Thursday, July 9, 2026

MHE. KIKWETE AWASILI WILAYA YA SIKONGE MKOANI TABORA, AENDELEA NA ZIARA YAKE YA KIKAZI KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora akiendelea na ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua, kuzindua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kusikiliza changamoto za wananchi katika Mkoa huo.

 












TASAF AWAMU YA III YAJA, VIONGOZI ZINGATIENI VIGEZO VYA KUWAPATA WALENGWA KUEPUSHA MALALAMIKO YALIYOJITOKEZA AWAMU ZILIZOPITA - Mhe. Ridhiwani

Na. Veronica Mwafisi-Manispaa ya Tabora

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amewataka Viongozi mkoani Tabora kuzingatia vigezo vya kuwapata walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaoratibiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).

 

Mhe. Kikwete amesema moja ya jambo kubwa ambalo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa akilisisitiza ni kusaidia Watanzania walio wanyonge. “TASAF awamu zilizopita illishia mwaka jana mwezi wa 9 lakini kwa upendo wake amepambana kuhakikisha fedha zinapatikana ili kusaidia Watanzania hao kuepukana na umaskini,” Mhe. Kikwete ameongeza.

 

Akizungumza na Wananchi katika Manispaa ya Tabora tarehe 9 Julai, 2026, baada ya kuhitimisha ziara yake kwa siku ya leo aliyoifanya katika Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Halmashauri ya Wilaya ya Tabora na Manispaa ya Tabora ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo, Mhe. Ridhiwani amesema sio sawa fedha hizo zikatumika kinyume kwa kuwaingiza kwenye Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini watu wasiostahili. “Niwaombe mliopewa dhamana ya kusimamia zoezi hili kutenda haki kwa kuwaweka walengwa stahiki,” Mhe. Kikwete ameongeza.

 

Amesema kuna baadhi ya maeneo yalilalamikiwa kwa kufanya mambo ya ajabu na kutowatendea haki walengwa katika fedha walizokuwa wakipewa, niwaombe sana, tunapoanza mpango unaokuja, nisingependa yale mapungufu yaliyojitokeza kipindi cha nyuma yajirudie.

 

Ametoa wito kwa Wananchi kushiriki katika mikutano ya kutambua walengwa ili wapatikane watu sahihi. “Wananchi nanyi kwa kuwa mnashiriki katika mikutano ya kuibua walengwa, mkisomewa majina ya walengwa kama kuna ambao wameachwa mseme ili waongezwe na kama wamewekwa wasiostahili pia mseme ili watolewe kwani mkikaa kimya ndio matokeo yake wanaingizwa wasiostahili na baadae kuleta malalamiko.” ameongeza

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Wananchi kuhusu Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Manispaa ya Tabora wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo aliyoifanya katika Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Halmashauri ya Wilaya ya Tabora na Manispaa ya Tabora iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Sehemu ya Wananchi katika Manispaa ya Tabora wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete alipokuwa akizungumza kuhusu Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Manispaa ya Tabora wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo aliyoifanya katika Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Halmashauri ya Wilaya ya Tabora na Manispaa ya Tabora iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifurahia jambo na Mjasiriamali wakati Waziri huyo alipokuwa akiwasili kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Manispaa ya Tabora wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo aliyoifanya katika Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Halmashauri ya Wilaya ya Tabora na Manispaa ya Tabora iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na Wazee wa Manispaa ya Tabora wakati Waziri huyo alipokuwa akiwasili kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Manispaa ya Tabora wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo aliyoifanya katika Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Halmashauri ya Wilaya ya Tabora na Manispaa ya Tabora iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama na Wananchi wa Manispaa ya Tabora wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi aliyoifanya katika Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Halmashauri ya Wilaya ya Tabora na Manispaa ya Tabora iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Sehemu ya Wananchi katika Manispaa ya Tabora wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete alipokuwa akizungumza kuhusu Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Manispaa ya Tabora wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo aliyoifanya katika Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Halmashauri ya Wilaya ya Tabora na Manispaa ya Tabora iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akicheza nyimbo ya ukaribisho katika Manispaa ya Tabora alipokuwa akiwasili kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Manispaa ya Tabora wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo aliyoifanya katika Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Halmashauri ya Wilaya ya Tabora na Manispaa ya Tabora iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

 

 

 



Wednesday, July 8, 2026

SIMAMIENI KIKAMILIFU UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO ILI THAMANI YA FEDHA IONEKANE-“Mhe. Ridhiwani

Na. Veronica Mwafisi-Sikonge na Tabora

Tarehe 09 Julai, 2026

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameisihi Kamati ya Miradi ya Maendeleo mkoani Tabora kusimamia kwa umakini miradi inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali mkoani humo ili iendane na thamani halisi ya fedha.

 

Mhe. Kikwete amesema hayo kwa nyakati tofauti leo tarehe 9 Julai, 2026 katika Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, Halmashauri ya Wilaya ya Tabora na Manispaa ya Tabora wakati akikagua na kuweka jiwe la msingi na kuzindua utekelezaji wa miradi ya maendeleo mkoani Tabora.

 

Amesema katika kuhakikisha nchi inakuwa na maendeleo kwenye sekta zote, Serikali itaendelea kutoa fedha za miradi ya maendeleo, hivyo ni jukumu la wasimamizi kusimamia kwa ufasaha ili miradi hiyo itekelezwe kikamilifu kulingana na fedha inayotolewa.

 

Akizungumza mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika kituo cha afya cha Igigwa, Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Mhe. Kikwete amesema ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho na kusema Serikali inahitaji eneo kubwa ili kujenga majengo mengi zaidi kwa lengo la kuwa na huduma mbalimbali za afya.

 

“Kituo hiki cha afya ni kwa ajili ya wagonjwa wa nje, hivyo tunahitaji eneo kubwa zaidi ili tuweke majengo mengi kwa lengo la kutoa huduma mbalimbali za afya kwa wananchi,” ameongeza.

 

Akizungumza katika hatua nyingine mara baada ya kuzindua majengo ya Shule ya Msingi Kigamboni katika Halmashauri ya Wilaya ya Tabora, Mhe. Kikwete amesema Sera ya Elimu ni kuhakikisha vijana wanapata elimu jirani badala ya kutembea umbali mrefu.

 

Amesema lengo la Serikali ni kupunguza adha ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kutafuta elimu na ndio maana inajenga shule jirani ili wapate muda mrefu wa kusoma badala ya kutumia muda huo kutembea.

 

Aidha, ameongeza kuwa wingi wa majengo unasaidia kupunguza idadi ya wanafunzi kurundikana kwenye darasa moja na kuwarahisishia Walimu kufundisha na wanafunzi kupata uelewa.

 

“Zamani wakati sisi tunasoma, darasa moja lilikuwa na wanafunzi wengi kwasababu madarasa yalikuwa machache, lakini sasa hivi madarasa mengi hivyo wanafunzi katika darasa moja hawazidi 45, aidha Walimu wanapata muda wa kuwa na wanafunzi karibu wanaoweza kuwamudu, wanafunzi sasa hivi mtake wenyewe kufeli,” ameongeza.

 

Amesema akiwa ndiye Waziri mwenye dhamana wa masuala ya Utumishi, atahakikisha anasimamia zoezi la kupatikana kwa Walimu wa kutosha ili wanafunzi wapate elimu bora.

 

“Majengo yamejengwa, ni mazuri, hata sehemu nyingine mjini hakuna majengo kama haya, hivyo wanafunzi muhakikishe mnafanya vizuri katika masomo yenu, tutaleta Walimu ili watoto wapate elimu bora huku akisisitiza utunzaji wa majengo hayo ili yadumu muda mrefu.

 

Suala la usimamizi wa miradi ya maendeleo amelisisitiza tena wakati akikagua na kuzindua kituo cha afya cha Maili Tano katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.

 

“Hongereni kwa kazi nzuri, kikubwa niwasisitize usimamizi katika miradi hii kama nilivyosema hapo awali, ili thamani ya fedha ionekane,” ameongeza.

 

Mhe. Ridhiwani amehitimisha ziara yake kwa siku ya leo kwa kuzungumza na Wananchi Manispaa ya Tabora ambapo alipata fursa pia ya kusikiliza   changamoto zao kwa lengo la kuzifanyia kazi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge baada ya kuweka jiwe la msingi katika kituo cha afya cha Igigwe wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.


Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya kuweka jiwe la Msingi katika kituo cha afya cha Igigwe wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akijadili jambo na Watendaji wa Mkoa wa Tabora baada ya kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge mkoani Tabora. 


Mwonekano wa Jengo la wagonjwa wa nje (OPD) lililopo katika kituo cha afya cha Maili Tano, katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akielekea kukagua jengo la Kitengo cha Tiba na Mionzi wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, mkoani Tabora. Wengine ni Viongozi, Watendaji, Madaktari na Wananchi. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akishauri jambo wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na Katibu Tawala Wilaya ya Tabora, Bi. Asha Churu wakati Waziri huyo ali[powasili katika Halmashauri ya Wilaya Tabora kukagua na kuzindua majengo ya Shule ya Msingi Kigamboni wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Tabora.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akipata maelezo kuhusu maabara ya kituo cha afya cha Igigwa wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.


Sehemu ya Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kigamboni wakimsikilza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akipiga makofi mara baada ya kuzindua kituo cha afya cha Maili Tano kilichopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. Wengine ni Viongozi na Watendaji wa mkoa huo.


Mwonekano wa jengo la Kitengo cha Tiba na Mionzi lililopo katika kituo cha afya cha Maili Tano, katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.

 


Mwonekano wa jengo la kituo cha afya cha Igigwa kilichopo katika  Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge mkoani Tabora.

 

 


Mwonekano wa jengo la Shule ya Msingi Kigamboni lililopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tabora