Thursday, July 9, 2026

MHE. KIKWETE AWASILI WILAYA YA SIKONGE MKOANI TABORA, AENDELEA NA ZIARA YAKE YA KIKAZI KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora akiendelea na ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua, kuzindua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kusikiliza changamoto za wananchi katika Mkoa huo.

 












Wednesday, July 8, 2026

MHE. KIKWETE AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KITUO CHA AFYA NA DARAJA IGUNGA ASISITIZA AMANI KWA MAENDELEO YA TAIFA

 Na. Veronica Mwafisi-Igunga

Tarehe 08 Julai, 2026

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameweka jiwe la msingi katika ujenzi wa kituo cha afya cha Kining’inila na daraja la Nyandekwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora huku akisisitiza kuilinda amani ya nchi kwa maendeleo ya taifa.

 

Akizungumza kwa nyakati tofauti leo tarehe 08 Julai, 2026 katika maeneo hayo, Mhe.  Kikwete amesema maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho cha afya na ujenzi wa daraja hilo yasingekuwepo kama kungekuwa hakuna amani.

 

“Tuendelee kufanya kazi kwa bidii, tuitunze amani ya nchi yetu, tumekusanyika hapa kwasababu tuna amani hivyo tusikubali kurubuniwa kuivuruga amani ya nchi yetu.” Amesisitiza.

 

Amesema, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuweka kipaumbele katika maeneo mbalimbali ikiwemo ujenzi wa vituo vya afya, miundombinu, maji lengo ni kutaka wananchi wafurahie matunda ya nchi yao.

 

“Kituo hiki cha afya cha Kiningínila ni mwanzo tu, kwani mpango wa Serikali ni kujenga majengo mengi zaidi ili mpate huduma mbalimbali ikiwemo ya afya ya mama na mtoto, huduma ya meno na nyingine nyingi,” amesisitiza

 

Aidha, amesema katika Mkoa wa Tabora, Serikali imeajiri watumishi 2200 ikiwemo watumishi wa afya ili wananchi waweze kupata huduma za kitabibu kama ilivyo katika maeneo mengine.

 

Kuhusu ujenzi wa daraja la Nyandekwa, Mhe. Kikwete amesema daraja hilo litaenda kuondoa adha ya muda mrefu ya kivuko iliyokuwa ikikwamisha shughuli za maendeleo ya wakazi wa Kijiji cha Manonga na maeneo jirani.

 

Amesema Mhe. Rais alitoa fedha zaidi ya milioni 700 kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo ili kutatua changamoto ya kivuko.

 

Mhe. Kikwete ameanza ziara ya kikazi ya siku tatu katika Mkoa wa Tabora inayolenga kukagua shughuli za maendeleo katika Mkoa huo ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi wa Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2025.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiweka jiwe la msingi katika Mradi wa ujenzi wa kituo cha afya cha Kining’inila katika Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mara baada ya kuweka jiwe la Msingi katika daraja la Nyandekwa mkoani Tabora wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoka kukagua daraja la Nyandekwa wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora. Wengine ni Viongozi na Wananchi wa Halmashauri hiyo.


Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete alipokuwa akizungumza nao mara baada ya kuweka jiwe la Msingi katika daraja la Nyandekwa mkoani Tabora wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifurahia jambo mara baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi daraja la Nyandekwa wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora. Wengine ni Viongozi na Wananchi wa Halmashauri hiyo.




Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akimsikiliza Dkt. Lucia Kafumo alipokuwa akimueleza jambo baada ya Waziri huyo kukagua Mradi wa ujenzi wa kituo cha afya cha Kining’inila katika Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akikagua Daraja daraja la Nyandekwa wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora. Wengine ni Viongozi na Wananchi wa Halmashauri hiyo.


Mwonekano wa daraja la Nyandekwa lililopo katika kata ya Nyandekwa, katika Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiweka jiwe la msingi katika Daraja daraja la Nyandekwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua na kuzindua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.


Mwonekano wa Nyuma Mradi wa ujenzi wa kituo cha afya cha Kining’inila kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora.

 






MHE. KIKWETE AWASILI MKOANI TABORA KWENYE ZIARA YAKE YA KIKAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora tayari kuanza ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua, kuzindua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kusikiliza changamoto za wananchi katika Mkoa huo.