Friday, August 21, 2026

WAZIRI KIKWETE: SERIKALI YAONGEZA TAASISI ZINAZOKAGULIWA KUHUSU UZINGATIAJI WA SHERIA KATIKA UTUMISHI WA UMMA ILI KUIMARISHA UWAJIBIKAJI

Na Lusungu Helela, Morogoro

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, amesema Serikali imeongeza idadi ya taasisi zitakazokaguliwa kuhusu uzingatiaji wa sheria katika usimamizi wa utumishi wa umma kutoka 160 mwaka 2025/26 hadi 300 mwaka 2026/27

Mhe. Kikwete ametoa kauli hiyo leo, Ijumaa, Agosti 21, 2026, mkoani Morogoro, wakati akizungumza na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, mara baada ya kuzindua zoezi la ukaguzi katika halmashauri hiyo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.

Amesema hatua hiyo inaonesha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuimarisha uadilifu, uwajibikaji na utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Amesema ukaguzi huo unafanyika kwa mujibu wa Kifungu cha 12(1)(c) cha Sheria ya Utumishi wa Umma, Sura ya 298, Marejeo ya Mwaka 2023, kwa lengo la kufuatilia na kutathmini kiwango cha uzingatiaji wa sheria, kanuni, taratibu na miongozo katika usimamizi wa masuala ya kiutumishi na kiutawala.

Kwa mujibu wa Mhe. Kikwete, ukaguzi huo utasaidia taasisi kubaini na kurekebisha kasoro za kiutendaji, kuimarisha uwajibikaji, kupunguza migogoro ya kiutumishi na kuongeza ufanisi katika utendaji kazi.

Ameongeza kuwa ukaguzi huo utaiwezesha Serikali kupata taarifa kuhusu hali ya utumishi wa umma nchini na kutoa mapendekezo ya kuboresha sera, sheria na kanuni za utumishi wa umma.

Katika hatua nyingine, Mhe. Kikwete amewataka watumishi wa umma kuzingatia maadili na wajibu wao, huku akiwaagiza waajiri kutoa motisha kwa wanaofanya vizuri na kuchukua hatua stahiki dhidi ya wanaokiuka maadili ya utumishi.

Amesisitiza kuwa rasilimaliwatu ni msingi muhimu wa maendeleo kwa kuwa ndiyo inayosimamia rasilimali nyingine zote, hivyo inapaswa kusimamiwa kwa ufanisi.

Aidha, Mhe. Kikwete amesema Serikali inaendelea kuboresha maslahi ya watumishi wa umma kwa kuzingatia uwezo wa bajeti, ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kwa weledi na ufanisi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma, Jaji Mstaafu Hamisa Kalombola, ameishukuru Serikali kwa kuiwezesha Tume kuendelea kuimarisha shughuli zake, ikiwemo matumizi ya mifumo ya TEHAMA katika kutekeleza majukumu ya ukaguzi.

Amesema matumizi ya teknolojia yamerahisisha kwa kiasi kikubwa kazi ya ukaguzi kwa kuwezesha ukusanyaji, uchambuzi na ufuatiliaji wa taarifa kwa ufanisi zaidi, hivyo kuongeza kasi na ubora wa utekelezaji wa majukumu ya Tume.

Awali, Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda, amesema ukaguzi huo ni muhimu katika kubaini maeneo yenye changamoto na kusaidia waajiri kuchukua hatua za kuboresha usimamizi wa rasilimaliwatu. “Lengo ni kuhakikisha waajiri na watumishi wanatekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu zilizowekwa ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi,” amesema Kipanda.

Ameongeza kuwa zoezi hilo la ukaguzi linafanyika katika mikoa 16 na linatekelezwa na wataalamu wa Tume hiyo anayoiongoza.

Naye, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Bw. Emmanuel Mkongo, amesema halmashauri hiyo itaendelea kushirikiana na Tume ya Utumishi wa Umma kuhakikisha usimamizi wa utumishi unazingatia Sheria na Kanuni zilizopo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro  mara baada ya kuzindua zoezi la ukaguzi katika halmashauri hiyo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na baadhi viongozi  wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na vingozi wa  Tume ya Utumishi wa Umma, mara baada ya kuwasili kwa ajili ya kuzindua zoezi la ukaguzi katika halmashauri hiyo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma, Jaji Mstaafu Hamisa Kalombola mara baada ya kuwasili kwa ajili ya kuzindua zoezi la ukaguzi katika halmashauri hiyo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, mara baada ya kuwasili kwa ajili ya kuzindua zoezi la ukaguzi katika halmashauri hiyo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.

Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma, Jaji Mstaafu Hamisa Kalombola akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kwa ajili ya kuzungumza  na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwenye uzinduzi wa zoezi la ukaguzi katika halmashauri hiyo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.

Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda akizungumza kabla Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete  kuzungumza  na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwenye uzinduzi wa zoezi la ukaguzi katika halmashauri hiyo,


Baadhi ya watumishi wa umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro wakimsililiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete wakati  akizungumza nao mara baada ya kuzindua zoezi la ukaguzi katika halmashauri hiyo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.


 

 

 

 

 

 

 

 

WAZIRI KIKWETE AISISITIZA TAKUKURU KUJIRIDHISHA NA USHAHIDI WA KESI ZA WATUHUMIWA KABLA YA KUZIPELEKA MAHAKAMANI


Na Lusungu Helela, Morogoro

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, ameisisitiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kujiridhisha na ushahidi wa kutosha kabla ya kufikisha kesi mahakamani ili kuepuka kuwapotezea watu muda, hasa pale ambapo mtuhumiwa huachiwa au kushinda kesi kutokana na kukosekana kwa ushahidi.

Mhe. Kikwete ametoa kauli hiyo leo  Alhamisi Juni 20, 2026, alipokuwa akizungumza na watumishi wa TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi.

Amesema katika miaka ya hivi karibuni TAKUKURU imeshindwa kufanikiwa kwenye baadhi ya kesi na hii sio kwamba inaonewa, yawezekana kuna sehemu katika ushahidi hawajajipanga vizuri.

“Nawaombeni sana Maafisa Uchunguzi wetu tujiridhishe, msitumike katika kuwapotezea watu muda, ni muhimu tukajiridhisha juu ya ushahidi wa kesi zetu na utayari wa kupeleka kesi Mahakamani. Haipendezi kesi kuendeshwa kwa zaidi ya miezi mitano, halafu mwisho mtuhumiwa ashinde kwa kukosekana kwa ushahidi wa kutosha,” amesema.

Ameongeza kuwa watumishi wa taasisi hiyo wanapaswa kuhakikisha haki inatendeka bila kumuonea haya mtu yeyote wala kupindisha Sheria, Taratibu na Kanuni katika kila hatua ya uchunguzi.

Aidha, ameipongeza Taasisi hiyo kwani pamoja na kutofanikiwa katika baadhi ya kesi kwa kukosa ushahidi lakini amewapongeza kwa kesi walizoshinda ambazo zilikuwa na ushahidi wa kutosha huku akiwataka kuendelea kufanya kazi kwa bidii.

Amesema takwimu za mwaka uliopita zinaonyesha TAKUKURU imeshinda zaidi ya asilimia 70 ya kesi za rushwa ilizofikisha mahakamani.

Awali , Mkurugenzi  Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin  Chalamila, amesema taasisi hiyo itaendelea kutanguliza uzalendo, weledi, uwajibikaji na haki katika kushughulikia kesi za rushwa na uhujumu uchumi.

Chalamila amesema TAKUKURU ina Kitengo cha Maadili ya Watumishi kinachoongozwa na Mkurugenzi na moja ya majukumu yake ya msingi ni kuchunguza watumishi wa taasisi hiyo ili kuhakikisha wanakuwa mfano bora kwa jamii.

“Tuna Kitengo cha Maadili ya Watumishi wa TAKUKURU na kinaongozwa na Mkurugenzi. Moja ya jukumu lake la msingi ni kuwachunguza watumishi ili tuwe mfano na kioo bora kwa jamii,” alisema


 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, (katikati) akiwa ameongozana na viongozi wengine akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Usimamizi Miliki ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Dkt. Emmanuel Kiabo kuhusiana na jengo la   Ofisi ya TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila 



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, akizungumza na watumishi wa TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi.

Baadhi ya Watumishi wa TAKUKURU  wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, wakati akizungumza nao leo Mkoani wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, akisalimiana na baadhi ya viongozi na  watumishi mara baada ya kuwasili katika  Ofisi za TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya viongozi na watumishi wa TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi.

 Mkurugenzi  Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, kuzungumza na watumishi wa TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Itumishi wa Umma na Utawala Bora, akipanda mti mara baada ya  kuzungumza na watumishi wa TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Itumishi wa Umma na Utawala Bora, akimwagilia  mti mara baada ya kuupanda katika Ofisi za  TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kukutana na watumishi wa taasisi zilizo chini ya Ofisi yake na kusikiliza changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi.

 

 

 

 

Karibu Tukuhudumie