Na Antonia Mbwambo - Dodoma
Tarehe 10 Agosti, 2026
Naibu
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Bi. Prisca Lwangili, amesisitiza umuhimu wa kuendelea kujenga ujuzi wa
kitaalamu na haiba ya uongozi katika kuwaandaa warithi wa madaraka ili
kuhakikisha kunakuwa na mwendelezo wa utendaji na utoaji wa huduma bora katika
Taasisi za umma.
Bi.
Lwangili ameyasema hayo leo, Agosti 10, 2026, wakati akihitimsha mafunzo ya
uelewa kuhusu Urithishanaji Madaraka yaliyofanyika katika eneo maalumu la Ofisi
ya Rais-UTUMISHI, Mtumba Jijini Dodoma.
Amesema
maandalizi ya urithishanaji madaraka yanapaswa kuanza mapema kwa kuwajengea
uwezo unaohitajika katika nafasi za uongozi wanazotarajiwa kuzishika.
Aidha,
Bi. Lwangili ameongeza kuwa ujuzi wa kitaalamu (Technical Skills) humwezesha Mtumishi kuwa na maarifa na uwezo wa
kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi, huku haiba ya uongozi ikimsaidia
kuwasiliana vizuri, kujiamini, kushirikiana na wengine, kuwa mwadilifu, kufanya
maamuzi na kuwajibika.
“Kuwa
na ujuzi wa kitaalamu pekee hakutoshi. Mtumishi anayejengwa kuwa Kiongozi wa
baadaye anapaswa pia kuwa na haiba inayomjengea uwezo wa kuwasiliana vizuri,
kujiamini, kushirikiana na wengine, kuwa mwadilifu, kufanya maamuzi na kubeba
majukumu kwa uwajibikaji,” amesema Bi. Lwangili.
Pia
Bi. Lwangili amesisitiza kuwa, Urithishanaji Madaraka si kumwandaa mtu kuchukua
nafasi ya Kiongozi aliyepo pekee, bali ni kuimarisha Taasisi kwa kuwa na
Watumishi wenye uwezo wa kuendeleza majukumu na huduma za umma.
Kwa
upande wake, Mchumi Mkuu kutoka Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bi. Bertha Bomani, ameeleza kuwa Urithishanaji Madaraka ni
mchakato wa kuwaandaa mapema Watumishi wenye uwezo na sifa stahiki kwa ajili ya
majukumu ya uongozi.
Bi. Bomani amebainisha mikakati ya
Urithishanaji Madaraka katika Utumishi wa Umma ikiwa ni pamoja na kuendelea
kutoa elimu ya uelewa na kujenga uwezo kwa Viongozi na Watumishi kuhusu manufaa
ya kuandaa na kutekeleza Mpango
wa Urithishanaji Madaraka,
pamoja na kuwakumbusha Waajiri kutenga fedha katika bajeti za Taasisi zao kwa
ajili ya uandaaji na utekelezaji wa mpango huo.
Naibu
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Bi. Prisca Lwangili akizungumza na Watumishi wa Ofisi hiyo (hawapo pichani) wakati
Naibu Katibu Mkuu huyo akihitimisha Mada ya mafunzo kuhusu Urithishanaji wa
Madaraka leo tarehe 10 Agosti, 2026 Mtumba Jijini Dodoma.
Baadhi ya Wakurugenzi na
Watumishi kutoka Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
wakifuatilia mafunzo ya Uelewa kuhusu Urithishanaji
Madaraka yaliyofanyika tarehe 10 Agosti,2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo
iliyopo Mtumba Jijini Dodoma
Naibu
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Bi. Prisca Lwangili (aliyesimama mbele) akizungumza na Watumishi wa Ofisi hiyo wakati
Naibu Katibu Mkuu huyo akihitimisha Mada ya mafunzo kuhusu Urithishanaji wa
Madaraka leo tarehe 10 Agosti, 2026 Mtumba Jijini Dodoma
Baadhi ya Watumishi kutoka
Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mafunzo
ya Uelewa kuhusu Urithishanaji
Madaraka yaliyofanyika tarehe 10 Agosti,2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo
iliyopo Mtumba Jijini Dodoma
Baadhi ya Watumishi kutoka
Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mafunzo
ya Uelewa kuhusu Urithishanaji
Madaraka yaliyofanyika tarehe 10 Agosti,2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo
iliyopo Mtumba Jijini Dodoma
Naibu
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Bi. Prisca Lwangili (wa pili kutoka kulia) akifuatilia mafunzo ya uelewa ambayo
hutolewa kila jumatatu ya wiki katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba Jijini
Dodoma leo tarehe 10, Agosti, 2026. Wengine ni Wakurugenzi na Wakurugenzi
wasaidizi wa Idara na Vitengo vya Ofisi hiyo.
Mkurugenzi
Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Leila Mavika akitoa ufafanuzi kuhusu Urithishanaji
Madaraka mara baada ya muwezeshaji ambaye pia ni Mchumi Mkuu wa Ofisi hiyo, Bi.
Bertha Bomani, kutoa maelezo kuhusu mada hiyo leo tarehe 10 Agosti, 2026 Jijini
Dodoma
Naibu
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Bi. Prisca Lwangili (wa kwanza kutoka kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa
TEHAMA Serikalini
Bw. Priscus Kiwango (wa pili kutoka kushoto) wakati wa
mafunzo ya uelewa kwa Watumishi wa Ofisi hiyo yaliyofanyika katika eneo maalumu la Ofisi hiyo
iliyopo Mtumba Jijini Dodoma
Baadhi
ya Wakurugenzi wasaidizi na Watumishi kutoka Ofisi ya Rais,Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mafunzo ya Uelewa kuhusu
Urithishanaji Madaraka yaliyofanyika tarehe 10 Agosti,2026 katika eneo maalumu
la Ofisi hiyo iliyopo Mtumba Jijini Dodoma
Baadhi ya Viongozi na
Watumishi kutoka Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
wakifuatilia mafunzo ya Uelewa kuhusu Urithishanaji
Madaraka yaliyofanyika tarehe 10 Agosti,2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo
iliyopo Mtumba Jijini Dodoma

















