Na. Antonia Mbwambo - Kagera
Tarehe: 2 Machi, 2026
Mwakilishi wa Katibu Mkuu Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bi. Leila Mavika amewaelekeza Wajumbe wa
Kamati ya Kitaifa na waratibu ngazi ya Wizara, Taasisi
zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za
Serikali za Mitaa kutekeleza majukumu yao
kwa weledi ili kujenga Utumishi wa Umma wenye afya, tija na
unaoendana na matarajio ya wananchi.
Bi. Mavika ameyasema hayo leo tarehe 02 Machi, 2026 wakati akifungua kikao kazi cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa Afua za kudhibiti VVU, UKIMWI na magonjwa Sugu Yasiyoambukiza ya kipindi cha robo ya pili ya Mwaka wa fedha 2025/2026 ngazi ya Mkoa na Taifa.
Aidha Bi. Mavika amezipongeza Taasisi za Umma ambazo zimekuwa zikifanya vizuri katika kusimamia afua za VVU, UKIMWI na MSY hasa kwenye Kuratibu kampeni za upimaji wa hiari wa VVU na utoaji wa elimu ya lishe bora, mazoezi na afya ya akili.
“Haya
mafanikio ni ya kujivunia, lakini bado tunayo safari ya kwenda kufikia malengo
tuliyojiwekea pamoja na mafanikio hayo” Bi. Mavika alisema.
Vilevile Bi. Mavika amesisitiza kuwa ushirikiano
wa Wadau na Taasisi simamizi za Kudhibiti VVU UKIMWI na
Magonjwa Yasiyoambukiza ikiwemo Wizara
ya Afya, Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), na wadau wengine ni muhimu katika kuhakikisha utekelezaji
wa afua hizo unaendana na miongozo ya kitaifa.
Amehitimisha kwa kuwataka Wajumbe wa
Kamati ya Kitaifa na waratibu kutekeleza
majukumu yao kwa weledi kwa kuweka vipaumbele vinavyoendana na hali halisi ya
watumishi na kuhakikisha kuwa kila taasisi ina mpango kazi unaotekelezeka.
Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi Anuai za Jamii na Mratibu wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Mwanaamani Mtoo amemshukuru Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI kwa utayari wake katika utekelezaji wa majukumu yaliyokasimiwa katika kuimarisha afya na ustawi wa Taifa.
Naye Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Kagera Bw. Bwai Biseko akizungumza kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera, amewashukuru waratibu kwa namna ambavyo wameshiriki kikamilifu katika kikao hicho na kutoa wito kwa kila mshiriki kuzingatia na kutekeleza yote yaliyoshauriwa.
Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, ambaye ni Mkurugenzi Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu wa Ofisi hiyo Bi. Leila Mavika akitoa hotuba ya Mgeni Rasmi katika kikao kazi cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa Afua za kudhibiti VVU, UKIMWI na magonjwa Sugu Yasiyoambukiza ya kipindi cha robo ya pili ya Mwaka wa fedha 2025/2026 ngazi ya Mkoa na Taifa kilichofanyika katika ukumbi wa ELCT Bukoba Mkoani Kagera
Mkurugenzi Msaidizi Anuai za Jamii na Mratibu wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukiza, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Mwanaamani Mtoo akitoa neno la shukrani kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI kwa utayari wake katika utekelezaji wa majukumu yaliyokasimiwa katika kuimarisha afya na ustawi wa Taifa wakati wa kikao kazi cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa Afua za kudhibiti VVU, UKIMWI na magonjwa Sugu Yasiyoambukiza ya kipindi cha robo ya pili ya Mwaka wa fedha 2025/2026 ngazi ya Mkoa na Taifa kilichofanyika katika ukumbi wa ELCT Bukoba Mkoani Kagera
Washiriki wa Kikao cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa Afua za kudhibiti VVU, UKIMWI na magonjwa Sugu Yasiyoambukiza ya kipindi cha robo ya pili ya Mwaka wa fedha 2025/2026 ngazi ya Mkoa na Taifa wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Leila Mavika akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati ya kitaifa ya kudhibiti VVU, UKIMWI na magonjwa Sugu Yasiyoambukiza baada ya Mgeni Rasmi kufungua kikao cha Afua kilichofanyika katika ukumbi wa ELCT Bukoba Mkoani Kagera
Kaimu Katibu Tawala Mkoa Mhe. Bwai Biseko
akitoa neno la Utangulizi kabla ya kumkaribisha mwakilishi wa Katibu Mkuu-UTUMISHI
ambaye ni Mkurugenzi Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu Bi. Leila
Mavika katika Ufunguzi wa kikao kazi cha kupokea
taarifa ya utekelezaji wa Afua za kudhibiti VVU, UKIMWI na magonjwa Sugu
Yasiyoambukiza ya kipindi cha robo ya pili ya Mwaka wa fedha 2025/2026 ngazi ya
Mkoa na Taifa kilichofanyika leo tarehe 2
Machi, 2026 katika ukumbi wa ELCT Bukoba Mkoani Kagera.
Mkurugenzi Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu wa
Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bi. Leila Mavika (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi Msaidizi Anuai za Jamii na Mratibu wa VVU, UKIMWI
na Magonjwa Yasiyoambukiza, wa Ofisi hiyo wakati wa kikao cha
kupokea taarifa ya utekelezaji wa Afua za kudhibiti magonjwa
hayo ya kipindi cha robo ya pili ya Mwaka wa fedha 2025/2026 ngazi ya Mkoa na
Taifa kilichofanyika katika ukumbi wa ELCT Bukoba
Mkoani
Kagera.
Mratibu wa Mkoa
wa Kagera Bw. Amosi Adonias akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Muongozo wa
kudhibiti VVU/UKIMWI katika kikao cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa
Afua za magonjwa hayo katika kipindi cha
robo ya pili ya Mwaka wa fedha 2025/2026 ngazi ya Mkoa na Taifa kilichofanyika katika ukumbi wa ELCT Bukoba Mkoani Kagera leo tarehe 2
Machi, 2026.
Mratibu wa Mkoa
wa Kagera Bw. Amosi Adonias akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Muongozo wa
kudhibiti VVU/UKIMWI katika kikao cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa
Afua za magonjwa hayo katika kipindi cha
robo ya pili ya Mwaka wa fedha 2025/2026 ngazi ya Mkoa na Taifa kilichofanyika katika ukumbi wa ELCT Bukoba Mkoani Kagera leo tarehe 2
Machi, 2026.
Mwakilishi wa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bi. Leila Mavika (aliyekaa
katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Waratibu wa Kamati ya kitaifa pamoja na
wajumbe ngazi ya Wizara na Mkoa baada ya kufungua Kikao cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa Afua za kudhibiti VVU, UKIMWI na
magonjwa Sugu Yasiyoambukiza ya kipindi cha robo ya pili ya Mwaka wa fedha
2025/2026 ngazi ya Mkoa na Taifa
Afisa
Ustawi wa jamii Mwandamizi Bi. Juliana Ntukey akiwasilisha mada kuhusu Mwongozo na Waraka wa
kudhibiti VVU, UKIMWI na MSY 2014 wakati
wa kikao kazi cha kupokea taarifa
ya utekelezaji wa Afua za kudhibiti magonjwa hayo ya kipindi cha robo ya pili
ya Mwaka wa fedha 2025/2026 ngazi ya Mkoa na Taifa kilichofanyika katika ukumbi wa ELCT Bukoba
Mkoani
Kagera.
Mwakilishi
wa Mtendaji Mkuu wa Tume ya kudhibiti UKIMWI Tanzania Dr. Hafidh Ameir akitoa
wasilisho kuhusu wakati wa kikao cha kupokea taarifa
ya utekelezaji wa Afua za kudhibiti VVU, UKIMWI na magonjwa Sugu Yasiyoambukiza
ya kipindi cha robo ya pili ya Mwaka wa fedha 2025/2026 ngazi ya Mkoa na Taifa







