Tuesday, March 31, 2026

MAAFISA RASILIMALIWATU WATAKIWA KUFANYA TATHMINI KWENYE SUALA LA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA

 

Na. Veronica Mwafisi na Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 01 Aprili, 2026.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw, Juma Mkomi ametoa wito kwa Maafisa Rasilimaliwatu kufanya tathmini kwenye suala la uhamisho kwa watumishi wa umma ili kuondoa vikwazo na kuongeza tija ya utendajikazi katika Utumishi wa Umma.

Bw. Mkomi ameyasema hayo leo jijini Dodoma alipokuwa akifunga mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi kwa Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma yaliyokuwa yakifanyika kwa siku tisa kuanzia tarehe 23 Machi hadi 01 Aprili, 2026 jijini Dodoma.

Bw. Mkomi amesema, uhamisho ni haki ya mtumishi na mwajiri kutaka kumtumia mtumishi fulani katika eneo fulani au ni haki ya mwajiri kuendelea kumtumia mtumishi husika sehemu anayotumikia vizuri.

Hivyo, Bw. Mkomi amewataka Maafisa Rasilimaliwatu hao kufanya tathmini katika maeneo yao ya kazi hasa katika Mfumo wa Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma (e-Msawazo)

“Nitoe msisitizo kuhusu tathmini ya mahitaji ya rasilimaliwatu, naamini ninyi ndio wasimamizi wakubwa katika maeneo mengi na ndio mnaoleta taarifa ya masuala husika ya kiutumishi, utaratibu wa uhamisho una vigezo na vinajulikana hivyo ni vema kupata usahihi wa taarifa za watumishi au mahitaji ya watumishi hao pasipo kuwa na vikwazo au mifarakano isiyokuwa na tija kwa sababu ya uhamisho,” amesisitiza Bw. Mkomi.

Aidha, Bw. Mkomi ameongeza kuwa, Maafisa Rasilimaliwatu wana jukumu la kumshauri vizuri mwajiri linapotokea suala la uhamisho kwa mtumishi ni vema kutoa vigezo sahihi baada ya kufanya tathmini ya kutosha.

“Tunatamani umwambie mwajiri uhamishio wa mtumishi huyu tusiutekeleze kwa sababu tathmini tuliyoifanya ya rasilimaliwatu katika eneo letu tuna upungufu wa afisa husika au uhamisho huu tuutekeleze kwa sababu tuna maafisa wa kutosha kadhaa kwenye eneo letu,” amesema Bw, Mkomi

Vilevile, Bw. Mkomi amesema eneo la uhamisho limeonekana kuwa na changamoto kutokana na watumishi wanaoomba uhamisho kuzuiliwa bila kuwa na sababu za kutosha.

Bw. Mkomi amewataka Maafisa hao kufanyia kazi mafunzo yote waliyoyapata watakaporudi kwenye maeneo yao ya kazi ili yakaongeze tija katika Utumishi wa Umma

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini, Bw. Hamis Mkunga amesema jumla ya washiriki 275 wamepatiwa mafunzo hayo hivyo amewataka washiriki hao kwenda kufanyia kazi ili kuleta matokeo chanya katika maeneo yao ya kazi kwa maendeleo ya ofisi au taasisi husika na taifa kwa ujumla.

Akitoa neno la shukrani Mwenyekiti wa Mafunzo hayo, Bi. Isabela Chilumba amemuahidi Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi kuwa kwa niaba ya washiriki wote watazingatia maelekezo ambayo ameyatoa ili waweze kuboresha utendaji kazi kwa ustawi wa Taifa.

 


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akizungumza na Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma wakati akifunga mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyofanyika kuanzia tarehe 23 Machi - 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.


Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini wa Ofisi hiyo Bw. Hamis Mkunga (kushoto) kabla ya kufunga Mafunzo ya Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma kuhusu Mfumo wa e-Watumishi yaliyofanyika kuanzia tarehe 23 Machi - 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 jijini Dododma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 jijini Dododma.

Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Hamis Mkunga (kushoto)  pamoja na Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya Usimamizi na Payrol Jeanfrida Mushumbusi (kulia)  wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo wakati alipokuwa akifunga mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyojumuisha Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma yaliyofanyika kuanzia tarehe 23 Machi - 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma. 

Afisa kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambaye pia ni Mkufunzi wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini wa Ofisi hiyo Bw. Hamis Mkunga (kulia), kabla ya Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) kufunga mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akimkabidhi cheti mmojawapo wa washiriki wa mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyojumuisha Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo hayo leo tarehe 1 Aprili, 2026 Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiteta jambo na Afisa Rasilimaliwatu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Chemba Bi. Zuhura Kizuguto baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyotolewa Jijini Dodoma kuanzia tarehe 23 Machi - 01 Aprili, 2026 kwa Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma .

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akimkabidhi cheti mmojawapo wa washiriki wa mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyojumuisha Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo hayo leo tarehe 1 Aprili, 2026 Jijini Dodoma.