Naibu Waziri Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Regina Qwaray amesema Miundo ya Maendeleo ya Utumishi huandaliwa kwa kuzingatia mahitaji ya kiutumishi, majukumu ya kada, pamoja na viwango vya elimu na sifa za kitaaluma vinavyotolewa na taasisi za elimu zilizoidhinishwa.
Mhe. Qwaray amebainisha hayo leo Septemba Mosi 2026 Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Mbulu Vijijini Mhe. Dkt. Emmanuel Qambaji Nuwas, lililouliza Serikali ina mpango gani wa kutambua kwenye Muundo wa Utumishi wa Umma Wataalam wa Kada ya Afya wenye Elimu ngazi ya ubobezi.
Akijibu swali hilo, amesema Ofisi ya Rais Utumishi, ilipokea mapendekezo ya Muundo wa Utumishi kwa Wataalamu wa Kada ya Afya wenye Elimu ngazi ya ubobezi na taratibu kwa ajili ya uchambuzi wa kina na hatua za kupata idhini zinaendelea.

No comments:
Post a Comment