Monday, March 23, 2026

SERIKALI YAWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUWA WAADILIFU

 Na. Antonia Mbwambo-Dodoma

Tarehe 23 Machi, 2026

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi amewataka watumishi wa Ofisi yake kuzingatia sheria na kanuni za maadili ya utumishi wa umma na kutumia ujuzi wa kitaaluma walionao ili kutoa huduma bora kwa umma.

Bw. Mkomi ameyasema hayo wakati akihitimisha mafunzo ya kila wiki ya kuwajengea uwezo watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora yaliyofanyika katika eneo maalumu la Ofisi hiyo lililopo Mtumba jijini Dodoma.

“Naomba nitoe rai kwenu kuwa kila mtumishi wa Umma kwa nafasi yake ahakikishe anatekeleza majukumu yake kwa uwazi, uaminifu, weledi na ufanisi ili kuepusha malalamiko ya wananchi kwa Serikali” alisema Bw. Mkomi.

Vile vile Bw. Mkomi amezishukuru na kuzipongeza Kurugenzi husika zilizoandaa mada pamoja na watoa Mada kwa uwasilishaji wao mzuri ambao umetoa uelewa utakaoboresha utendaji kazi wa watumishi wa umma.

Awali, Mchambuzi Kazi Mwandamizi kutoka Idara ya Uendelezaji Taasisi Bw. MacDonald Kiwis wakati akiwasilisha mada ya Uandishi wa Nyaraka za Serikali alisema kuwa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Taasisi zote za Umma kwa jumla hazina budi kufuata miongozo ya uandishi wa nyaraka za Serikali ili kuwa na viwango vinavyofanana.

Naye Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi kutoka Idara ya Usimamizi wa Maadili Bw.Hassan Kilenza akiwasilisha mada ya Utambuzi wa Watoa Mrejesho alisema kuwa watumishi wa umma wanatakiwa kutoa mrejesho kwa wateja wakizingatia taratibu na uwepo wa takwimu sahihi ili kuepuka uwepo wa taarifa zisizofanana.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akizungumza na watumishi wa Ofisi yake wakati akihitimisha Mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi hao Machi 23, 2026 jijini Dodoma



Sehemu ya Wakurugenzi wa Idara na Vitengo mbalimbali kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) akizungumza nao wakati alipokuwa akihitimisha mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Mtumba Jijini Dodoma.

Mchambuzi Kazi Mwandamizi kutoka Idara ya Uendelezaji Taasisi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. MacDonald Kiwis akitoa ufafanuzi kuhusu Miongozo ya Uandishi wa Nyaraka za Serikali wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI yaliyofanyika machi 23, 2026 jijini Dodoma.



Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi kutoka Idara ya Usimamizi wa Maadili Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora                            Bw.Hassan Kilenza akiwasilisha mada ya Utambuzi wa Watoa Mrejesho wakati wa mafunzo maalumu ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji watumishi wa Ofisi hiyo machi 23, 2026 Mtumba Dodoma.

Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati alipokuwa akihitimisha mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Mtumba Jijini Dodoma.

Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati alipokuwa akihitimisha mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Mtumba Jijini Dodoma.

Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati alipokuwa akihitimisha mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Mtumba Jijini Dodoma.

Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (hayupo pichani) wakati alipokuwa akihitimisha mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Mtumba Jijini Dodoma.


No comments:

Post a Comment