Thursday, February 23, 2023

MHE. NDEJEMBI AWAASA WATUMISHI WA UMMA KUWAHUDUMIA VIZURI WANANCHI ILI KUJENGA TASWIRA NZURI YA SERIKALI KWA UMMA

 Na. Veronica E. Mwafisi-Njombe

Tarehe 23 Februari, 2023

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi amewaasa watumishi wa umma nchini kuwahudumia vizuri wananchi ambao ndio walengwa wakuu wa huduma zitolewazo na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. 

Mhe. Ndejembi wito huo kwa watumishi wa umma, wakati wa kikao kazi chake na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Mji Njombe mkoani Njombe kilicholenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi hao katika halmashauri hiyo.

Mhe. Ndejembi amesema, kila mtumishi wa umma nchini akitimiza wajibu wake kuna uwezekano mkubwa wa kutatua matatizo ya wananchi kwani kila mtumishi wa umma kwa nafasi yake ni mwakilishi wa Serikali hivyo anapaswa kuilinda taswira ya Serikali kwa kutoa huduma nzuri kwa wananchi ili wananchi wajivunie uwepo wa serikali yao.

Mhe. Ndejembi ameongeza kuwa, watumishi wa umma wanapaswa kutoa huduma bora kwa wananchi kwani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesimamia na anaendelea kusimamia vema masilahi ya watumishi wote wa umma nchini, hivyo ni wajibu wa kila mtumishi kufanya kazi kwa bidii ikiwa ni sehemu ya kuthamini na kuunga mkono jitihada hizo za Rais wa Awamu ya Sita Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kwa Upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe, Mhe. Erasto Mpete amemshukuru Naibu Waziri Ndejembi kwa kufanya ziara ya kikazi katika Halmashauri ya Mji Njombe ili kuhimiza uwajibikaji, kusikiliza na kutatua kero za watumishi wa halmashauri hiyo kitendo ambacho kimejenga ari na morali ya utendaji kazi wa watumishi wa umma katika halmashauri yake.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi anaendelea na ziara yake ya kikazi  katika Halmashauri ya Mji Njombe kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma, kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa umma ikiwa ni pamoja na kukagua utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini Halmashauri hiyo ya mji mkoani Njombe.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Mji Njombe, wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji, kutatua changamoto zinazowakabili watumishi hao na kukagua utekelezaji wa Miradi ya TASAF katika Halmshauri hiyo ya mji mkoani Njombe.


Watumishi wa Umma wa Halmashauri ya Mji Njombe wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji, kutatua changamoto zinazowakabili watumishi hao na kukagua utekelezaji wa Miradi ya TASAF katika Halmshauri hiyo mkoani Njombe.


Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Mhe. Kissa Gwakisa akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi kuhimiza uwajibikaji, kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa umma na kukagua utekelezaji wa Miradi ya TASAF katika wilaya yake wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo katika Halmshauri ya Mji Njombe mkoani Njombe.


Mkuu wa Idara ya Utawala na Utumishi, Halmashauri ya Mji Njombe, Bi. Ester Zullu akisoma taarifa ya utumishi ya halmashauri hiyo ya mji kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji, kutatua changamoto zinazowakabili watumishi na kukagua utekelezaji wa Miradi ya TASAF katika Halmshauri hiyo ya mji.


Mtumishi wa Halmashauri ya Mji Njombe, Dkt. Stephano Mbapila akiwasilisha hoja ya kiutumishi kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji, kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa umma na kukagua utekelezaji wa Miradi ya TASAF katika Halmshauri hiyo ya mji mkoani Njombe.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akisikiliza hoja iliyokuwa ikiwasilishwa na mtumishi wa Halmashauri ya Mji Njombe wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji, kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa umma na kukagua utekelezaji wa Miradi ya TASAF katika Halmshauri hiyo ya mji mkoani Njombe.



No comments:

Post a Comment