Wednesday, August 7, 2024

OFISI YA RAIS-UTUMISHI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA WADAU WA SEKTA YA AFYA KATIKA KUHAKIKISHA WATUMISHI WA UMMA WANAPATA FURSA YA KUTAMBUA HALI ZAO ZA KIAFYA ILI KUONGEZA UFANISI KIUTENDAJI

Na. Veronica Mwafisi-Dodoma

Tarehe 07 Agosti, 2024

Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta ya afya ikiwemo Hospitali ya Kanda ya Benjamin Mkapa ili kuhakikisha watumishi wa umma wanapata fursa ya kutambua hali zao za kiafya na kuchukua hatua stahiki kwa lengo la kuongeza ufanisi kiutendaji.

Hayo yamesemwa leo na Mwakilishi wa Katibu Mkuu - UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Bw. Cyrus Kapinga wakati akizindua kambi maalum ya uchunguzi wa Magonjwa Yasiyoambukizwa kwa watumishi wa umma uliofanyika katika jengo dogo la Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mtumba jijini Dodoma.

Bw. Kapinga amesema Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora ambayo ndio msimamizi wa Utumishi wa Umma na Utawala Bora ina wajibu wa kuhakikisha Taasisi za Umma zinatekeleza dhana ya Utawala Bora ikiwemo kusimamia vema eneo la Menejimenti ya ujumuishwaji wa Anuai za Jamii ikiwemo udhibiti wa VVU, UKIMWI na MSY mahali pa kazi katika Utumishi wa Umma.

Aidha, Bw. Kapinga amewashukuru Viongozi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Wataalam wa afya kwa kushirikiana kuandaa kambi hiyo ambayo ni muhimu kwa watumishi wa umma kwani asilimia kubwa huathirika na magonjwa yasiyoambukiza pasipo wao kujua.

Pia amewapongeza waajiri wa Wizara na Taasisi zote ambao wameridhia watumishi wao kushiriki zoezi hilo muhimu kwani mwitikio umekuwa ni mkubwa.

Awali akitoa neno la utangulizi, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Profesa Abel Makubi ameishukuru Ofisi ya Rais-UTUMISHI kwa kuratibu na kusimamia kwa kushirikiana na Hospitali ya Benjamin Mkapa katika zoezi la Kambi ya Uchunguzi, Ushauri na Elimu ya Afya kwa watumishi wa Umma katika Wizara, Taasisi na sekta binafsi.

Naye, Mkurugenzi Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bw. Musa Magufuli amewashukuru Madaktari Bingwa wa Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa kukubali kushiriki zoezi hilo la Kambi ya Uchunguzi, Ushauri na Elimu ya Afya kwa watumishi wa Umma kwani mwitikio umekuwa mkubwa wa watumishi hao kutaka kujua hali zao za afya.

Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imeshirikiana na Hospitali ya Kanda ya Benjamin Mkapa katika kuratibu zoezi hilo ikilenga kuwafikia watumishi wa umma ili waweze kufahamu hali zao za afya na kupata ushauri wa kitaalam kutoka kwa Madaktari Bingwa.

 

Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Bw. Cyrus Kapinga akizungumza na Viongozi na Watumishi wa Umma wakati wa uzinduzi wa Kambi ya Uchunguzi, Ushauri na Elimu ya Afya uliofanyika katika jengo dogo la Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

Baadhi ya Wakurugenzi Wasaidizi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na watumishi wengine wa Wizara na Taasisi wakimsikiliza Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Bw. Cyrus Kapinga (hayupo pichani) wakati akizindua Kambi ya Uchunguzi, Ushauri na Elimu ya Afya uliofanyika katika jengo dogo la Ofisi hiyo Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Profesa Abel Makubi akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Bw. Cyrus Kapinga kuzindua Kambi ya Uchunguzi, Ushauri na Elimu ya Afya uliofanyika katika jengo dogo la Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Bw. Cyrus Kapinga akipatiwa huduma ya kupimwa macho wakati wa uzinduzi wa Kambi ya Uchunguzi, Ushauri na Elimu ya Afya uliofanyika katika jengo dogo la Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.


Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Profesa Abel Makubi (kushoto) akimkaribisha Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Bw. Cyrus Kapinga kuzindua Kambi ya Uchunguzi, Ushauri na Elimu ya Afya uliofanyika katika jengo dogo la Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma. Katikati ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu, Hospitali ya Benjamin Mkapa, Bi. Prisca Lwangili.


Mkurugenzi Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bw. Musa Magufuli akitoa neno la shukrani kwa Viongozi na Watumishi wa Umma waliohudhuria uzinduzi wa Kambi ya Uchunguzi, Ushauri na Elimu ya Afya uliofanyika katika jengo dogo la Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.


Baadhi ya Wakurugenzi na Watumishi wa Umma wa Wizara na Taasisi wakifanya mazoezi ya viungo kabla ya kusikiliza hotuba ya Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Bw. Cyrus Kapinga wakati wa uzinduzi wa Kambi ya Uchunguzi, Ushauri na Elimu ya Afya uliofanyika katika jengo dogo la Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.


Mkurugenzi Msaidizi Anuai za Jamii na Mratibu wa VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mwanaamani Mtoo akitoa utambulisho wa Viongozi na wageni waliohudhuria uzinduzi wa Kambi ya Uchunguzi, Ushauri na Elimu ya Afya uliofanyika katika jengo dogo la Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.


Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Cyrus Kapinga akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Madaktari Bingwa kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa wakati wa uzinduzi wa Kambi ya Uchunguzi, Ushauri na Elimu ya Afya uliofanyika katika jengo dogo la Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.


No comments:

Post a Comment