Na. Mwandishi wetu-Dodoma
Tarehe 20 Aprili, 2026.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi
amewakumbusha watumishi wa Ofisi yake kuweka na kutunza kumbukumbu za majukumu
wanayoyafanya kila siku ili kusaidia vizazi vijavyo kufanya marejeo pale
inapotakiwa kwa lengo la kuimarisha uendelevu wa taarifa katika utoaji wa
huduma.
Bw. Daudi ameyasema hayo
Aprili 20, 2026 wakati akihitimisha mafunzo ya uelewa kwa watumishi wa Ofisi
yake kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga
yaliyotolewa katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Aliongeza kuwa, watumishi wa
umma hawanabudi kuzingatia mafunzo ya kimkakati wanayopewa ili kuhakikisha
yanawajengea uwezo stahiki wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
‘’Majukumu ya Serikali
yanaishi, lakini watumishi wa Umma huondoka kutoka kituo kimoja kwenda kingine,
hivyo nyaraka zote zinapaswa kuhifadhiwa ipasavyo kwa kuzingatia usalama na
utaratibu unaofaa ili watumishi wanaobaki na watakaokuja waweze kurejerea’’ Bw.
Daudi alisema.
Aidha Bw. Daudi amewataka
viongozi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa Ofisi yake kufuatilia
na kujiridhisha iwapo mafunzo yanayotolewa kila jumatatu ya wiki yanaongeza
tija na ufanisi katika utendaji kazi.
Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi
wa Huduma na Mifumo ya TEHAMA Serikalini kutoka Ofisi ya Rais, UTUMISHI Bw.
Tiba Manoni amesema, Taasisi yoyote ni lazima ihakikishe inaweka mipango endelevu
ya kushughulikia majanga.
Kadhalika Mkurugenzi huyo
alibainisha kuwa majanga ya asili, ukosefu wa fedha, hitilafu za mifumo ya
teknolojia na magonjwa ya mlipuko ni sehemu ya majanga yanayoweza kutokea na
kupelekea kusitishwa kwa shughuli za utekelezaji wa majukumu na utoaji wa
huduma kwa umma.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Xavier Daudi akizungumza na watumishi wa Ofisi yake kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga wakati
akihitimisha mafunzo ya kuwajengea watumishi hao uelewa yaliyotolewa katika
eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Baadhi ya Wakurugenzi wasaidizi na Watumishi
wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo
ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao yaliyofanyika katika eneo la
Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Baadhi ya Viongozi na Watumishi
wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo
ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao yaliyofanyika katika eneo la
Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma
na Mifumo ya TEHAMA Serikalini kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Tiba Manoni akitoa
elimu kwa watumishi wa Ofisi hiyo kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga
katika mafunzo yaliyofanyika eneo maalum la Ofisi hiyo Aprili 20, 2026 jijini
Dodoma.
Baadhi ya Viongozi na Watumishi
wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo
ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao yaliyofanyika katika eneo la
Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Baadhi ya Viongozi na Watumishi
wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mafunzo
ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi hao yaliyofanyika katika eneo la
Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma.
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma
na Mifumo ya TEHAMA Serikalini kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Tiba Manoni akitoa
elimu kwa watumishi wa Ofisi hiyo kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga
katika mafunzo yaliyofanyika eneo maalum la Ofisi hiyo Aprili 20, 2026 jijini
Dodoma.
Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga iliyotolewa katika mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi hao katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma
Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga iliyotolewa katika mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi hao katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma
Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada kuhusu Mpango Endelevu wa Kushughulikia Majanga iliyotolewa katika mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi hao katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma
