Na Veronica Mwafisi-Tanga
Tarehe 20.02.2026
Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia
Suluhu Hassan imedhamiria kuinua elimu na kukuza uchumi wa wananchi katika Mkoa
wa Tanga kupitia mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) Kampasi
ya Tanga ambao umeanza kutekelezwa katika Kata ya Maweni, Kange tarehe 8
Februari, 2025.
Hayo
yamebainishwa leo tarehe 20 Februari, 2026 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete alipokuwa
akizungumza na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma na wananchi wa Mkoa wa
Tanga mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi huo na kabla ya kuweka jiwe la
msingi.
Waziri
Kikwete amesema Kampasi hiyo ikikamilika inategemea kuchukua jumla ya wanafunzi
2,000 lakini watakaonufaika sio wanafunzi hao pekee ambao watapata elimu, bali
na wananchi ambao watafanya shughuli mbalimbali za maendeleo na kuweza kuinua
kipato chao.
Amemshukuru
Mhe. Rais kwa kutambua umuhimu wa elimu katika mkoa huo na kutoa maelekezo ya
kujenga kampasi hiyo.
Aidha,
Mhe. Kikwete amewashukuru na kuwapongeza wananchi wa Mkoa wa Tanga Kange kwa
uzalendo wao mkubwa wa kutoa eneo kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali
ya maendeleo ikiwemo eneo hilo linapojengwa chuo hicho ili watoto wao wapate
elimu.
Amesema
Serikali itaendelea kushirikiana na wananchi kuhakikisha mambo yote yenye
athari chanya yanatekelezwa kwa ufanisi wa hali ya juu.
Ameupongeza
uongozi na Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Utumishi wa Umma kwa usimamizi mzuri wa
ujenzi. “Mimi sio mtaalam wa ujenzi lakini kwa macho unaona kazi
iliyofanyika ni nzuri na inaridhisha, hongereni sana,” Mhe. Kikwete ameongeza.
Ametoa
wito kwa watendaji wa Kampasi hiyo kuweka mazingira mazuri ya eneo hilo kwa
kupanda miti ya matunda na kivuli.
Amewasistiza
wananchi kushirikiana na viongozi wa Serikali katika kulinda miundombinu ya
Kampasi hiyo na ya miradi mbalimbali ya maendeleo katika mkoa huo.
Kwa
upande wake Mwakilishi wa Katibu Mkuu-UTUMISHI, SACP Ibrahimu Mahumi amemshukuru Mhe. Kikwete kwa maelekezo yake ya
kuboresha utendaji kazi ambayo amekuwa akiyatoa mara kwa mara kwa taasisi
zilizo chini ya ofisi anayoisimamia.
Akizungumza
kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Mhe. Dadi Kolimba ameishukuru Serikali kwa uamuzi
walioufanya wa kujenga Chuo hicho kwani wangeweza kujenga popote
“Mhe. Waziri kazi hii nzuri inayoonekana ni maelekezo yako ambayo umekuwa
ukiyatoa mara kwa mara kwa watendaji katika taasisi zilizo chini ya Ofisi
yako,” ameongeza,
Mhe.
Kolimba ameahidi yeye pamoja na viongozi wengine wa mkoa kusimamia kwa umakini
ujenzi wa chuo hicho na kukamilika kwa wakati ili kianze kutumika kama
ilivyotarajiwa.
Akiwasilisha
taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa Kampasi hiyo, Mkuu wa Chuo cha
Utumishi wa Umma na Mtendaji Mkuu, Dkt. Ernest Mabonesho amemshukuru Mhe.
Kikwete kwa kufanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi na kuweka jiwe la
msingi.
Dkt.
Mabonesho amesema kukamilika kwa Kampasi hiyo kutasaidia kuokoa fedha nyingi za
pango ambazo wamekuwa wakilipa sasa.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na watumishi wa Chuo cha
Utumishi wa Umma (TPSC) na wananchi wa Mkoa wa Tanga mara baada ya kukagua
utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi
ya Tanga.
Sehemu ya Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na wananchi wa Mkoa
wa Tanga wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo
pichani) mara
baada ya Waziri huyo kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla
ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.
Mwakilishi wa Katibu Mkuu-UTUMISHI, SACP Ibrahimu Mahumi akitoa
maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati)
kuzungumza na Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na Wananchi wa Mkoa wa
Tanga mara baada ya Waziri
huyo kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka
jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.
Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha
Utumishi wa Umma Tanzania, Dr. Ernest Mabonesho akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa Kampasi Chuo
cha Utumishi wa Umma Kampasi ya Tanga kwa Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia
kwake) mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa
ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi katika Kampasi hiyo.
Sehemu ya Viongozi, Wataalam wa ujenzi, Watumishi wa Chuo cha
Utumishi wa Umma (TPSC) na Wananchi wa Mkoa wa Tanga wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete
(hayupo pichani) mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla
ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisisitiza jambo
wakati akikagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa
Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete akijadili jambo na Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha
Utumishi wa Umma Tanzania, Dr. Ernest Mabonesho wakati Waziri huyo akikagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo
cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga. Wengine ni Watendaji wa TPSC na Wataalam wa
Ujenzi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifurahia
jambo wakati akizungumza na Wataalam wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga
alipokuwa akikagua utekelezaji wa mradi huo. Wengine ni Watendaji wa TPSC
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoka kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga. Wengine ni Watendaji wa TPSC na Wataalam wa Ujenzi.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete akipanda mti mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi
wa Umma (TPSC) na kuweka
jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.
Sehemu ya Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na
wananchi wa Mkoa wa Tanga wakimsikiliza Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo
hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati waliokaa)
akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wanaojenga Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya
Tanga mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi huo na kuweka jiwe la msingi.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi
wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga
mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi huo na kuweka jiwe la msingi.
Mwonekano wa jengo la mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga.