Na
Veonica Mwafisi-Dar es Salaam
Tarehe
05 Disemba, 2025
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete ameielekeza Menejimenti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)
kufanya tathmini na ufuatiliaji wa shughuli za Mpango
wa Kunusuru Kaya Maskini ili kuona ni kwa kiwango gani malengo ya Mpango huo yanafikiwa,
kubainisha changamoto na kuzishughulikia ili kuboresha utendaji kazi na matokeo
yanayotarajiwa.
Mhe.
Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 05 Disemba, 2025 alipokuwa akizungumza na
Menejimenti ya TASAF wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza
uwajibikaji kwa watumishi wa TASAF jijini Dar es Salaam.
Amesema
kufanya tathmini kutafichua mambo mengi ambayo yalikuwa hayajulikani katika
utekelezaji ambapo itasaidia kuboresha awamu nyingine ya Mpango. “Tufanye
tathmini tuangalie kwanini kunakuwa na utofauti katika mafanikio ili tuone
tunasaidiaje, je wasimamizi wa eneo fulani wana ubunifu zaidi kuliko wa eneo
lingine? Amejiuliza, na kuongeza kuwa haya mambo ni vizuri yakawa shirikishi
ili kuboresha zaidi tutakapoingia kwenye awamu nyingine ya Mpango,” Mhe.
Kikwete ameongeza
Aidha,
ameitaka TASAF kuzungumza mafanikio na changamoto za utekelezaji wa mradi huo
kwa walengwa na wananchi. “Tutoke, tuseme mafanikio na changamoto kwanini
wamekosa, watu waambiwe ukweli, TASAF imefanya mambo makubwa, tuwaonyeshe
waliohitimu, wamefanya nini mpaka kufanikiwa na walioshindwa kufanikiwa wanatakiwa
kufanya nini.” Mhe. Kikwete amesisitiza.
Mhe.
Kikwete ameipongeza taasisi hiyo kwa kazi nzuri waliyoifanya kwa uendelea kuhawilisha ruzuku kwa kaya maskini zinazokidhi vigezo vya
Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini pamoja na kutekeleza miradi ya maendeleo kwenye
Sekta za Afya, Elimu, Maji, Mazingira na ujasiriamali.
Pamoja na pongezi hizo ameitaka TASAF kuendelea
kuboresha shughuli za kuwezesha utekelezaji wa Miradi ya Jamii ya kutoa Ajira
ya muda ili kupunguza changamoto ya ukosefu wa Ajira, kuwezesha jamii
kutekeleza miradi ya kuendeleza miundombinu ya huduma za jamii katika Sekta za
Afya, Elimu, Maji, Mazingira na ujasiriamali na uendelea kufungamanisha
mikakati mbalimbali ya kuwezesha wananchi kiuchumi ili kuhakikisha matokeo
yanayopatika kwenye kila mkakati yanaharakisha kasi ya kuondoa umaskini wa
wananchi.
Vile vile ameitaka Taasisi hiyo kuimarisha miundombinu
ya mifumo ili kulinda usalama wa taarifa za walengwa na kuungamanisha mifumo wa
walengwa na mifumo mingine ya Serikali pamoja na kuongeza idadi ya walengwa
wanaolipwa kwa njia za kielektroniki ili kupunguza dosari za malipo ya ruzuku.
Mhe.
Kikwete amesema malengo makubwa ya yeye na Naibu Waziri Mhe. Mhe. Regina Qwaray
kutembelea TASAF leo ni kujitambulisha na kuendelea kufanya kazi kwa
ushirikiano ili kufikia malengo ya TASAF yaliyokusudiwa.
“Mimi
sio mgeni katika Ofisi hii, hivyo ninawaahidi tutaendelea kushirikiana kama
ambavyo tulikuwa tukifanya siku zote nilipokuwa hapa kwa nafasi ya Naibu Waziri.
Kuletwa kwangu katika Ofisi hii ni kuja kuongeza nguvu ili kupata matokeo
chanya ikiwemo ubunifu katika maeneo mbalimbali. Tufanye kazi tuliyopangwa
kufanya tukiongozwa na misingi yetu ya utendaji kazi. Lengo ni kujenga na
kumsaidia Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kupunguza kaya masikini katika
taifa letu.
Pia
Mhe. Kikwete amesema dhana ya ushirikishwaji wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru
Kaya Maskini ni nzuri kwani imewasaidia kubuni miradi mbalimbali na imepunguza
changamoto nyingi ikiwemo za miundo mbinu, afya na elimu.
Amesisitiza
kuwajengea uwezo wa kifikra walengwa, fedha ziwafikie kwa wakati, usimamizi mzuri
huku wakitambua kuwa msingi mkubwa wa Mpango huo walengwa wake ni wananchi na
si vinginevyo.
Kwa
upande wake Naibu Waziri Mhe. Regina Qwaray ameipongeza TASAF kwa kazi nzuri
wanayoifanya. “Mimi ni mgeni katika Ofisi hii, lakini napenda niwapongeze kwa
kazi nzuri mnayoifanya, TASAF sio ngeni masikioni mwangu, hii inaonyesha ni kwa
jinsi gani mnatekeleza majukumu yenu vizuri, naombeni ushirikiano ili tufanye
kazi kwa pamoja na kuwa na matokeo chanya,” amesema Mhe. Qwaray.
Akiwasilisha
taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF),
Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bw. Shadrack Mziray amesema Mfuko huo ulianzishwa
na Serikali mwaka 2000 kama mojawapo ya mikakati katika kupambana na umaskini
kwa kutumia dhana ya ushirikishaji jamii na imetekelezwa kwa awamu tatu tangu
kuanzishwa kwake.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Watendaji na Menejimeti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)
wakati alipofanya ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika ofisi hiyo
iliyopo jijini Dar es Salaam
Sehemu ya Watendaji na Menejimenti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii
(TASAF) wakimsikiliza Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati
Waziri huyo alipofanya ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika
ofisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina
Qwaray akizungumza na
Watendaji na Menejimeti ya Mfuko wa Maendeleo
ya Jamii (TASAF) kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyekaa) kuzungumza na Watendaji hao walipokuwa kwenye ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji
katika ofisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Bw. Shadrack
Mziray akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za TASAF
kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kuhimiza
uwajibikaji kwa watumishi wa ofisi hiyo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akifuatilia taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)
iliyokuwa ikiwasilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Shadrack Mziray
(hayupo pichani) wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kuhimiza
uwajibikaji katika ofisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Waziri,
Ofisi ya Rais-UTUMISHI na
Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) akifurahia jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Bw. Shadrack
Mziray (wa kwanza kulia) wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo
iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa ofisi hiyo jijini Dar es
Salaam. Wa kwanza kushoto ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Regina
Qwaray.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili
katika ofisi za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii
(TASAF) wakati alipofanya ziara ya kikazi katika ofisi hiyo iliyolenga kuhimiza
uwajibikaji kwa watumishi wa ofisi hiyo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akisalimiana na Naibu Waziri wa Ofisi
yake, Mhe. Regina Qwaray mara baada ya kuwasili katika ofisi za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kwa lengo la kufanya ziara ya kikazi
ili kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa ofisi hiyo jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina
Qwaray (Wa kwanza kulia) akizungumza jambo
na Viongozi na Watendaji wa Mfuko wa Maendeleo
ya Jamii (TASAF) mara baada ya Naibu Waziri huyo kuwasili katika ofisi hizo
kwenye ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji kwa Watumishi wa ofisi
hiyo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (meza kuu kushoto) na Naibu Waziri wa Ofisi yake, Mhe.
Regina Qwaray wakifuatilia taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) iliyokuwa
ikiwasilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Shadrack Mziray (aliyesimama) wakati wa
ziara ya kikazi ya Viongozi hao iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika ofisi hiyo
iliyopo jijini Dar es Salaam. Wengine ni Watendaji na Menejimenti ya TASAF.
Sehemu ya Watendaji na Menejimenti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii
(TASAF) wakimsikiliza Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati
Waziri huyo alipofanya ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika
ofisi hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (waliokaa katikati) akiwa katika picha ya
pamoja na Menejimenti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) jijini Dar es
Salaam wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji wa Watumishi wa ofisi
hiyo.