Tuesday, April 28, 2026

KIKAO KAZI CHA MAAFISA BAJETI KUTOKA OFISI YA RAIS, -UTUMISHI KWA KILICHOLENGA KUKAMILISHA MPANGO MKAKATI WA OFISI HIYO


Mkurugenzi wa Idara ya Mipango, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Cosmas Ngangaji (watatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa kikao kazi cha Maafisa Bajeti kutoka Ofisi hiyo kwa ajili ya hatua za kukamilisha Mpango Mkakati wa Ofisi hiyo kilichofanyika kuanzia tarehe 28 Aprili-2 May, 2026 katika Ukumbi wa Ofisi ya Idara ya kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma 

Washiriki wa kikao kazi cha Maafisa Bajeti kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, kilicholenga kukamilisha Mpango Mkakati wa Ofisi hiyo, wakiwa wanafuatilia Mafunzo katika Ukumbi wa Ofisi ya Idara ya kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma 

Washiriki wa kikao kazi cha Maafisa Bajeti kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, kilicholenga kukamilisha Mpango Mkakati wa Ofisi hiyo, wakiwa wanafuatilia Mafunzo katika Ukumbi wa Ofisi ya Idara ya kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma 



Monday, April 27, 2026

WATUMISHI WALIOZALIWA MWEZI APRILI WAPONGEZWA

 Na. Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 27 Aprili, 2026

Mkurugenzi Msaidizi Anuai za Jamii na Mratibu wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza wa Ofisi hiyo Bi. Mwanaamani Mtoo niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI amewapongeza na kuwatakia kila la kheri watumishi wawote waliozaliwa mwezi Aprili ambapo kwa kumbukizi hiyo wamepata nafasi ya kukata keki kama ishara ya kuendeleza umoja na mshikamano ili kuimarisha utendaji kazi.

Matukio mbalilmbali ya picha za watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, waliokuwa wanaadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa ya mwezi Aprili, yaliyofanyika katika Ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma