Na. Veronica Mwafisi-Dodoma
Tarehe 10 Machi, 2026.
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imeipongeza Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa usimamizi thabiti wa
miradi ya maendeleo
nchini.
Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro wakati akiongoza kikao cha Kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.
“Kwa niaba ya Kamati yangu nitoe pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan maana ndiye mwenye ofisi hii, kwa hakika mnafanya kazi nzuri kwa kumwakilisha Mhe. Rais.” Amesema Mhe. Dkt. Ndumbaro
Vilevile, Mhe. Dkt. Ndumbaro amempongeza na kumshukuru Waziri Kikwete kwa taarifa nzuri aliyoiwasilisha kwa Kamati hiyo iliyoelezea kwa kina utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo ambayo itaongeza chachu ya maendeleo nchini.
Mhe. Dkt. Ndumbaro ameiahidi Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora kuwa itashirikiana nayo katika usimamizi wa masuala mbalimbali ili kuleta matokeo chanya kwa ustawi wa Taifa.
Awali akiwasilisha taarifa ya utekelezaji
wa miradi ya
maendeleo iliyotengewa fedha kwa mwaka
2025/2026, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema, utekelezaji wa shughuli zilizopangwa katika kipindi husika umefanyika kwa kuzingatia fedha zilizopatikana pamoja na muda wa upatikanaji wake.
Mhe. Kikwete amesema kuwa, lengo la miradi hiyo ni kuongeza tija nchini lakini pia itaongeza chachu ya utendaji kazi kwa Watumishi wa Umma
Aidha, Mhe. Kikwete ameishukuru na kuiahidi Kamati hiyo kuwa Ofisi
anayoisimamia itaendelea kushirikiana nao katika kuimarisha na kuboresha
utendaji kazi ili kuleta tija katika kuwahudumia wadau mbalimbali kwa lengo la
kujenga na kuimarisha Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akiongoza kikao cha Kamati yake
na
Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo
chini ya ofisi hiyo jijini Dodoma leo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa
Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.
Sehemu ya Wajumbe
wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakiwa
katika kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya
Rais- UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo jijini Dodoma leo kilicholenga
kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha
katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi
ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026 kwa Kamati ya
Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria katika kikao kilichofanyika
Bungeni leo jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia)
akitazama nyaraka zake kabla ya kuwasilisha taarifa ya
Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha
2025/2026 kwa
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria katika kikao kilichofanyika
Bungeni leo jijini Dodoma. Kushoto ni Naibu Waziri wake Mhe. Regina Qwaray.
Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakiwa katika kikao cha Kamati hiyo na Watendaji
wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo kilicholenga
kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha
katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.
Sehemu ya Wajumbe
wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na
Sheria wakijadili jambo wakati wa kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa
Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo kilicholenga
kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha
katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.
Katibu
Mkuu-IKULU, Bw. Mululi Mahendeka (kushoto) na Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma
Mkomi (kulia) wakiwa kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga
kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha
katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.
Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakiwa katika kikao cha Kamati hiyo na Watendaji
wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo kilicholenga
kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha
katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.
Naibu
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi (kulia)
na Kamshina wa Maadili Mhe. Jaji
(Mst.) Sivangilwa Mwangesi (kushoto) wakiwa katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge
ya Utawala, Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa
ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha
2025/2026
Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakijadili jambo wakati wa kikao cha
Kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya
ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo
iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.
Sehemu ya
Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, wakimsikiliza Mwenyekiti
wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) wakati
akiongoza kikao cha Kamati yake na Watendaji wa ofisi hiyo kilicholenga
kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha
katika Mwaka wa Fedha 2025/2026
Watendaji wa Ofisi ya Rais-IKULU na Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakiwa
kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria
kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa
fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete
akifafanua jambo wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala,
Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya
Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha
2025/2026.
Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakifuatilia taarifa ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zilizo chini ya ofisi hiyo wakati wa kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa Ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.
Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Musa Magufuli (wa kwanza
kulia) pamoja na watendaji wa ofisi hiyo wakiwa kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge
ya Utawala, Katiba na Sheria, kilicholenga kuwasilisha taarifa
ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha
2025/2026.
Sehemu ya
Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, wakimsikiliza Mwenyekiti
wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) wakati
akiongoza kikao cha Kamati yake na Watendaji wa ofisi hiyo kilicholenga
kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha
katika Mwaka wa Fedha 2025/2026
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete
akifafanua hoja wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala,
Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya
Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha katika Mwaka wa Fedha
2025/2026.
Katibu
Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akifafanua hoja iliyowasilishwa na Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao kilicholenga
kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa fedha
katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.
Watendaji wa Ofisi ya Rais-IKULU na Ofisi ya
Rais-UTUMISHI wakiwa
kwenye kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria
kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyotengewa
fedha katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.

















No comments:
Post a Comment