Monday, August 31, 2026

NAIBU KATIBU MKUU LWANGILI AWATAKIA KHERI NA BARAKA WATUMISHI WALIOZALIWA MWEZI AGOSTI HUKU AKIWASISITIZA KUWATUMIKIA WANANCHI KWA UFASAHA

Na Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 31 Agosti, 2026

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili, ameungana na Menejimenti na Watumishi wa Ofisi hiyo kuwatakia kheri na baraka Watumishi waliozaliwa mwezi Agosti, katika kumbukizi ya siku zao za kuzaliwa huku akiwasisitiza kuwatumikia wananchi kwa ufasaha.

Bi. Lwangili ametoa pongezi hizo leo tarehe 31 Agosti, 2026 mara baada ya kuhitimisha mafunzo yaliyohusu Taratibu za Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu yaliyotolewa katika eneo maalumu la Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mtumba Jijini Dodoma

Ametumia fursa hiyo kuwashukuru Watumishi hao kwa kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa kujituma, uadilifu na kuzingatia uwajibikaji katika utumishi.

Amewatakia Watumishi hao afya njema, furaha na mafanikio katika maisha yao, huku akiwahimiza kuendelea kumshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai na nafasi ya kuwatumikia wananchi.

Aidha, amewaombea Mungu awabariki, awaongoze na awatimizie kila jambo jema alilolipanga kuwapa Mwenyezi Mungu katika maisha yao, huku akiwatakia maisha yenye amani, furaha, upendo na mafanikio.









NAIBU KATIBU MKUU LWANGILI ASISITIZA UZINGATIAJI WA SHERIA KATIKA USHUGHULIKIAJI WA MASHAURI YA NIDHAMU KATIKA UTUMISHI WA UMMA

Na Antonia Mbwambo – Dodoma

Tarehe 31 Agosti, 2026

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili, amesisitiza umuhimu wa kuzingatia Sheria, Taratibu na Kanuni katika kushughulikia mashauri ya nidhamu katika Utumishi wa Umma, akieleza kuwa uzingatiaji wa misingi hiyo ni muhimu katika kuhakikisha haki inatendeka.

Bi. Lwangili ameyasema hayo leo, tarehe 31 Agosti, 2026, wakati akihitimisha mafunzo ya uelewa kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI yaliyofanyika katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma.

Bi. Lwangili amesema katika kushughulikia masuala ya nidhamu ni muhimu kuhakikisha kuwa thamani na utu wa mtu vinalindwa, huku hatua zote zikichukuliwa kwa kuzingatia Sheria, Taratibu na Kanuni zilizowekwa.

“Ni muhimu kuhakikisha kuwa katika kushughulikia mashauri ya nidhamu, Sheria, Taratibu na Kanuni zinafuatwa ili haki itendeke, huku tukilinda thamani na utu wa mtu, amesema Bi. Lwangili.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuwakumbusha Watumishi wa Umma kuhusu madhara ya kutokuzingatia Sheria, Taratibu na Kanuni katika utekelezaji wa majukumu yao, akieleza kuwa uelewa huo utasaidia kupunguza makosa na kuwaepusha watumishi na changamoto ya kufikishwa katika mashauri ya kinidhamu.

Kwa upande wake mwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye ni  Afisa Sheria Mwandamizi, kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Edwin Bilikundi, amesema usimamizi wa nidhamu katika Utumishi wa Umma umejengwa katika dhana mbili kuu ambazo ni kurekebisha mwenendo wa Mtumishi (corrective measures) na utoaji wa adhabu (sanction approach). Amesema njia ya kurekebisha inalenga kumsaidia Mtumishi kutambua kosa na kujirekebisha, wakati utoaji wa adhabu hutumika pale kosa linapothibitika, hususan kwa makosa yanayojirudia au yenye uzito.

Bw. Bilikundi ameongeza kuwa mchakato wa kinidhamu unapaswa kuanza kwa uchunguzi wa awali unaolenga kubaini ukweli na uzito wa tuhuma, pamoja na kuamua hatua stahiki za kuchukua.

Amesisitiza kuwa uzingatiaji wa hatua na muda uliowekwa katika Sheria, Kanuni na Taratibu ni muhimu katika kuhakikisha mchakato wa nidhamu unakuwa wa haki na wenye msingi sahihi wa kisheria.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili akizungumza na Watumishi wa Ofisi hiyo (hawapo pichani) wakati Naibu Katibu Mkuu huyo akihitimisha mafunzo yaliyolenga kuwajengea Watumishi hao uelewa kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu katika Utumishi wa Umma, yaliyofanyika tarehe 31 Agosti, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo, Mtumba, jijini Dodoma.

Baadhi ya Wakurugenzi na Watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji leo tarehe 31 Agosti, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma

Afisa Sheria Mwandamizi, kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Edwin Bilikundi akiendesha mafunzo ya uelewa kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu katika Utumishi wa Umma kwa Watumishi wa Ofisi hiyo leo tarehe 31 Agosti 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo, Mtumba, jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Musa Magufuli akisisitiza jambo wakati wa mafunzo ya uelewa kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu katika Utumishi wa Umma Mtumba Jijini Dodoma


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili  akisisitiza jambo wakati akihitimisha mafunzo ya kuwajengea Watumishi hao uelewa kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu katika Utumishi wa Umma, yaliyofanyika tarehe 31 Agosti, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo, Mtumba, jijini Dodoma

Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji leo tarehe 31 Agosti, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma

Baadhi ya Wakurugenzi na Watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji leo tarehe 31 Agosti, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma

Baadhi ya Wakurugenzi na Watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji leo tarehe 31 Agosti, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili (wa pili kutoka kushoto) akifurahia jambo wakati alipokuwa akifuatilia mafunzo kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu katika Utumishi wa Umma leo Agosti 31, 2026 Mtumba Jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, SACP. Ibrahim Mahumi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI akisisitiza jambo wakati wa mafunzo ya uelewa kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu katika Utumishi wa Umma Mtumba Jijini Dodoma




 

Thursday, August 27, 2026

 WAZIRI KIKWETE: SOMALIA IMEKUJA KUJIFUNZA MAFANIKIO YA  MATUMIZI YA MIFUMO YA KIDIJITARI KATIKA UTUMISHI WA UMMA  NCHINI TANZANIA

 Na Lusungu Helela, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete, amesema uamuzi wa Serikali ya Somalia kumtuma Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma nchini Tanzania ni ishara ya kutambua mafanikio yaliyofikiwa na Tanzania katika eneo la matumizi ya mifumo katika masuala ya Utumishi wa Umma nchini.

Kikwete amesema hayo leo jijini Dodoma wakati akizungumza na ujumbe wa Serikali ya Somalia unaoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Hirsi  Ganni, uliofika nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu.

Amesema ujio wa ujumbe huo unaonyesha kuwa Somalia inatambua na kuthamini uzoefu wa Tanzania katika uendeshaji wa Serikali, utumishi wa umma na matumizi ya mifumo ya kidijitali katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

“Ukiona wenzako wanakufuata hasa katika eneo hili ambalo sisi ni watoa huduma, ni wazi kuwa huduma tunayotoa wapo wenzetu wanatambua na kuthamini tunachokifanya na ndiyo maana wameamua kuja kujifunza na kupata uzoefu,” amesema Mhe. Kikwete

Amesema anaamini uzoefu ambao Somalia itaupata kupitia ziara hiyo utasaidia kuboresha zaidi masuala ya utumishi wa umma nchini humo.

Mhe. Kikwete amesema ujumbe huo unapata fursa ya kujifunza maeneo mbalimbali, ikiwemo namna Serikali inavyohusiana na wananchi, uratibu wa masuala ya kazi na ajira, usalama wa wafanyakazi mahali pa kazi pamoja na mifumo ya pensheni kwa watumishi wanaostaafu katika taasisi za Serikali na sekta binafsi.

“Hii ziara ni kielelezo tosha kuwa Somalia imedhamiria, ndiyo maana haijaweza kutuma maafisa pekee, lakini Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma ameamua kuja mwenyewe na timu yake kwa lengo la kujifunza na kuja kuona kwa macho yake kazi kubwa iliyofanyika Tanzania,” amesisitiza Mhe. Kikwete

Kwa upande wake, Mhe. Hirsi Ganni amesema ujumbe wake umefika Tanzania kujifunza namna Tanzania ilivyofanikiwa katika masuala ya utumishi wa umma, hususan matumizi ya mifumo ya kidijitali katika kuboresha utoaji wa huduma.

Amesema Tanzania imekuwa ikifanya vizuri katika utoaji wa huduma kwa wananchi, huku watumishi wa umma wakitumia mifumo ya kidijitali kuwahudumia wananchi na kuhakikisha wanapata haki zao.

Mhe. Ganni amesema ujio wao ni muhimu kutokana na hatua ambazo Tanzania imepiga katika kuboresha utendaji wa Serikali na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Amesema wamevutiwa pia na namna mifumo ya Serikali inavyowawezesha watumishi kuwahudumia wananchi kwa ufanisi.

Akizungumzia mfumo wa e-Mrejesho,  Mhe. Ganni amesema ni miongoni mwa mifumo waliyoona ina umuhimu katika kuimarisha mawasiliano kati ya Serikali na wananchi, hivyo wanatarajia kujifunza namna unavyofanya kazi na uwezekano wa kutumia uzoefu huo katika kuboresha huduma nchini Somalia.

Ziara hiyo ya ujumbe wa Somalia inalenga pia kujifunza kuhusu mifumo ya Baraza la Mawaziri, usimamizi wa rasilimali watu, uajiri kwa kuzingatia sifa, Serikali mtandao, usimamizi wa ajira na mifumo ya taarifa za soko la ajira.

Ujumbe huo pia unatarajiwa kutembelea Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Kazi, Ajira na Mahusiano pamoja na Jiji la Serikali jijini Dodoma, kwa ajili ya kujionea namna shughuli za Serikali zinavyoratibiwa na kutekelezwa.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kikao na  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Mhe. Hirsi  Ganni,leo jijini Dodoma akioongoza  ujumbe wa Serikali ya Somalia, uliofika nchini kwa ziara ya siku tatu kwa lengo la kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo suala la matumizi ya mifumo ya kidigitali katika masuala ya utumishi wa umma nchini

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete akimkabidhi zawadi ya mfano wa mlango ambao unapatikana Zanzibar Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Mhe. Hirsi  Ganni,leo jijini Dodoma mara baada ya kikao na ujumbe wa Serikali ya Somalia unaoongozwa na Waziri huyo, uliofika nchini kwa ziara ya siku tatu kwa lengo la kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo suala la matumizi ya mifumo ya kidigitali katika masuala ya utumishi wa umma nchini

Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete kuzungumza kwenye kikao na  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Mhe. Hirsi  Ganni,leo jijini Dodoma akioongoza  ujumbe wa Serikali ya Somalia, uliofika nchini kwa ziara ya siku tatu kwa lengo la kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo suala la matumizi ya mifumo ya kidigitali katika masuala ya utumishi wa umma nchini


Baadhi ya Viongozi mbalimbali wakiwemo Wakurugenzi, Wataalamu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete kwenye kikao na  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Mhe. Hirsi  Ganni,leo jijini Dodoma akioongoza  ujumbe wa Serikali ya Somalia, uliofika nchini kwa ziara ya siku tatu kwa lengo la kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo suala la matumizi ya mifumo ya kidigitali katika masuala ya utumishi wa umma nchini

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Mhe. Hirsi  Ganni akizungumza kwenye kikao,leo jijini Dodoma akioongoza  ujumbe wa Serikali ya Somalia, uliofika nchini kwa ziara ya siku tatu kwa lengo la kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo suala la matumizi ya mifumo ya kidigitali katika masuala ya utumishi wa umma nchini mara baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete kufungua kikao hicho.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete akiwa kwenye picha ya pamoja  na  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Mhe.Hirsi Ganni,leo jijini Dodoma wakiwa pamoja na viongozi na wataalamu mbalimbali mara baada ya kikao cha  ujumbe wa Serikali ya Somalia, uliofika nchini kwa ziara ya siku tatu kwa lengo la kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo suala la matumizi ya mifumo ya kidigitali katika masuala ya utumishi wa umma nchini