Na. Antonia Mbwambo – Dodoma
13 Julai, 2026
Katibu
Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, amewataka Watumishi wa Umma
kuongeza kasi ya utendaji na kuzingatia weledi ili kuchangia kikamilifu katika
utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Katibu
Mkuu Mkomi ametoa wito huo leo Julai 13, 2026, wakati akihitimisha mafunzo
kuhusu umuhimu wa afya ya akili kwa Watumishi wa Umma yaliyofanyika katika eneo
maalumu la Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Mtumba, jijini Dodoma kwa lengo la
kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi hao.
Bw.
Mkomi amesema mafanikio ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050
yanategemea uwepo wa Watumishi wa Umma wenye afya bora ya akili, maadili ya
kazi, ubunifu na uwajibikaji, huku akisisitiza kuwa afya ya akili ni msingi wa
utendaji wenye tija na utoaji wa huduma bora Serikalini.
"Afya
ya akili si suala la mtu mmoja mmoja, bali ni msingi wa kuongeza tija katika Utumishi
wa Umma. Mtumishi mwenye afya bora ya akili anakuwa na uwezo mkubwa wa kutoa
huduma bora, kushirikiana na wenzake na kuleta matokeo chanya kwa Taasisi na
Taifa kwa ujumla," amesema Bw. Mkomi.
Aidha,
Bw. Mkomi amewaelekeza Wachumi wa Ofisi hiyo kufanya tafakuri za kitaaluma na
kuibua mawazo bunifu yatakayochangia Serikali kufikia malengo ya Dira ya Taifa
ya Maendeleo 2050.
Kwa
upande wake, Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma,
Dkt. Elihuruma Elias, ambaye alikuwa Mwezeshaji wa mafunzo hayo, amesema afya
ya akili ni nguzo muhimu ya ustawi wa mtumishi na ina mchango mkubwa katika
kuongeza tija pamoja na kuboresha mazingira ya kazi.
Ameeleza
kuwa changamoto za afya ya akili kwa watumishi wa Umma mara nyingi husababishwa
na mpangilio duni wa kazi, mzigo mkubwa wa majukumu unaozidi uwezo wao, kazi za
kujirudia rudia na mazingira magumu ya kazi. Amewahimiza watumishi kuzingatia
mtindo bora wa maisha kwa kufanya mazoezi ya mara kwa mara, kula lishe bora,
kupata mapumziko ya kutosha na kutafuta ushauri wa Wataalamu wanapokabiliwa na
changamoto za afya ya akili.
Aidha,
Dkt. Elias amewataka viongozi kuendelea kuzingatia usawa kwa watumishi
wanaowasimamia, kupinga unyanyapaa dhidi ya wenye changamoto za afya ya akili
na kutambua mapema dalili za changamoto hizo ili kuwawezesha watumishi kupata
huduma stahiki kwa wakati.
Katibu
Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akifurahia jambo wakati
alipokuwa akihitimisha mafunzo ya uelewa kwa Watumishi wa Ofisi hiyo Julai 13,
2026 Mtumba Jijini Dodoma
Katibu
Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (wa kwanza kutoka kushoto),
akifuatilia mada ya mafunzo kuhusu umuhimu wa afya ya akili kwa Watumishi wa
Umma yaliyokuwa yakitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi
Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma Elias (hayupo pichani) leo Julai 13,
2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba
jijini Dodoma. Kushoto kwake ni Mkurugenzi
wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Ofisi hiyo Bw. Musa
Magufuli.
Katibu
Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, akizungumza na Watumishi wa
Ofisi yake wakati alipokuwa akihitimisha Mafunzo ya uelewa kuhusu Umuhimu wa
Afya ya Akili kwa Watumishi wa Umma yaliyofanyika Julai 13, 2026 katika eneo
maalumu la Ofisi hiyo, Mtumba jijini Dodoma
Baadhi
ya Wakurugenzi kutoka Idara na Vitengo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa
Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo
pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika
eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma.
Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma
Bingwa
wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma
Elias akitoa mada ya mafunzo kuhusu Umuhimu wa Afya ya Akili kwa Watumishi wa Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora yaliyofanyika Julai
13, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Jijini Dodoma
Baadhi
ya Wakurugenzi kutoka Idara na Vitengo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa
Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo
pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika
eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma.
Bingwa
wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma
Elias akitoa mada ya mafunzo kuhusu Umuhimu wa Afya ya Akili kwa Watumishi wa Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora yaliyofanyika Julai
13, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Jijini Dodoma
Baadhi
ya Wakurugenzi kutoka Idara na Vitengo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa
Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo
pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika
eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma.
Baadhi
ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka
Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa
mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.
Baadhi
ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka
Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa
mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.
Baadhi
ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka
Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa
mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.





















