Friday, June 5, 2026
Wednesday, June 3, 2026
UTAWALA BORA NA USIMAMIZI MAKINI WA RASILIMALIWATU NI MSINGI WA UTUMISHI WA UMMA WENYE MATOKEO – MHE. QWARAY
Na
Antonia Mbwambo –Dodoma
Tarehe
3 Juni, 2026
Naibu
Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Regina Qwaray, amewataka Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
Serikalini kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele katika kusimamia haki,
uwajibikaji na uzingatiaji wa sheria katika Utumishi wa Umma ili kuongeza
ufanisi wa utoaji wa huduma kwa wananchi.
Mhe.
Qwaray ameyasema hayo Juni 3, 2026 wakati akifunga Kikao Kazi cha Wakuu wa
Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi waRasilimaliwatu Serikalini kilichowakutanisha
viongozi kutoka Wizara, Wakala, Taasisi za Umma, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka
za Serikali za Mitaa Jijini Dodoma.
Amesema,
mafanikio ya Serikali yanategemea kwa kiwango kikubwa ubora wa usimamizi wa
rasilimaliwatu.
“Rasilimaliwatu ndiyo injini ya maendeleo ya taifa;
isimamiwe kwa weledi, haki na uwajibikaji.” – Mhe. Regina
Qwaray alisema.
Aidha
Mhe. Qwaray alibainisha kuwa Serikali imeendelea kupokea malalamiko
yanayohusiana na ucheleweshaji wa kupandishwa vyeo, malipo ya stahili za
watumishi na ukiukwaji wa taratibu za kiutumishi, hivyo kuwataka wataalamu wa
Utawala na Rasilimaliwatu kuwa washauri waaminifu kwa viongozi wao na walinzi
wa utawala wa sheria katika taasisi wanazozihudumia.
Pia
alisisitiza umuhimu wa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma, matumizi salama
ya teknolojia na ulinzi wa taarifa za Serikali, huku akitoa wito kwa waajiri
kuwajengea watumishi uwezo kuhusu matumizi sahihi ya Akili Unde (AI) na mifumo
ya kidijiti.
Katika
kuongeza ufanisi wa utendaji kazi, aliagiza utekelezaji wa Mfumo wa e-Utendaji
usimamiwe kwa ukaribu zaidi, na kwamba wasimamizi watakaoshindwa kutekeleza
wajibu wao wa kutathmini utendaji wa watumishi wachukuliwe hatua kwa mujibu wa
sheria, kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma.
Ameongeza kuwa kufungwa kwa
kikao hicho hakumaanishi mwisho wa juhudi za kuboresha Utumishi wa Umma, bali
ni hatua ya kuanza kutekeleza kwa vitendo maazimio na maelekezo yaliyokubaliwa.
“Kumalizika
kwa kikao hiki si mwisho wa kazi, bali ni mwanzo wa utekelezaji wa maazimio na
maelekezo yaliyotolewa kwa lengo la kujenga Utumishi wa Umma sikivu, jumuishi, na
wenye matokeo,” alisisitiza Mhe. Qwaray.
Kwa upande wake Katibu
Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi amesema ni matarajio yake kuwa kikao hicho
kitaleta matokeo chanya kwa viongozi hao yatakayoboresha utekelezaji wa
majukumu na kuongea tija katika utumishi wa umma.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza katika kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu (hawapo pichani) wakati Naibu Waziri huyo alipokuwa akifunga kikao kazi kilicholenga kuimarisha utawala na usimamizi wa rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma tarehe 3 Juni, 2026 jijini Dodoma.
Com
Comm
Comments
Comme
Comme
KIKAO KAZI CHA WAKUU WA IDARA NA VITENGO VYA UTAWALA NA USIMAMIZI WA RASILIMALIWATU KATIKA WIZARA NA IDARA ZINAZOJITEGEMEA, WAKALA WA SERIKALI, TAASISI NA MASHIRIKA YA UMMA, SEKRETARIETI ZA MIKOA NA MAMLAKA YA SERIKALI ZA MTAA
Kikao kazi cha siku tatu cha
Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini
kinahitimishwa leo tarehe 3 Juni, 2026 jijini Dodoma na Naibu Waziri,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray.
kikao hicho kilifunguliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete
ambapo katika siku hizo tatu washiriki wamepewa uelewa wa namna ya kuimarisha utawala na usimamizi wa rasilimaliwatu katika Utumishi
wa Umma.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi, akizungumza na Wakuu wa Idara na vitengo vya
Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakati alipokuwa akiongoza majadiliano katika
kikao kazi na watumishi hao kilichofanyika Jijini Dodoma. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa
Utumishi wa Umma wa Ofisi hiyo, SACP. Ibrahimu Mahumi
,%20Huduma%20za%20afya%20kutokea%20Muhimbili,%20MOI,%20BMH,%20JKCI,%20H(7).png)








