Friday, January 9, 2026

MHE. QWARAY ASISITIZA UTUNZWAJI MIRADI YA TASAF

Na Antonia Mbwambo-Arusha

Tarehe 9 Januari, 2026

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe Regina Qwaray amesisitiza waratibu wa miradi ya TASAF kwa kushirikiana na kaya nufaika kulinda miradi dhidi ya waharifu wa miundombinu hiyo ili iweze kutumika kwa manufaa ya walengwa na taifa kwa jumla.

Mhe. Qwaray ameyasema hayo leo Januari 9, 2026 alipokuwa akizungumza na waratibu, wasimamizi na wanufaika wa miradi ya TASAF Mkoani Arusha.

Mhe. Qwaray amewapongeza TASAF kwa taarifa nzuri ya ujenzi wa shule ya sekondari Oldonuwas iliyopo kijiji cha Oldonuwas na ujenzi wa mfereji wa umwagiliaji uliopo Meru kijiji cha Ngabobo wilaya ya Meru.

“Nimesikiliza taarifa zenu na nimejionea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa miradi hiyo yenye manufaa kwa wanufaika wa TASAF na taifa kwa jumla, hivyo nitoe rai ya kuilinda na kuithamini ili tupate tija iiyokusudiwa na Serikali” alisema Mhe. Qwaray.

Aliongeza kuwa, Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi ili kuhakikisha watanzania hasa kaya maskini zinanufaika kupitia TASAF. Hivyo, amewaomba wananchi wa wanaozunguka miradi hiyo kuwa walinzi ili miradi hiyo iweze kunufaisha vizazi vya sasa na vile  vijavyo.

Aidha, Mhe. Qwaray amesema kuwa miradi ya TASAF ni chachu ya maendeleo kwa kuwa watanzania hasa wanaotoka katika kaya maskini wanajikwamua kutoka katika wimbi la umaskini kwa kupata elimu kutokana na ujenzi wa shule na wananufaika na mfereji wa umwagiliaji kwa kufanya kilimo cha mahindi, nyanya, vitunguu na maji kwa ajili ya mifugo.


Naibu Waziri,Ofisi yas Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, mhe. Regina Qwaray (wa pili kulia) akiwa anapewa maelezo ya maendeleo ya mradi wa ujenzi wa shule ya Oldnuwas na Mkurugenzi wa Hamashauri ya wilaya ya Arusha Bw. Seleman Msumi wakati wa ziara yake ya kikazi iliyofanyika mkoani Arusha leo tarehe 9 January, 2026.


 Mratibu wa TASAF Mkoa akitoa neno la Utangulizi kwa Naibu Waziri,Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kabla  kamati ya TASAF mkoa wa Arusha kusoma Taarifa ya utekelezaji wa miradi leo tarehe 9 Januari, 2026

Timu ya wataalam kutoka ofisi ya Mkuu wa mkoa na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru  wakioongozana na Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, mhe. Regina Qwaray kukagua mradi wa TASAF wa shule ya sekondari Oldonuwas iliyopo kijiji cha Oldonuwas jijini Arusha leo Januari 9, 2026.

 

Sehemu ya wananchi wa kijiji cha Oldonuwas wanaonufaika na mradi wa TASAF wa ujenzi wa shule ya sekondari Oldnuwas wakimsikiliza Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray alipokuwa akizungumza nao baada ya kuwasili kijijini hapo kuona maendeleo ya miradi hiyo leo tarehe 9 Januari, 2026 jijini Arusha

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF ambaye ni Afisa Miradi TASAF Bw.Agustino Ngude akitoa neno la Utangulizi kwa Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, mhe. Regina Qwaray kabla ya kupokea Taarifa ya maendeleo ya wa Mradi wa TASAF wa shule ya sekondari Oldonuwas iliyopo kijiji cha Oldonuwas na ujenzi wa mfereji wa umwagiliaji uliopo Meru kijiji cha Ngabobo wilaya ya Meru jijini Arusha

Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, mhe. Regina Qwaray (aliyevaa suti nyeusi) akiwa katika picha ya pamoja na sehemu ya viongozi wa Mkoa wa Arusha kabla ya kutembelea Mradi wa TASAF wa ujenzi wa shule ya sekondari Oldonuwas iliyopo kijiji cha Oldonuwas na ujenzi wa mfereji wa umwagiliaji uliopo Meru kijiji cha Ngabobo wilaya ya Meru.

sehemu ya wananchi ambao ni wanufaika wa mradi wa TASAF wa ujenzi wa mfereji wa umwagiliaji uliopo Meru kijiji cha Ngabobo wilaya ya Meru jijini Arusha wakimsikiliza Naibu Waziri,Ofisi yas Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, mhe. Regina Qwaraywakati alipofika kukaguia mradi huo tarehe 9 Januari,2026

Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, mhe. Regina Qwaray pamoja na timu waliyoongozana nayo wakikagua maendeleo ya ujenzi wa mfereji wa umwagiliaji uliopo Meru kijiji cha Ngabobo wilaya ya Meru jijini Arusha ambao umekuwa ukiwanufaisha wananchi katika undeshaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo kijijini hapo.






No comments:

Post a Comment