Na. Veronica Mwafisi-Dodoma
Tarehe
20 Julai, 2026.
Daftari la Huduma za Serikali (GSD) ni Mfumo
wa kidijitali ambao unalenga kuwapatia wananchi, wafanyabiashara na wageni
fursa taarifa na maombi ya huduma za serikali katika Wizara, Idara, Wakala,
Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa hivyo, kurahisisha utoaji
wa huduma kwa umma kwa njia ya kidijiti.
Hayo yameelezwa leo na Kaimu Mkurugenzi
Msaidizi, Sehemu ya Mifumo na Viwango vya Kimenejimenti kutoka Idara ya
Uendelezaji Taasisi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Noah Mkasanga wakati
akiwasilisha mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali kwenye mafunzo ya
kuwajengea uwezo Watumishi wa Ofisi hiyo iliyopo Mtumba Jijini Dodoma.
Bw. Noah amesema kuwa, kupitia mfumo wa GSD wananchi wataweza kupata huduma
zote za Serikali kidijitali kupitia dirisha moja, ikiwa ni pamoja na kuona
huduma zinazotolewa, gharama zake, masharti au vitu vinavyohitajika ili kupata
huduma na namna ya kuzipokea hata wakiwa nyumbani kwa kutumia anwani za makazi
(NAPA).
“Daftari hili linarahisisha utoaji wa huduma mbalimbali
za Serikali kwa umma kupitia dirisha moja kwa kuainisha huduma zote
zinazotolewa na taasisi za umma pamoja na mahitaji yao na kuziweka wazi kwa
wananchi wanapotaka kupata huduma husika kwa njia ya kidijiti”, amesema Bw. Noah.
Akifafanua
kuhusu umuhimu wa Daftari la Huduma za Serikali (GSD) Bw. Noah amesema, litaongeza
ufanisi na uwajibikaji ikiwa ni pamoja na kupunguza gharama kwa wateja na
urahisi wa kutoa huduma kupitia mfumo mmoja.
Kadhalika,
Bw. Noah, amesema kuwa Daftari la Huduma za Serikali (GSD) litasaidia
kupunguza mianya ya rushwa kwa kuwa huduma hiyo inatolewa kwa njia ya
kidijitali.
Kuanzishwa kwa Daftari la Huduma za Serikali (GSD) ni jitihada za Serikali za kutumia teknolojia ya kisasa katika
kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi na kuimarisha usalama wa taarifa za
umma.
Kaimu Mkurugenzi
Msaidizi, Sehemu ya Mifumo na Viwango vya Kimenejimenti kutoka Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Noah Mkasanga akiwasilisha mada kuhusu Daftari la Huduma za
Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika kila Jumatatu kwa
watumishi hao katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi Wasaidizi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Kaimu Mkurugenzi
Msaidizi, Sehemu ya Mifumo na Viwango vya Kimenejimenti kutoka Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Noah Mkasanga akifafanua jambo kuhusu Daftari la Huduma za
Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika kila Jumatatu kwa
watumishi hao katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi Wasaidizi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi, Wakurugenzi Wasaidizi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakisikiliza mada kuhusu Daftari la Huduma za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi
ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakiwa
katika mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji
wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakiwa katika mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.



























