Tuesday, April 21, 2026

WATUMISHI WA UMMA WASISITIZWA KUSHUGHULIKIA MREJESHO WA WANANCHI KWA HAKI NA KWA WAKATI

 Na. Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 21 Aprili, 2026

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli amewasisitiza Watumishi wa Umma kushughulikia kwa haki na kwa wakati mrejesho unaowasilishwa na wananchi kupitia Mfumo wa (e- Mrejesho) ili kujenga imani na heshima ya Serikali kwa umma.

Bi. Shuli ameyasema hayo leo Aprili 21, 2026 wakati akimuwakilisha Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi katika ufunguzi wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini yake.

“Ili kufikia utumishi wa umma unaowajibika na uliotukuka, ni vizuri tukashughulikia mrejesho wa wananchi kwa haki na uharaka zaidi.” Bi Shuli alisema.

Amesema, Watumishi wa Umma wanapaswa kuwa na mabadiliko katika fikra, mitazamo, mifumo na tabia walizonazo ili kuwa na Utumishi wa Umma wenye matokeo chanya na thamani halisi kwa mwananchi.

Bi Shuli ameongeza kuwa uzingatiaji wa maadili katika utumishi wa umma si kuzifuata tu Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo ya Utumishi wa Umma bali ni pamoja na kuutumia ipasavyo utaalamu unaohusu ushughulikiaji wa mrejesho wa wananchi .

Amesema ni jukumu la kila mshiriki kuonesha ushirikiano na kuzingatia utu hususani wanapotoa huduma kwa wateja pamoja na kuwa waaminifu hasa katika utunzaji siri kwa kuwa kazi watakazofanya zitahitaji kuwa na matumizi sahihi ya taarifa.

Aidha, amewapongeza washiriki wote kwa kuhudhuria mafunzo hayo na kuwataka wajifunze kwa bidii ili wawe wataalamu watakaowajibika kikamilifu

Kwa upande wake mwenyekiti wa kikao hicho ambaye ni Afisa TEHAMA kutoka Watumishi Housing Investiments (WHI) Bw. Albano Lukiano   amemshukuru Bi. Shuli kwa kuwafungulia mafunzo hayo na kuahidi kuwa yale yote watakayofundishwa watayazingatia na kuyafanyia kazi ili kutoa huduma bora kwa manufaa ya umma.



Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister (kushoto) akiteta jambo na Mwenyekiti wa mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho ambaye pia ni Afisa TEHAMA kutoka Watumishi Housing Investiments (WHI) Bw. Albano Lukiano (kulia) kabla ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo hayo jijini Dodoma.  


Mkurugenzi Msaidizi wa Maadili, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Janet Mishinga, akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha mgeni Rasmi kufungua mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi mara baada ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma. 

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli (kushoto) akifurahia jambo mara baada ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo ya kutumia Mfumo wa e-Mrejesho yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Maadili wa Ofisi hiyo Bi. Janet Mishinga


Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi mara baada ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma

Afisa tawala kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Semeni Muyabhaga akiwasilisha mada ya wakati wa mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho yaliyofanyika Aprili 21, 2026 katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma. 


Mwenyekiti wa kikao cha mafunzo ya kutumia Mfumo wa e-Mrejesho Bw. Albano Lukiano akitoa neno la shukrani kwa Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli mara baada ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma. 


Washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi wakifuatilia hotuba ya mgeni Rasmi wakati alipokuwa akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika leo Aprili 21, 2026 jijini Dodoma.

Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi Kutoka Idara ya Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Hassan Kilenza akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa mjadala wa hoja mbalimbali kuhusu matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho jijini Dodoma.

Washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi wakifuatilia hotuba ya mgeni Rasmi wakati alipokuwa akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika leo Aprili 21, 2026 jijini Dodoma.

Washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi wakifuatilia hotuba ya mgeni Rasmi wakati alipokuwa akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika leo Aprili 21, 2026 jijini Dodoma.

Washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi wakifuatilia hotuba ya mgeni Rasmi wakati alipokuwa akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika leo Aprili 21, 2026 jijini Dodoma.

Afisa Tawala kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Stella Teri akiwasilisha mada kuhusu uzingatiaji wa Kanuni za Maadili ya Utendeji kwa watumishi wa Umma wakati wa mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma

Afisa rasilimali watu mwaandamizi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Saada Ibrahim akiwasilisha mada ya    wakati wa mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho yaliyofanyika  Aprili 21, 2026 katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma. 


Afisa rasilimali watu mwandamizi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Nasra Iduri akiwasilisha mada ya wakati wa mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho yaliyofanyika Aprili 21, 2026 katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma

 

Monday, April 20, 2026

WATUMISHI WA UMMA WAKUMBUSHWA KUTUNZA KUMBUKUMBU ZA KAZI

 Na. Mwandishi wetu-Dodoma

Tarehe 20 Aprili, 2026.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi amewakumbusha watumishi wa Ofisi yake kuweka na kutunza kumbukumbu za majukumu wanayoyafanya kila siku ili kusaidia vizazi vijavyo kufanya marejeo pale inapotakiwa kwa lengo la kuimarisha uendelevu wa taarifa katika utoaji wa huduma.

Bw. Daudi ameyasema hayo Aprili 20, 2026 wakati akihitimisha mafunzo ya uelewa kwa watumishi wa Ofisi yake kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga yaliyotolewa katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.

Aliongeza kuwa, watumishi wa umma hawanabudi kuzingatia mafunzo ya kimkakati wanayopewa ili kuhakikisha yanawajengea uwezo stahiki wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

‘’Majukumu ya Serikali yanaishi, lakini watumishi wa Umma huondoka kutoka kituo kimoja kwenda kingine, hivyo nyaraka zote zinapaswa kuhifadhiwa ipasavyo kwa kuzingatia usalama na utaratibu unaofaa ili watumishi wanaobaki na watakaokuja waweze kurejerea’’ Bw. Daudi alisema.

Aidha Bw. Daudi amewataka viongozi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa Ofisi yake kufuatilia na kujiridhisha iwapo mafunzo yanayotolewa kila jumatatu ya wiki yanaongeza tija na ufanisi katika utendaji kazi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma na Mifumo ya TEHAMA Serikalini kutoka Ofisi ya Rais, UTUMISHI Bw. Tiba Manoni amesema, Taasisi yoyote ni lazima ihakikishe inaweka mipango endelevu ya kushughulikia majanga.

Kadhalika Mkurugenzi huyo alibainisha kuwa majanga ya asili, ukosefu wa fedha, hitilafu za mifumo ya teknolojia na magonjwa ya mlipuko ni sehemu ya majanga yanayoweza kutokea na kupelekea kusitishwa kwa shughuli za utekelezaji wa majukumu na utoaji wa huduma kwa umma.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Xavier Daudi akizungumza na watumishi wa Ofisi yake kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga wakati akihitimisha mafunzo ya kuwajengea watumishi hao uelewa yaliyotolewa katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.


Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga iliyotolewa katika mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi hao katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma


Baadhi ya Wakurugenzi wasaidizi na Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao yaliyofanyika katika eneo la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma
.

Baadhi ya Wakurugenzi wasaidizi na Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao yaliyofanyika katika eneo la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.

Baadhi ya Viongozi na Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao yaliyofanyika katika eneo la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.

Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma na Mifumo ya TEHAMA Serikalini kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Tiba Manoni akitoa elimu kwa watumishi wa Ofisi hiyo kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga katika mafunzo yaliyofanyika eneo maalum la Ofisi hiyo Aprili 20, 2026 jijini Dodoma.


Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga iliyotolewa katika mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi hao katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma


Baadhi ya Viongozi na Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao yaliyofanyika katika eneo la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.




Baadhi ya Viongozi na Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao yaliyofanyika katika eneo la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.


Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma na Mifumo ya TEHAMA Serikalini kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Tiba Manoni akitoa elimu kwa watumishi wa Ofisi hiyo kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga katika mafunzo yaliyofanyika eneo maalum la Ofisi hiyo Aprili 20, 2026 jijini Dodoma.

Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga iliyotolewa katika mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi hao katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma

Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga iliyotolewa katika mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi hao katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma

Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga iliyotolewa katika mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi hao katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma


Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga iliyotolewa katika mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi hao katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma



Friday, April 17, 2026

WAZIRI KIKWETE AWASILISHA BAJETI YA OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwasilisha Bajeti ya ofisi hiyo kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 leo April 17, 2026 jijini Dodoma.


Viongozi, Watendaji na Wakuu wa Taasisi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakifuatilia Bajeti ya ofisi hiyo iliyokuwa ikiwasilishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 leo April 17, 2026 jijini Dodoma.


Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia Bajeti ya ofisi hiyo iliyokuwa ikiwasilishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 leo April 17, 2026 jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akiteta jambo na Naibu Waziri wa Ofisi yake Mhe. Regina Qwaray kabla ya Waziri huyo kuwasilisha Bajeti ya ofisi hiyo kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwasilisha Bajeti ya ofisi hiyo kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 leo April 17, 2026 jijini Dodoma.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akifuatilia Bajeti ya Ofisi hiyo wakati Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akiwasilisha Bajeti ya ofisi hiyo kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 leo April 17, 2026 jijini Dodoma.

Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Watendaji wa Taasisi wa ofisi hiyo wakifuatilia Bajeti iliyokuwa ikiwasilishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 leo April 17, 2026 jijini Dodoma.


Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Watendaji wa Taasisi wa ofisi hiyo wakifuatilia Bajeti iliyokuwa ikiwasilishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 leo April 17, 2026 jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akifuatilia hoja mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na Waheshimiwa Wabunge mara baada ya Waziri huyo kuwasilisha Bajeti ya ofisi hiyo kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 leo April 17, 2026 jijini Dodoma. Kulia ni Naibu Waziri wa Ofisi hiyo, Mhe. Regina Qwaray.


Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakifuatilia Bajeti iliyokuwa ikiwasilishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 leo April 17, 2026 jijini Dodoma.

Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia Bajeti ya ofisi hiyo iliyokuwa ikiwasilishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 leo April 17, 2026 jijini Dodoma.


Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia Bajeti ya ofisi hiyo iliyokuwa ikiwasilishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 leo April 17, 2026 jijini Dodoma.