Na. Veronica Mwafisi-Dodoma
Katibu Mkuu ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma, Bw. Juma Mkomi ametoa rai kwa Watumishi wa Umma kuzingatia Itifaki
katika Utumishi wa Umma ili kuongeza uwajibikaji na uadilifu kiutendaji kwa maslahi mapana ya Taifa.
Bw. Mkomi ameyasema hayo jijini Dodoma wakati akizungumza na watumishi wa
ofisi hiyo katika eneo maalum la mafunzo
kwa watumishi hao mara baada ya mkufunzi aliyekuwa akitoa mafunzo kuhusu
Itifaki kuhitimisha mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa kwa lengo la kuwajengea uwezo na uelewa wa
Itifaki katika Utumishi wa Umma.
Akiwasilisha mada kuhusu Itifaki, Mwezeshaji wa Mafunzo, Mhadhiri wa Diplomasia, kutoka Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim, Bw. Lucas Humo amesema Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora ina majukumu mengi ikiwemo utoaji wa huduma mbalimbali za kiutumishi hivyo, ni muhimu kila mtumishi akajua wajibu wake ili aweze kuwahudumia Viongozi, Watumishi wa Umma na Wananchi kwa kuzingatia Itifaki mbalimbali zitakazosaidia kuonesha taswira nzuri ya ofisi.
Aidha, Bw. Humo amesema, Itifaki inahusisha namna inavyopaswa kuwasiliana, kushirikiana, na
kufanya maamuzi kwa njia inayoheshimu sheria na taratibu zilizowekwa.
“Watumishi wa umma
wanatakiwa kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia uadilifu na uwazi kwa namna
ya kuwasiliana, kushirikiana na kufanya maamuzi hivyo, wakifuata Itifaki na
kuzitekeleza kwa ufanisi itaboresha utendaji kazi”, amesema Bw. Humo.
Bw. Humo, amewaasa
watumishi hao kutunza taarifa za ofisi, kuzingatia muda wa kazi wakati wa
kuingia na kutoka, kuwajali wageni wanapowasilisha masuala yao ya kiutumishi, kuzingatia
mavazi wanapokuwa katika eneo la kazi pamoja na kuwatambua wageni wanapofika
katika ofisi hiyo kwa vyeo vyao ili kutoa huduma kwa haki na usawa.
Katibu
Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma,
Bw. Juma Mkomi akizungumza jambo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi kwa watumishi wa ofisi hiyo yaliyofanyika
katika Mji wa Serikali Mtumba,
jijini Dodoma.
Mhadhiri
wa Diplomasia, kutoka Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed
Salim, Bw. Lucas Humo akifafanua jambo wakati akiwasilisha mada kuhusu Itifaki wakati
wa mafunzo kwa watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI yaliyolenga kuwajengea
uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba,
jijini Dodoma. Wanaomsikiliza ni Wakurugenzi na Watumishi wa
ofisi hiyo.
Sehemu ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia mada kuhusu Itifaki wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini
Dodoma.
Sehemu ya Viongozi, Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia mada kuhusu Itifaki
wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo
Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Mhadhiri wa Diplomasia, kutoka
Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim, Bw. Lucas Humo (kulia)
akionyesha kwa vitendo Itifaki ya kusalimiana wakati wa mafunzo kwa watumishi
wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI yaliyolenga kuwajengea uwezo na kuimarisha
utendaji kazi yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma. Kushoto ni Mkurugenzi
wa Idara ya Uendelezaji wa Taasisi, ambaye ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa
Umma, Bw. Nolasco Kipanda.
Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia mada kuhusu Itifaki
wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo
Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.
Mtumishi
kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Joyce Atanas akiuliza swali kuhusu Itifaki mara baada ya Mhadhiri
wa Diplomasia, Bw. Lucas Humo (hayupo pichani) kuwasilisha mada kuhusu Itifaki
mbalimbali katika Utumishi wa Umma wakati wa mafunzo kwa watumishi wa ofisi hiyo yaliyolenga kuwajengea
uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba,
jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakurugenzi na Watumishi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI, wakifuatilia jambo wakati wa mafunzo ya kuwajengea
uwezo na kuimarisha utendaji kazi yaliyofanyika katika ofisi hiyo iliyopo Mji wa Serikali
Mtumba, jijini Dodoma.

No comments:
Post a Comment