Saturday, September 5, 2026

UTUMISHI SC YASHINDA 4-0 DHIDI YA MKONZE VETERANS

Na Eric Amani, Dodoma

Timu ya Utumishi Sports Club (UTUMISHI SC) imeendelea kuonyesha kiwango kizuri baada ya kupata ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Mkonze Veterans katika mchezo wa kirafiki wa soka uliochezwa leo Septemba 05, 2026 katika uwanja wa John Merlin Jijini Dodoma.

UTUMISHI SC ilitawala mchezo kwa kiasi kikubwa, ikionyesha umakini, nidhamu na ushirikiano mzuri wa kikosi katika maeneo yote ya uwanja. Ushindi huo unaongeza morali kwa timu huku ukiendelea kujenga maandalizi na ushindani kuelekea mashindano ya SHIMIWI 2026 Mkoani Kilimanjaro.

Uongozi na wachezaji wa UTUMISHI SC wameendelea kuhimizana kuzingatia maadili ya Utumishi wa Umma ndani na nje ya Viwanja kuwa nidhamu, upendo, mshikamano na kujituma katika kila mchezo, kwa lengo la kuiweka timu katika kiwango bora zaidi ili kuelekea kutetea ubingwa walioutwaa katika mashindano ya SHIMIWI kwa mwaka 2025 ambayo yalifanyika Jijini Mwanza

 










No comments:

Post a Comment