Friday, January 23, 2026

WATUMISHI WA UMMA WAANDALIWE KUWA VIONGOZI-MHE. KIKWETE

 Na. Veronica Mwafisi na Antonia Mbwambo-Dar es salaam

Tarehe 23 Januari, 2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema ni muhimu kwa Taasisi ya UONGOZI kuendelea kuwaandalia program za Uongozi Watumishi wa Umma wenye mwelekeo wa Uongozi “leadership potential” ili kuwa na Viongozi watakaokuwa na uzalendo na weledi katika taifa.

Waziri Kikwete ameyasema hayo leo tarehe 23 Januari, 2026 jijini Dar es salaam alipotembelea taasisi hiyo kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji.

Mhe. Kikwete amesema, uamuzi wa kushirikisha wafanyakazi wa Taasisi za Umma, binafsi na za kiraia  katika program hizo unatoa fursa kwa washiriki hao kubadilishana uzoefu na kuboresha utendaji.

Amesema ni wakati sahihi wa kuweka mikakati ya ujenzi wa Kituo cha Uongozi (Leadership Center) ambacho  zaidi kitawajengaViongozi katika Utumishi wa Umma.

Akihitimisha hotuba yake Mhe. Kikwete ameipongeza Menejimenti na Watumishi wote wa Taasisi ya Uongozi kwa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Kwa upande wake, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumteua katika nafasi ya Naibu Waziri wa Ofisi hiyo ambapo ameomba ushirikiano Ili kwa pamoja waweze kumsaidia Rais katika kutekeleza majukumu ya Utumishi na Utawala Bora.

Awali, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Taasisi yake, aliwashukuru Viongozi hao kwa kuwatembelea na kuhimiza uwajibikaji na kuahidi kuyafanya kazi maelekezo watakayopewa.



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na watumishi wa Taasisi ya UONGOZI (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa katika ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji katika taasisi hiyo leo jijini Dar es Salaam




Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo baada ya kuwasili Taasisi ya UONGOZI jijini Dar es Salaam katika ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza Uwajibikaji kwa watumishi wa Ofisi hiyo leo jijini Dar es Salaam. Katikati ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) akiteta jambo na Katibu Mkuu-IKULU, Bw. Mululi Mahendeka (kushoto) baada ya Waziri huyo kuzungumza na watumishi wa Taasisi ya UONGOZI wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji. Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo akimuonesha kitabu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) wakati Waziri huyo alipokuwa akipitishwa kwenye baadhi ya Idara za Taasisi hiyo wakati Waziri huyo alipofanya ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji. Kushoto ni Naibu Waziri wake Mhe, Regina Qwaray.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi wa Taasisi ya UONGOZI jijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji. Wa pili kulia waliokaa ni Naibu Waziri wake, Mhe. Regina Qwaray na wa pili kushoto waliokaa ni Katibu Mkuu-IKULU Bw. Mululi Mahendeka.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa taasisi yake kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo katika taasisi hiyo jijini Dar es Salaam iliyolenga kuhimiza uwajibikaji.

Sehemu ya Watumishi wa Taasisi ya UONGOZI jijini Dar es Salaam wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji.

Katibu Mkuu-IKULU, Bw. Mululi Mahendeka akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mh. Regina Qwaray ili amkaribishe Waziri wa Ofisi hiyo Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa kwanza kulia) kwa ajili ya kuzungumza na Watumishi wa Taasisi ya UONGOZI wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji.

Sehemu ya Watumishi wa Taasisi ya UONGOZI wakifuatilia wasilisho la taarifa ya utekelezaji wa taasisi hiyo iliyowasilishwa na Afisa Mtendaji Mkuu, Bw. Kadari Singo (hayupo pichani) wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete iliyolenga kuhimiza uwajibikaji jijini Dar es Salaam.




No comments:

Post a Comment