Friday, December 6, 2024

NENDENI MKALETE MAPINDUZI KATIKA MADAWATI YA KUSHUGHULIKIA MREJESHO KATIKA OFISI ZA UMMA- BI. LEILA MAVIKA

 


          Na. Lusungu Helela- Dodoma

 Mwakilishi wa  Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI,  Bi. Leila Mavika amewataka Waratibu wa Kushughulikia Mrejesho wakayatumie mafunzo waliyoyapata kuleta mapinduzi  katika  Madawati au Ofisi za Mrejesho zilizopo katika Taasisi zao  ili kufanikisha ushughulikiaji mrejesho kwa ufanisi na kwa wakati katika Ofisi za Umma kwa vile   wameaminiwa kutekeleza jukumu hilo kwa ufanisi.

 

Amewataka wakawe waaminifu na wenye haiba inayokubalika na  Wateja wa ndani na nje ya Taasisi ili kuwafanya Wateja wao  kuwa huru kufikisha malalamiko yao bila ya kuwa na wasiwasi wa aina yeyote.

 

Bi.Mavika ametoa kauli hiyo leo  jijini Dodoma wakati akifunga mafunzo maalum yaliyofanyika  kwa muda wa  siku tatu kwa Waratibu wa Kushughulikia Mrejesho kuhusu  uendeshaji wa mfumo wa e-Mrejesho katika Ofisi za Umma.

 

Bi.Mavika mewataka Waratibu hao kutoa  fursa sawa  kwa wananchi wote  kwa  kutumia mfumo wa  e-Mrejesho ili kuwawezesha wateja  kutuma  malalamiko, pongezi pamoja na maulizo kwa Serikali mahali popote na wakati wowote.

 

Aidha, Mwakilishi huyo wa Katibu Mkuu,UTUMISHI, Bi.Mavika amewaonya Waratibu hao kuacha tabia ya kushughulikia mrejesho wa wananchi mara tu wanaposikia kuna ukaguzi maalum kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

 

" Nendeni mkawe kioo fanyeni kazi muda wote, hatutegemei kuona mnashughulikia mrejesho kutoka wananchi mara tu mnaposikia kuna ukaguzi maalum" amesisitiza Bi.Mavika.

 

Awali Kaimu Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Bi. Janeth Mishinga ameeleza kuwa licha ya Waratibu hao kupewa mafunzo hayo ya kushughulikia mrejesho kwa wananchi kwa wakati pia wamepewa mafunzo ya mbalimbali ya kuwafanya kuwa Watumishi wa mfano katika jamii

Naye Mwenyekiti wa Waratibu wa kushughulikia Mrejesho, Denis Gondwe akizungumza kwa niaba ya Waratibu hao amesema mafunzo hayo yamekuwa ni muhimu sana kwao ikizingatiwa kuwa  shabaha ya Serikali ya awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan ni kutoa huduma bora kwa wananchi wote bila ubaguzi wa aina yoyote.

 

 


Mwakilishi wa Katibu Mkuu, UTUMISHI, Bi.Leila Mavika  akizungumza na Waratibu wa Kushughulikia Mrejesho  jijini Dodoma wakati akifunga mafunzo maalum yaliyofanyika kwa muda wa  siku tatu kwa Waratibu  hao kuhusu  uendeshaji wa mfumo wa e-Mrejesho katika Ofisi za Umma



 Kaimu Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Bi. Janeth Mishinga   akizungumza na Maafisa Mrejesho jijini Dodoma kabla ya kumkaribisha Mwakilishi wa Katibu Mkuu, UTUMISHI, Bi.Leila Mavika kufunga mafunzo maalum ya siku tatu kwa Waratibu hao kuhusu  uendeshaji wa mfumo wa e-Mrejesho katika Ofisi za Umma

 

 


Kaimu Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Bi. Janeth Mishinga akiwa ameongoza na  Mwakilishi wa Katibu Mkuu, UTUMISHI, Bi.Leila Mavika  akiwasili kwa ajili ya  kufunga mafunzo maalum ya siku tatu kwa Waratibu wa kushughulikia Mrejesho kuhusu  uendeshaji wa mfumo wa e-Mrejesho katika Ofisi za Umma

 


Mwakilishi wa Katibu Mkuu, UTUMISHI, Bi.Leila Mavika (katikati) akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Usimamizi wa Maadili, Bi. Janeth Mishinga kabla ya Mwakilishi wa Katibu Mkuu, UTUMISHI, Bi. Leila Mavika ya  kufunga mafunzo maalum ya siku tatu kwa Waratibu hao kuhusu  uendeshaji wa mfumo wa e-Mrejesho katika Ofisi za Umma, wa kwanza kulia ni  Mwenyekiti wa Waratibu wa kushughulikia Mrejesho, Denis Gondwe 

 

 

 




Baadhi ya Waratibu wa Kushughulikia Mrejesho wakimsikiliza Mwakilishi wa Katibu Mkuu, UTUMISHI, Bi.Leila Mavika  akizungumza nao leo  jijini Dodoma wakati akifunga mafunzo maalum yaliyofanyika kwa muda wa  siku tatu kwa Waratibu  hao kuhusu  uendeshaji wa mfumo wa e-Mrejesho katika Ofisi za Umma

 


 Mwenyekiti wa Waratibu wa kushughulikia Mrejesho, Denis Gondwe akizungumza Waratibu wa Kushughulikia Mrejesho  jijini Dodoma kabla ya Mwakilishi wa Katibu Mkuu, UTUMISHI, Bi. Leila Mavika kufunga mafunzo maalum yaliyofanyika kwa muda wa  siku tatu kwa Waratibu  hao kuhusu  uendeshaji wa mfumo wa e-Mrejesho katika Ofisi za Umma



Mwezeshaji wa mafunzo kwa  Waratibu wa kushughulikia Mrejesho, Bw. Hassan akizungumza Waratibu wa Kushughulikia Mrejesho  jijini Dodoma kabla ya Mgeni rasmi Mwakilishi wa Katibu Mkuu, UTUMISHI, Bi. Leila Mavika kufunga mafunzo maalum yaliyofanyika kwa muda wa  siku tatu kwa Waratibu  hao kuhusu  uendeshaji wa mfumo wa e-Mrejesho katika Ofisi za Umma


No comments:

Post a Comment