Saturday, August 31, 2019

SERIKALI KUWASILISHA MUSWADA BUNGENI WA KUWA NA MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt (Mst.) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akizungumza na Wataalam wa ndani wa TEHAMA (hawapo pichani) waliotengeneza Mfumo mpya wa Taarifa Shirikishi za Kiutumishi na Mishahara (HCMIS) na Mfumo wa Wazi wa Tathmini ya Utendaji Kazi wa  Kieletroniki (eOPRAS) ambayo inatarajiwa kukamilika hivi karibuni.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt (Mst.) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) akiwahimiza Wataalam wa ndani wa TEHAMA (hawapo pichani) waliotengeneza Mfumo mpya wa Taarifa Shirikishi za Kiutumishi na Mishahara (HCMIS) na Mfumo wa Wazi wa Tathmini ya Utendaji Kazi wa  Kieletroniki (eOPRAS) kuhakikisha wanakamilisha utengenezaji wa mifumo hiyo kwa ufanisi ili iwe na manufaa ya kiutendaji Serikalini.

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Serikali Mtandao (eGA), Dkt. Jabir K. Bakari akimuonesha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt (Mst.) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) namna Serikali Mtandao inavyofanya kazi, wakati waziri huyo alipoitembelea wakala hiyo kuhimiza uwajibikaji.

Sehemu ya muonekano wa Mfumo mpya wa Taarifa Shirikishi za Kiutumishi na Mishahara (HCMIS) uliotengenezwa na Wataalam wa ndani wa TEHAMA ambao unatarajiwa unatarajiwa kukamilika hivi karibuni.


Tuesday, August 27, 2019

WAAJIRI SERIKALINI WATAKIWA KUMALIZA ZOEZI LA UHAKIKI WA VYETI VYA WATUMISHI KWANI OFISI YA RAIS UTUMISHI IMEKUWA IKIPOKEATAARIFA YA UWEPO WA BAADHI YA WATUMISHI WENYE VYETI VYA KUGHUSHI



Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro akizungumzia utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kuhusiana uadilifu na uwajibikaji kwa watumishi wa umma.

Monday, August 26, 2019

MRADI WA KUFUA UMEME WA MAJI WA JULIUS NYERERE KATIKA MAPOROMOKO YA MTO RUFIJI UNAOTEKELEZWA NA SERIKALI ULIASISIWA NA BABA WA TAIFA MWAKA 1975



Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akisoma kitabu cha Tanzania News Review kinachoonyesha kuwa Mradi wa Kufua Umeme wa Maji wa Julius Nyerere katika Maporomoko ya Mto Rufiji unaojulikana kama Julius Nyerere HydroPower Project uliasisiwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius K. Nyerere mnamo mwaka 1975.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akishuhudia baadhi ya nyaraka muhimu zinazotunzwa na Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa wakati wa ziara yake ya kikazi katika Idara hiyo jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akishuhudia baadhi ya nyaraka za Waasisi wa Taifa zilizotunzwa katika maktaba ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake ya kikazi katika Idara hiyo.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akisisitiza uhifadhi mzuri wa nyaraka alipotembelea maktaba ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa jijini Dar es Salaam na kushuhudia baadhi ya watafiti wakipata huduma ya taarifa zitakazowawezesha kukamilisha tafiti zao.

Friday, August 9, 2019

WANUFAIKA WA TASAF WILAYANI KARAGWE WAISHUKURU SERIKALI KWA KUWATHAMINI



Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akilakiwa na wananchi wa kijiji cha Rulalo katika Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe Mkoani Kagera wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF na kuhimiza uwajibikaji kwa Watumishi wa Umma.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akifurahia jambo wakati alipokuwa akizungumza na wananchi na Wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini  katika kijiji cha Rulalo  juu ya utekelezaji wa miradi ya TASAF.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akiangalia zizi la mbuzi la mmoja wa Walengwa wa TASAF, Bi. Beatha Katushabe wa kijiji cha Rulalo wilayani Karagwe mkoani Kagera ambaye anamiliki mbuzi 25 aliowapata kutokana na ruzuku ya Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) (katikati) akipokea zawadi ya mkungu wa ndizi kutoka kwa Walengwa wa TASAF katika kijiji cha Rukole, Wilayani Karagwe mkoani Kagera wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF.

Mmoja wa Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika kijiji cha Rukole, Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera, Bi. Rhoda Ernest (wa tatu kushoto kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akionyesha kisima cha kuvuna maji ya mvua alichokijenga kwa kutumia na ruzuku ya TASAF. 

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akipokea zawadi ya mkeka uliosukwa na mmoja wa wanufaika wa TASAF, Bi.Rhoda Ernest katika kijiji cha Rukole, wilayani Karagwe Mkoani Kagera wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF.