Na Eric Amani, Dodoma
Ofisi
ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala na Utawala Bora kwa
kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni
(UNESCO), imeandaa programu maalum ya kuwajengea uwezo Watumishi wa Umma kuhusu
matumizi ya Akili Unde (Artificial Intelligence – AI)
Hayo
yamebainishwa leo Septemba 9, 2026 Mtumba jijini Dodoma na Kaimu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais -UTUMISHI, Bi.
Leila Mavika wakati wa kikao kazi
na wadau wa UNESCO katika kuboresha utendaji kazi na utoaji wa huduma bora kwa
wananchi.
Amesema
programu hiyo inalenga kuongeza uelewa na ujuzi wa Watumishi wa Umma kuhusu
matumizi sahihi na yenye tija ya Akili Unde katika mazingira ya kazi, pamoja na
kuwawezesha kutumia teknolojia hiyo katika kuongeza ufanisi, ubunifu na tija
katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.
Bi.
Mavika amesema programu hiyo inatekelezwa ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa
mapendekezo na maazimio yaliyotokana na Mkutano wa UNESCO wa mwaka 2025 kuhusu
masuala ya elimu ya Akili Unde na mabadiliko ya kidijitali.
Amesema
maendeleo ya teknolojia hiyo yanatoa fursa kwa Taasisi za Serikali kurahisisha
mchakato wa
kiutendaji, kuimarisha uchambuzi wa taarifa na kuboresha utoaji wa huduma kwa
wananchi.
“Matumizi
ya Akili Unde yanapaswa kuzingatia usalama wa taarifa, faragha, maadili, Sheria, Kanuni na Taratibu za Utumishi wa Umma,”
amesema Bi. Mavika.
Ameongeza
kuwa ushirikiano kati ya Ofisi ya Rais–UTUMISHI na UNESCO unalenga kujenga
Watumishi wa Umma wenye ujuzi na uwezo wa kukabiliana na mabadiliko ya
kiteknolojia na kutumia Akili Unde kwa uwajibikaji.
Programu
hiyo inatarajiwa kuongeza tija na ufanisi katika Utumishi wa Umma na kuimarisha
utoaji wa huduma bora kwa wananchi.
![]() |
Kaimu
Katibu Mkuu wa Ofisi
ya Rais -UTUMISHI, Bi. Leila Mavika wakati wa
kikao kazi
na wadau wa UNESCO katika kuboresha utendaji kazi na utoaji wa huduma bora kwa
wananchi Leo Septemba 9, 2026
![]() |
Mkurugenzi wa Mawasiliano Serikalini Bi. Mary Mwakapenda
akimsikiliza Kaimu
Katibu Mkuu wa Ofisi
ya Rais -UTUMISHI,
Bi. Leila Mavika (hayupo pichani) wakati wa kikao kazi Mtumba Dodoma. |
![]() |
Picha
ya pamoja ya Kaimu Katibu Mkuu Bi Leila Mavika (Katikati) na baadhi ya viongozi
kutokea shirika la UNESCO na Wizara ya Mawasiliano leo Septemba 9, 2026 |











