Thursday, March 12, 2026

KATIBU MKUU-UTUMISHI AWASISITIZA WATUMISHI WA UMMA KUFANYA KAZI KWA BIDII ILI KULETA TIJA KATIKA JAMII


 

Na. Antonia Mbwambo na Eric Amani-Dodoma.

Tarehe 12 machi, 2026

 

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, amewasisitiza Wajumbe wa Baraza la wafanyakazi la Ofisi yake kufanya kazi kwa bidii na weledi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za utendaji ili kuleta mabadiliko yenye tija kwa maendeleo ya taifa.

 

Bw. Mkomi ameyasema hayo leo tarehe 12 Machi, 2026 wakati wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora uliolenga kupitisha Mpango na Bajeti ya Ofisi hiyo ya Mwaka wa Fedha 2026/27 uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.

“Katika kufikia Utumishi wa Umma uliotukuka, nitoe wito kwa wajumbe wote wa baraza, kutekeleza majukumu yenu ipasavyo ili kutoa huduma bora itakayotatua changamoto za wananchi.” Bw. Mkomi alisema.

 Aidha Katibu Mkuu Mkomi amewataka wajumbe wa mkutano huo kuhakikisha kunakuwa na ushirikishwaji wa Watumishi katika mikakati inayopangwa na  kamati hiyo ili kuongeza uelewa wa masuala ya kiutumishi na kuwa na mtazamo chanya utakaoleta ufanisi katika utendaji wao .

 Ameongeza kuwa ni muhimu kukawa na mafunzo kwa wajumbe wa Baraza hilo ili kuwajengea uwezo kwa matokeo chanya katika maeneo yao ya kazi.

 Bw. Mkomi alimshukuru mwakilishi wa Katibu Mkuu TUGHE Taifa, ambaye ni Mwenyekiti wa TUGHE Mkoa wa Dodoma Bw. Maulidi Kipeneku kwa ushiriki wake katika mkutano huo na kuahidi kuwa Ofisi ya Rais-UTUMISHI itashirikiana na TUGHE wakati wote katika kuhakikisha Baraza linatekeleza majukumu yake kikamilifu.

 Awali Bw. Kipenuke aliipongeza Ofisi hiyo kwa kuzingatia sheria ya kufanya baraza ya wafanyakazi kwa wakati. “Mmekuwa kioo, mabaraza yanafanyika kwa wakati na ni shirikishi, huku akiwatasisitiza wajumbe kutoa michango yao ili kuwawakilisha kwa ufasaha watumishi katika Idara na Vitengo vyao.” Alisisitiza Bw. Kipenuke.   

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiweka Saini katika kitabu cha wageni leo katika uKumbi wa Nyaraka mara baada ya kuwasili kwa ajili ya mkutano wa baraza la wafanyakazi la Ofisi yar a Rais  - UTUMISHI leo  machi  12, 2026 Jijini Dodoma.


Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa TUGHE Taifa ambaye pia mwenyekiti wa TUGHE MKOA wa Dodoma Bw. Maulid Kipeneku akitoa neno la salamu kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - UTUMISHI Bw. Juma Mkomi na washiriki wote wa mkutano wa baraza la wafanyakazi katika ofisi ya Rais – UTUMISHI jijini Dodoma Machi 12, 2026.

Picha ya Pamoja ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiwa pamoja na Washiriki wa wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora mara baada ya Kumalizika kwa Mkutano wa Baraza hilo leo machi 12, 2026 Jijini Dodoma.



Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi katika Ofisi ya Rais – UTUMISHI ambaye pia ni Mkutubi mwandamizi katika kitengo cha Mawasiliano Bi. Halima Rauna akijiitambulisha wa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – UTUMISHI Bw. Juma Mkomi wakati wa utambulisho wa washiriki wote wa Mkutano huo Machi 12, 2026 katika ukumbi wa Nyaraka Uliyopo Jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakipitia agenda za mkutano wa Baraza la Wafanyakazi katika ofisi ya Rais – UTUMISHI leo Macji 12, 2026 jijini Dodoma. 


Afisa Mchumi kutokea Idara ya Mipango Ofisi ya Rais - UTUMISHI Ndg. Rifati H. Almasi akiwasilisha mada kwa Katibu Mkuu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Bw. Juma Mkomi wakati wa uwasilishaji mada katika na Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Machi 12, 2026 Jijini Dodoma

Picha ya Pamoja ya Washiriki wa Mkutano wa Baraza la wafanyakazi  katika Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora katika Mkutano wa baraza hilo uliyofanyika Leo Machi 12, 2026 jijini Dodoma ambapo Mkutano huo uliongozwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - UTUMISHI Bw. Juma Mkomi.



                                                                                                                                                                                             

NAIBU WAZIRI QWARAY ATOA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA KUTUMIA MFUNGO WA MWEZI WA RAMADHANI NA KWARESMA KUJITAFAKARI JUU YA HUDUMA WANAZOZITOA KWA WANANCHI

Na Mwandishi Wetu-Dodoma

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray ametoa wito kwa Watumishi wa Umma nchini kutumia kipindi hiki cha Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani na Mafungo ya Kwaresma kujitafakari juu ya namna wanavyotoa huduma kwa wananchi.

Naibu Waziri Qwaray ametoa wito huo wakati wa futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo katika kipindi hiki ambapo Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo wanakuwa katika mfungo.

Mhe. Qwaray amesema watumishi wa umma wanatakiwa kufanya kazi kwa uadilifu, huruma na unyenyekevu huku wakimtanguliza Mungu hivyo ni vema wakajitafakari  kama hayo yote yanafanyika. 

Ameongeza kuwa, kipindi cha mfungo kisiwe cha kushinda njaa bali iwepo thawabu kwa Mungu ambayo itatokana na huduma bora zitakazotolewa na watumishi hao kwa wananchi itakayoleta matokeo chanya kwa ustawi wa nchi.

Aidha, amepongeza Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa kuwakumbuka wahitaji ambao walijumuika nao katika futari hiyo maalum iliyokutanisha makundi ya watu tofauti ambayo yanasaidia kubadilishana uzoefu ili kuboresha utendakji kazi hasa katika kutoa huduma bora kwa wananchi.

Amesisitiza kuendelea kuiombea nchi na viongozi. “Niwasisitize tuendelee kuiombea nchi yetu na tuitunze amani tuliyonayo, sisi sote ni wamoja na ni Watanzania hatuulizani dini wala kabila,alisisitiza Mhe. Qwaray.

Awali Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Juma Mkomi alisema futari hiyo iliandaliwa kwa lengo la kuwaweka pamoja watu wa makundi mbalimbali hasa katika Mfungo wa Mwezi wa Ramadhani na Kwaresma.

Bw. Mkomi aliongeza kuwa ni fursa nzuri kukutana kwa wakati mmoja kwani ibada hizo huwafanya kuwa wacha Mungu jambo ambalo husaidia watumishi kuwa na maadili ya kuwatendea haki wananchi wanaowahudumia.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na Watendaji na Watumishi wa ofisi hiyo wakati wa futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray kuzungumza na Watendaji na Watumishi wa ofisi hiyo wakati wa futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.


Sehemu ya Watendaji na Watumishi wa ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa kwenye hafla ya futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akiwa katika picha ya pamoja na  Watendaji, Watumishi wa ofisi hiyo na wageni waalikwa mara baada ya kupata futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wakuu wa Taasisi wa Ofisi hiyo mara baada ya kupata  futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma. Wa pili kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa kwenye futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.

Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa kwenye futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.



Tuesday, March 10, 2026

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YAIPONGEZA OFISI YA RAIS-UTUMISHI KWA USIMAMIZI THABITI WA MIRADI YA MAENDELEO KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 10 Machi, 2026.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imeipongeza Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa usimamizi thabiti wa miradi ya maendeleo nchini.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro wakati akiongoza kikao cha Kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.

“Kwa niaba ya Kamati yangu nitoe pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan maana ndiye mwenye ofisi hii, kwa hakika mnafanya kazi nzuri kwa kumwakilisha Mhe. Rais.” Amesema Mhe. Dkt. Ndumbaro

Vilevile, Mhe. Dkt. Ndumbaro amempongeza na kumshukuru Waziri Kikwete kwa taarifa nzuri aliyoiwasilisha kwa Kamati hiyo iliyoelezea kwa kina utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo ambayo itaongeza chachu ya maendeleo nchini.

Mhe. Dkt. Ndumbaro ameiahidi Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora kuwa itashirikiana nayo katika usimamizi wa masuala mbalimbali ili kuleta matokeo chanya kwa ustawi wa Taifa.

Awali akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyotengewa fedha kwa mwaka 2025/2026, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema, utekelezaji wa shughuli zilizopangwa katika kipindi husika umefanyika kwa kuzingatia fedha zilizopatikana pamoja na muda wa upatikanaji wake.

Mhe. Kikwete amesema kuwa, lengo la miradi hiyo ni kuongeza tija nchini lakini pia itaongeza chachu ya utendaji kazi kwa Watumishi wa Umma

Aidha, Mhe. Kikwete ameishukuru na kuiahidi Kamati hiyo kuwa Ofisi anayoisimamia itaendelea kushirikiana nao katika kuimarisha na kuboresha utendaji kazi ili kuleta tija katika kuwahudumia wadau mbalimbali kwa lengo la kujenga na kuimarisha Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akiongoza kikao cha Kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo jijini Dodoma leo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.


Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakiwa katika kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais- UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo jijini Dodoma leo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria katika kikao kilichofanyika Bungeni leo jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akitazama nyaraka zake kabla ya kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria katika kikao kilichofanyika Bungeni leo jijini Dodoma. Kushoto ni Naibu Waziri wake Mhe. Regina Qwaray.


Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakiwa katika kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.

Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakijadili jambo wakati wa kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.


Katibu Mkuu-IKULU, Bw. Mululi Mahendeka (kushoto) na Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (kulia) wakiwa kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.


Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakiwa katika kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi (kulia) na Kamshina wa Maadili Mhe. Jaji (Mst.) Sivangilwa Mwangesi (kushoto) wakiwa katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026


Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakijadili jambo wakati wa kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.

Sehemu ya Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) wakati akiongoza kikao cha Kamati yake na Watendaji wa ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026


Watendaji wa Ofisi ya Rais-IKULU na Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakiwa kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifafanua jambo wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026. 


Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakifuatilia taarifa ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo wakati wa kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.


Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Musa Magufuli (wa kwanza kulia) pamoja na watendaji wa ofisi hiyo wakiwa kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.


Sehemu ya Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) wakati akiongoza kikao cha Kamati yake na Watendaji wa ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifafanua hoja wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026. 

Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akifafanua hoja iliyowasilishwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.


Watendaji wa Ofisi ya Rais-IKULU na Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakiwa kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.