Na. Veronica Mwafisi-Dodoma
Tarehe 13 Agosti, 2026
Kamati ya
Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imepokea taarifa ya utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambapo imeielekeza Taasisi hiyo kujikita
zaidi kidijiti katika utoaji wa huduma mbalimbali kuhusu namna Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma inavyofanya kazi jambo
ambalo litawasaidia Viongozi wanaowajibika chini ya Sheria ya Maadili kuhusu
Ujazaji wa Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni pamoja na Hati ya Ahadi ya
Uadilifu kwa Viongozi wa Umma na Uwajibikaji wa pamoja ili waweze kukamilisha
kwa wakati taarifa zitakazohitajika katika ujazaji wa fomu hizo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro ametoa kauli hiyo leo
jijini Dodoma alipokuwa akihitimisha kikao cha Kamati yake na Watendaji wa
Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kilichokuwa na lengo la kupokea
taarifa ya Utendaji wa Taasisi hiyo kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa
maadili ya Viongozi wa Umma ikiwemo uhakiki wa uzingatiaji wa ahadi za
uadilifu, tamko la mali na madeni na ushughulikiaji wa malalamiko na mashauri.
Mhe. Dkt Ndumbaro pia amesisitiza
suala la kuongeza juhudi za kutoa elimu zaidi ya
namna ya kujaza fomu mbalimbali za Maadili kwa Viongozi ili kuepukana na
changamoto ya kuchelewesha ujazaji wa taarifa kwani, kuna baadhi ya Viongozi
wanakuwa wapya katika uongozi hivyo inawalazimu kupewa uelewa mpana
utakaowaongoza katika ujazaji wa fomu hizo.
Ameongeza kuwa, utoaji wa elimu zaidi utasaidia jamii kuona namna
Taasisi hiyo inavyofanya kazi kubwa kwa maendeleo ya nchi.
“Ni vema kuongeza elimu zaidi
kuhusu ujazaji wa fomu za maadili kwa Viongozi wanaowajibika chini ya sheria
ili kuepukana na changamoto mbalimbali, wakati mwingine tunapata Viongozi wapya
ambao hawana uelewa mpana juu ya ujazaji wa fomu hizo, hivyo elimu itakapotolewa
itasaidia kupunguza changamoto hizo na kujaza kwa wakati fomu husika lakini pia
elimu hiyo itawapa wananchi uelewa zaidi wa namna Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma inavyotekeleza majukumu
yake kwa ufanisi,’’ Amesema Mhe. Dkt. Ndumbaro
Akiwasilisha
taarifa hiyo, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, Naibu Waziri wa ofisi
hiyo, Mhe. Regina Qwaray amesema Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ina jukumu
la kusimamia tabia na mienendo ya Viongozi wa Umma ili kukidhi matakwa ya
Sheria ya Maadili.
Mhe. Qwaray amesema, Majukumu ya Msingi ya Sekretarieti ya Maadili
ya Viongozi wa Umma ni pamoja na kupokea na kufanya uhakiki wa Matamko ya
Viongozi wa Umma kuhusu Rasilimali, kufanya utafiti juu ya hali ya Maadili na kushauri
na kuweka mikakati katika masuala yanayohusu Uadilifu nchini, kufanya uchunguzi
kuhusu ukiukwaji wa maadili yaliyotajwa na Sheria, kupokea na kushughulikia
malalamiko na taarifa za ukiukwaji wa Maadili kwa mujibu wa Sheria ya Maadili
ya Viongozi wa Umma kutoka kwa wananchi pamoja na kutoa elimu ya Maadili kwa
Viongozi wa Umma.
Naibu Waziri Qwaray ameongeza kuwa, Katika kipindi cha Julai 2025
hadi Juni 2026, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imetekeleza kazi za
usimamizi na ushughulikiaji wa maadili ya viongozi wa umma ikiwemo uhakiki wa
uzingatiaji wa ahadi za uadilifu, tamko la mali na madeni na ushughulikiaji wa
malalamiko na mashauri pamoja na kusaini hati husika pindi viongozi
wanapoteuliwa, kuajiriwa au kuchaguliwa
Pia Mhe. Qwaray amesema, elimu ya maadili itaendelea kutolewa
katika shule na vyuo kupitia klabu za maadili ili kuweza kujenga na kuimarisha
maadili ya kitaifa na kuyafanya yawe sehemu ya jamii pamoja na kuzuia
mmomonyoko wa maadili nchini pamoja na kutoa elimu
kwa wananchi kuhusu Sheria ya Ulinzi wa watoa taarifa ambayo inamhakikishia
usalama na ulinzi.
Akitoa neno la shukrani
kwa Kamati hiyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameishukuru Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria kwa kuendelea kutoa miongozo na
maelekezo ya kiutendaji ambayo yanaongeza chachu na ufanisi katika kuboresha na
kuimarisha utendaji kazi na kuleta tija katika kuwahudumia Viongozi na Wananchi
kwa lengo la kujenga na kuimarisha Utawala Bora nchini.
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria ikiwa katika
kikao na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kilichofanyika
Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa
Taasisi hiyo kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (wa kwanza kushoto)
akifuatilia taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti
ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakati wa kikao cha Kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya
Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Taasisi hiyo
kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifafanua hoja
Bungeni jijini Dodoma wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala,
Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu
usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akiwasilisha kwa Kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya
Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili
ya Viongozi wa Umma wakati wa kikao kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Aziza Ally (wa kwanza kulia) akiwasilisha hoja
kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa kikao kilicholenga
kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya
Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili
ya Viongozi wa Umma kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma.
Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa na Sehemu ya Wajumbe wa
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha
Kamati hiyo na Watendaji wa ofisi hiyo kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu
usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.
Kamshina wa Maadili Mhe. Jaji (Mst.) Sivangilwa Mwangesi (katikati), akiandika maoni yaliyokuwa yakiwasilishwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo Bungeni jijini Dodoma na Watendaji hao kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Taasisi hiyo kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Ahmed Ngwali (wa pili kutoka kulia)
akiwasilisha hoja kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa kikao
kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji
wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Yahaya Nawanda (katikati) akiwasilisha hoja kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa kikao kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Nyamizi Mhoja akifuatilia jambo
wakati wa kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika
Bungeni jijini Dodoma
na Watendaji wa Ofisi ya
Rais-UTUMISHI na Utawala Bora kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya
Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili
ya Viongozi wa Umma.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Mariam Yahya (wa kwanza kushoto) akiwasilisha
hoja kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa kikao
kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu
usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma kilichofanyika Bungeni jijini
Dodoma.
Watendaji na Maafisa wa Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa na Sehemu ya Wajumbe wa
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha
Kamati hiyo na Watendaji wa ofisi hiyo kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu
usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) akisikiliza hoja zilizokuwa zikiwasilishwa na sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa ofisi hiyo kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma. Wa kwanza kushoto ni Naibu Waziri wa ofisi yake Mhe. Regina Qwaray.
Watendaji na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria,
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza Bungeni jijini
Dodoma kwenye kikao cha
Kamati hiyo na Ofisi hiyo kilicholenga kuwasilisha taarifa ya Utendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhusu
usimamizi na ushughulikiaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma.














No comments:
Post a Comment