Monday, August 31, 2026

NAIBU KATIBU MKUU LWANGILI ASISITIZA UZINGATIAJI WA SHERIA KATIKA USHUGHULIKIAJI WA MASHAURI YA NIDHAMU KATIKA UTUMISHI WA UMMA

Na Antonia Mbwambo – Dodoma

Tarehe 31 Agosti, 2026

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili, amesisitiza umuhimu wa kuzingatia Sheria, Taratibu na Kanuni katika kushughulikia mashauri ya nidhamu katika Utumishi wa Umma, akieleza kuwa uzingatiaji wa misingi hiyo ni muhimu katika kuhakikisha haki inatendeka.

Bi. Lwangili ameyasema hayo leo, tarehe 31 Agosti, 2026, wakati akihitimisha mafunzo ya uelewa kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI yaliyofanyika katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba Jijini Dodoma.

Bi. Lwangili amesema katika kushughulikia masuala ya nidhamu ni muhimu kuhakikisha kuwa thamani na utu wa mtu vinalindwa, huku hatua zote zikichukuliwa kwa kuzingatia Sheria, Taratibu na Kanuni zilizowekwa.

“Ni muhimu kuhakikisha kuwa katika kushughulikia mashauri ya nidhamu, Sheria, Taratibu na Kanuni zinafuatwa ili haki itendeke, huku tukilinda thamani na utu wa mtu, amesema Bi. Lwangili.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuwakumbusha Watumishi wa Umma kuhusu madhara ya kutokuzingatia Sheria, Taratibu na Kanuni katika utekelezaji wa majukumu yao, akieleza kuwa uelewa huo utasaidia kupunguza makosa na kuwaepusha watumishi na changamoto ya kufikishwa katika mashauri ya kinidhamu.

Kwa upande wake mwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye ni  Afisa Sheria Mwandamizi, kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Edwin Bilikundi, amesema usimamizi wa nidhamu katika Utumishi wa Umma umejengwa katika dhana mbili kuu ambazo ni kurekebisha mwenendo wa Mtumishi (corrective measures) na utoaji wa adhabu (sanction approach). Amesema njia ya kurekebisha inalenga kumsaidia Mtumishi kutambua kosa na kujirekebisha, wakati utoaji wa adhabu hutumika pale kosa linapothibitika, hususan kwa makosa yanayojirudia au yenye uzito.

Bw. Bilikundi ameongeza kuwa mchakato wa kinidhamu unapaswa kuanza kwa uchunguzi wa awali unaolenga kubaini ukweli na uzito wa tuhuma, pamoja na kuamua hatua stahiki za kuchukua.

Amesisitiza kuwa uzingatiaji wa hatua na muda uliowekwa katika Sheria, Kanuni na Taratibu ni muhimu katika kuhakikisha mchakato wa nidhamu unakuwa wa haki na wenye msingi sahihi wa kisheria.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili akizungumza na Watumishi wa Ofisi hiyo (hawapo pichani) wakati Naibu Katibu Mkuu huyo akihitimisha mafunzo yaliyolenga kuwajengea Watumishi hao uelewa kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu katika Utumishi wa Umma, yaliyofanyika tarehe 31 Agosti, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo, Mtumba, jijini Dodoma.

Baadhi ya Wakurugenzi na Watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji leo tarehe 31 Agosti, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma

Afisa Sheria Mwandamizi, kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Edwin Bilikundi akiendesha mafunzo ya uelewa kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu katika Utumishi wa Umma kwa Watumishi wa Ofisi hiyo leo tarehe 31 Agosti 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo, Mtumba, jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Musa Magufuli akisisitiza jambo wakati wa mafunzo ya uelewa kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu katika Utumishi wa Umma Mtumba Jijini Dodoma


Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili  akisisitiza jambo wakati akihitimisha mafunzo ya kuwajengea Watumishi hao uelewa kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu katika Utumishi wa Umma, yaliyofanyika tarehe 31 Agosti, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo, Mtumba, jijini Dodoma

Baadhi ya Watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji leo tarehe 31 Agosti, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma

Baadhi ya Wakurugenzi na Watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji leo tarehe 31 Agosti, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma

Baadhi ya Wakurugenzi na Watumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakifuatilia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji leo tarehe 31 Agosti, 2026 katika eneo maalumu la Ofisi hiyo Mtumba jijini Dodoma

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili (wa pili kutoka kushoto) akifurahia jambo wakati alipokuwa akifuatilia mafunzo kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu katika Utumishi wa Umma leo Agosti 31, 2026 Mtumba Jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, SACP. Ibrahim Mahumi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI akisisitiza jambo wakati wa mafunzo ya uelewa kuhusu Ushughulikiaji wa Mashauri ya Nidhamu katika Utumishi wa Umma Mtumba Jijini Dodoma




 

No comments:

Post a Comment