Tuesday, July 23, 2024

TAASISI ZA UMMA KUFANYA UHAKIKI WA TAKWIMU ZA WATUMISHI WA UMMA WENYE VVU, UKIMWI NA MAGONJWA SUGU YASIYOAMBUKIZA

 Na. Veronica Mwafisi-Manyara

Tarehe 23 Julai, 2024

Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Cyprus Kapinga amezitaka Wizara na Taasisi za Umma kufanya uhakiki wa takwimu za watumishi wa umma wenye VVU, Ukimwi na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza (MSY) ili kulinda afya za watumishi hao.

Bw. Kapinga ametoa wito huo leo wakati akifungua kikao kazi cha Robo ya Nne ya Mwaka 2023/2024 kilichoshirikisha Kamati ya Kifaifa, Waratibu wa Wizara wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza (MSY) pamoja na Wajumbe, Wenyeviti, Makatibu wa Mkoa wa Manyara wanaosimamia magonjwa hayo.

“Tunatakiwa kuwa na takwimu sahihi ya watumishi hao ili kurahisisha zoezi la kupanga bajeti ya kuwahudumia na kuimarisha afya ya akili na kudhibiti msongo wa mawazo. Watumishi hao ni sehemu ya nguvu kazi ya Taifa inayohudumia wananchi” alisisitiza Bw. Kapinga.

Aidha, Bw. Kapinga ametoa rai kwa Maafisa Masuuli wote katika taasisi za umma kuunda na kuimarisha Kamati za VVU, Ukimwi na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza (MSY) zilizopo kwa kutoa nafasi kwa wanakamati hao kupata mafunzo na elimu itakayowafanya wawe na uwezo wa kushawishi watumishi kupima afya na hivyo kuwa na takwimu sahihi kwa  mipango bora na endelevu.

Awali akitoa neno la utangulizi, Katibu Tawala Mkoa wa Manyara, Bi. Maryam Muhaji aliwataka washiriki wa kikao kazi hicho kusikiliza na kufuatilila kwa makini mada zote zitakazowasilishwa ili wapate uwezo na ujuzi Madhubuti wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kupitia Idara ya Uendelezaji Sera ipo mkoani Manyara kwa lengo la kujadili utekelezaji wa mapambano dhidi ya VVU, Ukimwi na Magonjwa yasiyoambukiza (MSY) ili kuwalinda watumishi wa umma na kuhakikisha taifa linaondokana na vifo vitokanavyo na magonjwa hayo ifikapo mwaka 2030.

Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cyprus Kapinga akizungumza na Kamati ya Kifaifa, Waratibu wa Wizara wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza (MSY) pamoja na Wajumbe, Wenyeviti, Makatibu wa mkoa wa Manyara wanaosimamia magonjwa hayo wakati wa kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024.


Baadhi ya Wakurugenzi wa Rasilimaliwatu wa Kamati ya Kitaifa ya Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza (MSY) na Waratibu wa magonjwa hayo wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cyprus Kapinga (hayupo pichani) wakati akifungua kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024 kinachofanyika mkoani Manyara.


Katibu Tawala Mkoa wa Manyara, Bi. Maryam Muhaji akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cyprus Kapinga kufungua kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024 cha Kamati ya Kifaifa, Waratibu wa Wizara wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza (MSY) kinachofanyika mkoani Manyara.

Mkurugenzi Msaidizi Anuai za Jamii na Mratibu wa VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mwanaamani Mtoo akitoa utambulisho wa Kamati ya Kifaifa, Waratibu wa Wizara wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza (MSY) pamoja na Wajumbe, Wenyeviti, Makatibu wa mkoa wa Manyara wanaosimamia magonjwa hayo kwenye kikao kazi kilichofanyika mkoani Manyara.


Afisa Maendeleo ya Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Neema Range akiwasilisha mada kuhusu Ujumuishwaji wa Sehemu za Anuai za Jamii wakati wa kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024 kilichoshirikisha Kamati ya Kifaifa, Waratibu wa Wizara wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza (MSY) pamoja na Wajumbe, Wenyeviti, Makatibu wa mkoa wa Manyara.


Afisa Ustawi wa Jamii Mwandamizi na Mratibu wa Kitaifa wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Juliana Ntukey akiwasilisha mada kuhusu Mwongozo wa Waraka wa kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza mahali pa kazi katika Utumishi wa Umma (2014) wakati wa kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024.


Mratibu wa VVU, Ukimwi na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza (MSY), Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara, Bi. Marietha Kyomo akiwasilisha taarifa ya Mkoa wa Manyara kuhusu hali ya utekelezaji wa Afua za VVU, Ukimwi na MSY wakati wa kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024 kilichofanyika katika mkoa huo.


Mratibu wa Kinga na Mwitikio wa Kitaifa dhidi ya VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza, Dkt. Haffidh Ameir akitoa taarifa kuhusu hali halisi ya VVU na Ukimwi Nchini wakati wa kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024 kilichoshirikisha Kamati ya Kifaifa, Waratibu wa Wizara wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza (MSY) pamoja na Wajumbe, Wenyeviti, Makatibu wa mkoa wa Manyara.


Daktari Bingwa wa Afya na Magonjwa ya Akili, Dkt. Sadiki Mandari akiwasilisha mada kuhusu kuimarisha afya ya akili kwa Kamati ya Kifaifa, Waratibu wa Wizara wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza (MSY) pamoja na Wajumbe, Wenyeviti, Makatibu wa mkoa wa Manyara wanaosimamia magonjwa hayo wakati wa kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024 kinachofanyika mkoani Manyara.


Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cyprus Kapinga akiwa katika picha ya pamoja na sehemu ya Waratibu wa Wizara wa Kudhibiti VVU, Ukimwi na Magonjwa Sugu Yasiyoambukiza (MSY) wakati wa kikao kazi cha robo ya nne ya Mwaka 2023/2024 kinachofanyika mkoani Manyara.



 

Thursday, July 18, 2024

WAZIRI SIMBACHAWENE APIGA MARUFUKU WATUMISHI WA UMMA KUSUMBULIWA KUFUATILIA TAARIFA ZA UHAMISHO

 Na Lusungu Helela - Kibakwe

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amepiga marufuku Watumishi wa  Umma  kusumbuliwa kufuatilia taarifa zao za kiutumishi wanapohamia kwenye kituo kipya cha kazi badala yake wafanye kazi zao kwani hilo sio jukumu lao bali ni wajibu wa Waajiri.

 

Mhe. Simbachawene ametoa kauli hiyo leo wakati akizungumza na watumishi na wananchi kwenye mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mlimo katika Kata ya Lufu, Jimbo la Kibakwe, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa jijini Dodoma ambapo amesema suala la taarifa za Mtumishi ni jukumu la Mwajiri.

 

Amesema kitendo cha taarifa za watumishi kutohamishwa kumesababisha Watumishi hao kushindwa kupimwa kwenye mfumo wa e-tendaji kazi kwa vile kunakuwa hakuna taarifa za watumishi hao katika kituo kipya cha kazi na hivyo mwisho wake watumishi kusumbuliwa kufuatilia taarifa za kule walikotoka.  

 

Kufuatia hatua hiyo, Mhe. Simbachawene amemuelekeza Katibu Mkuu- UTUMISHI kushirikiana na Mamlaka zingine zilikokasimiwa madaraka hayo ya kuhamisha Watumishi kuhakikisha Mtumishi pindi anapohama kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine asisumbuliwe kuhusu taarifa hizo.

 

Hivyo Mhe. Simbachawene ametoa muda wa kuhamisha taarifa za watumishi waliohama kuwa ifikapo Agosti 15 mwaka huu taarifa za watumishi wote ziwe zimehamishwa na baada ya hapo hatua kali za kinidhamu zitachukuliwa kwa wote watakaoshindwa kutekeleza jukumu hilo.

 

Amesema suala la kuhamisha taarifa za Mtumishi kutoka alikokuwa na kwenda kituo kipya cha kazi ni jukumu la Mkurugenzi au anayeongoza Taasisi wakishirikiana na Maafisa utumishi na kuongeza kuwa wanatakiwa kuhakikisha taarifa hizo zinahamishwa ndani ya mwezi mmoja ili watumishi waliohamishwa waendelee kufanya kazi zao kwa ufasaha.

 

"Utapimaje utendaji kazi wa mtumishi au kumpatia ruhusa mtumishi aliyepata dharula ilhali taarifa zake zipo sehemu nyingine, hii sio sawa, huko ni kuwatesa watumishi "amehoji Mhe. Simbachawene.

 

Amesema malalamiko ya kutohamishwa kwa taarifa za watumishi yamekuwa mengi kutoka kwa watumishi huku akiwataka watumishi wanapohama kutekeleza majukumu yao na hakuna atakayesumbuliwa.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza leo na watumishi na wananchi wa Kijiji cha Mlimo, Kata ya Lufu iliyopo katika Jimbo la Kibakwe, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Jijini Dodoma, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kikazi.

Sehemu ya watumishi na wananchi wa Kijiji cha Mlimo, Tarafa ya Kibakwe iliyopo katika Jimbo la Kibakwe, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Jijini Dodoma wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene, wakati wa ziara yake ya kikazi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akisalimiana na baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Mlimo mara baada ya kuwasili, ikiwa ni ziara yake ya kikazi

Baadhi ya Madiwani wa Viti maalum wakiimba mbele ya   Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kabla ya kumkaribishwa kwa ajili ya kuzungumza na  watumishi na wafanyakazi  katika eneo hilo

Diwani wa Kata ya Lufu Mhe. Gilbert Msigala akizungumza na wananchi wa  Kijiji cha Mlimo Kata ya Lufu iliyopo katika Jimbo la Kibakwe, Halmashauri ya  Wilaya ya Mpwapwa jijini Dodoma wakati wa ziara ya kikazi ya  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa, Mhe. Richard Maponda akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Mlimo, Kata ya Lufu iliyopo katika Jimbo la Kibakwe, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa jijini Dodoma wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene.




Wednesday, July 17, 2024

JUKUMU LETU SOTE KUZINGATIA SHERIA KATIKA KUTOA NA KUPOKEA HUDUMA – Mhe.Simbachawene

 Na Mwandishi wetu - Kibakwe

 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Kibakwe, Mhe. George Simbachawene amewataka viongozi na wananchi kuzingatia Sheria za nchi katika kutoa na kupokea huduma.

Mhe. Simbachawene ametoa kauli hiyo leo wakati akizungumza na wananchi kwa nyakati tofauti kwenye mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Maswala na Kitongoji cha Ng'onje vilivyopo Katika Kata ya Pwaga, Jimbo la Kibakwe, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa jijini Dodoma, ikiwa ni mwendelezo wa katika Jimbo hilo.

Mhe. Simbachawene amesema ili kuendeleza amani na kuepusha machafuko basi sheria za nchi ni lazima zizingatiwe na kila mtu awe kiongozi au mwananchi wa kawaida.

Amesema Tanzania imejengwa kwa misingi ya haki na usawa na ndio maana rasilimali za nchi zinagawanywa kwa usawa katika maeneo yote ya nchi ili kuchagiza utawala bora na ndio maana imeendelea kuwa kisiwa cha amani.

Amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu ameendelea kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa kuzingatia utoaji wa haki na usawa kwa wananchi wote bila kujali mahali walipo.

Ameongeza kuwa katika Jimbo la Kibakwe analoliongoza miaka ya nyuma vijiji vingi havikuwa na huduma nyingi za kijamii ikiwemo shule na zahanati lakini kwa sasa huduma hizo zote zipo maeneo mengi na wananachi wanaendelea kuhudumiwa.

Katika hatua nyingine, Mhe. Simbachawene ametoa wito kwa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) pamoja na Wakala wa Umeme Vijijini (REA) kuhakikisha zinatoa kipaumbele cha huduma wanazozitoa kwa Taasisi za kijamii zilizopo katika Kata ya Pwaga.
 
Amesema huduma muhimu kama vile umeme na barabara ni muhimu zikafikishwa haraka katika maeneo ya shule, makanisa, misikiti pamoja na ofisi za vijiji.

Mhe.Simbachawene amesema Serikali imekuja na mpango mkakati wa ujazilizi ambapo vitongoji na maeneo yote ya pembezoni mwa miji itaanza kufikishiwa umeme.


Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Pwaga, Mhe. Wilfred Mgonela ametumia fursa hiyo kumshukuru Mhe. Simbachawene kwa ushirikiano ambao ameendelea kumpa katika kuhakikisha miradi ya maendeleo inaendelea kutekelezwa katika Kata anayoiongoza huku akiwaomba wananchi kuendelea kushirikiana naye ili kujiletea maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Kata kwa ujumla.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene   akizungumza leo na wananchi wa Kijiji cha Maswala, Kata ya Pwaga iliyopo katika Jimbo la Kibakwe,  Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Jijini Dodoma, ikiwa ni mwendelezo wa  ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi  katika Jimbo hilo.


 Sehemu ya wananchi wa Kitongoji cha Ng'onje kilichopo katika Kijiji cha Pwaga, Tarafa ya Kibakwe iliyopo katika Jimbo la Kibakwe, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Jijini Dodoma wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene, wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi katika Jimbo la Kibakwe.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akisalimiana na baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Maswala mara baada ya kuwasili, ikiwa ni ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi katika Jimbo hilo.

Baadhi ya Waheshimiwa Madiwani wa Tarafa y ya Kibakwe iliyopo katika  Jimbo la Kibakwe, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa jijini Dodoma wakitumbuiza kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene kuzungumza na wananchi hao ikiwa ni ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi katika Jimbo la Kibakwe.

Diwani wa Kata ya Kibakwe Mhe.Wilfred Mgonela  akizungumza na wananchi wa Kitongoji cha Ng'onje cha Kijiji cha Pwaga Kata ya Kibakwe iliyopo katika Jimbo la Kibakwe, Halmashauri ya  Wilaya ya Mpwapwa jijini Dodoma wakati wa ziara ya kikazi ya  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi katika Jimbo la Kibakwe.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa, Mhe. Richard Maponda akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Maswala, Kata ya Kibakwe iliyopo katika Jimbo la Kibakwe, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa jijini Dodoma wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi katika Jimbo la Kibakwe.