Wednesday, September 16, 2026

KIKAO KAZI

MRADI WA TANZANIA YA KIDIJITALI (DTP) UMELETA MAPINDUZI MAKUBWA YA MAWASILIANO YA KIMTANDAO YALIYORAHISISHA UTOAJI WA HUDUMA KWA UMMA











 

Tuesday, September 15, 2026

NUKUU ZA LEO ZA NAIBU WAZIRI MHE. RGINA QWARAY WAKATI AKIZUNGUMZA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA BUCHOSA






 

NAIBU WAZIRI MHE. QWARAY AWAAGIZA WAAJIRI KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI KWA WAKATI


Na. Antonia Mbwambo na  Lusungu Helela 

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina  Qwaray, amewaagiza waajiri kuhakikisha changamoto na stahiki za watumishi wa umma zinashughulikiwa kwa wakati, hatua inayolenga kuongeza ufanisi na kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Mhe. Qwaray ametoa agizo hilo leo Septemba 15, 2026  wakati akizungumza na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa mkoani Mwanza  kwa lengo la  kusikiliza changamoto za watumishi na kujadili namna ya kuboresha utendaji katika Utumishi wa Umma.

Amesema masuala yanayohusu kupandishwa vyeo, uhamisho, malimbikizo ya mishahara na mafao yanapaswa kushughulikiwa kwa wakati na mamlaka husika, badala ya kuendelea kucheleweshwa.

"Nawaagiza waajiri wote kuhakikisha changamoto na stahiki za watumishi, ikiwemo kupandishwa vyeo, uhamisho, malimbikizo ya mishahara na mafao, zinashughulikiwa kwa wakati,” amesema  Mhe Qwaray.

Aidha, amesisitiza kuwa madai ya watumishi yanapaswa kuhakikiwa ipasavyo na kuwasilishwa yakiwa na nyaraka zote muhimu ili kuwezesha malipo kufanyika kwa wakati.

Katika hatua nyingine, Mhe. Qwaray amezitaka Mamlaka za Ajira na Nidhamu kusimamia haki na wajibu wa watumishi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za Utumishi wa Umma, huku akiwataka kuachana na utendaji wa mazoea.

Amesema mambo yaliyo ndani ya mamlaka za waajiri na Mamlaka za Ajira na Nidhamu yanapaswa kushughulikiwa katika ngazi husika badala ya kuendelea kuwasilishwa Ofisini kwake.

Aidha, Mhe. Qwaray amesisitiza umuhimu wa watumishi kutumia mifumo ya kidijitali iliyobuniwa  na Serikali katika kusimamia utendaji na kupata huduma za kiutumishi.

Mifumo hiyo ni pamoja na e-Watumishi, Watumishi Portal, e-Utendaji (PEPMIS) na e-Mrejesho, ambayo imeimarishwa kwa ajili ya kurahisisha upatikanaji wa huduma, kuongeza uwajibikaji na kutoa fursa kwa wananchi na watumishi kuwasilisha maoni, pongezi, malalamiko na mapendekezo.

Amesema matumizi sahihi ya mifumo hiyo ni sehemu ya jitihada za kujenga Utumishi wa Umma unaozingatia haki, wajibu, uwajibikaji, ufanisi na matumizi ya teknolojia.

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Buchosa, Bw. Benson Mihayo amesema changamoto za watumishi zitaendelea kushughulikiwa kutokana na bajeti iliyopo huku akibainisha kuwa mwitikio wa watumishi katika suala  ujazaji PEPMIS limekuwa na mwitikio mkubwa ukilinganisha na hapo awali  hali inayopelekea malalamiko ya watumishi kupungua wakati wa upandaji wa madaraja. 

Naye Mbunge wa Buchosa, Mhe. Erick Shigongo ametumia fursa hiyo kuwashukuru Watumishi wa Halmashauri ya Buchosa kwa huduma bora wanazoendelea kutoa kwa wananchi wa Halmashauri hiyo.

" Hatua ya maendeleo unayoyaona leo hapa Buchosa ni kutokana na uwepo wa watumishi wazalendo waliojitoa kwa lengo la kuwahudumia wananchi" amesisitiza Mhe. Shigongo 

 

Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiwa na baadhi ya viongozi wakimsikiliza  Katibu Tawala wa wilaya hiyo  Bw. Cuthbert Midala  mara  baada ya  kumaliza   kuzungumza leo na Watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Buchosa iliyopo mkoani Mwanza

 

Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na  watumishi wa Ofisi ya Halmashauri ya Buchosa  Mkoani Mwanza mara  baada ya kuwasili leo mkoani humo kwa lengo la kuzungumza na kusikiliza changamoto zinazowakabili watumishi na kuzitafutia ufumbuzi 

 



3.    Watumishi wa Ofisi ya Halmashauri ya Buchosa iliyopo  Mkoani Mwanza wakiwa kwenye maombi kabla ya  Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray kuanza kuzungumza nao

 


Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akisalimiana na baadhi ya watumishi wa Ofisi ya   Mkoa wa  Mwanza mara  baada ya kuwasili leo mkoani humo kwa lengo la kuzungumza na kusikiliza changamoto zinazowakabili watumishi na kuzitafutia ufumbuzi    
Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na  Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CP Salum Hamduni  mara  baada Naibu Waziri huyo  kuwasili mkoani humo kwa lengo la kuzungumza na kusikiliza changamoto zinazowakabili watumishi na kuzitafutia ufumbuzi.