Wednesday, August 12, 2026

UTUMISHI, BODI YA MIKOPO ZANZIBAR ZASAINI MAKUBALIANO KUBADILISHANA TAARIFA

Na Eric Amani, Mji wa Serikali Mtumba.

Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imesaini makubaliano ya ushirikiano na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Zanzibar (ZHELB) kwa ajili ya kuwezesha kubadilishana taarifa kati ya Mfumo wa Taarifa za Watumishi wa Umma wa Tanzania Bara na mfumo wa Bodi hiyo.

Makubaliano hayo yamesainiwa leo, Agosti 12, 2026 na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Juma Selemani Mkomi na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Zanzibar Ndugu Umrat Mohamed.

Akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini, Katibu Mkuu Mkomi amesema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali za kutumia mifumo ya kidijitali kuboresha usimamizi wa taarifa na utoaji wa huduma kwa Watumishi wa Umma.

Amesema kubadilishana taarifa hizo kutasaidia kubaini wanufaika wa mikopo ambao ni watumishi wa umma na kuwezesha wale wenye madeni ya mikopo kutekeleza wajibu wao wa kurejesha fedha walizogharamiwa na Serikali.

“Utaratibu huu utasaidia kuhakikisha taarifa za watumishi wanaonufaika na mikopo zinapatikana kwa usahihi na kwa wakati, jambo litakalorahisisha urejeshaji wa mikopo na kuimarisha usimamizi wa fedha za Serikali,” amesema Mkomi.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Dkt. Mwanakhamis A. Ameir, ameishukuru Ofisi ya Utumishi kwa kuwezesha hatua hiyo, akieleza kuwa ushirikiano huo utasaidia kuimarisha mifumo ya taarifa na usimamizi wa mikopo ya elimu ya juu Zanzibar.

Amesema kuunganishwa kwa mifumo hiyo kutarahisisha upatikanaji na uhakiki wa taarifa za wanufaika, hivyo kuongeza ufanisi katika usimamizi wa mikopo na urejeshaji wake.

Makubaliano hayo yanatarajiwa kuimarisha ushirikiano wa Taasisi hizo katika usimamizi wa taarifa, kuongeza usahihi wa taarifa za wanufaika wa mikopo na kuwezesha huduma kutolewa kwa haraka, uwazi na ufanisi zaidi, sambamba na kuimarisha matumizi ya mifumo ya kidijitali katika utendaji wa Serikali.

Hatua hiyo pia inaweka msingi wa mifumo ya taarifa za watumishi wa umma wa Tanzania Bara na Zanzibar kuwasiliana na kubadilishana taarifa kwa ufanisi, kwa kuzingatia taratibu za usalama na usiri wa taarifa.



Picha ya Pamoja ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (katikati) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo elimu ya Juu ya Wanafunzi wa Ellimu ya Juu Zanzibar Bi. Umrat S. Mohamed (Kulia) na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Dr. Mwanakhamis Ameir (kushoto) na baadhi ya wakurungezi kutokea Ofisi ya Rais - UTUMISHI mara baada ya kutia saini ya makubaliano ya ushirikiano kwenye masuala ya mikopo ya elimu ya juu kwa watumishi wa umma Agosti 12, 2026 Mtumba Jijini Dodoma

Monday, August 10, 2026

NAIBU KATIBU MKUU LWANGILI ASISITIZA UJUZI NA HAIBA YA UONGOZI KATIKA URITHISHANAJI MADARAKA KWA WATUMISHI WA UMMA

Na Antonia Mbwambo - Dodoma

Tarehe 10 Agosti, 2026

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili, amesisitiza umuhimu wa kuendelea kujenga ujuzi wa kitaalamu na haiba ya uongozi katika kuwaandaa warithi wa madaraka ili kuhakikisha kunakuwa na mwendelezo wa utendaji na utoaji wa huduma bora katika Taasisi za umma.

Bi. Lwangili ameyasema hayo leo, Agosti 10, 2026, wakati akihitimsha mafunzo ya uelewa kuhusu Urithishanaji Madaraka yaliyofanyika katika eneo maalumu la Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Mtumba Jijini Dodoma.

Amesema maandalizi ya urithishanaji madaraka yanapaswa kuanza mapema kwa kuwajengea uwezo unaohitajika katika nafasi za uongozi wanazotarajiwa kuzishika.

Aidha, Bi. Lwangili ameongeza kuwa ujuzi wa kitaalamu (Technical Skills) humwezesha Mtumishi kuwa na maarifa na uwezo wa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi, huku haiba ya uongozi ikimsaidia kuwasiliana vizuri, kujiamini, kushirikiana na wengine, kuwa mwadilifu, kufanya maamuzi na kuwajibika.

“Kuwa na ujuzi wa kitaalamu pekee hakutoshi. Mtumishi anayejengwa kuwa Kiongozi wa baadaye anapaswa pia kuwa na haiba inayomjengea uwezo wa kuwasiliana vizuri, kujiamini, kushirikiana na wengine, kuwa mwadilifu, kufanya maamuzi na kubeba majukumu kwa uwajibikaji,” amesema Bi. Lwangili.

Pia Bi. Lwangili amesisitiza kuwa, Urithishanaji Madaraka si kumwandaa mtu kuchukua nafasi ya Kiongozi aliyepo pekee, bali ni kuimarisha Taasisi kwa kuwa na Watumishi wenye uwezo wa kuendeleza majukumu na huduma za umma.

Kwa upande wake, Mchumi Mkuu kutoka Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Bertha Bomani, ameeleza kuwa Urithishanaji Madaraka ni mchakato wa kuwaandaa mapema Watumishi wenye uwezo na sifa stahiki kwa ajili ya majukumu ya uongozi.

Bi. Bomani amebainisha mikakati ya Urithishanaji Madaraka katika Utumishi wa Umma ikiwa ni pamoja na kuendelea kutoa elimu ya uelewa na kujenga uwezo kwa Viongozi na Watumishi kuhusu manufaa ya kuandaa na kutekeleza Mpango wa Urithishanaji Madaraka, pamoja na kuwakumbusha Waajiri kutenga fedha katika bajeti za Taasisi zao kwa ajili ya uandaaji na utekelezaji wa mpango huo.

 

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili akizungumza na Watumishi wa Ofisi hiyo (hawapo pichani) wakati Naibu Katibu Mkuu huyo akihitimisha Mada ya mafunzo kuhusu Urithishanaji wa Madaraka leo tarehe 10 Agosti, 2026 Mtumba Jijini Dodoma.


Baadhi ya Wakurugenzi na Watumishi kutoka Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mafunzo ya Uelewa kuhusu Urithishanaji Madaraka yaliyofanyika tarehe 10 Agosti,2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo iliyopo Mtumba Jijini Dodoma

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili (aliyesimama mbele) akizungumza na Watumishi wa Ofisi hiyo wakati Naibu Katibu Mkuu huyo akihitimisha Mada ya mafunzo kuhusu Urithishanaji wa Madaraka leo tarehe 10 Agosti, 2026 Mtumba Jijini Dodoma

Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mafunzo ya Uelewa kuhusu Urithishanaji Madaraka yaliyofanyika tarehe 10 Agosti,2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo iliyopo Mtumba Jijini Dodoma

Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mafunzo ya Uelewa kuhusu Urithishanaji Madaraka yaliyofanyika tarehe 10 Agosti,2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo iliyopo Mtumba Jijini Dodoma

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili (wa pili kutoka kulia) akifuatilia mafunzo ya uelewa ambayo hutolewa kila jumatatu ya wiki katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma leo tarehe 10, Agosti, 2026. Wengine ni Wakurugenzi na Wakurugenzi wasaidizi wa Idara na Vitengo vya Ofisi hiyo.

Mkurugenzi Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Leila Mavika akitoa ufafanuzi kuhusu Urithishanaji Madaraka mara baada ya muwezeshaji ambaye pia ni Mchumi Mkuu wa Ofisi hiyo, Bi. Bertha Bomani, kutoa maelezo kuhusu mada hiyo leo tarehe 10 Agosti, 2026 Jijini Dodoma

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili (wa kwanza kutoka kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini Bw. Priscus Kiwango (wa pili kutoka kushoto) wakati wa mafunzo ya uelewa kwa Watumishi wa Ofisi hiyo yaliyofanyika katika eneo maalumu la Ofisi hiyo iliyopo Mtumba Jijini Dodoma


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili (wa kwanza kutoka kulia) akifuatilia mafunzo kuhusu Urithishanaji Madaraka kutoka kwa Mchumi Mkuu Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu, Bi. Bertha Bomani leo tarehe 10 Agosti, 2026 Mtumba jijini Dodoma. Kulia kwake ni Wakurugenzi na Wakurugenzi wasaidizi wa Vitengo vya Ofisi hiyo.

Baadhi ya Wakurugenzi wasaidizi na Watumishi kutoka Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mafunzo ya Uelewa kuhusu Urithishanaji Madaraka yaliyofanyika tarehe 10 Agosti,2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo iliyopo Mtumba Jijini Dodoma


Mchumi Mkuu kutoka Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Bertha Bomani, akielezea dhana ya Urithishanaji Madaraka kwa Watumishi wa Ofisi hiyo wakati wa Mafunzo ambayo hufanyika kila jumatatu ya wiki kwa lengo la kuwajengea Watumishi hao uwezo wa kiutendaji Mtumba Jijini Dodoma

Baadhi ya Viongozi na Watumishi kutoka Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mafunzo ya Uelewa kuhusu Urithishanaji Madaraka yaliyofanyika tarehe 10 Agosti,2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo iliyopo Mtumba Jijini Dodoma


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili (wa kwanza kutoka kushoto) akisalimiana na baadhi ya Wakurugenzi wa Ofisi hiyo, mara baada ya Naibu Katibu Mkuu huyo kuhitimisha mafunzo ya uelewa kuhusu Urithishanaji Madaraka yaliyofanyika Jijini Dodoma.