Thursday, March 31, 2022

MALALAMIKO YA UKIUKWAJI WA MAADILI KWA VIONGOZI YASHUGHULIKIWE KIKAMILIFU KWA MANUFAA YA TAIFA-Mhe. Jenista

 Na. James K. Mwanamyoto-Dodoma

Tarehe 31 Machi, 2022

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama ameielekeza Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kushughulikia malalamiko na tuhuma zinazowasilishwa na wananchi kuhusu Viongozi wa Umma wanaokiuka maadili ili kuwa na viongozi waadilifu wanaotekeleza majukumu yao kwa maendeleo ya taifa.

Mhe. Jenista ameyasema hayo leo alipokutana na Menejimenti ya Sekretarieti hiyo kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji na kukagua ujenzi wa Ofisi za makao makuu ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma jijini Dodoma.

Mhe. Jenista amesema, kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu mwenendo wa baadhi ya Viongozi wa Umma kwenye eneo la uadilifu, hivyo Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi ina jukumu kubwa la kuyapokea malalamiko hayo na kuyafanyia kazi ili viongozi wawe na maadili na miiko ya uongozi unaotakiwa.

“Mnapokea tuhuma zinazohusu ukiukwaji wa maadili ya viongozi, hivyo mna jukumu la kufanya uchunguzi ili kuthibitisha ukweli wa tuhuma hizo na kuzifanyia kazi kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na.13 ya Mwaka 1995,” Mhe. Jenista amesisitiza.

Aidha, Mhe. Jenista ameitaka Sekretarieti hiyo kutoa elimu ya uzingatiaji wa maadili kwa Viongozi wa Umma ili wasikiuke maadili na miiko ya uongozi kwa kutokuwa na uelewa.

“Katika kipindi hiki tujikite zaidi kutoa elimu ya uzingatiaji wa maadili ili viongozi wetu wa umma waelewe umuhimu wa kuzingatia maadili katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku, hii inatokana na baadhi ya viongozi kukiuka maadili kwa kutokuelewa na hatimaye kujihusisha na vitendo vya ukiukaji wa maadili.” Mhe. Jenista amehimiza.

Amesema azma ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan inamtaka kila Mtanzania ajifunze kutii sheria bila shuruti na kama ni kiongozi basi atii Sheria ya Maadili ya Viongozi bila kushurutishwa, hivyo suala ya utoaji wa elimu ya uzingatiaji wa maadili haliepukiki ili kuwa na uongozi unaozingatia utawala bora.

Kwa upande wake Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili wa Viongozi wa Umma, Mhe. Jaji Sivangilwa Sikalalilwa Mwangesi amezitaja kazi za msingi za Sekretarieti hiyo kuwa ni pamoja na kupokea matamko yanayotakiwa kutolewa na Viongozi wa Umma kwa mujibu wa Katiba na Sheria, kupokea malalamiko na tuhuma za ukiukwaji wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, kuanzisha na kufanya uchunguzi dhidi ya tuhuma za ukiukwaji wa maadili na kufanya uhakiki wa Matamko na Rasilimali na Madeni yanayotolewa na Viongozi wa Umma kwa mujibu wa Sheria.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na Menejimenti ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma alipokutana na Menejimenti hiyo kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji na kukagua ujenzi wa Ofisi za makao makuu ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma jijini Dodoma. Kulia kwake ni Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi na kushoto kwake ni Mkurugenzi Idara ya Ujenzi Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mhandisi Loishorwa Likimaitare.


Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi, Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama kuzungumza na Menejimenti hiyo kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji na kukagua ujenzi wa Ofisi za makao makuu ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma jijini Dodoma. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akiwa katika kikao kazi na Menejimenti ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma alipokutana na Menejimenti hiyo kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji na kukagua ujenzi wa Ofisi za makao makuu ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma jijini Dodoma. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akiwasili eneo la Ujenzi wa Ofisi ya makao makuu ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma unaoendelea jijini Dodoma wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kukagua ujenzi huo. Kushoto kwake ni Kamishna wa Sekretarieti wa Maadili ya Viongozi, Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza Meneja wa Mkoa Dodoma, Mbunifu Majengo (TBA) Bw. Victor Balthazar alipokuwa akimuonesha mchoro wa jengo la ofisi ya Sekretarieti ya Maadili Makao Makuu wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua Mradi wa Ujenzi wa Jengo hilo jijini Dodoma.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi, Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi alipokuwa akimuonesha miundombinu wakati wa ziara yake ya kikazi yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji na kukagua ujenzi wa ofisi hizo.



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akitoka kukagua jengo la la ofisi za makao makuu ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma linaloendelea kujengwa jijini Dodoma na Mkandarasi ambaye ni Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) wakati wa ziara yake ya kikazi yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji na kukagua ujenzi wa ofisi hizo.


Muonekano wa jengo la ofisi za makao makuu ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma linaloendelea kujengwa jijini Dodoma na Mkandarasi ambaye ni Wakala wa Majengo Tanzania (TBA)


No comments:

Post a Comment