Saturday, April 4, 2026
Thursday, April 2, 2026
Tuesday, March 31, 2026
MAAFISA RASILIMALIWATU WATAKIWA KUFANYA TATHMINI KWENYE SUALA LA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA
Na. Veronica Mwafisi na Antonia Mbwambo-Dodoma
Tarehe 01 Aprili, 2026.
Katibu
Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw, Juma Mkomi ametoa
wito kwa Maafisa Rasilimaliwatu kufanya tathmini kwenye suala la uhamisho kwa watumishi
wa umma ili kuondoa vikwazo na kuongeza tija ya utendajikazi katika Utumishi wa
Umma.
Bw.
Mkomi ameyasema hayo leo jijini Dodoma alipokuwa akifunga mafunzo ya Mfumo wa
e-Watumishi kwa Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi
mbalimbali za Umma yaliyokuwa yakifanyika kwa siku tisa kuanzia tarehe 23 Machi
hadi 01 Aprili, 2026 jijini Dodoma.
Bw.
Mkomi amesema, uhamisho ni haki ya mtumishi na mwajiri kutaka kumtumia mtumishi
fulani katika eneo fulani au ni haki ya mwajiri kuendelea kumtumia mtumishi
husika sehemu anayotumikia vizuri.
Hivyo,
Bw. Mkomi amewataka Maafisa Rasilimaliwatu hao kufanya tathmini katika maeneo
yao ya kazi hasa katika Mfumo wa Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika
Utumishi wa Umma (e-Msawazo)
“Nitoe
msisitizo kuhusu tathmini ya mahitaji ya rasilimaliwatu, naamini ninyi ndio
wasimamizi wakubwa katika maeneo mengi na ndio mnaoleta taarifa ya masuala husika
ya kiutumishi, utaratibu wa uhamisho una vigezo na vinajulikana hivyo ni vema kupata
usahihi wa taarifa za watumishi au mahitaji ya watumishi hao pasipo kuwa na
vikwazo au mifarakano isiyokuwa na tija kwa sababu ya uhamisho,” amesisitiza
Bw. Mkomi.
Aidha,
Bw. Mkomi ameongeza kuwa, Maafisa Rasilimaliwatu wana jukumu la kumshauri
vizuri mwajiri linapotokea suala la uhamisho kwa mtumishi ni vema kutoa vigezo
sahihi baada ya kufanya tathmini ya kutosha.
“Tunatamani
umwambie mwajiri uhamishio wa mtumishi huyu tusiutekeleze kwa sababu tathmini tuliyoifanya
ya rasilimaliwatu katika eneo letu tuna upungufu wa afisa husika au uhamisho
huu tuutekeleze kwa sababu tuna maafisa wa kutosha kadhaa kwenye eneo letu,”
amesema Bw, Mkomi
Vilevile,
Bw. Mkomi amesema eneo la uhamisho limeonekana kuwa na changamoto kutokana na
watumishi wanaoomba uhamisho kuzuiliwa bila kuwa na sababu za kutosha.
Bw.
Mkomi amewataka Maafisa hao kufanyia kazi mafunzo yote waliyoyapata
watakaporudi kwenye maeneo yao ya kazi ili yakaongeze tija katika Utumishi wa Umma
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu
Serikalini, Bw. Hamis Mkunga amesema jumla ya washiriki 275 wamepatiwa mafunzo
hayo hivyo amewataka washiriki hao kwenda kufanyia kazi ili kuleta matokeo chanya
katika maeneo yao ya kazi kwa maendeleo ya ofisi au taasisi husika na taifa kwa
ujumla.
Akitoa neno la shukrani Mwenyekiti
wa Mafunzo hayo, Bi. Isabela Chilumba amemuahidi Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi kuwa kwa niaba ya washiriki wote watazingatia
maelekezo ambayo ameyatoa ili waweze kuboresha utendaji kazi kwa ustawi wa
Taifa.

Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo
wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi
mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma
Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo
leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.
Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo
wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi
mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma
Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo
leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Idara ya
Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini wa Ofisi hiyo Bw. Hamis Mkunga (kushoto)
kabla ya kufunga Mafunzo ya Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka
Taasisi mbalimbali za Umma kuhusu Mfumo wa e-Watumishi yaliyofanyika kuanzia
tarehe 23 Machi - 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.
Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo
wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi
mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma
Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo
leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.
Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo
wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka Taasisi
mbalimbali za Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- UTUMISHI Bw. Juma
Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo
leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja
na Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu
na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga
mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 jijini Dododma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja
na Washiriki wa Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi ambao ni Maafisa Rasilimaliwatu
na Maafisa Tawala kutoka Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga
mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 jijini Dododma.
Mkurugenzi wa Idara ya
Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora, Bw. Hamis Mkunga (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya
Usimamizi na Payrol Jeanfrida
Mushumbusi (kulia) wakifuatilia
hotuba ya Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo wakati alipokuwa akifunga mafunzo ya Mfumo
wa e-Watumishi yaliyojumuisha Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka
Taasisi mbalimbali za Umma yaliyofanyika kuanzia tarehe 23 Machi - 01 Aprili,
2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.
Afisa kutoka Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambaye pia ni Mkufunzi wa
Mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Idara
ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini wa Ofisi hiyo Bw. Hamis Mkunga (kulia), kabla ya Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) kufunga
mafunzo hayo leo 01 Aprili, 2026 katika ukumbi wa St. Gaspa Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akimkabidhi cheti mmojawapo wa washiriki wa mafunzo ya Mfumo wa
e-Watumishi yaliyojumuisha Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka
Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo hayo leo tarehe
1 Aprili, 2026 Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiteta jambo na Afisa Rasilimaliwatu kutoka
Halmashauri ya Wilaya ya Chemba Bi. Zuhura Kizuguto baada ya Katibu huyo
kufunga mafunzo ya Mfumo wa e-Watumishi yaliyotolewa Jijini Dodoma kuanzia
tarehe 23 Machi - 01 Aprili, 2026 kwa Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala
kutoka Taasisi mbalimbali za Umma .
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akimkabidhi cheti mmojawapo wa washiriki wa mafunzo ya Mfumo wa
e-Watumishi yaliyojumuisha Maafisa Rasilimaliwatu na Maafisa Tawala kutoka
Taasisi mbalimbali za Umma baada ya Katibu huyo kufunga mafunzo hayo leo tarehe
1 Aprili, 2026 Jijini Dodoma.















