Na. Antonia Mbwambo na Helela Lusungu- Nyang’hwale -Geita
Tarehe 17 Septemba, 2026.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray,
amewataka Waajiri na Mamlaka za Ajira na Nidhamu kuhakikisha kuwa utekelezaji
wa majukumu ya kiutumishi unazingatia anuai za jamii na mahitaji ya makundi
mbalimbali bila ubaguzi, ili kujenga Utumishi wa Umma jumuishi na wenye usawa.
Mhe. Qwaray ametoa kauli hiyo leo, Septemba 17,
2026, wakati akizungumza na Watumishi wa Umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita,
katika ziara yenye lengo la kutembelea miradi ya maendeleo, kusikiliza
changamoto za Watumishi na kujadili namna ya kuboresha utendaji na utoaji wa
huduma.
Amesisitiza kuwa uzingatiaji wa anuai za jamii
unapaswa kuonekana katika utoaji wa huduma, usimamizi wa watumishi, upangaji wa
ajira, mazingira ya kazi na utekelezaji wa stahiki za watumishi.
“Waajiri
na Mamlaka za Ajira na Nidhamu wahakikishe kuwa utoaji wa huduma, usimamizi wa
Watumishi, upangaji wa ajira, mazingira ya kazi na utekelezaji wa stahiki
unazingatia mahitaji na tofauti za makundi mbalimbali ya jamii, bila ubaguzi,
ili kujenga Utumishi wa Umma jumuishi na wenye usawa,” amesema Mhe. Qwaray.
Aidha, Mhe. Qwaray amesema Tume ya Utumishi wa Umma inaendelea na ukaguzi wa utekelezaji wa sheria,
kanuni na taratibu za kiutumishi katika Taasisi za Umma, na kuwataka Waajiri na Mamlaka za
Ajira na Nidhamu kushirikiana kikamilifu, kurekebisha mapungufu yatakayobainika
na kutekeleza maelekezo ya Tume kwa wakati.
Kwa
upande wake, Katibu Tawala wa Wilaya ya Nyang’hwale, Bi.
Kaunga Amani,
amemshukuru Mhe. Qwaray kwa kutembelea miradi ya maendeleo na kukutana na
watumishi ili kusikiliza changamoto zao. Amesema Halmashauri imepokea maelekezo
yaliyotolewa na itaendelea kuyatekeleza ili kuboresha utendaji na utoaji wa
huduma kwa wananchi.
Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale (hawapo pichani) leo tarehe 17 Septemba 2026 wakati Naibu Waziri huyo alipokuwa katika ziara iliyolenga kutembelea miradi ya maendeleo, kusikiliza changamoto za Watumishi na kujadili namna ya kuboresha utendaji na utoaji wa huduma
Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray, akisalimiana na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale mara baada ya Naibu Waziri huyo kuwasili katika Ofisi hiyo katika ziara ya kikazi leo tarehe 17 Septemba, 2026 Mkoani Geita
Naibu Waziri,Ofisi ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina
Qwaray akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Mkuu
wa Wilaya ya Nyang’hwale katika ziara ya
kikazi Mkoani Geita
Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya
Wilaya ya Nyang’hwale Bi. Husna Toni wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri
huyo Mkoani Geita
Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale Bi. Grace Kingalame akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ,Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) kuzungumza na Watumishi wa Wilaya hiyo Mkoani Geita.
Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiwa katika picha ya
pamoja na Wakuu wa shule wa Halmashauri
ya Wilaya ya Nyang’hwale mara baada ya Naibu Waziri huyo kuzungumza na
Watumishi katika ziara yake ya kikazi Mkoani Geita
Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiagana na Watumishi na Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale mara baada ya Naibu Waziri huyo kuhiytimisha ziara ya kikazi leo tarehe 17 Septemba, 2026 Mkoani Geita
Mtumishi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale akiuliza swali kwa
Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Mhe. Regina Qwaray, wakati Naibu Waziri huyo alipokuwa akipokea
changamoto mbalimbali kutoka kwa Watumishi hao Septemba 17, 2026 Mkoani Geita
Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Nyang'hwale mara baada ya Naibu Waziri huyo kuzungumza na Watumishi leo tarehe 17 Septemba, 2026 Mkoani Geita
Watumishi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale wakimsikiliza Naibu Waziri,Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo
pichani) wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Geita














