Na. Mwandishi Wetu-Dodoma
Tarehe 5 Agosti, 2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameongoza mapokezi ya
Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bi. Prisca Lwangili aliyeteuliwa hivi karibuni
na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan baada
ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi kustaafu Utumishi
wa Umma.
Bi. Prisca Lwangili, amepokelewa rasmi leo na
Viongozi na Watumishi wa ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma.
Akizungumza wakati wa mapokezi hayo, Mheshimiwa
Kikwete amemkaribisha Bi. Lwangili na kumsihi kutumia uzoefu wake katika kazi kwa
lengo la kuimarisha utekelezaji wa majukumu ya ofisi hiyo ili kuongeza uwajibikaji
katika kuhudumia wananchi kwa ustawi wa Taifa
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Ofisi hiyo,
Mheshimiwa Regina Qwaray, amemkaribisha Bi. Lwangili na kueleza kuwa Viongozi pamoja
na Watumishi wa Ofisi hiyo wapo tayari kumpa ushirikiano katika kutekeleza
majukumu yake mapya, ili kuimarisha utendaji wa ofisi kwa manufaa ya umma.
Naye Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Juma Mkomi,
amesema uongozi na watumishi wa Ofisi hiyo wako tayari kushirikiana kwa karibu
na Naibu Katibu Mkuu huyo ili kuhakikisha majukumu ya Ofisi yanatekelezwa kwa
ufanisi na kufikia malengo yaliyowekwa na Serikali.
Kwa
upande wake, Bi. Lwangili amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumteua katika nafasi hiyo ambapo ameahidi kutekeleza
majukumu yake kwa kujituma na kuongeza ubunifu ili kuhakikisha malengo ya ofisi
hiyo yanafikiwa kwa manufaa ya Serikali na wananchi.
Aidha,
ameishukuru ofisi hiyo kwa mapokezi aliyopata na kuahidi kufanya kazi kwa
ufanisi katika kuwahudumia Wananchi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa ofisi hiyo mara baada ya kumpokea Naibu Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bi. Prisca Lwangili (hayupo pichani) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan baada ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi kustaafu Utumishi wa Umma.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili (kushoto) akipokea ua la ukaribisho mara baada ya kuwasili rasmi katika ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma baada ya kuteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan. Kulia ni Mtumishi wa ofisi hiyo Bi. Subira Swallah.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bi. Prisca Lwangili (kushoto) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan baada ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi kustaafu Utumishi wa Umma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya kumpokea Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bi. Prisca Lwangili (hayupo pichani) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan kabla ya kuwasili katika ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakisubiri kumpokea Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bi. Prisca Lwangili (hayupo pichani) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan kabla ya kuwasili katika ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifurahia jambo wakati wakisubiri kumpokea Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bi. Prisca Lwangili (hayupo pichani) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan baada ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi kustaafu Utumishi wa Umma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakisubiri kumpokea Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bi. Prisca Lwangili (hayupo pichani) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan kabla ya kuwasili katika ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (katikati) akizungumza jambo na Katibu Mkuu wa ofisi hiyo, Bw. Juma Mkomi (kulia) wakati wakisubiri kumpokea Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bi. Prisca Lwangili (hayupo pichani) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa ofisi hiyo Bw. Musa Magufuli.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili akisaini kitabu cha wageni alipowasili rasmi katika ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma baada ya kuteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili (kulia) akitoa neno la shukrani baada ya kuwasili rasmi katika ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma baada ya kuteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa pili kutoka kushoto mstari wa kwanza) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Wakurugenzi wa Idara na Vitengo wa ofisi hiyo mara baada ya kumpokea Naibu Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bi. Priscar Lwangili (wa kwanza kulia mstari wa mbele) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan baada ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi kustaafu Utumishi wa Umma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akisalimiana na kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bi. Prisca Lwangili (kushoto) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan baada ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi kustaafu Utumishi wa Umma.