Na. Veronica Mwafisi-Dodoma
Tarehe 12 Agosti, 2026
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imepokea taarifa
ya utendaji wa Tume ya Utumishi wa Umma na kusisitiza kutolewa kwa elimu zaidi kwa
Watumishi wa Umma ili waweze kuwasilisha rufaa na malalamiko kwa wakati na
mahali husika kwa lengo la kutimiza haki na wajibu katika utendajikazi.
Kauli hiyo imetolewa jijini Dodoma leo na Mwenyekiti wa Kamati ya
Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro alipokuwa
akiongoza kikao cha Kamati yake na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Tume
ya Utumishi wa Umma kilicholenga kupokea taarifa ya Utendaji wa Tume hiyo
katika kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka
za Ajira.
“Elimu inahitajika zaidi kwa Watumishi wa Umma kwenye maeneo yao ya
kazi ili kuongeza uelewa wa namna ya kushughulikia rufaa na malalamiko hayo
ikiwa ni pamoja na kupata utatuzi wa migogoro katika Utumishi wa Umma,’’
Amesisitiza Mhe. Dkt. Ndumbaro
Katika hatua nyingine, Mhe. Dkt. Ndumbaro amempongeza na kumshukuru Waziri Kikwete kwa taarifa nzuri
aliyoiwasilisha kwa Kamati hiyo iliyoelezea kwa kina taarifa ya utendaji ya Tume ya Utumishi wa Umma katika kushughulikia
rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira ambayo itaongeza chachu ya
utendaji kazi kwa Watumishi wa Umma.
Mhe. Dkt. Ndumbaro ameiahidi Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora
kuwa itashirikiana nayo katika usimamizi wa masuala mbalimbali ili kuleta
matokeo chanya kwa ustawi wa Taifa.
Awali akiwasilisha kwa Kamati hiyo taarifa ya utendaji ya Tume ya
Utumishi wa Umma katika kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi
wa Umma na Mamlaka za Ajira, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema, Tume ya
Utumishi wa Umma ni Mamlaka ya Rufaa kwa Watumishi wa Umma katika taasisi 554 waliopo
kwenye makundi mbalimbali ya Watumishi wa Umma, Serikali Kuu, Mamlaka ya
Serikali za Mitaa na Watumishi waliopo katika Taasisi za Umma.
Vilevile, Mhe. Kikwete amesema Tume hiyo ina jukumu la kupokea
malalamiko na rufaa kutoka kwa Watumishi wa Umma ambao hawakuridhika na uamuzi
wa mamlaka zao za ajira, mamlaka za nidhamu na waajiri baada ya uamuzi
walioufanya na mamlaka hizo hivyo, elimu itakayotolewa kwa Watumishi wa Umma
itasaidia kwa kiasi kikubwa kupata haki na wajibu kwa kila mmoja.
Aidha, Mhe. Kikwete ameishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala, Katiba na Sheria, kwa kuwa na majadiliano mazuri na ofisi anayoiongoza
ambayo wanaamini yatawasaidia kwa kiasi kikubwa katika kuongeza ufanisi na
utendaji wa majukumu yao.
“Mhe. Mwenyekiti, nitoe shukrani za dhati kwa niaba ya ofisi
ninayoiongoza mara zote tumepokea maoni, ushauri na michango mbalimbali kutoka
katika Kamati yako inayolenga kuboresha Utumishi wa Umma nchini kwa lengo la
kutimiza azma ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwa na Utumishi wa Umma
uliotukuka.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi
amesema Kamati hiyo imekuwa msaada mkubwa wa kuiongoza Ofisi ya Rais-UTUMISHI
na Utawala Bora kwa kuwapatia maarifa mengi kutoka kwa Wajumbe wote wa Kamati
hiyo yenye kuleta tija katika kuwahudumia wadau
mbalimbali na kuboresha utendajikazi.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria,
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (aliyesimama) akizungumza wakati wa kikao cha Kamati
yake kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma na Watendaji wa Ofisi ya
Rais-UTUMISHI na Taasisi ya Tume ya Utumishi wa Umma baada ya Tume hiyo
kuwasilisha taarifa kuhusu kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa
Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria,
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akizungumza wakati wa kikao cha Kamati yake kilichofanyika
Bungeni jijini Dodoma na Watendaji wa Ofisi ya
Rais-UTUMISHI na Taasisi ya Tume ya Utumishi wa Umma baada Tume hiyo
kuwasilisha taarifa kuhusu kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa
Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwasilisha kwa
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na
Mamlaka za Ajira wakati wa kikao kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma. Wengine
ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwasilisha kwa
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na
Mamlaka za Ajira wakati wa kikao kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma. Wengine
ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI
Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakifuatilia jambo wakati wa kikao cha
Kamati hiyo kilichofanyika Bungeni
jijini Dodoma na
Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na
Mamlaka za Ajira.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete
(kulia) akiwa katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na
Sheria
kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma na Watendaji wa Ofisi ya
Rais-UTUMISHI kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa
Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira. Kulia kwake ni Naibu Waziri wa ofisi yake
Mhe. Regina Qwaray.
Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakiwa kwenye kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI
kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia
rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira.
Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakifuatilia jambo wakati wa kikao cha
Kamati hiyo kilichofanyika Bungeni
jijini Dodoma na
Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na
Mamlaka za Ajira.
Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria,
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza wakati wa kikao cha Kamati hiyo Bungeni jijini Dodoma na Watendaji hao kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na
Mamlaka za Ajira.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akifafanua hoja
Bungeni jijini Dodoma wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala,
Katiba na Sheria kilicholenga kuwasilisha taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na
Mamlaka za Ajira.
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw.
Nolasco Kipanda (aliyesimama) akisikiliza maoni kutoka kwa Wajumbe wa Kamati ya
Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa kikao cha Kamati hiyo Bungeni jijini Dodoma na Watendaji hao kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na
Mamlaka za Ajira.
Katibu Mkuu-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi (aliyesimama)
akifafanua hoja iliyowasilishwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba
na Sheria wakati wa kikao kilicholenga kuwasilisha taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na
Mamlaka za Ajira kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Mariam Yahya (wa pili kutoka kushoto) akiwasilisha hoja kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa kikao kilicholenga kuwasilisha taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI
na Utawala Bora, Bi. Prisca Lwangili akishukuru baada ya kupokea pongezi kutoka
kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria ya kuteuliwa na Mhe.
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Naibu Katibu Mkuu wa ofisi hiyo. Pongezi
hizo zimetolewa baada ya kikao cha Kamati hiyo na Watendaji wa ofisi hiyo kilicholenga
kutoa taarifa ya kushughulikia
rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira.
Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria,
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza kwenye kikao cha Kamati hiyo Bungeni jijini Dodoma na Watendaji hao kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na
Mamlaka za Ajira.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Edwin Swalle (wa kwanza kulia) akiwasilisha hoja
kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati wa kikao kilicholenga
kuwasilisha taarifa ya kushughulikia
rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na Mamlaka za Ajira
kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma.
Watendaji na Maafisa kutoka Ofisi ya
Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria,
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza kwenye kikao cha Kamati hiyo Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na
Mamlaka za Ajira.
Watendaji na Maafisa kutoka Ofisi ya
Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria,
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza kwenye kikao cha Kamati hiyo Bungeni jijini Dodoma kilicholenga kutoa taarifa ya kushughulikia rufaa na malalamiko kutoka kwa Watumishi wa Umma na
Mamlaka za Ajira.


















No comments:
Post a Comment