Monday, July 13, 2026

KATIBU MKUU MKOMI AWATAKA WATUMISHI KUONGEZA KASI YA UTENDAJI KUFIKIA MALENGO YA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050

Na. Antonia Mbwambo – Dodoma

13 Julai, 2026

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, amewataka Watumishi wa Umma kuongeza kasi ya utendaji na kuzingatia weledi ili kuchangia kikamilifu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Katibu Mkuu Mkomi ametoa wito huo leo Julai 13, 2026, wakati akihitimisha mafunzo kuhusu umuhimu wa afya ya akili kwa Watumishi wa Umma yaliyofanyika katika eneo maalumu la Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Mtumba, jijini Dodoma kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi hao.

Bw. Mkomi amesema mafanikio ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 yanategemea uwepo wa Watumishi wa Umma wenye afya bora ya akili, maadili ya kazi, ubunifu na uwajibikaji, huku akisisitiza kuwa afya ya akili ni msingi wa utendaji wenye tija na utoaji wa huduma bora Serikalini.

"Afya ya akili si suala la mtu mmoja mmoja, bali ni msingi wa kuongeza tija katika Utumishi wa Umma. Mtumishi mwenye afya bora ya akili anakuwa na uwezo mkubwa wa kutoa huduma bora, kushirikiana na wenzake na kuleta matokeo chanya kwa Taasisi na Taifa kwa ujumla," amesema Bw. Mkomi.

Aidha, Bw. Mkomi amewaelekeza Wachumi wa Ofisi hiyo kufanya tafakuri za kitaaluma na kuibua mawazo bunifu yatakayochangia Serikali kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Kwa upande wake, Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma Elias, ambaye alikuwa Mwezeshaji wa mafunzo hayo, amesema afya ya akili ni nguzo muhimu ya ustawi wa mtumishi na ina mchango mkubwa katika kuongeza tija pamoja na kuboresha mazingira ya kazi.

Ameeleza kuwa changamoto za afya ya akili kwa watumishi wa Umma mara nyingi husababishwa na mpangilio duni wa kazi, mzigo mkubwa wa majukumu unaozidi uwezo wao, kazi za kujirudia rudia na mazingira magumu ya kazi. Amewahimiza watumishi kuzingatia mtindo bora wa maisha kwa kufanya mazoezi ya mara kwa mara, kula lishe bora, kupata mapumziko ya kutosha na kutafuta ushauri wa Wataalamu wanapokabiliwa na changamoto za afya ya akili.

Aidha, Dkt. Elias amewataka viongozi kuendelea kuzingatia usawa kwa watumishi wanaowasimamia, kupinga unyanyapaa dhidi ya wenye changamoto za afya ya akili na kutambua mapema dalili za changamoto hizo ili kuwawezesha watumishi kupata huduma stahiki kwa wakati.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akifurahia jambo wakati alipokuwa akihitimisha mafunzo ya uelewa kwa Watumishi wa Ofisi hiyo Julai 13, 2026 Mtumba Jijini Dodoma

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (wa kwanza kutoka kushoto), akifuatilia mada ya mafunzo kuhusu umuhimu wa afya ya akili kwa Watumishi wa Umma yaliyokuwa yakitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma Elias (hayupo pichani) leo Julai 13, 2026  katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Ofisi hiyo Bw. Musa Magufuli.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, akizungumza na Watumishi wa Ofisi yake wakati alipokuwa akihitimisha Mafunzo ya uelewa kuhusu Umuhimu wa Afya ya Akili kwa Watumishi wa Umma yaliyofanyika Julai 13, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo, Mtumba jijini Dodoma 

Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Idara na Vitengo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma.

Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma

Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma Elias akitoa mada ya mafunzo kuhusu Umuhimu wa Afya ya Akili kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora yaliyofanyika Julai 13, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Jijini Dodoma

Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Idara na Vitengo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma.

Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma Elias akitoa mada ya mafunzo kuhusu Umuhimu wa Afya ya Akili kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora yaliyofanyika Julai 13, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Jijini Dodoma

Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Idara na Vitengo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma.

Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.


Baadhi ya Wakurugenzi na Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma

Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.


Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.


Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.


Friday, July 10, 2026

AJIRA MPYA NI MOJAWAPO YA VIPAUMBELE VYA SERIKALI KUWEZESHA WANANCHI KUPATA HUDUMA BORA

 Na. Veronica Mwafisi-Uyui

Tarehe 10 Julai, 2026. 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anatambua changamoto ya ajira katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu na ndio maana kati ya vipaumbele vya Serikali vilivyopo, ajira ni mojawapo.

 

Mhe. Kikwete amesema hayo leo tarehe 10 Julai, 2026 wakati akizungumza na Viongozi, Watumishi wa Umma na Wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Uyui mkoani Tabora kabla ya kukagua na kuzindua Shule ya Msingi Ilolangula Mlimani katika Wilaya hiyo.

 

“Serikali inafahamu changamoto ya ajira hususan katika sekta ya Elimu na Afya na ndio maana Rais wetu mpendwa amekuwa akitoa vibali vya ajira, huku akifafanua kuwa mwaka huu wa fedha 2026/27 kibali cha ajira kwa watumishi 45,000 kimetolewa ambapo Sekta ya Elimu itafaidika pia,” amesisitiza Mhe. Kikwete.

 

Ameongeza kuwa haya yote yanafanyika kwasababu Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa akiwajali wananchi wake hasa katika kupata huduma bora huku akiwasisitiza wanafunzi wa shule hiyo kusoma kwa bidii kwani elimu ni muhimu kwa maendeleo ya mtu binafsi na taifa kwa ujumla.

 

“Suala la elimu linasisitizwa sana hata katika vitabu vyote vitakatifu vya dini, hivyo wanafunzi hamna budi kusoma kwa bidii ili kuwa na ufahamu wa mambo mengi kwa maendeleo ya taifa letu,” ameongeza.

 

Katika hatua nyingine Mhe. Kikwete amuelekeza Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kutenga bajeti kwa ajili ya kujenga Ofisi ya TAKUKURU wilayani Uyui.

 

Amesema Ofisi ya TAKUKURU ina umuhimu wake katika kuzuia na kupambana na rushwa katika miradi mbalimbali inayotekelezwa katika Wilaya hiyo.

 

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Uyui, Mhe. Mohamed Mtulyakwaku aliwasilisha changamoto kwa Mhe. Waziri Kikwete kuwa Wilaya yake inakabiliwa na uhaba wa Watumishi hasa katika Sekta ya Elimu na Afya, hivyo aliiomba Serikali kuwapatia watumishi hao ili waweze kuwadumia wananchi kikamilifu.

 

“Tunatambua kuwa Serikali imekuwa ikituletea watumishi wapya lakini bado tuna uhitaji, hivyo tunaomba mtufikirie katika hili,” aliongeza Mkuu wa Wilaya huyo.

 

Aidha, alizungumzia suala la kutokuwepo kwa Ofisi ya TAKUKURU katika Wilaya hiyo kwani wamekuwa wakisafiri mpaka Tabora mjini kufuata huduma hiyo pale wanapoihitaji.

 

Waziri Ridhiwani Kikwete anahitimisha leo ziara yake ya kikazi ya siku tatu mkoani Tabora ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Viongozi, Watumishi wa Umma na Wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Uyui kabla ya kukagua na kuzindua Shule ya Msingi lolangulu Mlimani katika Wilaya hiyo mkoani Tabora.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akiteta jambo na Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Tabora ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Mhe. Upendo Wella wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora



 

Viongozi, Watumishi wa Umma na Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya kukagua na kuzindua Shule ya Msingi lolangula Mlimani wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora


 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyevaa miwani) akielekea kukagua na kuzindua Shule ya Msingi lolangulu Mlimani wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora

 



 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wapili kutoka kushoto) akiweka jiwe la msingi mara baada ya kukagua na kuzindua Shule ya Msingi lolangula Mlimani wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora


Viongozi, Watumishi wa Umma na Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya kukagua na kuzindua Shule ya Msingi lolangulu Mlimani wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.

 



Sehemu ya Wanafunzi wa Shule ya Msingi lolangula Mlimani wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete alipokuwa akizungumza baada ya kukagua na kuzindua Shule ya Msingi lolangulu Mlimani wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.


Watumishi wa Umma na Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya kukagua na kuzindua Shule ya Msingi lolangulu Mlimani wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akiteta jambo na  Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui Mhe. Shabani Katalambula wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.




 

MHE. RIDHIWANI ASISITIZA WAAJIRI KUTILIA MKAZO SUALA LA MSAWAZO KWA WATUMISHI ILI KUPUNGUZA CHANGAMOTO YA UHABA WA WATUMISHI

Na. Veronica Mwafisi-Urambo

Tarehe 10 Julai, 2026

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amewakumbusha Waajiri katika Taasisi za Umma kutilia mkazo suala la msawazo kwa Watumishi ili kupunguza changamoto ya uhaba wa watumishi katika maeneo mbalimbali kwenye sekta hiyo ya umma kwa lengo la kuwatumikia wananchi kwa ufasaha.

 

Mhe. Kikwete amesema hayo leo tarehe 10 Julai, 2026 wakati akizungumza na Viongozi, Watumishi wa Umma na Wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Urambo mkoani Tabora baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa kituo cha Polisi Usoke.

 

Amesema kabla ya Waajiri kulalamika changamoto ya uhaba wa watumishi, ni vema wakakaa na kufanya msawazo ili kujiridhisha kama kweli wana changamoto hiyo katika maeneo yao kabla ya kuomba kupatiwa watumishi wapya.

 

“Utakuta kuna taasisi watumishi wa kada fulani wamerundikana katika kituo kimoja cha kazi huku kituo cha kazi cha jirani kina uhaba wa watumishi wa kada hiyo, au Waajiri kaeni, fanyeni msawazo, kabla ya kulalamikia changamoto hiyo ya uhaba wa watumishi,” ameongeza Mhe. Kikwete.

 

Ameongeza kuwa kuna taasisi unakuta kuna watumishi wa kada fulani ambao sio hawahitajiki sana katika taasisi fulani kutokana na majukumu yake lakini wapo huku taasisi yenye uhitaji wa watumishi wa kada hiyo hakuna.

 

Katika hatua nyingine Mhe. Kikwete amewataka wananchi wa Kata ya Usoke kukitunza kituo cha Polisi kinachojengwa katika kata hiyo ili kiwasaidie katika kupambana na uhalifu.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Viongozi, Watumishi wa Umma na Wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Urambo baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa kituo cha Polisi Usoke wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wakwanza kulia) akiwa katika mkutano mara baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi katika kituo cha Polisi Usoke, Halmashauri ya Wilaya ya Urambo wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akikata utepe kuzindua ujenzi wa kituo cha Polisi Usoke katika Halmashauri ya Wilaya ya Urambo baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyevaa miwani) akipiga makofi mara baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi katika kituo cha Polisi Usoke, Halmashauri ya Wilaya ya Urambo wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisikiliza taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa kituo cha Polisi Usoke katika Halmashauri ya Wilaya ya Urambo kabla ya kukagua na kuweka jiwe la msingi wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.


Viongozi, Watumishi wa Umma na Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi katika kituo cha Polisi Usoke, Halmashauri ya Wilaya ya Urambo wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tabora.