Tuesday, June 2, 2026

KIKAO KAZI CHA WAKUU WA IDARA NA VITENGO VYA UTAWALA NA USIMAMIZI WA RASILIMALIWATU KATIKA WIZARA NA IDARA ZINAZOJITEGEMEA, WAKALA WA SERIKALI, TAASISI NA MASHIRIKA YA UMMA, SEKRETARIETI ZA MIKOA NA MAMLAKA YA SERIKALI ZA MTAA

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Juma Mkomi akizungumza katika kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Wizara na Idara zinazojitegemea, Wakala wa Serikali, Taasisi na Mashirika ya Umma, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka ya Serikali za Mtaa, leo Juni 2, 2026 jijini Dodoma.

Kikao kazi hicho cha siku tatu, kimefunguliwa Juni mosi, 2026 na Waziri wa Nchi Ofisi hiyo Mhe. Ridhiwani Kikwete na kinatarajiwa kufungwa kesho na Naibu Waziri Ofisi ya Rais UTUMISHI Mhe. Regina Qwaray (Mb).

Aidha, kauli mbiu ya kikao kazi hicho ni “Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma Sikivu, Jumuishi, Wenye Matokeo na Uwajibikaji kuelekea Dira 2050”.



Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, akizungumza na Wakuu wa Idara na vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakati alipokuwa akiongoza majadiliano na watumishi hao katika kikao kazi kilichofanyika Jijini Dodoma.

Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala katika ukumbi wa Mabele Hall Jijini Dodoma.


Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi, akifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji katika kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu katika ukumbi wa Mabele Hall jijini Dodoma. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, SACP. Ibrahim Mahumi na kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi wa Ofisi hiyo.


Mkurugenzi wa Mipango kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Cosmas Ngangaji (kulia) akifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji wakati wa Kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu Jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini Bw. Hamis Mkunga Mkunga akiwasilisha mada  kuhusu Usimamizi wa rasilimaliwatu na usafishaji wa taarifa za kiutumishi na mishahara wakati wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu Jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bi Leila Mavika  akiwasilisha mada kuhusu Uratibu wa Ajira za Wtanzania  katika mashirika ya Kikanda na Kimataifa wakati wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu Jijini Dodoma

Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi, Bw. Kadari Singo akiwasilisha mada kwa Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu katika kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Mabele Hall jijini Dodoma


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Bw. Sospeter Mtwale akitoa wito kwa Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu katika Wizara na Idara zinazojitegemea, Wakala wa Serikali, Taasisi na Mashirika ya Umma, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka ya Serikali za Mtaa kuhusu uzingatiaji wa   maadili katika Utumishi wa umma tarehe 2 Juni, 2026 ikiwa ni siku ya pili ya kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Mabele hall jijini Dodoma



Mkurugenzi wa Huduma za Taasisi Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania TFRA Bi. Victoria Elangwa akitoa maelezo ya jambo kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu tarehe 2 Juni, 2026 ikiwa ni siku ya pili kati ya tatu zilizopangwa kikao hicho kufanyika Jijini Dodoma


Washiriki kutoka Sekretarieti Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji wakati wa Kikao kazi
cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu Jijini Dodoma.

Baadhi ya Wakurugenzi wasaidizi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora wakifuatilia mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji wakati wa Kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu tarehe 2 Juni, 2026 Jijini Dodoma




Baadhi ya Wakurugenzi wasaidizi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora wakifuatilia mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji wakati wa Kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu tarehe 2 Juni, 2026 Jijini Dodoma
 

Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia maelezo ya Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo wakati alipokuwa akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu tarehe 2 Juni, 2026 Jijini Dodoma.



Washiriki kutoka Sekretarieti Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji wakati wa Kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu Jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Priscus Kiwango, akiwasilisha mada kuhusu maboresho mbalimbali ya mifumo ambayo yamefanywa na Ofisi hiyo wakati wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu Jijini Dodoma


Baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora wakifuatilia mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji wakati wa Kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu tarehe 2 Juni, 2026 Jijini Dodoma]

Sunday, May 31, 2026

RIDHIWANI: SERIKALI YALIPA ZAIDI YA BILIONI 24 MADAI YA WATUMISHI AONYA WATUMISHI WANAOGHUSHI BARUA ZA UHAMISHO, ASEMA 6 MBARONI KESI UHUJUMU UCHUMI

Na. Jawadu Kinyobwa


Serikali imeendelea kuboresha ustawi wa watumishi wa umma kwa kulipa malimbikizo ya mishahara yenye thamani ya Tsh. Bilipni 24,699,256,645.7 na kulipa watumishi 1,249 waliokoma utumishi yenye thamani ya zaidi ya Tsh. Bilioni 5,548,386,177.90.


Hayo yamebainishwa Juni Mosi, 2026 Mabele Hall jijini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb) katika ufunguzi wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Wizara na Idara zinazojitegemea, Wakala wa Serikali, Taasisi na Mashirika ya Umma, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka ya Serikali za Mtaa.


Pamoja na maboresho hayo, Mhe. Ridhiwani amesema  wapo baadhi ya waajiri ambao hawatekelezi ipasavyo wajibu wao katika kushughulikia madai ya aina hiyo ambapo hadi kufikia Mei 28,2026 madai ya watumishi 18,021 yenye jumla ya Shilingi 50,917,523,216 hayajawasilishwa Ofisini kwake.


“Baadhi ya waajiri wamekuwa wakiwasilisha katika Ofisi hii madai yenye kasoro ambazo walipaswa kuzibaini kabla hawajayawasilishwa.  Vile vile, yapo madai ya malimbikizo ya mshahara yanayotokana na waajiri kutozingatia Sheria, Kanuni na Taratibu katika uendeshaji wa mashauri ya kinidhamu na hivyo kuzalisha madeni makubwa kwa Serikali” amesema.


Katika hatua nyingine, Mhe. Ridhiwani ametoa onyo kali kwa waajiri na viongozi wa taasisi za umma wanaokiuka sheria na taratibu za kiutumishi hususani kwa Waajiri kuchagua aina ya watu wa kufanya nao kazi, kutopokea watumishi wanaohamishiwa kwenye Taasisi zao, Waajiri kujimilikisha Taasisi na kuficha barua zenye maelekezo mahsusi ikiwemo barua za uhamisho.


Sambamba hayo, amesema Ofisi yake kwa kushirikiana na Taasisi za Haki Jinai imeanza kuchukua hatua mbalimbali kwa watumishi wanaojihusisha na ukiukwaji wa maadili ikiwemo kughushi barua za Ofisi hiyo ambapo hadi sasa jumla ya watuhumiwa Sita wamefikishwa mahakamani kwa makosa ya Uhujumu Uchumi na kesi zinaendelea.


Awali akizungumza Katibu Mkuu Ofisi hiyo Juma Mkomi, amesema kikao hicho kimeandaliwa mahsusi kwa lengo la kutathmini nafasi ya wasimamizi wa Utawala na Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma, kubadilishana uzoefu katika kuboresha ufanisi wa utekelezaji wa majukumu ya Serikali hususan katika Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma hasa tunapoelekea kwenye utekelezaji wa Dira Mpya ya Taifa ya 2050.


Pia, Mkomi  amesema kikao hicho kitajikita  zaidi katika kujadili masuala muhimu ya Usimamizi wa Utumishi wa Umma, Usimamizi  na matumizi ya Mifumo ya TEHAMA Serikalini, changamoto zilizopo katika utekelezaji wa majukumu ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu na namna bora ya kukabiliana nazo.


Kikao kazi hicho kina kauli mbiu isemayo “Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma Sikivu, Jumuishi, Wenye Matokeo na Uwajibikaji kuelekea Dira 2050”.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.Ridhiwani Kikwete akizungumza   na Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu  (hawapo pichani) katika ufunguzi wa kikao kazi kilichofanyika Juni 1, 2026 katika ukumbi wa Mabele Hall jijini Dodoma. 


Katibu Mkuu,Ofisi ya Raia-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi, akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.Ridhiwani Kikwete kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Wizara na Idara zinazojitegemea, Wakala wa Serikali, Taasisi na Mashirika ya Umma, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka ya Serikali za Mtaa kilichofanyika Juni 1, Jijini Dodoma.



Sehemu ya Viongozi na Watendaji kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.Ridhiwani Kikwete wakati alipokuwa akizungumza nao katika  wa ufunguzi wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Jijini Dodoma 


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akitoa utambulisho wa viongozi na washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kabla ya ufunguzi wa kikao hicho Juni 1, 2026 Jijini Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.Ridhiwani Kikwete (kulia ) akiteta jambo na Katibu Mkuu-UTUMISHI  Bw. Juma Mkomi (kushoto) wakati wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Wizara na Idara zinazojitegemea, Wakala wa Serikali, Taasisi na Mashirika ya Umma, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka ya Serikali za Mtaa kilichofanyika Juni 1, Jijini Dodoma. 



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.Ridhiwani Kikwete (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Ofisi hiyo mara baada ya Waziri huyo kufungua 
kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Jijini Dodoma

Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.Ridhiwani Kikwete wakati akizungumza nao katika ufunguzi wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Jijini Dodoma

Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (kulia) akiteta jambo na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi mara baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.Ridhiwani Kikwete kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Jijini Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.Ridhiwani Kikwete akizungumza   na Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu  (hawapo pichani) katika ufunguzi wa kikao kazi kilichofanyika Juni 1, 2026 katika ukumbi wa Mabele Hall jijini Dodoma. 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.Ridhiwani Kikwete (mwenye suti ya kijivu ) akifurahia jambo na viongozi wengine kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, mara baada ya Wazuri huyo kufungua kikao kazi kilichofanyika Juni 1, 2026 katika ukumbi wa Mabele Hall jijini Dodoma.