Tuesday, June 23, 2026

TIMU YA OFISI YA RAIS–UTUMISHI YAKAGUA MIRADI YA UJENZI WA NYUMBA ZA WATUMISHI DODOMA


Na Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 24 Juni, 2026

Timu ya wataalamu kutoka Ofisi ya Rais–UTUMISHI kwa kushirikiana na Watumishi Housing Investment imefanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya ujenzi wa nyumba za watumishi awamu ya pili katika Wilaya ya Dodoma, ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa kuzingatia ubora, thamani ya fedha na ratiba iliyopangwa.

Ziara hiyo imeongozwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, Bw. Patrick Allute, ambaye amesema Serikali imeendelea kuimarisha mazingira ya kazi na makazi ya watumishi wa umma ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Bw. Allute amesisitiza umuhimu wa usimamizi madhubuti wa miradi, matumizi sahihi ya rasilimali za umma na ukamilishaji wa kazi kwa wakati huku viwango vya ubora vikizingatiwa. Aidha, ametoa maelekezo kwa wasimamizi wa miradi na wakandarasi kushughulikia kwa haraka changamoto zilizobainika ili kuhakikisha malengo ya miradi hiyo yanafikiwa kama ilivyopangwa.

Ziara hiyo imekuwa sehemu ya juhudi za Serikali za kuimarisha ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo ili kuhakikisha uwekezaji unaofanywa unaleta matokeo yaliyokusudiwa kwa manufaa ya watumishi wa umma na wananchi kwa ujumla.

Katika ukaguzi huo, timu imetembelea miradi ya ujenzi wa nyumba za watumishi katika Kituo cha Afya Hombolo, Shule ya Sekondari Mtemichiloloma, Kituo cha Afya Mkonze na Shule ya Sekondari Bihawana, ambapo imejionea maendeleo ya utekelezaji wa miradi hiyo na imefanya majadiliano na wasimamizi pamoja na wakandarasi kuhusu hatua zilizofikiwa na changamoto zinazojitokeza.


Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (aliyesimama katikati) akiwa katika picha ya pamoja na timu nzima ya wataalamu wa ukaguzi wa miradi  mara baada ya  timu hiyo kukagua mradi wa ujenzi wa
 nyumba ya Watumishi  katika kituo cha Afya Mkonze , mtaa wa hospitali Mkoani Dodoma

Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma lililopo katika Kijiji cha hospitali, kata ya Mkonze,Wilaya ya Dodoma na Mkoa wa Dodoma.



Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (aliyenyoosha mkono) akitoa maelekezo kwa wasimamizi wa mradi wa shule ya sekondari Mtemichiloloma Hombolo
, Mkonze mara baada ya Mkurugenzi huyo na timu ta Wataalamu aliofuatana nao kuwasili katika mradi huo kwa ukaguzi Juni 25, 2026 jijini Dodoma

Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma lililopo mtaa wa Hombolo senta, kata ya Hombolo,Wilaya ya Dodoma Mkoani Dodoma


Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (wa tatu kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na timu ya Wataalamu aliofuatana nao mbele ya jengo la Mradi wa shule ya sekondari Bihawana uliopo Mkonze jijini Dodoma mara baada ya kukagua maendeleo ya Mradi huo Juni 24, 2026


Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (wa tatu kutoka kulia) akizungumza na Mwalimu ambaye ni Mtumishi katika shule ya sekondari Bihawana, Mkonze mara baada ya Mkurugenzi huyo na timu ta Wataalamu aliofuatana nao kuwasili katika mradi huo kwa ukaguzi Juni 25, 2026 jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Patrick Allute (aliyenyoosha mkono) akitaka ufafanuzi wa jambo kuhusu maendeleo ya ujenzi wa mradi wa Kituo cha Afya kilichopo mtaa wa Hospitali kata ya Mkonze Mkoani Dodoma  Juni 24,2025  


 Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma wa shule ya sekondari Bihawana lililopo  kata ya Mkonze, Wilaya ya Dodoma Mkoani Dodoma

Monday, June 22, 2026

PROF. SHEMDOE AZITAKA TAASISI ZA UMMA KUIMARISHA MATUMIZI YA MIFUMO YA KIDIJITI

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Tarehe 23 Juni, 2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe amezitaka taasisi zote za umma nchini kuimarisha matumizi ya mifumo ya kidijiti ili kuboresha utoaji wa huduma kwa Wananchi, kuongeza uwajibikaji na kuimarisha ufanisi katika utumishi wa umma.

Prof. Shemdoe ametoa kauli hiyo Juni 23, 2026 jijini Dodoma wakati akimwakilisha Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka, katika kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park.

Alisema, matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) yamekuwa nguzo muhimu katika kuimarisha utendaji wa Serikali kwa kurahisisha upatikanaji wa huduma, kuongeza uwazi na kupunguza gharama za utoaji wa huduma kwa wananchi.

Prof. Shemdoe alibainisha kuwa maadhimisho ya mwaka huu yamehusisha Taasisi 226 za umma zilizotoa huduma mbalimbali kwa wananchi, zikiwemo huduma za hati za viwanja, vyeti vya kuzaliwa, vitambulisho vya Taifa, huduma za afya za kibingwa pamoja na huduma mbalimbali za kiutumishi.

“Utaratibu huu wa kuwaletea Wananchi huduma karibu nao ni mzuri na unapaswa kuendelezwa kwa kuwa unarahisisha upatikanaji wa huduma, kuimarisha mawasiliano kati ya Serikali na Wananchi na kuongeza imani ya wananchi kwa Serikali yao,” alisema Prof. Shemdoe.

Katika hafla hiyo, Prof. Shemdoe alizindua mifumo ya GSD na NGAO inayolenga kuboresha utoaji wa huduma za Serikali na kuimarisha usalama wa mifumo ya kidijiti.

Alieleza kuwa mfumo wa GSD utawawezesha wananchi kupata huduma mbalimbali za Serikali kupitia dirisha moja kwa urahisi na kwa wakati, huku mfumo wa NGAO ukiimarisha usalama wa taarifa za Serikali kwa kutumia teknolojia ya uthibitishaji wa vipengele vingi (Multi-Factor Authentication).

Aidha, aliielekeza Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) kuendelea kusimamia uunganishaji wa mifumo ya Serikali ili kuhakikisha Taasisi za Umma zinabadilishana taarifa kwa ufanisi, kupunguza urudufu wa taarifa na kuongeza tija katika utoaji wa huduma.

Vilevile, Prof. Shemdoe aliagiza kufanyika kwa tathmini ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita ili kubaini mafanikio yaliyopatikana, changamoto zilizojitokeza na kuweka mikakati madhubuti ya kuboresha maadhimisho yajayo.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, alisema maadhimisho hayo yamelenga kuimarisha uwajibikaji, uwazi na ubora wa huduma kwa wananchi kupitia matumizi ya teknolojia za kisasa zinazowezesha utoaji wa huduma kwa haraka na kwa ufanisi zaidi.

Aliongeza kuwa maadhimisho hayo yameipa Serikali fursa ya kuonesha mafanikio ya uwekezaji uliofanyika katika sekta ya umma, hususan katika matumizi ya TEHAMA ambayo yamechangia kuboresha huduma na kuongeza kuridhika kwa wananchi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe akizungumza na Wananchi pamoja na Watumishi kwenye hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Juni 23, 2026 kabla ya Waziri huyo kufunga maadhimisho hayo katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma

Watumishi na Wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe (hayupo pichani) wakati hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Juni 23, 2026 iliyofanyika juni 23, 2026 katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma

Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipokuwa akizungumza nao katika hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Juni 23, 2026 Jijini Dodoma

Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipokuwa akizungumza nao katika hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Juni 23, 2026 Jijini Dodoma


Watumishi na Wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe (hayupo pichani) wakati hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Juni 23, 2026 iliyofanyika juni 23, 2026 katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma

Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipokuwa akizungumza nao katika hafla ya kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Juni 23, 2026 Jijini Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe (kushoto) akiteta jambo na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – UTUMISH, Bw. Juma Mkomi, wakati wahafla ya kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Juni 23, 2026 yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma

Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – UTUMISH, Bw. Juma Mkomi, akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe kufunga Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Juni 23, 2026 iliyofanyika juni 23, 2026 katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma




Sunday, June 21, 2026

WANANCHI WAHIMIZWA KUJITOKEZA KWA WINGI KILELE CHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2026

Wananchi wa Mkoa wa Dodoma na maeneo ya jirani wamehimizwa kujitokeza kwa wingi kesho, Juni 23, 2026, kushiriki kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.

Aidha, ushiriki wao utasaidia kupata huduma mbalimbali zinazotolewa na Serikali pamoja na kujionea mafanikio yaliyofikiwa katika sekta ya utumishi wa umma.

Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray, baada ya kutembelea mabanda ya maonesho ya Wizara na Taasisi za Umaa zinazoshiriki maadhimisho hayo.

 Mhe. Regina amesema maadhimisho hayo yamekuwa fursa muhimu kwa wananchi kupata huduma za papo kwa papo, ushauri na elimu kuhusu majukumu na huduma zinazotolewa na Serikali katika sekta mbalimbali.

Aidha, amezipongeza Wizara na Taasisi za Umma kwa juhudi kubwa wanazoendelea kufanya katika kutoa huduma na elimu kwa wananchi kupitia mabanda ya maonesho, hali ambayo imeongeza uelewa wa wananchi kuhusu huduma za Serikali na namna ya kuzifikia kwa urahisi.

Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2026 kitafanyika kesho, Juni 23, 2026.

Afisa kutoka Ofisi ya Rai, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Edwin Bilikundi, (wa pili kutoka kushoto) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri, wa Ofisi hiyo, Mhe. Regina Qwaray (wa pili kutoka kulia) kuhusu huduma zinazotolewa na Ofisi hiyo katika maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma leo Juni 22, 2026 katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma


 


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na Watumishi wa Wizara ya Ardhi mara baada ya kuwasili katika banda lao la maonesho kuona huduma zinazoendelea kutolewa kwa Wananchi kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma leo Juni 22, 2026 katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) mara baada ya kuwasili katika banda hilo la maonesho kuona huduma zinazoendelea kutolewa kwa Wananchi kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma leo Juni 22, 2026 katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (wa pili kutoka kulia ) akifurahia jambo wakati alipokuwa akitembelea mabanda ya maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma inayofanyika katika viwanja vya chinangali Park Jijini Dodoma



Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na Watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii mara baada ya kuwasili katika banda lao la maonesho kuona huduma zinazoendelea kutolewa kwa Wananchi kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma leo Juni 22, 2026 katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na Soko la Bidhaa Tanzania (TMX) mara baada ya kuwasili katika banda lao la maonesho kuona huduma zinazoendelea kutolewa kwa Wananchi kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma leo Juni 22, 2026 katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray 

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (kulia) akikabidhiwa zawadi na Mkurugenzi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Frimin M. Msiangi, kama ishara ya shukrani kwa Taasisi hiyo kwa kutembelea banda lao la  maonesho katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Jijini Dodoma



Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akisaini kitabu cha wageni, mara baada ya kufika katika banda la maonesho la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wakati wa 
maonesho katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Jijini Dodoma


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akipokea maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazoendelea kutolewa na  Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) mara baada ya Naibu Waziri huyo kuwasili katika banda la maonesho la Taasisi hiyo Juni 22, 2026 
katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma
 

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na Watumishi wa Bunge mara baada ya kuwasili katika banda lao la Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Jijini Ddoma