhuda wa namna Serikali ilivyomsaidia kuondokana na matumizi ya dawa za kulevya wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya kupiga vita Dawa za Kulevya duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Tangamano, jijini Tanga.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) akiteta jambo na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (Mb) wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya kupiga vita Dawa za Kulevya duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Tangamano, jijini Tanga.

Tuesday, June 25, 2019

WATUNZA KUMBUKUMBU NA MAAFISA RASILIMALIWATU WATAKIWA KUZINGATIA UADILIFU KATIKA UTUNZAJI WA KUMBUKUMBU NA NYARAKA ZA SERIKALI



Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi akimkaribisha Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Francis Michael kufungua kikao kazi cha siku tatu cha Watunza Kumbukumbu na Maafisa Rasilimaliwatu Serikalini chenye lengo la kujadili masuala ya utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka katika Utumishi wa Umma kilichoanza leo jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Francis Michael akifungua kikao kazi cha siku tatu cha Watunza Kumbukumbu na Maafisa Rasilimaliwatu Serikalini chenye lengo la kujadili masuala ya utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka katika Utumishi wa Umma kilichoanza leo jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Francis Michael akisisitiza jambo alipokuwa akifungua kikao kazi cha siku tatu cha Watunza Kumbukumbu na Maafisa Rasilimaliwatu Serikalini chenye lengo la kujadili masuala ya utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka katika Utumishi wa Umma kilichoanza leo jijini Dodoma.

Baadhi ya Washiriki wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Francis Michael (hayupo pichani) alipokuwa akifungua kikao kazi cha siku tatu cha Watunza Kumbukumbu na Maafisa Rasilimaliwatu Serikalini chenye lengo la kujadili masuala ya utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka katika Utumishi wa Umma kilichoanza leo jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Francis Michael akiwa katika kikao kazi cha siku tatu cha Watunza Kumbukumbu na Maafisa Rasilimaliwatu Serikalini chenye lengo la kujadili masuala ya utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka katika Utumishi wa Umma kilichoanza leo jijini Dodoma. Wa kwanza kushoto kwake ni Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi

Saturday, June 22, 2019

DKT. MWANJELWA ASHANGAZWA NA HALMASHAURI YA MANISPAA YA MOROGORO KUTOA KIWANJA KWA WAJASIRIAMALI KATIKA ENEO HATARISHI



Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Dkt. Kebwe Steven Kebwe alipomtembelea ofisini kwake kabla kuanza ziara ya kikazi ya kukagua vikundi vya wajasiriamali waliorasimishwa katika Manispaa ya Morogoro.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akisalimiana na Mwenyekiti wa kikundi cha usindikaji wa vyakula na viungo, Bi. Emmy Kiula wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua vikundi vya wajasiriamali waliorasimishwa katika Manispaa ya Morogoro.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akimsikiliza Mwenyekiti wa kikundi cha utengenezaji wa milango na madirisha ya chuma, Bw. Abdallah Chunga alipofanya ziara ya kikazi ya kukagua vikundi vya wajasiriamali waliorasimishwa katika Manispaa ya Morogoro.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akitoa maagizo kwa watendaji wa MKURABITA na Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro alipokuwa akihitimisha ziara yake ya kikazi ya kukagua vikundi vya wajasiriamali waliorasimishwa katika Manispaa ya Morogoro.

Friday, June 21, 2019

OFISI YA RAIS-UTUMISHI YAADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA KWA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro akizungumza na watumishi wa ofisi yake mara baada ya watumishi hao kukamilisha zoezi la usafi wa mazingira eneo la Mtumba jijini Dodoma ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2019. 

Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Maadili,  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Fabian Pokela akimwagilia maji moja ya mti uliopandwa  katika Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora eneo la Mtumba jijini Dodoma  ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2019. 

Baadhi ya watumishi  wa  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifanya usafi katika ofisi yao iliyopo Mji wa Serikali, eneo la Mtumba jijini Dodoma  ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2019.

Wednesday, June 19, 2019

SERIKALI HAITOSITA KUMCHUKULIA HATUA MTU YEYOTE ATAKAYEJIHUSISHA NA MASUALA YA RUSHWA



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt (Mst) Mhe. George Mkuchika (Mb), akifungua mjadala kuhusu Kuelekea Msimamo wa Pamoja wa Afrika kuhusu Urejeshwaji Mali wakati wa Kongamano la Siku Maalum ya Mapambano Dhidi ya Rushwa Barani Afrika iliyoadhimishwa kitaifa jijini Dodoma.

Baadhi ya washiriki wa Kongamano la Siku Maalum ya Mapambano Dhidi ya Rushwa Barani Afrika, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt (Mst) Mhe. George Mkuchika (Mb), alipokuwa akifungua mjadala kuhusu Kuelekea Msimamo wa Pamoja wa Afrika kuhusu Urejeshwaji Mali wakati wa kongamano hilo jijini Dodoma.

Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Kamishna wa Polisi, Diwani Athumani akitoa maelezo ya awali kuhusu Siku Maalumu ya Mapambano Dhidi ya Rushwa Barani Afrika wakati wa Kongamano la siku hiyo iliyoadhimishwa kitaifa jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt (Mst) Mhe. George Mkuchika (Mb) akimkabidhi mwongozo wa utendaji kazi mmoja wa wajumbe wa kamati ya uadilifu ya Chuo Kikuu cha Dodoma wakati wa Kongamano la Siku Maalum ya Mapambano Dhidi ya Rushwa Barani Afrika iliyoadhimishwa kitaifa jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt (Mst) Mhe. George Mkuchika (Mb) akipokea hati ya utambuzi wa mchango wake katika mapambano dhidi ya rushwa toka kwa viongozi wa Klabu ya Wapinga Rushwa ya Chuo Kikuu cha Dodoma, wakati wa Kongamano la Siku Maalum ya Mapambano Dhidi ya Rushwa Barani Afrika iliyoadhimishwa kitaifa jijini Dodoma.

Monday, June 17, 2019

MHE. MKUCHIKA AWAHIMIZA WAUMINI WA KIKRISTO KUCHANGIA HUDUMA ZA KIJAMII KWA MAENDELEO YA TAIFA

Waumini wa dini ya kikristo nchini wamehimizwa kutoa mchango kwenye maeneo mbalimbali  hususan katika kujenga makanisa, shule na hospitali ambazo zitatumika kutoa huduma za kijamii kwa ajili ya maendeleo ya taifa.
Wito huo umetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb) wakati wa ibada ya kuwawekea mikono Mashemasi na Makasisi wa   Kanisa la Anglikana Tanzania, Dayosisi ya Kondoa iliyofanyika katika kanisa la Mchungaji Mwema, Wilayani Kondoa.
Mhe. Mkuchika amewataka waumini wa kanisa hilo kuchangia maendeleo ya kanisa, kwani mafundisho ya kanisa yanawataka waumini kutoa kwa hiyari ili kuisaidia Serikali kuboresha huduma za kijamii ambazo ndio chachu ya maendeleo ya taifa.
 “Kanisa linatufundisha ni heri kutoa kuliko kupokea kwa kuwa tukitoa tunapata thawabu kwa Mungu” Mhe. Mkuchika amesisitiza.
Mhe. Mkuchika ameweka bayana kuwa, Kanisa la Anglikana Tanzania ni Kanisa la tatu kuwa na wafuasi wengi lakini katika shughuli za maendeleo limekuwa nyuma sana.
“Kanisa letu limekuwa nyuma katika uchangiaji wa shughuli za maendeleo hususan kujenga makanisa mengine, shule na hospitali. Ni lazima tubadilike kwa sababu Wamissionari wa Kigeni tuliowategemea sasa hawapo” Mhe. Mkuchika amesema.
Aidha, Mhe. Mkuchika alihamasisha uchangiaji wa ujenzi wa Kanisa ambapo takribani milioni nne zilipatikana.
Naye, Askofu Mkuu wa Kanisa hilo, Dkt. Given Gaula amemshukuru Mhe. Mkuchika kwa kujitoa katika kuhamasisha uchangiaji wa maendeleo ya kanisa na kuahidi kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali za kuleta  maendeleo katika Taifa.
“Pamoja na masuala ya kiimani na kiroho, Kanisa la Anglikana limejipanga kutoa elimu katika jamii kwa kujenga shule ya sekondari na ufundi katika Wilaya ya Chemba na shule ya awali katika eneo la Bicha” Dkt. Gaula amesema na kuongeza kuwa, kanisa hilo lina miradi mingine kama mradi wa hosteli na vikundi vya kijamii vya kujikwamua kiuchumi vinavyojulikana kama Church Community Mobilization Process.
Ibada ya kuwawekea mikono Mashemasi na Makasisi imehudhuriwa na viongozi wa serikali wa wilaya ya Kondoa, washirika wa Kanisa Anglikana kutoka Marekani, Uingereza na vikundi mbalimbali vya dini kutoka kanisa la Anglikana Dayosisi ya Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb) akizungumza wakati wa ibada ya kuwawekea mikono Mashemasi na Makasisi wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dayosisi ya Kondoa iliyofanyika katika kanisa la Mchungaji Mwema, Wilayani Kondoa.



Baadhi ya Mashemasi na Makasisi wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dayosisi ya Kondoa wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb) (hayupo pichani) wakati wa ibada ya kuwawekea mikono iliyofanyika katika kanisa la Mchungaji Mwema, Wilayani Kondoa.



Askofu wa Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Rochester, Uingereza, James Langstaff na Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Kondoa, Dkt. Given Gaula, wakiwawekea mikono Mashemasi wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dayosisi ya Kondoa wakati wa ibada iliyofanyika katika kanisa la Mchungaji Mwema, Wilayani Kondoa.

Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Kondoa, Dkt. Given Gaula akizungumza wakati wa ibada ya kuwawekea mikono Mashemashi na Makasisi wa Kanisa la Anglikana Tanzania Dayosisi ya Kondoa iliyofanyika katika kanisa la Mchungaji Mwema, Wilayani Kondoa.





Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Chemba, Mhe. Simon Odunga kabla ya kuanza kwa  wa ibada ya kuwawekea mikono Mashemasi na Makasisi wa  Kanisa la Anglikana Tanzania, Dayosisi ya Kondoa iliyofanyika katika kanisa la Mchungaji Mwema, Wilayani Kondoa.



Thursday, June 13, 2019

TANZANIA KURATIBU MAADHIMISHO YA SIKU YA UTUMISHI WA UMMA BARANI AFRIKA KWA MWAKA 2019



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt (Mst) Mhe. George Mkuchika (Mb), akizungumza na vyombo vya habari jijini Dododma kuhusu Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2019. Kulia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa

Baadhi ya Waandishi wa Habari wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt (Mst) Mhe. George Mkuchika (Mb), alipokuwa akizungumza nao kuhusu Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2019

MAKATIBU WA MAWAZIRI NA MAKATIBU WA NAIBU MAWAZIRI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUWAJENGEA UWEZO KIUTENDAJI


Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Francis Michael akifungua mafunzo ya Makatibu wa Mawaziri na wa Naibu Mawaziri ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji yaliyofanyika jijini Dodoma. 
Baadhi ya Makatibu wa Mawaziri na wa Naibu Mawaziri wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Francis Michael (hayupo pichani) alipokuwa akifungua mafunzo yao ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji yaliyofanyika jijini Dodoma. 
Mratibu wa Wasaidizi wa Viongozi, Bw. John Kiswaga akiwasilisha hoja kwa Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Francis Michael wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji yaliyofanyika jijini Dodoma. 
Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Francis Michael akiwa katika picha ya pamoja na Makatibu wa Mawaziri na wa Naibu Mawaziri baada ya kufungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji yaliyofanyika jijini Dodoma. 


Tuesday, June 11, 2019

Monday, June 10, 2019

KAMPASI ZA CHUO CHA UTUMISHI WA UMMA KUSHINDANISHWA KIUTENDAJI ILI KUBORESHA HUDUMA ZAKE



Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania kampasi ya Tabora katika kikao kilichofanyika chuoni hapo mkoani Tabora.

Kaimu Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) akiwasilisha ripoti ya chuo wakati wa kikao kati ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya UtumishiwaUmma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) (kulia) na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania kampasi ya Tabora.

Mkurugenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma kampasi ya Tabora, Dkt. Ramadhan Marijani akijibu hoja za Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) (kushoto) wakati wa kikao kati ya Naibu Waziri na watumishi wa chuo hicho.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akichapa kwa mashine alipotembelea Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania kampasi ya Tabora. Wanaoshuhudia ni Kaimu Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Dkt. Emmanuel Shindika (kushoto) na Mkurugenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma kampasi ya Tabora, Dkt. Ramadhan Marijani.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb)  akikagua jengo jipya la ghorofa mbili la Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania kampasi ya Tabora. Wengine ni Mkurugenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma tawi la Tabora, Dkt. Ramadhan Marijani na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania.