Na Veronica Mwafisi-Nyang’hwale
Tarehe 14 Machi, 2026
Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imewapongeza Viongozi
wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watendaji
wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa utekelezaji mzuri wa
Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2025 kuhusiana na mapambano dhidi ya rushwa.
Kauli
hiyo imetolewa leo tarehe 14 Machi, 2026 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt.
Damas Ndumbaro wakati wa ziara ya Kamati hiyo iliyolenga kukagua
mradi wa ujenzi wa jengo la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
(TAKUKURU) Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Akizungumza
kwa niaba ya Kamati yake, Mhe. Dkt. Ndumbaro amesema CCM ilipokuwa inaomba kura
kwa wananchi wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 iliahidi mambo mengi ikiwemo
kupambana na rushwa na kuitokomeza, jambo ambalo limetekelezwa kwa ufasaha kwa
kujenga Ofisi za TAKUKURU katika maeneo mbalimbali nchini na kuanzisha klabu za
wapinga rushwa mashuleni.
“Serikali
ya Awamu ya Sita inatekeleza Ilani, tumeona Ilani imetekelezwa kweli kweli
katika kuzuia na kupamba na rushwa. Chama kiliahidi, sisi kama Wabunge jukumu
letu ni kukagua kuona imetekelezwaje, hapa tunaona ilani imetekelezwa kwa
asilimia100 kwani tumeridhishwa na ujenzi huu wa Ofisi ya TAKUKURU Nyang’hwale,”
ameongeza.
Mhe. Dkt.
Ndumbaro ametoa maelekezo kwa Viongozi wa Ofisi hiyo kuendelea kusimamia ubora
wa majengo yote yatakayojengwa na ujenzi wa ofisi zote za TAKUKURU nchini.
Akitoa
maelezo ya awali ya utekelezaji wa mradi wa jengo la TAKUKURU Halmashauri ya
Wilaya ya Nyang’hwale, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameishukuru Kamati hiyo kwa
maelekezo na miongozi mbalimbali ambayo wamekuwa wakiyatoa na kufanikisha
utekelezaji mzuri wa majukumu ya Ofisi anayoiongoza ikiwemo ujenzi wa jengo
hilo la TAKUKURU.
Mhe.
Kikwete amesema mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi milioni 386 ambapo utekelezaji
wake ulifuata taratibu zote za manunuzi kwa kuongozwa na sheria ya manunuzi na
umetekelezwa kupitia Force Account.
Mhe.
Kikwete ameahidi kuendelea kutekeleza maelekezo yote ambayo yatatolewa na
Kamati hiyo ili kuboresha utendaji kazi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa maendeleo ya taifa.
Akiwasilisha
taarifa ya utekelezaji wa TAKUKURU, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin
Chalamila amesema tangu kuanzishwa kwake TAKUKURU imekuwa ikikabiliwa na uhaba
wa majengo lakini katika kutatua changamoto hiyo, Serikali imekuwa ikijitahidi
kujenga na kutafuta majengo ya kupanga ili kutekeleza majukumu yake ya kuzuia
na kupamba na rushwa.
Amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuweka kipeumbele na kuchukua hatua mbalimbali ili kuiimarisha taasisi hiyo katika utekelezaji wa majukumu yake ikiwemo kutenga bajeti kwa ajili ya kujenga majengo yenye miundombinu ya kisasa na kukarabati majengo ya zamani,” ameongeza Bw. Chalamila
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na
Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akizungumza mara baada ya kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Mwenyekiti wa Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas
Ndumbaro (kulia) akifuatilia jambo wakati walipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge
ya Utawala, Katiba na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani
Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akitoa maelezo ya awali kabla ya
kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro kuzungumza
na Watumishi wa TAKUKURU na Wananchi wakati Kamati hiyo ilipotembelea na
kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge
ya Utawala, Katiba na Sheria wakipata maelezo ya Mradi wa ujenzi wa jengo lililojengwa
katika Wilaya ya Nyang’hwale, mkoani Geita mara baada Wajumbe wa Kamati hiyo
kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU. Watatu kutoka kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa maelezo ya awali kabla ya
kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na
Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro kuzungumza na Watumishi
wa TAKUKURU na Wananchi wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi
wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Mwenyekiti wa Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas
Ndumbaro (Katikati) akifuatilia jambo wakati walipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete na kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila
Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin
Chalamila akieleze utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU kwa Wajumbe
wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria mara baada
ya Wajumbe hao kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo hilo lililopo Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge
ya Utawala, Katiba na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani
Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akitoa maelezo ya awali kabla ya
kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati hiyo kuzungumza na Watumishi wa TAKUKURU na
Wananchi wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo
la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Wakuu
wa Vitengo wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wakimsikiliza
Mwenyekiti wa Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas
Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya Kamati yake kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi
wa jengo la TAKUKURU lililopo
Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Muonekano wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’hwale,
Mkoani Geita ambalo Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala,
Katiba na Sheria walitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo
hilo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (wa pili kutoka kushoto) akifurahia jambo wakati walipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita. Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete na kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale Mhe. Grace Kingalame
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge
ya Utawala, Katiba na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani
Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akitoa maelezo ya awali kabla ya
kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati hiyo kuzungumza na Watumishi wa TAKUKURU na
Wananchi wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo
la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Maafisa
wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani)
alipokuwa akizungumza mara baada ya Kamati yake kutembelea na kukagua mradi wa
ujenzi wa jengo la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Sehemu
ya Watumishi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)
wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na
Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa
akizungumza nao mara baada ya Kamati yake kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi
wa jengo la TAKUKURU lililopo
Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisaini kitabu cha wageni mara baada
ya kuingia katika ofisi za TAKUKURU ambayo ni moja ya Taasisi zilizopo chini ya
ofisi yake ambapo Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria
ilitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale,
Mkoani Geita.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro
(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati hiyo mara baada ya
kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa
jengo la TAKUKURU, Wilaya
ya Nyang’wale, Mkoani Geita.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro
(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo wa
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mara baada ya Kamati hiyo kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa
jengo la TAKUKURU, Wilaya
ya Nyang’wale, Mkoani Geita.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro
(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wanafunzi wa klabu ya wapinga Rushwa
Wilaya ya Nyang’wale,
Mkoani Geita.
























