Na Eric Amani, Dodoma
Timu ya Utumishi Sports Club (UTUMISHI SC)
imeendelea kuonyesha kiwango kizuri baada ya kupata ushindi mnono wa mabao 4-0
dhidi ya Mkonze Veterans katika mchezo wa kirafiki wa soka uliochezwa leo
Septemba 05, 2026 katika uwanja wa John Merlin Jijini Dodoma.
UTUMISHI SC ilitawala mchezo kwa kiasi kikubwa,
ikionyesha umakini, nidhamu na ushirikiano mzuri wa kikosi katika maeneo yote
ya uwanja. Ushindi huo unaongeza morali kwa timu huku ukiendelea kujenga
maandalizi na ushindani kuelekea mashindano ya SHIMIWI 2026 Mkoani Kilimanjaro.
Uongozi na wachezaji wa UTUMISHI SC wameendelea
kuhimizana kuzingatia maadili ya Utumishi wa Umma ndani na nje ya Viwanja kuwa nidhamu,
upendo, mshikamano na kujituma katika kila mchezo, kwa lengo la kuiweka timu
katika kiwango bora zaidi ili kuelekea kutetea ubingwa walioutwaa katika
mashindano ya SHIMIWI kwa mwaka 2025 ambayo yalifanyika Jijini Mwanza
























