Monday, February 23, 2026

NAIBU KATIBU MKUU - UTUMISHI BW. XAVIER DAUDI AWAASA WATUMISHI WA UMMA KUWA KARIBU NA FAMILIA ZAO KUEPUSHA MSONGO WA MAWAZO NA ATHARI KATIKA UTENDAJI KAZI.

Na Eric Amani Dodoma, Tanzania

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi, amewahimiza Watumishi wa Umma nchini kutumia muda wao ipasavyo wakiwa pamoja na familia zao ili kuepuka msongo wa mawazo unaoweza kuathiri utendaji kazi wao.

Bw. Daudi ametoa wito huo wakati akizungumza na watumishi wa umma katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa ofisi hiyo leo Februari 23, 2026 jijini Dodoma ili kuimarisha ustawi wa watumishi mahali pa kazi, ambapo alisisitiza kuwa afya ya akili ni nyenzo muhimu katika kuongeza ufanisi na tija katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Amesema kuwa watumishi wengi hawatengi muda wa kutosha wa kupumzika au kuwa karibu na familia zao hali inayoweza kusababisha uchovu wa akili na hatimaye kupunguza ufanisi kazini.

''Ni muhimu kwa watumishi wa umma kuhakikisha wanapata muda wa kuwa na familia zao, kushiriki shughuli za kijamii na kupumzika ili kujenga afya njema ya akili ambayo itawawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi,'' amesema Bw. Daudi.

Kwa upande wake, alieleza kuwa Ofisi ya Rais - UTUMISHI itaendelea kuweka mazingira rafiki ya kazi kwa watumishi ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kwa weledi na ufanisi huku wakizingatia ustawi wao binafsi.

Aidha, Mwezeshaji ambaye ni Mwanasaikolojia, Mshauri Nasaha, Mtaalamu wa Mahusiano na Mwandishi Dkt. Chris Mauki wakati akitoa mafunzo hayo amesisitiza kuwa uwiano mzuri kati ya maisha ya kazi na familia husaidia kuongeza morali kazini, kupunguza msongo wa mawazo pamoja na kuboresha mahusiano kazini na nyumbani.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti Ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Xavier Daudi akizungumza na watumishi wa ofisi hiyo baada ya kukamilika kwa mafunzo ya kuwajengea uwezo ambayo hufanyika kila jumatatu kwenye ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma leo Februari 23, 2026.  


Sehemu ya Wakurugenzi na Wakurugenzi Wasaidizi Ofisi ya Rais – UTUMISHI wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na mwezeshaji Dkt. Chris Mauki (Hayupo kwenye Picha) wakati akitoa mafunzo kuhusu watumishi wa Umma kutumia muda vizuri na familia zao ili kuepusha msongo wa mawazo unaoathari utendaji wa kazi Leo Februari 23, 2026 Dodoma, Tanzania.


Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Utumishi wa Umma SACP Ibrahim Mahumi akitoa neno la Shukrani kwa Menejimenti na Uongozi wa Ofisi hiyo kwa niaba ya watumishi wote wenye kumbukizi ya Siku ya kuzaliwa mwezi Februari Mtumba Jijini Dodoma.


Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakisherekea kumbukizi ya tarehe yao ya kuzaliwa leo Februari 23, 2026 katika Ofisi hiyo iliyopo Mtumba Jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu Bi Leila Mavika akifuatilia kwa kina mada iliyokuwa ikitolea na Mwezeshaji Dkt. Chris Mauki (Hayupo kwenye Picha) februari 23, 2026 katika Mji wa Serikali Mtumba Dodoma.


Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais – UTUMISHI wakimsikiliza mwezeshaji Dkt. Chris Mauki (hayupo Pichani) wakati akitoa mafunzo kuhusu watumishi wa Umma kutumia muda vizuri na familia zao ili Kuepusha msongo wa mawazo unaoathari utendaji wa kazi Februari 23, 2026 Mtumba Jijini Dodoma.



Friday, February 20, 2026

“SERIKALI YADHAMIRIA KUINUA ELIMU NA KUKUZA UCHUMI WA WANATANGA KUPITIA UJENZI WA CHUO CHA UTUMISHI”-Mhe.Kikwete

Na Veronica Mwafisi-Tanga

Tarehe 20.02.2026

Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imedhamiria kuinua elimu na kukuza uchumi wa wananchi katika Mkoa wa Tanga kupitia mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) Kampasi ya Tanga ambao umeanza kutekelezwa katika Kata ya Maweni, Kange tarehe 8 Februari, 2025.

Hayo yamebainishwa leo tarehe 20 Februari, 2026 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete alipokuwa akizungumza na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma na wananchi wa Mkoa wa Tanga mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi huo na kabla ya kuweka jiwe la msingi.

Waziri Kikwete amesema Kampasi hiyo ikikamilika inategemea kuchukua jumla ya wanafunzi 2,000 lakini watakaonufaika sio wanafunzi hao pekee ambao watapata elimu, bali na wananchi ambao watafanya shughuli mbalimbali za maendeleo na kuweza kuinua kipato chao.

Amemshukuru Mhe. Rais kwa kutambua umuhimu wa elimu katika mkoa huo na kutoa maelekezo ya kujenga kampasi hiyo.

Aidha, Mhe. Kikwete amewashukuru na kuwapongeza wananchi wa Mkoa wa Tanga Kange kwa uzalendo wao mkubwa wa kutoa eneo kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo eneo hilo linapojengwa chuo hicho ili watoto wao wapate elimu.

Amesema Serikali itaendelea kushirikiana na wananchi kuhakikisha mambo yote yenye athari chanya yanatekelezwa kwa ufanisi wa hali ya juu.

Ameupongeza uongozi na Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Utumishi wa Umma kwa usimamizi mzuri wa ujenzi. Mimi sio mtaalam wa ujenzi lakini kwa macho unaona kazi iliyofanyika ni nzuri na inaridhisha, hongereni sana,” Mhe. Kikwete ameongeza.

Ametoa wito kwa watendaji wa Kampasi hiyo kuweka mazingira mazuri ya eneo hilo kwa kupanda miti ya matunda na kivuli.

Amewasistiza wananchi kushirikiana na viongozi wa Serikali katika kulinda miundombinu ya Kampasi hiyo na ya miradi mbalimbali ya maendeleo katika mkoa huo. 

Kwa upande wake Mwakilishi wa Katibu Mkuu-UTUMISHI, SACP Ibrahimu Mahumi amemshukuru Mhe. Kikwete kwa maelekezo yake ya kuboresha utendaji kazi ambayo amekuwa akiyatoa mara kwa mara kwa taasisi zilizo chini ya ofisi anayoisimamia.                                                                                                    

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Mhe.   Dadi Kolimba ameishukuru Serikali kwa uamuzi walioufanya wa kujenga Chuo hicho kwani wangeweza kujenga popote                                                                         

“Mhe. Waziri kazi hii nzuri inayoonekana ni maelekezo yako ambayo umekuwa ukiyatoa mara kwa mara kwa watendaji katika taasisi zilizo chini ya Ofisi yako,” ameongeza,

Mhe. Kolimba ameahidi yeye pamoja na viongozi wengine wa mkoa kusimamia kwa umakini ujenzi wa chuo hicho na kukamilika kwa wakati ili kianze kutumika kama ilivyotarajiwa.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa Kampasi hiyo, Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma na Mtendaji Mkuu, Dkt. Ernest Mabonesho amemshukuru Mhe. Kikwete kwa kufanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi na kuweka jiwe la msingi.

Dkt. Mabonesho amesema kukamilika kwa Kampasi hiyo kutasaidia kuokoa fedha nyingi za pango ambazo wamekuwa wakilipa sasa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na wananchi wa Mkoa wa Tanga mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Sehemu ya Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na wananchi wa Mkoa wa Tanga wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) mara baada ya Waziri huyo kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Mwakilishi wa Katibu Mkuu-UTUMISHI, SACP Ibrahimu Mahumi akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) kuzungumza na Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na Wananchi wa Mkoa wa Tanga mara baada ya Waziri huyo kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dr. Ernest Mabonesho akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa Kampasi Chuo cha Utumishi wa Umma Kampasi ya Tanga kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia kwake) mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi katika Kampasi hiyo.


Sehemu ya Viongozi, Wataalam wa ujenzi, Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na Wananchi wa Mkoa wa Tanga wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisisitiza jambo wakati akikagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akijadili jambo na Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dr. Ernest Mabonesho wakati Waziri huyo akikagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga. Wengine ni Watendaji wa TPSC na Wataalam wa Ujenzi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifurahia jambo wakati akizungumza na Wataalam wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga alipokuwa akikagua utekelezaji wa mradi huo. Wengine ni Watendaji wa TPSC


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoka kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga. Wengine ni Watendaji wa TPSC na Wataalam wa Ujenzi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akipanda mti mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Sehemu ya Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) na wananchi wa Mkoa wa Tanga wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho na kabla ya kuweka jiwe la msingi Kampasi ya Tanga.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wanaojenga Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi huo na kuweka jiwe la msingi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi huo na kuweka jiwe la msingi.


Mwonekano wa jengo la mradi wa ujenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) Kampasi ya Tanga.



 

 

Thursday, February 19, 2026