Friday, March 27, 2026

KATIBU MKUU MKOMI AWATAKA WADAU WA RASILIMALIWATU KATIKA SEKTA YA UMMA KUPENDEKEZA MKAKATI MADHUBUTI WA SULUHISHO LA UPUNGUFU WA WATUMISHI

 Na. Antonia Mbwambo na Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 27 Machi, 2026.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw, Juma Mkomi amewataka wadau wa Rasilimaliwatu Serikalini kupendekeza mkakati madhubuti utakaosaidia kuepukana na changamoto ya upungufu wa watumishi katika taasisi za umma.

Katibu Mkuu Mkomi ameyasema hayo leo jijini Dodoma alipokuwa akifungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka katika Wizara na Taasisi za Kimkakati kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya mahitaji ya rasilimaliwatu.

Amesema Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ilifanya zoezi la Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika taasisi za umma na kubaini kuwepo kwa upungufu wa watumishi kwenye baadhi ya taasisi na taasisi nyingine kuwepo kwa ziada ya watumishi.

Amesema kufuatia tathmni hiyo, Ofisi iliona ni vema ikaandaa kikao cha wadau hao ili kujadiliana kwa pamoja namna itakavyofaa kutafuta ufumbuzi wa changamoto hiyo ya muda mrefu.

Amesema kila mwaka wakati wa bajeti taasisi za umma zimekuwa na utaratibu wa kuomba watumishi, hivyo mkakati madhubuti uwekwe ili kupata suluhisho la changamoto hiyo ya upungufu wa watumishi.

“Lengo kubwa la kikao kazi hiki ni kupata usahihi wa taarifa za watumishi au mahitaji ya watumishi katika taasisi za umma, kuna maeneo yanahitaji watumishi kimkakati hivyo ni muhimu kuona namna ya kukubaliana katika kuwapata watumishi hao na kujadiliana kwa kina ili kupata mapendekezo yatakayosaidia kuwagawa Watumishi wa ajira mpya na watakaokuwa wakihamia katika vituo vingine vya kazi,” amesisitiza.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Taasisi, Bw. Nolasco Kipanda amesema kupitia kikao kazi hicho Serikali itapata taarifa zilizo sahihi  za mahitaji ya Watumishi wa Umma kwa miaka mitano ijayo.

Akitoa neno la shukrani Mwenyekiti wa Kikao kazi hicho ambaye ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Wizara ya Afya, Bw. Issa Ng’imba alimuahidi Katibu Mkuu Mkomi kuwa watazingatia maelekezo yote ambayo ameyatoa ili waweze kuboresha utendaji kazi kwa maendeleo ya Taifa

 


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akizungumza na washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu (hawapo pichani) kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati kabla ya Katibu huyo kufungua kikao hicho kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi kutoka Idara na Vitengo vya Ofisi hiyo mara baada ya Katibu huyo kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.


Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Wizara ya Nishati Bi. Bahati Mtono akitaka ufafanuzi wa jambo wakati wa majadiliano ya mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa katika kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati kilichofanyika kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma

Wajumbe wa Sekretarieti kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati akifungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati kilichofanyika kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.

Afisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Waziri Mkumbo akiwasilisha mada ya Mfumo wa e-Msawazo na matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za Kimkakati wakati wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati kilichofanyika kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Wizara na Taasisi za kimkakati baada ya Katibu huyo kufungua kikao kazi cha kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi hizo kilichofanyika kilichofanyika Machi 27, 2026 kilichofanyika kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.

Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kwenye kikao hicho kilichofanyika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu baada ya kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati kilichofanyika katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.

Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kwenye kikao hicho kilichofanyika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Taasisi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Nolasco Kipanda akitoa neno la utangulizi, kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Juma Mkomi kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilicholenga  kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati kilichofanyika  kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma

Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kwenye kikao hicho kilichofanyika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.



 

Wednesday, March 25, 2026

 Na. Veronica Mwafisi na Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 26 Machi, 2026.

 

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi amezielekeza Taasisi za Serikali kuanzisha Msimbo Mraba (QR CODE) utakaowezesha kutoa mrejesho wa huduma zinazotolewa na Taasisi hizo kwa wananchi.

Bw. Mkomi ametoa maelekezo hayo leo alipokuwa akifungua kikao kazi cha wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielekroni (e-Mrejesho) Toleo la Pili kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.

Bw. Mkomi amesema ushughulikiaji wa huduma za mrejesho zinazotolewa na Serikali ni utaratibu uliowekwa mahususi kwa lengo la kuimarisha uwajibikaji na usikivu ndani ya Taasisi za Umma pamoja na kukuza misingi ya Utawala Bora.

Katibu Mkuu Mkomi amewataka wasimamizi wa Rasilimaliwatu katika Taasisi hizo kuwa na uelewa wa pamoja katika kutoa huduma na kuona namna ya kupata mrejesho kwa jinsi inavyowaridhisha wahusika katika Utumishi wa Umma.

Vilevile, Bw. Mkomi amewataka washiriki wa kikao kazi hicho kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa Mfumo wa e-Mrejesho katika taasisi zao ili waweze kutoa elimu hiyo kwa watumishi wengine waliopo katika taasisi zao kwa lengo la kuimarisha utendaji kazi.

Kadhalika, Bw. Mkomi ameongeza kuwa ili kuboresha utekelezaji huo wa Mfumo wa e-Mrejesho amewataka Maafisa Tehama kutengeneza QR CODE kwenye taasisi zote ili kuwezesha wananchi kuutumia na kupeleka malalamiko yao au mrejesho kwenye taasisi husika  

“Katika wananchi 100 hautakosa wananchi 60 wenye simu za kupangusa hivyo, huduma hiyo ya       QR CODE kwa asilimia 60 itaenda mbali zaidi kwa muda mfupi,’’ amesema Bw. Mkomi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Bi. Felista Shuli amesema lengo la kikao kazi hicho ni washiriki kuwezeshwa, kupitishwa na kujadili kwa pamoja kuhusu usimamizi na utekelezaji wa mfumo wa mrejesho ambao ni mojawapo ya mifumo iliyowekwa na Serikali kwa lengo la kusimamia uwajibikaji katika Utumishi wa Umma.

Akitoa neno la shukrani kwa mgeni rasmi ambaye ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Mwenyekiti wa Kikao kazi hicho ambaye ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Michael John amemuahidi Katibu Mkuu Mkomi kuwa watazingatia maelekezo yote ambayo ameyatoa ili waweze kuboresha utendaji kazi kwa ustawi wa Taifa.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akizungumza na Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kabla ya kufungua Kikao kazi kuhusu matumizi na Usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma


Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati alipokuwa akifungua kikao kazi hicho kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma


Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati alipokuwa akifungua kikao kazi hicho kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma

Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati alipokuwa akifungua kikao kazi hicho kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felista Shuli (kushoto) akifuatilia majadiliano ya Mada mbalimbali za kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa kikao hicho,  Bw. Michael John.


Wakurugenzi wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakiwa katika kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili wa Ofisi hiyo Bi. Felister Shuli (kulia) baada ya kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.

Mkurugenzi Msaidizi wa Maadili kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Janeth Mishinga akiwasilisha mada kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) toleo la pili katika kikao cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akisalimiana na baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu baada ya kufungua Kikao kazi kuhusu matumizi na Usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akisalimiana na baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu baada ya kufungua Kikao kazi kuhusu matumizi na Usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi  akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kuhusu kujadili matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) kilichofanyika katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi kutoka Ofisi hiyo baada ya kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilichofanyika machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili wa ofisi hiyo Bi.Felista Shuli (kushoto). Kulia ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Michael John ambaye ni Mwenyekiti wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.  

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Sekretarieti ya Ofisi hiyo baada ya kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilichofanyika machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma 



 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Tuesday, March 24, 2026

 KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE  YAMPONGEZA RAIS MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN KWA KUWEKA KIPAUMBELE KWENYE SUALA LA AJIRA

Na. Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 24 Machi, 2026 

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kulipa kipaumbele suala la ajira katika utumishi wa umma. 

Pongezi hizo zimetolewa leo Machi 24, 2026 na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Edwin Swalle wakati akimwakilisha Mwenyekiti wa Kamati hiyo katika kikao cha  kupokea Utekelezaji wa Bajeti ya Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2025/26 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2026/27  kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma .

Amesema kasi ya kutoa vibali vya ajira kwa sasa imekuwa ni kubwa na ya kuridhisha ukilinganisha na miaka iliyopita. “Kwa niaba ya Kamati nipende kutoa pongezi nyingi kwa Mhe. Rais kwa kutoa vibali vya ajira pamoja na wewe Mhe. Waziri Kikwete na wasaidizi wote kwa utekelezaji kwani tumeona msukumo mkubwa kwenye suala la ajira katika Serikali hii ya Awamu ya Sita, hongereni sana,” ameongeza Mhe. Swalle.

Aidha, amewapongeza Viongozi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma kwa ushirikiano kwa kamati hiyo ambao umerahisisha utekelezaji wa majukumu ya kamati.

“Mhe. Waziri Kikwete umekuwa ukitupatia ushirikiano mkubwa sana katika utekelezaji wa majukumu yetu, wewe pamoja watendaji wote wa Ofisi hii, mmefanya kazi yetu kuwa rahisi sana, hata katika ziara ya kamati tuliyoifanya Kanda ya Ziwa hivi karibuni hukuwahi kutuacha, ulikuwa nasi bega kwa bega, tunakupongeza kwa kuonyesha uko makini sana na kazi yako,” ameongeza Mhe. Swalle.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema, Ofisi yake ipo tayari kutoa ushirikiano wowote unaohitajika katika kufanikisha utekelekezaji wa majukumu ya kamati ili kuweza kufikia malengo iliyojiwekea katika kuhudumia wananchi. 





Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Mhe. Edwin Swalle akitoa neno la pongezi kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kwa utendaji mzuri wa Ofisi yake katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria kilicholenga kupokea utekelezaji wa bajeti ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma  

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa maelezo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria kuhusu utekelezaji wa Bajeti ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma  


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani)  wakati akitoa maelezo kuhusu utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma 

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria kilicholenga kupokea utekelezaji wa bajeti ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa neno la shukrani kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria kwa kupokea na kujadili kwa kina kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Ofisi yake kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 jijini Dodoma.

Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakiwa kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma




Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakiwa kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria kilicholenga kupokea utekelezaji wa bajeti ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa neno la shukrani kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria kwa kupokea na kujadili kwa kina kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Ofisi yake kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 jijini Dodoma.

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe.Nyamizi Mhoja (aliyekaa katikati) akitaka ufafanuzi wa jambo baada ya wasilisho la utekelezaji wa bajeti ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe.Dkt Yahaya Nawanda akitaka ufafanuzi wa jambo baada ya wasilisho la utekelezaji wa bajeti ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma 

Katibu Mkuu Ikulu Bw. Mululi Mahendeka (kulia) akiteta jambo na  Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Xavier Daudi (kushoto) wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria,kilicholenga kupokea utekelezaji wa bajeti ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma 

Mkurugenzi wa Mipango kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Cosmas Ngangaji akitoa Ufafanuzi wa jambo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, wakati wa kikao cha kupokea utekelezaji wa bajeti ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma 

 

Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani)  wakati akitoa maelezo kuhusu utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Mick Kiliba akitoa maelezo ya jambo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, wakati wa kikao cha kupokea utekelezaji wa bajeti ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma 

Sehemu ya Wakurugenzi na Wakuu wa Taasisi zilizopo chini ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Waziri wa Ofisi hiyo Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani)  wakati akitoa maelezo kuhusu utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma

 

Sehemu ya wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Waziri wa Ofisi hiyo Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani)  wakati akitoa maelezo kuhusu utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma