Na. Antonia Mbwambo na Helela Lusungu – Geita
Naibu
Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Regina Qwaray, amesisitiza umuhimu wa kutunzwa na kutumiwa ipasavyo miradi
inayotekelezwa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ili iweze kutoa
huduma endelevu na kunufaisha wananchi.
Mhe.
Qwaray ametoa kauli hiyo alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua utekelezaji
wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa kupitia TASAF katika Mkoa wa Geita,
ikiwemo Mradi wa Ujenzi wa Jengo la Utawala katika Shule ya Sekondari
Fazilibucha, iliyopo Kata ya Bombambili, Manispaa ya Geita.
Aidha,
Mhe. Qwaray ametembelea na kukagua Mradi wa Ujenzi wa Jengo la Huduma za
Wagonjwa wa Nje (OPD) pamoja na jengo la Huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto (RCH)
katika Zahanati ya Kakora, iliyopo Kijiji cha Kakora, Halmashauri ya Wilaya ya
Nyang’hwale, Mkoa wa Geita.
Akizungumza
wakati wa ziara hiyo, Mhe. Qwaray amesema kuwa uwekezaji unaofanywa na Serikali
kupitia TASAF ni kwa ajili ya kuboresha huduma za kijamii na kuinua ustawi wa
wananchi, hivyo ni wajibu wa viongozi na Wananchi kuhakikisha miradi hiyo
inatunzwa na kutumika kwa madhumuni yaliyokusudiwa.
“Miradi hii ni mali ya wananchi na
imejengwa kwa lengo la kuwapatia huduma bora na endelevu. Ni muhimu kuhakikisha
inatunzwa vizuri, inatumika ipasavyo na kila mmoja anawajibika kulinda uwekezaji
huu ili uweze kunufaisha jamii.” – Mhe. Qwaray amesema.
Ameongeza
kuwa utunzaji wa miundombinu hiyo utasaidia kuongeza muda wa matumizi ya majengo
na kuhakikisha Wananchi wanaendelea kupata huduma muhimu za kijamii bila
kulazimika kutumia rasilimali nyingi katika ukarabati wa mara kwa mara.
Amesema
Serikali itaendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa
kuhakikisha inakamilika kwa wakati, inazingatia viwango vinavyohitajika na
inatumika kwa manufaa yaliyokusudiwa.
Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (kulia) akisikiliza
maelezo kuhusu vyumba vinavyotumika kutolea huduma mbalimbali za afya katika Zahanati ya Kakora, wakati wa ziara ya ukaguzi wa jengo la Huduma za Wagonjwa wa Nje (OPD) na Huduma za Afya ya Uzazi
na Mtoto (RCH) lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoa wa Geita.
Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale Bi. Grace Kingalame, akitoa neno la
utangulizi kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray kabla ya Naibu Waziri
huyo kukagua mradi wa maendeleo unayotekelezwa na TASAF Mkoani Geita
Wananchi
na wanafunzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale wakimsikiliza Naibu Waziri,Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray
wakati wa ziara ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya jamii (TASAF) Mkoani Geita
Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (kulia) akisikiliza
maelezo kuhusu vyumba vinavyotumika kutolea huduma mbalimbali za afya katika Zahanati ya Kakora, wakati wa ziara ya ukaguzi wa jengo la Huduma za Wagonjwa wa Nje (OPD) na Huduma za Afya ya Uzazi
na Mtoto (RCH) lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoa wa Geita.
Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (kushoto) akikagua utekelezaji
wa ujenzi wa mradi wa Zahanati iliyopo Kijiji cha Kakora,
Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale Mkoani Geita.
Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (kulia) akisikiliza maelezo kuhusu vyumba vinavyotumika kutolea huduma mbalimbali za afya katika Zahanati ya Kakora, wakati wa ziara ya ukaguzi wa jengo la Huduma za Wagonjwa wa Nje (OPD) na Huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto (RCH) lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoa wa Geita.
Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akisalimiana na viongozi
na wananchi wa, Halmashauri ya Wilaya ya
Nyang’hwale mara baada ya kuwasili katika ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa zahanati
ya kakora unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya jamii (TASAF) Septemba 17, 2026 .







