Friday, November 14, 2025
Thursday, November 13, 2025
Monday, November 10, 2025
KATIBU MKUU OFISI YA RAIS AWASISITIZA WATUMISHI WA UMMA KUDUMISHA AMANI
Na Eric Amani, Dodoma.
Katibu
Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi,
ametoa wito kwa Watumishi wa Umma nchini kuendelea kudumisha amani, mshikamano na
uzalendo katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku kwa manufaa ya Taifa.
Akizungumza
jijini Dodoma leo tarehe 10 Novemba,
2025 wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi wa ofisi hiyo
yanayofanyika kila siku ya Jumatatu,
Katibu Mkuu Mkomi amesema, Utumishi wa Umma una nafasi kubwa katika kulinda na kuimarisha
amani ya nchi kwa kutoa huduma bora, kuzingatia maadili ya kazi na kuepuka
vitendo vinavyoweza kuleta mgawanyiko katika jamii.
“Watumishi wa Umma ni kioo cha Serikali, hivyo mnapaswa kuwa mfano katika uadilifu, uvumilivu na
uzalendo,” alisema Katibu Mkuu Mkomi.
Bw.
Mkomi pia aliwakumbusha watumishi kuzingatia misingi ya utawala bora,
uwajibikaji, na matumizi sahihi ya rasilimali za umma, sambamba na kutumia
lugha na mienendo inayojenga taswira chanya ya Serikali.
Kwa upande wake mwewezeshaji ambaye ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Ulinzi na Usalama wa TEHEMA, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bw. Mussa Chiwelenje amewasisitiza Watumishi kutunza taarifa zao binafsi, za Ofisi na kutochezea miundombinu ya TEHAMA kwa usalama wa Taifa.
![]() |
| Mkurugenzi Kitengo cha Usalama wa Mtandao na TEHAMA Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Bw. Mussa Chiwelenje akiwasilisha Mada ya usalama wa Mtandao kwenye Mafunzo ya Kuwajengea uwezo watumishi wa ofisi ya Rais - UTUMISHI Novemba 10, 2025. |
![]() |
| Mkurugenzi Idara ya Utawala na Usimamizi Rasilimaliwatu Ofisi ya Rais - UTUMISHI Bw. Mussa Magufuli Novemba 10, 2025 akichangia Mada kwenye mafunzo ya Kuwajengea uwezo watumishi wa ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma. |
Monday, November 3, 2025
Wednesday, October 29, 2025
WATENDAJI WAKUU OFISI YA RAIS-UTUMISHI WAPIGA KURA, KATIBU MKUU MKOMI ATOA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA NA WANANCHI KUJITOKEZA KUTIMIZA HAKI YAO YA KIKATIBA
Na. Antonia Mbwambo na Veronica Mwafisi -Dodoma
Tarehe 29 Oktoba, 2025
Watendaji Wakuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora leo tarehe 29.10.2025 wameshiriki zoezi la kupiga kura katika
Vituo mbalimbali na kuchagua Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani.
Akishiriki zoezi hilo katika Kituo cha Kupiga Kura cha Msangalale
Mashariki, Kata ya Dodoma Makulu, jijini Dodoma, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi ametoa wito kwa Watumishi wa
Umma na Wananchi kujitokeza kuchagua viongozi wanaowahitaji kwa maendeleo ya Taifa.
“Namshukuru Mungu nimeshikiri salama zoezi hili muhimu la Kikatiba, nipende
kutoa wito kwa Watumishi wa Umma na Wananchi kwa ujumla kushikiriki pia kwani
ni haki yao ya msingi.” Bw. Mkomi amesisitiza.
Amesema hali katika Kituo hicho ni ya utulivu na wananchi wamekua
wakimiminika kwenda kupiga kura hivyo amewasisitiza kila mwenye haki ya
kushiriki zoezi hilo afanye hivyo.
Aidha, Bw. Mkomi amewapongeza Waratibu wa zoezi hilo katika Kituo hicho
kwa kuonyesha ushirikiano kwa wananchi wanaoenda kushiriki katika zoezi hilo na
kuhakikisha kila mwenye sifa anashiriki kikamilifu.
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Xavier Daudi
ameshiriki zoezi hili muhimu katika Kituo cha Mwatano, Kata ya Miyuji, Jijini
Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akiweka
fomu ya kupiga Kura katika sanduku la Kura mara baada ya kushiriki zoezi hilo
la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi
katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Dodoma
Makulu, Mtaa wa Msangalale jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akiweka fomu ya kupiga Kura katika sanduku la Kura
mara baada ya kushiriki zoezi hilo la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya
Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa
wa Mwatano jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (aliyesimama) akipokea fomu ya kushiriki
kupiga Kura kutoka kwa Wasimamizi wa Uchaguzi katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na
Madiwani leo tarehe 29 Oktoba,
2025 katika Kata ya Dodoma Makulu, Mtaa wa Msangalale jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (aliyesimama) akisubiri kupatiwa fomu ya kushiriki kupiga Kura kutoka kwa Wasimamizi wa Uchaguzi katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa wa Mwatano jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akionesha jina lake katika orodha ya wapiga Kura iliyobandikwa katika
kituo hicho kabla ya kushiriki kupiga kura katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Dodoma Makulu, Mtaa wa Msangalale
jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akishiriki kupiga Kura katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi
ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa
wa Mwatano jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akionesha kadi yake ya kupiga Kura kabla
ya kushiriki zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika
Kata ya Dodoma Makulu, Mtaa wa Msangalale jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akihakiki jina na picha yake kwenye daftari la kudumu
kabla ya kushiriki zoezi la kupiga Kura katika Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi ya
Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa
wa Mwatano jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi akipakwa wino mara baada ya
kushiriki kupiga Kura katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi kwenye ngazi ya Rais, Wabunge na
Madiwani leo tarehe 29 Oktoba,
2025 katika Kata ya Dodoma Makulu, Mtaa wa Msangalale jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi (wa kwanza kushoto) akipokea fomu ya
kushiriki kupiga Kura kutoka kwa Wasimamizi wa Uchaguzi katika zoezi la
Uchaguzi Mkuu wa Viongozi katika ngazi
ya Rais, Wabunge na Madiwani leo tarehe 29 Oktoba, 2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa wa Mwatano jijini
Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akionesha
kidole kilichopakwa wino mara baada ya kushiriki kupiga Kura katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Viongozi kwenye ngazi ya Rais, Wabunge na
Madiwani leo tarehe 29 Oktoba,
2025 katika Kata ya Miyuji, Mtaa wa Mwatano jijini Dodoma.
Monday, October 27, 2025
OFISI YA RAIS-UTUMISHI YAWAPONGEZA WASTAAFU WA OFISI HIYO KWA KULITUMIKIA TAIFA KIKAMILIFU
Na. Veronica Mwafisi-Dodoma
Tarehe 28 Oktoba, 2025
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora imewapongeza Watumishi wa Ofisi hiyo waliofikia ukomo katika
Utumishi wa Umma kutokana na utumishi uliotukuka kwa kutekeleza majukumu yao
kwa ufanisi ambao umechangia kutolewa kwa huduma bora katika Idara walizokuwa
wakifanyia kazi.
Akitoa pongezi hizo kwa niaba ya Katibu Mkuu, Ofisi
ya Rais-UTUMISHI, leo tarehe 27 Oktoba, 2025, Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, SACP. Ibrahim Mahumi amesema kufikisha umri wa
miaka 60 sio mchezo, ni jambo la kumshukuru Mungu.
“Hongereni sana, mmeondoka katika Utumishi wa
Umma mkiwa na sifa nzuri katika kulitumikia taifa na mkiwa na afya njema ni
mfano mzuri wa kuigwa na tunaoendelea kufanya kazi,” amesema SACP. Mahumi.
SACP. Mahumi amemshukuru Katibu Mkuu-UTUMISHI
kupitia Idara ya Utawala kwa kuanzisha utamaduni wa kukutana kila Jumatatu na
kuwa na ubunifu mbalimbali wa kuwaweka watumishi pamoja kwa lengo la kuboresha
utendaji.
“Tangu jambo hili la kukutana pamoja kila siku ya
Jumatatu kupata elimu ya kuboresha utendaji kumekuwa na mabadiliko makubwa ya
kiutendaji, nawasihi tuendelee kuyatumia mafunzo haya kuboresha utendaji
zaidi.” Amesisitiza.
Akitoa neno la shukrani, Mtumishi Mstaafu wa Ofisi
hiyo, Bw. Jerome Nchimbi amesema, ndani ya miaka 8 aliyofanya kazi katika ofisi
hiyo amejfunza masuala mengi ya Kiutumishi pamoja na kufundishwa upendo, ushirikiano
na kuwajali watu.
Kwa upande wake, Mstaafu mwingine, Bi. Godliver
Byemerwa ametoa wito kwa Watumishi wa ofisi hiyo kuendelea kuwahudumia Wananchi
kwa moyo wa upendo na ufanisi mkubwa kwa kuwa ofisi hiyo ni kioo cha jamii.
Aidha, Ofisi hiyo
imewapongeza Watumishi waliozaliwa mwezi Oktoba na kuwatakia heri katika maisha
yao ya Utumishi wa Umma ili kuwatumikia wananchi pamoja na kuongeza tija katika
utendajikazi.
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa
Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, SACP. Ibrahim Mahumi (wakwanza
kulia) akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa
Watumishi wa ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya
Kuzaliwa katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI
wakimsikiliza Mkurugenzi
wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa ofisi hiyo, SACP.
Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa
ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika
ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya
Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakiwasikiliza Watumishi wastaafu
Bw. Jerome Nchimbi na Bi. Godliver
Byemerwa (hawapo pichani) wa ofisi hiyo walipokuwa wakitoa
shukrani kwa Viongozi na Watumishi mara baada ya kufikia ukomo katika Utumishi
wa Umma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifurahia jambo wakati Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa ofisi hiyo, SACP.
Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa Watumishi wa
ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika
ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi
ya Rais-UTUMISHI, waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa
wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, SACP.
Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa nasaha kwa niaba ya
Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa Watumishi hao katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali
Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa ofisi hiyo, SACP.
Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa ofisi hiyo
waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika ofisi hiyo
iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi na
Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, wa ofisi hiyo, SACP.
Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa
ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika
ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Mtumishi Mstaafu wa Ofisi
ya Rais-UTUMISHI, Bw. Jerome Nchimbi akitoa neno la shukrani kwa Wakurugenzi na
Watumishi wa ofisi hiyo baada ya kuhitimisha Utumishi wake wa Umma.
Sehemu ya Wakurugenzi na
Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, SACP.
Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa
ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika
ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi
ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Mkurugenzi wa
Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa ofisi hiyo, SACP.
Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya
Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha
Siku ya Kuzaliwa katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini
Dodoma.
Mtumishi Mstaafu wa Ofisi
ya Rais-UTUMISHI, Bi. Godliver Byemerwa akitoa neno la shukrani kwa Wakurugenzi
na Watumishi wa ofisi hiyo baada ya kuhitimisha Utumishi wake wa Umma.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakimsikiliza Mkurugenzi wa
Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma wa ofisi hiyo, SACP.
Ibrahim Mahumi (hayupo pichani) wakati akitoa nasaha kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI kwa watumishi wa
ofisi hiyo waliostaafu na Watumishi wanaoadhimisha Siku ya Kuzaliwa katika
ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.























