Na. Antonia Mbwambo na Eric Amani-Dodoma.
Tarehe 12 machi, 2026
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw.
Juma Mkomi, amewasisitiza Wajumbe wa Baraza la wafanyakazi la Ofisi yake
kufanya kazi kwa bidii na weledi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za
utendaji ili kuleta mabadiliko yenye tija kwa maendeleo ya taifa.
Bw. Mkomi ameyasema hayo leo tarehe 12
Machi, 2026 wakati wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora uliolenga kupitisha Mpango na
Bajeti ya Ofisi hiyo ya Mwaka wa Fedha 2026/27 uliofanyika katika ukumbi wa
Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dodoma.
“Katika kufikia Utumishi wa Umma
uliotukuka, nitoe wito kwa wajumbe wote wa baraza, kutekeleza majukumu yenu
ipasavyo ili kutoa huduma bora itakayotatua changamoto za wananchi.” Bw. Mkomi
alisema.
Aidha Katibu Mkuu Mkomi amewataka
wajumbe wa mkutano huo kuhakikisha kunakuwa na ushirikishwaji wa Watumishi katika
mikakati inayopangwa na kamati hiyo ili
kuongeza uelewa wa masuala ya kiutumishi na kuwa na mtazamo chanya utakaoleta ufanisi
katika utendaji wao .
Ameongeza kuwa ni muhimu kukawa na mafunzo
kwa wajumbe wa Baraza hilo ili kuwajengea uwezo kwa matokeo chanya katika
maeneo yao ya kazi.
Bw. Mkomi alimshukuru mwakilishi wa
Katibu Mkuu TUGHE Taifa, ambaye ni Mwenyekiti wa TUGHE Mkoa wa Dodoma Bw. Maulidi Kipeneku kwa ushiriki wake katika mkutano huo na
kuahidi kuwa Ofisi ya Rais-UTUMISHI itashirikiana na TUGHE wakati wote katika
kuhakikisha Baraza linatekeleza majukumu yake kikamilifu.
Awali Bw. Kipenuke aliipongeza Ofisi
hiyo kwa kuzingatia sheria ya kufanya baraza ya wafanyakazi kwa wakati.
“Mmekuwa kioo, mabaraza yanafanyika kwa wakati na ni shirikishi, huku
akiwatasisitiza wajumbe kutoa michango yao ili kuwawakilisha kwa ufasaha
watumishi katika Idara na Vitengo vyao.” Alisisitiza Bw. Kipenuke.
 |
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiweka Saini katika kitabu cha
wageni leo katika uKumbi wa Nyaraka mara baada ya kuwasili kwa ajili ya mkutano
wa baraza la wafanyakazi la Ofisi yar a Rais - UTUMISHI leo machi 12,
2026 Jijini Dodoma. |
 |
Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa TUGHE Taifa
ambaye pia mwenyekiti wa TUGHE MKOA wa Dodoma Bw. Maulid Kipeneku akitoa neno
la salamu kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - UTUMISHI Bw. Juma Mkomi na washiriki wote wa mkutano wa baraza la
wafanyakazi katika ofisi ya Rais – UTUMISHI jijini Dodoma Machi 12, 2026. |
 |
Picha ya Pamoja ya Katibu Mkuu Ofisi ya
Rais – UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiwa pamoja na Washiriki wa wajumbe wa baraza
la wafanyakazi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
mara baada ya Kumalizika kwa Mkutano wa Baraza hilo leo machi 12, 2026 Jijini
Dodoma. |
 |
Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi katika
Ofisi ya Rais – UTUMISHI ambaye pia ni Mkutubi mwandamizi katika kitengo cha
Mawasiliano Bi. Halima Rauna akijiitambulisha wa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais –
UTUMISHI Bw. Juma Mkomi wakati wa utambulisho wa washiriki wote wa Mkutano huo
Machi 12, 2026 katika ukumbi wa Nyaraka Uliyopo Jijini Dodoma. |
 |
Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakipitia agenda za mkutano wa Baraza la Wafanyakazi katika ofisi ya Rais – UTUMISHI leo Macji 12, 2026 jijini
Dodoma. |
 |
| Afisa Mchumi kutokea Idara ya Mipango Ofisi ya Rais - UTUMISHI
Ndg. Rifati H. Almasi akiwasilisha mada kwa Katibu Mkuu ambaye pia ni
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Bw. Juma Mkomi wakati wa
uwasilishaji mada katika na Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya
Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Machi 12, 2026
Jijini Dodoma |
 |
Picha ya Pamoja ya Washiriki wa Mkutano wa
Baraza la wafanyakazi katika Ofisi ya Rais
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora katika Mkutano wa baraza hilo
uliyofanyika Leo Machi 12, 2026 jijini Dodoma ambapo Mkutano huo uliongozwa na
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - UTUMISHI Bw. Juma Mkomi. |
No comments:
Post a Comment