Na Antonia Mbwambo – Dodoma
Tarehe 31 Agosti, 2026
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili, amesisitiza umuhimu wa kuzingatia
Sheria, Taratibu na Kanuni katika kushughulikia mashauri ya nidhamu katika
Utumishi wa Umma, akieleza kuwa uzingatiaji wa misingi hiyo ni muhimu katika
kuhakikisha haki inatendeka.
Bi. Lwangili
ameyasema hayo leo, tarehe 31 Agosti, 2026, wakati akihitimisha mafunzo ya
uelewa kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI yaliyofanyika katika eneo
maalumu la Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma.
Bi. Lwangili amesema katika kushughulikia masuala ya nidhamu ni
muhimu kuhakikisha kuwa thamani na utu wa mtu vinalindwa, huku hatua zote
zikichukuliwa kwa kuzingatia Sheria, Taratibu na Kanuni zilizowekwa.
“Ni muhimu
kuhakikisha kuwa katika kushughulikia mashauri ya nidhamu, Sheria, Taratibu na
Kanuni zinafuatwa ili haki itendeke, huku tukilinda thamani na utu wa mtu,
amesema Bi. Lwangili.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuwakumbusha Watumishi wa Umma
kuhusu madhara ya kutokuzingatia Sheria, Taratibu na Kanuni katika utekelezaji
wa majukumu yao, akieleza kuwa uelewa huo utasaidia kupunguza makosa na
kuwaepusha watumishi na changamoto ya kufikishwa katika mashauri ya kinidhamu.
Kwa upande wake mwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye ni Afisa Sheria Mwandamizi, kutoka Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Edwin Bilikundi, amesema usimamizi wa nidhamu katika Utumishi
wa Umma umejengwa katika dhana mbili kuu ambazo ni kurekebisha mwenendo wa Mtumishi (corrective measures) na utoaji wa adhabu (sanction
approach). Amesema njia ya
kurekebisha inalenga kumsaidia Mtumishi kutambua kosa na kujirekebisha, wakati
utoaji wa adhabu hutumika pale kosa linapothibitika, hususan kwa makosa
yanayojirudia au yenye uzito.
Bw. Bilikundi ameongeza kuwa mchakato wa kinidhamu unapaswa
kuanza kwa uchunguzi wa awali unaolenga kubaini ukweli na uzito wa tuhuma,
pamoja na kuamua hatua stahiki za kuchukua.
Amesisitiza kuwa uzingatiaji wa hatua na muda uliowekwa katika
Sheria, Kanuni na Taratibu ni muhimu katika kuhakikisha mchakato wa nidhamu
unakuwa wa haki na wenye msingi sahihi wa kisheria.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili
akizungumza na Watumishi wa Ofisi hiyo (hawapo pichani) wakati Naibu Katibu
Mkuu huyo akihitimisha mafunzo yaliyolenga kuwajengea Watumishi hao uelewa
kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu katika Utumishi wa Umma,
yaliyofanyika tarehe 31 Agosti, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo, Mtumba,
jijini Dodoma.
Baadhi ya Wakurugenzi na
Watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifurahia jambo wakati walipokuwa
wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji leo tarehe 31 Agosti,
2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma
Afisa Sheria Mwandamizi,
kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Edwin Bilikundi akiendesha mafunzo ya uelewa
kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu katika Utumishi wa Umma kwa
Watumishi wa Ofisi hiyo leo tarehe 31 Agosti 2026 katika eneo maalumu la Ofisi
hiyo, Mtumba, jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala
na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora, Bw. Musa Magufuli akisisitiza jambo wakati wa mafunzo ya
uelewa kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu katika Utumishi wa Umma
Mtumba Jijini Dodoma
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili akisisitiza jambo wakati akihitimisha mafunzo ya
kuwajengea Watumishi hao uelewa kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu
katika Utumishi wa Umma, yaliyofanyika tarehe 31 Agosti, 2026 katika eneo
maalumu la Ofisi hiyo, Mtumba, jijini Dodoma
Baadhi ya Watumishi kutoka
Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakifuatilia
mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji leo tarehe 31 Agosti, 2026 katika
eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma
Baadhi ya Wakurugenzi na
Watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifurahia jambo wakati walipokuwa
wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji leo tarehe 31 Agosti,
2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma
Baadhi ya Wakurugenzi na
Watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifurahia jambo wakati walipokuwa
wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji leo tarehe 31 Agosti,
2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili (wa
pili kutoka kushoto) akifurahia jambo wakati alipokuwa akifuatilia mafunzo
kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu katika Utumishi wa Umma leo Agosti
31, 2026 Mtumba Jijini Dodoma
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, SACP. Ibrahim Mahumi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI
akisisitiza jambo wakati wa mafunzo ya uelewa kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri
ya Nidhamu katika Utumishi wa Umma Mtumba Jijini Dodoma