Thursday, August 27, 2015

WATUMISHI WA OFISI YA RAIS-UTUMISHI WAPATA MAFUNZO KUHUSU VVU NA UKIMWI NA NAMNA YA KUISHI KWA MTINDO BORA WA MAISHA

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. HAB Mkwizu (wa kwanza kutoka kulia) na baadhi ya watumishi wa Ofisi hiyo wakifuatilia mada kuhusu VVU na UKIMWI na namna ya kuishi kwa mtindo bora wa maisha katika mafunzo yaliyofanyika Ukumbi wa Utumishi mapema jana.

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. HAB Mkwizu (kushoto) akiwasisitiza watumishi wa Ofisi hiyo kuzingatia mafunzo waliyoyapata kuhusu VVU na UKIMWI na namna ya kuishi kwa mtindo bora wa maisha katika mafunzo yaliyofanyika Ukumbi wa Utumishi mapema jana. Kushoto kwake ni Dkt. Hafidh Ameir kutoka TACAIDS.

Mmoja wa watumishi wa Ofisi ya Rais-Utumishi (kulia) akipima VVU na UKIMWI baada ya kupata mafunzo kuhusu VVU na UKIMWI na namna ya kuishi kwa mtindo bora wa maisha katika mafunzo yaliyofanyika Ukumbi wa Utumishi mapema jana.

Wednesday, August 19, 2015

Mkutano wa mwaka wa Serikali Mtandao wafunguliwa rasmi jijini Arusha

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Y. Sefue akifungua mkutano wa kwanza wa Serikali Mtandao kwa Watendaji Wakuu na Viongozi wa Serikali, Arusha.

Sehemu ya washiriki wa mkutano wakimsikiliza mgeni rasmi Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Y. Sefue (hayupo pichani).

Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. HAB Mkwizu akimkaribisha mgeni rasmi kufungua mkutano.

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Y. Sefue akikaribishwa na Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. HAB Mkwizu katika mkutano kuhusu Serikali Mtandao katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC).

Thursday, August 13, 2015

Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Rais-Utumishi lafanyika

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. HAB Mkwizu akifungua mkutano wa  baraza la wafanyakazi la Ofisi ya Rais-Utumishi lililofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Utalii Dar es Salaam.
Baadhi ya Wajumbe wa  Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Rais-Utumishi wakiwa katika mkutano wa baraza hilo uliofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Utalii Dar es Salaam.