Saturday, March 14, 2026

“UJENZI WA OFISI YA TAKUKURU NYANG’HWALE NI UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM WA KUPAMBANA NA RUSHWA, HEKO KWA VIONGOZI WA OFISI YA RAIS UTUMISHI NA UTAWALA BORA NA WATENDAJI WA TAKUKURU’’- Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro

Na Veronica Mwafisi-Nyang’hwale

Tarehe 14 Machi, 2026

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imewapongeza Viongozi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watendaji wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa utekelezaji mzuri wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2025 kuhusiana na mapambano dhidi ya rushwa.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 14 Machi, 2026 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt.  Damas Ndumbaro wakati wa ziara ya Kamati hiyo iliyolenga kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.  

Akizungumza kwa niaba ya Kamati yake, Mhe. Dkt. Ndumbaro amesema CCM ilipokuwa inaomba kura kwa wananchi wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 iliahidi mambo mengi ikiwemo kupambana na rushwa na kuitokomeza, jambo ambalo limetekelezwa kwa ufasaha kwa kujenga Ofisi za TAKUKURU katika maeneo mbalimbali nchini na kuanzisha klabu za wapinga rushwa mashuleni.

“Serikali ya Awamu ya Sita inatekeleza Ilani, tumeona Ilani imetekelezwa kweli kweli katika kuzuia na kupamba na rushwa. Chama kiliahidi, sisi kama Wabunge jukumu letu ni kukagua kuona imetekelezwaje, hapa tunaona ilani imetekelezwa kwa asilimia100 kwani tumeridhishwa na ujenzi huu wa Ofisi ya TAKUKURU Nyang’hwale,” ameongeza.

Mhe. Dkt. Ndumbaro ametoa maelekezo kwa Viongozi wa Ofisi hiyo kuendelea kusimamia ubora wa majengo yote yatakayojengwa na ujenzi wa ofisi zote za TAKUKURU nchini.

Akitoa maelezo ya awali ya utekelezaji wa mradi wa jengo la TAKUKURU Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameishukuru Kamati hiyo kwa maelekezo na miongozi mbalimbali ambayo wamekuwa wakiyatoa na kufanikisha utekelezaji mzuri wa majukumu ya Ofisi anayoiongoza ikiwemo ujenzi wa jengo hilo la TAKUKURU.

Mhe. Kikwete amesema mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi milioni 386 ambapo utekelezaji wake ulifuata taratibu zote za manunuzi kwa kuongozwa na sheria ya manunuzi na umetekelezwa kupitia Force Account.  

Mhe. Kikwete ameahidi kuendelea kutekeleza maelekezo yote ambayo yatatolewa na Kamati hiyo ili kuboresha utendaji kazi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa maendeleo ya taifa.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa TAKUKURU, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila amesema tangu kuanzishwa kwake TAKUKURU imekuwa ikikabiliwa na uhaba wa majengo lakini katika kutatua changamoto hiyo, Serikali imekuwa ikijitahidi kujenga na kutafuta majengo ya kupanga ili kutekeleza majukumu yake ya kuzuia na kupamba na rushwa.

Amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuweka kipeumbele na kuchukua hatua mbalimbali ili kuiimarisha taasisi hiyo katika utekelezaji wa majukumu yake ikiwemo kutenga bajeti kwa ajili ya kujenga majengo yenye miundombinu ya kisasa na kukarabati majengo ya zamani,” ameongeza Bw. Chalamila



Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akizungumza mara baada ya kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (kulia) akifuatilia jambo wakati walipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita. Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro kuzungumza na Watumishi wa TAKUKURU na Wananchi wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakipata maelezo ya Mradi wa ujenzi wa jengo lililojengwa katika Wilaya ya Nyang’hwale, mkoani Geita mara baada Wajumbe wa Kamati hiyo kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU. Watatu kutoka kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro kuzungumza na Watumishi wa TAKUKURU na Wananchi wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Katikati) akifuatilia jambo wakati walipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita. Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete na kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila


Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila akieleze utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria mara baada ya Wajumbe hao kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo hilo lililopo Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati hiyo kuzungumza na Watumishi wa TAKUKURU na Wananchi wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.


Wakuu wa Vitengo wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya Kamati yake kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU lililopo Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.


Muonekano wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita ambalo Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria walitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo hilo.


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (wa pili kutoka kushoto) akifurahia  jambo wakati walipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita. Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete na kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale Mhe. Grace Kingalame


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati hiyo kuzungumza na Watumishi wa TAKUKURU na Wananchi wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.


Maafisa wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza mara baada ya Kamati yake kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.


Sehemu ya Watumishi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya Kamati yake kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU lililopo Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuingia katika ofisi za TAKUKURU ambayo ni moja ya Taasisi zilizopo chini ya ofisi yake ambapo Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria ilitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati hiyo mara baada ya kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’wale, Mkoani Geita. 


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mara baada ya Kamati hiyo kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’wale, Mkoani Geita. 


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wanafunzi wa klabu ya wapinga Rushwa Wilaya ya Nyang’wale, Mkoani Geita. 






 

 

 

 

Thursday, March 12, 2026

KATIBU MKUU-UTUMISHI AWASISITIZA WATUMISHI WA UMMA KUFANYA KAZI KWA BIDII ILI KULETA TIJA KATIKA JAMII


 

Na. Antonia Mbwambo na Eric Amani-Dodoma.

Tarehe 12 machi, 2026

 

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, amewasisitiza Wajumbe wa Baraza la wafanyakazi la Ofisi yake kufanya kazi kwa bidii na weledi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za utendaji ili kuleta mabadiliko yenye tija kwa maendeleo ya taifa.

 

Bw. Mkomi ameyasema hayo leo tarehe 12 Machi, 2026 wakati wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora uliolenga kupitisha Mpango na Bajeti ya Ofisi hiyo ya Mwaka wa Fedha 2026/27 uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.

“Katika kufikia Utumishi wa Umma uliotukuka, nitoe wito kwa wajumbe wote wa baraza, kutekeleza majukumu yenu ipasavyo ili kutoa huduma bora itakayotatua changamoto za wananchi.” Bw. Mkomi alisema.

 Aidha Katibu Mkuu Mkomi amewataka wajumbe wa mkutano huo kuhakikisha kunakuwa na ushirikishwaji wa Watumishi katika mikakati inayopangwa na  kamati hiyo ili kuongeza uelewa wa masuala ya kiutumishi na kuwa na mtazamo chanya utakaoleta ufanisi katika utendaji wao .

 Ameongeza kuwa ni muhimu kukawa na mafunzo kwa wajumbe wa Baraza hilo ili kuwajengea uwezo kwa matokeo chanya katika maeneo yao ya kazi.

 Bw. Mkomi alimshukuru mwakilishi wa Katibu Mkuu TUGHE Taifa, ambaye ni Mwenyekiti wa TUGHE Mkoa wa Dodoma Bw. Maulidi Kipeneku kwa ushiriki wake katika mkutano huo na kuahidi kuwa Ofisi ya Rais-UTUMISHI itashirikiana na TUGHE wakati wote katika kuhakikisha Baraza linatekeleza majukumu yake kikamilifu.

 Awali Bw. Kipenuke aliipongeza Ofisi hiyo kwa kuzingatia sheria ya kufanya baraza ya wafanyakazi kwa wakati. “Mmekuwa kioo, mabaraza yanafanyika kwa wakati na ni shirikishi, huku akiwatasisitiza wajumbe kutoa michango yao ili kuwawakilisha kwa ufasaha watumishi katika Idara na Vitengo vyao.” Alisisitiza Bw. Kipenuke.   

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiweka Saini katika kitabu cha wageni leo katika uKumbi wa Nyaraka mara baada ya kuwasili kwa ajili ya mkutano wa baraza la wafanyakazi la Ofisi yar a Rais  - UTUMISHI leo  machi  12, 2026 Jijini Dodoma.


Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa TUGHE Taifa ambaye pia mwenyekiti wa TUGHE MKOA wa Dodoma Bw. Maulid Kipeneku akitoa neno la salamu kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - UTUMISHI Bw. Juma Mkomi na washiriki wote wa mkutano wa baraza la wafanyakazi katika ofisi ya Rais – UTUMISHI jijini Dodoma Machi 12, 2026.

Picha ya Pamoja ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiwa pamoja na Washiriki wa wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora mara baada ya Kumalizika kwa Mkutano wa Baraza hilo leo machi 12, 2026 Jijini Dodoma.



Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi katika Ofisi ya Rais – UTUMISHI ambaye pia ni Mkutubi mwandamizi katika kitengo cha Mawasiliano Bi. Halima Rauna akijiitambulisha wa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – UTUMISHI Bw. Juma Mkomi wakati wa utambulisho wa washiriki wote wa Mkutano huo Machi 12, 2026 katika ukumbi wa Nyaraka Uliyopo Jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakipitia agenda za mkutano wa Baraza la Wafanyakazi katika ofisi ya Rais – UTUMISHI leo Macji 12, 2026 jijini Dodoma. 


Afisa Mchumi kutokea Idara ya Mipango Ofisi ya Rais - UTUMISHI Ndg. Rifati H. Almasi akiwasilisha mada kwa Katibu Mkuu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Bw. Juma Mkomi wakati wa uwasilishaji mada katika na Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Machi 12, 2026 Jijini Dodoma

Picha ya Pamoja ya Washiriki wa Mkutano wa Baraza la wafanyakazi  katika Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora katika Mkutano wa baraza hilo uliyofanyika Leo Machi 12, 2026 jijini Dodoma ambapo Mkutano huo uliongozwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - UTUMISHI Bw. Juma Mkomi.



                                                                                                                                                                                             

NAIBU WAZIRI QWARAY ATOA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA KUTUMIA MFUNGO WA MWEZI WA RAMADHANI NA KWARESMA KUJITAFAKARI JUU YA HUDUMA WANAZOZITOA KWA WANANCHI

Na Mwandishi Wetu-Dodoma

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray ametoa wito kwa Watumishi wa Umma nchini kutumia kipindi hiki cha Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani na Mafungo ya Kwaresma kujitafakari juu ya namna wanavyotoa huduma kwa wananchi.

Naibu Waziri Qwaray ametoa wito huo wakati wa futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo katika kipindi hiki ambapo Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo wanakuwa katika mfungo.

Mhe. Qwaray amesema watumishi wa umma wanatakiwa kufanya kazi kwa uadilifu, huruma na unyenyekevu huku wakimtanguliza Mungu hivyo ni vema wakajitafakari  kama hayo yote yanafanyika. 

Ameongeza kuwa, kipindi cha mfungo kisiwe cha kushinda njaa bali iwepo thawabu kwa Mungu ambayo itatokana na huduma bora zitakazotolewa na watumishi hao kwa wananchi itakayoleta matokeo chanya kwa ustawi wa nchi.

Aidha, amepongeza Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa kuwakumbuka wahitaji ambao walijumuika nao katika futari hiyo maalum iliyokutanisha makundi ya watu tofauti ambayo yanasaidia kubadilishana uzoefu ili kuboresha utendakji kazi hasa katika kutoa huduma bora kwa wananchi.

Amesisitiza kuendelea kuiombea nchi na viongozi. “Niwasisitize tuendelee kuiombea nchi yetu na tuitunze amani tuliyonayo, sisi sote ni wamoja na ni Watanzania hatuulizani dini wala kabila,alisisitiza Mhe. Qwaray.

Awali Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Juma Mkomi alisema futari hiyo iliandaliwa kwa lengo la kuwaweka pamoja watu wa makundi mbalimbali hasa katika Mfungo wa Mwezi wa Ramadhani na Kwaresma.

Bw. Mkomi aliongeza kuwa ni fursa nzuri kukutana kwa wakati mmoja kwani ibada hizo huwafanya kuwa wacha Mungu jambo ambalo husaidia watumishi kuwa na maadili ya kuwatendea haki wananchi wanaowahudumia.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na Watendaji na Watumishi wa ofisi hiyo wakati wa futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray kuzungumza na Watendaji na Watumishi wa ofisi hiyo wakati wa futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.


Sehemu ya Watendaji na Watumishi wa ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa kwenye hafla ya futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akiwa katika picha ya pamoja na  Watendaji, Watumishi wa ofisi hiyo na wageni waalikwa mara baada ya kupata futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wakuu wa Taasisi wa Ofisi hiyo mara baada ya kupata  futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma. Wa pili kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa kwenye futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.

Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa kwenye futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.