Na. Mwandishi Mwetu-Dodoma
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu ametoa pongezi kwa Wizara na Taasisi za Umma kwa kuwa na utayari wa kuwahudumia watumishi wa umma na wananchi katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.
“Tumekuwa tukifanya kliniki katika mikoa mbalimbali kwa ajili ya kutatua kero na changamoto mbalimbali zinazowakabili Watumishi wa Umma na Wananchi, lakini kupitia Maadhimisho haya ya Wiki ya Utumishi wa Umma yamekuwa suluhisho kwa kufanya kazi papo kwa hapo kwani Watumishi wa Umma na Wananchi wamekuja kuhudumiwa kwa wakati,hii inaonesha ni kwa namna gani mmekuwa na utayari wa kutoa huduma bora kwa maslahi ya taifa, hongereni sana,” Mhe. Sangu amesema
Aidha, Mhe. Sangu ametoa rai kwa Watanzania wote kufika katika Viwanja hivyo ili kupata huduma za moja kwa moja na elimu kuhusu shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na Wizara na taasisi za Umma.
Katika hatua nyingine, Mhe. Sangu amemshukuru
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali
watumishi wa umma nchini kwa kuboresha maeneo yao ya kazi kwa kuwa sehemu
salama ili watanzania waweze kupata huduma bora.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (kushoto) akisalimiana na
Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi (kulia) baada ya Naibu Waziri huyo
kuwasili katika Viwanja vya Chinangali Park kutembelea mabanda ya Wizara na
Taasisi zilizoshiriki Wiki ya Utumishi wa Umma jijini Dodoma.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (kushoto) akisisitiza jambo kwa Maafisa wa Baraza
la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) baada ya Naibu Waziri huyo
kutembelea banda la ofisi hiyo Viwanja vya Chinangali Park katika Wiki ya
Utumishi wa Umma jijini Dodoma.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (kulia) akisaini kitabu cha wageni
alipotembelea banda la ofisi ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (Upanga na
Mloganzila) yanapofanyika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma katika
Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (aliyekaa kushoto) akifurahia kucheza mchezo wa
drafti wakati alipotembelea banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na
Michezo katika Viwanja vya Chinangali Park kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma
jijini Dodoma.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (kulia) akizungumza na Kikosi cha Zimamoto na Uokozi-Zanzibar walipokuwa wakijitambulisha baada ya kutembelea Viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma kwemye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2025.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (kushoto) akimsikiliza Wakili wa Serikali Mwandamizi, Bi. Aveline Ombock
(aliyeshika kipaza sauti) alipokuwa akielezea namna walivyoshiriki na kutoa
huduma kwa wananchi katika Wiki ya Utumishi wa Umma
2025 inayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (kulia) akimsikiliza Afisa Usajili na Udhibiti Ubora-OSHA, Bw. Ramadhani
Kajembe alipokuwa akielezea ushiriki wa ofisi hiyo katika Wiki ya Utumishi wa
Umma 2025 inayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (kushoto) akimsikiliza Meneja
Utekelezaji Sheria na Kushughulikia Malalamiko (TIRA), Bw. Okoka Jailo alipokuwa
akielezea majukumu ya ofisi hiyo wakati Naibu Waziri huyo alipotembelea banda hilo
kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma
yanayofanyika Viwanja vya Chunangali Park jijini Dodoma.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (anayesaini kitabu) akifurahia jambo wakati
alipotembelea banda la ofisi ya Mamlaka ya Maeneo Maalum ya uzalishaji kwa
mauzo ya nje (EPZA) wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma
yanayofanyika Viwanja vya Chunangali Park jijini Dodoma. Kushoto kwake ni
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (kushoto) akimsikiliza Msanifu Majengo, Baraza la
Taifa la Ujenzi (NCC), Bi. Mariahildagard Byarufu alipokuwa akielezea majukumu
ya ofisi hiyo wakati Naibu Waziri huyo alipotembelea banda hilo kwenye
Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika Viwanja vya Chunangali
Park jijini Dodoma.
No comments:
Post a Comment