Na. Veronica Mwafisi-Dar es Salaam
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete amezindua tafiti tumizi sita zitakazokifanya Chuo cha
Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) kuwa kitovu cha maarifa na ushahidi wa
kisayansi kwa ajili ya kuboresha Utumishi wa Umma.
Akizungumza
katika hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma
Tanzania, Waziri Kikwete amesema Serikali inahitaji tafiti zitakazotoa
suluhisho kwa changamoto halisi zinazokabili taasisi za umma.
“Tunahitaji
tafiti zinatakazosaidia kufanya maamuzi sahihi ya sera, kuboresha mifumo ya
kazi, na kuongeza ufanisi wa huduma kwa wananchi”, amesema Mhe. Kikwete.
Aidha,
Waziri Kikwete amewapongeza watafiti wote walioshiriki katika kazi ya utafiti na
kutoa rai kwa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania kuendelea kuimarisha
ushirikiano na Wizara, Idara Zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Mamlaka za
Serikali za Mitaa, Vyuo Vikuu na taasisi nyingine ili tafiti zake ziwe na
mchango mkubwa katika maendeleo ya Taifa.
Waziri
Kikwete ameongeza kuwa, anaamini miaka 25 ijayo itakuwa kipindi cha mafanikio
makubwa zaidi, ambapo Chuo hicho kitaendelea kuwa kinara wa maendeleo ya
rasilimali watu, tafiti tumizi, na ushauri wa kitaalamu kwa ajili ya kuimarisha
Utumishi wa Umma na kuchochea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani
Kikwete akibonyeza kitufe wakati akizindua tafiti
tumizi sita wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo
cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) zitakazokifanya Chuo hicho kuwa kitovu cha
maarifa na ushahidi wa kisayansi kwa ajili ya kuboresha Utumishi wa Umma.
Viongozi mbalimbali, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakipiga makofi baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) kuzindua tafiti tumizi sita wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete
akizungumza baada ya kuzindua tafiti tumizi sita wakati
wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma
Tanzania (TPSC) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano
cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete (kushoto) akifurahia jambo na Katibu Mkuu wa ofisi yake, Bw.
Juma Mkomi (kulia) baada ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI kukabidhiwa Tuzo ya Utambuzi iliyotolewa na Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania
(TPSC) wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo hicho yaliyofanyika
katika Ukumbi wa Kituo
cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI
na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) akielekea katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha
Julius Nyerere wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya
Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC). Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha
Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Florens Turuka na kushoto kwake ni Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu, Chuo cha
Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Dkt. Ernest Mabonesho.
Menejimenti,
Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao baada ya kuzindua tafiti
tumizi sita wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha
Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi
wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius
Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Wadau
na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao baada ya kuzindua tafiti
tumizi sita wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha
Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi
wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius
Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.
Wadau
na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao baada ya kuzindua tafiti
tumizi sita wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha
Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi
wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius
Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.















