Na Mwandishi Wetu-Dodoma
Naibu
Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Regina Qwaray ametoa wito kwa Watumishi wa Umma nchini kutumia kipindi hiki cha Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa
Ramadhani na Mafungo ya Kwaresma kujitafakari juu ya namna wanavyotoa huduma kwa
wananchi.
Naibu
Waziri Qwaray ametoa wito huo wakati wa futari maalum iliyoandaliwa na
Menejimenti ya Ofisi hiyo katika kipindi hiki ambapo Watumishi wa imani ya Dini
ya Kiislam na Kikristo wanakuwa katika mfungo.
Mhe.
Qwaray amesema watumishi wa umma
wanatakiwa kufanya kazi kwa uadilifu,
huruma na unyenyekevu huku
wakimtanguliza Mungu hivyo ni vema wakajitafakari kama hayo yote
yanafanyika.
Ameongeza kuwa, kipindi cha
mfungo kisiwe cha kushinda njaa bali iwepo thawabu kwa Mungu ambayo itatokana
na huduma bora zitakazotolewa na watumishi hao kwa wananchi itakayoleta matokeo
chanya kwa ustawi wa nchi.
Aidha, amepongeza Menejimenti ya
Ofisi hiyo kwa kuwakumbuka wahitaji ambao walijumuika nao katika futari hiyo
maalum iliyokutanisha makundi ya watu tofauti ambayo yanasaidia kubadilishana
uzoefu ili kuboresha utendakji kazi hasa katika kutoa huduma bora kwa wananchi.
Amesisitiza kuendelea kuiombea
nchi na viongozi. “Niwasisitize tuendelee
kuiombea nchi yetu na tuitunze amani tuliyonayo, sisi sote ni wamoja na ni Watanzania
hatuulizani dini
wala kabila,” alisisitiza Mhe. Qwaray.
Awali
Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Juma Mkomi alisema futari hiyo iliandaliwa kwa lengo la kuwaweka
pamoja watu
wa makundi mbalimbali hasa
katika Mfungo
wa Mwezi
wa Ramadhani na Kwaresma.
Bw.
Mkomi aliongeza
kuwa ni fursa nzuri kukutana kwa wakati mmoja kwani ibada hizo huwafanya kuwa
wacha Mungu jambo ambalo husaidia watumishi
kuwa na maadili ya kuwatendea haki wananchi wanaowahudumia.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na Watendaji na Watumishi wa ofisi hiyo wakati wa futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.
Katibu
Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akitoa
maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Naibu
Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Regina Qwaray kuzungumza na Watendaji na Watumishi wa ofisi hiyo wakati wa
futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi
wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.
Sehemu
ya Watendaji na Watumishi wa ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora wakiwa kwenye hafla ya futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti
ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika
Mtumba jijini Dodoma.
Katibu
Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akiwa
katika picha ya pamoja na Watendaji, Watumishi wa ofisi hiyo na wageni
waalikwa mara baada ya kupata futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya
Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika
Mtumba jijini Dodoma.
Naibu
Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Regina Qwaray akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wakuu wa Taasisi wa
Ofisi hiyo mara baada ya kupata futari
maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa
imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma. Wa pili
kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa kwenye futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika Mtumba jijini Dodoma.
Sehemu
ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
wakiwa kwenye futari maalum iliyoandaliwa na Menejimenti ya Ofisi
hiyo kwa ajili ya Watumishi wa imani ya Dini ya Kiislam na Kikristo iliyofanyika
Mtumba jijini Dodoma.





No comments:
Post a Comment