Na. Antonia Mbwambo na Veronica Mwafisi-Dodoma
Tarehe 27 Machi, 2026.
Katibu Mkuu,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw, Juma Mkomi amewataka wadau wa Rasilimaliwatu Serikalini kupendekeza mkakati
madhubuti utakaosaidia kuepukana na changamoto ya upungufu wa watumishi katika
taasisi za umma.
Katibu Mkuu Mkomi ameyasema hayo leo jijini Dodoma alipokuwa
akifungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa
Rasilimaliwatu kutoka katika Wizara na Taasisi za Kimkakati
kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya mahitaji ya rasilimaliwatu.
Amesema Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
ilifanya zoezi la Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika taasisi za umma
na kubaini kuwepo kwa upungufu wa watumishi kwenye baadhi ya taasisi na taasisi
nyingine kuwepo kwa ziada ya watumishi.
Amesema kufuatia tathmni hiyo, Ofisi iliona ni vema ikaandaa kikao cha
wadau hao ili kujadiliana kwa pamoja namna itakavyofaa kutafuta ufumbuzi wa changamoto
hiyo ya muda mrefu.
Amesema kila mwaka wakati wa bajeti taasisi za umma zimekuwa na
utaratibu wa kuomba watumishi, hivyo mkakati madhubuti uwekwe ili kupata
suluhisho la changamoto hiyo ya upungufu wa watumishi.
“Lengo
kubwa la kikao kazi hiki ni kupata
usahihi wa taarifa za watumishi au mahitaji ya watumishi katika taasisi za umma, kuna maeneo yanahitaji watumishi kimkakati
hivyo ni muhimu kuona namna ya kukubaliana katika kuwapata watumishi hao na
kujadiliana kwa kina ili kupata mapendekezo yatakayosaidia kuwagawa Watumishi
wa ajira mpya na watakaokuwa wakihamia katika vituo vingine vya kazi,” amesisitiza.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara
ya Uendelezaji Taasisi, Bw. Nolasco Kipanda amesema kupitia kikao kazi hicho
Serikali itapata taarifa zilizo sahihi za mahitaji ya Watumishi wa Umma kwa miaka mitano ijayo.
Akitoa
neno la shukrani Mwenyekiti wa Kikao kazi hicho ambaye ni Mkurugenzi wa Utawala
na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Wizara ya Afya, Bw. Issa Ng’imba alimuahidi Katibu
Mkuu Mkomi kuwa watazingatia maelekezo yote ambayo ameyatoa ili waweze
kuboresha utendaji kazi kwa maendeleo ya Taifa
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akizungumza na washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu (hawapo pichani) kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati kabla ya Katibu huyo kufungua kikao hicho kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma
Katibu Mkuu Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi kutoka
Idara na Vitengo vya Ofisi hiyo mara baada ya Katibu huyo kufungua kikao
kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.
Wajumbe wa Sekretarieti kutoka
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
na Utawala Bora wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati akifungua kikao kazi
cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilicholenga
kujadili matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na
Taasisi za kimkakati kilichofanyika kilichofanyika Machi 27, 2026 katika
ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.
Afisa kutoka Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Waziri Mkumbo akiwasilisha mada ya Mfumo wa e-Msawazo na
matokeo ya Tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za
Kimkakati wakati wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na
Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya
Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati
kilichofanyika kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT
Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja
na Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Wizara na
Taasisi za kimkakati baada ya Katibu huyo kufungua kikao kazi cha kujadili
matokeo ya tathmini ya Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi hizo
kilichofanyika kilichofanyika Machi 27, 2026 kilichofanyika
kilichofanyika Machi 27, 2026 katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.
Washiriki wa kikao kazi cha
Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakifuatilia mada
mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, kwenye kikao hicho kilichofanyika ukumbi
wa NAOT Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Ofisi ya
Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja
na washiriki wa kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa
Rasilimaliwatu baada ya kufungua kikao kazi cha Wakuu wa Idara za Utawala na
Usimamizi wa Rasilimaliwatu kilicholenga kujadili matokeo ya tathmini ya
Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Sekta na Taasisi za kimkakati
kilichofanyika katika ukumbi wa NAOT Jijini Dodoma.
Washiriki wa kikao kazi cha
Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakifuatilia mada
mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, kwenye kikao hicho kilichofanyika ukumbi
wa NAOT Jijini Dodoma.
Washiriki wa kikao kazi cha
Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wakifuatilia mada
mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, kwenye kikao hicho kilichofanyika ukumbi
wa NAOT Jijini Dodoma.





No comments:
Post a Comment