Na. Veronica Mwafisi-Dodoma
Tarehe 14 Agosti, 2026
Bunge ya Utawala, Katiba na
Sheria imepokea taarifa kuhusu
hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi
cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III) na kutoa maelekezo ya
kuendeleza misingi ya
utekelezaji wenye ufanisi, uwazi na uwajibikaji katika kufikia walengwa
waliokusudiwa na kutimiza malengo ya PSSN III.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amezungumza hayo leo tarehe
14 Agosti, 2026 Bungeni jijini Dodoma alipokuwa akiongoza kikao cha Kamati yake
na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kilicholenga kupokea taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za
utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).
Vilevile, Mhe. Dkt. Ndumbaro ameipongeza TASAF kwa utekelezaji mzuri wa Miradi
ya Maendeleo ikiwemo ujenzi kwenye sekta ya elimu na afya.
“Kwa niaba ya Kamati yangu nitoe pongezi nyingi
kwa ofisi hii, kwa hakika mnafanya kazi nzuri katika mpango wa kunusuru kaya maskini, lakini pia mnatekeleza
vizuri Miradi ya Maendeleo ikiwemo ujenzi kwenye sekta ya elimu na afya, mnamwakilisha
vizuri Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika utekelezaji wa miradi hii’’
Amesema Mhe. Dkt. Ndumbaro
Awali akiwasilisha kwa Kamati hiyo taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za
utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III),
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina
Qwaray amesema, PSSN III iliidhinishwa na Serikali ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania na Benki ya Dunia tarehe 10 Aprili 2026, na kwa sasa
ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha maandalizi kabla ya kuanza
utekelezaji.
Naibu Waziri Qwaray amesema kuwa, katika maandalizi ya utekelezaji
wa PSSN III, hatua muhimu zimekamilika ikiwemo kukamilisha usanifu wa Mpango,
kuandaa nyaraka mbalimbali za utekelezaji, miongozo ya kiutendaji na kuimarisha
mifumo ya TEHAMA inayosimamia shughuli za Mpango.
Aidha ameongeza kuwa, mchakato wa utambuzi wa Mamlaka za Maeneo ya
Utekelezaji yatakayoshiriki kwenye utekelezaji wa Mpango unaendelea na
unaojumuisha timu ya wataalamu kutoka TASAF, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS),
Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar (OCGS), pamoja na wataalamu wa
mazingira ambapo uchambuzi na uchakataji huo utazingatia viwango vya umaskini
katika ngazi ya Halmashauri pamoja na viashiria vya athari za kimazingira,
ikiwemo uwezekano wa maeneo kuathiriwa na mabadiliko ya tabianchi na majanga
mbalimbali.
Vilevile, Mhe. Qwaray amesema kupitia mpango huo
unatarajiwa kuongeza uwezo wa kaya maskini na zilizo
katika mazingira hatarishi kukabiliana na changamoto za kiuchumi, kijamii na
kimazingira, kuongeza ujuzi na taaluma kwa vijana kutoka kaya maskini na
zinazoishi katika mazingira hatarishi zitakazoweza kujiajiri na kuajiriwa, kuwa
na masijala ya kitaifa (kanzi data) yenye taarifa muhimu ya kaya maskini na
zilizopo katika mazingira hatarishi pamoja na urasimishwaji wa TASAF kama
taasisi ya umma ya kutekeleza na kusimamia utoaji wa huduma za msaada ya
kijamii itakayohakikisha uendelevu, ufanisi na uratibu wa utoaji wa huduma hizo
nchini.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii
(TASAF) Bw. Shedrack Mziray ameishukuru Kamati hiyo kwa maoni na ushauri
mbalimbali ambao wameutoa na kuahidi kufanyia
kazi ili kuimarisha na kuboresha utendaji kazi wa Taasisi hiyo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria,
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akisisitiza jambo wakati wa kikao cha Kamati yake kilichofanyika
Bungeni jijini Dodoma na Watendaji wa Ofisi ya
Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kilicholenga kupokea taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za
utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (aliyesimama kulia)
akiwasilisha kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge
ya Utawala, Katiba na Sheria taarifa kuhusu
hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi
cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III). Wengine ni Viongozi
na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akifurahia jambo wakati
wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge
ya Utawala, Katiba na Sheria na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za
utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).
Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bw.
Shedrack Mziray akisikiliza maoni kutoka kwa
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao
cha Kamati hiyo Bungeni jijini
Dodoma na Watendaji hao
kilicholenga kuwasilisha
taarifa kuhusu hatua ya
mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu
cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Nyamizi Mhoja akiwasilisha hoja kwa Naibu Waziri,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina
Qwaray (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo
kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za
utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).
Viongozi na Watendaji wa
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa katika
kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu
hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi
cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Sikudhani Chikambo akiwasilisha hoja kwa Naibu Waziri,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina
Qwaray (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo
kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za
utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akifafanua hoja Bungeni
jijini Dodoma wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba
na Sheria na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za
utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (kulia) akiteta jambo na Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (kushoto) wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).
Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (aliyesimama)
akifafanua hoja iliyowasilishwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba
na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo kilicholenga
kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya
mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu
cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).
Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bw.
Shedrack Mziray (kulia) akiandika maoni yaliyokuwa yakiwasilishwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kilicholenga kuwasilisha taarifa
kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi,
matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru
kaya maskini (PSSN III). Kushoto ni Mkurugenzi
wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, SACP. Ibrahim Mahumi.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (aliyesimama mbele)
akiwasilisha kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge
ya Utawala, Katiba na Sheria taarifa kuhusu
hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi
cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III). Wengine ni Viongozi
na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Saashisha Mafuwe akiwasilisha hoja kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Yohana Msita akiwasilisha hoja kwa Naibu Waziri,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina
Qwaray (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Kamati hiyo na ofisi hiyo
kilicholenga kuwasilisha taarifa
kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za
utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).
Sehemu ya Wakurugenzi na Maafisa kutoka
Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria,
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza kwenye kikao Bungeni jijini Dodoma mara baada ya Watendaji wa ofisi hiyo kuwasilisha
taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za
utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).
Sehemu ya Wakurugenzi Wasaidizi na Maafisa
kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria,
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza kwenye kikao Bungeni jijini Dodoma mara baada ya Watendaji wa ofisi hiyo kuwasilisha
taarifa kuhusu hatua ya mchakato wa maandalizi, matarajio na hatua za
utekelezaji wa kipindi cha tatu cha mpango wa kunusuru kaya maskini (PSSN III).















































