Na. Antonia Mbwambo-Morogoro
Tarehe:
9 Februari, 2026
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Jakaya Kikwete ameziagiza Mamlaka zote za nidhamu nchini ikiwa ni pamoja na Mamlaka za Maji kusimamia na kuzingatia ipasavyo Sheria, Kanuni na Taratibu katika usimamizi na uendeshaji wa masuala ya rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma ili kuiepushia Serikali hasara zisizo za lazima kwa baadhi ya michakato ya mashauri ya nidhamu kurudiwa.
Mhe. Kikwete alisema hayo wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha Tume ya Utumishi wa Umma na Mamlaka za Maji nchini kuhusu utekelezaji wa sheria ya utumishi wa umma sura 298 na matumizi ya mfumo wa kielektroni wa kushughulikia rufaa na malalamiko na uwasilishaji wa taarifa za kiutumishi Tume.
“Nitumie fursa hii kuwakumbusha kuwa haki iliyocheleweshwa ni sawa na haki iliyonyimwa kwa kuwa ukiukwaji wa Sheria na Kanuni za Utumishi wa Umma unachelewesha upatikanaji wa haki za Watumishi kwa wakati kutokana na mashauri hayo kurejeshwa na Tume ili kuanzishwa upya” alisema Mhe. Kikwete.
Katika hotuba yake, Mhe. Kikwete alibainisha kuwa jumla ya rufaa 52 kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2023/2024 na 2024/2025 zilizopokelewa kutoka Mamlaka za Maji na kutolewa uamuzi na Tume, ingawa rufaa 20 sawa na asilimia 38 ya rufaa zote zilizopokelewa katika kipindi hicho zilionekana kuwa na ukiukwaji wa sheria, kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma na kusababisha Tume kuzirudisha ili mchakato wa mashauri ya kinidhamu uanze upya.
Mhe. Kikwete alisisitiza kuwa asilimia hizo ni nyingi na aliipongeza Tume kwa kuandaa kikao kazi hicho chenye lengo la kutoa mafunzo ya namna bora ya kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za Utumishi katika usimamizi na uendeshaji wa masuala ya rasilimaliwatu ili kuongeza ufanisi katika usimamizi na utoaji wa haki kwenye Utumishi wa Umma.
Tume ya Utumishi wa Umma ni chombo rekebu chini ya Ofisi ya Rais kilichoundwa ili kusimamia utoaji wa haki kwa kushughulikia rufaa na Malalamiko ya Watumishi wa Umma, kufanya ukaguzi, kutoa Miongozo na kutoa elimu kuhusu Sheria ya Utumishi wa Umma kwa Waajiri, Mamlaka za Ajira, Mamlaka za Nidhamu na Watumishi wa Umma ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Tume ya Utumishi wa Umma baada ya Waziri huyo kufungua kikao kazi cha mafunzo ya Tume ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka za Maji Tanzania cha Utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma na Matumizi ya Mfumo wa kielektroniki wa kushughulikia Rufaa na uwasilishwaji wa taarifa za masuala ya kiutumishi leo tarehe 9 Februari, 2026
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akisaini
kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika Ofisi za NSSF Mkoani Morogoro katika
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
Mhe. Ridhiwani Kikwete WTM5
Washiriki wa kikao kazi cha mafunzo
ya Tume ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka za Maji Tanzania cha Utekelezaji wa
Sheria ya Utumishi wa Umma na Matumizi ya Mfumo wa kielektroniki wa
kushughulikia Rufaa na uwasilishwaji wa taarifa za masuala ya kiutumishi
wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati Waziri huyo
alipokuwa akizungumza nao leo Mkoani Morogoro.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete
(aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Utawala kutoka
Mamlaka za Maji Tanzania baada ya Waziri huyo kufungua kikao kazi cha mafunzo
ya Tume ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka za Maji Tanzania cha Utekelezaji wa
Sheria ya Utumishi wa Umma na Matumizi ya Mfumo wa kielektroniki wa
kushughulikia Rufaa na uwasilishwaji wa taarifa za masuala ya kiutumishi leo
tarehe 9 Februari, 2026
Kaimu Katibu, Ofisi ya Rais,
Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. John Mbisso akitoa neno la Utangulizi kwa Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe.
Ridhiwani Kikwete baada ya Waziri huyo kuwasili katika ukumbi wa NSSF Mkoani
Morogoro katika kikao kazi cha mafunzo ya Tume ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka
za Maji Tanzania cha Utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma na Matumizi ya
Mfumo wa kielektroniki wa kushughulikia Rufaa na uwasilishwaji wa taarifa za
masuala ya kiutumishi leo tarehe 9 Februari, 2026.
Mkurugenzi wa Rasilimaliwatu
na Utawala Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira (AUWSA) Bw. Kazimil Kanyanza
akitoa neno la shukrani kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete baada ya Waziri huyo
kufungua kikao kazi cha mafunzo ya Tume ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka za Maji
Tanzania cha Utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma na Matumizi ya Mfumo wa
kielektroniki wa kushughulikia Rufaa na uwasilishwaji wa taarifa za masuala ya
kiutumishi kilichofanyika katika ukumbi
wa NSSF Mkoani Morogoro leo tarehe 9 February, 2026.






