Thursday, March 12, 2026

NAIBU WAZIRI QWARAY ATOA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA KUTUMIA MFUNGO WA MWEZI WA RAMADHANI NA KWARESMA KUJITAFAKARI JUU YA HUDUMA WANAZOZITOA KWA WANANCHI

Na Mwandishi Wetu-Dodoma

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray ametoa wito kwa Watumishi wa Umma nchini kutumia kipindi hiki cha Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani na Mafungo ya Kwaresma kujitafakari juu ya namna wanavyotoa huduma kwa wananchi.

Naibu Waziri Qwaray ametoa wito huo wakati wa futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo katika kipindi hiki ambapo Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo wanakuwa katika mfungo.

Mhe. Qwaray amesema watumishi wa umma wanatakiwa kufanya kazi kwa uadilifu, huruma na unyenyekevu huku wakimtanguliza Mungu hivyo ni vema wakajitafakari  kama hayo yote yanafanyika. 

Ameongeza kuwa, kipindi cha mfungo kisiwe cha kushinda njaa bali iwepo thawabu kwa Mungu ambayo itatokana na huduma bora zitakazotolewa na watumishi hao kwa wananchi itakayoleta matokeo chanya kwa ustawi wa nchi.

Aidha, amepongeza Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa kuwakumbuka wahitaji ambao walijumuika nao katika futari hiyo maalum iliyokutanisha makundi ya watu tofauti ambayo yanasaidia kubadilishana uzoefu ili kuboresha utendakji kazi hasa katika kutoa huduma bora kwa wananchi.

Amesisitiza kuendelea kuiombea nchi na viongozi. “Niwasisitize tuendelee kuiombea nchi yetu na tuitunze amani tuliyonayo, sisi sote ni wamoja na ni Watanzania hatuulizani dini wala kabila,alisisitiza Mhe. Qwaray.

Awali Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Juma Mkomi alisema futari hiyo iliandaliwa kwa lengo la kuwaweka pamoja watu wa makundi mbalimbali hasa katika Mfungo wa Mwezi wa Ramadhani na Kwaresma.

Bw. Mkomi aliongeza kuwa ni fursa nzuri kukutana kwa wakati mmoja kwani ibada hizo huwafanya kuwa wacha Mungu jambo ambalo husaidia watumishi kuwa na maadili ya kuwatendea haki wananchi wanaowahudumia.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na Watendaji na Watumishi wa ofisi hiyo wakati wa futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray kuzungumza na Watendaji na Watumishi wa ofisi hiyo wakati wa futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.


Sehemu ya Watendaji na Watumishi wa ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa kwenye hafla ya futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akiwa katika picha ya pamoja na  Watendaji, Watumishi wa ofisi hiyo na wageni waalikwa mara baada ya kupata futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wakuu wa Taasisi wa Ofisi hiyo mara baada ya kupata  futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma. Wa pili kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi


Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa kwenye futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.

Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa kwenye futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.



Tuesday, March 10, 2026

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YAIPONGEZA OFISI YA RAIS-UTUMISHI KWA USIMAMIZI THABITI WA MIRADI YA MAENDELEO KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 10 Machi, 2026.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imeipongeza Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa usimamizi thabiti wa miradi ya maendeleo nchini.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro wakati akiongoza kikao cha Kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.

“Kwa niaba ya Kamati yangu nitoe pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan maana ndiye mwenye ofisi hii, kwa hakika mnafanya kazi nzuri kwa kumwakilisha Mhe. Rais.” Amesema Mhe. Dkt. Ndumbaro

Vilevile, Mhe. Dkt. Ndumbaro amempongeza na kumshukuru Waziri Kikwete kwa taarifa nzuri aliyoiwasilisha kwa Kamati hiyo iliyoelezea kwa kina utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo ambayo itaongeza chachu ya maendeleo nchini.

Mhe. Dkt. Ndumbaro ameiahidi Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora kuwa itashirikiana nayo katika usimamizi wa masuala mbalimbali ili kuleta matokeo chanya kwa ustawi wa Taifa.

Awali akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyotengewa fedha kwa mwaka 2025/2026, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema, utekelezaji wa shughuli zilizopangwa katika kipindi husika umefanyika kwa kuzingatia fedha zilizopatikana pamoja na muda wa upatikanaji wake.

Mhe. Kikwete amesema kuwa, lengo la miradi hiyo ni kuongeza tija nchini lakini pia itaongeza chachu ya utendaji kazi kwa Watumishi wa Umma

Aidha, Mhe. Kikwete ameishukuru na kuiahidi Kamati hiyo kuwa Ofisi anayoisimamia itaendelea kushirikiana nao katika kuimarisha na kuboresha utendaji kazi ili kuleta tija katika kuwahudumia wadau mbalimbali kwa lengo la kujenga na kuimarisha Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akiongoza kikao cha Kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo jijini Dodoma leo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.


Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakiwa katika kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais- UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo jijini Dodoma leo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria katika kikao kilichofanyika Bungeni leo jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akitazama nyaraka zake kabla ya kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria katika kikao kilichofanyika Bungeni leo jijini Dodoma. Kushoto ni Naibu Waziri wake Mhe. Regina Qwaray.


Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakiwa katika kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.

Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakijadili jambo wakati wa kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.


Katibu Mkuu-IKULU, Bw. Mululi Mahendeka (kushoto) na Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (kulia) wakiwa kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.


Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakiwa katika kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi (kulia) na Kamshina wa Maadili Mhe. Jaji (Mst.) Sivangilwa Mwangesi (kushoto) wakiwa katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026


Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakijadili jambo wakati wa kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.

Sehemu ya Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) wakati akiongoza kikao cha Kamati yake na Watendaji wa ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026


Watendaji wa Ofisi ya Rais-IKULU na Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakiwa kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifafanua jambo wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026. 


Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakifuatilia taarifa ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo wakati wa kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.


Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Musa Magufuli (wa kwanza kulia) pamoja na watendaji wa ofisi hiyo wakiwa kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.


Sehemu ya Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) wakati akiongoza kikao cha Kamati yake na Watendaji wa ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifafanua hoja wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026. 

Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akifafanua hoja iliyowasilishwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.


Watendaji wa Ofisi ya Rais-IKULU na Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakiwa kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026. 














































 

Monday, March 9, 2026

WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUZINGATIA ELIMU YA USALAMA MAHALI PA KAZI

Na. Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe: 9 Machi, 2026.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi amewataka watumishi wa Ofisi hiyo kutumia na kuzingatia elimu waliyopewa ya Usalama Mahali Pa Kazi kuepukana na changamoto zinazoweza kujitokeza kutokana dharura mbalimbali ili kuondoa hofu ya kimwili na kiakili wanapokuwa wanawajibika katika maeneo yao ya kazi.

Bw. Daudi amesema hayo Machi 9, 2026 kwa Watumishi wa Ofisi hiyo wakati wa kuhitimisha mafunzo ya uelewa wa Usalama Mahali pa Kazi yaliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.

“Tumepatiwa elimu kuhusu Usalama Mahali pa Kazi, nitoe wito kwenu kuzingatia elimu hii kwa manufaa yetu sote ili kuondokana na hofu na kujenga uwajibikaji ulio bora tutakapokuwa tunatekeleza majukumu yetu katika maeneo ya kazi.” Bw. Daudi alisema.

Aidha, Bw. Daudi amewasisitiza watumishi hao kuzingatia suala la usafi wa mazingira wawapo katika maeneo yao ya kazi jambo ambalo litaongeza ufanisi katika utendajikazi kwani afya bora ni mtaji wa uwajibikaji utakaomwezesha mtumishi wa umma kutoa huduma bora itakayoongeza imani ya Wananchi kwa Serikali yao.

Vilevile, Bw. Daudi amempongeza Mkaguzi wa Mazingira ya Kazi kutoka Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), Bw. Thadei Mwasamila kwa kutoa elimu hiyo kwa ufasaha kwani itasaidia kuongeza chachu ya utendajikazi kwa Waajiri na Watumishi.

Kwa upande wake, Bw. Mwasamila ametoa rai kwa waajiri na watumishi wa umma kuhakikisha wanazuia ajali mahali pa kazi ili kuwa na amani na kuondokana na hofu wanapokuwa wanatekeleza majukumu yao. 

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora akizungumza na Watumishi wa Ofisi hiyo, kuhusu uzingatiaji wa elimu ya  Usalama Mahali Pa Kazi wakati alipokuwa akihitimisha mafunzo hayo yaliyofanyika leo tarehe 9 Machi,2026 Jijini Dodoma

Mkaguzi wa Mazingira ya Kazi kutoka Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), Bw. Thadei Mwasamila akiwasilisha mada ya Usalama Mahali Pa Kazi kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais -UTUMISHI wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yaliyofanyika Machi 9, 2026 katika Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma

Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na mwezeshaji juu ya Usalama Mahali Pa Kazi yaliyofanyika Mtumba Jijini Dodoma

Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu Usalama Mahali Pa Kazi iliyokuwa ikiwasilishwa na Mwezeshaji kutoka Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) Mtumba jijini Dodoma

Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu Usalama Mahali Pa Kazi iliyokuwa ikiwasilishwa na Mwezeshaji kutoka Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) Mtumba jijini Dodoma


Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu Usalama Mahali Pa Kazi iliyokuwa ikiwasilishwa na Mwezeshaji kutoka Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) Mtumba jijini Dodoma

Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na mwezeshaji juu ya Usalama Mahali Pa Kazi yaliyofanyika Mtumba Jijini Dodoma

Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na mwezeshaji juu ya Usalama Mahali Pa Kazi yaliyofanyika Mtumba Jijini Dodoma