Wednesday, June 17, 2026

WIKI YA UTUMISHI WA UMMA NI JUKWAA LA KUWAFIKISHIA WANANCHI HUDUMA ZA SERIKALI- Waziri Kikwete

Na. Mwandishi wetu – Dodoma

Tarehe 17 Juni, 2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Jakaya Kikwete (Mb), amesema Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ni jukwaa muhimu linalowawezesha wananchi kufahamu huduma mbalimbali zinazotolewa na Serikali pamoja na namna ya kuzipata kwa urahisi.

Mh. Ridhiwani ameyasema hayo Juni 17, 2026 wakati akifungua maadhimisho ya Wiki ya Utumishi ya Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.

Amesema, maadhimisho hayo yanatoa fursa kwa Taasisi za umma kujifunza, kubadilishana uzoefu na kuonesha mafanikio, ubunifu na maboresho yaliyofanyika katika utoaji wa huduma kwa umma.

Mhe. Ridhiwani amesema Serikali imeendelea kuimarisha Utumishi wa Umma kupitia maandalizi ya Programu ya Maboresho ya Utumishi wa Umma yenye lengo la kuongeza tija na ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Aidha, ameeleza kuwa programu hiyo itajikita katika maeneo matano ya kimkakati ambayo ni mabadiliko ya fikra katika Sekta ya umma, ujumuishaji na ushirikishwaji wa Wananchi, uongozi na uwajibikaji, usimamizi wa Rasilimaliwatu pamoja na mageuzi ya huduma za kidijiti.

Vilevile Waziri Kikwete amesema Serikali imeendelea kuboresha huduma kwa wananchi kupitia matumizi ya mifumo mbalimbali ya kidijiti ikiwemo e-Utendaji, e-Watumishi, e-Mrejesho, e-Ardhi, e-Office, TAUSI, GePG, MUVU na MAJIIS ili kuongeza uwazi, uwajibikaji na ufanisi katika utoaji wa huduma za Serikali.

Akizungumzia Ustawi wa Watumishi wa umma, Mhe. Ridhiwani amesema Serikali imepandisha vyeo watumishi 219,000 waliokidhi vigezo katika mwaka wa fedha 2025/26 ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wao na kuongeza motisha kazini. Amesisitiza kuwa zoezi hilo liendelee kutekelezwa kwa kuzingatia sera, sheria na miongozo ya Utumishi wa Umma ili kuhakikisha haki, usawa na uwazi vinazingatiwa kwa watumishi wote.

Katika eneo la ajira, Mhe. Kikwete amesema Serikali kupitia Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imeajiri watumishi 42,500 wa kada mbalimbali katika mwaka wa fedha 2025/26. Aidha, amesema Serikali imetenga nafasi mpya 45,000 za ajira kwa mwaka wa fedha 2026/27 ili kuongeza nguvu kazi katika sekta mbalimbali za utoaji huduma.

Mhe. Kikwete amesema Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya kazi na Ustawi wa Watumishi wa Umma kupitia miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa nyumba kwa watumishi wanaofanya kazi katika mazingira magumu. Amesema Serikali tayari imekamilisha nyumba 54 kwa watumishi wa sekta za afya na elimu katika mikoa mbalimbali na inaendelea na ujenzi wa nyumba nyingine 78.

Kwa upande wake Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi amesema ushiriki wa Taasisi nyingi katika maonesho hayo unaashiria wingi wa Huduma zinazoendelea kutolewa na kuwasihi Wananchi kutembelea mabanda ya maonesho ili kupata huduma mbalimbali ikiwemo kupata ufafanuzi wa masuala ya Kiutumishi na matumizi ya Mifumo ya TEHAMA pamoja na huduma zingine kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI kama gazeti la Serikali.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akiungumza na Viongozi, Watumishi kutoka Wizara na Taasisi za Umma, pamoja na Wananchi wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akiungumza na Viongozi, Watumishi kutoka Wizara na Taasisi za Umma, pamoja na Wananchi wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akiungumza na Viongozi, Watumishi kutoka Wizara na Taasisi za Umma, pamoja na Wananchi wakati wa Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma



Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi, akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkarimbisha  
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete kufungua Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Juni 17, 2026 jijini Dodoma


K
waya Kutoka  Taasisi ya Kuzuia 
Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ikitumbuiza mbele ya Mgeni Rasmi ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma


Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifurahia jambo wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akiteta jambo na 
Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi wakati wa hafla ya ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akifurahia jambo 
wakati wa hafla ya ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma


Katibu Mkuu-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi
(kushoto) akiteta jambo na Naibu Katibu Mkuu-wa Ofisi hiyo Bw. Xavier Daudi wakati wa hafla ya ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma


Baadhi ya Watumishi kutoka Wizara, Taasisi za Umma, na Wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipokuwa akitoa hotuba ya kufungua Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma


Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Boraakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipokuwa akitoa hotuba ya kufungua Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma 


Baadhi ya Watumishi kutoka Wizara, Taasisi za Umma, na Wananchi wakimsikiliza
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipokuwa akitoa hotuba ya kufungua Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma

Tuesday, June 16, 2026

Monday, June 15, 2026

MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

Wakurugenzi na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakitoa elimu kwa wananchi kuhusu huduma zinazotolewa na Ofisi hiyo wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma leo Juni 16, 2026 Chinangali Jijini Dodoma.

Aidha miongoni mwa Huduma zinazotolewa ni pamoja na elimu ya Mifumo ya e-Wekeza, GSP, e-Huduma, e-Mkopo, e-Msawazo, Gazeti la Serikali, e-Mrejesho, e-Utendaji, e-Watumishi, e-Likizo na e-Ajira.