Friday, November 8, 2024

KATIBU MKUU, UTUMISHI AFANYA MAZUNGUMZO NA MWAKILISHI MKAZI WA JICA

Na. Lusungu Helela

Katibu Mkuu, UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi amekutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan ( JICA), Bw. Ara Hitoshi kuhusu kuimarisha ushirikiano baina ya JICA na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora. 

 

Kikao hicho kimefanyika  leo Ijumaa Novemba 8, 2024  katika Ofisi zilizopo Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

 

Miongoni mwa masuala waliyojadili ni pamoja na kutoa fursa za mafunzo kwa watumishi pamoja na maombi  ya vibali vya ajira  kwa raia wa kutoka Japan wanaokuja kufanya kazi nchini katika miradi ya Serikali katika Utumishi wa Umma  ambapo fursa  hiyo huwasaidia Wazawa kubaki na ujuzi  unaoweza kutumika hata baada ya miradi ya maendeleo kukamilika 

 

Aidha, viongozi hao wamepongeza juhudi za ushirikiano wa nchi hizo mbili unaofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu wa Japan, Mhe.  Shigeru Ishiba.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akisalimiana  na  Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan ( JICA), Bw. Ara Hitoshi mara baada ya mazungumzo ya kuimarisha ushirikiano baina ya JICA na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora. 



Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akisalimiana  na  Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan ( JICA), Bw. Ara Hitoshi mara baada ya mazungumzo ya kuimarisha ushirikiano baina ya JICA na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora. 

 

 

 


 Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akiwa kwenye picha ya pamoja na  Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan ( JICA), Bw. Ara Hitoshi mara baada ya mazungumzo ya  kuimarisha ushirikiano baina ya JICA na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora. 

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, UTUMISHI Bw. Juma Mkomi akizungumza na   Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan ( JICA), Bw. Ara Hitoshi  kuhusu  kuimarisha ushirikiano baina ya JICA na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora. 



 

 

 

No comments:

Post a Comment