Friday, March 20, 2026
Tuesday, March 17, 2026
WAZIRI KIKWETE ASEMA SERIKALI ITAENDELEA KUWAHUDUMIA NA KUWAENZI VIONGOZI WA KITAIFA WASTAAFU KWA MCHANGO WAO MKUBWA KATIKA MAENDELEO YA TAIFA
Na Veronica Mwafisi-Chato
Tarehe 17 Machi, 2026
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete amesema Serikali itaendelea kuwahudumia na kuwaenzi Viongozi
wa Kitaifa Wastaafu kwa kiwango stahiki kwa mujibu wa sheria na kwa kuzingatia
maelekezo ya mara kwa mara yatakayotolewa na Mamlaka.
Mhe.
Kikwete ametoa kauli hiyo leo tarehe 17 Machi 2026 kwenye kumbukizi ya miaka mitano ya Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, Hayati Dkt John Joseph Magufuli yaliyofanyika Chato mkoani Geita.
Amesema,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ndiyo yenye
dhamana na Matunzo ya Viongozi wa Kitaifa Wastaafu kwa Mujibu wa Hati Idhini
ambayo Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aligawa majukumu kwa Mawaziri na
suala hili la kumbukizi ni mojawapo ya utekelezaji wa Sheria ya Mafao ya
Hitimisho la Kazi kwa Viongozi wa Kisiasa Sura 225 jambo ambalo hata Hayati
Dkt. John Joseph Magufuli, aliwahi kulitolea maelekezo.
“Kwa msingi
huo, tunatoa uhakika wa uendelevu wa huduma bora kwa Viongozi wa Kitaifa
Wastaafu na Wajane wa Viongozi wa Kitaifa Wastaafu,” amesisitiza Mhe. Kikwete.
Aidha,
ameongeza kuwa Rais wa Awamu ya Tano alielekeza kuwa suala la kumbukizi
linatakiwa kufanyika kwa umakini na ubora wa hali ya juu ili kuwafanya viongozi
waliostaafu na wanaojiandaa kustaafu kuwa na ari ya kufanya kazi kubwa ya
kulijenga Taifa wakiwa kazini kutokana na kupata uhakika wa uendelevu wa
mustabali wa maisha yao na kuweka misingi bora ya kukabidhi kijiti cha uongozi
wa nchi yetu.
Mhe. Kikwete
amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan kwa kutoa ruhusa na maelekezo mbalimbali kuhusu kufanyika kwa kumbukizi
hiyo.
“Nikiwa ndiye
Waziri mwenye dhamana na matunzo ya Viongozi wa Kitaifa Wastaafu naomba nikushukuru
wewe binafsi kwa kutoa fedha za kufanikisha shughuli hii sambamba na
kutusimamia katika kufanikisha jambo hili muhimu kwa Ofisi yetu, Serikali kwa
ujumla na Familia ya Hayati Dkt. John Joseph Magufuli, Rais wa Awamu ya Tano wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo hapa inaongozwa Mama Janeth, Mjane wa
Hayati Dkt. John P. J. Magufuli,” ameongeza.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza wakati wa kumbukizi ya
miaka mitano ya Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt John Joseph Magufuli yaliyofanyika Chato
mkoani Geita ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi (hayupo pichani)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi (katikati) akiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (wa
kwanza kushoto) akiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka
Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani
Geita.
Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya
Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt.
John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.
Askofu wa Jimbo Katoliki Rulenge – Ngara,
Mhashamu Severine Niwemugizi akiongoza Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya
Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato,
mkoani Geita.
Sehemu ya Mawaziri na Viongozi wengine wa
Serikali wakiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya
Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt.
John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa kwanza kulia)
akiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha
Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe
Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa
Rasilimaliwatu Bw. Musa Magufuli (Aliyeva suti ya blue) akifuatilia jambo
wakati wa Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais
wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe
Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.
Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha
Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John
Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.
Sehemu ya ndugu, jamaa na marafiki wa familia ya Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli wakiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais huyo iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.
Monday, March 16, 2026
SERIKALI KUPITIA TASAF YAIKOSHA KAMATI YA BUNGE KWA KUTEKELEZA MRADI WA ZAHANATI KATIKA ENEO LENYE CHANGAMOTO YA MIUNDOMBINU
Na Veronica Mwafisi-Mwanza
Tarehe 16 Machi, 2026
Serikali
kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) imepongezwa na Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kwa kutekeleza Mradi
wa Zahanati katika eneo lenye changamoto ya miundombinu na kuokoa maisha ya
wakazi wa eneo hilo.
Kauli
hiyo imetolewa leo tarehe 16 Machi, 2026 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt.
Damas Ndumbaro wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati hiyo iliyolenga kukagua
utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama iliyopo Kata ya Kitangiri,
Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.
Akizungumza
kwa niaba ya kamati yake, Mhe. Dkt.
Ndumbaro amesema ujenzi wa zahanati hiyo ni msaada mkubwa kwa wakazi wa
Mihama na Kata ya Kitangiri ambao ilikuwa ni changamoto kutoka katika eneo hilo
kutafuta huduma sehemu nyingine.
“Kwa changamoto ya kufika huku, niwapongeze
TASAF kwa kutekeleza mradi huu katika eneo hili kwani itaokoa maisha ya
wananchi wa eneo hili na gharama walizokuwa wakitumia kufuata huduma za
matibabu katika eneo lingine.” Ameongeza.
Mhe.
Ndumbaro ameongeza kuwa maendeleo haya ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha
Mapinduzi ambacho kimekusudia kuwajali wananchi wake kwa kuwapa huduma
mbalimbali ikiwemo za kijamii.
Aidha,
ametoa wito kwa uongozi wa Halmashauri hiyo ya Ilemela kuhakikisha zahanati
hiyo inawekwa chini ya Halmashauri hiyo. “TASAF imetekeleza, zahanati hii ni ya
kwenu sasa, mfanye utaratibu iwe chini ya Halmashauri,” amesisitiza Mhe. Dkt.
Ndumbaro.
Naye
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema zahanati ya Mihama ni sehemu ya vielelezo vya
miradi inayotekelezwa na TASAF kwa lengo la kuwahudumia wananchi.
Mhe. Kikwete amewataka wananchi wa Mihama na Kitangiri kuitunza zahanati hiyo ili iweze kuwahudumia kama ilivyokusudiwa.
Ameongeza
kuwa, katika kuhakikisha wananchi wanahudumiwa kikamilifu, katika ajira 12,000
zilizotolewa na Serikali ndani ya siku 100, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemelea
imepewa watumishi wa afya 37 na elimu 40.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa TASAF, Bw. Shadrack Mziray ameishukuru Kamati kwa
kuitembelea zahanati hiyo na kushuhudia maendeleo yaliyofanywa na Serikali
katika eneo hilo.
Akitoa neno
la shukurani kwa niaba ya wananchi wa eneo la Mihama, Bi. Mary Nyanda
ameishukuru Serikali kwa kujenga zahanati katika eneo hilo kwani walikuwa na
uhitaji mkubwa wa zahanati.
“Zahanati
hii ni mkombozi kwetu watu wa Mihama, kwa miaka 25 tumekuwa tukihangaika
kufuata huduma sehemu nyingine, tunaishukuru sana Serikali kwa kutekeleza
hili,” ameongeza Bi. Nyanda.
Kamati ya
Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, imehitimisha ziara yake ya kikazi
ya siku tatu ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Geita
na jijini Mwanza.
Mwenyekiti wa Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas
Ndumbaro akizungumza mara baada ya kukagua
utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo
ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya
Ilemela, Mkoani Mwanza.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani)
alipokuwa akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati
hiyo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro kuzungumza na Watumishi wa Zahanati
ya Mihama na Wananchi wa Mihama wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati hiyo iliyolenga kukagua
utekelezaji wa mradi wa Zahanati hiyo uliotekelezwa na TASAF iliyopo Kata ya
Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha
Mwenyekiti wa Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt, Damas Ndumbaro
wakati wa ziara ya kamati hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya
Mihama uliotekelezwa na TASAF iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri
ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.
Sehemu ya Wauguzi na
Maafisa Tabibu wa Zahanati ya Mihama wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas
Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya Mwenyekiti
huyo na Kamati yake kukagua
utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo
ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya
Ilemela, Mkoani Mwanza.
Mwenyekiti wa Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas
Ndumbaro na Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete
wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakikagua utekelezaji
wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii
(TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela,
Mkoani Mwanza. Wengine ni Viongozi wa Mkoa wa Mwanza, Watendaji wa TASAF na
Mganga Mfawidhi wa Zahanati hiyo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akifurahia jambo na Mkurugenzi
wa TASAF, Bw. Shadrack Mziray (kushoto) wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na
Sheria
iliyolenga kukagua
utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na TASAF iliyopo Kata
ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.
Sehemu ya Wananchi wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas
Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya Mwenyekiti
huyo na Kamati yake kukagua
utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo
ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya
Ilemela, Mkoani Mwanza.
Mwenyekiti wa Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas
Ndumbaro akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Viwanja vya
Zahanati ya Mihama wakati wa ziara ya kikazi iliyolenga
kukagua
utekelezaji wa mradi wa Zahanati hiyo uliotekelezwa
na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya
Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. Kulia ni
Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Edwin Swalle
Mwonekano wa jengo la Zahanati ya Mihami lililojengwa
na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) lililopo katika Kata ya
Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza ambapo Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria ilitembelea
kukagua mradi wa utekelezaji wa Zahanati hiyo.
Mkurugenzi
wa TASAF, Bw. Shadrack Mziray akitoa neno la shukrani kwa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kwa kufanya ziara ya kikazi kutembelea mradi
wa ujenzi wa Zahanati ya Mihama kwa lengo la kukagua
utekelezaji wa mradi wa Zahanati hiyo iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri
ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akijadili jambo na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kikazi kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati hiyo iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. Wa pili kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro
Bi. Mary
Nyanda akitoa shukrani kwa niaba ya Wananchi kwa Serikali kupitia TASAF kwa
kujenga zahanati ya Mihama iliyopo katika Kata ya Kitangiri, Halmashauri
ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.
Wanakikundi cha
Wasikivu-TASAF wakimsikiliza
Mwenyekiti wa Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas
Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya Mwenyekiti
huyo na Kamati yake kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya
Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya
Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.
Mwonekano wa vifaa vya Zahanati ya Mihama iliyopo katika Kata
ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.
Sehemu ya Watendaji wa Mfuko wa
Maendeleo ya Jamii (TASAF) pamoja na Maafisa wa Ulinzi na Usalama wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas
Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya Mwenyekiti
huyo na Kamati yake kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya
Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya
Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.




















