Friday, August 14, 2026

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YAIPONGEZA TASAF KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO, YASISITIZA KUENDELEZA UWAZI NA UWAJIBIKAJI KATIKA KUFIKIA WALENGWA WALIOKUSUDIWA ILI KUTIMIZA MALENGO YA PSSN III

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 14 Agosti, 2026 

Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imepokea taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III) na kutoa maelekezo ya kuendeleza misingi ya utekelezaji wenye ufanisi, uwazi na uwajibikaji katika kufikia walengwa waliokusudiwa na kutimiza malengo ya PSSN III.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amezungumza hayo leo tarehe 14 Agosti, 2026 Bungeni jijini Dodoma alipokuwa akiongoza kikao cha Kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kilicholenga kupokea taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).

Vilevile, Mhe. Dkt. Ndumbaro ameipongeza TASAF kwa utekelezaji mzuri wa Miradi ya Maendeleo ikiwemo ujenzi kwenye sekta ya elimu na afya.

“Kwa niaba ya Kamati yangu nitoe pongezi nyingi kwa ofisi hii, kwa hakika mnafanya kazi nzuri katika mpango wa kunusuru kaya maskini, lakini pia mnatekeleza vizuri Miradi ya Maendeleo ikiwemo ujenzi  kwenye sekta ya elimu na afya, mnamwakilisha vizuri Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika utekelezaji wa miradi hii’’ Amesema Mhe. Dkt. Ndumbaro

Awali akiwasilisha kwa Kamati hiyo taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III), Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray amesema, PSSN III iliidhinishwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Benki ya Dunia tarehe 10 Aprili 2026, na kwa sasa ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha maandalizi kabla ya kuanza utekelezaji.

Naibu Waziri Qwaray amesema kuwa, katika maandalizi ya utekelezaji wa PSSN III, hatua muhimu zimekamilika ikiwemo kukamilisha usanifu wa Mpango, kuandaa nyaraka mbalimbali za utekelezaji, miongozo ya kiutendaji na kuimarisha mifumo ya TEHAMA inayosimamia shughuli za Mpango.

Aidha ameongeza kuwa, mchakato wa utambuzi wa Mamlaka za Maeneo ya Utekelezaji yatakayoshiriki kwenye utekelezaji wa Mpango unaendelea na unaojumuisha timu ya wataalamu kutoka TASAF, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar (OCGS), pamoja na wataalamu wa mazingira ambapo uchambuzi na uchakataji huo utazingatia viwango vya umaskini katika ngazi ya Halmashauri pamoja na viashiria vya athari za kimazingira, ikiwemo uwezekano wa maeneo kuathiriwa na mabadiliko ya tabianchi na majanga mbalimbali.

Vilevile, Mhe. Qwaray amesema kupitia mpango huo unatarajiwa kuongeza uwezo wa kaya maskini na zilizo katika mazingira hatarishi kukabiliana na changamoto za kiuchumi, kijamii na kimazingira, kuongeza ujuzi na taaluma kwa vijana kutoka kaya maskini na zinazoishi katika mazingira hatarishi zitakazoweza kujiajiri na kuajiriwa, kuwa na masijala ya kitaifa (kanzi data) yenye taarifa muhimu ya kaya maskini na zilizopo katika mazingira hatarishi pamoja na urasimishwaji wa TASAF kama taasisi ya umma ya kutekeleza na kusimamia utoaji wa huduma za msaada ya kijamii itakayohakikisha uendelevu, ufanisi na uratibu wa utoaji wa huduma hizo nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bw. Shedrack Mziray ameishukuru Kamati hiyo kwa maoni na ushauri mbalimbali ambao wameutoa na kuahidi kufanyia kazi ili kuimarisha na kuboresha utendaji kazi wa Taasisi hiyo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akisisitiza jambo wakati wa kikao cha Kamati yake kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kilicholenga kupokea taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (aliyesimama kulia) akiwasilisha kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III). Wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akifurahia jambo wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bw. Shedrack Mziray akisikiliza maoni kutoka kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo Bungeni jijini Dodoma na Watendaji hao kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Nyamizi Mhoja akiwasilisha hoja kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).

Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Sikudhani Chikambo akiwasilisha hoja kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akifafanua hoja Bungeni jijini Dodoma wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (kulia) akiteta jambo na Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (kushoto) wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).

Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (aliyesimama) akifafanua hoja iliyowasilishwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bw. Shedrack Mziray (kulia) akiandika maoni yaliyokuwa yakiwasilishwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III). Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, SACP. Ibrahim Mahumi. 


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (aliyesimama mbele) akiwasilisha kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III). Wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora.


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Saashisha Mafuwe akiwasilisha hoja kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Yohana Msita akiwasilisha hoja kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).

Sehemu ya Wakurugenzi na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza kwenye kikao Bungeni jijini Dodoma mara baada ya Watendaji wa ofisi hiyo kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).

Sehemu ya Wakurugenzi Wasaidizi na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza kwenye kikao Bungeni jijini Dodoma mara baada ya Watendaji wa ofisi hiyo kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).






Thursday, August 13, 2026

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YAIELEKEZA SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA KUTOA HUDUMA KIDIJITI

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 13 Agosti, 2026


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imepokea taarifa ya utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambapo imeielekeza Taasisi hiyo kujikita zaidi kidijiti katika utoaji wa huduma mbalimbali kuhusu namna Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma inavyofanya kazi jambo ambalo litawasaidia Viongozi wanaowajibika chini ya Sheria ya Maadili kuhusu Ujazaji wa Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni pamoja na Hati ya Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi wa Umma na Uwajibikaji wa pamoja ili waweze kukamilisha kwa wakati taarifa zitakazohitajika katika ujazaji wa fomu hizo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro ametoa kauli hiyo leo jijini Dodoma alipokuwa akihitimisha kikao cha Kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kilichokuwa na lengo la kupokea taarifa ya Utendaji wa Taasisi hiyo kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa maadili ya Viongozi wa Umma ikiwemo uhakiki wa uzingatiaji wa ahadi za uadilifu, tamko la mali na madeni na ushughulikiaji wa malalamiko na mashauri.

Mhe. Dkt Ndumbaro pia amesisitiza suala la kuongeza juhudi za kutoa elimu zaidi ya namna ya kujaza fomu mbalimbali za Maadili kwa Viongozi ili kuepukana na changamoto ya kuchelewesha ujazaji wa taarifa kwani, kuna baadhi ya Viongozi wanakuwa wapya katika uongozi hivyo inawalazimu kupewa uelewa mpana utakaowaongoza katika ujazaji wa fomu hizo.

Ameongeza kuwa, utoaji wa elimu zaidi utasaidia jamii kuona namna Taasisi hiyo inavyofanya kazi kubwa kwa maendeleo ya nchi.

“Ni vema kuongeza elimu zaidi kuhusu ujazaji wa fomu za maadili kwa Viongozi wanaowajibika chini ya sheria ili kuepukana na changamoto mbalimbali, wakati mwingine tunapata Viongozi wapya ambao hawana uelewa mpana juu ya ujazaji wa fomu hizo, hivyo elimu itakapotolewa itasaidia kupunguza changamoto hizo na kujaza kwa wakati fomu husika lakini pia elimu hiyo itawapa wananchi uelewa zaidi wa namna Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma inavyotekeleza majukumu yake kwa ufanisi,’’ Amesema Mhe. Dkt. Ndumbaro

Akiwasilisha taarifa hiyo, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, Naibu Waziri wa ofisi hiyo, Mhe. Regina Qwaray amesema Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ina jukumu la kusimamia tabia na mienendo ya Viongozi wa Umma ili kukidhi matakwa ya Sheria ya Maadili.

Mhe. Qwaray amesema, Majukumu ya Msingi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ni pamoja na kupokea na kufanya uhakiki wa Matamko ya Viongozi wa Umma kuhusu Rasilimali, kufanya utafiti juu ya hali ya Maadili na kushauri na kuweka mikakati katika masuala yanayohusu Uadilifu nchini, kufanya uchunguzi kuhusu ukiukwaji wa maadili yaliyotajwa na Sheria, kupokea na kushughulikia malalamiko na taarifa za ukiukwaji wa Maadili kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kutoka kwa wananchi pamoja na kutoa elimu ya Maadili kwa Viongozi wa Umma.

Naibu Waziri Qwaray ameongeza kuwa, Katika kipindi cha Julai 2025 hadi Juni 2026, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imetekeleza kazi za usimamizi na ushughulikiaji wa maadili ya viongozi wa umma ikiwemo uhakiki wa uzingatiaji wa ahadi za uadilifu, tamko la mali na madeni na ushughulikiaji wa malalamiko na mashauri pamoja na kusaini hati husika pindi viongozi wanapoteuliwa, kuajiriwa au kuchaguliwa

Pia Mhe. Qwaray amesema, elimu ya maadili itaendelea kutolewa katika shule na vyuo kupitia klabu za maadili ili kuweza kujenga na kuimarisha maadili ya kitaifa na kuyafanya yawe sehemu ya jamii pamoja na kuzuia mmomonyoko wa maadili nchini pamoja na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu Sheria ya Ulinzi wa watoa taarifa ambayo inamhakikishia usalama na ulinzi.

Akitoa neno la shukrani kwa Kamati hiyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kwa kuendelea kutoa miongozo na maelekezo ya kiutendaji ambayo yanaongeza chachu na ufanisi katika kuboresha na kuimarisha utendaji kazi na kuleta tija katika kuwahudumia Viongozi na Wananchi kwa lengo la kujenga na kuimarisha Utawala Bora nchini.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria ikiwa katika kikao na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Taasisi hiyo kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (wa kwanza kushoto) akifuatilia taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakati wa kikao cha Kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Taasisi hiyo kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifafanua hoja Bungeni jijini Dodoma wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiwasilisha kwa Kamati ya  Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma wakati wa kikao kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma. 


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Aziza Ally (wa kwanza kulia) akiwasilisha hoja kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa kikao kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma.

Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa na Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa ofisi hiyo kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.


Kamshina wa Maadili Mhe. Jaji (Mst.) Sivangilwa Mwangesi (katikati), akiandika maoni yaliyokuwa yakiwasilishwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo Bungeni jijini Dodoma na Watendaji hao kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Taasisi hiyo kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.




Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Yahaya Nawanda (katikati) akiwasilisha hoja kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa kikao kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Nyamizi Mhoja akifuatilia jambo wakati wa kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Mariam Yahya (wa kwanza kushoto) akiwasilisha hoja kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa kikao kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma.


Watendaji na Maafisa wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa na Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa ofisi hiyo kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.

 



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) akisikiliza hoja zilizokuwa zikiwasilishwa na sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa ofisi hiyo kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma. Wa kwanza kushoto ni Naibu Waziri wa ofisi yake Mhe. Regina Qwaray.


Watendaji na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza Bungeni jijini Dodoma kwenye kikao cha Kamati hiyo na Ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.


Wednesday, August 12, 2026

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YAPOKEA TAARIFA YA UTENDAJI WA TUME YA UTUMISHI WA UMMA, YASISITIZA UTOAJI WA ELIMU KUHUSU RUFAA NA MALALAMIKO KWA WATUMISHI WA UMMA

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 12 Agosti, 2026


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imepokea taarifa ya utendaji wa Tume ya Utumishi wa Umma na kusisitiza kutolewa kwa elimu zaidi kwa Watumishi wa Umma ili waweze kuwasilisha rufaa na malalamiko kwa wakati na mahali husika kwa lengo la kutimiza haki na wajibu katika utendajikazi.

Kauli hiyo imetolewa jijini Dodoma leo na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro alipokuwa akiongoza kikao cha Kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Tume ya Utumishi wa Umma kilicholenga kupokea taarifa ya Utendaji wa Tume hiyo katika kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira.

“Elimu inahitajika zaidi kwa Watumishi wa Umma kwenye maeneo yao ya kazi ili kuongeza uelewa wa namna ya kushughulikia rufaa na malalamiko hayo ikiwa ni pamoja na kupata utatuzi wa migogoro katika Utumishi wa Umma,’’ Amesisitiza Mhe. Dkt. Ndumbaro

Katika hatua nyingine, Mhe. Dkt. Ndumbaro amempongeza na kumshukuru Waziri Kikwete kwa taarifa nzuri aliyoiwasilisha kwa Kamati hiyo iliyoelezea kwa kina taarifa ya utendaji ya Tume ya Utumishi wa Umma katika kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira ambayo itaongeza chachu ya utendaji kazi kwa Watumishi wa Umma.

Mhe. Dkt. Ndumbaro ameiahidi Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora kuwa itashirikiana nayo katika usimamizi wa masuala mbalimbali ili kuleta matokeo chanya kwa ustawi wa Taifa.

Awali akiwasilisha kwa Kamati hiyo taarifa ya utendaji ya Tume ya Utumishi wa Umma katika kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema, Tume ya Utumishi wa Umma ni Mamlaka ya Rufaa kwa Watumishi wa Umma katika taasisi 554 waliopo kwenye makundi mbalimbali ya Watumishi wa Umma, Serikali Kuu, Mamlaka ya Serikali za Mitaa na Watumishi waliopo katika Taasisi za Umma.

Vilevile, Mhe. Kikwete amesema Tume hiyo ina jukumu la kupokea malalamiko na rufaa kutoka kwa Watumishi wa Umma ambao hawakuridhika na uamuzi wa mamlaka zao za ajira, mamlaka za nidhamu na waajiri baada ya uamuzi walioufanya na mamlaka hizo hivyo, elimu itakayotolewa kwa Watumishi wa Umma itasaidia kwa kiasi kikubwa kupata haki na wajibu kwa kila mmoja.

Aidha, Mhe. Kikwete ameishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, kwa kuwa na majadiliano mazuri na ofisi anayoiongoza ambayo wanaamini yatawasaidia kwa kiasi kikubwa katika kuongeza ufanisi na utendaji wa majukumu yao.

“Mhe. Mwenyekiti, nitoe shukrani za dhati kwa niaba ya ofisi ninayoiongoza mara zote tumepokea maoni, ushauri na michango mbalimbali kutoka katika Kamati yako inayolenga kuboresha Utumishi wa Umma nchini kwa lengo la kutimiza azma ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwa na Utumishi wa Umma uliotukuka.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi amesema Kamati hiyo imekuwa msaada mkubwa wa kuiongoza Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora kwa kuwapatia maarifa mengi kutoka kwa Wajumbe wote wa Kamati hiyo yenye kuleta tija katika kuwahudumia wadau mbalimbali na kuboresha utendajikazi.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (aliyesimama) akizungumza wakati wa kikao cha Kamati yake kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi ya Tume ya Utumishi wa Umma baada ya Tume hiyo kuwasilisha taarifa kuhusu kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira.




Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akizungumza wakati wa kikao cha Kamati yake kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi ya Tume ya Utumishi wa Umma baada Tume hiyo kuwasilisha taarifa kuhusu kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwasilisha kwa Kamati ya  Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira wakati wa kikao kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma. Wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwasilisha kwa Kamati ya  Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira wakati wa kikao kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma. Wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI


Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakifuatilia jambo wakati wa kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akiwa katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira. Kulia kwake ni Naibu Waziri wa ofisi yake Mhe. Regina Qwaray.


Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakiwa kwenye kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira.


Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakifuatilia jambo wakati wa kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira.


Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza wakati wa kikao cha Kamati hiyo Bungeni jijini Dodoma na Watendaji hao kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifafanua hoja Bungeni jijini Dodoma wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira.


Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda (aliyesimama) akisikiliza maoni kutoka kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo Bungeni jijini Dodoma na Watendaji hao kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira.

Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (aliyesimama) akifafanua hoja iliyowasilishwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kilicholenga kuwasilisha taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili akishukuru baada ya kupokea pongezi kutoka kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria ya kuteuliwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Naibu Katibu Mkuu wa ofisi hiyo. Pongezi hizo zimetolewa baada ya kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa ofisi hiyo kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira.


Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza kwenye kikao cha Kamati hiyo Bungeni jijini Dodoma na Watendaji hao kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira.


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Edwin Swalle (wa kwanza kulia) akiwasilisha hoja kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa kikao kilicholenga kuwasilisha taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma.


Watendaji na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza kwenye kikao cha Kamati hiyo Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira.


Watendaji na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza kwenye kikao cha Kamati hiyo Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira.