Wednesday, January 14, 2026

“TUENDELEZE USHIRIKIANO ILI KUJENGA UTUMISHI WA UMMA ULIOTUKUKA” BW. XAVIER DAUDI ASISITIZA

 Na. Antonia Mbwambo -Dodoma

Tarehe 15 Januari, 2026

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Xavier Daudi ametoa wito kwa baadhi ya wakurugenzi wa Idara za Ofisi yake pamoja na Ofisi ya Rais, Katiba Sheria na Utawala Bora ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuendeleza ushirikiano uliopo ili kuleta mageuzi na kujenga Utumishi wa Umma uliotukuka kwa ustawi wa Taifa.

Bw. Daudi ameyasema hayo leo tarehe 15 Januari, 2026 wakati akimwakilisha Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Juma Mkomi katika kikao cha kubadilishana uzoefu wa utekelezaji wa majukumu ya kiutumishi kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi hiyo uliyopo Mtumba jijini Dodoma.

“Ili kujenga na kuboresha Utumishi wa Umma wenye tija ni vizuri tukashirikiana wenyewe kwa wenyewe hasa kwa yale mazuri tuliyo nayo ndani ya muungano” Bw. Xavier alisema.

Nae Naibu Katibu Mkuu Utumishi na Utawala Bora wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Bw. Omar Haji Gora ameushukuru uongozi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI chini ya Katibu wake Mkuu Bw. Juma Mkomi kwa Kuwaonesha ushirikiano kila wakati na kuahidi kuwa yale yote waliyojifunza wataenda kuyafanyia kazi ili kuleta mageuzi katika Utumishi wa Umma.

“Tumepata faraja kuwa hapa, na yale ambayo tumejifunza tunaenda kuyafanyia kazi ili kuendelea kujenga utumishi wa umma ulio Bora” Bw. Gora alisema.

 

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Xavier Daudi akizungumza na wakurugenzi wa Idara za Ofisi yake pamoja na Viongozi kutoka Ofisi ya Rais, Katiba Sheria na Utawala Bora ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kikao cha kubadilishana uzoefu wa utekelezaji wa majukumu ya kiutumishi kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi hiyo uliyopo Mtumba jijini Dodoma


Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) kikao cha kubadilishana uzoefu wa utekelezaji wa majukumu ya kiutumishi kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi hiyo uliyopo Mtumba jijini Dodoma

Naibu Katibu Mkuu Utumishi na Utawala Bora Bw. Omar Haji Gora akitoa neno la shukrani kwa Uongozi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora baada ya kuhitimisha kikao cha kubadilishana uzoefu wa utekelezaji wa majukumu ya kiutumishi kilichofanyika leo tarehe  15 Januari, 2026 katika ukumbi wa Ofisi hiyo uliyopo Mtumba jijini Dodoma

Sehemu ya Washiriki kutoka Ofisi Kuu ya Utumishi wa Umma Zanzibar wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) akizungumza nao katika kikao cha kubadilishana uzoefu wa utekelezaji wa majukumu ya kiutumishi kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi hiyo uliyopo Mtumba jijini Dodoma

Sehemu ya washiriki wa kikao cha kubadilishana uzoefu wa utekelezaji wa majukumu ya kiutumishi wakisikiliza fafanuzi mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (hawapo pichani) katika kikao cha kubadilishana uzoefu wa utekelezaji wa majukumu ya kiutumishi kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi hiyo uliyopo Mtumba jijini Dodoma

Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) katika kikao cha kubadilishana uzoefu wa utekelezaji wa majukumu ya kiutumishi kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi hiyo uliyopo Mtumba jijini Dodoma

Sehemu ya washiriki wa kikao cha kubadilishana uzoefu wa utekelezaji wa majukumu ya kiutumishi wakisikiliza wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Xavier Daudi (hayupo pichani) katika kikao cha kubadilishana uzoefu wa utekelezaji wa majukumu ya kiutumishi kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi hiyo uliyopo Mtumba jijini Dodoma




No comments:

Post a Comment