Na Antonia Mbwambo-Dodoma
Tarehe 8 Juni, 2026
Naibu
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw.
Xavier Daudi amewataka Watumishi wa Umma kuendelea kuzingatia maadili ya kazi,
kuwa na tabia njema na kuwahudumia wananchi kwa weledi ili kuongeza ufanisi wa
huduma za umma utakaochangia katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo
2050.
Bw.
Daudi ametoa rai hiyo wakati akihitimisha mada ya mafunzo kuhusu Usimamizi wa
Utendaji Kazi yaliyotolewa kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi
hao Juni 8, 2026 katika eneo maalumu la
Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Bw.
Daudi alisema, mafanikio ya Taasisi za Umma hayapimwi tu kwa utekelezaji wa
Mipango na Sera, bali pia kwa namna Watumishi wanavyowahudumia Wananchi
wanaowategemea katika kupata huduma. Alisisitiza kuwa tabia njema, uadilifu na
uwajibikaji ni sifa muhimu zinazopaswa kuonekana kwa kila Mtumishi wa Umma.
“Tunapaswa
kutambua kuwa kila Mwananchi anayefika kupata huduma ni mteja muhimu wa Serikali.
Jukumu letu ni kuhakikisha anahudumiwa kwa heshima, usikivu na kwa wakati. Hii
ndiyo njia bora ya kujenga imani ya Wananchi kwa Taasisi za Umma na kuimarisha
utawala bora,” Bw. Daudi alisema.
Aliongeza
kuwa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inalenga kuwa na taifa lenye maendeleo
jumuishi, uchumi imara na huduma bora za kijamii, hali ambayo inahitaji
Watumishi wa Umma kuwa sehemu ya mabadiliko hayo kwa kuzingatia maadili na
kuongeza ufanisi katika kazi zao.
Kwa
upande wake mwezeshaji kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Bw. Oswin Mkinga, alieleza kuwa usimamizi wa utendaji kazi ni
muhimu katika kuboresha matokeo ya Taasisi za Umma kwa kuwa utendaji bora
huanza kwa upangaji mzuri wa malengo, ufuatiliaji wa utekelezaji wake na
tathmini ya mara kwa mara ili kubaini mafanikio na maeneo yanayohitaji
maboresho.
Bw.
Mkinga alisisitiza kuwa, usimamizi wa utendaji kazi ni chombo muhimu katika kuimarisha
uwajibikaji wa Watumishi na kuongeza thamani ya huduma zinazotolewa kwa Wananchi
hivyo, ni lazima kila mtumishi akaelewa mchango wake katika kufanikisha malengo
ya taasisi na taifa kwa ujumla.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi akihitimisha mada ya mafunzo kuhusu Usimamizi wa Utendaji Kazi leo Juni 8, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Baadhi ya Viongozi na Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji katika eneo la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Afisa kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Oswin Mkinga akifafanua mada kuhusu
Usimamizi wa Utendaji Kazi kwa watumishi wa Ofisi hiyo wakati wa mafunzo ambayo
hufanyika kila jumatatu ya wiki katika eneo maalumu la Ofisi hiyo kwa lengo la
kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao.

,%20Huduma%20za%20afya%20kutokea%20Muhimbili,%20MOI,%20BMH,%20JKCI,%20H(7).png)
