Tuesday, March 17, 2026

WAZIRI KIKWETE ASEMA SERIKALI ITAENDELEA KUWAHUDUMIA NA KUWAENZI VIONGOZI WA KITAIFA WASTAAFU KWA MCHANGO WAO MKUBWA KATIKA MAENDELEO YA TAIFA

 Na Veronica Mwafisi-Chato

Tarehe 17 Machi, 2026

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema Serikali itaendelea kuwahudumia na kuwaenzi Viongozi wa Kitaifa Wastaafu kwa kiwango stahiki kwa mujibu wa sheria na kwa kuzingatia maelekezo ya mara kwa mara yatakayotolewa na Mamlaka.

Mhe. Kikwete ametoa kauli hiyo leo tarehe 17 Machi 2026 kwenye kumbukizi ya miaka mitano ya Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt John Joseph Magufuli yaliyofanyika Chato mkoani Geita.

Amesema, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ndiyo yenye dhamana na Matunzo ya Viongozi wa Kitaifa Wastaafu kwa Mujibu wa Hati Idhini ambayo Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aligawa majukumu kwa Mawaziri na suala hili la kumbukizi ni mojawapo ya utekelezaji wa Sheria ya Mafao ya Hitimisho la Kazi kwa Viongozi wa Kisiasa Sura 225 jambo ambalo hata Hayati Dkt. John Joseph Magufuli, aliwahi kulitolea maelekezo.

“Kwa msingi huo, tunatoa uhakika wa uendelevu wa huduma bora kwa Viongozi wa Kitaifa Wastaafu na Wajane wa Viongozi wa Kitaifa Wastaafu,” amesisitiza Mhe. Kikwete.

Aidha, ameongeza kuwa Rais wa Awamu ya Tano alielekeza kuwa suala la kumbukizi linatakiwa kufanyika kwa umakini na ubora wa hali ya juu ili kuwafanya viongozi waliostaafu na wanaojiandaa kustaafu kuwa na ari ya kufanya kazi kubwa ya kulijenga Taifa wakiwa kazini kutokana na kupata uhakika wa uendelevu wa mustabali wa maisha yao na kuweka misingi bora ya kukabidhi kijiti cha uongozi wa nchi yetu.

Mhe. Kikwete amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa ruhusa na maelekezo mbalimbali kuhusu kufanyika kwa kumbukizi hiyo.

“Nikiwa ndiye Waziri mwenye dhamana na matunzo ya Viongozi wa Kitaifa Wastaafu naomba nikushukuru wewe binafsi kwa kutoa fedha za kufanikisha shughuli hii sambamba na kutusimamia katika kufanikisha jambo hili muhimu kwa Ofisi yetu, Serikali kwa ujumla na Familia ya Hayati Dkt. John Joseph Magufuli, Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo hapa inaongozwa Mama Janeth, Mjane wa Hayati Dkt. John P. J. Magufuli,” ameongeza.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza wakati wa kumbukizi ya miaka mitano ya Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt John Joseph Magufuli yaliyofanyika Chato mkoani Geita ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi (hayupo pichani)


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi (katikati) akiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (wa kwanza kushoto) akiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Wananchi mbalimbali wakifuatilia Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Askofu wa Jimbo Katoliki Rulenge – Ngara, Mhashamu Severine Niwemugizi akiongoza Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Sehemu ya Mawaziri na Viongozi wengine wa Serikali wakiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa kwanza kulia) akiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita. 


Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Bw. Musa Magufuli (Aliyeva suti ya blue) akifuatilia jambo wakati wa Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.


Sehemu ya ndugu, jamaa na marafiki wa familia ya Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli wakiwa katika Ibada ya Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitano ya Kifo cha Rais huyo iliyofanyika leo Machi 17, 2026 Chato, mkoani Geita.






Monday, March 16, 2026

SERIKALI KUPITIA TASAF YAIKOSHA KAMATI YA BUNGE KWA KUTEKELEZA MRADI WA ZAHANATI KATIKA ENEO LENYE CHANGAMOTO YA MIUNDOMBINU

Na Veronica Mwafisi-Mwanza

Tarehe 16 Machi, 2026

Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) imepongezwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kwa kutekeleza Mradi wa Zahanati katika eneo lenye changamoto ya miundombinu na kuokoa maisha ya wakazi wa eneo hilo.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 16 Machi, 2026 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt.  Damas Ndumbaro wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. 

Akizungumza kwa niaba ya kamati yake, Mhe. Dkt.  Ndumbaro amesema ujenzi wa zahanati hiyo ni msaada mkubwa kwa wakazi wa Mihama na Kata ya Kitangiri ambao ilikuwa ni changamoto kutoka katika eneo hilo kutafuta huduma sehemu nyingine.

 “Kwa changamoto ya kufika huku, niwapongeze TASAF kwa kutekeleza mradi huu katika eneo hili kwani itaokoa maisha ya wananchi wa eneo hili na gharama walizokuwa wakitumia kufuata huduma za matibabu katika eneo lingine.” Ameongeza.

Mhe. Ndumbaro ameongeza kuwa maendeleo haya ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ambacho kimekusudia kuwajali wananchi wake kwa kuwapa huduma mbalimbali ikiwemo za kijamii.

Aidha, ametoa wito kwa uongozi wa Halmashauri hiyo ya Ilemela kuhakikisha zahanati hiyo inawekwa chini ya Halmashauri hiyo. “TASAF imetekeleza, zahanati hii ni ya kwenu sasa, mfanye utaratibu iwe chini ya Halmashauri,” amesisitiza Mhe. Dkt. Ndumbaro.

Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema zahanati ya Mihama ni sehemu ya vielelezo vya miradi inayotekelezwa na TASAF kwa lengo la kuwahudumia wananchi.

Mhe. Kikwete amewataka wananchi wa Mihama na Kitangiri kuitunza zahanati hiyo ili iweze kuwahudumia kama ilivyokusudiwa.

Ameongeza kuwa, katika kuhakikisha wananchi wanahudumiwa kikamilifu, katika ajira 12,000 zilizotolewa na Serikali ndani ya siku 100, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemelea imepewa watumishi wa afya 37 na elimu 40.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa TASAF, Bw. Shadrack Mziray ameishukuru Kamati kwa kuitembelea zahanati hiyo na kushuhudia maendeleo yaliyofanywa na Serikali katika eneo hilo.

Akitoa neno la shukurani kwa niaba ya wananchi wa eneo la Mihama, Bi. Mary Nyanda ameishukuru Serikali kwa kujenga zahanati katika eneo hilo kwani walikuwa na uhitaji mkubwa wa zahanati.

“Zahanati hii ni mkombozi kwetu watu wa Mihama, kwa miaka 25 tumekuwa tukihangaika kufuata huduma sehemu nyingine, tunaishukuru sana Serikali kwa kutekeleza hili,” ameongeza Bi. Nyanda.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, imehitimisha ziara yake ya kikazi ya siku tatu ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Geita na jijini Mwanza.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akizungumza mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. 


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro kuzungumza na Watumishi wa Zahanati ya Mihama na Wananchi wa Mihama wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati hiyo uliotekelezwa na TASAF iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt, Damas Ndumbaro wakati wa ziara ya kamati hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na TASAF iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.



Sehemu ya Wauguzi na Maafisa Tabibu wa Zahanati ya Mihama wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya Mwenyekiti huyo na Kamati yake kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakikagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. Wengine ni Viongozi wa Mkoa wa Mwanza, Watendaji wa TASAF na Mganga Mfawidhi wa Zahanati hiyo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akifurahia jambo na Mkurugenzi wa TASAF, Bw. Shadrack Mziray (kushoto) wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria iliyolenga kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na TASAF iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.


Sehemu ya Wananchi wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya Mwenyekiti huyo na Kamati yake kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Viwanja vya Zahanati ya Mihama wakati wa ziara ya kikazi iliyolenga kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati hiyo uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Edwin Swalle


Mwonekano wa jengo la Zahanati ya Mihami lililojengwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) lililopo katika Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza ambapo Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria ilitembelea kukagua mradi wa utekelezaji wa Zahanati hiyo.


Mkurugenzi wa TASAF, Bw. Shadrack Mziray akitoa neno la shukrani kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kwa kufanya ziara ya kikazi kutembelea mradi wa ujenzi wa Zahanati ya Mihama kwa lengo la kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati hiyo iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akijadili jambo na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kikazi kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati hiyo iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. Wa pili kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro


Bi. Mary Nyanda akitoa shukrani kwa niaba ya Wananchi kwa Serikali kupitia TASAF kwa kujenga zahanati ya Mihama iliyopo katika Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.


Wanakikundi cha Wasikivu-TASAF wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya Mwenyekiti huyo na Kamati yake kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.


Mwonekano wa vifaa vya Zahanati ya Mihama iliyopo katika Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.


Sehemu ya Watendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) pamoja na Maafisa wa Ulinzi na Usalama wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya Mwenyekiti huyo na Kamati yake kukagua utekelezaji wa mradi wa Zahanati ya Mihama uliotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyopo Kata ya Kitangiri, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.