Wednesday, July 22, 2026

WARATIBU WA KUDHIBITI VVU, UKIMWI NA MAGONJWA SUGU YASIYOAMBUKIZA WATAKIWA KUTOA ELIMU JUU YA UDHIBITI MAGONJWA MAHALI PA KAZI ILI KUFIKIA MALENGO YA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050

 Veronica Mwafisi -Dodoma

Tarehe 22 Julai, 2026

Waratibu wa ngazi ya Mikoa Mahali pa Kazi katika Utumishi wa Umma wametakiwa Kutoa elimu kwa watumishi wa umma juu ya udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza ili kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inayolenga kujenga taifa lenye watu wenye afya, tija, ustawi na ufanisi ambao watatoa huduma bora kwa wananchi.

Kauli hiyo imetolewa leo na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato wakati akifungua semina elekezi kwa Waratibu wa ngazi ya Mikoa kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.

Dkt. Kato amesema katika kutekeleza afua za kuimarisha afya kwa watumishi ni vema kuwa na program za upimaji wa afya pamoja na mazoezi ya viungo kwa watumishi katika maeneo yao ya kazi ili kufikia utekelezaji huo wa Dira 2050.

Ameongeza kuwa, itakuwa vema kuandaa mafunzo pia kwa watumishi pamoja na msaada wa kisaikolojia ili kuwasaidia zaidi katika utekelezaji wa majukumu yao.   

Aidha, Dkt. Kato amewataka waratibu hao kuandaa taarifa za utekelezaji wa Mwongozo na Waraka Na. 2 wa mwaka 2014 kuhusu kudhibiti VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali pa Kazi katika Utumishi wa Umma ikiwa ni pamoja na kuwajengea uwezo.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii ambaye ni Afisa Ustawi wa Jamii Mkuu, Bi. Herieth Mpili akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi amesema kuwa lengo la semina hiyo ni kukuza uelewa na ufahamu juu ya majukumu ya Waratibu hao na kuwawezesha kuandaa mipango ya muda mrefu na mfupi wa utekelezaji wa afua za kudhibiti Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali pa Kazi katika Utumishi wa Umma ili kuleta ufanisi katika utekelezaji wa majukumu kama ilivyokusudiwa na Serikali.

Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora itaendelea kushirikiana na Sekretarieti za Mikoa yote nchini kwa lengo la kusimamia masuala ya Anuai za Jamii na kutoa mafunzo kwa maafisa au waratibu watakaoteuliwa kuratibu afua hizo katika mikoa yao ili kuhakikisha kunakuwa na afya imara na ustawi wa watumishi wote nchini.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato akizungumza na Waratibu wa ngazi ya Mikoa wakati wa semina elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.


Sehemu ya Waratibu wa ngazi ya Mikoa wakimsikiliza, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato wakati akifungua semina elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.


Sehemu ya Waratibu wa ngazi ya Mikoa wakimsikiliza, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato wakati akifungua semina elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.


Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii ambaye ni Afisa Ustawi wa Jamii Mkuu, Bi. Herieth Mpili akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Dkt. Charles Kato kuzungumza na Waratibu wa ngazi ya Mikoa wakati wa semina elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.


Afisa Maendeleo ya Jamii, Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Neema Range akifafanua jambo wakati akiwasilisha mada kuhusu Anuai za Jamii na Ujumuishwaji wa Mwongozo Wa Kudhibiti VVU, UKIMWI na MSY na Waraka (2014) kwa Waratibu wa ngazi ya Mikoa wakati wa semina elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.


Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Dkt. Garvin Kweka akisisitiza jambo wakati akiwasilisha mada kuhusu Afya ya Akili kwa Waratibu wa ngazi ya Mikoa wakati wa semina elekezi iliyoandaliwa na Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.


Sehemu ya Waratibu wa ngazi ya Mikoa wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa semina elekezi iliyoandaliwa na Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma. 


Mratibu wa ngazi ya Mkoa kutoka Kagera ambaye ni Afisa Rasilimaliwatu Mkuu, Bw. Emily Ishegoma akiwasilisha maoni yake wakati wa majadiliano kwenye semina elekezi iliyoandaliwa na Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.


Mwakilishi kutoka Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania, Dkt. Theresiaglory Tety akifafanua jambo alipokuwa akiwasilisha mada kuhusu Hali Halisi kuhusu VVU na UKIMWI wakati wa semina elekezi kwa Waratibu wa ngazi ya Mikoa iliyoandaliwa na Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.


Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Waratibu wa ngazi ya Mikoa mara baada ya kufungua semina elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.


Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Waratibu wa ngazi ya Mikoa mara baada ya kufungua semina elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.


Maafisa kutoka Idara ya Uendelezaji Sera, Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia jambo wakati wa semina elekezi kwa Waratibu wa ngazi ya Mikoa kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.


Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Sekretarieti kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI mara baada ya kufungua semina elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.


Sehemu ya Waratibu wa ngazi ya Mikoa wakimsikiliza, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato wakati akifungua semina elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.





 

Monday, July 20, 2026

DAFTARI LA HUDUMA ZA SERIKALI (GSD) KUIMARISHA UTOAJI WA HUDUMA ZA UMMA KWA NJIA YA KIDIJITI

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 20 Julai, 2026.

 

Daftari la Huduma za Serikali (GSD) ni Mfumo wa kidijitali ambao unalenga kuwapatia wananchi, wafanyabiashara na wageni fursa taarifa na maombi ya huduma za serikali katika Wizara, Idara, Wakala, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa hivyo, kurahisisha utoaji wa huduma kwa umma kwa njia ya kidijiti.

 

Hayo yameelezwa leo na Kaimu Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Mifumo na Viwango vya Kimenejimenti kutoka Idara ya Uendelezaji Taasisi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Noah Mkasanga wakati akiwasilisha mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali kwenye mafunzo ya kuwajengea uwezo Watumishi wa Ofisi hiyo iliyopo Mtumba Jijini Dodoma.

Bw. Noah amesema kuwa, kupitia mfumo wa GSD wananchi wataweza kupata huduma zote za Serikali kidijitali kupitia dirisha moja, ikiwa ni pamoja na kuona huduma zinazotolewa, gharama zake, masharti au vitu vinavyohitajika ili kupata huduma na namna ya kuzipokea hata wakiwa nyumbani kwa kutumia anwani za makazi (NAPA).

“Daftari hili linarahisisha utoaji wa huduma mbalimbali za Serikali kwa umma kupitia dirisha moja kwa kuainisha huduma zote zinazotolewa na taasisi za umma pamoja na mahitaji yao na kuziweka wazi kwa wananchi wanapotaka kupata huduma husika kwa njia ya kidijiti”, amesema Bw. Noah.

 

Akifafanua kuhusu umuhimu wa Daftari la Huduma za Serikali (GSD) Bw. Noah amesema, litaongeza ufanisi na uwajibikaji ikiwa ni pamoja na kupunguza gharama kwa wateja na urahisi wa kutoa huduma kupitia mfumo mmoja.

Kadhalika, Bw. Noah, amesema kuwa Daftari la Huduma za Serikali (GSD) litasaidia kupunguza mianya ya rushwa kwa kuwa huduma hiyo inatolewa kwa njia ya kidijitali.

 

Kuanzishwa kwa Daftari la Huduma za Serikali (GSD) ni jitihada za Serikali za kutumia teknolojia ya kisasa katika kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi na kuimarisha usalama wa taarifa za umma.

Kaimu Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Mifumo na Viwango vya Kimenejimenti kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Noah Mkasanga akiwasilisha mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika kila Jumatatu kwa watumishi hao katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi Wasaidizi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Kaimu Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Mifumo na Viwango vya Kimenejimenti kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Noah Mkasanga akifafanua jambo kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika kila Jumatatu kwa watumishi hao katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi Wasaidizi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi, Wakurugenzi Wasaidizi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakiwa katika mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakiwa katika mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.



Monday, July 13, 2026

KATIBU MKUU MKOMI AWATAKA WATUMISHI KUONGEZA KASI YA UTENDAJI KUFIKIA MALENGO YA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050

Na. Antonia Mbwambo – Dodoma

13 Julai, 2026

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, amewataka Watumishi wa Umma kuongeza kasi ya utendaji na kuzingatia weledi ili kuchangia kikamilifu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Katibu Mkuu Mkomi ametoa wito huo leo Julai 13, 2026, wakati akihitimisha mafunzo kuhusu umuhimu wa afya ya akili kwa Watumishi wa Umma yaliyofanyika katika eneo maalumu la Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Mtumba, jijini Dodoma kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi hao.

Bw. Mkomi amesema mafanikio ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 yanategemea uwepo wa Watumishi wa Umma wenye afya bora ya akili, maadili ya kazi, ubunifu na uwajibikaji, huku akisisitiza kuwa afya ya akili ni msingi wa utendaji wenye tija na utoaji wa huduma bora Serikalini.

"Afya ya akili si suala la mtu mmoja mmoja, bali ni msingi wa kuongeza tija katika Utumishi wa Umma. Mtumishi mwenye afya bora ya akili anakuwa na uwezo mkubwa wa kutoa huduma bora, kushirikiana na wenzake na kuleta matokeo chanya kwa Taasisi na Taifa kwa ujumla," amesema Bw. Mkomi.

Aidha, Bw. Mkomi amewaelekeza Wachumi wa Ofisi hiyo kufanya tafakuri za kitaaluma na kuibua mawazo bunifu yatakayochangia Serikali kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Kwa upande wake, Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma Elias, ambaye alikuwa Mwezeshaji wa mafunzo hayo, amesema afya ya akili ni nguzo muhimu ya ustawi wa mtumishi na ina mchango mkubwa katika kuongeza tija pamoja na kuboresha mazingira ya kazi.

Ameeleza kuwa changamoto za afya ya akili kwa watumishi wa Umma mara nyingi husababishwa na mpangilio duni wa kazi, mzigo mkubwa wa majukumu unaozidi uwezo wao, kazi za kujirudia rudia na mazingira magumu ya kazi. Amewahimiza watumishi kuzingatia mtindo bora wa maisha kwa kufanya mazoezi ya mara kwa mara, kula lishe bora, kupata mapumziko ya kutosha na kutafuta ushauri wa Wataalamu wanapokabiliwa na changamoto za afya ya akili.

Aidha, Dkt. Elias amewataka viongozi kuendelea kuzingatia usawa kwa watumishi wanaowasimamia, kupinga unyanyapaa dhidi ya wenye changamoto za afya ya akili na kutambua mapema dalili za changamoto hizo ili kuwawezesha watumishi kupata huduma stahiki kwa wakati.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akifurahia jambo wakati alipokuwa akihitimisha mafunzo ya uelewa kwa Watumishi wa Ofisi hiyo Julai 13, 2026 Mtumba Jijini Dodoma

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, akizungumza na Watumishi wa Ofisi yake wakati alipokuwa akihitimisha Mafunzo ya uelewa kuhusu Umuhimu wa Afya ya Akili kwa Watumishi wa Umma yaliyofanyika Julai 13, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo, Mtumba jijini Dodoma 

Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Idara na Vitengo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma.

Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma

Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma Elias akitoa mada ya mafunzo kuhusu Umuhimu wa Afya ya Akili kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora yaliyofanyika Julai 13, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Jijini Dodoma

Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Idara na Vitengo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma.

Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma Elias akitoa mada ya mafunzo kuhusu Umuhimu wa Afya ya Akili kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora yaliyofanyika Julai 13, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Jijini Dodoma

Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Idara na Vitengo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma.

Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.


Baadhi ya Wakurugenzi na Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma

Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.


Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.


Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.


Sunday, July 12, 2026

ZIARA YA KIKAZI YA MHE. RIDHIWANI KIKWETE MKOANI TABORA

YALIYOJIRI KATIKA ZIARA YA KIKAZI YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA, MHE. RIDHIWANI KIKWETE ILIYOLENGA KUKAGUA NA KUZINDUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI TABORA