Na. Veronica Mwafisi-Dar es Salaam
Mradi wa Tanzania ya Kidijitali (DTP) umeleta mapinduzi makubwa ya mawasiliano ya kimtandao yaliyorahisisha utoaji wa huduma za serikali kwa wananchi.
Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Priscus Kiwango ameyasema hayo alipokuwa akimwakilisha Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wakati wa kikao kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Bw. Kiwango amesema kupitia DTP, miradi mingi imetekelezwa na kuleta mafanikio makubwa ikiwemo minara ya simu iliyopelekwa kwenye maeneo mengi ya vijijini ambayo mawasiliano yalikuwa hayapatikani na kwa sasa yanapatikana kwa ubora wa 3G na 4G.
Vilevile amesema, mradi huo umeweka Mawasiliano ya kimtandao kwenye Taasisi za Serikali ikiwemo kwenye Mamlaka ya Serikali za Mitaa kwa ajili ya kutumia mifumo mbalimbali ya serikali kidijitali.
Bw. Kiwango ameongeza kuwa, mradi huo umeleta mafanikio makubwa ya kuunganishwa kwa mifumo mingi ya Serikali ambayo ilikuwa ni maelekezo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kubadilishana taarifa kwa taasisi za umma.
Aidha Bw. Kiwango amesema, kupitia mradi huo, Mfumo unaotumika na Taasisi za Umma Kupima Utendaji Kazi wa Watumishi wa Umma (PEPMIS) umetekelezeka.
Bw. Kiwango ametaja mafanikio mengine ya mradi huo wa DTP kuwa ni kupatikana
kwa Mfumo wa Daftari la Huduma za Serikali (GSD) unaowawezesha
wananchi, wafanyabiashara na wageni kupata taarifa mbalimbali za huduma za
serikali katika Wizara, Idara, Wakala, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za
Serikali za Mitaa hivyo, kurahisisha utoaji wa huduma kwa umma kwa njia ya
kidijiti.
Kwa
upande wake Mratibu wa Mradi huo ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano kutoka
Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Bw. Bakari Mwamgugu, amesema lengo
kuu la mradi huo ni kupeleka mawasiliano sehemu ambazo hazikuwa na mawasiliano
na kuboresha huduma bora kwa mwananchi kidijitali.
Ameongeza kuwa,
Minara 304 imeboreshwa kutokana na mabadiliko ya teknolojia kutoka kwenye 2G
Kwenda kuwa na 3G na 4G.
Mradi wa Tanzania ya Kidijitali ulianza mwaka 2021 na unatarajia kukamilika mwaka huu 2026.
Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Priscus Kiwango akizungumza wakati wa kikao kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wa kikao kilicholenga
kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wakimsikiliza Mwakilishi
wa Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni
Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Bw. Priscus Kiwango (hayupo pichani) alipokuwa
akizungumza nao wakati wa kikao hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi kutoka Benki ya Dunia, Bw. Paul
Seadin akizungumza wakati wa kikao kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi
wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wa kikao kilicholenga
kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wakimsikiliza Mwakilishi
wa Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni
Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini, Bw. Priscus Kiwango (hayupo pichani) alipokuwa
akizungumza nao wakati wa kikao hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wa kikao kilicholenga
kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wakijadili jambo wakati
wa kikao hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Msaidizi wa Anuai za Jamii, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bi.
Mwanaamani Mtoo (kushoto) akifuatilia jambo wakati wa kikao cha kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya
Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Meneja wa Kituo cha
Utafiti, Ubunifu na Uendelezaji wa Serikali Mtandao, Dkt. Jaha Mvulla.
Baadhi ya washiriki wa kikao kilicholenga
kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali wakifuatilia jambo wakati
wa kikao hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Wizara ya
Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini,
Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Priscus Kiwango (waliokaa katikati)
akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi kutoka Ofisi ya
Rais-UTUMISHI na Utawala Bora (waliosimama) baada ya kikao kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa
Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Wizara ya
Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini,
Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Priscus Kiwango (waliokaa katikati)
akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki (waliosimama) wa kikao
kilicholenga kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali
kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Wakurugenzi
kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakifuatilia jambo wakati wa kikao
cha kujadili utekelezaji wa
Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini Dar es Salaam
Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Wizara ya
Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini,
Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Bw. Priscus Kiwango (waliokaa katikati)
akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa kikao kilicholenga
kujadili utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kilichofanyika jijini
Dar es Salaam.











No comments:
Post a Comment