Monday, July 13, 2026

KATIBU MKUU MKOMI AWATAKA WATUMISHI KUONGEZA KASI YA UTENDAJI KUFIKIA MALENGO YA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050

Na. Antonia Mbwambo – Dodoma

13 Julai, 2026

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, amewataka Watumishi wa Umma kuongeza kasi ya utendaji na kuzingatia weledi ili kuchangia kikamilifu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Katibu Mkuu Mkomi ametoa wito huo leo Julai 13, 2026, wakati akihitimisha mafunzo kuhusu umuhimu wa afya ya akili kwa Watumishi wa Umma yaliyofanyika katika eneo maalumu la Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Mtumba, jijini Dodoma kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi hao.

Bw. Mkomi amesema mafanikio ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 yanategemea uwepo wa Watumishi wa Umma wenye afya bora ya akili, maadili ya kazi, ubunifu na uwajibikaji, huku akisisitiza kuwa afya ya akili ni msingi wa utendaji wenye tija na utoaji wa huduma bora Serikalini.

"Afya ya akili si suala la mtu mmoja mmoja, bali ni msingi wa kuongeza tija katika Utumishi wa Umma. Mtumishi mwenye afya bora ya akili anakuwa na uwezo mkubwa wa kutoa huduma bora, kushirikiana na wenzake na kuleta matokeo chanya kwa Taasisi na Taifa kwa ujumla," amesema Bw. Mkomi.

Aidha, Bw. Mkomi amewaelekeza Wachumi wa Ofisi hiyo kufanya tafakuri za kitaaluma na kuibua mawazo bunifu yatakayochangia Serikali kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Kwa upande wake, Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma Elias, ambaye alikuwa Mwezeshaji wa mafunzo hayo, amesema afya ya akili ni nguzo muhimu ya ustawi wa mtumishi na ina mchango mkubwa katika kuongeza tija pamoja na kuboresha mazingira ya kazi.

Ameeleza kuwa changamoto za afya ya akili kwa watumishi wa Umma mara nyingi husababishwa na mpangilio duni wa kazi, mzigo mkubwa wa majukumu unaozidi uwezo wao, kazi za kujirudia rudia na mazingira magumu ya kazi. Amewahimiza watumishi kuzingatia mtindo bora wa maisha kwa kufanya mazoezi ya mara kwa mara, kula lishe bora, kupata mapumziko ya kutosha na kutafuta ushauri wa Wataalamu wanapokabiliwa na changamoto za afya ya akili.

Aidha, Dkt. Elias amewataka viongozi kuendelea kuzingatia usawa kwa watumishi wanaowasimamia, kupinga unyanyapaa dhidi ya wenye changamoto za afya ya akili na kutambua mapema dalili za changamoto hizo ili kuwawezesha watumishi kupata huduma stahiki kwa wakati.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akifurahia jambo wakati alipokuwa akihitimisha mafunzo ya uelewa kwa Watumishi wa Ofisi hiyo Julai 13, 2026 Mtumba Jijini Dodoma

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, akizungumza na Watumishi wa Ofisi yake wakati alipokuwa akihitimisha Mafunzo ya uelewa kuhusu Umuhimu wa Afya ya Akili kwa Watumishi wa Umma yaliyofanyika Julai 13, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo, Mtumba jijini Dodoma 

Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Idara na Vitengo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma.

Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma

Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma Elias akitoa mada ya mafunzo kuhusu Umuhimu wa Afya ya Akili kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora yaliyofanyika Julai 13, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Jijini Dodoma

Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Idara na Vitengo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma.

Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma Elias akitoa mada ya mafunzo kuhusu Umuhimu wa Afya ya Akili kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora yaliyofanyika Julai 13, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Jijini Dodoma

Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Idara na Vitengo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma.

Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.


Baadhi ya Wakurugenzi na Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo jijini Dodoma

Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.


Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.


Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Bingwa wa Afya ya Akili kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma, Dkt. Elihuruma (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya uelewa yaliyofanyika tarehe 13 Julai, 2026 jijini Dodoma.


Saturday, July 11, 2026

MHE. RIDHIWANI AWAASA WANAFUNZI “TABORA BOYS” KULINDA JINA ZURI LA SHULE YAO KWA KUJIEPUSHA NA TABIA ZISIZOFAA

Na. Veronica Mwafisi-Tabora

Tarehe 11 Julai, 2026

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amewaambia wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wavulana Tabora kuishi katika maadili wawapo shuleni na hata baada ya kumaliza shule ili wajiepusha na tabia ambazo zitawafanya wajiingize katika makundi yasiyofaa ya uvunjivu wa amani.

 

Mhe. Ridhiwani amesema hayo leo tarehe 11 Julai, 2026 alipotembelea shule hiyo kabla ya kikao cha majumuisho ya ziara yake ya kikazi ya siku tatu mkoani Tabora kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo Cha Ualimu mkoani humo.

 

Amesema kuna maisha baada ya kumaliza shule, hivyo wanafunzi hao wanatakiwa wakawe mfano mzuri katika maadili na uzalendo kwa wengine huko wanakoenda kutokana na sifa za shule hiyo.

 

“Shule hii imetoa viongozi wengi sana, waadilifu na wazalendo, hivyo mtunze heshima yake, mkajitofautishe na wengine, msiige tabia ambazo sio nzuri,” amesisitiza.

 

Amepongeza uongozi wa shule hiyo kwa matokeo mazuri ya kidato cha sita mwaka huu na miaka iliyopita na ufaulu mzuri pia hata kwa kidado cha nne na kuwasihi kuendelea kufanya vizuri zaidi ili elimu hiyo iwakomboe wao binafsi na taifa kwa ujumla.

 

Aidha, ametoa wito kwa Viongozi wa Mkoa wa Tabora kuwa karibu na wanafunzi wa shule hiyo na shule nyingine zote ili wawasaidie kukua kimaadili.

 

“Watoto hawa ni wadogo, tuwasaidie hata watakapotoka hapa waendelee kuwa na sifa nzuri huko watakakokwenda.


 







MHE. RIDHIWANI AWAELEKEZA WAAJIRI MKOANI TABORA KUMALIZA CHANGAMOTO ZOTE ZA WATUMISHI MWAKA HUU WA FEDHA

Na. Veronica Mwafisi-Tabora

Tarehe 11 Julai, 2026


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amewaelekeza Waajiri katika Sekta ya Umma mkoani Tabora kufanyia kazi madai ya watumishi ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufasaha.

 

Akifanya kikao cha majumuisho na Viongozi na Watumishi wa Umma wa Mkoa wa Tabora leo tarehe 11 Julai, 2026 baada ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi ya siku tatu katika mkoa huo, Mhe. Kikwete amesema katika mwaka huu wa fedha Waajiri washughulikie masuala yote ya kiutumishi ikiwemo kupanda madaraja, kulipa malimbikizo, kuwabadilisha kada wanaostahili pamoja na madai mengine.

 

Amesema Ofisi yake imekuwa ikipokea malalamiko mbalimbali ya watumishi kuhusiana na kutoshughulikiwa stahiki zao jambo ambalo limekuwa likishusha ari ya utendaji kazi na kushindwa kuwahudumia wananchi kikamilifu.

 

“Rais wetu mpendwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anataka wananchi wake wapate huduma bora, mwaka huu wa fedha tushughulikie changamoto zote za watumishi ili watoe huduma kwa furaha,” amesisiza.

 

Kuna watumishi wana sifa ya kupandishwa madaraja, wengine kubadilishiwa kada na wengine wana madai yao mbalimbali. “Ninaelekeza wote wanaostahili watekelezewe na kama kuna changamoto yoyote mnayokutana nayo katika utekelezaji wa hili mtuletee Ofisini tuone namna ya kulitatua,” ameongeza

 

Aidha, amewataka Maafisa Rasilimaliwatu kutoa ushauri kwa Waajiri utakaosaidia kutatua changamoto za kiutumishi.

 

Amesema changamoto za kiutumishi zikishindwa kutatuliwa basi wa kulaumiwa si mwingine bali ni Maafisa Rasilimaliwatu kwani wanayo nafasi kubwa ya kutoa ushauri mzuri kulingana na taaluma zao.

 

Mhe. Kikwete amewapongeza Viongozi na Watumishi wa Mkoa huo kwa ushirikiano mzuri baina ya Serikali na Chama Cha Mapinduzi uliochangia utekelezaji mzuri wa majukumu ya miradi ya maendeleo.

 

 “Tunatekeleza Ilani ya Chama kilichoko madarakani, niwapongeze kwa ushirikiano baina yenu, endeleeni kufanya kazi kwa pamoja kwani ndio msingi wa maendeleo ya taifa letu,” ameongeza

 

Vile vile Waziri Kikwete ametoa wito kwa Viongozi na Watumishi wa Mkoa huo kuzungumza na wananchi ikiwemo vijana na kusikiliza changamoto zao badala ya kusubiria viongozi wengine kutoka maeneo ya mbali kuzungumza.

 

Amesema kujua changamoto za vijana hao kunasaidia kwani wengine unakuta wanahitaji kitu kidogo cha kujiendeleza kiuchumi na kumuepusha kuingia katika masuala yasiyo na maadili.

 

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tabora ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Bi. Upendo Wella amemshukuru Mhe. Kikwete kwa ziara aliyoifanya katika mkoa huo ambayo itaenda kuboresha utendaji wa Watumishi kwa maendeleo ya taifa.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Viongozi, Watumishi wa Umma na Wakuu wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa Mkoa wa Tabora baada ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi ya siku tatu katika mkoa huo iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.


Sehemu ya Viongozi, Watumishi wa Umma na Wakuu wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa Mkoa wa Tabora wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao baada ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi ya siku tatu katika mkoa huo iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Sehemu ya Viongozi na Watumishi wa Umma wa Mkoa wa Tabora wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao baada ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi ya siku tatu katika mkoa huo iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.


Waheshimiwa Wabunge wa Mkoa wa Tabora, Viongozi na Watumishi wa Umma wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao baada ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi ya siku tatu katika mkoa huo iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

 

Sehemu ya Watumishi wa Umma wa Mkoa wa Tabora wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao baada ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi ya siku tatu katika mkoa huo iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Sehemu ya Viongozi na Watendaji wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tabora wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao baada ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi ya siku tatu katika mkoa huo iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.