Tuesday, March 24, 2026

 KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE  YAMPONGEZA RAIS MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN KWA KUWEKA KIPAUMBELE KWENYE SUALA LA AJIRA

Na. Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 24 Machi, 2026 

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kulipa kipaumbele suala la ajira katika utumishi wa umma. 

Pongezi hizo zimetolewa leo Machi 24, 2026 na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Edwin Swalle wakati akimwakilisha Mwenyekiti wa Kamati hiyo katika kikao cha  kupokea Utekelezaji wa Bajeti ya Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2025/26 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2026/27  kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma .

Amesema kasi ya kutoa vibali vya ajira kwa sasa imekuwa ni kubwa na ya kuridhisha ukilinganisha na miaka iliyopita. “Kwa niaba ya Kamati nipende kutoa pongezi nyingi kwa Mhe. Rais kwa kutoa vibali vya ajira pamoja na wewe Mhe. Waziri Kikwete na wasaidizi wote kwa utekelezaji kwani tumeona msukumo mkubwa kwenye suala la ajira katika Serikali hii ya Awamu ya Sita, hongereni sana,” ameongeza Mhe. Swalle.

Aidha, amewapongeza Viongozi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma kwa ushirikiano kwa kamati hiyo ambao umerahisisha utekelezaji wa majukumu ya kamati.

“Mhe. Waziri Kikwete umekuwa ukitupatia ushirikiano mkubwa sana katika utekelezaji wa majukumu yetu, wewe pamoja watendaji wote wa Ofisi hii, mmefanya kazi yetu kuwa rahisi sana, hata katika ziara ya kamati tuliyoifanya Kanda ya Ziwa hivi karibuni hukuwahi kutuacha, ulikuwa nasi bega kwa bega, tunakupongeza kwa kuonyesha uko makini sana na kazi yako,” ameongeza Mhe. Swalle.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema, Ofisi yake ipo tayari kutoa ushirikiano wowote unaohitajika katika kufanikisha utekelekezaji wa majukumu ya kamati ili kuweza kufikia malengo iliyojiwekea katika kuhudumia wananchi. 





Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Mhe. Edwin Swalle akitoa neno la pongezi kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete kwa utendaji mzuri wa Ofisi yake katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria kilicholenga kupokea utekelezaji wa bajeti ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma  

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa maelezo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria kuhusu utekelezaji wa Bajeti ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma  


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani)  wakati akitoa maelezo kuhusu utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma 

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria kilicholenga kupokea utekelezaji wa bajeti ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa neno la shukrani kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria kwa kupokea na kujadili kwa kina kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Ofisi yake kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 jijini Dodoma.

Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakiwa kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma




Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakiwa kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria kilicholenga kupokea utekelezaji wa bajeti ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa neno la shukrani kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria kwa kupokea na kujadili kwa kina kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Ofisi yake kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 jijini Dodoma.

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe.Nyamizi Mhoja (aliyekaa katikati) akitaka ufafanuzi wa jambo baada ya wasilisho la utekelezaji wa bajeti ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe.Dkt Yahaya Nawanda akitaka ufafanuzi wa jambo baada ya wasilisho la utekelezaji wa bajeti ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma 

Katibu Mkuu Ikulu Bw. Mululi Mahendeka (kulia) akiteta jambo na  Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Xavier Daudi (kushoto) wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria,kilicholenga kupokea utekelezaji wa bajeti ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma 

Mkurugenzi wa Mipango kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Cosmas Ngangaji akitoa Ufafanuzi wa jambo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, wakati wa kikao cha kupokea utekelezaji wa bajeti ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma 

 

Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani)  wakati akitoa maelezo kuhusu utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Mick Kiliba akitoa maelezo ya jambo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, wakati wa kikao cha kupokea utekelezaji wa bajeti ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma 

Sehemu ya Wakurugenzi na Wakuu wa Taasisi zilizopo chini ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Waziri wa Ofisi hiyo Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani)  wakati akitoa maelezo kuhusu utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma

 

Sehemu ya wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Waziri wa Ofisi hiyo Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani)  wakati akitoa maelezo kuhusu utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Sheria katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma 


Monday, March 23, 2026

SERIKALI YAWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA WAADILIFU

 Na. Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 23 Machi, 2026

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi amewataka watumishi wa Ofisi yake kuzingatia sheria na kanuni za maadili ya utumishi wa umma na kutumia ujuzi wa kitaaluma walionao ili kutoa huduma bora kwa umma.

Bw. Mkomi ameyasema hayo wakati akihitimisha mafunzo ya kila wiki ya kuwajengea uwezo watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora yaliyofanyika katika eneo maalumu la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijini Dodoma.

“Naomba nitoe rai kwenu kuwa kila mtumishi wa Umma kwa nafasi yake ahakikishe anatekeleza majukumu yake kwa uwazi, uaminifu, weledi na ufanisi ili kuepusha malalamiko ya wananchi kwa Serikali” alisema Bw. Mkomi.

Vile vile Bw. Mkomi amezishukuru na kuzipongeza Kurugenzi husika zilizoandaa mada pamoja na watoa Mada kwa uwasilishaji wao mzuri ambao umetoa uelewa utakaoboresha utendaji kazi wa watumishi wa umma.

Awali, Mchambuzi Kazi Mwandamizi kutoka Idara ya Uendelezaji Taasisi Bw. MacDonald Kiwis wakati akiwasilisha mada ya Uandishi wa Nyaraka za Serikali alisema kuwa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zote za Umma kwa jumla hazina budi kufuata miongozo ya uandishi wa nyaraka za Serikali ili kuwa na viwango vinavyofanana.

Naye Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi kutoka Idara ya Usimamizi wa Maadili Bw.Hassan Kilenza akiwasilisha mada ya Utambuzi wa Watoa Mrejesho alisema kuwa watumishi wa umma wanatakiwa kutoa mrejesho kwa wateja wakizingatia taratibu na uwepo wa takwimu sahihi ili kuepuka uwepo wa taarifa zisizofanana.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akizungumza na watumishi wa Ofisi yake wakati akihitimisha Mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi hao Machi 23, 2026 jijini Dodoma



Sehemu ya Wakurugenzi wa Idara na Vitengo mbalimbali kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akihitimisha mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Mtumba Jijini Dodoma.

Mchambuzi Kazi Mwandamizi kutoka Idara ya Uendelezaji Taasisi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. MacDonald Kiwis akitoa ufafanuzi kuhusu Miongozo ya Uandishi wa Nyaraka za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI yaliyofanyika machi 23, 2026 jijini Dodoma.



Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi kutoka Idara ya Usimamizi wa Maadili Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora                            Bw.Hassan Kilenza akiwasilisha mada ya Utambuzi wa Watoa Mrejesho wakati wa mafunzo maalumu ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi wa Ofisi hiyo machi 23, 2026 Mtumba Dodoma.

Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati alipokuwa akihitimisha mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Mtumba Jijini Dodoma.

Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati alipokuwa akihitimisha mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Mtumba Jijini Dodoma.

Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati alipokuwa akihitimisha mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Mtumba Jijini Dodoma.

Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati alipokuwa akihitimisha mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Mtumba Jijini Dodoma.