Wednesday, September 2, 2026

TRAMPA YAWASILISHA RIPOTI YA MAANDALIZI YA MKUTANO MKUU WA 14 WA CHAMA HICHO KWA WAZIRI MHE. RIDHIWANI KIKWETI


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Viongozi wa TRAMPA waliofika ofisini kwake kwa ajili ya kuwasilisha ripoti ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 14 wa chama hicho utakaofanyika Jijini Dodoma tarehe 21-25 Septemba, 2026. Aliyesimama ni Mwenyekiti wa TRAMPA Bi. Devota Mrope.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akipokea ripoti ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 14 wa TRAMPA utakaofanyika Jijini Dodoma kutoka kwa Mwenyekiti wa TRAMPA Bi. Devota Mrope. Zoezi hilo limefanyika ofisini kwake Mtumba Jijini Dodoma Septemba 1, 2026.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Viongozi wa TRAMPA mara baada ya kupoke ripoti ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 14 wa TRAMPA utakaofanyika Jijini Dodoma tarehe 21-25 Septemba, 2026.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wakurugenzi wa Ofisi yake na Viongozi wa TRAMPA mara baada ya kupoke ripoti ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 14 wa TRAMPA utakaofanyika Jijini Dodoma tarehe 21-25 Septemba, 2026.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Viongozi wa TRAMPA (hawapo pichani) mara baada ya kupoke ripoti ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 14 wa TRAMPA utakaofanyika Jijini Dodoma tarehe 21-25 Septemba, 2026.

Tuesday, September 1, 2026

KATIBU MKUU MKOMI AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU YA UFUATILIAJI NA TATHIMINI

 Na Eric Amani, Dodoma

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma Mkomi ameongoza Kikao cha Kamati Kuu ya Ufuatiliaji na Tathmini kilichojadili Taaifa ya Ufuatiliaji wa Utekelezaji wa Majukumu ya Ofisi ya Rais – Utumishi kwa Robo ya Nne ya Mwaka wa Fedha 2025/2026.

Kikao hicho kimefanyika leo Septemba 01, 2026 katika ukumbi wa Nyaraka Jijini Dodoma kwa lengo la kupitia na kutathmini kiwango cha utekelezaji wa majukumu, mipango, shughuli na malengo yaliyowekwa na Ofisi katika kipindi cha robo ya nne ya mwaka wa fedha 2025/2026.

Akizungumza wakati wa kikao hicho, Bw. Mkomi amesisitiza umuhimu wa ufuatiliaji na tathmini katika kuhakikisha kuwa mipango na shughuli za Ofisi zinatekelezwa kwa ufanisi, kwa wakati na kwa kuzingatia viashiria vya utendaji vilivyowekwa.

Amesema ufuatiliaji na tathmini ni nyenzo muhimu katika kupima matokeo ya utekelezaji wa mipango ya Serikali, kutambua maeneo yanayohitaji maboresho na kuwezesha uongozi kufanya maamuzi yanayozingatia ushahidi.

“Ni muhimu taarifa za ufuatiliaji na tathmini zisitumike tu kwa ajili ya kuonesha kiwango cha utekelezaji, bali pia ziwe msingi wa kufanya maboresho na kuchukua hatua stahiki pale ambapo utekelezaji haujafikia malengo yaliyokusudiwa,” amesema Bw. Mkomi.

Katika hatua nyingine, amewataka viongozi na watendaji wa Ofisi kuhakikisha utekelezaji wa majukumu yao unaendana na mipango na vipaumbele vilivyowekwa, huku wakizingatia matumizi bora ya rasilimali, uwajibikaji na utoaji wa huduma zenye tija kwa wananchi.

Pamoja na mambo mengine, kamati pia imejadili maeneo yanayohitaji kuimarishwa katika kipindi kijacho, ikiwemo kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa mipango, kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa shughuli na kuhakikisha taarifa za utendaji zinawasilishwa kwa wakati na kwa kuzingatia viashiria vilivyowekwa.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akizungumza na viongozi mbalimbali wa Ofisi ya Rais – UTUMISHI wakati wa Kikao cha Kamati Kuu ya Ufuatiliaji na Tathmini katika Ukumbi wa Nyaraka Jijini Dodoma Agosti 1, 2026


Baadhi ya Wakurugenzi kutokea Ofisi ya Rais – UTUMISHI wakifatilia Kikao cha Kamati Kuu ya Ufuatiliaji na Tathmini katika Ukumbi wa Nyaraka Jijini Dodoma Agosti 1, 2026


Viongozi Mbalimbali kutokea Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (Aliyeshikilia Mic) wakati wa Kikao cha Kamati Kuu ya Ufuatiliaji na Tathmini Septemba 1, 2026 Jijini Dodoma



Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma Bw. Nolasco J. Kipanda akifatilia Kikao cha Kamati Kuu ya Ufuatiliaji na Tathmini kinacho ratibiwa na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Septemba 1, 2026 katika Ukumbi wa Nyaraka uliyopo Jijini Dodoma


Meneja Mipango na Maendeleo Bi. Mwanaidi Mdee kutokea Chuo Cha Utumishi wa Umma (TPSC) akiwasilisha mada katika Kikao cha Kamati Kuu ya Ufuatiliaji na Tathmini Septemba 1, 2026 


Monday, August 31, 2026

NAIBU KATIBU MKUU LWANGILI AWATAKIA KHERI NA BARAKA WATUMISHI WALIOZALIWA MWEZI AGOSTI HUKU AKIWASISITIZA KUWATUMIKIA WANANCHI KWA UFASAHA

Na Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 31 Agosti, 2026

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili, ameungana na Menejimenti na Watumishi wa Ofisi hiyo kuwatakia kheri na baraka Watumishi waliozaliwa mwezi Agosti, katika kumbukizi ya siku zao za kuzaliwa huku akiwasisitiza kuwatumikia wananchi kwa ufasaha.

Bi. Lwangili ametoa pongezi hizo leo tarehe 31 Agosti, 2026 mara baada ya kuhitimisha mafunzo yaliyohusu Taratibu za Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu yaliyotolewa katika eneo maalumu la Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mtumba Jijini Dodoma

Ametumia fursa hiyo kuwashukuru Watumishi hao kwa kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa kujituma, uadilifu na kuzingatia uwajibikaji katika utumishi.

Amewatakia Watumishi hao afya njema, furaha na mafanikio katika maisha yao, huku akiwahimiza kuendelea kumshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai na nafasi ya kuwatumikia wananchi.

Aidha, amewaombea Mungu awabariki, awaongoze na awatimizie kila jambo jema alilolipanga kuwapa Mwenyezi Mungu katika maisha yao, huku akiwatakia maisha yenye amani, furaha, upendo na mafanikio.