Na. Mwandishi wetu-Dodoma
Tarehe7
Septemba, 2026
Serikali
imesisitiza umuhimu wa watumishi wa umma kuzingatia Sheria, Sera, Kanuni,
Taratibu, Miongozo na Maadili ya Utumishi wa Umma ili kuongeza ufanisi katika
utoaji wa huduma kwa wananchi.
Hayo
yamesemwa leo Septemba 7, 2026 jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray
(Mb), alipotembelea Bodi ya Usajili wa Wahandisi kukagua utekelezaji wa zoezi
la Ukaguzi wa Uzingatiaji wa Sheria katika Usimamizi wa Utumishi wa Umma kwa
mwaka wa fedha 2026/2027.
Mhe.
Qwaray amesema ukaguzi huo unaofanywa na Tume ya Utumishi wa Umma ni muhimu kwa
Serikali kupata taarifa kuhusu hali ya uzingatiaji wa sheria katika usimamizi
wa masuala ya kiutumishi, pamoja na kubaini maeneo yanayohitaji maboresho ili
kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na kwa wakati.
Amesema
taarifa zinazotokana na ukaguzi huo huisaidia Serikali kufanya maamuzi na
kupanga mipango ya rasilimali watu kwa kuzingatia ushahidi, huku pia zikitoa
mrejesho kuhusu utekelezaji wa Sera, Sheria, Kanuni na Taratibu za Utumishi wa
Umma na kusaidia kuweka ulinganifu katika tafsiri na utekelezaji wake.
Aidha,
ameipongeza Tume ya Utumishi wa Umma kwa kuanzisha Mfumo wa Kielektroniki wa
Ukaguzi wa Uzingatiaji wa Sheria katika Usimamizi wa Utumishi wa Umma, akieleza
kuwa matumizi ya mfumo huo yanaendana na jitihada za Serikali za kutumia TEHAMA
katika kuboresha utendaji na usimamizi wa shughuli za Serikali.
Ameeleza
kuwa Serikali imeendelea kujenga mifumo mbalimbali ikiwemo e-Watumishi na
e-Utendaji kwa lengo la kuongeza ufanisi katika usimamizi wa watumishi wa umma.
Katika
hatua nyingine, Mhe. Qwaray amewataka watumishi na wasimamizi kuzingatia
maelekezo ya utekelezaji wa PEPMIS, akibainisha kuwa changamoto ya baadhi ya
watumishi kushindwa kufikia asilimia 75 zinazohitajika katika mchakato wa
kupandishwa vyeo inaweza kuchangiwa na kutokuzingatiwa ipasavyo kwa majukumu na
taratibu za mfumo huo.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Regina Qwaray (Mb),
akizungumza na Watumishi wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB) (hawapo pichani),
mara baada ya Naibu Waziri huyo kuwasili katika zoezi la Ukaguzi wa Uzingatiaji
wa Sheria katika Usimamizi wa Utumishi wa Umma leo Septemba 7, 2026 jijini
Dodoma
Washiriki kutoka Bodi ya
Usajili wa Wahandisi na Tume ya Utumishi wa Umma wakimsikiliza Naibu Waziri,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakati Naibu
Waziri huyo alipotembele Bodi hiyo kukagua zoezi la Ukaguzi wa Uzingatiaji wa
Sheria katika Utumishi wa Umma Jijini Dodoma
Washiriki kutoka Bodi ya
Usajili wa Wahandisi na Tume ya Utumishi wa Umma wakimsikiliza Naibu Waziri,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakati Naibu
Waziri huyo alipotembele Bodi hiyo kukagua zoezi la Ukaguzi wa Uzingatiaji wa
Sheria katika Utumishi wa Umma Jijini Dodoma
Baadhi ya Viongozi na
Watumishi kutoka Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB) wakimsikiliza Naibu Waziri
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Regina
Qwaray (hayupo pichani) wakati Naibu Waziri huyo alipokuwa akizungumza nao mara
baada ya kupitishwa na kuona namna mfumo wa Kielektroniki wa Ukaguzi wa
Uzingatiaji wa Sheria katika Usimamizi wa Utumishi wa Umma unavyofanya kazi leo
Septemba 7, 2026 jijini Dodoma.
Watumishi kutoka Bodi ya
Usajili wa Wahandisi (ERB) wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakati Naibu Waziri huyo
alipotembelea Bodi hiyo kuona zoezi la Ukaguzi wa Uzingatiaji wa Sheria katika
Utumishi wa Umma linavyoendeshwa Jijini Dodoma
Watumishi kutoka Bodi ya
Usajili wa Wahandisi (ERB) wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakati Naibu Waziri huyo
alipotembelea Bodi hiyo kuona zoezi la Ukaguzi wa Uzingatiaji wa Sheria katika
Utumishi wa Umma linavyoendeshwa Jijini Dodoma
Watumishi kutoka Bodi ya
Usajili wa Wahandisi (ERB) wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakati Naibu Waziri huyo
alipotembelea Bodi hiyo kuona zoezi la Ukaguzi wa Uzingatiaji wa Sheria katika
Utumishi wa Umma linavyoendeshwa Jijini Dodoma
Mtumishi kutoka Tume ya
Utumishi wa Umma akifafanua jambo kuhusu Mfumo wa Ukaguzi wa Uzingatiaji wa
Sheria katika Usimamizi wa Utumishi wa Umma unavyofanya kazi mara baada ya Naibu
Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe.
Regina Qwaray kuwasili katika Bodi ya Usajili wa Wahandisi kuoa (ERB) kuona
zoezi hilo leo Septemba 7, 2026 jijini Dodoma.
























