Sunday, June 28, 2026

TIMU YA WATAALAMU OFISI YA RAIS - UTUMISHI NA WATUMISHI HOUSING INVESTMENTS (WHI) YAFANYA UKAGUZI WA UTEKELEZAJI WA MIRADI RUANGWA NA MASASI.

Timu ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watumishi Housing Investments (WHI) ipo katika ziara ya kukagua miradi ya ujenzi wa nyumba za Watumishi ambapo leo tarehe 28 Juni, 2026 imekagua maendeleo ya mradi wa Ujenzi wa nyumba ya Watumishi 6:1 katika Shule ya Sekondari Samia Suluhu Hassan - Ruangwa, pamoja na mradi wa Ujenzi wa Nyumba ya Watumishi 3:1 katika Kituo cha Afya Mtandi , Masasi-Mtwara


Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Watumishi Housing Investments (WHI) ikijadili jambo, mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Afya Mtandi , Masasi-Mtwara Juni 28, 2026


Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma shule ya sekondari Samia Suluhu Hassan katika Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi


Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma shule ya sekondari Samia Suluhu Hassan katika Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi


Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Watumishi Housing Investments ikiongozwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Patrick Allute ikikagua mradi wa maendeleo wa Ujenzi wa nyumba ya Watumishi 6:1 katika Shule ya Sekondari Samia Suluhu Hassan Wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi

Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Watumishi Housing Investments (WHI) ikijadili jambo, mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Afya Mtandi , Masasi-Mtwara Juni 28, 2026


Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma
katika Kituo cha Afya Mtandi -Mtwara


Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Watumishi Housing Investments (WHI) na baadhi ya Watumishi wa Kituo cha Afya Mtandi –Mtwara, wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya timu hiyo kukagua maendeleo ya mradi wa makazi ya Watumishi wa Kituo hicho Juni 28, 2026


Saturday, June 27, 2026

TIMU YA WATAALAMU OFISI YA RAIS - UTUMISHI NA WATUMISHI HOUSING INVESTMENTS (WHI) YAENDELEA NA UKAGUZI WA UTEKELEZAJI MIRADI

Timu ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watumishi Housing Investments (WHI) imeendelea na ziara ya kukagua miradi ya ujenzi wa nyumba za Watumishi katika Mkoa wa Lindi ambapo leo tarehe 27 Juni, 2026 imekagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba za Watumishi katika Kituo cha Afya Hoteli Tatu, Shule ya Sekondari Matanda, Shule ya Msingi Runyu, Kituo cha Afya Mvuleni na Shule ya Sekondari Mvuleni.


Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma la Kituo cha Afya Hoteli tatu kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, mkoani Lindi


Timu ya wataalamu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ikikagua ubora wa kazi za ujenzi wa nyumba ya watumishi katika Kituo cha Afya Hoteli Tatu, Wilaya ya Kilwa, Mkoani Lindi leo tarehe 27 Juni 2026


Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Patrick Allute (wa tano kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na timu ya wataalamu kutoka Ofisi hiyo na Watumishi Housing Investment mara baada ya kukamilisha ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa nyumba ya Watumishi katika Kituo cha Afya Hoteli Tatu, Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, Mkoani Lindi


Muonekano wa mbele wa jengo la
mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma wa shule ya sekondari Mvuleni kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Patrick Allute (aliyenyoosha mkomo) akijadili jambo na Wataalamu kutoka Ofisi hiyo na Watumishi Housing Investments (WHI) mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa nyumba za Watumishi wa Shule ya Sekondari Mvuleni iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi,Mkoa wa Lindi


Muonekano wa mbele wa jengo la
mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma wa shule ya sekondari Mvuleni kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi

Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma wa Kituo cha Afya Mvuleni kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi.

Muonekano wa ndani wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma wa Kituo cha Afya Mvuleni kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi.

Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Watumishi Housing Investments ikiongozwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Patrick Allute kukagua mradi wa maendeleo wa ujenzi wa Kituo cha Afya Mvuleni kilichopo Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi.


Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma wa Kituo cha Afya Mvuleni kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi


Mhandisi Salum Chanzi kutoka Watumishi Housing Investments (wa nne kutoka kulia) akifafanua jambo wakati wa ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya Mvuleni kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi