Saturday, August 31, 2024

RAIS MHE. DKT. SAMIA ACHANGIA MILIONI 50 KANISA LA MENNONITE

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene ametoa rai kwa waamini wa Kanisa la Mennonite Tanzania ya kuendelea kulinda umoja, amani, uhuru, mshikamano na ustawi wa watanzania kwa maendeleo ya Taifa la Tanzania.

Mhe. Simbachawene ametoa rai hiyo wakati alipomwakilisha Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye harambee ya kuchangia ujenzi wa Kituo cha Elimu Mkamba cha Kanisa la Mennonite Tanzania, iliyofanyika katika kanisa la Mennonite Dayosisi ya Mashariki, Jijini Dar es salaam.

“Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatambua umuhimu wa elimu kwa watanzania, hivyo anachangia milioni 50 ikiwa ni jitihada za kuhakikisha kituo kinajengwa haraka ili watoto wetu waweze kupata elimu ya dunia na ya kiroho, na mimi nilitamani kuchangia milioni 2.5 lakini kwa mahubiri ya Baba Askofu Gabriel Magwega, Askofu wa Kanisa la Mennonite Tanzania, Dayosisi ya Mashariki yamenigusa kutoa zaidi, sasa nitatoa sadaka milioni 5 ili kujenga kituo hiki cha kuandaa rasilimaliwatu” Mhe. Simbachawene.

Mhe. Simbachawene aliongeza kuwa rasilimawatu ikiandaliwa vizuri na kupata elimu bora, nchi itapata viongozi wenye hofu ya Mungu na watakuwa na uwezo wa kuongoza nchi kwa kuzingatia maadili mema, hivyo kuleta maendeleo ya haraka kwa taifa na wananchi kwa jumla.

Aidha, aliongeza kuwa Serikali inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan iko tayari kushirikiana na Kanisa katika kuondoa maadui watatu yaani ujinga, maradhi na umaskini. Kwa hiyo ujenzi wa Kituo hicho cha Elimu cha Mkamba ni msingi wa kupambana na maadui hao.

Awali, Baba Askofu Nelson Kisare, Askofu Mkuu wa Kanisa la Mennonite Tanzania alisema kuwa Serikali imeridhia Malengo 17 ya Umoja wa Mataifa kuhusu Elimu (SDG) ambapo katika malengo hayo lengo namba 4 linahusu elimu hususani Elimu Jumuishi, kwa mantiki hiyo Kanisa la Mennonite Tanzania linaunga mkono Serikali katika jitihada za kutekeleza malengo hayo kwa kuandaa mazingira bora ya kutoa elimu kwa watanzania.

Vilevile, aliongeza kuwa Kanisa litaendelea kushirikiana na Serikali katika utoaji wa elimu bora kwa wasichana na wavulana ili kuunga mkono jitihada za kuondoa ujinga, maradhi na umaskini. Pia, kanisa litahakikisha katika shule hiyo linatoa vijana wa kitanzania waliolelewa katika misingi ya neno la Mungu, wenye kumcha Mungu na wenye hofu ya  Mungu ndani ya mioyo yao.

“Waziri, Mhe. Simbachawene tunaomba utufikishie salaam zetu za shukurani kwa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kupokea barua yetu, kukubali mwaliko na kukutuma wewe kuja kumuwakilisha, jambo hili ni kubwa sana na sisi tutaendelea kumuombea kwa Mungu ili aendelee kuongoza nchi hii kwa amani, furaha na upendo daima” alisema Baba Askofu Kisare.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene akitoa hotuba kwa niaba ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye harambee ya kuchangia ujenzi wa Kituo cha Elimu Mkamba cha Kanisa la Mennonite Tanzania, Jijini Dar es salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene akiteta jambo na Baba Askofu Nelson Kisare, Askofu Mkuu wa Kanisa la Mennonite Tanzania wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa Kituo cha Elimu Mkamba cha Kanisa la Mennonite Tanzania, Jijini Dar es salaam.

Wachungaji na Waamini wa Kanisa la Mennonite wakifuatilia hatuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene akimwakilisha Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye harambee ya kuchangia ujenzi wa Kituo cha Elimu Mkamba cha Kanisa la Mennonite Tanzania, Jijini Dar es salaam.





Waumini wa Kanisa la Mennonite Tanzania, Dayosisi ya Mashariki wakifuatilia hatuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene akimwakilisha Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye harambee ya kuchangia ujenzi wa Kituo cha Elimu Mkamba cha Kanisa la Mennonite Tanzania, Jijini Dar es salaam.






Friday, August 30, 2024

KAMATI YA BUNGE YATOA MAELEKEZO KWA TAKUKURU NA SEKRETARIETI YA AJIRA

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Florent Kyombo na Wajumbe wa Kamati hiyo wamezielekeza taasisi za TAKUKURU na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kufanya kazi kwa ufanisi ili kujenga imani kwa wananchi juu ya huduma wanazozitoa.

Mhe. Kyombo amesema hayo leo jijini Dodoma wakati wa semina kwa wajumbe wa kamati hiyo iliyotolewa na TAKUKURU kwa kushirikiana na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma. Semina hiyo ililenga kuwajengea Wajumbe uelewa mpana ili waweze kufanya uamuzi wa masuala mabalimbali kwa maslahi mapana ya nchi.

Mhe. Kyombo ameielekeza Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kutoa elimu kwa wananchi kuhusu namna mchakato wa ajira unavyofanyika ili kuondoa dhana ya wananchi kuwa nafasi za kazi ni kwa ajili ya kundi fulani.

"Wananchi wote wanahaki ya kuomba nafasi ya kulitumikia taifa lao kwa kuomba Ajira Serikalini kupitia Sekretarieti hii, hivyo waelimisheni kuwa mchakato ni wazi kwa yeyote mwenye sifa na akishinda anapata nafasi" alisisitiza Mhe. Kyombo.

Kadhalika Mhe. Kyombo ameipongeza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa kuwa na watumishi waadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao.

Mhe. Kyombo ametoa wito kwa taasisi hiyo kujikita zaidi katika kuongeza rasilimali fedha na vitendea kazi ili kutoa mchango wenye tija katika kufanya kazi na kufikia lengo la kutoa huduma bora kwa wananchi.

Kwa upande wake, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu ameihakikishia Kamati hiyo kuwa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora kupitia taasisi hizo na taasisi nyingine zilizo chini ya ofisi hiyo zitafanya kazi kwa weledi na ufanisi.

Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mjumbe wa Kamati hiyo ambaye ni Mbunge wa Chonga Pemba (ACT), Mhe. Salum Shaafi amezishukuru taasisi hizo kwa kuwapatia mafunzo hayo ambayo yamepanua uelewa wap kuhusu majukumu ya taasisi hizo muhimu kwa taifa.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Florent Kyombo akizungumza wakati akifungua semina iliyotolewa na TAKUKURU na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa Wajumbe wa Kamati hiyo jijini Dodoma.


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakifuatilia mada kutoka kwa Mkurugenzi wa Elimu kwa Umma-TAKUKURU, Bw. Joseph Mwaiswelo (hayupo pichani) wakati wa semina iliyotolewa na Taasisi hiyo.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Florent Kyombo (hayupo pichani)  kuzungumza wakati wa semina iliyotolewa na TAKUKURU na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma jijini Dodoma.


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Kaimu Katibu, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma ambaye ni Mkuu wa Idara ya TEHAMA, Mhandisi Samwel Tanguye (hayupo pichani) wakati wa semina iliyotolewa na TAKUKURU na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma jijini Dodoma.



Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akifuatilia mada kuhusu mwelekeo wa Serikali kwenye vita dhidi ya Rushwa. Kulia ni Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi.


Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila akielezea lengo kuu la semina inayotolewa na taasisi yake kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria iliyofanyika jijini Dodoma.



Kaimu Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma ambaye ni Mkuu wa Idara ya TEHAMA, Mhandisi Samwel Tanguye akifanya wasilisho la mada kuhusu utekelezaji wa kibali cha ajira mpya kwa mwaka wa fedha 2023/2024 kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria.


Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akijibu moja ya hoja iliyowasilishwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakati wa semina iliyotolewa TAKUKURU na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa Kamati hiyo jijini Dodoma. Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bi. Neema Mwakalyelye


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Seif Gulamali akiwasilisha hoja kwa Mkurugenzi wa Elimu kwa Umma-TAKUKURU, Bw. Joseph Mwaiswelo (hayupo pichani) mara baada ya kuwasilisha mada kwenye semina kuhusu mwelekeo wa Serikali kwenye vita dhidi ya Rushwa.

Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cyrus Kapinga (katikati) na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, SACP. Ibrahim Mahumi (wa kwanza kulia) wakifuatilia mada mbalimbali kwenye semina iliyotolewa na TAKUKURU na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma jijini Dodoma. Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bi. Neema Mwakalyelye.

Baadhi ya Watumishi wa TAKUKURU wakiwa katika semina iliyotolewa kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Utawala, Katiba na Sheria kuhusu utekelezaji wa majukumu ya TAKUKURU na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa umma iliyofanyika jijini Dodoma.

























Thursday, August 29, 2024

MHE. SIMBACHAWENE: TUTAZUIA WATUMISHI KUINGIA OFISINI NA SIMU ZA MKONONI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene ametoa rai kwa Waajiri na Viongozi wa Matawi ya TUGHE Tanzania kuhamasisha Watumishi wa Umma katika sehemu zao za kazi kujituma na kutoa huduma bora kwa wananchi.

Mhe. Simbachawene ametoa rai hiyo wakati akifunga semina ya Waajiri na Viongozi wa Matawi ya TUGHE iliyofanyika kuanzia tarehe 26 hadi 29 Agosti, 2024 katika Hoteli ya Lushgarden jijini Arusha.

Katika hotuba yake alisitiza Waajiri na Viongozi hao kutafuta namna bora na kuishauri Serikali ili kuweka utaratibu wa kuzuia watumishi wa umma kuingia kazini na simu zao za mkononi kwa kuwa zimekuwa kikwazo kwa utoaji wa huduma bora kwa umma.

“Nchi nyingine watumishi hawatumii simu wakiwa ofisini, kazi yao ni kutoa huduma kwa umma, lakini sisi tunachati tu badala ya kufanya kazi. Piteni kwenye ofisi mbalimbali za umma muone watumishi walivyobize na matumizi ya simu zao za mkononi tangu wanapoingia kazini, mathalani mtumishi ana magrupu ya ‘WhatsApp’ zaidi ya ishirini na anasoma yote na kujibu, hivyo kutumia muda wa mwajiri kwa manufaa binafsi. Ninawasihi muingilie kati na kuishi kaulimbiu yenu ya Huduma Bora, Maslahi Zaidi”.

Aliongeza kuwa, Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye ndiye Mkuu wa Utumishi wa Umma anafanya jitihada kubwa za kuboresha masilahi ya watumishi ikiwa ni pamoja na kuelekeza kufanya maboresho ya kikokotoo, kupandisha madaraja na mishahara, kulipa malimbikizo na kutoa ajira mpya kwa lengo la kuboresha utumishi wa umma.

Aidha, alibainisha kuwa wajibu wa msingi kwa mtumishi wa umma ni kuwahudumia wananchi wakati wote ili waweze kufanya shughuli zao za kujenga taifa kwa urahisi, lakini watumishi wamekuwa hawawajibiki ipasavyo na hivyo kuathiri mnyororo wa kuwatumikia wananchi.

Awali, Mwenyekiti wa TUGHE Taifa Bw. Joel Kaminyoge amesema wameamua kuwakutanisha waajiri na viongozi wa TUGHE kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya chama na waajiri na zaidi kubainisha changomoto katika utumishi wa umma na kuzitafutia ufumbuzi wa haraka.

Bw. Kaminyoge amempongeza Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwa msikivu wakati wote wanapowasilisha shida zao na kuzitafutia ufumbuzi haraka. Hivyo, yeye na viongozi wenzake waliahidi kuendelea kushirikiana na Serikali katika utatuzi wa changamoto zinazojitokeza katika utumishi wa umma.

Halikadhalika, Katibu wa Mkuu wa TUGHE Taifa Bw. Hery Mkunda aliongeza kwa kumshukuru Mhe. Simbachawene kwa kutenga muda na kuitikia wito wa kuwa mgeni rasmi wakati wa kufunga semina hiyo ambayo wamepata kujifunza masuala mbalimbali yenye manufaa kwa washiriki na taifa kwa jumla.

Bw. Mkunda, amewapongeza waajiri wote walioruhusu watumishi wao kushiriki semina hiyo na amesema hawatajuta kuwaruhusu viongozi hao kwa kuwa wameongezeka thamani kutokana na elimu iliyotolewa katika semina hiyo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene  akitoa hatuba yake wakati wa kufunga Semina ya Waajiri na Viongozi wa Matawi ya TUGHE katika Hoteli ya Lushgarden jijini Arusha.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene  akitoa hatuba yake wakati wa kufunga Semina ya Waajiri na Viongozi wa Matawi ya TUGHE katika Hoteli ya Lushgarden jijini Arusha.


Baadhi ya Washiriki wakifuatilia hatuba ya ufungaji wa Semina ya Waajiri na Viongozi wa Matawi ya TUGHE kutoka kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene (Hayupo pichani) katika Hoteli ya Lushgarden jijini Arusha.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene  akitoa cheti cha ushiriki wa Semina ya Waajiri na Viongozi wa Matawi ya TUGHE kwa Bw. John Mboya katika Hoteli ya Lushgarden jijini Arusha.

Mkurugenzi Msaidizi -Idara ya Usimamizi wa Rasilimawatu Serikalini Bi. Jeanfrida Mshumbusi akishiriki katika Semina ya Waajiri na Viongozi wa Matawi ya TUGHE iliyofanyika katika Hoteli ya Lushgarden jijini Arusha tarehe 26 hadi 29 Agosti, 2024.

Baadhi ya Washiriki wakifuatilia hatuba ya ufungaji wa Semina ya Waajiri na Viongozi wa Matawi ya TUGHE kutoka kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene (Hayupo pichani) katika Hoteli ya Lushgarden jijini Arusha.

















Wednesday, August 28, 2024

VIONGOZI WASHIRIKI UFUNGUZI WA KIKAO CHA WENYEVITI WA BODI AICC

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simabachawene (Wa kwanza kushoto, mstari wa Pili) na viongozi wengine wakifuatilia Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa kufungua Kikao Kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Wakuu wa Taasisi za Umma kinachofanyika katika ukumbi wa AICC, Jijini Arusha tarehe 28 Agosti, 2024.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara mbalimbali baada ya kufungua Kikao Kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Wakuu wa Taasisi za Umma kinachofanyika katika ukumbi wa AICC Jijini Arusha tarehe 28 Agosti, 2024


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Juma Mkomi akiwa katika Kikao Kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Wakuu wa Taasisi za Umma Kinachofanyika katika ukumbi wa AICC Jijini Arusha. Kikao hicho kimefunguliwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tarehe 28 Agosti, 2024.



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simabachawene akiteta jambo na Waziri wa Sanaa, Utamaduni na Michezo  Mhe. Damas Ndumbaro wakati wakisubiri ufunguzi rasmi wa Kikao Kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Wakuu wa Taasisi za Umma uliofaywa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan uliofanyika katika ukumbi wa AICC Jijini Arusha tarehe 28 Agosti, 2024.











SERIKALI INAFANYA KAZI KUPITIA NYARAKA - Mhe. Sangu

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu amesema kuwa msingi mkuu wa ufanyaji kazi wa Serikali ni kwa kupitia nyaraka ambazo zinaisaidia Serikali kutimiza uwajibikaji katika kutekeleza majukumu yake kupitia miongozo ya nyaraka hizo.  

Naibu Waziri Sangu, ameyazungumza hayo leo wakati wa ziara yake ya kikazi katika ofisi ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa iliyolenga kuhimiza uwajibikaji.

Naibu Waziri Sangu amesema kuwa utunzaji wa nyaraka kupitia Idara hiyo ni jukumu adhimu linalohitaji viwango vikubwa vya usimamizi ili kuleta haki na uwazi katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya Serikali kwa kutumia nyaraka hizo.

Aidha Mhe. Sangu ameipongeza Idara hiyo kwa namna wanavyofanya kazi kubwa ya kuwaenzi waasisi wa Taifa la Tanzania kwa kukusanya na kutunza kumbukumbu zao zitakazosaidia vizazi vijavyo kufahamu historia ya nchi kupitia waasisi hao.

Awali, Mkurugenzi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa vibali vya ajira na kuwezesha idadi ya watumishi kuongezeka kila mwaka kwa lengo la kuongeza ufanisi.

Naye, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bi. Editha Beda, wakati akitoa neno la shukrani amesema menejimenti imepokea maelekezo yote na kuahidi kuyafanyia kazi kwa ukamilifu ili kuongeza ufanisi katika utendajikazi kwa ustawi wa taifa.

 

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akizungumza na viongozi na watumishi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa (hawapo pichani) wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji jijini Dodoma.

Baadhi ya watumishi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi katika ofsi hiyo jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi akielezea utekelezaji wa majukumu ya ofisi hiyo kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (hayupo pichani) wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji.

Baadhi ya watumishi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara yake ya kikazi katika ofsi hiyo jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi (kulia) akimuonesha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu moja ya nyaraka zinazohifadhiwa katika ofisi hiyo wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji.


Afisa Kumbukumbu, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bi. Maryam Ayoub (wa kwanza kulia) akifafanua jambo kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu wakati Naibu Waziri huyo alipofanya ziara ya kikazi katika ofisi hiyo.


Mkurugenzi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi (kulia) akisalimiana na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu mara baada ya kuwasili katika ofisi hiyo alipofanya ziara ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (aliyevaa tai nyekundu) akipata maelezo kuhusu namna ya kudurufu nyaraka mbalimbali kidijitali wakati wa ziara yake ya kikazi katika ofisi hiyo.


Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu, Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bi. Editha Beda akitoa neno la shukrani kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu mara baada ya kuhitimisha ziara ya kikazi katika ofisi hiyo.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (aliyevaa tai nyekundu) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na watendaji wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa mara baada ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi.



NAIBU WAZIRI SANGU AJIBU MASWALI BUNGENI

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akijibu swali Bungeni wakati wa Mkutano wa 16 wa Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.











Friday, August 23, 2024

MHE. SANGU ATOA RAI KWA VIONGOZI WA UMMA

 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Sangu ametoa rai kwa Viongozi wa Umma kuwa waadilifu kwa kuwa wana dhamana ya kusimamia taasisi na kufanya maamuzi katika Utumishi wa Umma.

Mhe. Sangu ametoa rai hiyo leo Agosti 23, 2024 wakati alipofanya ziara katika ofisi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma iliyopo katika jengo la Maadili (Maadili House) Jijini Dodoma kwa lengo la kujifunza majukumu yanayotekelezwa na taasisi hiyo.

“Hakikisheni mnatumia Sheria, Miongozo na Kanuni katika kusimamia maadili ya Viongozi katika Utumishi wa Umma, maadili ndio kila kitu, iwapo hatutaweka msingi wa maadili vizuri utoaji wa huduma Serikalini hautokuwa na tija na malalamiko ya wananchi hayawezi kukoma” amesisitiza Mhe. Sangu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anataka kuona wananchi wanapata huduma vizuri lakini baadhi ya viongozi wa umma wanashindwa kuzingatia maadili katika utoaji wa huduma, hivyo kuathiri nia njema ya Rais.

Aidha amebainisha kuwa, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ni taasisi muhimu sana kwa kuwa chimbuko lake ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977. Hivyo, wanatakiwa kufanya kazi kwa kiwango cha hali ya juu wakizingatia kwamba ni taasisi tegemewa kwa ustawi wa Taifa.

Aidha, amesema kuwa, Viongozi wa Umma wasipozingatia utalaam, uaminifu na kutimiza wajibu wao ipasavyo matokeo yake ni kuvunja Sheria, kuwa na mwenendo usioridhisha na kufanya matukio yenye athari na hasara kwa wananchi na taifa kwa jumla.

Awali, Kaimu Kamishna wa Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Waziri  Kipacha amebainisha kuwa moja ya changamoto kubwa katika usimamizi ni kwa baadhi ya viongozi wa umma ambao wamebainika kujaza taarifa zisizo sahihi kwenye matamko ya rasilimali na madeni, hivyo wamebaini mbinu za kisasa katika kufanya uchunguzi wa masuala ya  kimaadili.

Aidha, amesema kuanzia Oktoba 2024, Viongozi wote watatakiwa  kutumia mfumo wa Online Declaration System (ODS) unaopatikana kupitia tovuti ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa ajili ya kujaza taarifa za Matamko ya Rasilimali na Madeni na kuziwasilisha kwa njia mtandao.

“Sisi kama Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Tutakupa ushirikiano wa kutosha katika kutekeleza majukumu uliyopewa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan” amesema Bw. Kipacha.

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ina Ofisi  Dodoma, Morogoro, Dar es Salaam, Arusha, Mwanza, Tabora, Mtwara na Mbeya ambazo zinaendelea na majukumu yake ikiwemo kuchunguza mwenendo na tabia za viongozi wa utumishi wa umma.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu akizungumza na viongozi na watumishi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma (hawapo pichani) wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji jijini Dodoma.


Baadhi ya watumishi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu alipokuwa akizungumza wakati wa ziara yake ya kikazi katika ofsi hiyo jijini Dodoma.



Kaimu Kamishna wa Maadili ya Viongozi wa Umma, Bw. Waziri Kipacha (Aliyesimama) akielezea utekelezaji wa majukumu ya ofisi hiyo kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (hayupo pichani) wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji.


Mkurugenzi Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bi. Teddy Njau akitoa utambulisho wa viongozi na watumishi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kabla ya kuanza kwa kikao cha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu.

Watumishi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu wakati akizungumza nao alipotembelea ofisi hiyo kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji.


Mkaguzi Mkuu wa Ndani, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Bi. Margaret Kahurananga akitoa neno la shukrani kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu mara baada ya kuhitimisha ziara ya kikazi katika ofisi hiyo.



Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu (katikati aliyekaa) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na watendaji wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma mara baada ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi jijini Dodoma.