Thursday, March 12, 2026

KATIBU MKUU-UTUMISHI AWASISITIZA WATUMISHI WA UMMA KUFANYA KAZI KWA BIDII ILI KULETA TIJA KATIKA JAMII


 

Na. Antonia Mbwambo na Eric Amani-Dodoma.

Tarehe 12 machi, 2026

 

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi, amewasisitiza Wajumbe wa Baraza la wafanyakazi la Ofisi yake kufanya kazi kwa bidii na weledi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za utendaji ili kuleta mabadiliko yenye tija kwa maendeleo ya taifa.

 

Bw. Mkomi ameyasema hayo leo tarehe 12 Machi, 2026 wakati wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora uliolenga kupitisha Mpango na Bajeti ya Ofisi hiyo ya Mwaka wa Fedha 2026/27 uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.

“Katika kufikia Utumishi wa Umma uliotukuka, nitoe wito kwa wajumbe wote wa baraza, kutekeleza majukumu yenu ipasavyo ili kutoa huduma bora itakayotatua changamoto za wananchi.” Bw. Mkomi alisema.

 Aidha Katibu Mkuu Mkomi amewataka wajumbe wa mkutano huo kuhakikisha kunakuwa na ushirikishwaji wa Watumishi katika mikakati inayopangwa na  kamati hiyo ili kuongeza uelewa wa masuala ya kiutumishi na kuwa na mtazamo chanya utakaoleta ufanisi katika utendaji wao .

 Ameongeza kuwa ni muhimu kukawa na mafunzo kwa wajumbe wa Baraza hilo ili kuwajengea uwezo kwa matokeo chanya katika maeneo yao ya kazi.

 Bw. Mkomi alimshukuru mwakilishi wa Katibu Mkuu TUGHE Taifa, ambaye ni Mwenyekiti wa TUGHE Mkoa wa Dodoma Bw. Maulidi Kipeneku kwa ushiriki wake katika mkutano huo na kuahidi kuwa Ofisi ya Rais-UTUMISHI itashirikiana na TUGHE wakati wote katika kuhakikisha Baraza linatekeleza majukumu yake kikamilifu.

 Awali Bw. Kipenuke aliipongeza Ofisi hiyo kwa kuzingatia sheria ya kufanya baraza ya wafanyakazi kwa wakati. “Mmekuwa kioo, mabaraza yanafanyika kwa wakati na ni shirikishi, huku akiwatasisitiza wajumbe kutoa michango yao ili kuwawakilisha kwa ufasaha watumishi katika Idara na Vitengo vyao.” Alisisitiza Bw. Kipenuke.   

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiweka Saini katika kitabu cha wageni leo katika uKumbi wa Nyaraka mara baada ya kuwasili kwa ajili ya mkutano wa baraza la wafanyakazi la Ofisi yar a Rais  - UTUMISHI leo  machi  12, 2026 Jijini Dodoma.


Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa TUGHE Taifa ambaye pia mwenyekiti wa TUGHE MKOA wa Dodoma Bw. Maulid Kipeneku akitoa neno la salamu kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - UTUMISHI Bw. Juma Mkomi na washiriki wote wa mkutano wa baraza la wafanyakazi katika ofisi ya Rais – UTUMISHI jijini Dodoma Machi 12, 2026.

Picha ya Pamoja ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiwa pamoja na Washiriki wa wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora mara baada ya Kumalizika kwa Mkutano wa Baraza hilo leo machi 12, 2026 Jijini Dodoma.



Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi katika Ofisi ya Rais – UTUMISHI ambaye pia ni Mkutubi mwandamizi katika kitengo cha Mawasiliano Bi. Halima Rauna akijiitambulisha wa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – UTUMISHI Bw. Juma Mkomi wakati wa utambulisho wa washiriki wote wa Mkutano huo Machi 12, 2026 katika ukumbi wa Nyaraka Uliyopo Jijini Dodoma.


Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakipitia agenda za mkutano wa Baraza la Wafanyakazi katika ofisi ya Rais – UTUMISHI leo Macji 12, 2026 jijini Dodoma. 


Afisa Mchumi kutokea Idara ya Mipango Ofisi ya Rais - UTUMISHI Ndg. Rifati H. Almasi akiwasilisha mada kwa Katibu Mkuu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Bw. Juma Mkomi wakati wa uwasilishaji mada katika na Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Machi 12, 2026 Jijini Dodoma

Picha ya Pamoja ya Washiriki wa Mkutano wa Baraza la wafanyakazi  katika Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora katika Mkutano wa baraza hilo uliyofanyika Leo Machi 12, 2026 jijini Dodoma ambapo Mkutano huo uliongozwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - UTUMISHI Bw. Juma Mkomi.



                                                                                                                                                                                             

No comments:

Post a Comment