MKANDARASI ATAKIWA KUKAMILISHA JENGO LA MAADILI KANDA YA ZIWA MWEZI JUNI, 2026
Na Veronica Mwafisi-Mwanza
Tarehe 15 Machi, 2026
Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imetoa malekezo ya
kukamilika kwa wakati Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma
Kanda ya Ziwa ili kuweza kuwahudumia kwa ufasaha viongozi katika maeneo ya
kanda hiyo.
Kauli
hiyo imetolewa leo tarehe 15 Machi, 2026 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt.
Damas Ndumbaro wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati hiyo iliyolenga
kukagua utekelezaji wa Mradi wa ujenzi wa jengo hilo lililopo eneo la Buswelu, Halmashauri
ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.
Akitoa
maelekezo hayo kwa niaba ya kamati yake, Mhe. Dkt. Ndumbaro amesema kukamilika
kwa jengo hilo kutawaondolea adha viongozi wa Kanda ya Ziwa wanaohitaji huduma
katika Ofisi za Maadili ya Viongozi wa Umma.
“Jengo
hili limeanza kujengwa tangu mwaka 2024 na sasa tuko mwaka 2026, Mkandarasi,
kamilisha jengo hili mwezi Juni, 2026, Serikali haijawahi kudhulumu mtu, fedha
zako utalipwa tu,” Mhe. Dkt. Ndumbaro ameongeza.
Aidha,
ameielekeza taasisi hiyo kuboresha utaratibu wa ujazaji wa Tamko la Rasilimali
na Madeni, badala ya kusubiri mpaka mwisho wa mwaka basi mfumo uwe wazi ili
kurahisisha ujazaji wake na kuepuka ujazaji wa pamoja ambapo wakati mwingine
mtandao umekuwa ukizidiwa.
Naye
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema lengo la ujenzi wa Jengo la Maadili Kanda ya
Ziwa ni kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa Viongozi wanaotumia muda mwingi
kusafiri kufuata huduma hizo jijini Dodoma.
“Mhe.
Mwenyekiti, tupo tayari wakati wote kupokea maelekezo ya Kamati yako kwani
ukaguzi mnaoufanya unatusaidia kuboresha na kusimamia suala la maadili kwa
umakini,” ameongeza
Akiwasilisha
taarifa ya mradi wa ujenzi wa jengo hilo, Kamishna wa Maadili, Mhe. Jaji
(Stahiki) Sivangilwa Mwangesi amesema jengo hilo likikamilika litaokoa kiasi
cha milioni 70 ambazo zimekuwa zikilipwa kila mwaka kwa ajili ya pango.
Kamishna
Mwangesi ameahidi kuendelea kuchukua hatua mbalimbali kwa lengo la kuhakikisha
mradi huo unakamilika kwa wakati na kutoa huduma kama ilivyokusudiwa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na
Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akizungumza mara baada ya kukagua
utekelezaji wa Mradi wa ujenzi wa Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi
wa Umma wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati hiyo iliyolenga kukagua
utekelezaji wa Mradi
wa jengo hilo lililopo Buswelu, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani
Mwanza.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala, Katiba na Sheria wakifuatilia hotuba ya Mwenyekiti
wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria,
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza mara
baada ya kukagua utekelezaji wa Mradi wa ujenzi wa
Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma lililopo Buswelu,
Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. Wengine ni Watendaji wa
Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria,
Mhe. Dkt, Damas Ndumbaro wakati wa ziara ya kikazi katika Mradi wa ujenzi wa jengo la Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma iliyolenga kukagua utekelezaji wa Mradi wa jengo hilo lililopo
Buswelu, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala, Katiba na Sheria wakitoka kusikiliza maelezo kuhusu Mradi wa ujenzi wa jengo la Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi
wa Umma wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa Mradi wa jengo
hilo lililopo Buswelu, Halmashauri ya Wilaya ya
Ilemela, Mkoani Mwanza.
Mwenyekiti wa Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas
Ndumbaro (wa pili kutoka kulia) akielekea kukagua utekelezaji wa Mradi wa ujenzi wa jengo la Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakati wa ziara ya
kikazi ya Kamati hiyo eneo la Buswelu, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela,
Mkoani Mwanza. Wa kwanza kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete
Kamshina wa Maadili Mhe. Jaji (Mst.) Sivangilwa Mwangesi (aliyesimama)
akielezea utekelezaji wa Mradi wa
ujenzi wa Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakati
wa ziara ya kikazi ya Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria iliyolenga kukagua utekelezaji wa Mradi wa jengo hilo lililopo Buswelu,
Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.
Mwonekano
wa jengo la Mradi wa ujenzi wa Ofisi za
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma lililopo Buswelu, Halmashauri
ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisisitiza jambo kwa Msimamizi
wa ujenzi wa jengo la Ofisi za
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, kutoka Kampuni ya Kiure
Engineering Mhandisi Sumai Mbezi mara baada ya Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kukagua utekelezaji wa Mradi wa jengo hilo lililopo Buswelu, Halmashauri
ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.
Mwenyekiti wa Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas
Ndumbaro (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Kamati yake mara baada ya
kukagua utekelezaji
wa Mradi wa ujenzi wa Ofisi za Sekretarieti ya
Maadili ya Viongozi wa Umma iliyopo Buswelu, Halmashauri ya Wilaya ya
Ilemela, Mkoani Mwanza. Kulia kwake ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI
na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete na kushoto kwake ni Kamshina wa Maadili Mhe. Jaji
(Mst.) Sivangilwa Mwangesi.
Mwenyekiti wa Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas
Ndumbaro (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Watendaji na Watumishi wa
Ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma
mara baada ya kukagua utekelezaji wa Mradi wa ujenzi wa Ofisi hiyo iliyopo Buswelu,
Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza. Kulia kwake ni Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete na kushoto kwake
ni Kamshina wa
Maadili Mhe. Jaji (Mst.) Sivangilwa Mwangesi.








No comments:
Post a Comment