Tuesday, March 31, 2026

MAAFISA RASILIMALIWATU WATAKIWA KUFANYA TATHMINI KWENYE SUALA LA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA

 

Na. Veronica Mwafisi na Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 01 Aprili, 2026.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw, Juma Mkomi ametoa wito kwa Maafisa Rasilimaliwatu kufanya tathmini kwenye suala la uhamisho kwa watumishi wa umma ili kuondoa vikwazo na kuongeza tija ya utendajikazi katika Utumishi wa Umma.

Bw. Mkomi ameyasema hayo leo jijini Dodoma alipokuwa akifunga mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi kwa Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma yaliyokuwa yakifanyika kwa siku tisa kuanzia tarehe 23 Machi hadi 01 Aprili, 2026 jijini Dodoma.

Bw. Mkomi amesema, uhamisho ni haki ya mtumishi na mwajiri kutaka kumtumia mtumishi fulani katika eneo fulani au ni haki ya mwajiri kuendelea kumtumia mtumishi husika sehemu anayotumikia vizuri.

Hivyo, Bw. Mkomi amewataka Maafisa Rasilimaliwatu hao kufanya tathmini katika maeneo yao ya kazi hasa katika Mfumo wa Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma (e-Msawazo)

“Nitoe msisitizo kuhusu tathmini ya mahitaji ya rasilimaliwatu, naamini ninyi ndio wasimamizi wakubwa katika maeneo mengi na ndio mnaoleta taarifa ya masuala husika ya kiutumishi, utaratibu wa uhamisho una vigezo na vinajulikana hivyo ni vema kupata usahihi wa taarifa za watumishi au mahitaji ya watumishi hao pasipo kuwa na vikwazo au mifarakano isiyokuwa na tija kwa sababu ya uhamisho,” amesisitiza Bw. Mkomi.

Aidha, Bw. Mkomi ameongeza kuwa, Maafisa Rasilimaliwatu wana jukumu la kumshauri vizuri mwajiri linapotokea suala la uhamisho kwa mtumishi ni vema kutoa vigezo sahihi baada ya kufanya tathmini ya kutosha.

“Tunatamani umwambie mwajiri uhamishio wa mtumishi huyu tusiutekeleze kwa sababu tathmini tuliyoifanya ya rasilimaliwatu katika eneo letu tuna upungufu wa afisa husika au uhamisho huu tuutekeleze kwa sababu tuna maafisa wa kutosha kadhaa kwenye eneo letu,” amesema Bw, Mkomi

Vilevile, Bw. Mkomi amesema eneo la uhamisho limeonekana kuwa na changamoto kutokana na watumishi wanaoomba uhamisho kuzuiliwa bila kuwa na sababu za kutosha.

Bw. Mkomi amewataka Maafisa hao kufanyia kazi mafunzo yote waliyoyapata watakaporudi kwenye maeneo yao ya kazi ili yakaongeze tija katika Utumishi wa Umma

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini, Bw. Hamis Mkunga amesema jumla ya washiriki 275 wamepatiwa mafunzo hayo hivyo amewataka washiriki hao kwenda kufanyia kazi ili kuleta matokeo chanya katika maeneo yao ya kazi kwa maendeleo ya ofisi au taasisi husika na taifa kwa ujumla.

Akitoa neno la shukrani Mwenyekiti wa Mafunzo hayo, Bi. Isabela Chilumba amemuahidi Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi kuwa kwa niaba ya washiriki wote watazingatia maelekezo ambayo ameyatoa ili waweze kuboresha utendaji kazi kwa ustawi wa Taifa.

 


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akizungumza na Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma wakati akifunga mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyofanyika kuanzia tarehe 23 Machi - 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.


Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini wa Ofisi hiyo Bw. Hamis Mkunga (kushoto) kabla ya kufunga Mafunzo ya Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma kuhusu Mfumo wa e-Watumishi yaliyofanyika kuanzia tarehe 23 Machi - 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 jijini Dododma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 jijini Dododma.

Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Hamis Mkunga (kushoto)  pamoja na Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya Usimamizi na Payrol Jeanfrida Mushumbusi (kulia)  wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo wakati alipokuwa akifunga mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyojumuisha Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma yaliyofanyika kuanzia tarehe 23 Machi - 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma. 

Afisa kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambaye pia ni Mkufunzi wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini wa Ofisi hiyo Bw. Hamis Mkunga (kulia), kabla ya Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) kufunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akimkabidhi cheti mmojawapo wa washiriki wa mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyojumuisha Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo hayo leo tarehe 1 Aprili, 2026 Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiteta jambo na Afisa Rasilimaliwatu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Chemba Bi. Zuhura Kizuguto baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyotolewa Jijini Dodoma kuanzia tarehe 23 Machi - 01 Aprili, 2026 kwa Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma .

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akimkabidhi cheti mmojawapo wa washiriki wa mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyojumuisha Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo hayo leo tarehe 1 Aprili, 2026 Jijini Dodoma.





 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Monday, March 30, 2026

WATUMISHI WA UMMA WAHIMIZWA KUONGEZA UWAJIBIKAJI KATIKA KUTOA HUDUMA BORA

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 30 Machi, 2026.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma                                                                                                                                     na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi amewahimiza Watumishi wa Umma kuongeza uwajibikaji katika kuwahudumia wananchi.

Bw. Daudi ametoa wito huo leo alipokuwa akiwapongeza Watumishi wa Ofisi hiyo waliozaliwa mwezi Machi, 2026 mara baada ya kuhitimishwa kwa mafunzo yanayofanyika kila siku ya Jumatatu Mtumba Jijini Dodoma kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi watumishi wa ofisi hiyo.

Bw. Daudi amesema, mtumishi wa umma anapoongeza umri imsaidie kuongeza chachu ya utendajikazi ili kutimiza malengo ya Serikali ya kutoa huduma bora kwa wananchi.

''Nitoe wito kwa Watumishi wa Umma mnapoongeza umri na kusherehekea siku yenu ya kuzaliwa, hakikisheni mnawajibika ipasavyo katika maeneo yenu ya kazi hasa mnapotoa huduma kwa Watumishi wa Umma wenzenu na Wananchi, hakikisheni kuwa mnatimiza malengo ya Serikali katika kutoa huduma bora kwa kila Mtanzania.” amesema Bw. Daudi.


Awali katika mafunzo hayo, Afisa Rasilimaliwatu Mkuu kutoka katika ofisi hiyo, Idara ya Mishahara, Maslahi na Marupurupu, Bi. Magreth Banogile akiwasilisha mada kuhusu Motisha katika Utumishi wa Umma alisema, motisha ni manufaa anayoyapata mtumishi baada ya mshahara kutokana na majukumu anayoyatekeleza hivyo ni wajibu wa kila mtumishi wa umma kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi ili aweze kupata stahiki ya motisha husika.

Ameongeza kuwa baadhi ya motisha katika Utumishi wa Umma ni pamoja na mazingira bora ya kazi, vitendea kazi, fursa za mafunzo, huduma ya usafiri wa kwenda na kurudi kutoka kazini, pamoja na fursa ya muda wa kufanya mazoezi.

Aidha, katika mafunzo hayo kulikuwa na mada mbalimbali zilizowasilishwa na Maafisa kutoka katika Idara hiyo ya Mishahara, Maslahi na Marupurupu ambapo Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi Bw. Baraka Kilagu aliwasilisha mada kuhusu Miundo ya Maendeleo ya Utumishi chini ya Wizara pamoja na Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi, Bw. Imani Mtumbi aliyewasilisha mada kuhusu Miundo ya Mishahara katika Utumishi wa Umma.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi (wa tano kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa ofisi hiyo waliokuwa wakiadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa kwao mwezi Machi, 2026. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Musa Magufuli.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akifurahia jambo alipokuwa akizungumza na Watumishi wa ofisi hiyo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yanayofanyika kila Jumatatu kwenye Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Miundo ya Maendeleo ya Utumishi chini ya Wizara wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika ofisi hiyo jijini Dodoma.


Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Idara ya Mishahara, Maslahi na Marupurupu, Bw. Baraka Kilagu (aliyesimama) akiwasilisha mada kuhusu Miundo ya Maendeleo ya Utumishi chini ya Wizara wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika ofisi hiyo jijini Dodoma. Waliokaa wa kwanza kulia ni Afisa Rasilimaliwatu Mkuu kutoka ofisi hiyo Bi. Magreth Banogile na katikati ni Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi, Bw. Imani Mtumbi


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Miundo ya Mishahara katika Utumishi wa Umma wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo ambayo hufanyika katika ofisi hiyo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Miundo ya Mishahara katika Utumishi wa Umma wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo ambayo hufanyika katika ofisi hiyo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika ofisi hiyo jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Musa Magufuli (aliyesimama) akizungumza jambo kabla ya kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi kuzungumza na Watumishi wa ofisi hiyo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji yaliyofanyika katika ofisi hiyo jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Miundo ya Mishahara katika Utumishi wa Umma wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo ambayo hufanyika katika ofisi hiyo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Mhasibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Tumwimbilege Ilomo akikata keki kwa niaba ya Watumishi wa ofisi hiyo wanaoadhimisha  kumbukizi ya kuzaliwa kwao mwezi Machi, 2026.


Mhasibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Tumwimbilege Ilomo (kulia) akimlisha keki Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Maadili, Bi. Felister Shuli (kushoto) kwa niaba ya Watumishi wote waliozaliwa Mwezi Machi, 2026.