Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais UTUMISHI na Utawala Bora Bw. Xavier Daudi akutana na kufanya mazungumzo na Viongozi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) Ofisini kwake Mtumba Jijini Dodoma. Viongozi hao wamemtambulisha Mwakilishi Mkuu Mpya Bw.Kuge Katsuya baada ya Bw.Ara Hitoshi kumaliza muda wake.
Wednesday, April 22, 2026
NAIBU KATIBU MKUU,OFISI YA RAIS-UTUMISHI BW. XAVIER DAUDI AKUTANA NA VIONGOZI WA JICA KWA MAZUNGUMZO
Tuesday, April 21, 2026
WATUMISHI WA UMMA WASISITIZWA KUSHUGHULIKIA MREJESHO WA WANANCHI KWA HAKI NA KWA WAKATI
Na. Antonia Mbwambo-Dodoma
Tarehe
21 Aprili, 2026
Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli amewasisitiza Watumishi wa Umma kushughulikia kwa haki na kwa wakati mrejesho unaowasilishwa na wananchi kupitia Mfumo wa (e- Mrejesho) ili kujenga imani na heshima ya Serikali kwa umma.
Bi. Shuli ameyasema hayo leo
Aprili 21, 2026 wakati akimuwakilisha Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi katika
ufunguzi wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko,
mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi
zilizo chini yake.
“Ili kufikia utumishi wa umma unaowajibika
na uliotukuka, ni vizuri tukashughulikia mrejesho wa wananchi kwa haki na
uharaka zaidi.” Bi Shuli alisema.
Amesema, Watumishi wa Umma
wanapaswa kuwa na mabadiliko katika fikra, mitazamo, mifumo na tabia walizonazo
ili kuwa na Utumishi wa Umma wenye matokeo chanya na thamani halisi kwa mwananchi.
Bi Shuli ameongeza kuwa uzingatiaji
wa maadili katika utumishi wa umma si kuzifuata tu Sheria, Kanuni, Taratibu na
Miongozo ya Utumishi wa Umma bali ni pamoja na kuutumia ipasavyo utaalamu unaohusu
ushughulikiaji wa mrejesho wa wananchi .
Amesema ni jukumu la kila
mshiriki kuonesha ushirikiano na kuzingatia utu hususani wanapotoa huduma kwa
wateja pamoja na kuwa waaminifu hasa katika utunzaji siri kwa kuwa kazi
watakazofanya zitahitaji kuwa na matumizi sahihi ya taarifa.
Aidha, amewapongeza washiriki
wote kwa kuhudhuria mafunzo hayo na kuwataka wajifunze kwa bidii ili wawe
wataalamu watakaowajibika kikamilifu
Kwa upande wake mwenyekiti wa
kikao hicho ambaye ni Afisa TEHAMA kutoka Watumishi Housing Investiments (WHI) Bw.
Albano Lukiano amemshukuru Bi. Shuli kwa
kuwafungulia mafunzo hayo na kuahidi kuwa yale yote watakayofundishwa watayazingatia
na kuyafanyia kazi ili kutoa huduma bora kwa manufaa ya umma.
Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya
Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister (kushoto)
akiteta jambo na Mwenyekiti wa mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho
ambaye pia ni Afisa TEHAMA kutoka Watumishi Housing Investiments (WHI) Bw.
Albano Lukiano (kulia) kabla ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo hayo jijini
Dodoma.
Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya
Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli (aliyekaa
katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea
na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi mara
baada ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa
Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya
Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli
(kushoto) akifurahia jambo mara baada
ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo ya kutumia Mfumo wa e-Mrejesho
yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za
Taifa Jijini Dodoma. Kulia ni Mkurugenzi
Msaidizi wa Maadili wa Ofisi hiyo Bi. Janet Mishinga
Afisa
tawala kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
Bi. Semeni Muyabhaga akiwasilisha mada ya Uwasilishwaji wa Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi kwa kutumia Mfumo wa e-Mrejesho wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika Aprili 21, 2026 katika ukumbi wa
Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa kikao cha mafunzo ya kutumia Mfumo wa e-Mrejesho Bw. Albano Lukiano akitoa neno la shukrani kwa Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felister Shuli mara baada ya Mkurugenzi huyo kufungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma.
Afisa
Rasilimaliwatu Mwandamizi Kutoka Idara ya Usimamizi wa Maadili, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Hassan Kilenza akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa mjadala
wa hoja mbalimbali kuhusu matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho jijini Dodoma.
Washiriki
wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko,
mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi wakifuatilia hotuba ya mgeni
Rasmi wakati alipokuwa akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika leo Aprili 21, 2026
jijini Dodoma.
Washiriki
wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko,
mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi wakifuatilia hotuba ya mgeni
Rasmi wakati alipokuwa akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika leo Aprili 21, 2026
jijini Dodoma.
Washiriki
wa mafunzo ya matumizi ya kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko,
mapendekezo, maulizo na pongezi kwa watumishi wakifuatilia hotuba ya mgeni
Rasmi wakati alipokuwa akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika leo Aprili 21, 2026
jijini Dodoma.
Afisa Tawala kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Stella Teri akiwasilisha mada kuhusu uzingatiaji wa Kanuni za Maadili ya Utendeji kwa watumishi wa Umma wakati wa mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa e-Mrejesho yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma
Afisa
rasilimali watu mwaandamizi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora Bi. Saada Ibrahim akiwasilisha mada ya Mwngozo wa Ushughulikiaji wa Mrejesho katika Utumishi wa Umma katika mafunzo ya matumizi ya Mfumo huo yaliyofanyika Aprili 21, 2026 katika ukumbi wa Ofisi
ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Jijini Dodoma.
Monday, April 20, 2026
WATUMISHI WA UMMA WAKUMBUSHWA KUTUNZA KUMBUKUMBU ZA KAZI
Na. Mwandishi wetu-Dodoma
Tarehe 20 Aprili, 2026.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi
amewakumbusha watumishi wa Ofisi yake kuweka na kutunza kumbukumbu za majukumu
wanayoyafanya kila siku ili kusaidia vizazi vijavyo kufanya marejeo pale
inapotakiwa kwa lengo la kuimarisha uendelevu wa taarifa katika utoaji wa
huduma.
Bw. Daudi ameyasema hayo
Aprili 20, 2026 wakati akihitimisha mafunzo ya uelewa kwa watumishi wa Ofisi
yake kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga
yaliyotolewa katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Aliongeza kuwa, watumishi wa
umma hawanabudi kuzingatia mafunzo ya kimkakati wanayopewa ili kuhakikisha
yanawajengea uwezo stahiki wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
‘’Majukumu ya Serikali
yanaishi, lakini watumishi wa Umma huondoka kutoka kituo kimoja kwenda kingine,
hivyo nyaraka zote zinapaswa kuhifadhiwa ipasavyo kwa kuzingatia usalama na
utaratibu unaofaa ili watumishi wanaobaki na watakaokuja waweze kurejerea’’ Bw.
Daudi alisema.
Aidha Bw. Daudi amewataka
viongozi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa Ofisi yake kufuatilia
na kujiridhisha iwapo mafunzo yanayotolewa kila jumatatu ya wiki yanaongeza
tija na ufanisi katika utendaji kazi.
Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi
wa Huduma na Mifumo ya TEHAMA Serikalini kutoka Ofisi ya Rais, UTUMISHI Bw.
Tiba Manoni amesema, Taasisi yoyote ni lazima ihakikishe inaweka mipango endelevu
ya kushughulikia majanga.
Kadhalika Mkurugenzi huyo
alibainisha kuwa majanga ya asili, ukosefu wa fedha, hitilafu za mifumo ya
teknolojia na magonjwa ya mlipuko ni sehemu ya majanga yanayoweza kutokea na
kupelekea kusitishwa kwa shughuli za utekelezaji wa majukumu na utoaji wa
huduma kwa umma.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Xavier Daudi akizungumza na watumishi wa Ofisi yake kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga wakati
akihitimisha mafunzo ya kuwajengea watumishi hao uelewa yaliyotolewa katika
eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Baadhi ya Wakurugenzi wasaidizi na Watumishi
wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo
ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao yaliyofanyika katika eneo la
Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Baadhi ya Viongozi na Watumishi
wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo
ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao yaliyofanyika katika eneo la
Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma
na Mifumo ya TEHAMA Serikalini kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Tiba Manoni akitoa
elimu kwa watumishi wa Ofisi hiyo kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga
katika mafunzo yaliyofanyika eneo maalum la Ofisi hiyo Aprili 20, 2026 jijini
Dodoma.
Baadhi ya Viongozi na Watumishi
wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo
ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao yaliyofanyika katika eneo la
Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Baadhi ya Viongozi na Watumishi
wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo
ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao yaliyofanyika katika eneo la
Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma
na Mifumo ya TEHAMA Serikalini kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Tiba Manoni akitoa
elimu kwa watumishi wa Ofisi hiyo kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga
katika mafunzo yaliyofanyika eneo maalum la Ofisi hiyo Aprili 20, 2026 jijini
Dodoma.
Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga iliyotolewa katika mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi hao katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma
Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga iliyotolewa katika mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi hao katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma
Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga iliyotolewa katika mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi hao katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma
