Tuesday, June 30, 2026
Monday, June 29, 2026
KATIBU MKUU MKOMI AMPONGEZA NA KUMTAKIA HERI KATIBU MTEULE WA TUME YA UTUMISHI WA UMMA, AMUASA KUZINGATIA FALSAFA YA KAZI NA UTU KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU
Na. Veronica Mwafisi-Dodoma
Katibu Mkuu ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma, Bw. Juma Mkomi amempongeza na kumtakia heri aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye
ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda.
Katibu Mkuu Mkomi ameyasema hayo jijini Dodoma
baada ya kuhitimishwa kwa mafunzo yanayofanyika kila Jumatatu kwa watumishi wa
Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambapo pia alitumia wasaa huo kumuaga Bw. Kipanda.
Bw. Mkomi amemuasa Katibu mteule huyo kutumia
falsafa ya kazi na utu wakati wa utekelezaji wa majukumu yake ili aweze kutenda
haki katika kufanya maamuuzi.
Amesema, matatizo mengi yanayowapata Watumishi wa Umma
wakati mwingine yanatokana na kukosekana kwa utu wa waajiri hivyo, amemtaka Bw.
Kipanda kufanya maamuzi yaliyo sahihi ili kutenda haki.
“Ninaamini Bw. Kipanda
utaenda kutenda haki na kutuwakilisha vizuri, fanya kazi kwa kuzingatia Sheria,
Kanuni, Taratibu na Utu. Taasisi uliyoteuliwa kufanya kazi inahusika na utoaji
wa haki kwa Watumishi wa Umma, hivyo pamoja na kutumia taratibu, ukazingatie
pia suala la utu katika kufanya maamuzi.
Vilevile, Bw. Mkomi amemuahidi
Bw. Kipanda ushirikiano pale atakapohitaji ikiwa ni pamoja na ushauri katika
kazi kwani itasaidia kuimarisha zaidi utendaji kazi.
Kwa upande wake Katibu
Mteule wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda amemshukuru Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na
kumteua kuiongoza Taasisi hiyo.
Bw. Kipanda amewashukuru
Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora kwa kufanya kazi nao kwa muda mrefu na kuomba kuendelea kumpatia
ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake mapya kwa maendeleo ya Taifa.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimeti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Katibu Mkuu Mstaafu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (kushoto). Kulia ni aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda
Katibu Mkuu,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akizungumza
jambo kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa
Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya
Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda baada ya kumaliza mafunzo kwa
watumishi wa ofisi hiyo yaliyolenga kuwajengea uwezo katika Mji wa Serikali
Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa nasaha wakati wa kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda
Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda (kulia)akipokea keki alipokuwa akiagwa na Watumishi wa Ofisi hiyo mara baada ya kuteuliwa kuwa Katibu wa Tume hiyo.
Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya
Uendelezaji wa Taasisi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Bw. Nolasco Kipanda ambaye kwa sasa ni Katibu wa Tume ya Utumishi
wa Umma akikata keki akiwa anaagwa na watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI
jijini Dodoma
Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa
Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.
Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco
Kipanda akitoa neno la shukrani
kwa Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI alipokuwa
akiwaaga katika ofisi hiyo Mji wa Serikali
Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye
ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipanda (hayupo pichani) wakati akitoa neno
la shukrani kwa Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI
alipokuwa akiwaaga baada ya kupata teuzi hiyo.
Mkurugenzi wa Idara ya
Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bw. Musa Magufuli akimlisha keki aliyekuwa Mkurugenzi wa
Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya
Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco Kipandabaada ya kutoa neno la shukrani kwa
Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI alipokuwa akiwaaga
baada ya kupata teuzi hiyo.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakimsikiliza Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi
(hayupo pichani) alipokuwa akitoa nasaha wakati wa kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa
Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.
Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nolasco
Kipanda.


