Monday, June 29, 2026

JICHO LA PEPMIS, BADO SIKU 1

 


KATIBU MKUU MKOMI AMPONGEZA NA KUMTAKIA HERI KATIBU MTEULE WA TUME YA UTUMISHI WA UMMA, AMUASA KUZINGATIA FALSAFA YA KAZI NA UTU KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Katibu Mkuu ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi amempongeza na kumtakia heri aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda.

Katibu Mkuu Mkomi ameyasema hayo jijini Dodoma baada ya kuhitimishwa kwa mafunzo yanayofanyika kila Jumatatu kwa watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambapo pia alitumia wasaa huo kumuaga Bw. Kipanda.

Bw. Mkomi amemuasa Katibu mteule huyo kutumia falsafa ya kazi na utu wakati wa utekelezaji wa majukumu yake ili aweze kutenda haki katika kufanya maamuuzi.

Amesema, matatizo mengi yanayowapata Watumishi wa Umma wakati mwingine yanatokana na kukosekana kwa utu wa waajiri hivyo, amemtaka Bw. Kipanda kufanya maamuzi yaliyo sahihi ili kutenda haki.

“Ninaamini Bw. Kipanda utaenda kutenda haki na kutuwakilisha vizuri, fanya kazi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na Utu. Taasisi uliyoteuliwa kufanya kazi inahusika na utoaji wa haki kwa Watumishi wa Umma, hivyo pamoja na kutumia taratibu, ukazingatie pia suala la utu katika kufanya maamuzi.

Vilevile, Bw. Mkomi amemuahidi Bw. Kipanda ushirikiano pale atakapohitaji ikiwa ni pamoja na ushauri katika kazi kwani itasaidia kuimarisha zaidi utendaji kazi.

Kwa upande wake Katibu Mteule wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumteua kuiongoza Taasisi hiyo.

Bw. Kipanda amewashukuru Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa kufanya kazi nao kwa muda mrefu na kuomba kuendelea kumpatia ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake mapya kwa maendeleo ya Taifa.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Katibu Mkuu Mstaafu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (kushoto). Kulia ni aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda 

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akizungumza jambo kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda baada ya kumaliza mafunzo kwa watumishi wa ofisi hiyo yaliyolenga kuwajengea uwezo katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa nasaha wakati wa kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda 


Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda (kulia)akipokea keki alipokuwa akiagwa na Watumishi wa Ofisi hiyo mara baada ya kuteuliwa kuwa Katibu wa Tume hiyo. 


Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Nolasco Kipanda ambaye kwa sasa ni Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma akikata keki akiwa anaagwa na watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI jijini Dodoma  


Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda akitoa neno la shukrani kwa Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI alipokuwa akiwaaga katika ofisi hiyo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda (hayupo pichani) wakati akitoa neno la shukrani kwa Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI alipokuwa akiwaaga baada ya kupata teuzi hiyo.


Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bw. Musa Magufuli akimlisha keki aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipandabaada ya kutoa neno la shukrani kwa Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI alipokuwa akiwaaga baada ya kupata teuzi hiyo.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa nasaha wakati wa kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda.