Friday, July 10, 2026

MHE. RIDHIWANI ASISITIZA WAAJIRI KUTILIA MKAZO SUALA LA MSAWAZO KWA WATUMISHI ILI KUPUNGUZA CHANGAMOTO YA UHABA WA WATUMISHI

Na. Veronica Mwafisi-Urambo

Tarehe 10 Julai, 2026

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amewakumbusha Waajiri katika Taasisi za Umma kutilia mkazo suala la msawazo kwa Watumishi ili kupunguza changamoto ya uhaba wa watumishi katika maeneo mbalimbali kwenye sekta hiyo ya umma kwa lengo la kuwatumikia wananchi kwa ufasaha.

 

Mhe. Kikwete amesema hayo leo tarehe 10 Julai, 2026 wakati akizungumza na Viongozi, Watumishi wa Umma na Wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Urambo mkoani Tabora baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa kituo cha Polisi Usoke.

 

Amesema kabla ya Waajiri kulalamika changamoto ya uhaba wa watumishi, ni vema wakakaa na kufanya msawazo ili kujiridhisha kama kweli wana changamoto hiyo katika maeneo yao kabla ya kuomba kupatiwa watumishi wapya.

 

“Utakuta kuna taasisi watumishi wa kada fulani wamerundikana katika kituo kimoja cha kazi huku kituo cha kazi cha jirani kina uhaba wa watumishi wa kada hiyo, au Waajiri kaeni, fanyeni msawazo, kabla ya kulalamikia changamoto hiyo ya uhaba wa watumishi,” ameongeza Mhe. Kikwete.

 

Ameongeza kuwa kuna taasisi unakuta kuna watumishi wa kada fulani ambao sio hawahitajiki sana katika taasisi fulani kutokana na majukumu yake lakini wapo huku taasisi yenye uhitaji wa watumishi wa kada hiyo hakuna.

 

Katika hatua nyingine Mhe. Kikwete amewataka wananchi wa Kata ya Usoke kukitunza kituo cha Polisi kinachojengwa katika kata hiyo ili kiwasaidie katika kupambana na uhalifu.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Viongozi, Watumishi wa Umma na Wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Urambo baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa kituo cha Polisi Usoke wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wakwanza kulia) akiwa katika mkutano mara baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi katika kituo cha Polisi Usoke, Halmashauri ya Wilaya ya Urambo wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akikata utepe kuzindua ujenzi wa kituo cha Polisi Usoke katika Halmashauri ya Wilaya ya Urambo baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyevaa miwani) akipiga makofi mara baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi katika kituo cha Polisi Usoke, Halmashauri ya Wilaya ya Urambo wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisikiliza taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa kituo cha Polisi Usoke katika Halmashauri ya Wilaya ya Urambo kabla ya kukagua na kuweka jiwe la msingi wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.


Viongozi, Watumishi wa Umma na Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi katika kituo cha Polisi Usoke, Halmashauri ya Wilaya ya Urambo wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.


 







 

No comments:

Post a Comment