Monday, April 13, 2026

WAZIRI KIKWETE AFUNGUA MKUTANO WA 13 WA KAMATI TENDAJI YA SHIRIKISHO LA MAMLAKA ZA KUPAMBANA NA RUSHWA BARANI AFRIKA ATAJA MAENEO MANNE YATAKAYOSAIDIA KUKABILIANA NA RUSHWA

 Na. Veronica Mwafisi-Arusha

Tarehe 13 Aprili, 2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema ili Afrika iweze kuwa na uwezo uliojitosheleza ni lazima kuwe na azimio endelevu la pamoja la kukabiliana na rushwa.

Mhe. Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 13 Aprili, 2026 wakati akifungua Mkutano wa 13 wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika ulioanza leo katika Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.

Waziri Kikwete ameainisha maeneo manne ya kuchukua hatua za makusudi za kukabiliana na rushwa Barani Afrika ikiwemo kuendelea kuimarisha ushirikiano mipakani kwani rushwa imekuwa ni tatizo la kimataifa ambalo linahusisha mtiririko wa fedha haramu na masuala ya kimtandao, huku akisisitiza kubadilishana habari katika maeneo ya urejeshaji wa mali na uchunguzi wa kifedha.

Amesema ni lazima kukubali kuwa teknolojia ina nguvu katika kukuza uwazi na kupunguza mianya ya rushwa ambapo mifumo ya kidijiti imeongeza uwajibikaji kwa kiasi kikubwa katika ununuzi wa umma, ukusanyaji wa mapato na utoaji wa huduma .

Amesisitiza kuwa ni lazima kukuza uongozi wa kimaadili na uadilifu katika ngazi zote za kijamii kwani vita dhidi ya rushwa huanza na maadili ambayo lazima yaonekane katika utumishi wa umma na tabia binafsi. 

Aidha, ameongeza kuwa ni muhimu kushirikisha wananchi, mashirika ya kiraia, na sekta binafsi kama washirika hai katika mapambano dhidi ya rushwa kwani suala hili sio la mtu mmoja au taasisi moja pekee.

Amesema rushwa ni kikwazo katika utoaji haki na huduma muhimu kama vile afya, elimu na miundombinu kwa wananchi wa kawaida, vilevile ni tishio katika mabadiliko ya kiuchumi na inapunguza kasi ya maendeleo katika mataifa yetu.

“Ni imani yangu kwamba mkutano huu utatumika kama jukwaa muhimu la kuimarisha ushirikiano, kubadilishana uzoefu, na kuimarisha azimio letu la pamoja katika kushughulikia mojawapo ya changamoto sugu zinazoendelea kuikabili Afrika,” Mhe. Kikwete amesisitiza.

 

Amesema katika kupambana na rushwa, Tanzania chini ya uongozi wa Rais Mhe.
Dkt. Samia Suluhu Hassan, imekuwa na dhamira thabiti ya kuendeleza uwazi,
uwajibikaji na utawala bora kwa kuimarisha mifumo ya kisheria na kitaasisi,
mifumo ya usimamizi wa fedha za umma na kuboresha utoaji wa huduma katika
sekta zote,” Mhe. Kikwete amesisitiza.

Ameongeza kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ina jukumu muhimu katika kutekeleza ajenda ya kitaifa ya kupambana na rushwa kwa kuhakikisha rasilimali za umma zinasimamiwa kwa manufaa ya wananchi wote.

Amesema kwa pamoja, tunaweza kuijenga Afrika inayofafanuliwa si kwa rushwa, bali kwa uadilifu, si kwa fursa zilizopotea, bali kwa mafanikio ya pamoja, si kwa mifumo dhaifu, bali na taasisi imara na zinazoaminika. Mkutano huu ukaashirie hatua nyingine muhimu kuelekea siku zijazo.

Akitoa neno la utangulizi, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila, amesema lengo la mkutano huo ni kujadili na kubadiliashana uzoefu kuhusu namna bora ya kukabiliana na rushwa ambalo ni tatizo kubwa katika Bara la Afrika. “Tutabadilishana uzoefu kwani tunatamani rushwa itokomezwe kabisa katika Bara la Afrika,” amesisitiza.

Wajumbe wa Kamati Tendaji ya AAACA ni Wakuu wa Mamlaka za Kuzuia na Kupambana na Rushwa kutoka Nchi 9 Wanachama ambazo ni Egypt, Mali, Cameroon, Congo Brazaville, Algeria, SieraLeone, Burundi, Zimbabwe pamoja na Tanzania.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza wakati akifungua Mkutano wa 13 wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katika Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.


Sehemu ya Washiriki wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akifungua Mkutano wa 13 wa Kamati hiyo uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katia Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.


Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila (kulia) akizungumza jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA), Bw. Ali Ali kabla ya kuanza kwa Mkutano wa 13 wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Barani Afrika uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katika Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.


Sehemu ya Washiriki wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akifungua Mkutano wa 13 wa Kamati hiyo uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katia Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akifurahia jambo na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila (kushoto) kabla Waziri huyo kufungua Mkutano wa 13 wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katika Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.


Sehemu ya Washiriki wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akifungua Mkutano wa 13 wa Kamati hiyo uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katia Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza wakati akifungua Mkutano wa 13 wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katika Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.


Sehemu ya Washiriki wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika (mstari wa mbele) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akifungua Mkutano wa 13 wa Kamati hiyo uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katia Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha. Wengine ni Watendaji na Wakurugenzi wa TAKUKURU. 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifuatilia Mkutano wa 13 wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika mara baada ya kufungua mkutano huo uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katika Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Sehemu ya Washiriki wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Mamlaka za Kupambana na Rushwa Barani Afrika mara baada ya Waziri huyo kufungua Mkutano wa 13 wa Kamati hiyo uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katika Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi, Watendaji na Wakurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mara baada ya Waziri huyo kufungua Mkutano wa 13 wa Kamati hiyo uliofanyika leo tarehe 13 Aprili, 2026 katika Hoteli ya Forest Hill jijini Arusha. 




Friday, April 10, 2026

WAZIRI KIKWETE AISISITIZA WAKALA YA NDEGE ZA SERIKALI KUENDELEA KUSIMAMIA MISINGI IMARA ILIYOACHWA NA BODI YA USHAURI YA TAASISI HIYO ILI KULETA TIJA KWA TAIFA

 

Na. Antonia Mbwambo-Dodoma.

Tarehe 10 Aprili, 2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameisisitiza Wakala ya Ndege za Serikali kuendeleza misingi imara iliyoachwa na Bodi ya Ushauri ya Wakala hiyo hususan katika usimamizi wa rasilimali mbalimbali ili ziweze kutumika ipasavyo na kuleta tija kwa Serikali na Taifa kwa ujumla.

Mhe. Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 10 Aprili, 2026 jijini Dodoma wakati wa hafla fupi ya kuwaaga Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Ndege za Serikali iliyomaliza muda wake.

Waziri Kikwete ameishukuru na kuipongeza Bodi hiyo kwa utendaji kazi mzuri walioufanya wakati wote walipokuwa wakitekeleza majukumu yao ya kumshauri. “Kimuundo, Bodi hii ni chombo cha kumshauri Waziri. Ninakiri kuwa nimekuwa nikipata ushauri wa namna ya kuboresha ufanisi wa Wakala hii ili kuweza kufikia malengo ya Serikali na kupitia ushauri huo, malengo ya Wakala yameweza kufanikiwa na utekelezaji wa masuala mbalimbali unaendelea kufanyika kama ilivyoshauriwa,” Mhe. Kikwete amesisitiza.

Ameongeza kuwa, Bodi hiyo imekuwa ikifanya kazi kwa weledi na uzalendo pamoja na kumpa ushirikiano mkubwa katika utekelezaji wa majukumu na kufanya kazi yake kuwa nyepesi. “Nina kila sababu ya kujivunia mafanikio na hatua mbalimbali za mchango wa Bodi hii katika kufanikisha shughuli za Wakala,” ameongeza.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Ndege za Serikali, Prof. Mhandisi Idrissa Mshoro amemshukuru Waziri Kikwete kwa kuendelea kuiamini Bodi hiyo kwa kipindi chote tangu ilipoteuliwa hadi kukamilisha kipindi cha pili cha miaka mitatu.

Naye Afisa Mtendaji wa Wakala ya Ndege za Serikali, Capt. Budodi Budodi amesema Bodi hiyo ya Ushauri iliyomaliza muda wake ilizinduliwa kuhudumu kwa kipindi cha pili kuanzia mwezi Agosti, 2023 na imefikia ukomo wake kwa mujibu wa Sheria.

Capt. Budodi ameyataja majukumu ya Wakala ya Ndege za Serikali kuwa ni pamoja na kumsafirisha kwa njia ya anga Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Viongozi Wakuu wengine wa Kitaifa, kuratibu na kusimamia ununuzi na ukodishaji wa ndege za Serikali kwa Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) na kusimamia mikataba ya ukodishaji ndege hizo, kufanya matengenezo ya ndege za Serikali zinazotoa huduma kwa Viongozi Wakuu wa Kitaifa na kuhakikisha usimamizi madhubuti wa Wakala.

Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Ndege za Serikali, wakimpokea Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete mara baada ya Waziri huyo kuwasili katika hafla ya kuwaaga wajumbe hao jijini Dodoma. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyevaa miwani) akifurahia jambo wakati alipokuwa katika hafla ya kuwaaga Wajumbe wa
Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Ndege za Serikali iliyofanyika Aprili 10, 2026 jijini Dodoma. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Ndege za Serikali iliyomaliza muda wake wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wajumbe hao iliyofanyika Aprili 10, 2026 Jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Ndege za Serikali, Prof. Mhandisi Idrissa Mshoro wakati Waziri huyo alipokuwa akiwasili katika hafla ya kuwaaga wajumbe hao iliyofanyika Aprili 10, 2026 Jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji wa Wakala ya Ndege za Serikali, Capt. Budodi Budodi akitoa neno la utangulizi kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wajumbe wa Bodi hiyo Jijini Dodoma