Wednesday, June 3, 2026

UTAWALA BORA NA USIMAMIZI MAKINI WA RASILIMALIWATU NI MSINGI WA UTUMISHI WA UMMA WENYE MATOKEO – MHE. QWARAY

Na Antonia Mbwambo –Dodoma

Tarehe 3 Juni, 2026

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray, amewataka Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele katika kusimamia haki, uwajibikaji na uzingatiaji wa sheria katika Utumishi wa Umma ili kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma kwa wananchi.

Mhe. Qwaray ameyasema hayo Juni 3, 2026 wakati akifunga Kikao Kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi waRasilimaliwatu Serikalini kilichowakutanisha viongozi kutoka Wizara, Wakala, Taasisi za Umma, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Jijini Dodoma.

Amesema, mafanikio ya Serikali yanategemea kwa kiwango kikubwa ubora wa usimamizi wa rasilimaliwatu.

“Rasilimaliwatu ndiyo injini ya maendeleo ya taifa; isimamiwe kwa weledi, haki na uwajibikaji.” – Mhe. Regina Qwaray alisema.

Aidha Mhe. Qwaray alibainisha kuwa Serikali imeendelea kupokea malalamiko yanayohusiana na ucheleweshaji wa kupandishwa vyeo, malipo ya stahili za watumishi na ukiukwaji wa taratibu za kiutumishi, hivyo kuwataka wataalamu wa Utawala na Rasilimaliwatu kuwa washauri waaminifu kwa viongozi wao na walinzi wa utawala wa sheria katika taasisi wanazozihudumia.

Pia alisisitiza umuhimu wa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma, matumizi salama ya teknolojia na ulinzi wa taarifa za Serikali, huku akitoa wito kwa waajiri kuwajengea watumishi uwezo kuhusu matumizi sahihi ya Akili Unde (AI) na mifumo ya kidijiti.

Katika kuongeza ufanisi wa utendaji kazi, aliagiza utekelezaji wa Mfumo wa e-Utendaji usimamiwe kwa ukaribu zaidi, na kwamba wasimamizi watakaoshindwa kutekeleza wajibu wao wa kutathmini utendaji wa watumishi wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma.

Ameongeza kuwa kufungwa kwa kikao hicho hakumaanishi mwisho wa juhudi za kuboresha Utumishi wa Umma, bali ni hatua ya kuanza kutekeleza kwa vitendo maazimio na maelekezo yaliyokubaliwa.

Kumalizika kwa kikao hiki si mwisho wa kazi, bali ni mwanzo wa utekelezaji wa maazimio na maelekezo yaliyotolewa kwa lengo la kujenga Utumishi wa Umma sikivu, jumuishi, na wenye matokeo,” alisisitiza Mhe. Qwaray.

Kwa upande wake Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi amesema ni matarajio yake kuwa kikao hicho kitaleta matokeo chanya kwa viongozi hao yatakayoboresha utekelezaji wa majukumu na kuongea tija katika utumishi wa umma.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza katika kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu (hawapo pichani) wakati Naibu Waziri huyo alipokuwa akifunga kikao kazi kilicholenga kuimarisha utawala na usimamizi wa rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma  tarehe 3 Juni, 2026 jijini Dodoma.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (kulia) akimkabidhi Mkurugenzi wa Uendelezaji Taasisi wa Ofisi hiyo Bw. Nolasco Kipanda tuzo ya shukrani kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI mstaafu Dkt. Laurean Ndumbaro, kwa kushiriki na kuwasilisha mada katika kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini jijini Dodoma

Com

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray,(kulia) akiteta jambo na Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Huma Mkomi, wakati wa kufunga kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini Tarehe 3 Juni, 2026 jijini Dodoma

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray,(kushoto) akisalimiana na viongozi wa Ofisi hiyo mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa Mabele jijini Dodoma kufunga kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini leo Tarehe 3 Juni, 2026 jijini Dodoma

Comm


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi hiyo, mara baada ya Naibu Waziri huyo kufunga kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini leo Tarehe 3 Juni, 2023 jijini Dodoma


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi hiyo, mara baada ya Naibu Waziri huyo kufunga kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini leo Tarehe 3 Juni, 2023 jijini Dodoma

Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray kufunga kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini leo Tarehe 3 Juni, 2023 jijini Dodoma

Comments

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiwa katika picha ya pamoja na Sekretarieti ya watumishi kutoka Ofisi hiyo, mara baada ya Naibu Waziri huyo kufunga kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini leo Tarehe 3 Juni, 2023 jijini Dodoma.



Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (wa pili kushoto) mara baada ya Naibu Waziri huyo kufunga kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini leo Tarehe 3 Juni, 2026 jijini Dodoma. Wa pili kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (wa pili kulia) akimkabidhi Mkurugenzi wa Huduma za Uwezeshaji katika Taasisi ya Uongozi Bw. Deo Usangira tuzo ya shukrani kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa Taasisi hiyo, Bw. Kadari Singo kwa kushiriki na kuwasilisha mada katika kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini jijini Dodoma

Comme

Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (kushoto) akimkabidhi Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray kwa kushiriki katika mkutano wa Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini leo Tarehe 3 Juni, 2023 jijini Dodoma

Comme

KIKAO KAZI CHA WAKUU WA IDARA NA VITENGO VYA UTAWALA NA USIMAMIZI WA RASILIMALIWATU KATIKA WIZARA NA IDARA ZINAZOJITEGEMEA, WAKALA WA SERIKALI, TAASISI NA MASHIRIKA YA UMMA, SEKRETARIETI ZA MIKOA NA MAMLAKA YA SERIKALI ZA MTAA

 

Kikao kazi cha siku tatu cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini kinahitimishwa leo tarehe 3 Juni, 2026 jijini Dodoma na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray.

kikao hicho  kilifunguliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ambapo katika siku hizo tatu washiriki wamepewa uelewa wa namna ya kuimarisha utawala na usimamizi wa rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma.


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi, akizungumza na Wakuu wa Idara na vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakati alipokuwa akiongoza majadiliano katika kikao kazi na watumishi hao kilichofanyika Jijini Dodoma. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa Ofisi hiyo, SACP. Ibrahimu Mahumi


Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji mbalimbali leo tarehe 3 Juni, 2026 katika ukumbi wa Mabele Hall Jijini Dodoma.


Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia maelezo ya Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi wakati alipokuwa akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu leo tarehe 3 Juni, 2026 Jijini Dodoma


Baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora wakifuatilia mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji wakati wa Kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu leo tarehe 3 Juni, 2026 Jijini Dodoma


Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji mbalimbali leo tarehe 3 Juni, 2026 katika ukumbi wa Mabele Hall Jijini Dodoma.


Washiriki kutoka Sekretarieti Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji wakati wa Kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu Jijini Dodoma.


Baadhi ya Wakurugenzi wasaidizi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora wakifuatilia mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji wakati wa Kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu leo tarehe 3 Juni, 2026 Jijini Dodoma


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi, (kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa Ofisi hiyo, SACP. Ibrahimu Mahumi

Tuesday, June 2, 2026

KIKAO KAZI CHA WAKUU WA IDARA NA VITENGO VYA UTAWALA NA USIMAMIZI WA RASILIMALIWATU KATIKA WIZARA NA IDARA ZINAZOJITEGEMEA, WAKALA WA SERIKALI, TAASISI NA MASHIRIKA YA UMMA, SEKRETARIETI ZA MIKOA NA MAMLAKA YA SERIKALI ZA MTAA

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Juma Mkomi amezungumza katika kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Wizara na Idara zinazojitegemea, Wakala wa Serikali, Taasisi na Mashirika ya Umma, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka ya Serikali za Mtaa, leo Juni 2, 2026 jijini Dodoma.

Kikao kazi hicho cha siku tatu, kimefunguliwa Juni mosi, 2026 na Waziri wa Nchi Ofisi hiyo Mhe. Ridhiwani Kikwete na kinatarajiwa kufungwa kesho na Naibu Waziri Ofisi ya Rais UTUMISHI Mhe. Regina Qwaray (Mb).

Aidha, kauli mbiu ya kikao kazi hicho ni “Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma Sikivu, Jumuishi, Wenye Matokeo na Uwajibikaji kuelekea Dira 2050”.



Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, akizungumza na Wakuu wa Idara na vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakati alipokuwa akiongoza majadiliano katika kikao na watumishi hao  Jijini Dodoma.

Washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala katika ukumbi wa Mabele Hall Jijini Dodoma.


Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi, akifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji katika kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu katika ukumbi wa Mabele Hall jijini Dodoma. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, SACP. Ibrahim Mahumi na kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi wa Ofisi hiyo.


Mkurugenzi wa Mipango kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Cosmas Ngangaji (kulia) akifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji wakati wa Kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu Jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini Bw. Hamis Mkunga Mkunga akiwasilisha mada  kuhusu Usimamizi wa rasilimaliwatu na usafishaji wa taarifa za kiutumishi na mishahara wakati wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu Jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais – UTUMISHI, Bi Leila Mavika  akiwasilisha mada kuhusu Uratibu wa Ajira za Wtanzania  katika mashirika ya Kikanda na Kimataifa wakati wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu Jijini Dodoma

Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi, Bw. Kadari Singo akiwasilisha mada kwa Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu katika kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Mabele Hall jijini Dodoma


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Bw. Sospeter Mtwale akitoa wito kwa Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu katika Wizara na Idara zinazojitegemea, Wakala wa Serikali, Taasisi na Mashirika ya Umma, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka ya Serikali za Mtaa kuhusu uzingatiaji wa   maadili katika Utumishi wa umma tarehe 2 Juni, 2026 ikiwa ni siku ya pili ya kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Mabele hall jijini Dodoma



Mkurugenzi wa Huduma za Taasisi Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania TFRA Bi. Victoria Elangwa akitoa maelezo ya jambo kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu tarehe 2 Juni, 2026 ikiwa ni siku ya pili kati ya tatu zilizopangwa kikao hicho kufanyika Jijini Dodoma


Washiriki kutoka Sekretarieti Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji wakati wa Kikao kazi
cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu Jijini Dodoma.

Baadhi ya Wakurugenzi wasaidizi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora wakifuatilia mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji wakati wa Kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu tarehe 2 Juni, 2026 Jijini Dodoma




Baadhi ya Wakurugenzi wasaidizi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora wakifuatilia mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji wakati wa Kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu tarehe 2 Juni, 2026 Jijini Dodoma
 

Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia maelezo ya Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo wakati alipokuwa akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu tarehe 2 Juni, 2026 Jijini Dodoma.



Washiriki kutoka Sekretarieti Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji wakati wa Kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu Jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Priscus Kiwango, akiwasilisha mada kuhusu maboresho mbalimbali ya mifumo ambayo yamefanywa na Ofisi hiyo wakati wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu Jijini Dodoma


Baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora wakifuatilia mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji wakati wa Kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa rasilimaliwatu tarehe 2 Juni, 2026 Jijini Dodoma]