Na Eric Amani, Dodoma
Timu
ya Mpira wa Pete ya Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora imeendelea kuonyesha kiwango kizuri na kuimarika kuelekea mashindano ya
SHIMIWI 2026, baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 68–42 dhidi ya timu ya Dom
Kings katika mchezo wa mazoezi uliofanyika Agosti 2, 2026 jijini Dodoma.
Katika
mchezo huo, Utumishi ilionesha uwezo mzuri wa kiufundi, kasi, umakini na
ushirikiano wa wachezaji, hali iliyoiwezesha kutawala mchezo na kupata ushindi
wa mabao 68, huku Dom Kings ikiambulia mabao 42.
Mchezo
huo ni sehemu ya maandalizi ya timu hiyo kuelekea Mashindano ya Michezo ya
Wizara, Idara za Serikali na Mikoa (SHIMIWI) 2026, yanayotarajiwa kufanyika
mkoani Kilimanjaro. Maandalizi ya mashindano hayo yameendelea kushika kasi,
huku taasisi mbalimbali za Serikali zikiendelea kuimarisha timu zao kupitia
mazoezi na michezo ya kirafiki.
Ushindi
dhidi ya Dom Kings unaongeza morali kwa kikosi cha Utumishi na kutoa fursa kwa
benchi la ufundi kuendelea kutathmini uwezo wa wachezaji, kubaini maeneo
yanayohitaji maboresho na kujenga muunganiko bora wa timu kabla ya kuingia
kwenye ushindani wa SHIMIWI 2026.








No comments:
Post a Comment