Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (aliyevaa suti) akifurahia
pongezi kutoka kwa mwananchi aliyefika katika banda la Ofisi ya Rais-UTUMISHI kwenye
Wiki ya Utumishi wa Umma katika Viwanja vya Chinangali
Park jijini Dodoma.
Maafisa kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora wakimhudumia Mtumishi wa Umma aliyefika katika banda la
ofisi hiyo kupata huduma za kiutumishi kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mary Mwakapenda (kulia) akimkaribisha Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Ernest Mabonesho (kushoto) kusaini kitabu cha wageni katika banda la Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakati wa Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.
Afisa TEHAMA, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Selemani Sultan akifafanua jambo kuhusu huduma za e-Utendaji kwa Watumishi wa Umma waliofika banda la ofisi hiyo kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika Viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.
Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakitoa fafanuzi mbalimbali kuhusu majukumu ya ofisi hiyo kwa Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Anazak walipotembelea banda la ofisi hiyo kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma inayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.
Afisa Sheria Mwandamizi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI,
Bi. Aveline Ilahuka akiwa na Mtumishi wa Umma kutoka Jeshi la Polisi baada ya
kumpatia huduma kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma
inayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.
Afisa Utumishi kutoka
Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Loveness Choga akimhudumia mteja aliyefika katika
banda la Ofisi ya Rais-UTUMISHI kupata huduma za kiutumishi wakati wa Maonesho
ya Wiki
ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park Jijini
Dodoma.
Afisa Utumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Aristides Masigati akiwahudumia wananchi waliofika katika banda la Ofisi ya Rais-UTUMISHI kupata huduma za kiutumishi wakati wa Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.
No comments:
Post a Comment