Sunday, March 16, 2025

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YAVUTIWA NA UBUNIFU WA TASAF KWA KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO YENYE UHITAJI KWENYE JAMII


Na Lusungu Helela -  MUHEZA

 

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imesema  imeridhishwa na uwekezaji wa miundombinu ya elimu inayoendelea kutekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika Mikoa ya  Tanga na Pwani  huku ikisema miradi hiyo  iliyoibuliwa ni hitaji kubwa la wananchi katika Mikoa hiyo.

 

Amesema TASAF mbali ya kutoa fedha kwa Walengwa, imeanza kujipambanua kwa kuibua miradi ya maendeleo ya elimu ambayo imekuwa msaada mkubwa kwa watoto ambao wengi wao walikuwa wakikatiza masomo kutokana na kukosekana kwa miundombinu hiyo.

 

Kamati hiyo, imetoa pongezi hizo kwa nyakati tofauti baada ya kutembelea na kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa sita, ofisi zWalimu pamoja matundu 12 ya vyoo katika Shule ya Sekondari Magila  iliyopo katika Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga pamoja na Shule ya Sekondari Mwavi iliyopo Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani  zinazojengwa na TASAF.

 

Madarasa hayo ya kisasa yatasaidia kuwafanya wanafunzi wa maeneo hayo kusoma kwa bidii katika mazingira mazuri na rafiki hali itakayochangia kuongezeka kwa kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi katika shule hizo.

 

Akizungumza leo kwa niaba ya Kamati hiyo mara  baada ya kutembelea miradi hiyo, Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Dkt. Joseph Mhagama amesema, ujenzi wa miundombinu hiyo ya elimu  ni kielelezo na  dhamira ya dhati ya  Serikali ya  kuhakikisha wanafunzi wanatimiza ndoto zao kwa kupata elimu bora ili kutokomeza umaskini katika jamii

 

Tunaipongeza Ofisi ya Rais, menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa usimamizi mzuri wa miradi mbalimbali iliyo chini ya Ofisi hiyo kwani tunaona kazi nzuri zinazofanywa na taasisi hizo, tumejionea miradi ya TASAF ilivyotekelezwa kwa viwango na ubora wa hali ya juu,  miradi ya aina hii ni muhimu sana kwani inachochea ari  ya kusoma kwa wanafunzi wetu,” Mhe. Mhagama alisisitiza.

 

Tumeona ni miradi inayoleta tija na imetekelezwa kwa ubora na thamani ya fedha imeonekana, hii ni kazi nzuri ambayo Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweza kuifanya kupitia TASAF lakini pia kwa  usimamizi mzuri na wananchi wa maeneo husika " ameongeza.

 

Kwa upande wake, Naibu Waziri,  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,  Mhe. Deus Sangu, amesema utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa miundombinu ya utoaji huduma za kijamii unaofanywa na TASAF unalenga kusogeza huduma za kijamii karibu na wanachi  pamoja na kuboresha huduma hizo.

 

TASAF imeweza kujenga shule, madarasa, vituo vya afya, zahanati, madaraja, barabara pamoja na miundombinu ya maji na umwagiliaji, hii yote ni kutaka  kuboresha upatikanaji wa huduma za kijamii kama ambavyo Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa akisisitiza mara kwa mara." amesema Mhe.Sangu

 

Akizungumzia ujenzi wa shule katika Kijiji cha Mwavi Wilayani Bagamoyo, Mhe. Sangu amesema kukosekana kwa shule katika eneo hilo  kulipelekea wanafunzi kutembea umbali mrefu na kushindwa  kuhudhuria shule kupindi cha mvua lakini TASAF itakuwa mkombozi kwa watoto hao kwa kuwa karibu na shule hali itakayosababisha mahudhurio na ufaulu kuwa mzuri tofauti na ilivyokuwa mwanzo. 

 

Mbali na hilo, Mhe. Sangu amesema Kamati imejionea na imeridhika na  thamani halisi ya fedha ya ujenzi miundombinu katika Shule ya Sekondari Magila na hivyo kuwafanya watoto hao kusoma shule katika mazingira mazuri na rafiki kwa ajili ya mustakabali ya maisha yao ya badae.

 

Kamati imejionea baadhi ya majengo ambayo yamechakaa sana yaliyojengwa tangu mwaka 1932 ambayo ni hatarishi na yenye mazingira magumu kwa wanafunzi kusoma kwa bidii lakini TASAF imebadilisha hata mandhari ya eneo hili kwani miundombinu iliyopo inavutia na kuwafanya wanafunzi kusoma kwa bidii’’ amesisitiza Mhe. Sangu

 

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imekagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika Mikoa ya Pwani na Tanga ambapo kesho itaendelea na ziara hiyo katika Mkoa wa Kilimanjaro kukagua miradi ya TASAF na TAKUKURU.





Mwenyekiti wa Kamati ya ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Joseph Mhagama akizungumza na baada ya kutembelea na kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa sita, ofisi zWalimu pamoja matundu 12 ya vyoo katika Shule ya Sekondari Magila  iliyopo katika Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga  zinazojengwa na TASAF.




Naibu Waziri,  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,  Mhe. Deus Sangu akizungumza na baada ya  Wajumbe wa  Kamati ya ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheriakutembelea na kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa sita, ofisi zWalimu pamoja matundu 12 ya vyoo katika Shule ya Sekondari Magila  iliyopo katika Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga  zinazojengwa na TASAF.



Mwenyekiti wa Kamati ya ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Joseph Mhagama akiwa ameongozana na baadhi ya ya  Wajumbe wa  Kamati ya ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria akisalimiana na baadhi ya viongozi  baada ya kuwasili kwa ajili ya  kutembelea na kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa sita, ofisi zWalimu pamoja matundu 12 ya vyoo katika Shule ya Sekondari Magila  iliyopo katika Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga  zinazojengwa na TASAF.




Mwenyekiti wa Kamati ya ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Joseph Mhagama akiwa ameongozana na baadhi ya ya  Wajumbe wa  Kamati ya  Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakisalimiana na baadhi ya wenyeji baada ya juwasili kwa ajili ya   kutembelea na kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa sita, ofisi zWalimu pamoja matundu 12 ya vyoo katika Shule ya Sekondari Magila  iliyopo katika Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga  zinazojengwa na TASAF.


Muonekano wa madarasa yaliyojengwa katika shule ya Sekondari ya Magila kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo katika Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga 




Muonekano wa jengo la jengo la Utawala lililojengwa  katika shule ya Sekondari ya Magila kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo katika Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga 



Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Batlida Burian akizngumza mara baada ya kuwakaribisha ofisini kwake Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria walipowasili Mkoani hapo kwa lengo la kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Mkoani humo


Naibu Waziri,  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,  Mhe. Deus Sangu akisalimiana na baadhi ya wenyeji mara baada ya kuwasili kwa ajili ya kutembelea na kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa sita, ofisi zWalimu pamoja matundu 12 ya vyoo katika Shule ya Sekondari Magila  iliyopo katika Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga  zinazojengwa na TASAF.

Naibu Waziri,  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,  Mhe. Deus Sangu akizungumza na baadhi ya wananchi baada ya kuwasili na Kamati ya Bunge ya Utawala, Katib na Sheria kwa ajili ya kutembelea na kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa sita, ofisi zWalimu pamoja matundu 12 ya vyoo katika Shule ya Sekondari Magila  iliyopo katika Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga  zinazojengwa na TASAF.




NAIBU WAZIRI MHE.SANGU : UTASHI WA KISIASA WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN UMEIWEZESHA TAKUKURU KUWAJIBIKA

Na.Lusungu Helela-KILIMANJARO

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus  Sangu amesema utashi wa kisiasa wa Rais  Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan umeiwezesha  TAKUKURU kupata vitendea kazi na kutimiza majukumu yake kwenye mazingira wezeshi.

Amesema katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita zaidi ya Watumishi 1000 wameajiriwa na TAKUKURU, ikiwa ni jitihada  za Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuiwezesha TAKUKURU.

Mhe.Sangu ametoa kauli hiyo wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la  TAKUKURU,  Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro, ikiwa ni muendelezo wa ziara ya  Kamati hiyo kukagua  miradi mbalimbali iliyotekelezwa na   Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora.

Amesema mbali na magari 88 TAKUKURU iliyowezeshwa, inatarajia kwa mara nyingine tena  kupokea jumla magari 100 ili kuwasaidia  maafisa hao kutekeleza majukumu yao mahali popote na saa yeyote wanakohitajika.

Amesema hiyo ni nia ya dhati ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha  TAKUKURU inakuwa na vitendea kazi vya kutosha na vya kisasa.

"Taasisi yetu sio tu inaziangalia Taasisi nyingine bali imekuwa mfano na kioo kwa Taasisi nyingine katika kuonesha thamani halisi ya fedha iliyotumika katika ujenzi wa jengo hili la Rombo" Mhe. Sangu amefafanua.

Katika hatua nyingine Mhe.Sangu ametoa  pongezi kwa Kamati hiyo  kwani ndiyo imekuwa ikifanya  mambo yatokee, " mmekuwa mkipaza sauti kwa  kufanya mapendekezo ya marekebisho ya bajeti kwenye miradi ya maendeleo kwenye Taasisi yetu ya TAKUKURU" 

Amefafanua kuwa mwaka jana bajeti ya TAKUKURU ilikuwa Sh. Bilion 4.5 ambayo Kamati hiyo iliwatupigania na mwaka huu wa fedha imekuwa Sh. Bil. 6, "Bila kelele ya Kamati yako Mhe.Mwenyekiti tusingepata fedha hizi" amesisitiza
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus  Sangu akizungumza mara baada ya Wajumbe wa Kamati ya  Kudumu ya  Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kutembelea na  kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la  TAKUKURU,  Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro

 

Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Crispin Chalamila akizungumza kabla  Wajumbe wa Kamati ya  Kudumu ya  Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kuanza  kutembelea na  kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la  TAKUKURU,  Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro

 

Mwenyekiti wa Kamati ya  Kudumu ya  Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Joseph  Mhagama (katikati)  akiwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa Kamati hiyo mara baada ya kutembelea na  kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la  TAKUKURU,  Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro. Wengine ni Viongozi na Watumishi wa TAKUKURU
Muonekano wa jengo la  TAKUKURU,  Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro ambapo Wajumbe wa Kamati ya  Kudumu ya  Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria waliptembelea na  kukagua mradi wa ujenzi wa jengo hilo.

 


TAKUKURU NI CHOMBO MUHIMU KWA MAENDELEO YA TAIFA - DKT.MHAGAMA

Na.Lusungu Helela-KILIMANJARO

Mwenyekiti wa Kamati ya  Kudumu ya  Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Joseph  Mhagama amesema Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ni chombo muhimu kwa ustawi na maendeleo ya Taifa la Tanzania na Watu wake.

 

Amesema ndoto ya Tanzania ijayo haiwezi kutimia bila uwepo wa chombo hicho.

 

Mhe. Dkt. Mhagama ametoa kauli hiyo leo  Jumamosi Machi 15, 2025 wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Utawala, Katiba na Sheria ya kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la  TAKUKURU,  Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro  ambapo amesisitiza kuwa suala la TAKUKURU kuwa na majengo yake ya kisasa ni jambo lisiloepukika.

 

Amesema Kamati hiyo iliamua kuweka kipaumbele cha kuhakikisha TAKUKURU inatekeleza majukumu yake ipasavyo ambapo moja ya kipaumbele hicho ni TAKUKURU kuwa na  majengo ya kisasa yatakayokuwa rafiki na wezeshi katika kusimika  vifaa vya kidijitali ili kurahisisha utendaji kazi.

 

"Tumehakikisha TAKUKURU inakuwa na majengo ya kisasa yenye hadhi na faragha ili iweze  kutimiza majukumu yake na sio majengo ya kupanga kama ilivyokuwa mwanzo amesisitiza Mhe. Dkt. Mhagama.

 

Amesema Kamati hiyo imeendelea kuipigania Taasisi hiyo ili iendelee kuongezewa  bajeti ya fedha kila mwaka.

 

Kufuatia hatua hiyo Mhe. Dkt. Mhagama amesema huo ni mwelekeo wa Serikali katika kuhakikisha kuwa TAKUKURU inakuwa chombo huru, chenye uwezo wa kutenda haki kwenye Taifa.

 

"Sisi Wajumbe wa Kamati hii kwa pamoja tunatoa pongezi zetu za dhati kwa  Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kusimama imara kwenye masuala ya rushwa katika Uongozi wake " amesisitiza 

 

Ameongeza kuwa "TAKUKURU  mnafanya kazi yetu ya Kamati kuwa nyepesi, sisi Wanakamati  tunajisikia fahari na heshima kwa jinsi mnavyowatendea Watanzania, hakika tumeridhishwa sana na utendaji wenu" 

 

Akizungumzia kuhusu ujenzi wa jengo hilo, Mhe. Dkt. Mhagama amesema Kamati yake  imeridhishwa na ujenzi wa jengo hilo huku akisisitiza kuwa thamani ya fedha inaonekana dhahiri kuanzia kwenye lango kuu hadi ndani ya jengo.

 

Kwa upande wake, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus  Sangu amesema utashi wa kisiasa wa Rais  Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan umeiwezesha  TAKUKURU kupata vitendea kazi na kutimiza majukumu yake kwenye mazingira wezeshi.

 

Amesema katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita zaidi ya Watumishi 1000 wameajiriwa na TAKUKURU, ikiwa ni jitihada  za Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuiwezesha TAKUKURU.

 

Amesema mbali na magari 88 TAKUKURU iliyowezeshwa, inatarajia kwa mara nyingine tena  kupokea jumla magari 100 ili kuwawezesha maafisa hao kutekeleza majukumu yao mahali popote na saa yeyote wanakohitajika.

 

Amesema hiyo ni nia ya dhati ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha  TAKUKURU inakuwa ni chombo chenye uhalali katika jamii.

 

"Taasisi yetu sio tu inaziangalia Taasisi nyingine bali imekuwa mfano na kioo kwa Taasisi nyingine katika kuonesha thamani halisi ya fedha iliyotumika katika ujenzi wa jengo hili la Rombo" Mhe. Sangu amefafanua.

 

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala Katiba na Sheria imehitimisha ziara yake ya siku tatu ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika Mikoa ya Pwani, Tanga na Kilimanjaro na kukagua mradi wa jengo la Ofisi ya TAKUKURU katika Halmashauri ya Wilaya ya Rombo.

 

 

 

Mwenyekiti wa Kamati ya  Kudumu ya  Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Joseph  Mhagama akizungumza mara baada ya kutembelea na  kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la  TAKUKURU,  Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro

 

Muonekano wa jengo la  TAKUKURU,  Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro ambapo Wajumbe wa Kamati ya  Kudumu ya  Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria waliptembelea na  kukagua mradi wa ujenzi wa jengo hilo.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus  Sangu akizungumza mara baada ya Wajumbe wa Kamati ya  Kudumu ya  Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kutembelea na  kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la  TAKUKURU,  Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro

 

Mwenyekiti wa Kamati ya  Kudumu ya  Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Joseph  Mhagama (katikati)  akiwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa Kamati hiyo mara baada ya kutembelea na  kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la  TAKUKURU,  Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro.

 

Wajumbe wa Kamati ya  Kudumu ya  Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakipata maelezo ya miradi ya ujenzi wa majengo yanayojengwa katika mikoa na wilaya mbalimbali nchini  mara baada Wajumbe wa Kamati hiyo kutembelea na  kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la  TAKUKURU,  Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro

  Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Crispin Chalamila akizungumza kabla  Wajumbe wa Kamati ya  Kudumu ya  Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kuanza  kutembelea na  kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la  TAKUKURU,  Wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro