Thursday, August 6, 2026

KIKWETE AFUNGUA PAREDI YA MIFUGO NA KITUO CHA HUDUMA KWA WATEJA NANENANE

Na Eric Amani, Dodoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesisitiza wafugaji kuendelea kutumia mbinu bora za ufugaji katika kuongeza thamani ya mifugo ili kukidhi matakwa ya soko la ushindani wa mifugo ndani na nje ya nchi.

Mhe. Kikwete amebainisha hayo leo tarehe 5 Agosti, 2026 wakati akifungua Paredi ya Mifugo katika Maonesho ya Kitaifa ya Wakulima maarufu kama Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela Jijini Dodoma.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa paredi hiyo, Mhe. Kikwete alisema kuwa sekta ya mifugo ina mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa taifa kupitia uzalishaji, biashara na ajira. Hivyo, hatuna budi kuongeza juhudi na jitihada za kuimarisha mbinu za ufugaji bora kwa maslahi ya taifa.

Vile vile, Mhe. Kikwete aliwataka wadau wa sekta ya mifugo kuendelea kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa sera na programu mbalimbali zinazolenga kuboresha huduma za ugani, udhibiti wa magonjwa ya mifugo na kuimarisha miundombinu ya masoko.

Nitumie fursa kuwahamasisha wafugaji wote nchini kubadilisha mtazamo wa ufugaji wa kimazoea kwenda ufugaji unaotumia sayansi, takwimu na teknolojia na pia kushiriki na kuleta mifugo yao kwa ajili ya gwaride na mashindano kwa mwaka ujao 2027” alisema Kikwete.

Aidha,  Paredi hiyo ilihusisha maonesho ya aina mbalimbali za mifugo ikiwemo ng'ombe, mbuzi na mifugo mingine ambapo wafugaji na taasisi mbalimbali walipata fursa ya kuonesha ubora wa mifugo yao pamoja na teknolojia na ubunifu unaotumika katika kuendeleza sekta hiyo.

Waziri Kikwete pia alitoa rai kwa taasisi za fedha nchini kuendelea kutoa mikopo yenye masharti nafuu na kubuni huduma za kifedha zinazokidhi mahitaji ya wafugaji, hususan wanawake na vijana, ili waweze kuwekeza katika sekta hii.

Pamoja na ufunguzi wa paredi ya mifugo, Mhe. Kikwete amezindua rasmi kituo cha huduma kwa wateja cha Wizara ya Kilimo na Uvuvi ambacho kitakuwa mahususi kwa ajili ya kutoa nakupokea taarifa za Kilimo na Uvuvi.

Amewataka watumishi watakaokuwa katika kituo hicho kupokea na kujibu hoja za wakulima, wafugaji na wavuvi kwa wakati ili kurahisisha zoezi la uzalishaji na uuzaji wa bidhaa za kilimo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akihotubia Wadau wa Sekta ya Mifugo na Uvuvi na wananchi (Hawapo Pichani) katika Siku ya Mifugo iliyofanyika katika viwanja vya nanenane kwenye sikukuu ya wakulima (nanenane) Agosti 05, 2026.

Mkuu wa Wilaya ya Singida Mjini Bw. Godwin Gondwe ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Singida katika maonesho ya sikukuu ya Mkulima (nanenane) akisikiliza hotuba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – UTUMISHI Mhe. Kikwete (hayupo pichani) Agosti 05, 2026 katika viwanja vya nanenane 

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Damas Kamani akizungumza na Wadau wa Sekta ya Mifugo na Uvuvi na wananchi (Hawapo Pichani) katika Siku ya Mifugo iliyofanyika katika viwanja vya nanenane kwenye sikukuu ya wakulima (nanenane) Agosti 05, 2026. Aidha Mgeni Rasmi katika Siku hiyo alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (Hayupo Pichani)

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete alipowasili katika viwanja vya nanenane kwa ajili ya kufungua kwa paredi ya mifugo Agosti 05, 2026 Jijini Dodoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete alipotembelea banda la Sekretariati ya Ajira katika maonesho ya nanenane katika viwanja vya malecela vilivyopo Nzuguni Dodoma


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akikata utepe baada ya kuzindua rasmi kituo cha huduma wa mteja kutoka Wizara ya Uvuvi na Mifugo katika Viwanja vya nanenane wakati wa maadhimisho ya sikukuu ya wakulima Agosti 05, 2026


Sehemu ya Wadau wa sekta ya uvuvi na mifugo wakisikiliza hotuba kutoka kwa Waziri Wa Nchi Ofisi ya Rais – UTUMISHI Mhe. Ridhiwani Kikwete (ayupo pichani) wakati wa Ufunguzi wa Paredi ya Mifugo katika viwanja vya nanenane Jijini Dodoma 





Wednesday, August 5, 2026

MHESHIMIWA KIKWETE AONGOZA MAPOKEZI YA NAIBU KATIBU MKUU, OFISI YA RAIS – UTUMISHI BI. PRISCA LWANGILI

 Na. Mwandishi Wetu-Dodoma

Tarehe 5 Agosti, 2026.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameongoza mapokezi ya Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bi. Prisca Lwangili aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan baada ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi kustaafu Utumishi wa Umma.

Bi. Prisca Lwangili, amepokelewa rasmi leo na Viongozi na Watumishi wa ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma.

Akizungumza wakati wa mapokezi hayo, Mheshimiwa Kikwete amemkaribisha Bi. Lwangili na kumsihi kutumia uzoefu wake katika kazi kwa lengo la kuimarisha utekelezaji wa majukumu ya ofisi hiyo ili kuongeza uwajibikaji katika kuhudumia wananchi kwa ustawi wa Taifa

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Ofisi hiyo, Mheshimiwa Regina Qwaray, amemkaribisha Bi. Lwangili na kueleza kuwa Viongozi pamoja na Watumishi wa Ofisi hiyo wapo tayari kumpa ushirikiano katika kutekeleza majukumu yake mapya, ili kuimarisha utendaji wa ofisi kwa manufaa ya umma.

Naye Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Juma Mkomi, amesema uongozi na watumishi wa Ofisi hiyo wako tayari kushirikiana kwa karibu na Naibu Katibu Mkuu huyo ili kuhakikisha majukumu ya Ofisi yanatekelezwa kwa ufanisi na kufikia malengo yaliyowekwa na Serikali.

Kwa upande wake, Bi. Lwangili amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumteua katika nafasi hiyo ambapo ameahidi kutekeleza majukumu yake kwa kujituma na kuongeza ubunifu ili kuhakikisha malengo ya ofisi hiyo yanafikiwa kwa manufaa ya Serikali na wananchi.

Aidha, ameishukuru ofisi hiyo kwa mapokezi aliyopata na kuahidi kufanya kazi kwa ufanisi katika kuwahudumia Wananchi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa ofisi hiyo mara baada ya kumpokea Naibu Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bi. Prisca Lwangili (hayupo pichani) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan baada ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi kustaafu Utumishi wa Umma.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili (kushoto) akipokea ua la ukaribisho mara baada ya kuwasili rasmi katika ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma baada ya kuteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan. Kulia ni Mtumishi wa ofisi hiyo Bi. Subira Swallah.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bi. Prisca Lwangili (kushoto) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan baada ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi kustaafu Utumishi wa Umma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya kumpokea Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bi. Prisca Lwangili (hayupo pichani) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan kabla ya kuwasili katika ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakisubiri kumpokea Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bi. Prisca Lwangili (hayupo pichani) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan kabla ya kuwasili katika ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma.

Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifurahia jambo wakati wakisubiri kumpokea Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bi. Prisca Lwangili (hayupo pichani) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan baada ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi kustaafu Utumishi wa Umma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakisubiri kumpokea Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bi. Prisca Lwangili (hayupo pichani) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan kabla ya kuwasili katika ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (katikati) akizungumza jambo na Katibu Mkuu wa ofisi hiyo, Bw. Juma Mkomi (kulia) wakati wakisubiri kumpokea Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bi. Prisca Lwangili (hayupo pichani) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa ofisi hiyo Bw. Musa Magufuli.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili akisaini kitabu cha wageni alipowasili rasmi katika ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma baada ya kuteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan.



Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili (kulia) akitoa neno la shukrani baada ya kuwasili rasmi katika ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma baada ya kuteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa pili kutoka kushoto mstari wa kwanza) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Wakurugenzi wa Idara na Vitengo wa ofisi hiyo mara baada ya kumpokea Naibu Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bi. Priscar Lwangili (wa kwanza kulia mstari wa mbele) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan baada ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi kustaafu Utumishi wa Umma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akisalimiana na kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bi. Prisca Lwangili (kushoto) aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan baada ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi kustaafu Utumishi wa Umma.

MHESHIMIWA RIDHIWANI KIKWETE AONGOZA ZOEZI LA KUMPOKEA NAIBU KATIBU MKUU WA OFISI HIYO BI. PRISCA LWANGILI

HABARI KATIKA PICHA

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA, MHE. RIDHIWANI KIKWETE AONGOZA ZOEZI LA KUMPOKEA NAIBU KATIBU MKUU WA OFISI HIYO BI. PRISCA LWANGILI AMBAYE ALITEULIWA HIVI KARIBUNI NA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN MARA BAADA YA ALIYEKUWA NAIBU KATIBU MKUU WA OFISI HIYO BW. XAVIER DAUDI KUSTAAFU UTUMISHI WA UMMA.