Friday, July 3, 2026

MIAKA 25 YA CHUO CHA UTUMISHI WA UMMA TANZANIA, MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA KUJENGA RASILIMALIWATU YENYE TIJA

Na. Veronica Mwafisi-Dar ES Salaam

Tarehe 03 Julai, 2026

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) ina nafasi ya kipekee katika kujenga na kuendeleza uwezo wa kiutendaji wa watumishi wa umma ambao ndio watekelezaji wa majukumu ya Serikali kila siku.

 

Waziri Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 03 Julai, 2026 wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya TPSC yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.

 

Mhe. Kikwete amesema, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuweka kipaumbele katika uimarishaji wa Utumishi wa Umma ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, za haraka na zenye tija.

 

Mhe. Kikwete ameongeza kuwa, Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania si tu taasisi ya mafunzo, bali ni nguzo muhimu ya Serikali katika kujenga rasilimaliwatu yenye maarifa, stadi, maadili na uzalendo unaohitajika katika kutumikia umma kwa ufanisi.

 

Katika hatua nyingine, Mhe. Kikwete amesema kuwa, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inatutaka kuwa na Taifa lenye uchumi wa kisasa, ushindani wa kimataifa, matumizi makubwa ya teknolojia, na huduma za umma zenye ufanisi wa hali ya juu. Hivyo, mafanikio ya Dira hiyo yatategemea kwa kiasi kikubwa uwepo wa watumishi wenye sifa, ujuzi na uwezo wa kuongoza mabadiliko hayo.

 

“Chuo hiki kina wajibu mkubwa wa kuhakikisha  Watumishi wa Umma wanapata maarifa na stadi zinazolingana na mahitaji ya karne ya ishirini na moja ili kuwepo wa watumishi wenye sifa, ujuzi na uwezo wa kuongoza mabadiliko hayo,” amesema Waziri Kikwete.

 

Aidha, Mhe. Kikwete amewapongeza watangulizi wake kwa usimamizi mzuri ambao umechangia mafanikio makubwa ya Chuo hicho huku akimshukuru Katibu Mkuu wa Ofisi yake, Bw. Juma Mkomi kwa kuendelea kusimamia Chuo hicho kiutendaji.

 

Vilevile, Waziri Kikwete ameipongeza Bodi ya Ushauri ya TPSC, Menejimenti, Watumishi, Wanafunzi na wadau wote kwa mchango wao katika safari ya kutimiza miaka 25 ya mafanikio ya chuo hicho.

 

Akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mhe. Waziri kuzungumza na wadau katika hafla hiyo, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi ametoa wito kwa waajiri kutumia Kampasi za TPSC zilizo katika kanda zao ili kuwawezesha watumishi ikiwemo waajiriwa wapya kupata mafunzo ya awali.

 

“Kampasi katika Kanda hizo zimewekwa kimkakati ili kusogeza huduma za chuo katika mikoa mbalimbali, hivyo Waajiri wazitumie kikamilifu kwa watumishi kupata mafunzo kwa lengo la kuboresha utendaji kazi.” Amesisitiza Katibu Mkuu Mkomi.

 

Amezitaja Kampasi hizo kuwa ni Dar es Salaam, Mbeya, Tanga, Singida, Tabora na Mtwara na kuongeza kuwa Ofisi ya Rais-UTUMISHI itaendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na TPSC za kumiliki majengo yao ambapo Kampasi ya Singida inaendelea na ujenzi wa majengo 30 na Kampasi ya Tanga majengo 15.

 

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TPSC, Dkt. Florens Turuka amesema Bodi itaendelea kutoa ushauri ili Chuo kiendelee kuwa kinara katika masuala mbalimbali ikiwemo kujenga rasilimaliwatu yenye maadili, na yenye tija kwa taifa.

 

Akiwasilisha taarifa ya miaka 25 ya TPSC, Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Ernest Mabonesho amesema tangu kuanzishwa kwake, Chuo kimepata mafanikio makubwa katika maeneo mbalimbali ikiwemo taaluma, rasilimaliwatu na miundombinu.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


Viongozi mbalimbali, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akiteta jambo na Katibu Mkuu wa ofisi yake Bw. Juma Mkomi (kulia) wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


Menejimenti, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akifurahia jambo na Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu, Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Dkt. Ernest Mabonesho (kushoto) wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao kwenye hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


Menejimenti, Wadau na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa hafla ya kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo Jijini Dar es Salaam.


 

 

Thursday, July 2, 2026

SERIKALI YARIDHISHWA NA MAENDELEO YA MIRADI YA NYUMBA ZA WATUMISHI WA UMMA KIGOMA

 Na. Antonia Mbwambo–Kigoma

Tarehe 2 Julai, 2026

Serikali imeeleza kuridhishwa na Maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa Ujenzi wa Nyumba za Watumishi wa Umma Awamu ya Pili katika Mkoa wa Kigoma kufuatia ukaguzi uliofanywa na timu ya Wataalamu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa kushirikiana na Watumishi Housing Investimentsl.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Bw. Patrick Allute, wakati wakihitimisha ziara ya ukaguzi wa miradi ya makazi ya Watumishi wa Umma Mkoani Kigoma ambapo timu ilikagua mradi ya nyumba za Watumishi katika Shule ya Sekondari Muhunga, Wilaya ya Kasulu, na Kituo cha Afya Muyama, Wilaya ya Buhigwe,Mkoa wa Kigoma

Akizungumza baada ya kuhitimisha ziara hiyo, Bw. Allute amepongeza wasimamizi wa mradi, Watumishi Housing na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa usimamizi unaowezesha miradi hiyo kutekelezwa kwa ufanisi. Amesema hatua iliyofikiwa inaakisi dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuboresha mazingira ya kazi na ustawi wa Watumishi wa Umma.

Aidha, ameutaja mradi wa nyumba za Watumishi katika Kituo cha Afya Muyama kuwa miongoni mwa miradi iliyofanya vizuri zaidi kati ya miradi 15 iliyokaguliwa katika Mikoa mbalimbali ya Tanzania kutokana na kasi ya utekelezaji na ubora wa kazi inayoendelea kuonekana.

"Mradi wa nyumba za Watumishi katika Kituo cha Afya Muyama umeonesha kiwango cha juu cha utekelezaji. Kazi nyingi muhimu, ikiwemo mfumo wa umeme, zimekamilika na mradi umebakiza hatua chache kabla ya kukamilika na kuanza kutumika," amesema Bw. Allute.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Mradi wa Kituo cha Afya Muyama ameishukuru timu ya ukaguzi kwa ushauri na maelekezo yaliyotolewa, akisema yataendelea kufanyiwa kazi ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na kuanza kutoa huduma kwa Watumishi wa Umma waliokusudiwa kunufaika nao.

 

Wataalamu kutoka Ofisi ya Rais–UTUMISHI na Watumishi Housing Investment (WHI) wakijadili jambo mara baada ya kufanya ukaguzi wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Muyama, Wilaya ya Buhigwe, Mkoani Kigoma

Timu ya wataalamu kutoka Ofisi ya Rais–UTUMISHI na Watumishi Housing Investment (WHI) wakiwa katika picha ya pamoja na Kaimu Mganga Mfawidhi Kituo cha Afya Muyama Bw. Kwima Juma Buanza (wa tatu kutoka kushoto), mara baada ya timu hiyo kukamilisha ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa nyumba za watumishi wa kituo hicho kiiilichopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma.


Muonekano wa nyuma wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma wa Kituo cha Afya Muyama kwenye Wilaya ya Buhigwe Mkoa wa Kigoma

Mkurugenzi wa Fedha na Uwekezaji kutoka Watumishi Housing Investiment (WHI) Bw. Paskali Massawe (aliyenyoosha mkono) akielezea jambo kwa Wataalamu alioambatana nao katika ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Muyama, Wilaya ya Buhigwe, Mkoani Kigoma, mara baada ya kufika kwenye eneo hilo Julai 2, 2026 

Wataalamu kutoka Ofisi ya Rais–UTUMISHI na Watumishi Housing Investment (WHI) wakijadili jambo mara baada ya kufanya ukaguzi wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya Watumishi wa Shule ya Sekondari Muhunga iliyopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Patrick Allute (wa tano kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mipango na Bajeti, wa Ofisi hiyo, Bi. Julieth Magambo wakati wa ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa nyumba ya makazi ya watumishi wa Shule ya Sekondari Muhunga iliyopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma.

Wataalamu kutoka Ofisi ya Rais–UTUMISHI na Watumishi Housing Investment (WHI) wakijadili jambo mara baada ya kufanya ukaguzi wa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya Watumishi wa Shule ya Sekondari Muhunga iliyopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, Bw. Patrick Allute, (aliyenyoosha mikono), akitoa maelekezo kwa Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Muhunga Mwl. Beatus Damiani,(wa pili kutoka kushoto) wakati wa ukaguzi wa SHule hiyo iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Mkoa wa Kigoma, leo tarehe 2 Julai, 2026.

Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma Shule ya Sekondari Muhunga iliyopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma.


Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Patrick Allute (wanne kutoka kushoto) akiagana na Kaimu Afisa Elimu Sekondari, Halmashauri ya Mji wa Kasulu Mwl. Jeremiah Ntiboneka mara baada ya Timu ya Wataalamu kutoka Ofisi ya Rais–UTUMISHI na Watumishi Housing Investment (WHI) kukagua mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari Muhunga iliyopo Wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma.