Thursday, April 30, 2026
Tuesday, April 28, 2026
KIKAO KAZI CHA MAAFISA BAJETI KUTOKA OFISI YA RAIS, -UTUMISHI KWA KILICHOLENGA KUKAMILISHA MPANGO MKAKATI WA OFISI HIYO
Mkurugenzi
wa Idara ya Mipango, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Cosmas
Ngangaji (watatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya
pamoja na washiriki wa kikao kazi cha Maafisa Bajeti kutoka Ofisi hiyo kwa
ajili ya hatua za kukamilisha Mpango Mkakati wa Ofisi hiyo kilichofanyika
kuanzia tarehe 28 Aprili-2 May, 2026 katika Ukumbi wa Ofisi ya Idara ya
kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma
Washiriki wa kikao kazi cha
Maafisa Bajeti kutoka Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, kilicholenga kukamilisha Mpango Mkakati
wa Ofisi hiyo, wakiwa wanafuatilia Mafunzo katika Ukumbi wa Ofisi ya Idara ya
kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma
Washiriki wa kikao kazi cha
Maafisa Bajeti kutoka Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, kilicholenga kukamilisha Mpango Mkakati
wa Ofisi hiyo, wakiwa wanafuatilia Mafunzo katika Ukumbi wa Ofisi ya Idara ya
kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma
Monday, April 27, 2026
WATUMISHI WALIOZALIWA MWEZI APRILI WAPONGEZWA
Na. Antonia Mbwambo-Dodoma
Tarehe
27 Aprili, 2026
Mkurugenzi Msaidizi Anuai za Jamii na Mratibu wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza wa Ofisi hiyo Bi. Mwanaamani Mtoo niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI amewapongeza na kuwatakia kila la kheri watumishi wawote waliozaliwa mwezi Aprili ambapo kwa kumbukizi hiyo wamepata nafasi ya kukata keki kama ishara ya kuendeleza umoja na mshikamano ili kuimarisha utendaji kazi.
Matukio mbalilmbali ya picha za watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, waliokuwa wanaadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa ya mwezi Aprili, yaliyofanyika katika Ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma