Tuesday, July 28, 2026
Monday, July 27, 2026
KAPINGA AHIMIZA WATUMISHI WA UMMA KUTUMIA KUWEKEZA KUPITIA MFUMO WA e-WEKEZA
Na. Eric Amani, Dodoma
27 Julai, 2026
Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Cyrus Kapinga, amewahimiza watumishi wa umma nchini kujenga utamaduni wa uwekezaji kwa kutumia mfumo wae-Wekeza kwa kuwa ni mfumo salama na wenye uwazi katika uwekezaji unakuza kipato.
Bw. Kapinga ametoa wito huo leo, Julai 27, 2026, wakati wa mafunzo ya kila Jumatatu yanayoandaliwa na Ofisi hiyo na kufanyika katika eneo maalum la mafunzo Mtumba, Jijini Dodoma.
Bw. Kapinga aliongeza kuwa uwekezaji ni nguzo muhimu ya kujenga ustawi wa kifedha wa mtumishi wa umma, hivyo ametoa rai kwa kila mtumishi wa umma kutumia fursa zilizopo ili kuweka akiba, kuongeza kipato na uwezo wa kukabiliana na changamoto za kiuchumi zinazoweza kumfanya mtumishi kushindwa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.
“Ni muhimu kwa mtumishi wa umma kujenga tabia ya kuwekeza mapema na taratibu kupitia mfumo wa e-Wekeza ili kuimarisha ustawi wa kifedha,” alisema Bw. Kapinga.
Bw. Kapinga amesema matumizi ya teknolojia kupitia mfumo wa e-Wekeza yameondoa vikwazo vilivyokuwa vinawakabili wawekezaji wengi kwa kuwawezesha kupata huduma za uwekezaji mahali popote walipo bila kulazimika kufika katika ofisi za taasisi husika.
Kwa upande wao, wataalamu kutoka Watumishi Housing Investments (WHI), ambao ndio wasimamizi wa mfumo wa e-Wekeza, walieleza kuwa mfumo huo umeundwa ili kurahisisha ushiriki wa watumishi wa umma katika uwekezaji kwa njia ya kidijiti.
![]() |
Afisa
Masoko Kutokea Watumishi Housing Investment (WHI) Bw, Jafari Yakubu akiwasilisha
mada ya uwekezaji katika mfuko wa Pamoja (FAIDA FUND) kupitia dirisha la e-
Wekeza (WATUMISHI PORTAL) kwa watumishi wa Ofisi ya Rais - UTUMISHI wakati
wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa
Serikali Mtumba, jijini Dodoma. |
Wednesday, July 22, 2026
WARATIBU WA KUDHIBITI VVU, UKIMWI NA MAGONJWA SUGU YASIYOAMBUKIZA WATAKIWA KUTOA ELIMU JUU YA UDHIBITI MAGONJWA MAHALI PA KAZI ILI KUFIKIA MALENGO YA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050
Veronica Mwafisi -Dodoma
Tarehe 22 Julai, 2026
Waratibu
wa ngazi ya Mikoa Mahali
pa Kazi katika Utumishi wa Umma wametakiwa Kutoa elimu kwa watumishi wa umma juu ya udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa
Yasiyoambukiza ili kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050
inayolenga kujenga taifa lenye watu wenye afya, tija, ustawi na ufanisi ambao watatoa
huduma bora kwa wananchi.
Kauli
hiyo imetolewa leo na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya
Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu
ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles
Kato wakati akifungua semina elekezi kwa Waratibu wa ngazi ya Mikoa
kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika
Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.
Dkt.
Kato amesema katika kutekeleza afua za kuimarisha afya kwa watumishi ni vema
kuwa na program za upimaji wa afya pamoja na mazoezi ya viungo kwa watumishi
katika maeneo yao ya kazi ili kufikia utekelezaji huo wa Dira 2050.
Ameongeza
kuwa, itakuwa vema kuandaa mafunzo pia kwa watumishi pamoja na msaada wa
kisaikolojia ili kuwasaidia zaidi katika utekelezaji wa majukumu yao.
Aidha,
Dkt. Kato amewataka waratibu hao kuandaa taarifa za utekelezaji wa
Mwongozo na Waraka Na. 2 wa mwaka 2014 kuhusu kudhibiti VVU, UKIMWI na Magonjwa
Yasiyoambukiza Mahali pa Kazi katika Utumishi wa Umma ikiwa ni pamoja na
kuwajengea uwezo.
Kwa upande wake, Kaimu
Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii ambaye ni Afisa Ustawi
wa Jamii Mkuu, Bi. Herieth Mpili akitoa neno la utangulizi kabla ya
kumkaribisha mgeni rasmi amesema kuwa lengo la semina hiyo ni kukuza uelewa na
ufahamu juu ya majukumu ya Waratibu hao na kuwawezesha kuandaa mipango ya muda
mrefu na mfupi wa utekelezaji wa afua za kudhibiti Magonjwa Yasiyoambukiza
Mahali pa Kazi katika Utumishi wa Umma ili kuleta ufanisi katika utekelezaji wa majukumu kama
ilivyokusudiwa na Serikali.
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora itaendelea kushirikiana na Sekretarieti za Mikoa yote
nchini kwa lengo la kusimamia masuala ya Anuai za Jamii na kutoa mafunzo kwa
maafisa au waratibu watakaoteuliwa kuratibu afua hizo katika mikoa yao ili
kuhakikisha kunakuwa na afya imara na ustawi wa watumishi wote nchini.
Kaimu
Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi
Msaidizi Sehemu ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato akizungumza
na Waratibu wa ngazi ya Mikoa wakati wa semina elekezi kuhusu udhibiti
wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa
Umma iliyofanyika jijini
Dodoma.
Sehemu ya Waratibu
wa ngazi ya Mikoa wakimsikiliza, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya
Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu
ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato wakati
akifungua semina
elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa
Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.
Sehemu ya Waratibu
wa ngazi ya Mikoa wakimsikiliza, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya
Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu
ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato wakati
akifungua semina
elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa
Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.
Kaimu
Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii ambaye ni Afisa Ustawi
wa Jamii Mkuu, Bi. Herieth Mpili akitoa neno la utangulizi kabla ya
kumkaribisha Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI,
Dkt. Charles Kato kuzungumza na Waratibu wa ngazi ya Mikoa wakati wa semina
elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa
Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.
Afisa Maendeleo ya Jamii, Sehemu
ya Menejimenti Anuai za Jamii,
Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Neema Range akifafanua jambo wakati akiwasilisha
mada kuhusu Anuai za Jamii na Ujumuishwaji wa Mwongozo Wa Kudhibiti VVU, UKIMWI
na MSY na Waraka (2014) kwa Waratibu wa ngazi ya Mikoa wakati wa semina elekezi kuhusu
udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika
Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.
Bingwa
wa Afya ya Akili kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Dkt. Garvin
Kweka akisisitiza jambo wakati akiwasilisha mada kuhusu Afya ya Akili kwa Waratibu
wa ngazi ya Mikoa wakati
wa semina elekezi iliyoandaliwa na Sehemu ya
Menejimenti Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI kuhusu udhibiti wa VVU,
UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma
iliyofanyika jijini Dodoma.
Sehemu ya
Waratibu wa ngazi ya Mikoa wakifuatilia mada
mbalimbali wakati wa semina elekezi iliyoandaliwa na
Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI kuhusu udhibiti wa
VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma
iliyofanyika jijini Dodoma.
Mratibu
wa ngazi ya Mkoa kutoka Kagera ambaye ni Afisa Rasilimaliwatu Mkuu, Bw. Emily
Ishegoma akiwasilisha maoni yake wakati wa majadiliano kwenye semina elekezi
iliyoandaliwa na Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI
kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika
Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.
Mwakilishi
kutoka Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania, Dkt. Theresiaglory Tety akifafanua
jambo alipokuwa akiwasilisha mada kuhusu Hali Halisi kuhusu VVU na UKIMWI wakati
wa semina elekezi kwa Waratibu wa ngazi ya Mikoa iliyoandaliwa
na Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI kuhusu udhibiti
wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa
Umma iliyofanyika jijini Dodoma.
Kaimu
Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni
Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato (katikati) akiwa katika picha ya pamoja
na Waratibu wa ngazi ya Mikoa mara baada ya
kufungua semina elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa
Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini
Dodoma.
Kaimu
Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni
Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato (katikati) akiwa katika picha ya pamoja
na Waratibu wa ngazi ya Mikoa mara baada ya
kufungua semina elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa
Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini
Dodoma.
Maafisa
kutoka Idara ya Uendelezaji Sera, Sehemu ya Menejimenti Anuai za Jamii,
Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia jambo wakati wa semina elekezi kwa Waratibu
wa ngazi ya Mikoa kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza
Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.
Kaimu
Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni
Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato (katikati) akiwa katika picha ya pamoja
na Sekretarieti kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI mara
baada ya kufungua semina elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa
Yasiyoambukiza Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini
Dodoma.
Sehemu ya Waratibu
wa ngazi ya Mikoa wakimsikiliza, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya
Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu
ya Uchambuzi Sera wa ofisi hiyo, Dkt. Charles Kato wakati
akifungua semina
elekezi kuhusu udhibiti wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza Mahali Pa
Kazi katika Utumishi wa Umma iliyofanyika jijini Dodoma.















