Sunday, June 22, 2025

HUDUMA ZA KIUTUMISHI ZATOLEWA NA OFISI YA RAIS-UTUMISHI KWENYE WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2025


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (aliyevaa suti) akifurahia pongezi kutoka kwa mwananchi aliyefika katika banda la Ofisi ya Rais-UTUMISHI kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. 

Maafisa kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimhudumia Mtumishi wa Umma aliyefika katika banda la ofisi hiyo kupata huduma za kiutumishi kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. 

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mary Mwakapenda (kulia) akimkaribisha Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Ernest Mabonesho (kushoto) kusaini kitabu cha wageni katika banda la  Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakati wa Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.

 

Afisa TEHAMA, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Selemani Sultan akifafanua jambo kuhusu huduma za e-Utendaji kwa Watumishi wa Umma waliofika banda la ofisi hiyo kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika Viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma


Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI wakitoa fafanuzi mbalimbali kuhusu majukumu ya ofisi hiyo kwa Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Anazak walipotembelea banda la ofisi hiyo kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma inayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.

Afisa Sheria Mwandamizi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Aveline Ilahuka akiwa na Mtumishi wa Umma kutoka Jeshi la Polisi baada ya kumpatia huduma kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma inayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.



Afisa Utumishi kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Aristides Masigati akiwahudumia wananchi waliofika katika banda la Ofisi ya Rais-UTUMISHI kupata huduma za kiutumishi wakati wa Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.


No comments:

Post a Comment