Friday, February 20, 2026

“SERIKALI YADHAMIRIA KUINUA ELIMU NA KUKUZA UCHUMI WA WANATANGA KUPITIA UJENZI WA CHUO CHA UTUMISHI”-Mhe.Kikwete

Na Veronica Mwafisi-Tanga

Tarehe 20.02.2026

Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imedhamiria kuinua elimu na kukuza uchumi wa wananchi katika Mkoa wa Tanga kupitia mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) Kampasi ya Tanga ambao umeanza kutekelezwa katika Kata ya Maweni, Kange tarehe 8 Februari, 2025.

Hayo yamebainishwa leo tarehe 20 Februari, 2026 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete alipokuwa akizungumza na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma na wananchi wa Mkoa wa Tanga mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi huo na kabla ya kuweka jiwe la msingi.

Waziri Kikwete amesema Kampasi hiyo ikikamilika inategemea kuchukua jumla ya wanafunzi 2,000 lakini watakaonufaika sio wanafunzi hao pekee ambao watapata elimu, bali na wananchi ambao watafanya shughuli mbalimbali za maendeleo na kuweza kuinua kipato chao.

Amemshukuru Mhe. Rais kwa kutambua umuhimu wa elimu katika mkoa huo na kutoa maelekezo ya kujenga kampasi hiyo.

Aidha, Mhe. Kikwete amewashukuru na kuwapongeza wananchi wa Mkoa wa Tanga Kange kwa uzalendo wao mkubwa wa kutoa eneo kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo eneo hilo linapojengwa chuo hicho ili watoto wao wapate elimu.

Amesema Serikali itaendelea kushirikiana na wananchi kuhakikisha mambo yote yenye athari chanya yanatekelezwa kwa ufanisi wa hali ya juu.

Ameupongeza uongozi na Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Utumishi wa Umma kwa usimamizi mzuri wa ujenzi. Mimi sio mtaalam wa ujenzi lakini kwa macho unaona kazi iliyofanyika ni nzuri na inaridhisha, hongereni sana,” Mhe. Kikwete ameongeza.

Ametoa wito kwa watendaji wa Kampasi hiyo kuweka mazingira mazuri ya eneo hilo kwa kupanda miti ya matunda na kivuli.

Amewasistiza wananchi kushirikiana na viongozi wa Serikali katika kulinda miundombinu ya Kampasi hiyo na ya miradi mbalimbali ya maendeleo katika mkoa huo. 

Kwa upande wake Mwakilishi wa Katibu Mkuu-UTUMISHI, SACP Ibrahimu Mahumi amemshukuru Mhe. Kikwete kwa maelekezo yake ya kuboresha utendaji kazi ambayo amekuwa akiyatoa mara kwa mara kwa taasisi zilizo chini ya ofisi anayoisimamia.                                                                                                    

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Mhe.   Dadi Kolimba ameishukuru Serikali kwa uamuzi walioufanya wa kujenga Chuo hicho kwani wangeweza kujenga popote                                                                         

“Mhe. Waziri kazi hii nzuri inayoonekana ni maelekezo yako ambayo umekuwa ukiyatoa mara kwa mara kwa watendaji katika taasisi zilizo chini ya Ofisi yako,” ameongeza,

Mhe. Kolimba ameahidi yeye pamoja na viongozi wengine wa mkoa kusimamia kwa umakini ujenzi wa chuo hicho na kukamilika kwa wakati ili kianze kutumika kama ilivyotarajiwa.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa Kampasi hiyo, Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma na Mtendaji Mkuu, Dkt. Ernest Mabonesho amemshukuru Mhe. Kikwete kwa kufanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi na kuweka jiwe la msingi.

Dkt. Mabonesho amesema kukamilika kwa Kampasi hiyo kutasaidia kuokoa fedha nyingi za pango ambazo wamekuwa wakilipa sasa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na wananchi wa Mkoa wa Tanga mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Sehemu ya Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na wananchi wa Mkoa wa Tanga wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) mara baada ya Waziri huyo kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Mwakilishi wa Katibu Mkuu-UTUMISHI, SACP Ibrahimu Mahumi akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) kuzungumza na Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na Wananchi wa Mkoa wa Tanga mara baada ya Waziri huyo kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dr. Ernest Mabonesho akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa Kampasi Chuo cha Utumishi wa Umma Kampasi ya Tanga kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia kwake) mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi katika Kampasi hiyo.


Sehemu ya Viongozi, Wataalam wa ujenzi, Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na Wananchi wa Mkoa wa Tanga wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisisitiza jambo wakati akikagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akijadili jambo na Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dr. Ernest Mabonesho wakati Waziri huyo akikagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga. Wengine ni Watendaji wa TPSC na Wataalam wa Ujenzi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifurahia jambo wakati akizungumza na Wataalam wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga alipokuwa akikagua utekelezaji wa mradi huo. Wengine ni Watendaji wa TPSC


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoka kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga. Wengine ni Watendaji wa TPSC na Wataalam wa Ujenzi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akipanda mti mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Sehemu ya Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na wananchi wa Mkoa wa Tanga wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wanaojenga Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi huo na kuweka jiwe la msingi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi huo na kuweka jiwe la msingi.


Mwonekano wa jengo la mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga.



 

 

Thursday, February 19, 2026

TAARIFA HII IPUUZWE


 

“SISI SOTE TUNAFANYA KAZI KWA NIABA YA MHE.RAIS, TUACHE TABIA YA KUHAMISHA WATUMISHI PALE TUNAPOPATA TEUZI”- Mhe. Kikwete

Na Veronica Mwafisi-Arusha

Tarehe 19.02.2026

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amekea tabia ya baadhi ya Waajiri kuwahamisha watumishi wanaowakuta katika Ofisi walizoteuliwa na kutaka wahamishiwe katika vituo vingine vya kazi.

Waziri Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 19 Februari, 2026 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha wakati akifunga rasmi mkutano wa sita wa Serikali Mtandao ulioanza tarehe 17 Februari, 2026.

Amesema kama ikitokea mtumishi ana tatizo lolote la kiutumishi linalohitaji hatua za kinidhamu, apelekwe kwenye vikao vya kinidhamu ili adhabu stahiki itolewe na sio kuwaonea watu kwasababu ya unyonge wao.

“Nataka niwakumbushe kuwa, kila mmoja aliingia kwa sifa zake, wengine wameingizwa kupitia mitihani ya ajira, wengine kwa nafasi za uteuzi, hivyo kila mmoja akitimiza wajibu wake ni wazi kuwa matokeo mazuri yataonekana.

Aidha, amepiga marufuku watumishi wa umma kutumia barua pepe binafsi kutuma taarifa za ofisi badala ya kutumia barua pepe rasmi za serikali. 

“Ni changamoto kubwa sana, bado tunao watumishi wa umma wanaotumia mitandao binafsi kutuma taarifa rasmi za serikali, tunachokifanya ni jambo la hatari sana, tutumie mifumo yetu iliyotengenezwa na wataalam wetu wa ndani,” Mhe. Kikwete ameongeza.

Waziri Kikwete amewapongeza e-GA kwa kazi nzuri wanayofanya na kuwasisitiza Waajiri kutumia wataalam hao kutengeneza mifumo katika taasisi zao.

Ametoa wito kwa wataalamu wa TEHAMA kuendelea kujifunza kila wakati ili waweze kukabiliana na changamoto mbambali ikiwemo shambulio la mifumo ya TEHAMA.

Akitoa salamu kwa niaba ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro amemshukuru Waziri Kikwete kwa kuona umuhimu wa kuishirikisha kamati hiyo. “Mmetambua uwepo wa mhimili wa Bunge, mngeweza hata kufanya wenyewe bila hata ya kutushirikisha,” ameongeza Mhe. Dkt. Ndumbaro.

Amesema yeye sio mtaalam wa TEHAMA, lakini bado anatambua umuhimu wa serikali mtandao na kuongeza kuwa, kwa dunia ya leo hatuwezi kusonga mbele bila ya TEHAMA.

Amesema, Tanzania imepata mafanikio makubwa ambayo yanatokana na kazi nzuri ya Serikali kupitia Chama Cha Mapinduzi pamoja, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA).

“Sisi kama kamati na Bunge tunatambua mafanikio hayo. Mafanikio ya kupeleka huduma kwa umma, kunganisha mifumo, kutuhakikishia usalama mtandaoni ni kazi nzuri yenye mafanikio makubwa

Tuko tayari kushirikiana na Wizara kuhakikisha changamoto zinazohusu sera, sharia na bajeti zinafanyiwa kazi. Kila mawasiliano ya Bunge yanakwenda kwa mtandao.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Mhandisi Benedict Ndomba amemshukuru Waziri Kikwete pamoja na uongozi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa maelekezo na msisitizo kuhusu uzingatiaji wa Sheria, Kanuni, Viwango na Miongozo ya Serikali Mtandao kwani vimeongeza uzito, mwelekeo na ari mpya kwa washiriki wote. “Tunathamini sana mchango wako na w viongozi wote katika kuendeleza ajenda ya mageuzi ya kidijitali Serikalini,” Mhandisi Ndomba amesisitiza.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Maafisa Masuuli, Maafisa TEHAMA na watumiaji wa Mifumo ya TEHAMA Serikalini wakati akifunga mkutano wa sita wa Serikali Mtandao katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.


Sehemu ya Maafisa Masuuli, Maafisa TEHAMA na watumiaji wa Mifumo ya TEHAMA Serikalini wakiwa kwenye mkutano wa sita wa Serikali Mtandao uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifurahia jambo wakati akielekea kutembelea mabanda mbalimbali kabla ya kufunga mkutano wa sita wa Serikali Mtandao uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika viwanja vya AICC Arusha kwa ajili ya kufunga mkutano wa sita wa Serikali Mtandao.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) akisikiliza maelezo kuhusu mifumo mbalimbali wakati alipotembelea banda la Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) kabla ya kufunga mkutano wa sita wa Serikali Mtandao uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha. Kulia kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA), Mhandisi Benedict Ndomba


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifurahia jambo wakati akitembelea mabanda mbalimbali kabla ya kufunga mkutano wa sita wa Serikali Mtandao uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA), Mhandisi Benedict Ndomba


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifurahia jambo wakati akitembelea mabanda mbalimbali kabla ya kufunga mkutano wa sita wa Serikali Mtandao uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA), Mhandisi Benedict Ndomba


Sehemu ya Washirkiki na Wanakamati wa mkutano wa sita wa Serikali Mtandao wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.

Sehemu ya Maafisa Masuuli, Maafisa TEHAMA na watumiaji wa Mifumo ya TEHAMA Serikalini wakiwa kwenye mkutano wa sita wa Serikali Mtandao uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.

Sehemu ya Maafisa Masuuli, Maafisa TEHAMA na watumiaji wa Mifumo ya TEHAMA Serikalini wakiwa kwenye mkutano wa sita wa Serikali Mtandao uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.