Thursday, August 27, 2026

 WAZIRI KIKWETE: SOMALIA IMEKUJA KUJIFUNZA MAFANIKIO YA  MATUMIZI YA MIFUMO YA KIDIJITARI KATIKA UTUMISHI WA UMMA  NCHINI TANZANIA

 Na Lusungu Helela, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete, amesema uamuzi wa Serikali ya Somalia kumtuma Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma nchini Tanzania ni ishara ya kutambua mafanikio yaliyofikiwa na Tanzania katika eneo la matumizi ya mifumo katika masuala ya Utumishi wa Umma nchini.

Kikwete amesema hayo leo jijini Dodoma wakati akizungumza na ujumbe wa Serikali ya Somalia unaoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Hirsi  Ganni, uliofika nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu.

Amesema ujio wa ujumbe huo unaonyesha kuwa Somalia inatambua na kuthamini uzoefu wa Tanzania katika uendeshaji wa Serikali, utumishi wa umma na matumizi ya mifumo ya kidijitali katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

“Ukiona wenzako wanakufuata hasa katika eneo hili ambalo sisi ni watoa huduma, ni wazi kuwa huduma tunayotoa wapo wenzetu wanatambua na kuthamini tunachokifanya na ndiyo maana wameamua kuja kujifunza na kupata uzoefu,” amesema Mhe. Kikwete

Amesema anaamini uzoefu ambao Somalia itaupata kupitia ziara hiyo utasaidia kuboresha zaidi masuala ya utumishi wa umma nchini humo.

Mhe. Kikwete amesema ujumbe huo unapata fursa ya kujifunza maeneo mbalimbali, ikiwemo namna Serikali inavyohusiana na wananchi, uratibu wa masuala ya kazi na ajira, usalama wa wafanyakazi mahali pa kazi pamoja na mifumo ya pensheni kwa watumishi wanaostaafu katika taasisi za Serikali na sekta binafsi.

“Hii ziara ni kielelezo tosha kuwa Somalia imedhamiria, ndiyo maana haijaweza kutuma maafisa pekee, lakini Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma ameamua kuja mwenyewe na timu yake kwa lengo la kujifunza na kuja kuona kwa macho yake kazi kubwa iliyofanyika Tanzania,” amesisitiza Mhe. Kikwete

Kwa upande wake, Mhe. Hirsi Ganni amesema ujumbe wake umefika Tanzania kujifunza namna Tanzania ilivyofanikiwa katika masuala ya utumishi wa umma, hususan matumizi ya mifumo ya kidijitali katika kuboresha utoaji wa huduma.

Amesema Tanzania imekuwa ikifanya vizuri katika utoaji wa huduma kwa wananchi, huku watumishi wa umma wakitumia mifumo ya kidijitali kuwahudumia wananchi na kuhakikisha wanapata haki zao.

Mhe. Ganni amesema ujio wao ni muhimu kutokana na hatua ambazo Tanzania imepiga katika kuboresha utendaji wa Serikali na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Amesema wamevutiwa pia na namna mifumo ya Serikali inavyowawezesha watumishi kuwahudumia wananchi kwa ufanisi.

Akizungumzia mfumo wa e-Mrejesho,  Mhe. Ganni amesema ni miongoni mwa mifumo waliyoona ina umuhimu katika kuimarisha mawasiliano kati ya Serikali na wananchi, hivyo wanatarajia kujifunza namna unavyofanya kazi na uwezekano wa kutumia uzoefu huo katika kuboresha huduma nchini Somalia.

Ziara hiyo ya ujumbe wa Somalia inalenga pia kujifunza kuhusu mifumo ya Baraza la Mawaziri, usimamizi wa rasilimali watu, uajiri kwa kuzingatia sifa, Serikali mtandao, usimamizi wa ajira na mifumo ya taarifa za soko la ajira.

Ujumbe huo pia unatarajiwa kutembelea Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Kazi, Ajira na Mahusiano pamoja na Jiji la Serikali jijini Dodoma, kwa ajili ya kujionea namna shughuli za Serikali zinavyoratibiwa na kutekelezwa.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kikao na  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Mhe. Hirsi  Ganni,leo jijini Dodoma akioongoza  ujumbe wa Serikali ya Somalia, uliofika nchini kwa ziara ya siku tatu kwa lengo la kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo suala la matumizi ya mifumo ya kidigitali katika masuala ya utumishi wa umma nchini

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete akimkabidhi zawadi ya mfano wa mlango ambao unapatikana Zanzibar Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Mhe. Hirsi  Ganni,leo jijini Dodoma mara baada ya kikao na ujumbe wa Serikali ya Somalia unaoongozwa na Waziri huyo, uliofika nchini kwa ziara ya siku tatu kwa lengo la kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo suala la matumizi ya mifumo ya kidigitali katika masuala ya utumishi wa umma nchini

Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete kuzungumza kwenye kikao na  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Mhe. Hirsi  Ganni,leo jijini Dodoma akioongoza  ujumbe wa Serikali ya Somalia, uliofika nchini kwa ziara ya siku tatu kwa lengo la kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo suala la matumizi ya mifumo ya kidigitali katika masuala ya utumishi wa umma nchini


Baadhi ya Viongozi mbalimbali wakiwemo Wakurugenzi, Wataalamu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete kwenye kikao na  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Mhe. Hirsi  Ganni,leo jijini Dodoma akioongoza  ujumbe wa Serikali ya Somalia, uliofika nchini kwa ziara ya siku tatu kwa lengo la kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo suala la matumizi ya mifumo ya kidigitali katika masuala ya utumishi wa umma nchini

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Mhe. Hirsi  Ganni akizungumza kwenye kikao,leo jijini Dodoma akioongoza  ujumbe wa Serikali ya Somalia, uliofika nchini kwa ziara ya siku tatu kwa lengo la kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo suala la matumizi ya mifumo ya kidigitali katika masuala ya utumishi wa umma nchini mara baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete kufungua kikao hicho.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhwani Kikwete akiwa kwenye picha ya pamoja  na  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Utumishi wa Umma, Mhe.Hirsi Ganni,leo jijini Dodoma wakiwa pamoja na viongozi na wataalamu mbalimbali mara baada ya kikao cha  ujumbe wa Serikali ya Somalia, uliofika nchini kwa ziara ya siku tatu kwa lengo la kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo suala la matumizi ya mifumo ya kidigitali katika masuala ya utumishi wa umma nchini




Sunday, August 23, 2026

TUZO YA RAIS WA AWAMU YA KWANZA NA MBEBA MAONO WA TAIFA LA TANZANIA, HAYATI MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE

Tuzo ya Rais wa Awamu ya Kwanza na mbeba maono wa Taifa la Tanzania, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kwa kutambua mchango wake katika kuasisi na kuwa na maono ya ujenzi wa Mradi wa Bwawa la Mwalimu Julius Nyerere.

Imepokelewa kwa niaba yake na   Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili.

Tuzo hii ni ishara ya heshima na kutambua mchango wake katika kuasisi maono ya Taifa ya kuwa ba umeme wa uhakika kwa maendeleo ya Tanzania.



TUZO YA RAIS WA AWAMU YA TATU, HAYATI BENJAMIN WILLIAM MKAPA

Tuzo ya Rais wa Awamu ya Tatu, Hayati Benjamin William Mkapa, kwa kutambua, mchango wake katika kuhakikisha utekelezaji wake wa Mradi wa Bwawa la Mwalimu Julius Nyerere.

Imepokelewa kwa niaba yake na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili.

Tuzo hii ni ishara ya heshima na kutambua mchango wake katika kutimiza maono ya Taifa ya kuwa na umeme wa uhakika kwa maendeleo ya Tanzania.