Monday, March 30, 2026

WATUMISHI WA UMMA WAHIMIZWA KUONGEZA UWAJIBIKAJI KATIKA KUTOA HUDUMA BORA

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 30 Machi, 2026.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma                                                                                                                                     na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi amewahimiza Watumishi wa Umma kuongeza uwajibikaji katika kuwahudumia wananchi.

Bw. Daudi ametoa wito huo leo alipokuwa akiwapongeza Watumishi wa Ofisi hiyo waliozaliwa mwezi Machi, 2026 mara baada ya kuhitimishwa kwa mafunzo yanayofanyika kila siku ya Jumatatu Mtumba Jijini Dodoma kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi watumishi wa ofisi hiyo.

Bw. Daudi amesema, mtumishi wa umma anapoongeza umri imsaidie kuongeza chachu ya utendajikazi ili kutimiza malengo ya Serikali ya kutoa huduma bora kwa wananchi.

''Nitoe wito kwa Watumishi wa Umma mnapoongeza umri na kusherehekea siku yenu ya kuzaliwa, hakikisheni mnawajibika ipasavyo katika maeneo yenu ya kazi hasa mnapotoa huduma kwa Watumishi wa Umma wenzenu na Wananchi, hakikisheni kuwa mnatimiza malengo ya Serikali katika kutoa huduma bora kwa kila Mtanzania.” amesema Bw. Daudi.


Awali katika mafunzo hayo, Afisa Rasilimaliwatu Mkuu kutoka katika ofisi hiyo, Idara ya Mishahara, Maslahi na Marupurupu, Bi. Magreth Banogile akiwasilisha mada kuhusu Motisha katika Utumishi wa Umma alisema, motisha ni manufaa anayoyapata mtumishi baada ya mshahara kutokana na majukumu anayoyatekeleza hivyo ni wajibu wa kila mtumishi wa umma kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi ili aweze kupata stahiki ya motisha husika.

Ameongeza kuwa baadhi ya motisha katika Utumishi wa Umma ni pamoja na mazingira bora ya kazi, vitendea kazi, fursa za mafunzo, huduma ya usafiri wa kwenda na kurudi kutoka kazini, pamoja na fursa ya muda wa kufanya mazoezi.

Aidha, katika mafunzo hayo kulikuwa na mada mbalimbali zilizowasilishwa na Maafisa kutoka katika Idara hiyo ya Mishahara, Maslahi na Marupurupu ambapo Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi Bw. Baraka Kilagu aliwasilisha mada kuhusu Miundo ya Maendeleo ya Utumishi chini ya Wizara pamoja na Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi, Bw. Imani Mtumbi aliyewasilisha mada kuhusu Miundo ya Mishahara katika Utumishi wa Umma.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi (wa tano kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa ofisi hiyo waliokuwa wakiadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa kwao mwezi Machi, 2026. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Musa Magufuli.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akifurahia jambo alipokuwa akizungumza na Watumishi wa ofisi hiyo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yanayofanyika kila Jumatatu kwenye Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Miundo ya Maendeleo ya Utumishi chini ya Wizara wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika ofisi hiyo jijini Dodoma.


Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Idara ya Mishahara, Maslahi na Marupurupu, Bw. Baraka Kilagu (aliyesimama) akiwasilisha mada kuhusu Miundo ya Maendeleo ya Utumishi chini ya Wizara wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika ofisi hiyo jijini Dodoma. Waliokaa wa kwanza kulia ni Afisa Rasilimaliwatu Mkuu kutoka ofisi hiyo Bi. Magreth Banogile na katikati ni Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi, Bw. Imani Mtumbi


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Miundo ya Mishahara katika Utumishi wa Umma wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo ambayo hufanyika katika ofisi hiyo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Miundo ya Mishahara katika Utumishi wa Umma wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo ambayo hufanyika katika ofisi hiyo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika katika ofisi hiyo jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Musa Magufuli (aliyesimama) akizungumza jambo kabla ya kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi kuzungumza na Watumishi wa ofisi hiyo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji yaliyofanyika katika ofisi hiyo jijini Dodoma.


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakifuatilia wasilisho la mada kuhusu Miundo ya Mishahara katika Utumishi wa Umma wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo ambayo hufanyika katika ofisi hiyo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.


Mhasibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Tumwimbilege Ilomo akikata keki kwa niaba ya Watumishi wa ofisi hiyo wanaoadhimisha  kumbukizi ya kuzaliwa kwao mwezi Machi, 2026.


Mhasibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Tumwimbilege Ilomo (kulia) akimlisha keki Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Maadili, Bi. Felister Shuli (kushoto) kwa niaba ya Watumishi wote waliozaliwa Mwezi Machi, 2026.






Friday, March 27, 2026

KATIBU MKUU MKOMI AWATAKA WADAU WA RASILIMALIWATU KATIKA SEKTA YA UMMA KUPENDEKEZA MKAKATI MADHUBUTI WA SULUHISHO LA UPUNGUFU WA WATUMISHI

 Na. Antonia Mbwambo na Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 27 Machi, 2026.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw, Juma Mkomi amewataka wadau wa Rasilimaliwatu Serikalini kupendekeza mkakati madhubuti utakaosaidia kuepukana na changamoto ya upungufu wa watumishi katika taasisi za umma.

Katibu Mkuu Mkomi ameyasema hayo leo jijini Dodoma alipokuwa akifungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka katika Wizara na Taasisi za Kimkakati kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya mahitaji ya rasilimaliwatu.

Amesema Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ilifanya zoezi la Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika taasisi za umma na kubaini kuwepo kwa upungufu wa watumishi kwenye baadhi ya taasisi na taasisi nyingine kuwepo kwa ziada ya watumishi.

Amesema kufuatia tathmni hiyo, Ofisi iliona ni vema ikaandaa kikao cha wadau hao ili kujadiliana kwa pamoja namna itakavyofaa kutafuta ufumbuzi wa changamoto hiyo ya muda mrefu.

Amesema kila mwaka wakati wa bajeti taasisi za umma zimekuwa na utaratibu wa kuomba watumishi, hivyo mkakati madhubuti uwekwe ili kupata suluhisho la changamoto hiyo ya upungufu wa watumishi.

“Lengo kubwa la kikao kazi hiki ni kupata usahihi wa taarifa za watumishi au mahitaji ya watumishi katika taasisi za umma, kuna maeneo yanahitaji watumishi kimkakati hivyo ni muhimu kuona namna ya kukubaliana katika kuwapata watumishi hao na kujadiliana kwa kina ili kupata mapendekezo yatakayosaidia kuwagawa Watumishi wa ajira mpya na watakaokuwa wakihamia katika vituo vingine vya kazi,” amesisitiza.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Taasisi, Bw. Nolasco Kipanda amesema kupitia kikao kazi hicho Serikali itapata taarifa zilizo sahihi  za mahitaji ya Watumishi wa Umma kwa miaka mitano ijayo.

Akitoa neno la shukrani Mwenyekiti wa Kikao kazi hicho ambaye ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Wizara ya Afya, Bw. Issa Ng’imba alimuahidi Katibu Mkuu Mkomi kuwa watazingatia maelekezo yote ambayo ameyatoa ili waweze kuboresha utendaji kazi kwa maendeleo ya Taifa

 


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akizungumza na washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu (hawapo pichani) kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati kabla ya Katibu huyo kufungua kikao hicho kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi kutoka Idara na Vitengo vya Ofisi hiyo mara baada ya Katibu huyo kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.


Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Wizara ya Nishati Bi. Bahati Mtono akitaka ufafanuzi wa jambo wakati wa majadiliano ya mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa katika kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati kilichofanyika kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma

Wajumbe wa Sekretarieti kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati akifungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati kilichofanyika kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.

Afisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Waziri Mkumbo akiwasilisha mada ya Mfumo wa e-Msawazo na matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za Kimkakati wakati wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati kilichofanyika kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Wizara na Taasisi za kimkakati baada ya Katibu huyo kufungua kikao kazi cha kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi hizo kilichofanyika kilichofanyika Machi 27, 2026 kilichofanyika kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.

Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kwenye kikao hicho kilichofanyika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu baada ya kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati kilichofanyika katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.

Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kwenye kikao hicho kilichofanyika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Taasisi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Nolasco Kipanda akitoa neno la utangulizi, kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Juma Mkomi kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilicholenga  kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati kilichofanyika  kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma

Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kwenye kikao hicho kilichofanyika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.



 

Wednesday, March 25, 2026

 Na. Veronica Mwafisi na Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 26 Machi, 2026.

 

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi amezielekeza Taasisi za Serikali kuanzisha Msimbo Mraba (QR CODE) utakaowezesha kutoa mrejesho wa huduma zinazotolewa na Taasisi hizo kwa wananchi.

Bw. Mkomi ametoa maelekezo hayo leo alipokuwa akifungua kikao kazi cha wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielekroni (e-Mrejesho) Toleo la Pili kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.

Bw. Mkomi amesema ushughulikiaji wa huduma za mrejesho zinazotolewa na Serikali ni utaratibu uliowekwa mahususi kwa lengo la kuimarisha uwajibikaji na usikivu ndani ya Taasisi za Umma pamoja na kukuza misingi ya Utawala Bora.

Katibu Mkuu Mkomi amewataka wasimamizi wa Rasilimaliwatu katika Taasisi hizo kuwa na uelewa wa pamoja katika kutoa huduma na kuona namna ya kupata mrejesho kwa jinsi inavyowaridhisha wahusika katika Utumishi wa Umma.

Vilevile, Bw. Mkomi amewataka washiriki wa kikao kazi hicho kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa Mfumo wa e-Mrejesho katika taasisi zao ili waweze kutoa elimu hiyo kwa watumishi wengine waliopo katika taasisi zao kwa lengo la kuimarisha utendaji kazi.

Kadhalika, Bw. Mkomi ameongeza kuwa ili kuboresha utekelezaji huo wa Mfumo wa e-Mrejesho amewataka Maafisa Tehama kutengeneza QR CODE kwenye taasisi zote ili kuwezesha wananchi kuutumia na kupeleka malalamiko yao au mrejesho kwenye taasisi husika  

“Katika wananchi 100 hautakosa wananchi 60 wenye simu za kupangusa hivyo, huduma hiyo ya       QR CODE kwa asilimia 60 itaenda mbali zaidi kwa muda mfupi,’’ amesema Bw. Mkomi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Bi. Felista Shuli amesema lengo la kikao kazi hicho ni washiriki kuwezeshwa, kupitishwa na kujadili kwa pamoja kuhusu usimamizi na utekelezaji wa mfumo wa mrejesho ambao ni mojawapo ya mifumo iliyowekwa na Serikali kwa lengo la kusimamia uwajibikaji katika Utumishi wa Umma.

Akitoa neno la shukrani kwa mgeni rasmi ambaye ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Mwenyekiti wa Kikao kazi hicho ambaye ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Michael John amemuahidi Katibu Mkuu Mkomi kuwa watazingatia maelekezo yote ambayo ameyatoa ili waweze kuboresha utendaji kazi kwa ustawi wa Taifa.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akizungumza na Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kabla ya kufungua Kikao kazi kuhusu matumizi na Usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma


Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati alipokuwa akifungua kikao kazi hicho kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma


Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati alipokuwa akifungua kikao kazi hicho kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma

Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati alipokuwa akifungua kikao kazi hicho kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Ofisi Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Felista Shuli (kushoto) akifuatilia majadiliano ya Mada mbalimbali za kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa kikao hicho,  Bw. Michael John.


Wakurugenzi wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakiwa katika kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili wa Ofisi hiyo Bi. Felister Shuli (kulia) baada ya kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.

Mkurugenzi Msaidizi wa Maadili kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Janeth Mishinga akiwasilisha mada kuhusu matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) toleo la pili katika kikao cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akisalimiana na baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu baada ya kufungua Kikao kazi kuhusu matumizi na Usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akisalimiana na baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu baada ya kufungua Kikao kazi kuhusu matumizi na Usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) Toleo la pili kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi  akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kuhusu kujadili matumizi na usimamizi wa Mfumo wa Kielektroni (e-Mrejesho) kilichofanyika katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi kutoka Ofisi hiyo baada ya kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilichofanyika machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili wa ofisi hiyo Bi.Felista Shuli (kushoto). Kulia ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Michael John ambaye ni Mwenyekiti wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilichofanyika Machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.  

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Sekretarieti ya Ofisi hiyo baada ya kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilichofanyika machi 26, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma